Wednesday 29 April 2020

MAJAMBAZI WAVAMIA KANISA KATOLIKI KATOLIKI PAROKIA YA MODEKO MOROGORO..KANISA LAFUNGWA KWA KUFURU

Na Angela Kibwana, Morogoro Na P. Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.
Mheshimiwa Padre Lazarus Vitalis Msimbe, S.D.S., Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Katoliki la Morogoro nchini Tanzania amefunga Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Mtakatifu baada ya kuwasiliana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Ubalozi wa Vatican nchini Tanzania. 

Kuanzia tarehe 27 Aprili 2020 Kanisa la Parokia ya Modeko limefungwa na halitaweza kutumika kwa sasa hadi pale, Tabernakulo mpya itakapowekwa wakfu.

 Ibada hii inatarajiwa kuadhimishwa wakati wa Sherehe ya Ekaristi Takatifu, fursa makini kwa waamini kutangaza na kushuhudia imani ya Kanisa kuhusu Fumbo la Ekaristi Takatifu, yaani uwamo wa Kristo katika maumbo ya Mkate na Divai. 

Mababa wa Kanisa wanathibitisha kwamba, kwa nguvu ya imani ya Kanisa na uwezo wa Neno la Kristo Yesu, na tendo la Roho Mtakatifu, kwamba, mageuzo ya Mkate na Divai yanakuwa ni Mwili na Damu Azizi ya Kristo.

Padre Nikodemas Masong, Paroko wa Parokia ya Modeko, Jimbo Katoliki la Morogoro amesema, watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi tarehe 27 Aprili 2020 walivamia na kuvunja mlango wa Kanisa la Parokia ya Modeko na kufanikiwa kuiba Tabernakulo iliyokuwa inahifadhi Ekaristi Takatifu na kutokomea mahali kusikojulikana. 

Walivunja pia milango ya ofisi za Parokia na kufanikiwa kuiba kiasi cha shilingi laki tatu na nusu, mali ya Chama cha Watumishi wa Altare Parokiani hapo. Walifanikiwa pia kuiba “Mixer” inayotumika kwa ajili ya mawasiliano Parokiani hapo.

 Familia ya watu wa Mungu ndani na nje ya Jimbo Katoliki la Morogoro imesikitishwa sana na kufuru hizi dhidi ya mahali na mambo matakatifu yanayogusa undani wa imani ya watu.


Via Vatican News
Share:

WAZIRI JAFO ATOA MAELEKEZO KUHUSU MPANGO WA UFUNDISHAJI WANAFUNZI KIELEKTRONIKI

Nteghenjwa Hosseah – OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)Selemani Jafo amelitaka Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA) na Taasisi ya Elimu Tanzania(TET), kuhakikisha utaratibu wa kufanya marejeo ya mitihani ulioanza kwa kidato cha sita uhusishe madarasa yote yanayotarajia kufanya mitihani ya Taifa.

Aidha, amewataka wanafunzi kuzingatia ratiba ya masomo inayotolewa ili wasikose vipindi vinavyorushwa kwenye redio,runinga na mitandao ya kijamii.

Jafo alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa masomo kwa njia ya runinga,redio na mitandao ya kijamii.

Alitaka taassi hizo kuangalia utaratibu huo wa marejeo kwa madarsa mengine kama kidato cha pili,cha nne,darasa la saba na la nne ili nao wawe na umahiri katika kujibu mitihani yao.

Alisema Serikali kupitia wadau mbalimbali imetoa fursa hiyo muhimu ambayo inapaswa kuzingatiwa na watu wote wakiwemo wazazi,walimu na wanafunzi wenyewe.

“Niwatake wanafunzi wote hasa wa kidato cha sita ambao sasa maandalizi ya kufanya marejeo yanafanyika,tutumie fursa hii vizuri ya kujiandaa kwa utaratibu mpya utakaotumika kuanzia mwaka huu wa kupima umahiri tofauti na ule wa awali wa kuulizana maswali tuliouzoea,”alisema Jafo.

Aliongeza kuwa “Wanafunzi tumieni fursa hii iliyoletwa kwenu,zingatia ratiba,jipimeni uwezo wenu ili wenzio wasikuache nyuma pindi mkirudi shuleni,someni kwa bidii kwa maana tunataka kuelekea kwenye Taifa lenye uchumi imara.”

Aliwataka walimu kutumia fursa hiyo kujijengea uwezo wao wenyewe pia lakini kuwawezesha kuwa na uelewa zaidi ili wanafunzi wao watakapohitaji msaada pale watakapokwama wawe wanajua nini kinachoendelea.

“Walimu wetu najua mtu huwezi kuwa mkamilifu kwenye maeneo yote,kwa upande wenu hii pia ni fursa ya kujijengea uwezo kupitia walimu waliopo kwenye program hii ili ukirudi shuleni unakuwa umeongeza kitu kipya,lakini mwanafunzi wako anaweza kukupigia simu ameshindwa kuelewa sehemu Fulani hivyo inakuwa rahisi kumuelewesha,”alisema Jafo.

Waziri Jafo alisema kama Waziri anayesimamia elimu ya awali,msingi na sekondari amefarijika kuanza kwa utaratibu huo na ni imani yake kuwa pengo la vijana waliokuwa wanakaa nyumba bila ya msaada wowote wa kimasomo linaenda kuzibika.

“Wazazi wapeni nafasi watoto wenu ya kushiriki vipindi vyote vinavyotolewa, inawezekana vipindi vinaendelea wewe mzazi umempa mtoto wako kazi nyingine anafanya hilo sio sahihi, toa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha watoto wanasoma na kufanya mazoezi yote yanayotolewa na walimu,”alisisitiza Jafo.

Jafo alivitaja vyombo vya habari ambavyo vinashiriki kikamilifu katika mpango huu wa ufundishaji wa vipindi kwa njia ya Televisheni na Radio kuwa ni TBC, ZBC, Azam Tv, Channel Ten, Clouds Fm, Global Tv, Gel Tv na Radio mbalimbali.

Pia aliwakumbusha wazazi na wanafunzi wote kuwa vipindi hivyo vitakua vinarushwa kupitia mtandao wa Youtube kwa ajili ya marudio ili kujenga uelewa zaidi.

“Mitandao ya Youtube itakayokuwa inarusha vipindi hivyo ni ya Baraza la Mitihani – NECTA, Taasisi ya Elimu Tanzania – TEA, Global Education Link – GEL, Global Tv, Azam Tv, ZBC TV na EATV” alisisitiza Jafo.

Alizipongeza taasisi zote binafsi zilizoshirikiana na Serikali kuhakikisha lengo lake linatimia katika kipindi hiki cha mpito cha ugonjwa wa Corona unaosababisha homa kali ya mapafu(COVID 19).

Alizataja Taasisi hizo kuwa ni Mawakala wa Vyuo Vikuu Nje ya Nchi yaan Global Education Link (GEL), UNESCO na Taasisi ya Elimu Solution.


Share:

LHRC YAZINDUA RIPOTI YA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA 2019


Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga (katikati), Afisa Utafiti, Fundikila Wazambi (kushoto) na Mkurugenzi wa Uwajibikaji na Uwezeshaji wa Kituo hicho, Felista Mauya (kulia) wakionesha nakala za Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2019 mara baada ya uzinduzi leo Jumatano  leo Aprili 29, 2020 katika ofisi za LHRC jijini Dar es Salaam na wadau kufuatilia kwa njia ya mtandao.
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga (katikati) akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2019. Uzinduzi huo uliofanyika  leo Aprili 29, 2020 katika ofisi za LHRC jijini Dar es Salaam na wadau kufuatilia kwa njia ya mtandao.

***
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimezindua Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2019 inayoangazia hali ya haki za binadamu kwa mwaka 2019 na kufanya ulinganisho wa hali ilivyokuwa mwaka 2018. 

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatano, Aprili 29, 2020 kwa njia ya mtandao kufuatia mlipuko wa virusi vya Corona. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC amesema ripoti hiyo inahusisha matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu sambamba na mapendekezo kwa ajili ya uboreshaji wa sera, sheria na utendaji katika jamii. 

Anna amesema ripoti hiyo inaangazia hali ya haki za binadamu katika nyanja za haki za kiraia na kisiasa; haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni; haki za makundi yaliyo hatarini; mifumo ya Ulinzi wa Haki za binadamu na haki za kijumla.

“Ripoti hii ni matokeo ya taarifa mbalimbali zilizokusanywa na LHRC ikiwemo taarifa kutoka kwa waangalizi wa haki za binadamu walio nchi nzima, wasaidizi wa kisheria walio katika wilaya mbalimbali, taarifa rasmi toka taasisi za Serikali, Bunge, Mahakama, jeshi la polisi, vyombo vya habari na asasi mbalimbali za kiraia zisizo za Serikali. Taarifa hii pia hutumia taarifa mbalimbali za kitaifa lakini pia na za kimataifa, hasa zinazolenga kuelezea hali ya haki za binadamu nchini”, amesema Anna Henga.

Kwa mujibu wa Ripoti hiyo, haki tano zilizokiukwa zaidi kwa mwaka 2019 ni pamoja na:

Haki ya Kuishi ambapo matukio kama vile mauaji ya wanawake, mauaji ya watoto, mauaji yanayotokana na kujichukulia sheria mkononi, mauaji yanayotokana na imani za kishirikina pia yameendelea kuripotiwa.

Uhuru dhidi ya ukatili; ambapo matukio yaliyoripotiwa ni Ukatili wa kingono na kimwili dhidi ya watoto; ukatili wa kingono na kimwili dhidi ya wanawake. Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2017 hadi mwezi Juni 2019, jumla ya matukio 88,612 ya ukatili wa kijinsia yameripotiwa.Matukio ya ukatili wa kingono dhidi ya watoto jumla ya matukio 3,709 ya ubakaji yaliripotiwa katika vituo vya polisi nchini ikiwa ni matukio 126 zaidi ya yale yaliyoripotiwa katika kipindi kama hicho mwaka 2018. ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu na wazee nao umeendelea kushika kasi katika tukio moja, bibi wa miaka aliripotiwa kubakwa hadi kufariki. 

Uhuru wa Kujieleza; muendelezo wa uminywaji wa uhuru wa kujieleza ambapo kumekuwepo na Sheria kandamizi, ukamataji na uwekaji kizuizini waandishi wa habari kinyume na sheria pamoja na kufungiwa kwa vyombo vya habari

Haki ya kuwa Huru na Salama; Ripoti imeripoti matukio kadhaa yanayopelekea kuminywa kwa haki hiyo kama vile Mashambulizi na mauaji ya madereva bodaboda pamoja na Matukio ya utekaji, watu waliopotea na matukio ya ukamataji na uwekaji kizuizini kinyume na sheria.

Haki ya Kujumuika na Kukusanyika; zimeendelea kukiukwa hasa kipindi hiki ambapo tunaelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Vyama vya siasa, hususan vya upinzani, viliendelea kulalamikia maamuzi haya kwamba yanakiuka haki yao inayolindwa na Katiba, jambo linaloathiri pia ushindani wao kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. Vyama hivi pia vililalamika kwamba marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa yanaminya uhuru wao wa kujumuika na kukusanyika.

LHRC kupitia Mkurugenzi Mtendaji wake, Anna Henga wametoa rai kwa serikali na wanajamii kwa ujumla kuchukau hatua katika kulinda na kudumisha haki za binadamu. 

“Tunatoa rai kwa serikali, taasisi na jamii ya Watanzania kuendelea kulinda haki za binadamu na kuwawajibisha wale ambao wameshindwa kuheshimu haki hizo bila ubaguzi wa kikabila, kidini, kisiasa na kijinsia ili tuweze kuifikia jamii yenye haki na usawa”,amesisitiza Anna Henga.

Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2019 ni muendelezo wa ripoti za kituo hicho zinazotolewa kila mwaka kwa lengo la kuonesha hali na kutoa mapendekezo ya maboresho.
Share:

RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA MBUNGE WA SUMVE, RICHARD NDASSA




Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO



Zati 50
Full Power


Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

WAGONJWA WA CORONA KENYA WAFIKA 384


Idadi ya walioambukizwa virusi vya Corona nchini Kenya yafikia 384, ni baada ya wagonjwa wapya 10 kuongezeka ambapo tisa ni kutoka Mombasa na mmoja ni kutoka Nairobi.



Akiongea na Waandishi wa habari leo, Aprili 29, 2020 Katibu wa Afya Mercy Mwangangi amesema katika saa 24 zilizopita sampuli 580 kutoka kaunti 24 zilipimwa dhidi ya homa hiyo.
 


Share:

MUME NA MKE WACHARANGWA MAPANGA NA MKWE WAO AKILIPIZA KISASI WAMEMBANIA KURUDIANA NA MKE WAKE

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwanaume aitwaye Mwandu Chalya (75) na mke wake aitwaye Gigwa Kwangu (70) wamenusurika kufa wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao baada kukatwa na kitu chenye ncha kali na mkwe wao Masele Boniface akilipiza kisasi walivyokataa asirudiane na mke wake kutokana na kupeana talaka mahakamani. 

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Aprili 29,2020 majira ya saa nane usiku katika kitongoji cha N'halange, kijiji cha Mwamasololo, kata ya Sekebugoro, tarafa ya mondo, wilaya ya Kishapu. 

Amesema Mwandu Chalya (75) pamoja na mke wake aitwaye gigwa Kwangu (70) wote wakazi wa Mwamasololo walijeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za miili yao na mtu aliyetambulika kwa jina la Masele Boniphace ambaye ni mkwe wao wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao. 

“Chanzo cha tukio hili ni chuki /kulipiza kisasi baada ya wazazi hao wa mke wake aitwaye Emiliana Mwandu (31) mkazi wa Mwamasololo kumkataza kurudiana na Masele Boniface baada ya kutengana kwa kupeana talaka mahakamani mnamo tarehe 06/05/2019 kwa sababu za ukatili aliokuwa akifanyiwa na mtuhumiwa kwa kupigwa hadi kupoteza fahamu kipindi hicho 2019”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

Amesema majeruhi wanapatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga na hali zao zinaendelea vizuri. 

Kamanda Magiligimba amesema mtuhumiwa alikimbia mara baada ya tukio hilo na juhudi za kumtafuta na kumkamata zinaendelea. 



Kamanda Magiligimba ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuacha kabisa tabia ya kujichukulia sheria mkononi na inapotokea kutoridhika na maamuzi ya mahakama ni vyema kuchukua hatua ya kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya mahakama badala ya kujichukulia sheria mkononi.
Share:

BUNGE LAAHIRISHWA KUFUATIA KIFO CHA MBUNGE WA SUMVE, RICHARD NDASSA


Spika wa Bunge, Job Ndugai, leo Aprili, 29, 2020, ameahirisha Mkutano wa 19, Kikao cha 9, cha Bunge hadi kesho, kufuatia kifo cha Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa.



Ndassa anakuwa mbunge wa pili wa CCM, kufariki dunia wakati Mkutano huu wa Bunge la 19 ukiendelea, baada ya Mbunge wa Viti Maalumu Mchungaji Getrude Rwakatare kufariki dunia wiki iliyopita.

“Waheshimiwa wabunge, ninaomba kuwajulisha kuwa bunge letu limepata na msiba mwingine mkubwa wa kuondokewa na mbunge mwenzetu wa Jimbo la Sumve  ambaye amefariki usiku wa kuamkia leo hapa Dodoma.

“Kufuatia msiba huo, taratibu mbalimbali za mazishi zimeanza kufanyika kwa mawasiliano kati ya Ofisi ya Bunge na familia ya marehemu na serikali na kila tukipata taarifa zadi za kuwataarifu tutafanya hivyo,” amesema.

Aidha, akimueleze Ndassa, Spika Ndugai amesema; “Marehemu Ndassa ni mmoja wa wabunge waliokuwa wanaitwa senetors, alikuwa ni mmoja wa wabunge waandamizi walioingia bungeni tangu mwaka 1995, amekuwa mbunge wa Sumve kwa vipindi vitano na miezi… hii inaonyesha imani kubwa waliyokuwa nayo wananchi wa Sumve na wabunge wengi tunaweza tukajifunza uongozi bora kwa kufuata nyayo zake.

Pamoja na mambo mengine, Spika Ndugai amesema kwa mujibu wa Kanuni ya 151 ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la 2016, kwa siku ya leo hawataendelea na kikao cha bunge badala yake watakuwa na maombolezo ya msiba wa mbunge huyo.

“Tutajitahidi sana iwezekanavyo kuhakikisha kwamba ndugu yetu anazikwa kule Sumve kesho jioni, tutajitahidi sana sana… kwa sababu kwa mila zetu za Kiafrika kwa kweli kumzika mtu popote pale ni jambo linalotupa ugumu fikiria wote tuliopo hapa upate jambo kama hilo halafu  unawekwa popote, kwa hiyo tutajitahidi sana. Kwa hiyo ofisi yangu itashirikiana na serikali kuona kila kinachowezekana kinafanyika,” amesema Spika Ndugai.


Share:

Serikali ya Uganda yatathmini uwezekano wa kulegeza masharti ya watu kutembea...Museven Katoa Masharti Kwa Madereva wa Malori

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema hivi karibuni atatangaza iwapo atalegeza masharti ya watu kukaa nyumbani kutokana na mamabukizi ya Corona, katika taifa hilo ambalo limeshuhudia maambukizi ya watu 79.

Wakati huo huo rais Yoweri Museveni ametangaza hatua mpya za kudhibiti mienendo ya madereva wa malori yanayoingia nchini humo kutoka mataifa jirani baada ya zaidi ya madereva 20 kupatikana na ugonjwa wa Covid-19.

Hatua hizo ni pamoja na kila lori kuwa na mtu mmoja - dereva pekee yake ambaye hataruhusiwa kulala hotelini wala nyumbani kwa watu.

Katika hotuba yake kwa taifa usiku wa Jumanne rais Museveni amebaini kwamba madereva hao ni tishio katika mapambano ya nchi hiyo dhidi ya Corona akitoa mfano wa janga la Ukimwi la miaka ya 1980 na miaka ya tisini wakati ambapo madereva wa malori katika kanda hiyo waliaambukiza watu virus vya HIV katika kila miji waliyopitia wakiwa safarini. Muda wa watu kubaki nyumbani unamalizika tarehe 5 Mei 2020.

Wakati hayo yakijiri Shirika la Kimataifa la Kutoa Misaada (IRC) limeonya kuwa watu bilioni moja huenda wakaambukizwa virusi vya Corona kote duniani, huku likisema nchi zisizojiweza zinahitaji usaidizi wa haraka.


Share:

Idadi ya Vifo Vya Corona Nchini Marekani Yazidi Idadi ya Wamarekani Waliofariki Wakati wa Vita Vya Vietnam

Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani imeongezeka na kufikia zaidi ya Milioni moja, huku idadi ya watu walipoteza maisha ikifikia zaidi ya 58,000.

Takwimu za kiafya zinaonesha kuwa kwa sasa Marekani ina visa vya maambukizi 1,035,765  huku idadi ya watu walipoteza maisha ikifikia zaidi ya Elfu 59.

Wachambuzi wa mambo nchini humo wanasema idadi ya watu walipoteza maisha sasa inazidi ile iliyoshuhudiwa wakati wa vita nchini Vietnam.

Kulingana na ripoti ya Chuo Kikuu cha Johns Hopkins, watu 59,266 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa Covid-19 nchini Marekani, nchi iliyoathirika zaidi ulimwenguni, wakati askari 58,220 wa nchi hiyo walipoteza maisha wakati wa vita vya Vietnam (1955-1975), kulingana na ripoti rasmi iliyochapishwa kwenye Jalada la kitaifa.

Ongezeko la maambukizi na vifo linatishia hatma ya kisiasa ya rais Donald Trump ambaye atatetea kiti chake wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Novemba.


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa: Tutaendelea Kuboresha Huduma Za Afya

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekabidhi magari 10 ya kubebea wagonjwa kwa wabunge ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za dhati za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora za afya karibu na makazi yao.

Magari hayo 10 ni kati ya magari 50 ya kubebea wagonjwa yenye thamani ya sh. bilioni sita yaliyonunuliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Global Fund. Kati ya magari hayo, 18 yatapelekwa kwenye Hospitali za Rufaa za Mikoa na 32 ni kwa ajili ya hospitali za Halmashauri pamoja na vituo vya afya.

Waziri Mkuu amekabidhi magari hayo leo (Jumatano, Aprili 29, 2020) kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. Ambapo amesema mbali na magari hayo kutolewa kwa ajili ya kuboresha huduma za mama na mtoto pia yatatumika kuwahudumia wagonjwa wa corona ili kuokoa maisha ya wananchi.

“Eneo hili tumeliwekea nguvu za kutosha na Watanzania wote ni mashahidi kwa namna ambavyo Serikali imejitahidi sana katika kupunguza vifo vya mama na mtoto kwenye jamii zetu. Magari haya yatakwenda kutumika kwa ajili ya mama na mtoto lakini kwa kuwa gari litakuwepo kituoni litawahudumia na wagonjwa wengine.”

Waziri Mkuu amewashukuru wabunge wote kwa namna wanavyoishauri Serikali katika kufanya maboresho ya sekta mbalimbali za maendeleo ikiwa ni pamoja na sekta ya afya ambapo leo wameshuhudia matunda ya ushauri wanaoutoa.

“Magari haya yatakwenda kufanya kazi ya kuokoa maisha ya Watanzania wengi kwa kuwasafirisha wagonjwa wa rufaa kutoka kituo cha afya kwenda hospitali ya wilaya na hospitali ya wilaya kwenda hospitali ya rufaa.”

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema ununuzi wa magari hayo ni utekelezaji wa ahadi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuboresha zaidi huduma afya kwa wananchi.
 
Waziri Ummy amesema Wizara imenunua magari hayo ili kuimarisha huduma za rufaa kwa wagonjwa hususani kwa akina mama wajawazito hata hivyo kutokana na changamoto ya ugonjwa wa corona pia magari hayo yatatumika kwa ajili ya kubebea wagonjwa wa corona.

“Watanzania wameshuhuduia kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli, wameshuhudia upatikanaji wa dawa, wameshuhudia maboresho makubwa katika upatikanaji wa vifaa tiba, ujenzi wa vituo vya afya, ujenzi wa hosptali za halmashauri pamoja na hospitali za rufaa za mikoa na uboreshwaji wa miundombinu ya kutolea huduma za afya.”

Akizungumza kwa niaba ya wabunge waliopokea magari hayo, Mbunge wa Ileje, Janneth Mbenne amemshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kitendo hicho cha kihistoria. “Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa mawazo na maono makubwa ya maendeleo ya Taifa. Magari haya yatakwenda kuboresha huduma za afya katika majimbo yetu.”

Naye Mbunge wa Kilolo, Venance Mwamoto ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2015-2020 kwa vitendo. “…moyo usio na shukurani hukausha mema yote na heri wale wanaowajali wagonjwa kwa maana ufalme wa Mungu ni wao.”

Pia, Mbunge wa Nyasa na Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Stella Manyanya amesema kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Nyasa wanamshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa msaada huo kwani walikuwa na changamoto kubwa na gari la kubebea wagonjwa.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Breaking : MBUNGE WA SUMVE RICHARD NDASSA AFARIKI DUNIA


Habari zilizotufikia hivi punde zinasema Mbunge wa Jimbo la Sumve Mhe. Richard Ndassa (CCM) amefariki dunia leo Jumatano Aprili  29,2020.

Page Liked · 30 mins 

Miaka hii mitatu imenikumbusha sana namna tulivyo viumbe dhaifu hapa duniani na kwamba hakuna jambo moja lililo la uhakika kwenye maisha yetu. Maana leo upo, na kesho haupo. Sekunde hii Mzima, na ijayo hujui nini kitatokea. Tuswali sana na kuomba radhi za Allah ndugu zangu. RIP Mzee wangu, Mhe. Ndasa.

Tutawalete taarifa kamili hivi punde..
Share:

Picha : WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKABIDHI MAGARI 50 YA KUBEBEA WAGONJWA KWA WABUNGE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Dodoma Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri , Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde wakati alipokabidhi magari 50 ya kubebea wagonjwa  kwa wabunge yenye thamani ya  shilingi bilioni 6, Aprili 29, 2020.


Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na wa tatu kulia ni Mbunge wa Nyasa ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi, Stella Manyanya.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) wakifurahia wakati  Mbunge wa Urambo, Margaret Sitta (kulia) alikionyesha ufunguo wa gari la kubebea wagonjwa baada ya kukabidhiwa wakati Waziri Mkuu alipokabidhi magari 50 ya kubebea wagonjwa  kwa wabunge yenye thamani ya  shilingi bilioni 6, Aprili 29, 2020. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kilolo, Venance Mwamoto (kulia) wakati alipokabidhi magari 50 ya kubebea wagonjwa  kwa wabunge yenye thamani ya  shilingi bilioni 6, Aprili 29, 2020. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga wakati alipokabidhi magari 50 ya kubebea wagonjwa  kwa wabunge yenye thamani ya   shilingi bilioni 6, Aprili 29, 2020. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma. Katikati ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Share:

WAGONJWA WA CORONA TANZANIA WAFIKIA 480 ....KUNA ONGEZEKO LA WAGONJWA WAPYA 196


Na.WAMJW,Dodoma
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ametoa taarifa ya mwenendo wa Ugonjwa wa Corona nchini ambapo amesema kuwa kuna maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa watanzania 196 ambapo kati yao; kutoka Bara ni 174, Zanzibar 22 na kufanya jumla ya watu waliopata maambukizi kuwa ni 480.

Aidha,Waziri Majaliwa amesema kuwa idadi ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 167, (Zanzibar wako 36, Bara ni 83). 

Hali kadhalika vifo 6 vimetokea na kufanya jumla ya waliofariki kwa ugonjwa wa Corona kufikia 16 hadi sasa. 

Waziri Mkuu ametoa rai kwa Watanzania kuacha kutoa taarifa za uzushi za vifo kuwa kila Kifo kinachotokea hakisababishwi na Ugonjwa wa Corona.
Share:

NAIBU WAZIRI NYONGO AONGOZA KIKAO CHA MARIDHIANO NA KUPOKEA OMBI LA MWEKEZAJI


NAIBU Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Nzega ili kusikiliza maombi na kutatua  changamoto za wachimbaji wadogo wa madini Aprili 27 mwaka huu
NAIBU Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo kulia akihoji jambo kwa wachimbaji waliokuwa wakilalamika kutopewa leseni kwenye eneo ambalo waliliomba jambo ambalo RMO alipaswa kukaa na pande hizo kutafuta muafaka
NAIBU Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akizungumza na waandishi wa habari juu ya makubaliano yaliyofikiwa mara baada ya wajumbe kujadili maombi ya mwekezaji ya kutaka kupunguziwa gharama ya ununuzi wa madini ya dhahabu baada ya uchenjuaji wa marudio wa mchanga wa dhahabu ulioachwa na mwekezaji mkubwa wa madini wa kampuni ya  Resolute iliyokuwa ikifanya shughuli zake wilaya ya Nzega kufunga mgodi      
NAIBU waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Nzega kulia Godfrey Nyapula wakati wa kikao na wachimbaji wadogo wa madini kilichofanyika kwenye ofisi za Mkuu huyo wa wilaya Aprili 27 mwaka huu
KATIBU Mtendaji wa Tume ya Madini Proffesa Shukrani Manyaa akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua zinazofuata baada ya kikao cha kuridhia ombi la mekezaji ili utekelezaji wake uwekwe katika utaratibu unaokubalika kisheria


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, akiongoza kikao kilichohudhuriwa na Katibu Mtendaji wa TumeyaMadini, Prof. ShukraniManya, MkuuwaWilayayaNzega, Godfrey Ngupula, Afisa  Madini Mkazi wa Mkoa waTabora, Mhandisi Mayingi Makalobela, Mkuu wa Chuo cha Nzega, Nuru Shaban Kamati ya Ulinzi na Usalama  wilaya ya Nzega pamoja na mwekezaji wa uchenjuaji wa marudio, RashedShabout Said.

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa waTabora, Mhandisi Mayingi Makalobela akitoa maoni yake juu ya ombi la mwekezaji Rashed Shabout Said wa uchenjuaji wamarudio ya mchanga ulioachwa na kampuni ya resolute baada ya mgodi huo kufungwa.


SERIKALI  imeridhia ombi la kupunguza gharama ya ununuzi wa dhahabu unaofanywa na mwekezaji Rashed Shabout Said wa kampuni ya Ashery Construction &Matinje gold Extraction yauchenjuaji wa marudio ya mchanga wa dhahabu ulioachwanakampuniya Resolute iliyofunga shughuli zake za uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu mwaka 2014.

Makubaliano hayo yalifikiwa Aprili 27, 2020 wakati wa kikao kilichoongozwa na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus  Nyongo kilicholenga kujadili ombi la mwekezaji Rashed Shabout Said anayechenjua dhahabu kwenye mabaki hayo ya mchanga wa dhahabu ulioachwa na kampuni ya Resolute iliyokuwa ikichimba dhahabu wilayani Nzega,MkoaniTabora.

Pamoja na NaibuWaziri Nyongo kikao hicho kiliwahusisha Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini,Profesa Shukrani Manya, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tabora Mayingi Makalobela, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Godfrey Ngupula, Mkuuwa Chuo cha Madini kampasi yaNzega, Nuru Shabani, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nzega pamoja na  ujumbe ulioambatana na mwekezaji huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao hicho, Naibu Waziri Nyongo alisema, kikao kimeridhia ombi moja kati ya matatu yaliyowasilishwa na mwekezaji ikiwa ni kushusha bei ya kumwuzia dhahabu kiasi kilichopunguzwa kimsaidie kulipia  gharama nyingine anazozitumia katika uwekezaji huo.

Nyongo alisema Rashed aliomba kupunguzi wa gharama ya dhahabu anayoinunua serikalini mara baada ya uchenjuaji, kuondolewa gharama za watumishi wanaoshiriki katika kusimamia mchakato mzima wa uchenjuaji wa mchanga huo pamoja na kuondolewa malipo ya mrabaha nakurudishiwa pesa zilizolipwa kama mrabaha kwa awali mbili za uchenjuaji zilizopita.

Nyongo alibainisha kuwa Wizara kwa kushirikiana na Tume ya madini zimeridhia kupunguza gharama ya kuuza dhahabu kwa  mwekezaji huyo na kwamba huduma nyingine na malipo ya mrabaha yatapaswa kulipwa kama kawaida  kwa mujibu wa sheria.




Kwaupande wake, KatibuMtendajiwaTumeyaMadini, Prof. Shukrani Manya alisema ombi la mwekezaji limepokelewa na kwamba hatua inayofuata nikwenda kupitia na kurekebisha mkataba ikiwani pamoja na kupeleka maoni yaliyofikiwa na kikao hicho kwa mamlaka nyingine ili kumwezesha mwekezaji huyo kufanya kazi yake kwa tija na bila manung’uniko.


Akizungumza na waandishi wa habari mwekezaji Rashed, aliishukuru serikali kwa kupokea na kufanyia kaziombi lake na kukiri hakutegemea kuwa angesaidiwa kw aharaka namna ilivyofanyika nakukiri kwamba hakika Serikali ya Awamu ya Tano inasikilizana kutatua changamoto za wananchi.


“Nashukuru sana kwa serikali hadi Naibu Waziri kuja kunisikiliza kwa kweli Wizara ya madini nisikivu sana, nashukuru sana” Rashed alikazia.

Akizungumzia changamoto wanazokutana nazo kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa corona Rashed alisema kumekuwa na changamoto ya usafirishaji wa madini kutokana na ndege nyingi za nje kusitisha safari zanje hivyo inakuwa ngumu kwa kuendesha biashara.

Share:

Digital Support Executive at Vodacom Tanzania

Digital Support Executive Posting Country:  Tanzania, United Republic of Date Posted:  28-Apr-2020 Full Time / Part Time:  Full Time Contract Type:  Permanent Joining Vodacom is more than a job, what we do matters. We don’t just carry minutes, texts and data – we carry people’s lives. And that’s a huge responsibility. If you think for a minute about the people you rely… Read More »

The post Digital Support Executive at Vodacom Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

KIJANA AMUUA BABA YAKE KWA KUMKATA PANGA AKIDAI URITHI WAKE

NB- Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Israel Mwaisaka, Sumbawanga
Jeshi la Polisi mkoani Rukwa linamshikilia kijana mmoja mkazi wa Kijiji cha Mtenga Tarafa Namanyere wilayani Nkasi, kwa tuhuma za kumuua kwa kumkata kata mapanga kichwani baba yake mzazi aitwaye Ntemi Seni (65) akidai urithi wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Justine Masejo amesema kuwa tukio la kuuawa kwa mzee huyo lilitokea Aprili 25, mwaka huu majira ya saa 09:30 usiku huko Kijiji Mtenga wilayani Nkasi.

Amesema, kijana huyo mwenye umri wa miaka 36 jina linahifadhiwa inadaiwa alikuwa akitaka baba yake mzazi ampe urithi wa mali alizonazo ili ziweze kumsaidia kupata kuendesha maisha yake pasipo utegemezi.

Masejo amesema, baada ya kijana huyo kushinikiza mara kadhaa apewe sehemu ya mali ya mzazi wake kama urithi na baba yake kukataa kufanya hivyo kulizuka vurugu baina yao ndipo kijana huyo alipochukua panga na kuanza kumkimbiza na kisha kumkamata na kuanza kumkata kata na mapanga kichwani.

Kamanda amesema, Baba huyo alivuja damu nyingi katika sehemu ya kichwa na kufariki dunia muda mfupi baadae kutokana na kukosa msaada wa haraka wa kufikishwa hospitalini kwa matibabu.

Amesema, mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi na atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa awali kukamilika.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger