Thursday 31 October 2019

Job Opportunity at Coca Cola – Kwanza Limited, Warehouse Team Leader

WAREHOUSE TEAM LEADER (CCB191030-8) Closing date: 2019/11/12 Job Title WAREHOUSE TEAM LEADER Function Logistics, Warehouse & Distribution Company: Coca-Cola Kwanza (Tanzania) Job Type Permanent Location – Country Tanzania Location – Province Not Applicable Location – Town / City Dar es Salaam Job Description  Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Logistics Department. We are looking for a… Read More »

The post Job Opportunity at Coca Cola – Kwanza Limited, Warehouse Team Leader appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Business Performance Lead Job at Diageo Tanzania

Position: Business Performance Lead Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description : Are you looking to grow and develop as your role rapidly increases the value it brings to the organization? The finance functions within Diageo both at the headquarters and in markets has a mission to be great business partners driving great business performance‟. As business partners,… Read More »

The post Business Performance Lead Job at Diageo Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MWANAFUNZI APIGWA VIBOKO MPAKA KUFA DARASANI

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 14 huko nchini Burundi amefariki baada ya kupigwa na mwalimu wake, baba wa mtoto huyo ameiambia BBC.

Mtoto huyo, Chadia Nishimwe alipigwa viboko kwenye maeneo ya shingo na miguuni , kipigo ambacho kilimpelekea kutokwa damu puani na masikioni, alisema Jean-Marie Misago.

"Alikufa darasani mara baada ya kupigwa na mwalimu wake, na wakaenda kumtelekeza katika ofisi ya mwalimu mkuu," Bwana Misago alisema.

Mkuu wa shule alijaribu kumuwahisha hospitalini mtoto huyo wakati mtoto ameshakufa tayari, aliongeza baba huyo.

BBC imejaribu kutafuta taarifa zaidi katika sekta ya elimu bila mafanikio.

Mtoto huyo aliuwawa siku ya jumanne na kuzikwa siku hiyo hiyo .

Nchini Burundi, adhabu ya kuchapwa kwa mwanafunzi ni kinyume na sheria ingawa bado wanafunzi wanachapwa.
Chanzo - BBC
Share:

WANANCHI KIWALANI WAIPONGEZA SERIKALI KUWAJENGEA SOKO KUBWA...DC MJEMA ASISITIZA UBORA

Share:

DC MJEMA ATAKA WAFANYABIASHARA WALIOHAMA KATIKA VIZIMBA SOKO LA BUGURUNI NA KUFANYA BIASHARA NJE YA SOKO WARUDI MARA MOJA


Mkuu wa Wilaya  ya Ilala Mhe. Sophia Mjema amewataka wafanyabiashara wa soko la Buguruni waliohama katika vizimba na kufanya biashara nje ya soko kwa kigezo cha kuwa na Kitambulisho cha Ujasiriamali warudi mara moja.

Agizo hilo amelitoa Oktoba 30/2019 katika ziara yale kufuatia malalamiko ya baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo ambapo amesema wale watakaokaidi watachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha katika kuona suala hilo linafanyiwa kazi, amemuagiza Afisa masoko,Ally Baruani , kufanya kikao na wafanyabiashara hao mara baada ya ziara kumalizika ili kuwarudisha ndani ya soko kwani kitendo hicho kinainyima Manispaa mapato. 

Mkuu huyo wa wilaya amesema soko hilo lipo kwa ajili ya manufaa ya wafanyabiashara wote na sio kwa watu wachache.

"Kwa hili sitowasamehe, mnawaumiza wenzenu, kwaninni mkwepe ushuru wakati wenzenu wanalipa, nataka mrudi haraka na wasiotaka tunawachukulia hatua, " amesema Mjema.

Aidha amesema kutumia vitambulisho vya Mjasiriamali ni kosa kubwa kwani mfanyabiashara yeyote anayefanya sokoni kwa kupangiwa kizimba anapaswa kulipa ushuru kwa mujibu wa sheria za soko na utaratibu, kwani kutofanya hivyo kunaikosesha serikali mapato.

Amesema anatambua wote wafanya biashara lakini kila mfanyabiashara anatambulika kwa mujibu wa sheria na kanuni , hivyo wanaostahili vitambulisho vya Mjasiriamali na mlipa ushuru sifa zao zinatofautiana.

Mbali na wakwepa ushuru amewataka madalali wa biashara waache kuwakandamiza wafanyabiashara badala yake watumie mikataba katika makabidhiano yao ya kibiashara.

Aidha amesema wale madalali watakaoonekana wanakiuka Sheria wataondolewa katika soko hilo.

Kwa upande wa Mkurugenzi Manispaa ya Ilala Mhe. Jumanne Shauri, ameshauri kuwepo kwa mikataba maalumu ya kisheria kati ya mfanyabiashara na dalali ili kila mmoja kuweza kunufaika

Share:

Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning)

Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning) Job Title: Director – Monitoring, Evaluation and Learning Location: Dar es salaam Job Summary Pathfinder Overview: Pathfinder International is a global leader in sexual and reproductive health. We place reproductive health care at the center of all that we do—believing that it is not only a fundamental… Read More »

The post Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jinsi Ya Kuandika CV Nzuri Ambayo Itamvutia Mwajiri na Kukufanya Upate KAZI Kirahisi

WATU wengi nchini wamekosa ajira  kwa sababu ya makosa wanayoyafanya wakati wa kuandika CV zao.

Kumbuka,  makampuni  karibia yote yanayotangaza nafasi za kazi hupokea wastani wa maombi 200-500 ya kazi kwa tangazo moja la kazi. 

Hivyo, CV yako lazima ikae vizuri ili kumshawishi mwajiri. Utaratibu wa kuomba kazi unaweza ukawa tofauti kati ya makampuni na mashirika, ila yote yatahitaji uwatumie CV.

CV ni nini?
CV ni maelezo ya ujumla kwa kiundani ya historia yako ya kazi na shule. Kawaida, inatumika kwenye maombi ya kazi ya nafasi za kati, za juu na za utafiti.

Mambo yafuatayo yatasaidia kuifanya CV yako iwe bora na hivyo, kukusaidia kupata interview za kazi.

👉Soma na kuelewa maelezo ya kazi
Una ujuzi gani? Mwajiri anatafuta mfanyakazi wa aina gani? Maswali haya ni muhimu kujua kama utaiweza hiyo kazi au la. Pia, ni vizuri kujua nini hasa ni muhimu kwa muajiri na kufanya maombi yako yaendane zaidi na mahitaji ya mwajiri.

Kwa mfano, kama kazi inaweka umuhimu kwenye ujuzi wa kutumia mitandao ya kijamii kwa matangazo, hakikisha CV yako ina kazi zote zilizohitaji matumizi ya mitandao ya kijamii.

👉Andika maneno muhimu yaliyotumika kwenye maelezo ya kazi, uyatumie kwenye CV
Usichukue sentensi nzima kutoka kwenye maelezo ya kazi na ukaitumia vile vile kwenye CV yako. Ila, tumia lugha na baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye CV.

👉Fanya utafiti juu ya kampuni iliyotangaza kazi
Pamoja na kuchambua maelezo ya kazi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya kampuni yenyewe. Kama wana tovuti au wapo kwenye mitandao ya kijamii, jaribu kujua ni kazi gani na sekta ipi wanayohusika nayo. 

Pia, ikiwezekana jaribu kuwajua wafanyakazi/meneja wa kampuni hiyo. Hii itakusaidia kujua maadili na muelekeo wa kampuni. Hii itakusaidia kuweka maombi yako ya kazi yaendane na kampuni hiyo.

👉Orodhesha ujuzi wako wakufanya kazi
Hapa, usiweke kazi zote ulizozifanya maishani mwako ila, weka zile ambazo zilikuongezea ujuzi utakayo kusaidia kufanya kazi unayoomba.

==>Format/Staili inayotumika zaidi kwenye kuandika CV:
   1. Lengo la CV na ujuzi wako
    2.Ujuzi wako wa kazi
   3. Mafanikio maalum
   4. Elimu
   5. Ujuzi muhimu binafsi

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Angalizo:
  1.  Tumia maandishi ya kawaida ya Times New Roman
  2.  Tumia size 9 – 12 ya herufi
  3.   Hakikisha unatumia staili moja ya kuandaa CV kote
  4.   CV isiwe zaidi ya ukursasa 2
  5.   Usitumie sentensi ndefu
  6.  Hakikisha CV yako inasomeka kiurahisi na inawasilisha   mafanikio yako kwa uwazi.
  7.  Anza na kazi yako ya sasa hivi au ya hivi karibuni alafu rudi nyuma.
   ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 
   ==>.Hakikisha Yafuatayo:
1.Ukiwa unaandika jina la kampuni uliyo fanya kazi, andika jina la kampuni kikamilifu. 
2.Eleza kwa ufupi kampuni yao inahusika na nini. 
3.Tatu, weka muda uliyofanyakazi hapo (mwezi na mwaka).  
4.Baada ya hapo, orodhesha kazi na majukumu yako kwenye hiyo kampuni.
5.Usidanganye

👉Maandalizi ya Mwisho

1.Pitia kila kitu kwa mara ya mwisho
 -Print CV yako alafu ipitie. Hii huwa inasaidia kuona makosa yako.

2.Mpe Rafiki  yako apitie CV
-Muombe rafiki yako apitie CV yako. Macho manne ni bora zaidi ya mawili!

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Hatua ya kwanza kwenye kupata kazi unayotaka ni kutuma maombi. Tunatumaini kwamba maelezo yaliyoelezwa humu yatakusaidia kuandaa CV bora kwa ajili ya mwajiri.

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kuandika CV nzuri, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini.

AU 



Share:

Nafasi za kazi 2019 – Nafasi za ajira zilizotangazwa Leo- Jobs in Tanzania

Browse all latest Jobs Today  in Tanzania:  Here is the list of new jobs advertised in Tanzania, Apply Now!! JOB ADVERTISEMENTS FROM GOVERNMENT, TANZANIA NGOs AND INTERNATIONAL NGOs Tanzania Jobs in October (30-31), 2019 Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive Jobs Opportunities at Simba Logistics Limited Ltd (SLL)… Read More »

The post Nafasi za kazi 2019 – Nafasi za ajira zilizotangazwa Leo- Jobs in Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer

Background – ETDCO M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company (ETDCO) Limited) is a Subsidiary Company of TANESCO Limited established with the Objective of providing reliable electrical services for the TANESCO Transmission and Distribution Infrastructure countrywide and construction of new infrastructure for TANESCO and other companies within the country and beyond the borders. ETDCO Limited hereby… Read More »

The post Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive

Job Title: HR EXECUTIVE  Location: Arusha Job Summary Sense of Africa is a footprint brand of Tourvest Destination Management, a division of the Tourvest Integrated Group of Companies. Sense of Africa operates wholly owned offices in Kenya, Tanzania, Uganda, Namibia and Botswana. In keeping up with our current business needs, we are pleased to  announce the vacancy of… Read More »

The post Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Waziri Mpina Atangaza Neema Kubwa Kwa Wafugaji

Na Mwandishi Wetu, Katavi
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja.

Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote.

Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya saa moja kuhutubia huku akinyeshewa na mvua na kuwathibishia wananchi kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi kwa vitendo hasa katika sekta ya mifugo.

Alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 25 kipengele  inaiagiza Serikali kuhakikisha mifugo yote inaogeshwa ili kuweze kuzuia magonjwa yote yanayoenezwa na kupe ambapo asilimia 72 ya vifo vya mifugo vinasababishwa na kupe.

Hivyo uogeshaji huo utawezesha mifugo kujikinga na maradhi na vifo ambapo Serikali itaogesha michonyo milioni 38 kwa Ng’ombe, michonyo milioni 18 ya Mbuzi, michovyo milioni 7 ya Kondoo, na michovyo 2500 ya Punda hivyo utaliwezesha taifa  kupata mifugo bora ambayo haina magonjwa.

Waziri Mpina alibainisha kuwa katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja Serikali imekarabati majosho 400 na kwamba majosho yaliyobaki ambayo  hayajakarabatiwa ni 639 na kusisitiza kuwa yote yatakarabatiwa ili kuongeza kasi ya uogeshaji mifugo.

Waziri Mpina alisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa hivyo uamuzi wa Serikali kuogesha mifugo pia umelenga kupambana na magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Hivyo juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono na watendaji wote wa Serikali, wafugaji wote ili kuboresha afya za mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo ikiwemo nyama, maziwa na ngozi sambamba na kuwakinga wananchi na maradhi yanayoweza kuambizwa kutoka kwenye mifugo.

Kufuatia uzinduzi huo, Waziri Mpina ameagiza kila kijiji nchini kiwe na josho kwenye  vijiji vyote zaidi ya 12,000 ili kila kijiji kiweze kuogesha mifugo na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Magufuli itakuja na mkakati wa kuhakikisha kila kijiji kinapata josho kama sehemu ya kuboresha afya za mifugo.

Pia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha majosho yote yamekarabatiwa ndani ya mwezi mmoja na wizara itahakikisha inasambaza dawa kwenye majosho yote mabovu.

Aidha amesisitiza wanaokwenda kuogesha mifugo wafuate sheria za uogeshaji kuhakikisha mifugo inaogeshwa lakini kwa fedha ambayo Serikali imeitangaza ya sh 50 kwa kichwa na ng’ombe na sh 10 kwa kichwa cha mbuzi na zoezi hili litafanyika mfululizo kwa kipindi cha miezi 6 na kumuagiza  Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Madaktari ya Mifugo wa Mikoa, na Wilaya kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa vizuri kuhakikisha wananchi hawatapeliwi

Pia Waziri Mpina ameweka wazi kuwa Serikali itatangaza bei elekezi ya chanjo ifikapo 15 Novemba mwaka huu na hakuna mtu mwingine atakayekwenda kuwaibia wafugaji tena na kwamba  chanjo ya homa ya mapafu ya ng’ombe itauzwa kwa sh 350 tofauti na siku za nyuma ambapo walichanja kwa sh 2000 kwa kichwa cha ng’ombe.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Komredi Juma Homera amemhakikishia Waziri Mpina kuwa Serikali ya mkoa huo inatasimamia maagizo yote na kwamba hakuna mfugaji atakayeonewa au kudhulumiwa na kwamba bei elekezi iliyotangazwa ya sh 50 kwa kichwa ngombe na 10 kwa mbuzi italeta neema kubwa kwa wafugaji.

Pia kuhusu malalamiko ya wafugaji kupigwa faini kubwa kuuawa kwa mifugo yao amemkabidhi nyaraka za malalamiko hayo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi na kuwakamata watu wote waliotajwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hezron Nonga amesema zoezi hilo la ugeshaji litafanyika nchi nzima na kuwataka wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao ili kuikinga na maradhi.


Share:

Waziri Hasunga Awaasa Watumishi Wizara Ya Kilimo Kuwa Waadilifu

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Kilimo wameaswa kuwa waadilifu na kuzingatia ubora wa kazi wakati wanatoa huduma kwa wananchi.

Mwito huo umetolewa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) jana tarehe 30 Octoba 2019 wakati akizungumza na watumishi Jijini Dodoma alipotembelea ofisi za wizara hiyo eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mhe Hasunga amesema kuwa udilifu, nidhamu na weledi kwa watumishi wa umma ni kinga dhidi ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na ni moja kati ya njia zinazowawezesha watumishi wa umma kuwa wachapakazi hodari.

“Kiwango cha juu cha Ubora wa kazi zetu na utendaji wa kazi unaozingatia weledi vitaweza tu kufikiwa kwa kuajiri watumishi wenye sifa stahiki, maadili, na bidii ya kuchapa kazi na wanaoweza kwenda sambamba na kasi kubwa ya mageuzi katika wizara ya kilimo,” Alisisitiza Mhe Hasunga

Alisema kuwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yam  mwaka 2015-2020.

Amewataka watumishi hao kusimama imara katika kufanya kazi na kutumia weledi wao kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kwamba uadilifu ndiyo silaha muhimu katika kufanya kazi ya Umma.

Amesema mtumishi atakayetumia vibaya rasilimali za serikali atahesabika adui namba moja wa Serikali na eneo analofanyia kazi huku akibainisha kuwa mtumishi wa aina hiyo kamwe hatohamishwa badala yake ataachishwa kazi.

Ziara ya waziri wa Kilimo kukutana na watumishi hao ilikuwa na lengo la kusalimiana na kusikiliza changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi.


Share:

Watu Waliokutwa na tausi wa Ikulu wahukumiwa kulipa Milioni 6

Watu watatu wanaodaiwa kukutwa na ndege aina ya tausi wa Ikulu wamehukumiwa kulipa fidia zaidi ya Sh6.8 milioni baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya uhujumu uchumi kwa kujihusisha na nyara za Serikali bila kibali.

Kadhalika mahakama hiyo imetaifishwa ndege hao kuwa mali ya serikali. Pia imewaachia huru kwa masharti ya kutokutenda kosa ndani ya miezi sita.

Hukumu hiyo ilisomwa jana na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salumu Ally, baada ya washtakiwa kumwandikia Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) barua ya kukiri makosa yao.

“Mahakama hii inawaamuru washtakiwa kulipa fidia ya Sh. 6,890,000, ndege hao wanataifishwa kuwa mali ya serikali na inawaachia huru kwa masharti kwamba wasitende kosa la jinai ndani ya miezi sita,” alisema Hakimu Ally wakati akisoma hukumu hiyo.

Awali, washtakiwa walidaiwa kujihusisha na genge la uhalifu, kukutwa na nyara za serikali ikiwamo ndege aina ya tausi watatu wa Ikulu ya Tanzania.

Washtakiwa hao ni David Graha, Mohammed Hatibu na Mohammed Mahamoud, wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa hao walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Vick Mwaikambo.

Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, alidai kuwa shtaka la kwanza, kati ya Juni Mosi, 2015 na Oktoba 14, mwaka huu waliratibu mipango ya uhalifu kwa kujihusisha na biashara ya ndege hao wenye thamani ya Dola za Marekani 1,500 (sawa na Sh. 3,444,150).

Nchimbi alidai katika shtaka la pili, washtakiwa walikutwa na ndege watatu aina ya tausi wenye thamani hiyo ya fedha.


Wankyo alidai katika shtaka la tatu, Oktoba 14, mwaka huu eneo la Mikocheni, mshtakiwa wa tatu Mahamoud alikutwa na tausi hao.
 


Share:

Jafo Atolea Ufafanuzi Malalamiko Yaliyowasilishwa Kwenye Zoezi La Uchukuaji Na Urejeshaji Wa Fomu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo ametolea maelekezo malalamiko yaliyowasilishwa na wadau wa uchaguzi kuwa zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi za uongozi uzingatie Kanuni za uchaguzi na miongozo iliyotolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni Ofisini kwake Mtumba Jafo ameelekeza Wasimamizi/Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi, Vyama vya Siasa na wadau wengine woote kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi yake anazingatia masharti na miongozo iliyotolewa kuhusiana na uchukuaji na urejeshaji wa fomu.

Amebainisha baadhi ya malalamiko yaliyowasilishwa toka kwa vyama vya siasa kuwa ni kutokuwepo vituoni kwa baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi, baadhi ya wasimamizi kutofungua kwa wakati vituo vya kuchukulia fomu, mihuri na masuala mengine ya Kikanuni.

“Malalamiko yaliyopokelewa yanaendelea kufanyiwa kazi, hata hivyo wadau na vyama vya siasa wanapaswa kuwasilisha malalamiko yao kwenye kamati za rufaa zilizopo katika maeneo ya uchaguzi,” alibainisha.


Akieleza maendeleo ya uchaguzi huo jana jijini hapa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, alisema dosari zilizojitokeza ni chache kwenye baadhi ya mikoa.

Alisema katika Kata 3,959 ni kata 72 pekee ndizo amepokea malalamiko na kutaja maeneo machache kama vile Songwe, Lindi, Sengerema (Mwanza) na Moshi (Kilimanjaro).

Hata hivyo, Jafo alisema malalamiko kuhusu fomu zinazotolewa kwa wagombea kutogongwa muhuri, vyama vya siasa vinapaswa kufahamu kuwa, zitagongwa muhuri   pindi watakaporudisha au wakati wa uteuzi.

Kadhalika, alitoa msisitizo kwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi kuzingatia kanuni za uchaguzi kama zilivyowekwa.

Juzi, Waziri Jafo alitangaza wagombea kwenye uchaguzi huo kuanza kuchukua fomu kwenye ofisi za wasimamizi wa uchaguzi hadi Novemba nne mwaka huu.

Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Mtaa, Kitongoji, Kijiji, Wajumbe wa Kamati ya  Mtaa, Waju,mbe wa Serikali ya Kijiji.

Uchaguzi huo ambao ni wa sita tangu kuanza mfumo wa vyama vya siasa nchini, unatarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu ambapo wapigakura zaidi ya milioni 19 wanatarajiwa kushiriki



Share:

SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020

SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020 Sokoine University of Agriculture was established on the 1st July, 1984 by parliamentary Act No.6 of the same year, which was repealed by the Universities Act No.7 of 2005 from which the SUA charter was granted in 2007… Read More »

The post SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi October 31




Share:

WAZIRI MPINA ATANGAZA NEEMA KUBWA KWA WAFUGAJI UOGESHAJI WA MIFUGO

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akishirikiana na wafugaji kuingiza ng'ombe kwenye josho la Kijiji cha Kikonko wilayani Mlele mkoani Katavi wakati wa uzinduzi wa uogeshaji mifugo awamu ya pili na kutangaza ng'ombe mmoja sasa ataogeshwa kwa sh 50 tu badala ya sh 500 waliokuwa wanatozwa miaka ya nyuma.Picha na Mpiga Picha Wetu


Na Mwandishi Wetu, Katavi

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja.

Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote.

Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya saa moja kuhutubia huku akinyeshewa na mvua na kuwathibishia wananchi kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi kwa vitendo hasa katika sekta ya mifugo.

Alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 25 kipengele  inaiagiza Serikali kuhakikisha mifugo yote inaogeshwa ili kuweze kuzuia magonjwa yote yanayoenezwa na kupe ambapo asilimia 72 ya vifo vya mifugo vinasababishwa na kupe.

Hivyo uogeshaji huo utawezesha mifugo kujikinga na maradhi na vifo ambapo Serikali itaogesha michonyo milioni 38 kwa Ng’ombe, michonyo milioni 18 ya Mbuzi, michovyo milioni 7 ya Kondoo, na michovyo 2500 ya Punda hivyo utaliwezesha taifa  kupata mifugo bora ambayo haina magonjwa.

Waziri Mpina alibainisha kuwa katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja Serikali imekarabati majosho 400 na kwamba majosho yaliyobaki ambayo  hayajakarabatiwa ni 639 na kusisitiza kuwa yote yatakarabatiwa ili kuongeza kasi ya uogeshaji mifugo.

Waziri Mpina alisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa hivyo uamuzi wa Serikali kuogesha mifugo pia umelenga kupambana na magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Hivyo juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono na watendaji wote wa Serikali, wafugaji wote ili kuboresha afya za mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo ikiwemo nyama, maziwa na ngozi sambamba na kuwakinga wananchi na maradhi yanayoweza kuambizwa kutoka kwenye mifugo.

Kufuatia uzinduzi huo, Waziri Mpina ameagiza kila kijiji nchini kiwe na josho kwenye  vijiji vyote zaidi ya 12,000 ili kila kijiji kiweze kuogesha mifugo na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Magufuli itakuja na mkakati wa kuhakikisha kila kijiji kinapata josho kama sehemu ya kuboresha afya za mifugo.

Pia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha majosho yote yamekarabatiwa ndani ya mwezi mmoja na wizara itahakikisha inasambaza dawa kwenye majosho yote mabovu.

Aidha amesisitiza wanaokwenda kuogesha mifugo wafuate sheria za uogeshaji kuhakikisha mifugo inaogeshwa lakini kwa fedha ambayo Serikali imeitangaza ya sh 50 kwa kichwa na ng’ombe na sh 10 kwa kichwa cha mbuzi na zoezi hili litafanyika mfululizo kwa kipindi cha miezi 6 na kumuagiza  Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Madaktari ya Mifugo wa Mikoa, na Wilaya kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa vizuri kuhakikisha wananchi hawatapeliwi

Pia Waziri Mpina ameweka wazi kuwa Serikali itatangaza bei elekezi ya chanjo ifikapo 15 Novemba mwaka huu na hakuna mtu mwingine atakayekwenda kuwaibia wafugaji tena na kwamba  chanjo ya homa ya mapafu ya ng’ombe itauzwa kwa sh 350 tofauti na siku za nyuma ambapo walichanja kwa sh 2000 kwa kichwa cha ng’ombe.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Komredi Juma Homera amemhakikishia Waziri Mpina kuwa Serikali ya mkoa huo inatasimamia maagizo yote na kwamba hakuna mfugaji atakayeonewa au kudhulumiwa na kwamba bei elekezi iliyotangazwa ya sh 50 kwa kichwa ngombe na 10 kwa mbuzi italeta neema kubwa kwa wafugaji.

Pia kuhusu malalamiko ya wafugaji kupigwa faini kubwa kuuawa kwa mifugo yao amemkabidhi nyaraka za malalamiko hayo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi na kuwakamata watu wote waliotajwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hezron Nonga amesema zoezi hilo la ugeshaji litafanyika nchi nzima na kuwataka wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao ili kuikinga na maradhi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger