Thursday 2 April 2020

Tangaza Biashara Yako Au Bidhaa Yako Kwenye Mtandao huu Kwa BEI NZURI Kabisa


Tunakaribisha  matangazo  ya  aina  zote( Bishara, Viwanja, Bidhaa, matangazo ya Vyuo na mengine mengi)  .Bei  zetu  ni  nzuri  sana  na  kamwe  hutajuta  kutangaza  biashara  yako  kupitia  mtandao  huu....

Kwa mwezi tunafunga na Pageviews zaidi  ya  milioni 4
Kama  una  tangazo, basi  wasiliana  nasi   sasa.

Email  yetu:  mpekuziblog@gmail.com
Simu:     +255682493833 ( Whatsapp ONLY)



Share:

Madaktari Waomba Vifaa vya Kujikinga na Corona.....Washauri Wagonjwa Wenye kisukari, shinikizo la damu, maumivu ya mgongo Wapewe Dawa za Muda Mrefu Kupunguza Msongamano

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), kimeiomba Serikali kurefusha matumizi ya dawa kwa wagonjwa wa kisukari, shinikizo la damu, maumivu ya mgongo na misuli ili kupunguza mrundikano wa wagonjwa katika hospitali ikiwa ni juhudi za kupambana na virusi vya Corona.

Akizungumza leo Alhamisi Apirli 02, jijini Dar es salaam Rais wa chama hicho, Dk. Elisha Osati amesema wagonjwa hao wanaweza kupewa dawa na kutumia kwa miezi mitatu.

“Tunaona kuwa wagonjwa wenye magonjwa kama hayo wana hatari zaidi kupata madhara ya virusi vya corona ndio maana tunapendekeza wapewe dawa za muda mrefu ili kuondoa msongamano wa wagonjwa.

“Tunaamini kuwa wagonjwa hao wakibaki nyumbani wanajikinga zaidi, utafiti mdogo tuliofanya unaonesha asilimia 70 ya wagonjwa hao huenda hospitali kwa marudio au kuchukua dawa,” amesema Dk. Osati.

Aidha ameiomba serikali kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kujikinga kwa wafanyakazi wa sekta ya afya.

“Tunaomba serikali na wadau wote wa afya nchini kuelewa na kutambua mchango wa watumishi wa sekta ya afya hivyo vitu kama mask N95 ni muhimu sana kwetu ukizingatia idadi ya wagonjwa wa Covid-19 inaongezeka siku hadi siku,”amesema.


Share:

Rais Wa Urusi Vladimir Putin 'Ajifungia Nyumbani' Kukabiliana na Corona

Rais wa Urusi Vladimir Putin kuanzia sasa atakuwa akifanya kazi akiwa nyumbani kwake huko Novo-Ogarevo, karibu na jiji la Moscow, msemaji wa Kremlin amesema siku moja baada ya daktari aliyekutana na rais Putin wiki iliyopita kukapatikana na virusi vya Corona.

Kiongozi wa Urusi anatarajiwa leo mchana kuongoza mkutano na wajumbe wa serikali yake kwa njia ya video, Dmitry Peskov amewaambia waandishi wa habari, akibaini kwamba Vladimir Putin, ambaye kwa mujibu wa Kremlin yuko katika afya njema, sasa ameamuwa kutumika akiwa nyumbani kwake.

"Kila mtu sasa anajitenga na wengine kutokana na hali inayojiri kwa sasa," Dmitry Peskov ameongeza.

Visa 2,777 vya maambukizi ya virusi vya Corona vimethibitishwa nchini Urusi ambapo watu 24 wamefariki dunia kwa ugonjwa huo ambao ulianzia nchini china mwezi Desemba mwaka 2019, kabla ya kusambaa katika zaidi ya nchi 200 kote ulimwenguni.

Katika kujaribu kukabiliana na kuenea kwa virusi vya Corona, hasa katika mji mkuu, ambao umekuwa kitovu cha janga nchini, siku ya Jumapili manispaa ya mji wa Moscow ilitangaza marufuku ya kutoka nje.

-RFI


Share:

Watu 884 Wafariki Kwa Virusi Vya Corona Nchini Marekani Ndani ya Masaa 24.....Idadi ya Vifo Yafika 5000

Zaidi ya watu 5,000 wamefariki dunia nchini Marekani kwa sababu ya janga la Corona, ambapo zaidi ya watu 215,000 nchini hump wameambukizwa virusi hivyo, Chuo Kikuu cha Johns-Hopkins kimetangaza, shirika la habari la AFP limeandika.

Hii ni baada ya watu 884   kuripotiwa kufariki dunia katika masaa 24, japo idadi hiyo ya Marekani ni ya chini ikilinganishwa na Italia na uhispania wakati huu maafa zaidi yakitrajiwa.

Wakati huo huo rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kwamba anatathmini juu ya uwezekano wa kusitisha safari za ndege za ndani katika miji ya Marekani iliyoathiriwa zaidi na janga la Covid-19 (Corona), ambalo linaweza kuua watu wasiopungua 100,000 nchini humo, kulingana na ripoti ya mamlaka ya afya ya nchini Marekani.

"Tunatatmini hili, lakini mara tu hatua kama hiyo itakapochukuliwa, tutakuwa tumefunga sekta ambayo ni muhimu sana," Rais wa Marekani amesema wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Ikulu ya White House.

Jumanne wiki hii Donald Trump alionya, siku mbili baada ya kuongeza hatua za kuangamiza janga la Corona hadi mwisho wa mwezi wa Aprili, kwamba wiki mbili "mbaya zaidi" zinatarajia kushuhudiwa nchini Marekani katika vita dhidi ya ugonjwa huo.


Share:

Serikali ya Uganda kuwapatia chakula wananchi milioni 1.5 Walioko Majumbani kutokana na virusi vya Corona

Waziri mkuu wa Uganda Bw. Ruhakana Rugunda amesema serikali ya Uganda itawapatia chakula watu maskini walioko mjini kuanzia Jumamosi wiki hii, ili kupambana na virusi vya Corona.

Bw. Rugunda amesema wizara ya mambo ya maafa itawapatia chakula watu wasiopungua milioni 1.5 walioko Kampala na Wakiso, ikiwa ni pamoja na wazee, wagonjwa, na madereva wa taxi, ambao kila mtu atapewa kilo 6 za unga wa mahindi, kilo 3 za maharagwe na chumvi. 

Zaidi ya hayo, akina mama wanaonyonyesha na wagonjwa watapewa kilogram 2 za maziwa ya unga na kilo 2 za sukari.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda Jumatatu wiki hii alitangaza kuwa serikali itawapatia chakula madereva na wale wanaopoteza kazi kutokana na hatua za kupambana na virusi vya Corona. 

Serikali ya Uganda imechukua hatua za mfululizo katika kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona, ikiwa ni pamoja na amri ya kutotembea usiku, kusimamisha usafiri binafsi na umma, kufunga mpaka wa nchi, na kupiga marufuku mikusanyiko yote ya watu.


Share:

Wasafiri 84 Wawekwa Karantini Tunduma

Katika kutekeleza maagizo ya serikali ya kuhakikisha wasafiri wote wanaotoka katika nchi zenye maambukizi Zaidi ya Virusi vya Corona wanatengwa, jumla ya wasafiri 84 kutoka Nchi ya Afrika Kusini wamewekwa karantini kwa muda wa siku 14 Katika halmashauri ya Mji wa Tunduma.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ameyasema hayo alipofanya ukaguzi wa maandalizi ya utayari wa kupambana na Ugonjwa wa Virusi vya Corona  kwa Mkoa wa Songwe hususani maeneo ya Mipakani yaani katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje na Halmashauri ya Mji wa Tunduma.

Brig. Jen. Mwangela amesema wasafiri hao ambao ni watanzania 55 na raia wengine kutoka Congo, Afrika Kusini, Kenya na Uganda walipoingia nchini kupitia mpaka wa Tunduma walipimwa na kukutwa hawana dalili za virusi vya Corona na kwakuwa wametoka katika nchi yenye maambukizi Zaidi wametengwa katika karantini.

Amesema utaratibu huo ni kwaajili ya kuwaaangalia ndani ya siku 14 kama watakuwa hawana dalili za Ugonjwa wa Virusi vya Corona wataruhusiwa kuendelea na safari zao.

Brig. Jen. Mwangela amewaagiza viongozi katika sekta mbalimbali kuendelea kutoa elimu ya namna ya kujikinga na Virusi vya Corona pia katika ofisi na taasisi zote usafi uzingatiwe huku suala la kunawa mikono kwa maji na sabuni liwekwe kipaumbele kila mahali.

Aidha ameliagiza jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe kufanya msako katika maeneno ya stendi za mabasi endapo kutakuwa na raia kutoka katika nchi zenye maambukizi Zaidi ya Virusi vya Corona na wamepitia njia zisizo rasmi waweze kuwekwa karantini.

Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe George Kyando amesema jeshi hilo limepiga marufuku kwa mabasi kujaza abiria kuliko uwezo wa gari, kutokuwa na vitakasa mikono kwenye mabasi au maji na sabuni kwa ajili ya kunawa na marufuku ya mabasi kuanza safari bila kupuliziwa dawa.

Amesema yeyote atakayepuuzia marufuku hizo ambazo zimelenga kuweka tahadhari ya kutosambaza ugonjwa wa Virusi vya Corona atakuwa anataka kusambaza ugonjwa kwa makusudi jambo ambalo ni kosa kisheria hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma Dkt Enock Mwambalaswa amesema wasafiri wote waliowekwa karantini wanapimwa mara mbili kwa siku ili kufuatilia maendeleo ya afya zao na endapo atatokea mwenye dalili za Virusi vya Corona hatua za haraka zitachukuliwa lakini hadi sasa wote wanaendelea vizuri na hakuna aliyebainika kuwa na viashiria vya ugonjwa huo.


Share:

Waziri Wa Kilimo Na Waziri Wa Viwanda Waongoza Kikao Kazi Kujadili Ufungamanishaji Wa Sekta Ya Kilimo Na Mikakati Ya Kutafuta Masoko

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo kadhalika, Wizara ya Viwanda na Bishara, na Taasisi za soko la Bidhaa Tanzania (TMX), Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) na Taasisi ya kuendeleza Kilimo Afrika (AGRA) wamekutana Jijini Dodoma kujadili kwa pamoja namna ambavyo Wizara hizo mbili zinaweza kuongeza mshikamano na weledi wa kiutendaji kwa ajili ya kufungamanisha uchumi wa Kilimo na Viwanda.

Katika kikao hicho kilichotuama katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo maarufu kama Kilimo IV kikiongoza na mawaziri kutoka pande mbili, Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) na Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Nashungwa (Mb) kwa pamoja wamesisitiza ulazima wa wataalamu hao kuunganisha nguvu kwa pamoja baina ya Wizara na Taasisi za umma na binafsi ili kuimarisha upatikanaji wa takwimu sahihi kuhusu Uzalishaji, uhifadhi, Ubora kwa Mazao ya kimkakati na mchanganyiko.

Akizungumza katika kikao hicho Waziri wa Kilimo Mhe Japhet hasunga (Mb) amewataka Wataalamu hao kuimarisha intelijensia ya masoko kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo na ufuatiliaji wa karibu wa mwenendo wa masoko ya Mazao na bidhaa ulimwenguni.

Hasunga amesema kuwa  pamoja na mikakati ya masoko lakini wataalamu hao wanaweza kujadili na kuona namna ya kuimarisha uhifadhi wa Mazao ya wakulima baada ya kuvuna kwani Barani Afrika nafaka myingi hupotea mara baada ya kuvuna.

Amewataka wataalamu hao pamoja na mambo mengine amewataka kuhakikisha kuwa wanaimarisha miundombinu ya masoko ikiwemo maghala ya kisasa ya kuhifadhia Mazao na bidhaa.

Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Innocent Bashungwa (Mb) amesema kuwa intelijensia ya masoko inapaswa kuhakikisha kwa haraka inatumia Balozi za Tanzania nje ya nchi katika kutafuta fursa za masoko ya Mazao  na bidhaa pamoja na kuanzisha madawati ya biashara (Trade/Commercial attache) Kwenye balozi hizo.

Pia amesema mpango mkakati wa kuwaunganisha wakulima na wasindikaji ndani na nje ya nchi ni muhimu kutekeleza haraka iwezekanavyo ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo zaidi katika kuongeza Uzalishaji wenye tija ili kukidhi nahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. 

Kadhalika Waziri Bashungwa ameongeza kuwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) wanapaswa kukutana na Shirika la Chakula Duniani (WFP) kujadili uimarishaji wa masoko ya Mazao mbalimbali.

Pamoja na mambo mengine Waziri Bashungwa ameitaka Taasisi ya kuendeleza Kilimo Barani Afrika (AGRA) kushirikiana na wadau wengine wa sekta ya Kilimo ili kutafuta ufunguzi wa namna ya kuimarisha masoko ya Mazao ya wakulima nchini.

MWISHO



Share:

Taarifa Ya Upotoshaji Inayosambaa Kwenye Mitandao Ya Kijamii Dhidi Ya Waziri Wa Mambo Ya Ndani Ya Nchi George B. Simbachawene




Share:

FULL POWER , ZATI 50 SULUHISHO LA KUDUMU NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi April 2





















Share:

Wednesday 1 April 2020

LIVE: Waziri Mkuu Akihutubia Bungeni

LIVE:  Waziri Mkuu Akihutubia Bungeni


Share:

Marekani Yasema Huenda Watu 240,000 Wakafariki Kwa Corona Nchini Humo...Trump Atangaza Hali Ngumu Zaidi Wiki Mbili Zijazo

Rais Donald Trump wa Marekani jana amesema nchi hiyo inakumbwa na changomoto kubwa zaidi kihistoria, na wiki mbili zijazo zitakuwa kipindi kigumu zaidi kwa nchi yake, na kusisitiza kuwa kufuata pendekezo la kujikinga na virusi vya Corona kunahusiana na uhai wa watu.

Mtaratibu wa Ikulu ya Marekani anayeshughulikia mambo ya kupambana na virusi vya Corona Bibi Deborah Birx amewaambia wanahabari kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya hali ya virusi vya Corona nchini humo. 

Makadirio yaliyotolewa naye yanaonyesha kuwa idadi ya vifo vya watu kutokana na virusi hivyo inaweza kufikia 100,000 hadi 2,40,000 chini ya hatua za udhibiti, na idadi hiyo ingefikia milioni 1.5 hadi milioni 2.2 bila ya kuchukua hatua hizo.

Ripoti iliyotolewa na Chuo cha udaktari katika Chuo Kikuu cha Washington imetabiri kuwa, hali mbaya zaidi ya kuenea kwa virusi vya Corona itatokea katika mwezi huu nchini humo, na itaendelea hadi mwezi Juni, na huenda ikatokea tena katika majira ya mpukutiko na majira ya baridi mwaka huu.

Kufikia sasa, janga la corona limesababisha zaidi ya vifo 3500 nchini humo na maambukizi ya zaidi ya watu 170,000.

Source:DW, CRI


Share:

Ndege ya Urusi Yaelekea Marekani Na Vifaa vya Kukabiliana Na Virusi Vya Corona

Wizara ya afya nchini Urusi imesema leo kuwa ndege ya nchi hiyo iliyobeba vifaa vya tiba imeondoka nchini humo kuelekea Marekani, huku ikulu ya Kremlini ikitanua ushawishi wake wakati huu wa janga la virusi vya corona.

Video iliyotolewa na wizara hiyo, ilionyesha ndege hiyo ya mizigo iliyobeba masanduku ikijiandaa kuondoka katika uwanja wa ndege wa kijeshi wa Moscow mapema leo. 

Kwa mujibu wa shirika la habari la Ufaransa la AFP, wizara hiyo ilikataa kutoa habari zaidi kuhusu hatua hiyo inayokuja baada ya rais wa Urusi Vladmir Putin kuzungumza na mwenzake wa Marekani Donald Trump siku ya Jumatatu. 

Awali Urusi ilituma vifaa vya matibabu na watalaamu wa virusi vya corona katika taifa la Italia lililoathirika pakubwa kutokana na virusi hivyo kama sehemu ya juhudi zake za kibinadamu ambazo wachambuzi wanasema zimebeba ushawishi mkubwa wa kijiografia na kisiasa.

-DW


Share:

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi kufuatia kifo cha Mtangazi wa TBC, Marin Hassan

“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko taarifa za kifo cha ghafla cha mtangazaji maarufu na mahiri Ndg. Marin Hassan kilichotokea leo asubuhi Jijini Dar es Salaam. Marin Hassan aliipenda kazi yake ya uandishi wa habari, aliifanya kwa weledi wa hali ya juu, alikuwa mzalendo wa kweli na alidhamiria kuitumikia nchi yake kupitia chombo cha habari cha Taifa (TBC) kwa nguvu na juhudi zake zote”.

Hii ni sehemu ya salamu za rambirambi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alizozitoa kufuatia kifo cha Mwandishi wa Habari Mwandamizi na mtangazaji maarufu wa Shirika la Utangazji Tanzania (TBC) Bw. Marin Hassan Marin kilichotokea leo asubuhi tarehe 01 Aprili, 2020 katika Hospitali ya Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Katika salamu hizo, Mhe. Rais Magufuli ametoa pole kwa familia ya Marin Hassan, Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayub Rioba, Wafanyakazi wote wa TBC, Waandishi wa Habari wote na wote walioguswa na kifo cha mwanahabari huyo nguli hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli amesema alimfahamu Marin Hassan kama mtu aliyetoa mchango mkubwa katika ustawi wa Uandishi wa Habari nchini Tanzania na kwa juhudi zake kubwa ndani ya TBC ambapo aliliripoti habari kwa ubunifu na mvuto wa hali ya juu, alibuni na kufanya vipindi vilivyopendwa na Watanzania ikiwemo vipindi vya Uchaguzi Mkuu, Safari ya Dodoma na mabadiliko makubwa yaliyoanza juzi ambapo TBC inatangaza habari zake kupitia ARIDHIO.

“Marin Hassan ameondoka wakati ambapo tunamhitaji zaidi, Marin Hassan ni shujaa wa habari Tanzania, aliipenda sana TBC na nchi yake Tanzania. Naungana na familia yake, TBC na Waandishi wa Habari wote kumuombea apumzike mahali pema peponi, Amina” amesema Mhe. Rais Magufuli. Inna Lillahi wa inna ilayhi raji’un

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato
01 Aprili, 2020


Share:

Mtoto wa Hayati Edward Moringe Sokoine Azikwa, Mamia Wamsindikiza

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo ameongoza watumishi wa Ofisi yake katika mazishi ya Alazaro Sokoine ambaye ni mtoto Mkubwa wa Hayati Edward Moringe Sokoine. Mazishi hayo yamefanyika jana Monduli Juu Mkoani Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, ndugu, jamaa na Marafiki.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (kushoto) akiweka shada la maua pamoja wanafamilia katika kaburi la kaka yake mkubwa Alazaro Sokoine. Mazishi yamefanyika jana Monduli Mkoani Arusha.
Mkurugenzi wa Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu Bi. Emma Lyimo akitoa heshima za mwisho katika ibaada ya kuaga mwili wa Alazaro Sokoine ambae ni mtoto mkubwa wa Hayati Edward Moringe Sokoine. Mazishi yamefanyika jana Monduli Mkoani Arusha.
Wakuu wa Mikoa ya Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka, Morogogo – Mhe. Loata Sanare, Tanga – Mhe. Martine Shigela na Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakiweka shada la maua katika kaburi la Alazaro Sokoine, Monduli Mkoani Arusha.


Share:

CORONA YASAMBAA KATIKA NCHI 50 AFRIKA

Kituo cha udhibiti na kuzuia magonjwa vya Umoja wa Afrika kimesema kuwa watu 172 wamepoteza maisha baada ya kuambukizwa virusi vya Covid-19 barani Afrika.

Ugonjwa wa corona umeenea katika nchi 50 barani. Kwa ujumla, watu 5,413 wameambukizwa.

Mpaka sasa hakuna taarifa zozote za maambukizi nchini Lesotho, Sudani Kusini, visiwa Sao Tome na Principe, comoro na Malawi.

Hapo jana eno lililojitangazia uhuru wake Somaliland lilithibitisha kuwepo na maambukizi ya watu wawili. Redio Kulmiye imesema mmoja kati ya walioambukizwa ni raia wa China aliyekuwa akiishi katika mji wa Berbera. Mwingine ni raia wa Somalia ambaye hivi karibuni alirejea kutoka nchini Uingereza.

Somaliland imesambaza vikosi vyake mitaani na kupiga marufuku utafunaji wa mirungi mitaani kuepuka kusambaa kwa virusi.

Afrika Kusini ina idadi kubwa ya maambukizi,ikiwa imefikia 1,353, watu saba wakiwa wamepoteza maisha.

Watu 11 wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya corona tangu jana nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo na kufanya idadi ya walioambukizwa kufikia 109 na vifo vinane.

Wangojwa wa tatu hadi sasa wameripotiwa kupona lakini mgojwa wa kwanza hadi sasa yungali hospitalini , serikali haijamruhusu kurejea nyumbani kwake.

Mashirika ya kiraia yamelaani serikali kupuuza kufuatilia kwa karibu utelekezaji wa maagizo ya kuepusha kuenea kwa virusi nchini.

Wiki jana, serikali ilitangaza kusitisha hatua yake ya kuzuia raia wa kinshasa kutoka nyumbani.

Miongoni mwa maagizo , Rais Felix Tshisekedi aliomba viongozi wa mitaa kuweka maji na sabuni barabarani,lakini hadi sasa vifaa hivyo vya kiafya bado havijasambazwa katika mitaa ya Kinshasa.
 CHANZO - BBC
Share:

KARIBU NNIENET LINGEIRIES STORE SHINYANGA MJINI KWA NGUO ZA NDANI 'UNDER WEAR'

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger