Monday 2 December 2019

Fahmi Dovutwa Avuliwa Uenyekiti Chama cha United People's Democratic Party (UPDP)

Halmashauri Kuu Taifa ya Chama cha United People's Democratic Party (UPDP) imemvua uenyekiti Fahmi Dovutwa baada ya kubainika kufanya kosa la kukisemea chama hicho kinyume na katiba.

Uamuzi huo ulitangazwa jana Jumapili Desemba 2, 2019 Mjini Unguja, Zanzibar na Kaimu Mwenyekiti wa UPDP Taifa, Abdalla Mohammed Khamis akisema uamuzi huo umefikiwa baada ya kikao hicho kujadili kwa kina makosa alioyafanya Dovutwa.

Alisema kosa kuu lililopelekea kuvuliwa kwa wadhifa wake ni kukisema chama hicho kuwa hakitoshiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa  uliofanyika Novemba 24, 2019, kitendo ambacho alikifanya bila kuagizwa wala kupata ridhaa ya uongozi wa chama hicho.

Alisema suala la chama hicho kutoingia katika uchaguzi wa serikali za mitaa imekiathiri kwani utekelezaji wa agizo alilotoa Dovutwa limesababisha chama kukosa  wenyeviti  wa serikali hizo ambao wataweza kuwakilisha chama.

Khamis alisema Dovutwa anaweza kukata rufaa endapo atahisi amevunjiwa haki yake kisheria na kikatiba na kwa sasa atabaki kuwa mwanachama wa kawaida.


Share:

Integration Program Manager at Millicom (Tigo)

Job Purpose You will be responsible to define and coordinate deliverables of all functional workstreams and ensure timely achievements of the agreed milestones across the organization as well as provide weekly project reports to the Chief Integration Officer   Key Responsibilities Managing projects across multiple functions within the organization. Define project deliverables across multiple workstreams ensuring scope completeness.… Read More »

The post Integration Program Manager at Millicom (Tigo) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Production Shift Manager at Radar Recruitment

Accountabilities:   Ensure that present and future transport and distribution policies and practices of the company achieve the most efficient and economical operations. Establish and ensure efficient control of all costs within the transport and distribution section. Design, implement and maintain scheduling systems that will ensure efficient and economic distribution of bulk products at all company Installations. Ensure… Read More »

The post Production Shift Manager at Radar Recruitment appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Private Sector Engagement Adviser at Vso Tanzania

Volunteer role: Private Sector Engagement Adviser Type of role: Business, management and IT Location: Mtwara and Lindi, Tanzania Application Closing Date: 16 Dec 2019 Interview date: TBC Start date: January 2020 VSO is the world’s leading international development organisation that works through volunteers to fight poverty. Working in 24 countries around the world, our unique role in international development… Read More »

The post Private Sector Engagement Adviser at Vso Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali Yapinga Kuwafukuza Wakimbizi Wa Burundi

Na Abubakari Akida,MOHA
Serikali ya Tanzania imepinga tuhuma zinazoelekezwa kwake kwamba imekua ikiwafukuza wakimbizi kutoka nchini Burundi wanaoishi katika makazi na kambi mbalimbali katika mikoa ya Kigoma,Tabora na Katavi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Kangi Lugola katika kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam kikihusisha pande tatu;Serikali ya Tanzania,Serikali ya Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi(UNHCR),huku mkataba maalumu ukisainiwa na pande hizo tatu lengo ni kuwezesha urejeshwaji wa wakimbizi walioomba kurejea nchini kwao baada ya amani kurejea.

“Ni vyema tukaliweka hili wazi ili jumuiya za kimataifa na Mataifa mengine yajue kwamba tunaposema tunawarejesha wakimbizi wa Burundi sisi na Serikali ya Burundi tunachofanya ni kuhamasisha,kuhimiza wale ambao wako na hiari warudi Burundi,baada ya kugundua amani imerejea Burundi,sasa tunapofanya hivyo wenzetu wanatafasiri kwamba tunawafukuza wakimbizi,hiyo sio sahihi,serikali ya Tanzania na wananchi wake kwa ujumla wamekua wakipokea wakimbizi kutoka nchi mbalimbali na hatujaanza leo tumekua tukiwahifadhi na amani inaporejea wanaomba warejee katika nchi zao” alisema Lugola

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri wa Mambo ya Ndani kutoka nchini Burundi,Pascal Barandagiye amesemaBurundi sasa ina amani na wameona ipo haja ya raia wake warejee ili kuweza kuijenga nchi yao.

“Tunawahakikishia kwamba kama nchi tuna uwezo wa kupokea warundi 2000 kwa wiki na sisi tutahakikisha warundi wote wanarejea nyumbani,tutawafuata popote walipo,tunawahitaji warudi nyumbani ili tuje tujenge nchi yetu pamoja,” alisema Barandagiye

Kwa upande wa Kamishna Msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi(UNHCR),George Okoth Obbo alisema wameshirikiana na nchi mbili za Tanzania na Burundi katika kuhakikisha yanakuwepo mazingira salama na yenye utu katika uendeshaji wa zoezi hilo huku akiwashukuru Watanzania kwa mwema wao wa kuendelea kuwapokea wakimbizi.

“Tanzania imekua nchi rafiki kwa wakimbizi,mawaziri wote wawili wamekubaliana suala la kurudi wa warundi nchini kwao,tuko hapa kuhakikisha zoezi hilo litaenda salama likizingatia ustawi wa pande zote tatu” alisema Okoth

Ni takribani mwezi mmoja umepita tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Magufuli kwenye ziara yake katika mkoa wa Katavi kuagiza pande zote zinazohusiana na masuala ya wakimbizi wakutane ili kuweza kujadili suala la warundi wanaojiandikisha kwa hiari kurudi nchini kwao,akiwaambia umefika wakati sasa wakurudi katika nchi zao kwenda kuzijenga   huku akiwaonya wakimbizi wanaoshiriki katika matukio ya uhalifu hapa nchini.


Share:

BABU WA MIAKA 104 MWENYE WATOTO NA WAJUKUU 70 AFUNGUA SHULE


Mzee Laibon, Mfugaji mwenye watoto zaidi ya 60 na wajukuu zaidi ya 70

Mzee Meshuku Mapi Mukari almaarufu mzee Laibon, kutoka jamii ya kifugaji, mwenye umri wa miaka 102 na wake wapatao nane, watoto zaidi ya 60 na wajukuu zaidi 70, amesema kuwa licha ya kuwa na idadi kubwa ya watu nyumbani kwake, lakini wameweza kuishi kwa amani bila migongano yoyote.

Mzee Laibon ni Mkazi wa Kijiji cha Esilalei, wilayani Monduli, mkoani Arusha, anasema kuwa amelazimika kufungua Shule ambayo itaweza kuwa mkombozi kwa wajukuu zake na wale watoto wanaoishi jirani na eneo hilo, ambayo imechagiza hamasa ya elimu katika jamii hiyo ya kifugaji, ambayo kwa muda mrefu imekuwa nyuma katika masuala ya elimu.

Akizungumza na EATV, Mwalimu Abel Langa, ambaye ni mmoja ya walimu katika Shule iliyoanzishwa na Mzee Laibon, amesema muitikio wa elimu katika jamii hiyo, umeendelea kuwa mkubwa na hii imetoa hamasa kubwa ya elimu kwa jamii hiyo.

Aidha katika hatua nyingine, familia ya Mzee Laibon, imeanza kufuata na kuabudu imani ya Kikristo na kuachana na baadhi ya mila potofu kama vile ukeketaji na unyanyasaji wa kijinsia.
Chanzo - EATV
Share:

Picha : LINDI WAZINDUA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI


Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (wa pili kulia) akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano akiwa ameambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Godfrey Zambi (kushoto) pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi. Wengine katika picha ni Mstahiki Meya wa Lindi mjini Ndugu Mohamed Liumbwe pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg.Shaibu Issa Ndemanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa na kutambulisha meza kuu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Godfrey Zambi akitoa salamu kwa mgeni rasmi pamoja na wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya kuzindua wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk.Tausi Kida Dk. Hoseana Lunogelo akitoa salamu za ESRF kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo wakati wa hafla ya kuzindua wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mkuu wa Ukuaji wa Maendeleo Jumishi na Mtaalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Miradi ya Maendeleo (UNDP), Ernest Salla akitoa salamu za UNDP kwa niaba ya Mwakilishi Mkaazi wa UNDP nchini Tanzania.Bi. Christne Musisi wakati wa hafla ya kuzindua wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk.Tausi Kida Dk. Hoseana Lunogelo akikabidhi Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi kwa mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa tayari kuzinduliwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa mwongozo huo wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (wa pili kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi sambamba na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Godfrey Zambi wakati wa hafla ya uzinduzi wa mwongozo huo uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg.Shaibu Issa Ndemanga pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (katikati) akionyesha nakala za Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi mara baada ya kuzindua rasmi wakati wa hafla iliyofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg.Shaibu Issa Ndemanga, Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge Mstahiki Meya wa Lindi mjini Ndugu Mohamed Liumbwe pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg.Shaibu Issa Ndemanga.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akikabidhi nakala ya Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi kwa Mkuu wa Ukuaji wa Maendeleo Jumishi na Mtaalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Miradi ya Maendeleo (UNDP), Ernest Salla wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo huo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akikabidhi nakala ya Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi kwa Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) - Utalii na Huduma za Biashara Bw. Imani Nkuwi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo huo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mtafiti Mwandamizi wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo (kulia) pamoja na Mtafiti mshiriki kutoka ESRF Musa Martine wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mwekezaji wa hoteli za fukwe za bahari mkoani Lindi Bw. Sultan Ahmed kutoka Kilwa akitoa ushuhuda kuhusu fursa zilizopo ndani ya mkoa wa Lindi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Pichani juu na chini ni sehemu ya wageni waalikwa walioshiriki hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa na meza kuu wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wakuu wa wilaya za Lindi na Wilaya za Mtwara wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa na meza kuu wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wadau waliowekeza kwenye mkoa wa Lindi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa na meza kuu wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wadau kutoka ESRF, UNDP, Equinor, Shell, taasisi mbalimbali za serikali na sekta binfasi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa na meza kuu wakiwa kwenye picha ya pamoja na kamati ya maandalizi ya mkoa wa Lindi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji wa mkoa wa Lindi uliofanyika katika hoteli ya Sea View Beach Resort mkoani Lindi.
****
Na Mwandishi Wetu, Lindi

MKOA wa Lindi umezindua Mwongozo wa Uwekezaji mkoani humo ambao umeanisha fursa za uwekezaji zilizopo Lindi ili kuvutia wawekezaji kwa lengo la kukuza uchumi wa mkoa na kuimarisha pato la mtu mmoja mmoja na taifa. Mwongozo huo umezinduliwa tarehe 27 Novemba 2019 na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa.

Mwongozo huo umeandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na wataalam wa Mkoa wa Lindi chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

Akizindua mwongozo huo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa alitaka fursa hizo zilioanishwa kutekelezwa kimkakati ili kuongeza kipato cha wananchi na Mkoa wa Lindi.

Alisema mkoa wa Lindi umefanyakazi kubwa ya kuongeza kilimo cha korosho na ufuta na kusema hiyo ni fursa kubwa kama ilivyo katika utalii kutokana na kuwa na misitu mingi ya hifadhi na fukwe nzuri zaidi za kitalii nchini na duniani. Alisema inawezekana pia kuanzisha siku maalum ya kula nyama pori wilayani Kilwa ili kuchochea utalii.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi M kuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi alisema Kongamano la Biashara na Uwekezaji lililoandaliwa na Mkoa kwa kushirikiana na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Machi mwaka huu limeleta wawekezaji wa ndani na nje ya mkoa kuja kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Alisema Chuo cha Usafirishaji (NIT) jijini Dar es Salaam ni kati ya taasisi zilizoonesha nia ya kuwekeza na kimepewa ekari 150 za ardhi bure kwa ajili ya Chuo cha Kujenga Boti na Meli. Mwekezaji mwingine ni Sarah Masasi anayetaka kujenga Kiwanda cha kubangua korosho na amepatiwa ekari 50 bure za ujenzi huo.

Alisema kampuni ya kimataifa ya Norway inatarajia kuwekeza kituo cha sayansi, ufugaji na kilimo na kampuni kutoka India kuwekeza kwenye uvuvi. Hakutaja majina ya kampuni. Aidha kampuni kutoka Ujerumani, Filloship inafanya mazungumzo kuwekeza mkoani hapa.

Katika hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, kampuni za mafuta na gesi za Equinor, Shell, wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji wa halmashauri za wilaya na manispaa, taasisi za umma, wawekezaji na sekta binafsi, Zambi alisema kutokana na kongamano hilo walianzisha ofisi ya uratibu wa uwekezaji.

''Tunaishukuru TSN (wachapishaji wa magazeti ya HabariLEO, Daily News na SpotiLeo) kutufungulia mlango kupata wawekezaji Marekani, Ujerumani, India na nchini,'' alisema Zambi. Pia, aliwashukuru Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Lindi.

Alisema kuna miradi mikubwa ambayo inashughulikiwa na serikali kuu hapa mkoani ikiwa ni pamoja na mradi wa kiwanda cha mbolea Kilwa. Mkoa una fursa ya kuwa na kiwanda cha usindikaji chumvi, utengenezaji wa mvinyo kw akutumia korosho, viwanda vya vifungashio, viwatilifu, kubangua korosho na usindikaji wa mafuta ya nazi, alizeti, nishati mbadala nk.

Aidha alisema kwamba fursa katika ngazi ya halmashauri ni pamoja na makundi madogo ya wachambuaji korosho, misitu na utalii na pia kuongeza mnyororo wa thamani katika bidhaa mbalimbali za Kilimo katika ngazi za wilaya na halmashauri.

Alisema kuna utajiri mkubwa wa urithi wa utamaduni na wanamatarajio taaaisi za kitaifa kama Tawa zitasaidia kuwepo na utalii unaowezesha kuchangia kwa kiasi kikubwa pato.

Katika masuala ya uwekezaji katika utalii, mmoja wa wafanyabiashara mkoani Lindi, Sultani Ahmed Sultani alizungumzia kwa kina katika mada yake namna bora ya kuwezesha sekta ya utalii akitaka sekta binafsi kuwezeshwa ili kushiriki katika nafasi hiyo.

Alisema Lindi ina nafasi kubwa ya kuleta watalii kutoka kaskazini na Kusini mwa Afrika kupitia mpango maalumu unaoweza kuungwa na Zanzibar na matunda yake yataonekana.

Dkt. Hoseana Lunogelo, Mtafiti Mwandamizi akizungumzia Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Lindi kwa niaba ya Dkt. Tausi Kida, Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), alisema watafiti wake wameona fursa nyingi sana na ziko katika sekta na ngazi zote.

“Kwa hapa Lindi fursa kubwa ipo kwenye mnyororo wa thamani wa zao la Korosho, utalii na madini bila kuisahau gesi. Pia kuna fursa nyingi katika Sekta ya Viwanda, Kilimo, Uvuvi, Miundombinu na Huduma. “ alisema Dk Kida katika hotuba yake iliyosomwa na Dkt. Lunogelo.

Alisema fursa hizo zilizoainishwa katika mwongozo zikitumika vizuri zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha maisha ya wananchi.

Mpaka sasa ESRF imesaidia Mikoa 24 kuandaa Miongozo ya Uwekezaji ambapo mikoa 14 imekamilisha na Mikoa 10 iko katika hatua mbalimbali. ESRF tayari imeanza kusaidia zoezi hili katika mikoa iliyobaki.

Naye Bw. Ernest Salla akitoa neno kwa niaba ya Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Christine Musisi ameisihi mikoa iliyokwisha tengenezewa miongozo kuhakikisha kwamba wanafanyaia kazi miongozo hiyo ili kuleta tija.

Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Bw. Ernest Salla alisema kwamba baada ya kuzinduliwa kwa amwongozo ipo haja kwa mkoa wa Lindi sasa kuangalia vipaumbele na kuchambua vilivyotayari ili kuyafanyiakazi kwa haraka.

Aidha hatua nyingine ya pili ni kutangaza fursa zilizopo na kuandaa mikutano ya uwekezaji kwa kuwakutanisha wawekezaji. Pia watumishi wanaoshughulikia uwekezaji ni vyema wakaandaliwa kusaidia kusukuma mbele gurudumu hilo na kutayarisha nyaraka mbalimbali kielektroniki ili kila mmoja aweze kuzipata.

Pia aligusia haja ya kuhakikisha fursa hizo zinatambuliwa kwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na mabalozi wetu nje ili kuuza fursa hizo na kutafuta mitaji ili kuiwezesha sekta binafsi inashiriki kikamilifu.

Mwakilishi Mkazi wa UNDP alisema shirika lake litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania na ESRF katika kuhakikisha kwamba wanakamilisha kutengeneza Miongozi kwa mikoa iliyobaki.

Share:

Taasisi Ya Saratani Ocean Road Yazidi Kuimarisha Huduma Zake Kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
SERIKALI kupitia Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) imenunua na kusimika mashine mbili za kisasa za huduma ya uchunguzi na tiba za kutibu saratani aina ya LINA na CT Simulator zenye thamani ya Tsh Bilioni 9.5/-  hatua inayolenga kupunguza muda wa kusubiri tiba mionzi kutoka wiki sita hadi kufikia wiki mbili.

Hayo yamebainishwa  leo Jumatatu (Desemba 2, 2019) Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dkt. Julius Mwaiselage  wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya ORCI katika kipindi cha miaka minne ya Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano unaoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.

Dkt. Mwaiselage alisema mashine hizo za kisasa zinazotumia teknolojia ya 3D zinapatikana katika hospitali yoyote kubwa ya saratani duniani kama India, Ulaya na Marekani, ambapo tangu mashine hizo zianze kutoa huduma za uchunguzi na tiba mwezi Septemba 2018 tayari wagonjwa 1,141 wamepatiwa matibabu.

‘’Kwa wagonjwa 1,141 waliotibiwa kwa kipindi hicho, takribani wagonjwa 208 wangepelekwa nje ya nchi kama  mashine hizi zisingekuwepo na hivyo Serikali imeweza kuokoa Tsh. Bilioni 10.4 ambazo zingetumika kutibu wagonjwa hao nje ya nchi ambapo mgonjwa mmoja hugharimu Tsh Milioni 50’’ alisema Dkt. Mwaiselage.

Dkt. Mwaiselage alisema mshine ya CT Simulator imesaidia kuanzisha huduma za kupima CT Scan katika taasisi hiyo ambapo hadi kufikia mwezi Septemba mwaka huu, jumla ya wagonjwa 1,430 walikuwa wamepata kipimo cha CT Scan, hivyo kupunguza usumbufu kwa wagonjwa ambao walitakiwa kwenda hospitali nyingine kupata huduma hiyo.

Kuhusu rufaa za wagonjwa kwenda nje ya nchi, Dkt. Mwaiselage alisema katiks mwaka 2015, jumla wagonjwa 164 wa saratani walipatiwa rufaa kwenda nje ya nchi, lakini baada ya kuboresha huduma za saratani nchini, kuanzia  mwaka 2018 hadi 2019 ni wagonjwa 39 pekee waliosafirishwa nje ya nchi, ambapo wagonjwa hao wengi walikuwa wakienda nje kwa upasuaji na tiba mionzi ya kisasa.

Akibainisha mafanikio mengine, Dkt. Mwaiselage alisema ORCI pia imekarabati wodi mbili za kutolea tiba kemia ikiwemo kufungwa viyoyozi na kununua vitanda maalum vya kutolea tiba kemia hivyo kuongeza utoaji wa tiba kemia kutoka wagonjwa 40 kwa mara moja hadi wagonjwa 100 kwa mara moja, ambapo awali huduma hiyo ilikuwa inatolewa katika wodi 1 pekee.

‘’Kuongezeka kwa wodi na vitanda imesaidia kupunguza muda wa kuanza tiba kemia kutka siku 10 hadi tatu pekee, ikimaanisha mgonjwa anaweza kuanza tiba ndani ya siku tatu kama majibu ya vipimo vyake vyote vitakuwa sawa kupata tiba hiyo’’ alisema Mwaiselage.

Aidha Dkt. Mwaiselage anasema Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamiii, Jinsia na Wazee na Watoto imewezesha kuimarisha uhakika wa upatikanaji wa dawa kutoka asilimia 4 mwaka 2014/15 hadi kufikia  asilimia 95 mwaka 2018/19, na upatikanaji wa dawa upo kwa asilimia 100 kwa wagonjwa wenye saratani za mlango wa kizazi, matiti, Kaposi sarcoma, tezi dume, njia ya chakula, kooni, damu, matezi, ngozi na kibofu cha mkojo.

Akifafanua zaidi Dkt. Mwaiselage alisema asilimia 5 ya dawa  zinazopungua, hupatikana katika Duka la Dawa la Jamii la Taasisi ililolianzisha ili kuimarisha upatikanaji wa dawa za saratani na dawa zake hupatikana kwa bei nafuu sana ulikinganisha na maduka mengine ya binafsi.

Dkt. Mwaiselage alisema kuwa kutokana na kuimarika kwa huduma za saratani katika taasisi hiyo, wagonjwa kutoka nchi jirani za Kenya, Comoro, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na Burundi wameongezeka kuja kupata huduma za tiba saratani na hivyo kuongeza mapato ya Taasisi kwani wananchi wasio raia wanalipia huduma hizo.

MWISHO



Share:

Waziri Simbachawene aiagiza TAREA kutafiti matumizi nishati jadidifu Dar, Ataka mataifa yasimwage TV na Friji mbovu Afrika

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Simbachawene, ameiagiza Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA) kufanya utafiti katika Jiji la Dar es Salaam ili kubaini kiasi cha matumizi ya nishati jadidifu.

Alitoa agizo hilo wakati akifungua Maonesho ya 14 ya Kitaifa ya Siku ya Nishati Jadidifu yaliyofanyika Mnazi Mmoja, Dar es Salaam yakiwa na kauli mbiu: “NISHATI JADIDIFU KUFIKIA TANZANIA YA VIWANDA 2025” yaliyoandaliwa na TAREA na kufanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Dar Salaam.

Aidha, ameyataka mataifa yaliyoendelea kuacha kuleta bidhaa chakavu za kielektroniki zikiwamo runinga na friji katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania kuacha kwa kuwa ni majanga.

Alikuwa akijibu risala ya TAREA iliyosomwa kwake na Makamu Mwenyekiti wa TAREA, Mhandisi Prosper Magali aliyesema licha ya TAREA na wadau mbalimbali kuhamisisha matumizi teknolojia ya nishati jadidifu, zipo changamoto kubwa za kudhibiti taka zitokanazo na bidhaa za kielektroniki zikiwamo runinga na friji.

Simbachawene alisema inasikitisha kuona vifaa vilivyotumika na kuchakaa katika mataifa yaliyoendelea bado zikiwamo friji na TV bado zinaletwa katika mataifa yaliyoendelea ikiwamo Tanzania.

Akasema: “Kwa nchi zilizoendelea, kama kitu ni kibaya, tusikitumie wote; tusione ni kibaya tukapeleka Afrika maana madhara yake tabaka la ozini ni makubwa. Uchafuzi wa hali ya hewa husababisha kumomonyoka kwa tabaka la ozoni na kubadilika kwa tabianchi huathiri watui wote.”

Alisema serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira, imeandaa kanuni mpya za udhibiti na usimamizi wa taka hatarishi za mwaka 2019 zilizoanza kutumika Septemba mwaka huu.

“Kanuni hizi zinasimamia taka hatarishi mbalimbali zikiwamo betri chakavu, hivyo serikali inawahakikishia kuwa itaendelea kusimamia kanuni hizo ipsavyo ili kudhibiti uchafuzi unaoweza kutokea na utupaji usio salama,” alisema na kuongeza kuwa, matumizi ya niashati ya kuaminika na endelevu hayaepukiki kwa maendeleo ya taifa na kuelekea uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Simbachawene alisema: “Mafanikio katika sekta zote za uchumi, huduma za jamii na maendeleo yanategemea upatikanaji wa kuaminika na endelevu wa nishati ya kutosha usiokuwa na madhara katika mazingira.”

Alisema sekta ya viwanda kutumia fursa hiyo kujipatia umeme katika vyanzo vya nishati safi na nafuu kwa shughuli za viwanda kwa mifumo na kazi kama kuchemsha mahji, kuvuta maji kwa ajili ya umwagiliaji na majiko sanifu kwa taasisi za umama kama shule na majeshi.

“Natoa mwito kwa taasisi za umma kama majeshi, magereza, hospitali, shule na vyuo kuingia katika matumizi ya teknolojia ya nishati jadidifu maana miti mingi inakatwa na magereza na shule hivyo, uharibifu wa mazingira ni mkubwa,” alisema

Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Jeroen Verheul alisema ili teknolojia ya nishati jadidifu isambae na kutumika zaidi kwa umma, lazima kuwepo mazingira rafiki zaidi ya kisera na kisheria na kwamba, sula hjili linahitahji ubia wa dhati.

Alisema nchi yake itaendelea kushitrikiana na Tanzania katika kusaidia matumizi ya teknolojia ya nishati jadidifu am,bayo ni msaada katika mapambano ya kidunia dhidi ya majanga yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi.

Awali, Mhandisi Magali ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa TAREA na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya maonesho hayo, alimwambia waziri kuwa, licha ya TAREA na wadau mbalimbali kuhamisisha matuimizi yteknolojia ya nishati jadidifu, zipo changamoto kubwa za kudhibiti taka zitokanazo na bidhaa za kielektrponiki zikiwamo runinga na friji.

“Taka za kielektroniki zimeendelea kuongezeka na tupo kwenye hatari kubwa ya uchafuzi wa mazingira kupitia taka hizi,” alisema magali.

Akaongeza: “Tunaomba Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira kukamilisha utungaji wa sheria za kusimamia biashara ya taka za kielektroniki ili kuwezesha shughuli za urejelezaji wa taka hizo ili kuhifadhi mazingira”.


Share:

Watu 1,252,205 Wanaishi Na Virusi Vya Ukimwi Nchini Tanzania

Na.WAMJW-Mwanza
Mpaka kufikia mwezi Septemba 2019 takribani watu 1,252,205 kati ya wananchi 1,600,000 wanaokadiriwa kuishi na VVU nchini walikuwa wamepima na kufahamu hali zao za maambukizi ya VVU.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Ummy Mwalimu wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya UKIMWI duniani kitaifa yaliyofanyika jijini Mwanza.

“Hii ni sawa na asilimia 78.3 ya lengo la 90 ya kwanza.
Miongoni mwao wanaume walikuwa 413,985 sawa na asilimia 33, na wanawake walikuwa 838,220 sawa na asilimia 77″.

Kwa upande wa vijana Waziri Ummy amesema kuwa Vijana balehe (umri wa miaka 10 – 19) walikuwa 57,167 sawa na asilimia 4.6, na vijana (umri wa miaka 15 – 24) walikuwa 96,006 sawa na asilimia 7.7.

Aidha, amesema kati ya waliopima na kutambua afya zao watu 1,221,799 sawa na asilimia 97.6 wanatumia ARV.

Hata hivyo alisema Lengo la 90 ya pili ambalo ni asilimia ya kuwa watu waliopimwa na kugundulika kuwa wana maambukizi ya VVU wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU (yaani ARV’s), tayari tumefikia takriban asilimia 98 wanatumia zawa za kupunguza makali ya VVU yaani ARV.

“Lengo la 90 ya tatu, ambalo ni kuhakikisha kuwa asilimia 90 ya wanaotumia ARV’s wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini Waziri huyo alisema wamefanya vizuri sana,”ni kuwa tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hali za watu wanaotumia dawa za kupunguza makali ya VVU”.Alisema

Waziri Ummy alitaja mafanikio mengine ya kujikinga dhidi ya maambukizi ni tohara kwa wanaume ambapo kuanzia mwaka 2009 hadi Agosti 2019 jumla ya wanaume 4,456,511 wamefanyiwa tohara kupitia njia za mkoba na huduma katika vituo vya huduma

Takwimu zinaonesha kwamba watu 953,973 sawa na asilimia 89 ya watu 1,072,650 waliopimwa wingi wa VVU wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini jambo ambalo ni muhimu katika kinga dhidi ya UKIMWI.Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Jamii ni chachu ya mabadiliko,tuungane kupunguza maambukizi mapya ya VVU”


Share:

Hage Geingob Achaguliwa Tena Kuwa Rais wa Namibia.....Umoja wa Afrika Watoa Neno, Rais Magufuli Ampongeza

Rais wa sasa wa Namibia Hage Geingob ameshinda kwa muhula wa pili licha ya kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa idadi ya wapiga kura wanaomuunga mkono. Rais Geingob amepata  ushindi wa asilimia 56.3  ikilinganishwa na asilimia 86.7 ya mwaka 2014.

Tume ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Umoja wa Afrika (AUEOM) imesema uchaguzi huo umefanyika kwa kufuata sheria za ndani na kukidhi vigezo vya kimataifa.

Taarifa iliyotolewa  na tume hiyo imepongeza serikali na watu wa Namibia kwa kufanya uchaguzi mkuu kwa amani, na kusema uchaguzi huo uliofanyika Novemba 27 umewapatia watu wa Namibia fursa ya kuwa na uhuru wa kueleza maoni yao.

Tume hiyo pia imeipongeza serikali ya Namibia kwa kuidhinisha Katiba ya Afrika kuhusu Demokrasia, Chaguzi na Utawala iliyopendekezwa na Umoja wa Afrika kufuatia uchaguzi mkuu wa mwaka 2014. 


Rais wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli ni miongoni mwa Marais waliotuma salamu za Pongezi kwa   Hage Geingob kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais ya Namibia kwa Muhula wa Pili.

"Hongera sana Mhe. Rais Hage Geingob. Your re-election is clear testimony of the trust and confidence that Namibians have bestowed on you. I wish to assure you of our continued support to further strengthen the historical ties between our two brotherly countries."Ameandika Rais Magufuli kupitia ukurasa wake wa Twitter


Share:

DKT :ANASTAZIA JAMII BADO HAIJABADILIKA KUWANYANYAPAA KWA WATU WANAIOSHI NA VVU

Share:

Waziri Mhagama Akagua Maandalizi Ya Sherehe Za Uhuru Mwanza.

NA.MWANDISHI WETU
Maandalizi ya maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru yamefikia hatua za kuridhisha huku Serikali ikieleza kuwa sherehe hiyo itapambwa na onesho maalum la Jeshi la Jadi la sungusungu kutoka Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameeleza itakuwa ni mara ya kwanza kwa jeshi hilo kuonesha namna wanavyofanya kazi za ulinzi katika maeneo yao ili kuendelea kuenzi nia ya Rais wa Awamu ya Tano Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli ya kuilinda amani na utulivu uliopo nchini.

Waziri alieleza hayo mapema Novemba 30, 2019 alipotembelea na kukagua maandalzii ya onesho hilo yanayoendelea katika Kijiji cha Hunghumalwa Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

“Hii itakuwa ni mara ya kwanza kuwa na onesho hili maalum ambalo linatukumbusha nia ya Mhe. Rais ya kuilinda amani iliyopo na kuhakikisha haichezewi kwa gharama yoyote na kuona namna tunavyojivunia jeshi hili lililoundwa katika misingi na maadili mema ya amani na utulivu,” alisema waziri Mhagama

Aliongezea kuwa, Jeshi hilo litajumuisha zaidi ya sungusungu 1300 watakaoshiriki kwa siku hiyo kwa kuongozwa na Manji wao pamoja na Mtemi wa Wilaya Mogan Shimbi.

Sambamba na hilo maandalizi mengine ikiwemo, uandaaji wa uwanja wa CCM Kilumba, mazoezi ya Majeshi (Gwaride), Usafi wa mazingira pamoja na vikundi vya burudani yanaendelea mkoani hapo.

“Maandalizi muhimu ikiwa ni pamoja na marekebisho ya miundombinu katika uwanja yanaendelea pamoja na maandalizi muhimu ikiwemo, kutoa mialiko, kuandaa  malazi kwa wageni, kuandaa vikundi vya ngoma za asili, kuandaa gwaride , kuandaa wanafunzi wa watakaoumba umbo la bendera, pamoja na nyimbo za kizazi kipya  na mahitaji mengine muhimu yapo katika hatua za kuridhisha,” alisema Waziri Mhagama

Aidha, kutakuwa na vikundi vya burudani ikiwemo; ngoma za asili kutoka mkoa wa Mara (Ritungu) na mkoa wa Mwanza, wimbo maalum kutoka Zanzibar pamoja na kwaya ya AIC Mwanza na bendi ya Tanzania One Theatre (T.O.T) vitatumbuiza.

Alifafanua kuwa maonyesho hayo yatakayofanyika Desemba 9 yatajumuisha gwaride maalumu la heshima lililoandaliwa na vikosi vya ulinzi na usalama nchini.

 “Watoto 3200 kutoka shule za msingi na sekondari za mkoa wa Mwanza wataonesha umbo la bendera ya Taifa letu,” alisema Waziri Mhagama

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella aliwasihi Watanzania kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuendelea kuilinda amani iliyopo kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu pamoja na kuendelea kuwa na uzalendo na kufanya kazi kwa bidiii kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

Pia, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo na kuendelea kujiandaa kwa bidii, usanifu na ubunifu wa kipekee katika kuiadhimisha siku hiyo muhimu.

“Ninamshukuru sana Mhe. Rais kwa kuelekeza maadhimisho haya kufanyika mkoani kwetu, niiwaase wananchi wa Mwanza kuitumia heshima tuliyopewa kwa kujitokeza kwa wingi katika siku hiyo ili kuunga mkono jituhada za Mhe. Rais wetu,” Alisisitiza Mongella.

Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri kwa mwaka huu (2019) kitaifa yatafanyika Mkoani Mwanza katika viwanja vya CCM Kilumba ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli na kupambwa na kauli mbiu inayosema “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Tifa letu”.


Share:

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Chashiriki Safari Ya Majaribio Ya Treni Ya Abiria Kutoka Dar Es Salaam Kwenda Moshi Kilimanjaro

Tarehe 1 Disemba 2019, Ndg. Humphrey Polepole Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameshiriki safari ya kwanza ya majaribio ya treni ya abiria kutoka Dar Es Salaam kwenda Moshi, Kilimanjaro.

Ndg. Polepole amesema kuanza kwa safari hii ya kwanza ya majaribio kutoka Dar es Salaam kwenda Moshi, Kilimanjaro ni sehemu ya Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020 katika eneo la usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo ambapo miradi mikubwa mitatu inatekelezwa kwa pamoja ikiwamo; ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa (standard gauge railway -SGR) kutoka Dar mpaka Makutopola, Dodoma awamu ya kwanza, maboresho makubwa ya reli ya kati kutoka Dar Es Salaam mpaka Isaka ili kuiongezea ufanisi na ubebaji mzigo mkubwa zaidi pamoja na ufufuaji na ukarabati mkubwa wa reli njia ya kaskazini inayojumuisha Mikoa ya Dar Es Salaam, Pwani, Tanga na Kilimanjaro awamu ya kwanza.

Treni hiyo ya abiria inayofanya safari yake ya kwanza ya majaribio tangu iliposimamishwa kutoa huduma hiyo miaka 25 iliyopita imevutwa na kichwa cha kisasa cha treni “9013 Classic” na imefunga mabehewa 9 yakiwamo mabehewa ya daraja la kwanza, daraja la pili, daraja la tatu, behewa lenye mgahawa unaotoa vyakula vya aina yote, vinywaji baridi na vikali pamoja na behewa la uendeshaji, usalama na usimamishaji wa treni.

Safari hii ya kwanza na ya kihistoria imeleta hamasa kubwa mno ambapo katika kila stesheni mamia ya wananchi walizuia treni kwa shangwe, nderemo na vifijo.

Ndugu Polepole amepongeza uongozi wa Shirika la Reli kwa kuipanga kwa mafanikio safari hii ya kwanza ya treni ya abiria na ametoa rai kwa vyombo vya ulinzi na usalama na Shirika kuimarisha ulinzi na kutoa elimu ya ujirani wema kati ya reli na jamii ziishizo pembezoni mwa reli ili kuitunza na kuilinda reli hii muhimu kwa maendeleo.

Pamoja na Ndg. Polepole Katibu wa itikadi na Uenezi wa CCM, watendaji wa Shirika la Reli wameongozwa na Ndg. Masanja Kadogosa, Mkurugenzi Mkuu wa TRC na Maafisa waandamizi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa usafiri wa ardhini (LATRA).

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)


Share:

John Heche Apigwa Mweleka Uchaguzi CHADEMA

Mbunge wa Tarime mjini, Ester Matiko amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti kwa kupata kura 44 na kumshinda Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche aliyepata kura 38.

Akitangaza matokeo hayo jana Jumapili, msimamizi wa uchaguzi huo, Boniface Jacob ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Ubungo jijini Dar es salaam alisema wajumbe 85 walipiga kura.

Katika uchaguzi huo, Gimbi Masaba alichaguliwa kwa kura 45 kuwa makamu Mwenyekiti huku Maendeleo Makoye akishinda uweka hazina kwa kupata kura 42.


Share:

Afya Moja Kutumika Kuimarisha Afya Ya Binadamu Kwa Magonjwa Ya Sokwe

Afya Moja ambayo ni dhana inayojumuisha sekta ya Afya ya binadamu, Mifugo, Wanyamapori na Mazingira katika kujiandaa, kubaini, kufuatilia na kukabili magonjwa yanayoathiri sekta hizo, hivi karibuni umezinduliwa  Mradi wa kimkakati wa kuimarisha udhibiti wa magonjwa ambukizi kati ya  binadamu na wanyama hususan Sokwe,  ujulikanao kama Bush to Base, mradi huo utatekelezwa mkoani Kigoma katika Halmashauri ya wilaya ya Uvinza kwa 18 vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa  milima ya Mahale.

 Lengo la mradi huo unaosimamiwa na kuratibiwa na  shirika lisilo la kiserikali la Bush-To-Base (B2B),  ni  kuongeza kasi ya ushirikiano kati ya Wizara za Kisekta na kuongeza uelewa wa dhana ya Afya Moja miongoni mwa wataalamu na wadau wengine wa sekta za afya ya wanyama, binadamu, kilimo na mazingira ili kuwa na mikakati shirikishi ya uchunguzi, utambuzi na udhibiti wa magonjwa.

Akiongea wakati wa kuzindua Mradi huo mkoani Kigoma, Katibu Tawala wa mkoa wa Kigoma, Rashid Mchatta alifafanua kuwa Mradi huo ni muhimu katika kuimarisha usalama wa afya ya wananchi wa mkoa wa Kigoma na taifa kwa ujumla kwa kuwa  Kume kuwa na mwingiliano mkubwa kati ya  watu na wanyama katika mazingira yao hivyo dhana dhana ya afya moja haina budi kutumika kwakuwa ni utaratibu ulioratibiwa kwa kushirikisha sekta zote za Afya.

“Kwa kuwa tafiti zinabainisha kuwa vimelea vingi vinavyo sabababisha magonjwa kwa binadamu zaidi ya 60% vinatoka  kwa wanyama pori na mifugo na maambukizi yanatokea pale binadamu anapoingilia maskani ya wanyama hao bila tahadhari, hatuna budi kuongeza ushirikiano na mawasilaino katika nyanja za afya ya binadamu, wanyama na mazingira ili kuwa na ufanisi katika kudhibiti magonjwa yanayoambukiza” alisistiza Mchatta.

Kwa upande wake Rais wa  shirika lisilo la kiserikali la Bush-To-Base (B2B), Dkt Teresa Sylvin amefafanua kuwa  mradi huo unajikita katika matokeo ya tafiti za kisayansi kuhusu afya ya Sokwe katika Hifadhi ya Taifa milima ya Mahale ambazo amezifanya kwa zaidi ya miaka 25.

“Kimsingi huu mradi unakusudia kutumia dhana ya afya moja kwa kutumia matokeo ya tafiti ili kuweza kuzishirikisha sekta za afya ya wanyama, binadamu, kilimo na mazingira ili kuwa na mikakati shirikishi ya uchunguzi, utambuzi na udhibiti wa magonjwa yatokanayo na Sokwe kwenda kwa binadamu. Lakini tunalenga kuishirikisha jamii ambayo inaishi katika mazingira ya mradi huu, naamini kwa kutumia afya moja tutafanikiwa ” alisema Dkt.Teresa

Mradi huo utakaotekelezwa kwa miaka mitatu mkoani Kigoma utakuwa ukifanya kazi za uratibu kwa kushirikiana na Ofisi yaWaziri Mkuu, Kupitia Dawati la Afya moja, tayari umepata ufadhili kutoka serikali ya Marekani chini ya Mfuko wa Sayansi na mwingine unajihusisha na Samaki na Wanyamapori.

MWISHO.


Share:

Video Mpya ya Rayvanny – Naogopa

Video Mpya ya  Rayvanny – Naogopa


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger