Thursday 23 January 2020

GST Yaibua Maeneo Mapya Utalii Wa Jiolojia.....Kamati yataka Sheria ya MRI kuharakishwa

Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imewezesha kuibuliwa maeneo Mapya ya Utalii wa Jiolojia kufuatia kukamilika kwa utafiti wa Jiolojia katika maeneo ya ramani  Nne (4) za Jiolojia  (QDS 38,39,52 na 53).

Hayo yameleezwa na Mtendaji Mkuu wa GST  Dkt. Mussa Budeba wakati akiwasilisha taarifa  kuhusu Utekelezaji na Hali ya upatikanaji wa fedha za maendeleo kwa taasisi hiyo kwa kipindi cha Nusu Mwaka  kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.

Dkt. Budeba ameeleza kuwa, GST ilifanya utafiti huo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro na kuongeza kuwa, suala hilo limeongeza vituo vya utalii wa Jiolojia nchini.

Akizungumzia huduma za  maabara ya GST kwa wadau wa sekta ya madini, kilimo na ujenzi amesema kuwa, baada ya kufanya maboresho  mbalimbali ikiwemo ununuzi wa baadhi ya vifaa vya kisasa, kuboresha mifumo ya uendeshaji wa maabara na kutoa mafunzo kwa watumishi, GST iliweza kupata ITHIBATIya kimataifa ya uchunguzi wa sampuli za dhahabu kwa njia ya tanuru kutoka shirika la SADCAS.

Aidha, akizungumzia mafanikio ya taasisi hiyo ameyataja kuwa ni pamoja na kushiriki katika mashindano ya kuchakata visawe vya mbali (Remote Sensing) yaliyofanyika nchini Botswana na kushinda nafasi ya Nne ambapo mwakilishi mmoja kutoka GST alitunukiwa Cheti cha kuwa mkufunzi kwa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Dkt. Budeba ameyataja mafanikio mengine ni kuweza kukusanya na kuhakiki jumla ya taarifa 109 kutoka kwenye kampuni mbalimbali za utafiti na uchimbaji wa madini pamoja na kukamilisha kazi ya ugani wa jiolojia na jiokemia katika QDS 293 iliyopo katika maeneo ya wilaya ya Nachingwea na Ruangwa mkoani Lindi.

Akizungumzia tukio lililosadikiwa kuwa ni volcano lililotokea katika Kata ya Ndembezi Manispaa ya Mji wa Shinyanga, ameieleza kamati kuwa, uchunguzi uliofanywa na GST ulibaini kwamba kulikuwa na tope lililochanganyika na maji likiwa linabubujika kutoka ardhini na kutengeneza rundo kubwa la tope la udongo juu ya uso wa ardhi mfano wa kichuguu na kwamba tukio hilo kwa lugha ya kigeni hujulikana kama " liquefaction".

‘’Mheshimiwa Mwenyekiti matukio haya ni ya kawaida kutokea katika maeneo ambayo ni tambarare, yenye kiasi kingi cha maji ardhini na pindi pakitokea msukumo ama mgandamizo katika  matabaka ya miamba ardhini, husababisha chembechembe za udongo kuchanganyika na maji na kusababisha tope ambalo husukumwa kuja juu ya  uso wa ardhi ambapo tukio hilo hutokea,’’ amesema Dkt. Budeba.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Dustan Kitandula akizungumza katika kikao hicho, ameitaka kuharakishwa suala la kuandaliwa Sheria ya Chuo cha Madini kutokana na umuhimu wa chuo hicho kuzalisha wataalam wa sekta ya madini na kutaka zifanyike jitihada mahusus kukamilishwa suala hilo. Mwenyekiti Kitandula ametoa msisitizo baada ya wajumbe wa kamati hiyo kutaka suala hilo kukamilishwa haraka.

Pia, Mwenyekiti na wajumbe wa kamati hiyo wameishauri wizara kupitia chuo hicho kuangalia namna ya kuzalisha wataalam zaidi na ambao watakuwa na uwezo wa kujiajiri wenyewe bila kutegemea ajira ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kushiriki katika shughuli za madini hususan kwenye uchimbaji.

‘’ Najua hili si jambo la leo lakini ni vizuri kama wizara mkaanza kulitafakari,’’ amesema Mwenyekiti, Kitandula.

Awali, akitoa taarifa kwa Kamati, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Madini Emmanuel Kapira ameieleza kuwa, tayari Rasimu ya Sheria ya kuanzishwa kwa Chuo cha Madini imeandaliwa na kupelekwa katika Mamlaka husika kwa hatua zaidi.

Pia, Kapira ameieleza kamati hiyo kuwa, katika kuwasaidia wachimbaji wadogo kupata mafunzo yanayotolewa chuoni hapo, kimetengeneza mfumo wa kufundisha kwa lugha ya Kiswahili kwa waajiriwa na wachimbaji.

Naye, Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo amesema ipo haja ya wadau wa madini kujifunza elimu ya biashara ya madini  kwa kuzingatia fursa zilizopo katika sekta hiyo na kuongeza kuwa, suala  hilo linatoa nafasi nzuri  ya kibiashara na uwekezaji kupitia sekta ya madini . Aidha, Naibu Waziri Nyongo ameishukuru kamati hiyo kwa kuendelea kuishauri wizara ili iweze kusimamia vema sekta ya madini.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila akitolea ufafanuzi suala la maabara ya GST baada ya kupata ITHIBATI ya Kimataifa, amewaomba wajumbe wa kamati hiyo kusaidia kutoa elimu kwa wadau  wa madini katika maeneo yao ili waweze kutumia maabara hiyo ikizingatiwa kuwa  gharama zake ni nafuu na ina viwango vya kimataifa.

Akizungumzia suala la Chuo cha Madini kulelewa na Chuo Kikuu cha Dar es salaam, amesema pamoja na mambo mengine ni kukiwezesha kuwa bora zaidi na kuendesha programu zinazoendana na soko la ajira.

 Vikao kati ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Wizara ya Madini vilivyoanza Januari 20, vimehitimishwa leo Januari 22, 2020.

Chanzo: Wizara ya Madini



Share:

PLANT INSPECTOR II – 1 POST | Occupational Safety and Health Authority (OSHA)

POST PLANT INSPECTOR II – 1 POST POST CATEGORY(S) ENGINEERING AND CONSTRUCTION EMPLOYER Occupational Safety and Health Authority (OSHA) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-22 2020-02-05 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Carry out work place inspections and keep records; ii. Conduct plant safety risk assessment; iii. Compile and prepare monthly and annual reports; iv. Planning and implementing specific plant… Read More »

The post PLANT INSPECTOR II – 1 POST | Occupational Safety and Health Authority (OSHA) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wanafunzi 900 Wa Kidato Cha Tano Na Sita Mkoani Tabora Wapigwa Msasa Kuhusu Sekta Ya Angaa Na TCAA

NA TIGANYA VINCENT
JUMLA ya wanafunzi 900 wa Kidato cha Tano na Sita mchepuo wa Sayansi katika shule za sekondari tatu za Mkoani Tabora wamepewa elimu juu ya kujiunga na sekta ya usafiri wa Anga pindi watakapoliza shahada zao za vyuo vikuu katika fani za Sayansi.

Mafunzo hayo ya siku moja yamehusisha wanafunzi 500 wa Shule ya Sekondari ya Milambo, 200 WA Tabora Wavulana  na 200  wa Tabora wasichana.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Tabora mara baada ya mafunzo hayo, Afisa Habari wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini(TCAA)  Bestina Magutu alisema lengo la elimu hiyo ni kuwasaidia wanafunzi wanasoma masomo ya sayansi kuwa na uelewa mpana na kuchangamkia fursa ya masomo yanayohusu sekta ya anga.

Alisema lengo jingine ni kuwahamasisha ili waanze kujiandaa kwa ajili kusomea fani mbalimbali za sekta ya anga kama vile urubani , uongozaji ndege, ufundi wa ndege , usimamizi wa usalama wa usafiri wa anga na huduma kwa wateja.

Kwa upande wa Mkufunzi kutoka Chuo cha Usafiri wa Anga Thamarat Salim alisema sekta ya usafiri wa Anga hapa nchini inakuwa kwa kasi ni vema wanafunzi wanasoma masomo ya sayansi wakachangamkia fursa hiyo kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kuelekea uchumi wa Kati.

Alisema kozi nyingi za sekta ya usafiri wa anga zinamtaka mwanafunzi anayetaka kusomea kozi hizo ni vema awe amesoma masomo ya sayansi.

Naye Mwalimu kutoka Shule ya Sekondari ya Milambo Euphrahim Daffa alisema mafunzo yanayotolewa na TCAA kwa wanafunzi wanachukua masomo ya sayansi yamesaidia kuwaelimu sio tu wanafunzi hata walimu ya kujua kuwa hata wanafunzi anayechukua Fizikia ,Kemia na  Bioloji ( PCB) anaweza kujiunga na kozi za sekta ya anga.

Alisema hatua imesaidia kuwafumbua macho na kutambua kuwa kusoma PCB sio tu atasomea masomo ya sekta ya afya na  kilimo au walimu pekee yake bali  hata sekta ya anga wanayofursa.

Meneja wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga  nchini Mkoa wa Tabora Daniel Nyimbo alitoa wito kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kuchangamkia fursa ya masomo hayo usafiri wa anga pindi zinapotangazwa katika vyombo vya habari mbalimbali hapa nchini.

Alisema kumekuwepo na fursa za kupata ufadhili wa kusomeshwa na TCAA kupitia kufanya usahili na pindi wanaposhindwa kusomeshwa kwenye kozi mbalimbali na kusema kuwa wanapoona hivyo wameombe.

TCAA inaendelea na utoaji wa elimu ya sekta ya anga kwa ajili ya kuwahamasisha wanafunzi wengi kusoma masomo ya sayansi kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano ya ujenzi wa Kati ambao msingi wake mkubwa ni viwanda.

MWISHO


Share:

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara Laendelea Kuusaka Mwili wa Mtoto Aliyesombwa na Maji kwa Siku Tatu sasa

Na John Walter-Babati
Mwili wa Mwanafunzi wa kiume (10) aliekuwa akisoma darasa la nne katika shule ya Msingi Darajani iliopo Mjini Babati mkoani Manyara  anaesadikiwa kusombwa na maji wakati akiogelea kwenye mto eneo linalojulikana kama  Darajani  unaotiririsha Maji kuelekea Ziwa Manyara bado haujapatikana kwa siku ya tatu sasa.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara, Kamishna msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Julishaeli Mfinanga, amewataka wananchi wawe watulivu katika kipindi wanachoendelea na utafutaji.

Amesema mwelekeo wa kumpata mtoto huyo upo kwa sababu tabia ya maji huwa baada ya mtu kuzama kwenye kina kirefu cha  maji baada ya siku tatu humuibua juu na kumtupa kando ya mto.

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mji wa Babati,Viongozi wa serikali na Siasa wamejitokeza kwa wingi kusaidiana na vyombo vya ulinzi na Usalama katika kufanikisha zoezi la kuupata mwili wa mtoto huyo.

Hata hivyo  baaadhi ya wananchi wakizungumza na kituo hiki, wamesema kuwa kwa kipindi hiki cha mvua mto huu huwa unafurika maji mengi ambayo yana kasi kubwa, hivyo tahadhari inahitajika kwa wanaovuka katika eneo la mto huo pamoja na kuwa makini na watoto.

Mtoto huyo alisombwa na maji jumatatu Januari 20  majira ya saa saba mchana wakati wakiwa wanaogelea yeye na wenzake ambao walinusurika.


Share:

LIQUORER GRADE II – 1 POST – Tanzania Coffee Board

POST LIQUORER GRADE II – 1 POST POST CATEGORY(S) RESEARCH,SCIENCE AND BIOTECH EMPLOYER Tanzania Coffee Board APPLICATION TIMELINE: 2020-01-22 2020-02-05 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Carries out coffee roasting outturns and pre-auction cupping preparations; ii. Safe keeps and updates liquoring files of catalogues; iii. Assists in writing bulking instructions and dispatches them to factories; iv. Conducts… Read More »

The post LIQUORER GRADE II – 1 POST – Tanzania Coffee Board appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Zaidi ya mifuko mbadala 1400 isiyokuwa na viwango yakamatwa Njombe

Na Amiri kilagalila-Njombe
Baraza la taifa la hifadhi ya mazingira NEMC kanda ya nyanda za juu kusini wamefanya oparesheni mjini Njombe na kukamata vifungashio zaidi ya 1400 visivyokidhi ubora wa soko katika maduka mbalimbali ya wafanyabiashara.

Katika oparesheni hiyo mifuko mbadala ambayo haina nembo ya ubora TBS na maelezo ya ubora wa mfuko pamoja na mifuko ya plastiki inayotumika kufungashia nyama mabuchani,karanga na hata mahindi ya kukaangwa imekamatwa .

Baadhi ya wafanyabiashara waliokamatwa akiwemo Afla Sanga na Anitha Mgaya, wamekiri kufahamu kuwa wamekiuka sheria na wengine wamedai kuwa  hawajui chochote kwa kuwa wengine sio wamiliki wa maduka bali ni wafanyakazi.

“Kwa mimi elimu hiyo sikuwa nayo,kwasabau unajikuta umeenda kununua mfuko wa kifungashio unafika pale unachukuwa mfuko unaoonekana sokoni na kuja kuuza”alisema Afla Sanga

Kwa niaba ya afisa mtendaji wa mtaa wa kwivaha uliopo mjini Njombe mjumbe wa mtaa huo  bwana Willy Kiswaga anasema sheria zichukue mkondo wake kwa kuwa mifuko hiyo ilishapigwa marufuku.

Milton Mponda ni afisa mazingira kutoka NEMC  kanda ya nyanda za juu kusini amesema zoezi la kukamata na kutaifisha mifuko hiyo ni endelevu huku akitoa wito kwa wafanyabiashara kujiepusha na uuzaji wa vifungashio feki kwa kuwa faini yake ni jela miezi mitatu au faini ya kuanzia shilingi laki moja hadi laki tano kutegemeana na wingi wa mzigo.

“Mpaka sasa tumekamata pisi sio chini ya 1500,mingi tumekamata kwasababu haiikidhi viwango,na ile iliyokidhi tumeacha tumeacha waendelee ktumia na ndio inayoruhusiwa kisheria”alisema Milton Mponda

Mponda amesema mfuko mbadala ni lazima uwe na taarifa za mzalishaji pamoja na nembo ya TBS kwa maana ya kukidhi viwango vya TBS VSM 70 pamoja na kuonyesha uwezo wa mfuko kubeba mzigo


Share:

Waziri Mpina Aunda Timu Uchunguzi Ukwepaji Wa Kodi Kampuni Ya Ufugaji Samaki

NA MWANDISHI WETU, MAFIA
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameunda timu ya wataalamu kufanya uhakiki wa takwimu, mauzo, uzalishaji na uendeshaji wa Kampuni ya Alphakrust inayojishughulisha na uzalishaji wa samaki aina ya Kambamiti pamoja na uhalali wa mapato ya Serikali kufuati kuwepo udanganyifu kwenye biashara hiyo.

Kulingana na takwimu za mauzo ya Kambamiti nje ya nchi kampuni hiyo ilipaswa kulipa shilingi milioni 300 kama ushuru wa huduma kwa Halmashauri hiyo lakini imekuwa ikilipa shilingi milioni 100 kwa mwaka na hivyo kuipunja Serikali kiasi cha shilingi milioni 200 kila mwaka.

Waziri Mpina amebaini njama hiyo inayofanywa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kushirikiana na Mwekezaji wa Kampuni ya Alphakrust inayofuga samaki aina ya Kambamiti kisiwani humo kwa lengo la kuiibia Serikali mapato yake yanayotakiwa kutozwa kama ushuru wa huduma yaani ‘Service Levy’

Alisema Halmashauri ya Mafia imetengeza makadirio ya kutoza ushuru wa huduma ya shilingi milioni 9 kwa mwezi kutoka Kampuni ya Apha Krust na kuacha Kanuni maalumu iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya ukokotoaji wa mapato yanayopatikana ya kutakiwa kulipa asilimia 3 ya mapato yote yanayopatikana kwenye biashara husika.

Udanganyifu huo umebainika wakati wa ziara ya Waziri Mpina ya kukagua Kituo cha kutotoleshea vifaranga na Shamba la ufugaji samaki aina ya Kambamiti lilomilikiwa na Kampuni ya Alphakrust kisiwani Mafia.

Waziri Mpina katika ziara hiyo aliambatana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mafia ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaib Nnunduma, Wakurugenzi na Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mpina alihoji iweje Halmashauri ya Mafia itoze ushuru kinyume cha Sheria wakati kanuni za ukokotoaji wa mapato zinajulikana na hivyo kuamini kuwa huo ni mkakati wa siri uliosukwa baina ya Halmashauri ya Mafia na Kampuni ya Apha Krust kwa lengo la kukwepa kulipa mapato stahiki ya Serikali.

“Haiwezekani Halmashauri ya Mafia ikaacha kufuata fumula ya uchukuaji wa ‘service levy’ uliowekwa na Serikali na kutengeneza utaratibu wake yenyewe..mwisho wa siku watu wa nje tunachoweza kukielewa ni njama inayowekwa baina ya Halmashauri na Mwekezaji kuiibia Serikali” alisema Mpina.

“Kwanini mkokotoo huo usizingatie sheria takwimu za makusanyo zipo, bei inayotumika kuuza na masafirisho ya nje ipo kwanini haikutumika kukokotoa..kwanini itumike fumula ya kukubalina nje ya utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria”alihoji Waziri Mpina.

Waziri Mpina alisema kama halmashauri inatoza fedha nyingi zaidi za ushuru wa huduma tofauti na iliyowekwa kwenye Sheria ni makosa kwani Serikali haiwezi ikatoza fedha ambazo haziko kwenye utaratibu wa sheria lakini kama halmashauri inakusanya fedha kidogo kuliko sheria inavyosema nalo ni kosa kwa mujibu wa sheria.

“Kwanini uchukue fedha kidogo wakati fomula ya kupata makusanyo halisi kwa niaba ya wananchi ipo..kwanini wewe utumie fumula ya kwako ya kubuni wewe wakati fumula ya kisheria ipo”alihoji Waziri Mpina.

Mbali na dosari hizo za ukwepaji kodi, Waziri Mpina alielezea kusikitishwa kwake na kitendo cha mwekezaji huyo kushindwa kuwashirikisha wananchi wanaozunguka eneo hilo kujifunza teknolojia hiyo ili kukuza sekta ya ukuzaji viumbe maji hasa ufugaji wa Kambamiti.

Alisema Serikali haijapokea maombi yoyote ya upungufu wa wataalamu wenye utaalamu na uzoefu maalum kuendesha mradi kwani wataalamu hao wanazalishwa katika vyuo vyetu kikiwemo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Vyuo vya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA).

“Mradi huu unaendeshwa kwa usiri na wivu mkubwa kiasi kwamba wananchi wa kawaida hawawezi kupata utaalamu kupitia mradi huu..kwenye taarifa yenu sikuona mkichukua vijana wanaomaliza vyuo au kuingia makubaliano na vyuo (MOU) kufanya mafunzo ya vitendo kwenye mradi huu na kuwalipa kima cha chini cha mshahara”alihoji Waziri Mpina.

Alisema wawekezaji kutoka nje wanapofika nchini wanalojukumu katika mikataba yao ya kusambaza taaluma katika eneo lao la uwekezaji ili kuwawezesha watanzania wengi kunufaika na uwekezaji wao na kueleza kusikitishwa kwake na kampuni hiyo kuwabagua wazawa na kuwapa nafasi wageni hata kwenye kazi ambazo zingeweza kufanywa na watanzania.

“Toka nimeanza kutembelea miradi hii kuanzia Dar es Salaam nimekuja kwenye shamba la kambamiti na kituo cha kutotoleshea vifaranga mapokezi na utolewaji wa maelezo na ufafanuzi unafanywa na wageni hii ni ishara kwamba uongozi wote umeundwa na wageni au ni sehemu ya kuficha ukweli juu ya undeshaji wa biashara hiyo’ alihoji Waziri Mpina

Mbali na hilo Waziri Mpina alisema Serikali inazo taarifa za vijana wanaokwenda kufanya kazi kwenye uwekezaji huo wanashindwa kufanya kazi kutokana na ujira mdogo wanaolipwa na mwekezaji huyo na kuvunjika moyo na kisha kuondoka.

“Kulipwa mshahara mdogo haijulikani wanalipwa hivyo ili wakate tamaa waondoke na baadae itengeneze nafasi ya ajira kutoka nje ya nchi au tatizo ni nini”alihoji Waziri Mpina.

Kwa upande wake Meneja wa Alphakrust, Ganeshan Vedagiri amelalamikia kukosa wataalamu wenye weledi na pindi watanzania wanapoajiriwa wanakaa muda mfupi na kuondoka huku akilalamikia kudaiwa ushuru kwenye halmashauri zaidi ya moja

Alisema mradi huo wa Mafia una mabwawa 31 ya Kambamiti ambapo kwa mwaka huzalisha wastani wa tani 400 huku asilimia 90 ya samaki hao wakiuzwa nchini ufaransa huku asilimia 10 zikiuzwa hapa nchini. 
 
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafia, Chuchu Silvery licha ya kuwepo kwenye ziara hiyo hakuweza kuzungumzia chochote kuhusiana na dosari hizo.


Share:

Serikali Kuipatia Bilioni Mbili Kcmc Kwa Ajili Ya Jengo La Mionzi

Na. Catherine Sungura-Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeahidi kuipatia kiasi cha shilingi bilioni mbili hospitali ya rufaa ya kanda KCMC ili kuweza kutoa huduma za tiba za mionzi hospitalini hapo.
 
Hayo yamesemwa jana  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akijibu maswali kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii jijini hapo.
 
“Tumekubaliana na Katibu Mkuu kuitafuta hiyo bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa jengo la mionzi (bunker) kwa hospitali hii tutawapatia”.
 
Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa wizara yake inayo muelekeo kwa hospitali zote za rufaa za kanda kutoa huduma za mionzi hivyo hakutakuwa na haja ya wagonjwa wa kanda ya kaskazini kusafiri hadi Ocean road kupata huduma za mionzi.
 
“Wizara tumeanza kutoa huduma za mionzi,mwaka jana tulizindua hospitali ya Bugando,lengo letu ni kuweka huduma hizi kwenye hospitali zote za rufaa za kanda kama Mbeya  na tunafikiria kuweka na hapa kwenye hosputali ya Benjamin Mkapa”.Alisisitiza Waziri Ummy
 
Hata hivyo Waziri Ummy  amesema wizara imeweza kuwapatia hospitali ya KCMC fedha kwa ajili ya watumishi pamoja na dawa kiasi cha shilingi bilioni 5 katika kipindi cha miezi sita.”Kama serikali itaendelea kuthamini suala la ubia katika utoaji wa huduma za afya na mashirika ya dini na watu binafsi”.
 
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa KCMC Dkt. Gilliard Masenga amesema kuwa asilimia sitini ya wagonjwa wa saratani wanahitaji huduma ya mionzi na hospitali  hiyo imeweza kuona jumla ya wagonjwa 4323 kwa kipindi cha mwaka jana na kufanya uchunguzi wa magonjwa ya saratani ambapo kati yao watoto 239 na watu wazima ni 4084,aidha wamefanya kampeni maalum ya upimaji na ushauri katika wilaya ya Arumeru na watu 307 walipatiwa huduma ya uchunguzi wa awali wa saratani


Share:

TUTORIAL ASSISTANT – 3 POST – Dar es Salaam Maritime Institute (DMI)

POST TUTORIAL ASSISTANT – 3 POST POST CATEGORY(S) TRANSPORT AND LOGISTICS WATER, MINING AND NATURAL RESOURCES EMPLOYER Dar es Salaam Maritime Institute (DMI) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-22 2020-02-05 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i.Teach up to NTA level 6 (Ordinary Diploma); ii.Assist in conducting tutorial, seminars and practical exercises for students under close supervision; iii.Prepare learning resources for… Read More »

The post TUTORIAL ASSISTANT – 3 POST – Dar es Salaam Maritime Institute (DMI) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

QUAULITY ASSURANCE OFFICER III – 15 POST AT NHIF

POST QUAULITY ASSURANCE OFFICER III – 15 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-22 2020-02-05 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i.Conduct inspection and supportive supervisions of health facilities; ii.Deals with verification and checking of prescriptions; iii.Makes researches or market surveys with a view to establishing the… Read More »

The post QUAULITY ASSURANCE OFFICER III – 15 POST AT NHIF appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) Jobs | CBE, SUA, OSHA, TCB, KCMC,ISW ,TBC, EASTC, MUHAS,NHIF , (IFM

VACANCIES ANNOUNCEMENT Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) on behalf of Sokoine University of Agriculture (SUA), College of Business Education (CBE), Occupational Safety and Health Authority (OSHA), Tanzania Coffee Board (TCB), Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC), Institute of Social Work (ISW) and Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) East Africa Statistical Training Centre (EASTC), Muhimbili University of Health and Allied Sciences… Read More »

The post Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) Jobs | CBE, SUA, OSHA, TCB, KCMC,ISW ,TBC, EASTC, MUHAS,NHIF , (IFM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi January 23

















Share:

Wednesday 22 January 2020

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania, na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC)




Share:

T-MARC TANZANIA YATOA MSAADA WA DIAPERS ZA SMILEY HOSPITALI YA MWANANYAMALA, DAR ES SALAAM

Mmoja wa wanawake waliojifungua katika hospitali ya Mwananyamala, Rebecca Nelson akifurahia Diapers mpya za Smiley baada ya kukabidhiwa na balozi wa bidhaa hizo za T-MARC Tanzania, Dinah Marrios (kushoto),wengine pichani ni watumishi waandamizi wa hospitali hiyo na kutoka taasisi yak T-MARC.

Mkurugenzi wa bidhaa za kijamii wa T-MARC Tanzania , Flavian Ngole, (kulia) akikabidhi msaada wa diapers mpya za Smiley zilizozinduliwa katika soko nchini karibuni na T-MARC, kwa mzazi, Rebecca Nelson, katika wodi ya wazazi ya hospitali ya Mwananyamala jijiji Dar es Salaam, wakati wa hafla ya taasisi hiyo kukabidhi msaada wa bidhaa hizo hospitalini hapo , (katikati) ni Balozi wa Smiley , Dinah Marrios, wengine (kutoka kushoto) ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo , Dk.Mussa Wambura na Muuguzi Rosa Moses.
Wauguzi Waandamizi wa hospitali ya Mwananyamala wakipokea msaada wa Diapers za Smiley zlizozinduliwa hivi karibuni kutoka kwa Mkurugenzi wa bidhaa za kijamii wa T-MARC Tanzania, Flavian Ngole (kushoto) na balozi wa bidhaa hizo, Dinah Marrios.
Share:

WAZIRI MPINA AUNDA TIMU UCHUNGUZI UKWEPAJI WA KODI KAMPUNI YA UFUGAJI SAMAKI AINA KAMBAMITI



WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (katikati) akiangalia namna vifaranga vya samaki aina ya Kambamiti vinavyozalishwa na Kampuni ya Aphakrust alipofanya ziara kukagua uzalishaji wa kampuni hiyo kisiwani Mafia. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ganeshan Vedagiri na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Sera na Mipango Wizara ya Mifugo na Uvuvi, James Mganga. Picha na Mpiga Picha Wetu.


WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akivua samaki aina Kambamiti alipotembelea mabwawa ya Kampuni ya Aphakrust kisiwani Mafia. Kwenda kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ganeshan Vedagiri na Mkurugenzi Ukuzaji Viumbemaji, Dk. Nazael Madala na Mkurugenzi wa Uvuvi, Magese Bulayi. Picha na Mpiga Picha Wetu.
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Alphakrust, Ganeshan Vedagiri (katikati) alipotembelea mabwawa ya ufugaji kambamiti kisiwani Mafia mwingine Mkurugenzi Ukuzaji Viumbemaji, Dk. Nazael Madala. Picha na Mpiga Picha Wetu.



NA MWANDISHI WETU, MAFIA


WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameunda timu ya wataalamu kufanya uhakiki wa takwimu, mauzo, uzalishaji na uendeshaji wa Kampuni ya Alphakrust inayojishughulisha na uzalishaji wa samaki aina ya Kambamiti pamoja na uhalali wa mapato ya Serikali kufuati kuwepo udanganyifu kwenye biashara hiyo.

Kulingana na takwimu za mauzo ya Kambamiti nje ya nchi kampuni hiyo ilipaswa kulipa shilingi milioni 300 kama ushuru wa huduma kwa Halmashauri hiyo lakini imekuwa ikilipa shilingi milioni 100 kwa mwaka na hivyo kuipunja Serikali kiasi cha shilingi milioni 200 kila mwaka.

Waziri Mpina amebaini njama hiyo inayofanywa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kushirikiana na Mwekezaji wa Kampuni ya Alphakrust inayofuga samaki aina ya Kambamiti kisiwani humo kwa lengo la kuiibia Serikali mapato yake yanayotakiwa kutozwa kama ushuru wa huduma yaani ‘Service Levy’

Alisema Halmashauri ya Mafia imetengeza makadirio ya kutoza ushuru wa huduma ya shilingi milioni 9 kwa mwezi kutoka Kampuni ya Apha Krust na kuacha Kanuni maalumu iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya ukokotoaji wa mapato yanayopatikana ya kutakiwa kulipa asilimia 3 ya mapato yote yanayopatikana kwenye biashara husika.

Udanganyifu huo umebainika wakati wa ziara ya Waziri Mpina ya kukagua Kituo cha kutotoleshea vifaranga na Shamba la ufugaji samaki aina ya Kambamiti lilomilikiwa na Kampuni ya Alphakrust kisiwani Mafia.

Waziri Mpina katika ziara hiyo aliambatana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mafia ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaib Nnunduma, Wakurugenzi na Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mpina alihoji iweje Halmashauri ya Mafia itoze ushuru kinyume cha Sheria wakati kanuni za ukokotoaji wa mapato zinajulikana na hivyo kuamini kuwa huo ni mkakati wa siri uliosukwa baina ya Halmashauri ya Mafia na Kampuni ya Apha Krust kwa lengo la kukwepa kulipa mapato stahiki ya Serikali.

“Haiwezekani Halmashauri ya Mafia ikaacha kufuata fumula ya uchukuaji wa ‘service levy’ uliowekwa na Serikali na kutengeneza utaratibu wake yenyewe..mwisho wa siku watu wa nje tunachoweza kukielewa ni njama inayowekwa baina ya Halmashauri na Mwekezaji kuiibia Serikali” alisema Mpina.

“Kwanini mkokotoo huo usizingatie sheria takwimu za makusanyo zipo, bei inayotumika kuuza na masafirisho ya nje ipo kwanini haikutumika kukokotoa..kwanini itumike fumula ya kukubalina nje ya utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria”alihoji Waziri Mpina.

Waziri Mpina alisema kama halmashauri inatoza fedha nyingi zaidi za ushuru wa huduma tofauti na iliyowekwa kwenye Sheria ni makosa kwani Serikali haiwezi ikatoza fedha ambazo haziko kwenye utaratibu wa sheria lakini kama halmashauri inakusanya fedha kidogo kuliko sheria inavyosema nalo ni kosa kwa mujibu wa sheria.

“Kwanini uchukue fedha kidogo wakati fomula ya kupata makusanyo halisi kwa niaba ya wananchi ipo..kwanini wewe utumie fumula ya kwako ya kubuni wewe wakati fumula ya kisheria ipo”alihoji Waziri Mpina.

Mbali na dosari hizo za ukwepaji kodi, Waziri Mpina alielezea kusikitishwa kwake na kitendo cha mwekezaji huyo kushindwa kuwashirikisha wananchi wanaozunguka eneo hilo kujifunza teknolojia hiyo ili kukuza sekta ya ukuzaji viumbe maji hasa ufugaji wa Kambamiti.

Alisema Serikali haijapokea maombi yoyote ya upungufu wa wataalamu wenye utaalamu na uzoefu maalum kuendesha mradi kwani wataalamu hao wanazalishwa katika vyuo vyetu kikiwemo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Vyuo vya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA).

“Mradi huu unaendeshwa kwa usiri na wivu mkubwa kiasi kwamba wananchi wa kawaida hawawezi kupata utaalamu kupitia mradi huu..kwenye taarifa yenu sikuona mkichukua vijana wanaomaliza vyuo au kuingia makubaliano na vyuo (MOU) kufanya mafunzo ya vitendo kwenye mradi huu na kuwalipa kima cha chini cha mshahara”alihoji Waziri Mpina.

Alisema wawekezaji kutoka nje wanapofika nchini wanalojukumu katika mikataba yao ya kusambaza taaluma katika eneo lao la uwekezaji ili kuwawezesha watanzania wengi kunufaika na uwekezaji wao na kueleza kusikitishwa kwake na kampuni hiyo kuwabagua wazawa na kuwapa nafasi wageni hata kwenye kazi ambazo zingeweza kufanywa na watanzania.

“Toka nimeanza kutembelea miradi hii kuanzia Dar es Salaam nimekuja kwenye shamba la kambamiti na kituo cha kutotoleshea vifaranga mapokezi na utolewaji wa maelezo na ufafanuzi unafanywa na wageni hii ni ishara kwamba uongozi wote umeundwa na wageni au ni sehemu ya kuficha ukweli juu ya undeshaji wa biashara hiyo’ alihoji Waziri Mpina

Mbali na hilo Waziri Mpina alisema Serikali inazo taarifa za vijana wanaokwenda kufanya kazi kwenye uwekezaji huo wanashindwa kufanya kazi kutokana na ujira mdogo wanaolipwa na mwekezaji huyo na kuvunjika moyo na kisha kuondoka.

“Kulipwa mshahara mdogo haijulikani wanalipwa hivyo ili wakate tamaa waondoke na baadae itengeneze nafasi ya ajira kutoka nje ya nchi au tatizo ni nini”alihoji Waziri Mpina.

Kwa upande wake Meneja wa Alphakrust, Ganeshan Vedagiri amelalamikia kukosa wataalamu wenye weledi na pindi watanzania wanapoajiriwa wanakaa muda mfupi na kuondoka huku akilalamikia kudaiwa ushuru kwenye halmashauri zaidi ya moja

Alisema mradi huo wa Mafia una mabwawa 31 ya Kambamiti ambapo kwa mwaka huzalisha wastani wa tani 400 huku asilimia 90 ya samaki hao wakiuzwa nchini ufaransa huku asilimia 10 zikiuzwa hapa nchini. 


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafia, Chuchu Silvery licha ya kuwepo kwenye ziara hiyo hakuweza kuzungumzia chochote kuhusiana na dosari hizo.
Share:

Simbachawene Agoma Kufungua Machinjio Ya Msalato jijini Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene hii leo amegoma kufungua machinjio ya Msalato jijini Dodoma kwa kutokidhi vigezo vya ubora vinavyoridhisha ikiwemo ukarabati wa kiwango cha chini na kutoa muda wa wiki ya moja kurekebisha dosari zilizobainika.
 
Ametoa uamuzi huo wakati akitembelea jengo la machinjio ya Msalato jijini Dodoma wakati wa ziara aliyoifanya na kubaini kasoro mbalimbali zinazotakiwa kupatiwa ufumbuzi. “Sifungui hii machinjio kwa sababu hamjajiandaa na ujenzi uko hovyo kwahiyo siwezi kufungua kitu cha hovyo namna hii” Simbachawene alisisitiza.
 
Akiongea katika ziara hiyo amesema amesikitishwa sana na ukarabati wa kurekebisha machinjio hayo kwani haukidhi viwango na ujenzi wake ni wa kiwango cha chini hivyo amemuagiza Afisa Mipango Miji wa Jiji la Dodoma Bwana Shabani Juma kuhakikisha ndani ya wiki ya moja kila kitu alichotolea maelekezo kifanyiwe marekebisho.
 
“Sijafurahishwa kwa kwakweli, majengo ya Serikali yanatakiwa kujengwa na mafundi classic, vitu vya Serikali viwe State of Art” Simbachawene alisisitiza.
 
Waziri Simbachene pia amegiza kuandaliwa kwa taarifa rasmi ya ukarabati huo ikiwa ni pamoja na thamani ya fedha zilizotumika katika zoezi zima la ukarabati na ujenzi wa  mifumo ya maji safi na maji taka.
 
Naye Diwani wa Kata ya Msalato Mheshimwa. Ali Mohamed amesema kuwa amesikitishwa sana kwa kutofunguliwa kwa machinjio hiyo kwani wakazi wengi wa Kata yake wanategemea machinjio kwa shughuli zao za kila siku kwa sababu ni Wafugaji. Pia alisema Maelekezo yote yaliyotolewa na Mheshiwa Waziri Simbachawene wameyapokea na naamini kuwa yatarekebishwa kwa wakati.
 
Machinjio hiyo ya Msalato ilifungwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimazi wa Mazingira (NEMC) tarehe 31 Oktoba 2019 kutokana na sababu za mazingira yasiyokua safi na salama, kufuatia ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira.


Share:

Bilioni 23.5 Zaokolewa na TANESCO Kila Mwaka

Na  mwandishi wetu - Dodoma
Shilingi Bilioni 23.5 zinaokolewa kila mwaka baada ya Serikali kupitia Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) kuzima mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta mazito.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Shirika hilo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya tano, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika hilo Dkt. Tito Mwinuka amesema kuwa Shirika hilo limefanikiwa kujiendesha bila kupokea ruzuku  kufuatia hatua zilizochukuliwa na Serikali ikiwemo kuzimwa kwa mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta.

“Tumezima mitambo ya kuzalisha umeme kwa mafuta mazito katika maeneo ya  Makambako, Tunduru, Liwale, Namtumbo, Ludewa, Madaba  na kuyaunganisha na gridi ya Taifa hali inayochangia kuongeza kasi ya maendeleo katika maeneo hayo na kupunguza gharama za uendeshaji ;” Alisisitiza Dkt. Mwinuka

Akitaja baadhi ya mitambo iliyozimwa Dkt. Mwinuka amesema kuwa ni  ile ya IPTL, AGRECO, Syimbion na mingine  katika maeneo mbalimbali hapa nchini iliyokuwa ikitumia mafuta katika uzalishaji wa umeme.

Akifafanua amesema kuwa hali hiyo imechangia katika kuongeza mapato ya Shirika hilo kutoka Shilingi takribani trilioni 1.2 mwaka 2012 hadi kufikia zaidi ya trilioni 1.5 kwa mwaka kwa sasa hali inayoliwezesha Shirika hilo kuendelea kuongeza tija katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wa wateja waliounganishiwa umeme wameongezeka kutoka milioni 1.6 waliokuwepo kufikia mwaka 2015 hadi zaidi ya milioni 2.7 kufikia mwaka 2019 sawa na ongezeko la wateja zaidi ya milioni 1.05 katika kipindi hicho ambao ni asilimia 63.84.

Akizungumzia miradi ya kimkakati Dkt. Mwinuka amesema kuwa ni pamoja na mradi wa kufua umeme wa Mwalimu Nyerere katika Mto Rufiji megawati 2115 unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya shilingi trilioni 6.55, Rusumo megawati 80, Kakono megawati 87, Mradi wa kuzalisha umeme kwa gesi mkoani Mtwara megawati 300.

Akieleza zaidi, Dkt. Mwinuka amesema kuwa miradi mingine inatekelezwa katika maeneo mengine katika mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na huduma ya umeme.

Kwa upande wa Vijiji vilivyounganishiwa umeme vimeongezeka kutoka 2018 mwaka 2015 hadi Vijiji 8236 kufikia Desemba 2019 ikiwa ni ongezeko la asimia 67 hali inayotokana na jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kuwa wananchi wote wanafikiwa na nishati ya umeme katika maeneo yote.

Katika kipindi cha miaka 4 umeme ulioongezwa kwenye gridi ya Taifa ni Megawati 400 zinazotokana na utekelezaji wa miradi ya kimkakati ikiwemo ya Kinyerezi namba 1 na namba 2.

“Kwa upande wa wateja wa viwanda  wameongezeka kutoka 2571 mwaka 2015 hadi  3787 mwezi Desemba 2019;” Alisisitiza Dkt. Mwinuka

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya uzalishaji, usambazaji na uwekezaji katika sekta ya nishati ili kukuza uchumi na ustawi wa wananchi.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger