Monday 9 December 2019

MWANAMKE AFUFUKA.... MAPIGO YAKE YA MOYO YALIZIMA SAA SITA...MADAKTARI WASIMULIA

Audrey alikosa fahamu kwa saa sita baada ya mapigo yake ya moyo kusimama

Mwanamke wa Uingereza ambaye alipata mshtuko wa moyo baada ya mapigo yake ya moyo kuacha kufanya kazi kwa saa sita amefufuka tena katika kile ambacho madaktari wamesema ni jambo ambalo halijawahi kutokea hapo kabla.

Audrey Schoeman alipata mshtuko wa moyo alipopigwa na dhoruba ya theluji wakati anapanda mlima Pyrenees akiwa na mumewe mnamo mwezi Novemba.

Madaktari wanasema huo ndiyo muda mrefu zaidi kwa mtu kuwahi kupata mshtuko wa moyo nchini Uhispania.

Audrey, ambaye kwa sasa anakaribia kurejea katika hali yake ya kawaida, amesema anatarajia kupanda tena mlima huo msimu wa masika.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 34 anayeishi Barcelona, alianza kupata matatizo ya kuzungumza hali ya hewa ilipobadilika alipokuwa akipanda mlima na baadaye akapoteza fahamu.

Hali yake ilizorota zaidi wakati akisubiri kupata huduma za dharura na mume wake Rohan akaamini kwamba mkewe anakufa.

Akizungumza na vyombo vya habari Alhamisi iliyopita, Mumewe Rohan alikiambia kituo cha televisheni cha TV3: "Nilikuwa najaribu kumgusa, mapigo yake ya moyo hayakuwa yanapiga kabisa... Sikuweza kuhisi akipumua."Mume wa Audrey Schoeman, Rohan, ambaye alidhani mkewe amekufa

Timu ya uokoaji ilipofika saa mbili baadaye, joto la mwili la Audrey lilikuwa limeshuka hadi nyuzijoto 18.

Alipowasili katika hospitali ya Vall d'Hebron huko Barcelona, hakuwa na dalili zozote za kurejesha uhai.

Hata hivyo kiwango cha chini cha joto ambacho kilisababisha Audrey augue, pia kilimsaidia kunusuru maisha yake, amesema daktari wake Eduard Argudo.

"Alionekana kana kwamba amekufa,"amesema hivyo katika taarifa aliyotoa.

"Lakini tulichokifahamu hasa katika mshtuko wa moyo, tulijua kwamba kulikuwa na uwezekano wa Audrey kufufuka."

Joto la mwili lililinda mwili na ubongo wake usizorote zaidi wakati akiwa amepoteza fahamu, daktari Argudo amesema, licha ya kwamba alikuwa anaelekea kufa.

Aliongeza: "Kama angekuwa katika mshtuka wa moyo kwa kipindi hicho kirefu, joto la mwili wake likiwa kawaida, angekuwa amekufa."

Wakiwa katika hali ya kukimbizana na muda, madaktari wa Audrey waligeukia mashine maalum inayoweza kuondoa damu na badala yake wakamuingiza hewa ya oksijeni.

Joto la mwili wake lililofikia nyuzijoto 30, walitumia kifaa cha kufanya moyo uanze kupiga tena, saa sita baada ya kupata huduma ya kwanza.Audrey na Rohan Schoeman na walioshughulika kumpa huduma ya kwanza

Audrey alitolewa hospitali siku 12 baadaye, akiwa tu na matatizo ya hisia kwa sababu ya kiwango cha joto alichokuwa nacho wakati amepoteza fahamu.

"Tulikuwa na wasiwasi kuhusu madhara atakayopata katika mfumo wake wa neva," amesema daktari Argudo.

"Hasa ukizingatia kwamba hakuna mtu ambaye moyo wake ulisita kupiga kwa muda kama huo kisha ukuanza tena kufanya kazi."

Akizungumza baada ya kurejea katika hali yake ya kawaida, Audrey anasema hafahamu chochote kuhusu kilichotokea.

"Kwa siku ya kwanza na pili, sikujua kile kinachoendelea, eti nipo katika chumba cha wagonjwa mahututi," amesema.

"Lakini tangu wakati huo, nimekuwa nikijitahidi kusoma zaidi hasa kuhusu joto la mwili na kwa kweli na hisi furaha sana kuona nilinusurika kifo."

Audrey anasema anahisi yeye ni mwenye bahati na pia amewashukuru wafanyakazi wa hospitali hiyo.

"Ni kama miujiza na pia madaktari walichangia pakubwa, Audrey amesema.

Ameongeza kwamba kuna uwezekano mkubwa hatarejea tena kupanda mlima katika kipindi hiki.

"Kwa muda huu haitowezekana lakini nina imani kwamba msimu wa masika nitaweza kuupanda tena. Sitaki tukio hili liwe sababu ya kuachana na kile ambacho nimekuwa nikikipenda," amesema.
CHANZO - BBC
Share:

URUSI YAFUNGIWA MIAKA MINNE KUTOJIHUSISHA NA MCHEZO WOWOTE DUNIANI


Timu ya taifa ya soka ya Urusi

Urusi imefungiwa miaka 4 kutojihusisha na mchezo wowote duniani, baada ya kupatikana na hatia ya kufanya udanganyifu kuhusu vipimo na maabara juu ya utengenezwaji na matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni.

Taarifa ya Shirika la kupinga dawa za kuongeza nguvu michezoni 'World Anti-Doping Agency' (WADA) leo Desemba 9, 2019, imeeleza kuwa Urusi inatakiwa kusimamishwa na mashirikisho yote yanayosimamia michezo duniani ikiwemo FIFA kwa upande wa soka pamoja na Kamati ya kimataifa ya Olimpiki (IOC).

Kufungiwa huko ni wazi kuwa Urusi itakosa michuano mbalimbali mikubwa ndani ya miaka hiyo ikiwemo Olimpiki 2020, itakayofanyika jijini Tokyo Japan, pamoja na FIFA World Cup 2022 nchini Qatar.

Uamuzi huu umekuja ikiwa ni miaka minne imepita tangu uchunguzi mkali uanze kufanyika, ambapo tayari viongozi mbalimbali wa michezo nchini humo, wameshafungiwa kwa hatia hizo hizo za kuhusika kuruhusu wanamichezo kutumia dawa za kuongeza nguvu.

WADA wameweka wazi kuwa Urusi kupitia maabara zao za Moscow, waligoma kuchunguzwa na baadaye walipokubali walitoa taarifa feki na kisha kufuta baadhi ya taarifa ambazo zingeeleza ukweli juu ya suala hilo.

Kwa upande wa klabu ya Saint Petersburg ambayo inajiandaa na mchezo wake dhidi ya Man City kwenye ligi ya mabingwa Ulaya, wao wataendelea pamoja na timu ya taifa itacheza EURO 2020 kutokana na michuano yote hiyo kuandaliwa na UEFA na sio FIFA.

Hata hivyo wamepewa siku 21 kuweza kukata rufaa katika mahakama ya kimataifa ya michezo 'Court of Arbitration for Sport' (CAS).
Share:

LOWASSA : KAMA RAIS MAGUFULI AKIACHIWA AKAPIGA MIAKA YAKE KUMI NCHI HII ITABADILIKA


Waziri mkuu za zamani, Edward Lowassa amesema Rais Magufuli akiongoza nchi kwa miaka 10 itapiga hatua kubwa katika maendeleo.


Lowassa  ametoa kauli hiyo katika maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika yaliyofanyika mjini Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba.

"Amani ndio msingi anaoutumia mheshimiwa Magufuli leo kuongoza nchi yetu, kuleta mshikamano na umoja, nampongeza amefanya kazi nzuri sana…kama akiachiwa akapiga miaka yake kumi…kumi mheshimiwa nchi hii itabadilika,” – Amesema Lowassa

Lowassa alikihama Chama Cha Mapinduzi (CCM)  mwaka 2015 na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako alipitishwa kugombea urais mwaka 2015 na kushika nafasi ya pili nyuma ya Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu, lakini baadaye Machi Mosi, 2019, alirejea CCM.


Share:

SERIKALI YAITAKA TAASISI YA UHASIBU TANZANIA (TIA) KUBORESHA ZAIDI MITAALA YAKE

Mgeni Rasmi Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi ( kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango) akimkabidhi mmoja wa Wahitimu Shahada yake. 

Na Abby Nkungu, Singida

SERIKALI imeitaka Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kuboresha zaidi mitaala yake ili iweze kuzalisha wataalamu mahiri wenye ujuzi na weledi kwa ajili ya kujibu changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa Sera ya uchumi wa Viwanda  hivyo kuwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kipato cha kati kabla ya mwaka 2025.


Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi  kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango mjini Singida wakati wa Mahafali ya 17 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Wahitimu 1,688 wa kozi za Cheti cha Awali, Astashahada, Stashahada na Shahada kutoka Kampasi za Mwanza, Kigoma na Singida.

Katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi, Waziri Mpango alisema fani za Uhasibu, Ununuzi na Ugavi, Usimamizi wa biashara na Uongozi wa raslimali watu ambako Kampasi za Kigoma, Mwanza na Singida  zimejikita, ni muhimu katika kuendesha uchumi wa Taifa; hususan katika kusimamia mapato na matumizi ya fedha za umma. 

Alisisitiza kuwa Sera ya nchi kwa sasa ni Uchumi wa Viwanda, hivyo umahiri wa Wataalamu wanaozalishwa na Taasisi hiyo lazima uonekane dhahiri ili kufanikisha azma ya Serikali ya Tanzania ya Viwanda. 

"Ili kukabiliana na changamoto za Usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma, mahitaji ya soko, ushindani na utandawazi mnapaswa kuboresha mitaala yenu kukidhi viwango vya Kimataifa katika umahiri badala ya maarifa tu ili kukabiliana na changamoto za utekelezaji wa Sera ya viwanda. Tunahitaji wataalamu wenye weledi, maarifa na umahiri wa kutatua changamoto na si kuongeza changamoto", alifafanua.

Aidha, aliwasihi wahitimu hao kuweka mbele suala la uaminifu na uadilifu kwa kuwa hiyo ndiyo silaha na dira sahihi ya maisha yao ya kila siku. “Uhasibu ni taaluma iliyotukuka; hivyo ni vyema ninyi mliosomea mkazingatia kwa kiwango cha juu miiko, kanuni na taratibu zinazotawala fani hiyo”.

Alieleza  kuwa kashfa mbalimbali zinazosikika nchini na kwingineko duniani ni matokeo ya  watu kukosa uaminifu na uadilifu.  “Mtakapotoka hapa baada ya kuhitimu masomo yenu, mtakutana na changamoto mbalimbali, ila mkumbuke ni uadilifu na uaminfu pekee ndio utakaowaongoza katika maisha yenu yote” ,aliwaasa.


Dk Mpango aliwataka wahitimu hao kutumia vyema elimu waliyoipata katika kubuni, kuanzisha na kusimamia shughuli mbali mbali za kibiashara zitakazowasaidia wao na jamii yote ya Watanzania katika kujiletea maendeleo.


“Hatua mliyofikia iwe chachu ya kujiimarisha zaidi kitaaluma ili kuweza kushindana katika soko la ajira na kujiajiri. Msipojiimarisha, mtajikuta kazi zenu zinachukuliwa na watu wa nje" alisema na kutoa angalizo; 

"Soko letu la ajira rasmi ni dogo na kwa kweli halikidhi mahitaji ya wahitimu wote nchini. Ili kukabiliana na changamoto ya soko la ajira, ni vyema mkaelekeza mawazo yenu kwenye kujiajiri badala ya kuajiriwa".

Ofisa Mtendaji Mkuu wa TIA, Bi Luciana Hembe alitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili Taasisi hiyo kuwa ni pamoja na gharama kubwa za pango katika Kampasi za Kigoma na Mwanza kutokana na kukosa majengo yao wenyewe na uhaba wa miundombinu ya majengo Kampasi ya Singida kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TIA, Saidi Chiguma aliwataka wahitimu hao kuzingatia uadilifu, nidhamu na uzalendo wakati wote ili kujipambanua na wahitimu wa vyuo vingine. 
Share:

Rais Magufuli Asamehe Wafungwa 5,533 Sherehe za Miaka 58 ya Uhuru

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, ametangaza kuwaachia wafungwa 5533 ambao walikuwa wamefungwa katika Magereza mbalimbali nchini.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho wa miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara, ambapo kuna idadi kubwa ya wafungwa ambao wapo Magerezani kwa makosa ya kawaida sana.

“Nilitembelea Magereza nikashuhudia kuna mlundikano wa wafungwa, mpaka leo kuna Wafungwa 17,547 na Mahabusu 18,256, hii ni idadi kubwa, kwa hao wafungwa kuna baadhi wamefungwa makosa madogo, sijui kaiba kuku, kujibizana na mpenzi wake.

“Leo natangaza kuwasamehe wafungwa 5,533, ni mara ya kwanza kwa msamaha mkubwa kama huu kutokea, najua watu watashangaa lakini nimetumia siku hii ya Uhuru kusamehe, sifurahi kuongoza nchi yenye watu wengi Magerezani.

“Msamaha huu utawahusisha wafungwa waliofungwa kati ya kipindi cha siku moja hadi mwaka mmoja, na wale Wafungwa waliofungwa Miaka mingi kama 30, 20, 10 au mitano na wamebakiza muda mfupi kumaliza. Aliyewasamehe ni Mungu.” Rais Magufuli.


Share:

Form One Selection 2020 Ruvuma Region 2020/2021

Form One Selection 2020 Ruvuma Region 2020/2021 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Ruvuma.go.tz/ Form one selection for the academic year 2019/2020  The following students have been selected to join form one for Ruvuma Secondary schools for… Read More »

The post Form One Selection 2020 Ruvuma Region 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ruvuma Form one selection 2020

Form one selection – Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ruvuma Form one selection 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://ruvuma.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020/2021  The following students have been selected to join… Read More »

The post Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ruvuma Form one selection 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form One Selection 2020 Geita Region

Form One Selection 2020 – Waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020/2021  Geita Region for 2020/2021  Geita The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Geita.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020/2021  The following students have been selected to… Read More »

The post Form One Selection 2020 Geita Region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

KAULI YA MBOWE LIVE MBELE YA RAIS MAGUFULI KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 58 YA UHURU


Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowea,amehudhuria maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru katika Uwanja wa CCM Kirumba,jijini Mwanza.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni hakuvaa sare maalum za chama wala kombati ambazo zinatumiwa kama vazi maalum chama chao lakini amepigilia suti nyeusi, shati jeupe na tai.


Taarifa ya kushiriki kwenye maadhimisho kwa Mwenyekiti wa CHADEMA ilitolewa juzi na Kamati Kuu ya chama hicho kwa kumuagiza Mwenyekiti wake kwenda kukiwakilisha chama hicho kwenye Sherehe hizo za Uhuru. Hii ni mara ya kwanza kwa CHADEMA kushiriki kwenye maadhimisho ya Uhuru tangu mwaka 2015.

Akizungumza baada ya kupewa nafasi na rais Magufuli leo,Mhe. Mbowe ametoa kauli zifuatazo

"Nimekujua kuhudhuria maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru kama Uthibitisho wa Ulazima wa uwepo wa maridhiano,uwepo upendo,uwepo mshikamano katika taifa letu.

Nawapongeza sana Watanzania kwa siku ya leo na namuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango tuweze kuishi kama taifa la watu wanaopendana,tuvumiliane,tukosoane turuhusu demokrasia tujenge taifa lenye upendo na mshikamano 

Na Mhe. Rais kwa nafasi ya pekee tuna nafasi ya kuweka historia ya maridhiano katika taifa kwani kuna wengine wanalalamika,wengine wanaumia,Mhe. Rais tumia nafasi ukaliweke taifa katika hali ya utengamano" - Mbowe

Share:

Form One Selection 2020 Lindi Region

Form One Selection 2020 – Waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020 Lindi Region for 2020/2021 Lindi The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here>> http://www.lindi.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020/2021  The following students have been selected to… Read More »

The post Form One Selection 2020 Lindi Region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tangazo La Nafasi Za Masomk Form One, Darasa la Kwanza, Pili na Wanaotaka Kuhamia shule za lake Tanganyika

Tangazo ! Tangazo ;
Uongozi wa shule za lake Tanganyika zilizopo kijiji cha Mkigo wilaya ya kigoma vijijini mkoani kigoma unapenda kuwatangazia nafasi za masomo kwa mwaka 2020 kama ifuatavyo;


1.Nafasi za masomo kwa nursery, darasa la  kwanza, pili na tatu 

2.Nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza,na pia nafasi za kuhamia kwa kidato cha pili na tatu 

3.Pia kuna nafasi kuhamia za kidato cha tano  kwa comb HGK,HKL,HGL 

Shule ina  mazingira mazuri na ina  walimu wazoefu
Shule za lake Tanganyika zinamilikiwa na waktisto (SDA ) 

Ada zetu ni nafuu sana na zinalipwa awamu nne  kwa mwaka kwa upande wa secondary ada kwa mwaka ni 700000/= laki saba tu,na A- level karo ni laki saba na hamsini elfu ,750000/= na kwa upande wa  primary ada ni laki Tisa 900000/= tu kwa mwaka 

Nyote mnakaribishwa lake Tanganyika high school and pre and primary English medium 

Shule zote ni za bweni na kutwa kwa primary tu na pia ni mchanganyiko wavulana na wasichana 

Karibu lake Tanganyika ndo   suhulisho la  mwanao 

Kwa mawasiliano; 0769697667
0763091810
0756417203
0742208879
0692212326
0627557839 


Share:

WASHINDI WA WIKI PROMOSHENI YA KISHINDO CHA KUFUNGA MWAKA WALAMBA MIL.5


Mkurugenzi wa Tigo Kanda Ya Kaskazini Aidan Komba Akimkabidhi Elizabeth Makala Mshindi Wa Milioni Tano Katika Promosheni Ya Kishindo Cha Kufunga Mwaka Mkoani Arusha.
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazin Aidan Komba akimkabidhi Julita Kimaro Mshindi Wa Milioni Moja katika promosheni ya kishindo cha kufunga Mwaka mkoani Arusha.
Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Daniel Mainoya Akimkabidhi. Tegemeo Enos Mshindi Wa Milioni Tano katika promosheni ya kishindo ch kufunga Mwaka mkoani Mwanza. 
Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Gwamaka Mwakilembe Akimkabidhi Mausel Magesa Mshindi Wa Milioni Tano katika promosheni ya kishindo ch kufunga Mwaka mkoani Mwanza.

Share:

JINSI MBOWE NA NYALANDU WALIVYOINGIA CCM KIRUMBA


Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda yaKati, Lazaro Nyalandu wamewasili katika Uwanja wa CCM Kirumba,jijini Mwanza,  kuhudhuria maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru.


Hata hivyo, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati, Lazaro Nyalandu hawakuvaa sare maalum za chama wala kombati ambazo zinatumiwa kama vazi maalum chama chao lakini wamepigilia suti nyeusi, mashati meupe na tai.

Taarifa ya kushiriki kwenye maadhimisho kwa Mwenyekiti wa CHADEMA ilitolewa juzi na Kamati Kuu ya chama hicho kwa kumuagiza Mwenyekiti wake kwenda kukiwakilisha chama hicho kwenye Sherehe hizo za Uhuru.

Hii ni mara ya kwanza kwa CHADEMA kushirii kwenye maadhimisho ya Uhuru tangu mwaka 2015.


Share:

Picha: RAIS MAGUFULI ALIVYOPOKELEWA KWA SHANGWE UWANJA WA CCM KIRUMBA


Rais Magufuli ameingia Uwanjani wa CCM Kirumba Mwanza jijini Mwanza huku akipokewa kwa shangwe na vigeregere kutoka kila kona ya uwanja huo uliofurika.



Rais Magufuli aliingia uwanjani hapo saa 3: 14 asubuhi leo Jumatatu Desemba 9, 2019 akiwa kwenye gari la wazi akiongozwa na pikipiki nane gari moja mbele na nyingine nyuma.


Ameingilia mkono wa kushoto mwa uwanja na kuuzunguka akiwapungia wananchi mikono huku akishangiliwa kila alipopita wakati ukiimbwa wimbo wa taifa.




Share:

LIVE: Sherehe Za Miaka 58 Ya Uhuru Wa Tanzania Bara CCM - Kirumba Jijini Mwanza

Live: Maadhimisho Ya Miaka 58 Ya Uhuru Mwanza


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu December 9






















Share:

Sunday 8 December 2019

Bilionea Ali Mufuruki Afariki Dunia

Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Infotech Investment Group ambaye aliwahi pia kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, Ali Mufuruki (60), amefariki  Dunia usiku wa kuamkia leo Disemba 8, 2019  akiwa Afrika Kusini akipatiwa matibabu.

Mufuruki ni kati ya matajiri wakubwa 10 wa Tanzania akiwa ni mmiliki wa Kampuni ya Infotech Investment Group Limited na maduka ya Wolworth.

Oktoba 18, 2019 Mufuruki alijiuzulu nafasi yake ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Vodacom Tanzania ili kupata muda zaidi wa kuendelea na biashara zake.

Mwenyekiti wa sasa wa Ceort, Sanjay Rughan amethibitisha kutokea kwa kifo hicho kilichotokea saa tisa alfajiri katika Hospitali ya Morningside.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger