Monday 30 December 2019

HUU NDIYO MJI WENYE PAKA WENGI ZAIDI KULIKO WATU


Kundi la paka katika barabara za mji wa Kafr Nabl

Baada ya miezi kadhaa ya mashambulio ya mabomu kutoka kwa vikosi vya Syria na Urusi, mji wa Kafr Nabl nchini Syria sasa umesalia kuwa makaazi ya paka wengi kuliko watu.

Watu wachache waliosalia katika mji huo wa Syria uliolipuliwa wanajiliwaza na mamia au pengine maelfu wa paka, kama ilivyobaini BBC.

Baadhi ya wakaazi hujificha chini ya kifusi cha nyumba zilizobomolewa ili kujikinga dhidi ya mabomu yanayodondoshwa kutoka angani.

Mmoja wao ni Salah Jaar mwenye umri wa miaka 32 (katika picha hapo juu), lakini kama unavyoona hayuko peke yake.

Katika kifusi kilicho karibu naye kuna mamia ya paka waliojipata katoka hali kama yake.

"Unafarijika paka akiwa karibu nawe," alisema. 'Zinafanya sahali milipuko ya mabomu, kuporomoka kwa majengo, mateso, na uwoga."

Nyumbani kwa Salah katika mji wa Kafr Nabl, wakati mmoja ulikuwa makazi ya watu 40,000, lakini sasa ni watu chini ya 100 waliosalia.

Ni vigumu kubaini ni paka wangapi waliopo hapo - ni mamia kwa hakika lakini huenda wamefikia maelfu.Mji wa Kafr Nabl

"Watu wengi sana wamehama mji wa Kafr Nabl hali iliyofanya idadi ya watu kuwa ndogo sana. Kwa kuwa paka wanahitaji watu wakuwatunza kuwapa maji na chakula, wamehamia katika nyumba za watu walioamua kubaki katika mji huo mahame. Kila nyumba ina karibu paka 15, au hata zaidi," Salah anasema.

Salah bado anafanya kazi ya uandishi habari katika kituo cha radio cha, Fresh FM, japo studi za kituo hicho zilibomolewa katika mashambulizi ya angani ya hivi karibuni.

Walikuwa na bahati shughuli za kituo hicho zilihamishiwa mji ulio karibu kutokana na sababu za kiusalama,muda mfupi kabla ya mashambulio hayo.

Kituo hicho ambacho huwatangazia watu kuhusu kitisho cha mashambuliuo kupitia habari, na vipindi vingine kilipata umaarufu kutokana na paka.

Makumi kati ya paka hao walifanya ofisi za kituo hicho kuwa makaazi yao. Muasisi wa kituo hicho na mwanaharakati Raed Fares, aliyeuawa na wanamgambo wa Kiislam wenye silaha mwezi November 2018, alitenga fedha za kuwanunulia maziwa na chakula.

"Paka wengi walizaliwa katika jengo hilo. Mmoja wao aliyekuwa na rangi nyeupe na madoa ya hudhurungi alimpenda sana Raed. Angeliandamana nae kila mahali na hata kulala kando yake," anasema Salah.

Anapondoka katika mabaki ya iliyokuwa nyumba yake, anakaribishwa na sauti za paka kutoka kila upande, Hili humfanyikia kila mtu, anasema.

"Wakati mwingine tunapotembea njiani tunaweza kupatana na paka 20 au 30 wanaoandamana na sisi kila tunapoenda. Baadhi yao walitufuata hadi nyumbani."

Giza linapoingia milio ya mbwa wasio na wenyewe husikika kutoka kila upande wa mji huo. Wao pia wana njaa na hawana pakwenda. Hali ya kupigania mabaki ya chakula na mahali pa kulala inawafanya kushindana na paka wa Kafr Nabl.

Katika makabiliano kati ya paka na mbwa mshindi ni nani?

"Bila shaka mshindi ni paka! Wako wengi sana kuwawaliko mbwa hao." Salah anasisistiza.

Wengi wao walikuwa wanapendwa sana na familia zilizotoroka mji huo baada ya vikosi vya utawala wa Syria kuanzisha oparesheni ya kuukomboa mji wa Idlib mwezi Aprili iliyopita.

Sasa baada ya kukosa wa kuwatunza na chakula cha mara kwa mara wamelazimika kutafuta makaazi mapya chini ya kifusi cha mijengo iliyoporomoka.

Na japo watu kama Salah hawana matumaini ya kuishi, bila kujua chakula kinatoka wapi, wanajiliwaza na paka hawa ambao wamegeuka kuwa marafiki wa dhati.

"Kila ninapokula, nao hula, iwe ni maboga, spageti au hata mkate uliokauka. Katika hali hii nahisi sote ni viumbe wadhaifu na tunahitaji kusaidiana," anasema.

Sio ajabu kwa paka kujeruhiwa pamoja na watu kutokana na mashambulio ya mabomu ya mara kwa mara.

Lakini licha ya uhaba wa dawa, sawa na vifa vingine muhimu, Salah anasema wanajaribu kila wanaloweza kuwatunza paka hao.

"Nina rafiki ambaye anaishi na paka nyumbani kwake. Mmoja wao alijeruhiwa kwa roketi ambayo ilimvunja mguu. Lakini alifanikiwa kumpeleka hadi mji wa Idlib kwa matibabu na sasa anatembea vizuri kama awali,"anasema.

Huku vikosi vya rais Bashar al-Assad vikikaribia Kafr Nabl, mji huo huenda ukavamiwa hivi karibuni. Salah anakiri kuwa na hofu, sio kwake tu bali pia kwa usalama wa paka ambao ni marafiki zake walio wengi.
Chanzo - BBC
Share:

Re-advertised: AFR Senior Program Support Specialist – WaSH at Senior Manager of Human Resources at Compassion International – Africa Region

Re-advertised: AFR Senior Program Support Specialist – WaSH at Senior Manager of Human Resources at Compassion International – Africa Region   Overview The primary purpose of this role is to provide technical oversight for the Water, Hygiene and Sanitation (WaSH) sector in Africa Region. The Senior Program Support Specialist- WaSH is expected to provide strategic leadership and serve… Read More »

The post Re-advertised: AFR Senior Program Support Specialist – WaSH at Senior Manager of Human Resources at Compassion International – Africa Region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Call for Experts at RTI – Tanzania Environment

Around the globe, RTI brings together private- and public-sector stakeholders to manage natural resources and promote sustainable livelihoods while conserving unique biodiversity. By enhancing institutions, policy, and technical capacity, we strengthen natural resource management in protected areas and their surrounding environments. We work with governments, communities, and key stakeholders interested in applying data-driven conservation and biodiversity management approaches.RTI… Read More »

The post Call for Experts at RTI – Tanzania Environment appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali Yavunja Mkataba Na Kurejesha Umiliki Wa Machinjio Ya Dodoma

Waziri wa Uvuvi na Mifugo, Luhaga Mpina, amesema Serikali imevunja mkataba wa mauzo ya mali za machinjio ya Dodoma baina ya Serikali na Kampuni ya Uwekezaji wa Taifa (NICOL) uliosainiwa mwaka 2008 kutokana na kampuni hiyo kusababisha hasara ya shilingi bilioni 9.7

Sambamba na hilo, vyombo vya ulinzi na usalama vimeagizwa kuwachukulia hatua za kisheria watendaji wote wa NICOL, NARCO na TMCL waliohusika na ubadhirifu wa mali za TMCL na kuisababishia hasara serikali tangu mwaka 2008.

Hatua hiyo ilifikiwa jana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, katika kikao cha wadau kujadili namna ya kunusuru machinjio hayo.

Mpina alisema mkataba huo umevunjwa kwa kuzingatia ibara ya 7 na 13 ya mkataba wa mauzo ya mali na hivyo kuanzia sasa machinjio hiyo itakuwa chini ya serikali.

“NICOL ilipe serikali Sh. 9,712,127,660 ambazo serikali ilipunjwa katika biashara ya machinjio na pia NICOL ilipe madeni yote inayodaiwa kampuni ya ubia TMCL kiasi cha Sh. 5,248,084,000,” alisema.

Aidha, aliitaka kampuni ya NARCO ijiondoe katika kampuni ya Ubia TMCL ndani ya siku 60 kuanzia jana.

“Huduma za uchinjaji zitaendelea kutolewa kama kawaida katika kipindi cha mpito chini ya usimamizi wa serikali wakati mchakato wa kumpata mwekezaji mahiri wa mpito na wa kudumu unaendelea,” alieleza.


Share:

Vacancies at PAN AFRICAN POSTAL UNION (PAPU)

VACANCIES AT PAN AFRICAN POSTAL UNION (PAPU) The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), is quasi-independent Government body established under the Tanzania Communications Regulatory Act No.12 of 2003 to regulate communications and broadcasting sectors in Tanzania, on behalf of Pan African Postal Union (PAPU) a continental African organization, based in Arusha, Tanzania which brings governments and industries together to… Read More »

The post Vacancies at PAN AFRICAN POSTAL UNION (PAPU) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ajali ya Coaster na lori Yaua Watu 6 Dodoma

Watu sita wamefariki Dunia na wengine zaidi ya kumi kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari aina ya Toyota Coaster na lori eneo la Kisasa Dodoma usiku wa kuamkia leo Dec 30,2019, Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Dodoma Dr.Ernest Ibenzi amethibitisha kupokea miili ya Watu sita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kwamba chanzo chake ni dereva wa lori baada ya kuona korongo kubwa katikati ya barabara, akajaribu kulikwepa.

Amesema wakati anahama kukwepa korongo hilo, tayari lile basi dogo la abiria lilikuwa limeshafika karibu, na bodi la lori likaliangukia basi hilo la abiria na kusababisha vifo na majeruhi.Dereva alikimbia, Polisi wanaendelea kumsaka


Share:

Katibu Mkuu Ccm Awaomba Wananchi Kupuuza Kauli Za Viongozi Zinazowahimiza Kufanya Starehe Badala Ya Kufanya Kazi

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiru Ally, amewaomba wananchi kupuuza sera na kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa nchini zikitaka wananchi wale bata (wafanye starehe) badala ya kufanya kazi jambo ambalo likiachwa bila kukemewa litafanya kuwa na taifa legelege la kupenda starehe badala ya kazi.

Dkt. Bashiru amesema kuwa, katika nchi ambayo wananchi wanapambana kujikomboa kiuchumi, hasa katika nchi zetu za Afrika ambazo bado tupo nyuma kimaendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, kutokea kiongozi mmoja kuwaambia watu wafanye kazi kwa starehe ni usaliti mkubwa wa mapambano ya kiuchumi ambayo kama taifa tunayahimiza.

Katibu Mkuu ameyasema hayo alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya CCM Kata ya Bwanjai wilayani Misenyi tarehe 28 Desemba, 2019 na kuzungumza na wanachama na wananchi waliojitokeza katika ukaguzi huo.

“Nchi hii ambayo tunaongoza mapambano ya kujikomboa kiuchumi, inamuhitaji kila mtu kwa nafasi yake kuhimiza kufanya kazi kwa bidii, na huku CCM kuna kauli mbalimbali za kuhimiza kazi zikiwemo, Hapa Kazi tu, Kazi na Maendeleo, Uhuru na Kazi na Kazi ni Utu, ila kuna baadhi ya Vyama wao wanahubiri kazi na starehe, na huo ndio utofauti wa Chama kiongozi na Vyama vya uchaguzi.’’ Dkt. Bashiru ameeleza

Ameongeza kwa kusisitiza kuwa, “Unaposema kazi na bata, maana yake ni kudharirisha wanawake na mama zetu ambao wakati wote wamekuwa wakifanya kazi kusomesha watoto wao, wakifanya kazi kulisha familia zao, na sote hapa ni matokeo ya juhudi kubwa za mama zetu, ambao kuwambia wale bata, ni sawa na kuwataka washinde kwenye starehe huku watoto wakidharirika kwa kutokwenda shule, hizi ni kauli za kipumbavu za Vyama vya uchaguzi, ambazo hatuna budi kuzidharau na kuzipuuza.”

Aidha ameongeza kuwa, Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuwa chama cha kutetea haki za wanyonge na kitaendelea kusisitiza sekta zote za serikali zikiwemo afya, elimu, miundombimu na maji kutoa huduma kwa wananchi bila usumbufu wala ubaguzi na kuthamini utu wa watu wote.

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera mama Costancia Buhiye na Mkuu wa wilaya ya Misenyi Kanal Mstaafu Denis Mwila

Ikumbukwe kuwa, Dkt. Bashiru yupo nyumbani kwake Bukoba mkoani Kagera kwa mapumnziko ya siku kumi, na anatarajiwa kumaliza mapumziko hayo mapema mwezi Januari, 2020.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Disemba 30












Share:

Sunday 29 December 2019

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.



Share:

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,Kusafisha nyota, Mvuto wa Mwili na Biashara, ...Miguu kufa ganzi na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...


Share:

Diamond Platnumz Apokelewa Kishujaa Kigoma

Mwanamuziki Diamond Platnumz amepokewa na mabango wakati akiwasili stesheni ya Nguruka Mkoani Kigoma katika kuadhimisha miaka yake kumi katika muziki.

Umati wa watu umejitokeza katika stesheni ya Nguruka Mkoani Kigoma wakiwa na mabango yaliyobeba jumbe mbalimbali kwa mwanamuziki huyo.

Moja ya mabango hayo lilikuwa limeandikwa “Karibu Diamond kwenu Kigoma tuijenge Kigoma, Sisi Nguruka tulishaanza ujenzi wa madarasa saba na vyoo 12. Tunaomba tuunge mkono, watoto 494 hawana pakusoma.”

Diamond aliyeanza safari ya kuelekea Kigoma jana Desemba 28, 2019 akiwa na mashabiki wake katika treni lengo lake kubwa ni kujumuika na watu wa mkoa huo kusheherekea miaka kumi tangu kuanza muziki.

Nguruka ikiwa ndio stesheni ya kwanza unapoingia Mkoa wa Kigoma, Diamond alikutana na umati wa watu ukimsubiri.

Baada ya kuwasili eneo hilo Diamond alipanda jukwaani na kuanza kuwaimbisha wakazi hao wimbo wa Baba lao .
Hata hivyo ilifika mahali mzuka ukampanda kweli kama moja ya kibwagizo kilichopo katika wimbo huo kinachosema 'mzuka ukipanda hata nguo nitavua, nivue muone'walipoitikia mashabiki akavua fulana yake aliyokuwa ameivaa ambapo watu wake waliichukia na baadaye kumrudishia


Share:

Jeshi la Polisi Lafanikiwa Kumtia Mbaroni Aliyemuua Mkewe Kwa Kumkata na Shoka

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limefanikiwa kumkamata muimba kwaya Moses Pallangyo (28), aliyemuua mke wake Mary Mushi, kwa kumkata na shoka kichwani, katika kijiji cha Kilinga wilayani Arumeru na kwamba baada ya mahojiano, mtuhumiwa huyo amekiri kufanya mauaji hayo.

Akizungumza leo Disemba 29, 2019, Kamanda wa Polisi mkoani humo Jonathan Shanna, amesema kuwa jeshi hilo lilimsaka mhalifu huyo kwa kutumia kikosi cha Mbwa ambacho ndicho kilichofanikisha kumkamata, akiwa mafichoni kuelekea nchini Kenya.

"Jana Disemba 28 saa 11: 30 jioni, tumefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo, ambaye tuliahidi kumtafuta kwa namna yoyote ile na 'Dog Style' ndiyo imeleta mafanikio ya kumkamata yaani ilikuwa bandika bandua, mtuhumiwa tumemhoji kwa kina na amekiri kufanya kitendo hicho cha kikatili, na tulitaka kujua kwanini amefanya kitendo hicho akasema ni shetani alimpitia" amesema Kamanda Shanna.

Tukio hilo lilitokea Disemba 25, 2019 majira ya mchana, jambo ambalo hapo awali lilihusishwa na ugomvi wa kifamilia ikiwemo wivu wa mapenzi.


Share:

Waziri Mkuu Atoa Agizo Zito Kwa Wakuu Wa Mikoa kote Nchini

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa nchini wahakikishe wanasimamia ipasavyo ujenzi wa vyumba vya madarasa vikamilike kwa wakati ili wanafunzi wote waliochagulia kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2020 waanze masomo kwa pamoja.

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wanafunzi wote wanaanza kusoma kwa pamoja kwa sababu wakipishana muda wa kuanza masomo baadhi yao wanashindwa kufanya vizuri jambo ambalo si sahihi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Desemba 29, 2019) wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015/2020 kwenye mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Ruangwa.

Jumla ya watahiniwa  933,369  sawa  na  asilimia  98.55 ya  waliosajiliwa  walifanya  mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2019 na kati yao watahiniwa  759,737  wamefaulu ambao ni sawa na asilimia 81.50.

Kati  yao  wasichana  ni  395,738  ambao  ni  sawa  na  asilimia  80.87  na wavulana  ni  363,999  sawa  na  asilimia  82.20.  Mwaka  2018  watahiniwa waliofaulu  walikuwa  asilimia  77.72,  hivyo  kuna  ongezeko  la  ufaulu  kwa asilimia  3.78.

“Wakuu wa Mikoa hakikisheni vyumba vya madarasa vinakamilika ili wanafunzi wote waliofaulu waanze masomo kwa pamoja. Kitendo cha wanafunzi kupishana kuanza masomo kinawafanya waliochelewa kutofanya vizuri katika mitihani yao.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amewasisitiza viongozi hao wahakikishe wanasimamia vizuri elimu kwa watoto wa kike na kuwachukulia hatua watu wote watakaobainika kuwakatisha masomo iwe kwa kuwaoa, kuwaozoesha au kuwapa ujauzito.

Amesema Serikaliimeweka sheria kali ya kumlinda mtoto wa kike lengo ni kumuwezesha amalize masomo yake ili aweze kujikwamua kiuchumi na aondokane na utegemezi, hivyo ni marufuku kuwakatisha masomo.

“Watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii na Serikali itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa au kumpa ujauzito.”

Waziri Mkuu amesema Serikali inataka kuona idadi kubwa ya watoto wa kike wanatimiza malengo yao kielimu, hivyo ni lazima wakaondolewa vishawishi  kwa kuboresha mazingira yao ya kujifunzia ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya mabweni.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ikiwemo na wilaya ya Ruangwa ambayo imepewa sh. bilioni 38 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ruangwa kwa kubuni mradi wa kimkakati wa ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao na pembejeo linalojengwa katika kijiji cha Lipande. Ujenzi huo unaogharimu sh bilioni 5.45.

Ghala hilo ambalo limeanza kutumika lina uwezo wa kuhifadhi tani 20,000 litaiwezesha halmashauri kujiongezea mapato ya ndani na kusaidia kupunguza utegemezi kutoka Serikali Kuu na wafadhili. Pia litapunguza gharama za usafirishaji wa korosho walizokuwa wanatozwa wakulima wakati wa kusafirisha mazao.

Amesema katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano miradi mingi ya kimkakati imetekelezwa nchini ambayo ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), upanuzi wa bandari za Mtwara, Dar es Salaam na Tanga, uboreshwaji wa viwanja vya ndege, ununuzi wa rada na ununuzi wa ndege mpya.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano tangu ilipoingia madarakani mwaka 2015, kipaumbele chake kilikuwa ni kukuza kiwango cha uchumi kutoka cha chini kwenda cha kati ifikapo mwaka 2025 kupitia sekta ya viwanda.

(mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAPILI, DESEMBA 29, 2019.


Share:

PICHA: Katibu Mkuu CHADEMA John Mnyika Apewa Uchifu Wa Wasukuma

Katibu Mkuu Chadema, Mheshimiwa John Mnyika leo amesimikwa kuwa Chifu wa Wasukuma na kupewa jina la Maronja likiwa na maana ya MREKEBISHAJI. Mnyika yupo mapumzikoni kijijini kwao mkoani Mwanza.



Share:

Rais Magufuli Arejesha fomu ya tamko kuhusu Rasirimali na Madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Rais Magufuli amewasilisha fomu ya tamko kuhusu Rasirimali na Madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo Dar es Salaam.

Fomu hizo zimewasilisha leo Jumapili Desemba 29, 2019 na katibu wake, Ngusa Samike kwa niaba ya Rais Magufuli aliyepo wilayani Chato mkoani Geita kwa mapumziko.

Akipokea fomu hizo, Kamishna wa Maadili, Jaji mstaafu Harold Nsekela amempongeza Rais Magufuli kwa hatua hiyo akisema ametekeleza matakwa ya Kikatiba na Sheria ya Maadili.

“Viongozi kurejesha tamko ni jambo la kikatiba kwa mujibu wa ibara ya 132 (5)b. Ibara hii inasema msingi wa maadili wa viongozi wa umma, itawataka watu fulani walioshika nafasi fulani za madaraka kutoa mara kwa mara maelezo kuhusu mapato, rasirimali na madeni yao.

“Katiba ndiyo inatatuka sisi viongozi kutoa maelezo haya kila mwaka. Ukija katika sheria yetu namba 13 ya mwaka 1995 kifungu 9 inaeleza kila mwisho wa mwaka kiongozi anatakiwa kumpelekea kamishna tamko la maandishi,” amesema Jaji Nsekela.

Jaji Nsekela amempongeza Rais Magufuli kwa kurejesha tamko la mapato, madeni na rasirimali zake kama kiongozi wa umma, huku akiwataka viongozi wasiorejesha kufanya hima kutekeleza mchakato huo kwa sababu zimebaki siku mbili pekee.


Share:

CHADEMA Watoa wito kwa wananchi Njombe kwenda kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura

Na Amiri kilagalila-Njombe
Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema mkoa wa Njombe,kimetoa wito kwa wananchi kwenda kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura linalotarajia kuanza disemba 30,2019 mpaka januari 5,2020 mkoani humo.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Njombe Rose Mayemba wakati akizungumza na vyombo vya habari.

“Tunafahamu kwamba wananchi wamekatishwa tamaa sana na zoezi lililopita kwenye serikali za mitaa,wengi ile hari imekufa, lakini nitoe rai kwa wananchi wasiache wajibu wao wa kwenda kujiandikisha” alisema Rose Mayemba

Mwenyekiti Rose Mayemba amewaagiza viongozi wa chama hicho kuto kuacha kuwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha mara baada zoezi hilo kukamilika katika maeneo mengine ya nchi na sasa zoezi hilo linatarajia kuanza mkoani humo.

Aidha amesema kama vilivyowekwa vipaumbele vya chama hicho ikiwemo kudai tume huru ya uchaguzi,chama hicho hakitaweza kwenda kwenye uchaguzi bila ya kuwa na tume huru.


Share:

Ufafanuzi Juu ya Madai Kuwa Serikali Ya Tanzania Imewazuia Kuingia Nchini Raia wa Nigeria




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger