Tuesday 1 October 2019

Finance and Administrative Officer at Winrock International

Finance and Administrative Officer Tabora, Tanzani PROGRAM SUMMARY: The ARISE program is a high-quality, results-oriented program to prevent and help eliminate child labor through improved awareness of the hazards of child labor, greater livelihoods opportunities for vulnerable households, and improved access to education for children and youth. The position has an anticipated start date of September 1, 2019. This… Read More »

The post Finance and Administrative Officer at Winrock International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Naibu Waziri Mabula Ataka Majina Ya Watumishi Wa Ardhi Waliokacha Kwenda Mafia

Na Munir Shemweta, MAFIA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameagiza kupatiwa majina ya watumishi saba wa sekta ya ardhi awaliopangiwa kuhamia halmashauri ya wilaya ya Mafia mkoani Pwani lakini wameshindwa kuripoti katika kituo chao kipya cha kazi.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo jana mwamzoni mwa ziara yake ya siku mbili katika wilaya ya Mafia mkoani Pwani kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi, kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi kwa njia ya kielektroniki, kukagua Masijala ya ardhi pamoja na kutatua migogoro ya ardhi.

Kauli ya Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inafuatia kuelezwa na Mkuu wa wilaya ya Mafia Shaib Nnunduma kuwa wilaya yake ina mtumishi mmoja wa sekta ya ardhi jambo linaloifanya wilaya hiyo kushindwa kutekeleza majukumu ya sekta hiyo ipasavyo.

Dkt Mabula alisema, Wizara yake italifanyia kazi suala hilo mapema kwa kuwa ni vigumu wilaya kufanya kazi vizuri katika sekta ya ardhi kwa kutegemea mtumishi mmoja hasa ikizingatiwa sekta hiyo inahitaji kuwa na wapimaji, wathamini pamoja na wataalamu wa mipango miji.

‘’Mafia mna mtumishi mmoja wa sekta ya ardhi? Suala hili inabidi lifanyiwe kazi mapema na wizara yangu italifanyia kazi kuhakikisha wilaya inakuwa na watumishi wa njanja zote katika sekta ya ardhi’’ alisema Dkt Mabula

Awali Mkuu wa Wilaya ya Mafia Shaib Nnunduma alimueleza Naibu Waziri Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa, changamoto kubwa inayoikabili wilaya yake kwa upande wa sekta ya ardhi ni kukosekana watumishi wa kutosha ambapo wilaya hiyo imekuwa na mtumishi mmoja wa sekta hiyo kwa muda mrefu baada ya mtumishi mmoja wa Uthamini kupangiwa majukumu mengine.

Kwa mujibu wa Nnunduma, jitihada za wilaya yake kufuatilia upatikanaji Watumishi wa sekta ya ardhi zimeonekana kukwama kwa kuwa hadi sasa hawajapata mtumishi mwingine jambo linaloifanya wilaya hiyo kushindwa kutekeleza vyema majukumu ya sekta hiyo.

‘’Watumishi saba walipangiwa kuja Mafia lakini wameshindwa kuripoti na hapa unavyotuona tuna mtumishi mmoja, hatuna wataalamu kama wangekuwepo wangesaidia upangaji. Wilaya ni kama imesimama katika sekta ya ardhi’’ alisema Nnunduma

Nnunduma alisema, ujio wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaweza kuwa faraja kwao kupata watumishi kwa kuwa tangu kuteuliwa kwake na Rais John Pombe Magufuli kuongoza wilaya ya Mafia ndiyo anashuhudia Waziri wa kwanza wa sekta ya ardhi kwenda wilaya hiyo aliyoieleza kuwa kama itatumiwa vizuri basi itaiwezesha serikali kuingiza mapato mengi kupitia sekta ya utalii.

Mbunge wa jimbo la Mafia Mbaraka Dau alimueleza Dkt Mabula kuwa, pamoja na changamoto nyingine lakini Wilaya hiyo inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa la Baraza la Ardhi la nyumba  la wilaya jambo linalowalazimu wananchi kufunga safari hadi katika Baraza la Mkuranga kitu alichokieleza kinawafanya baadhi ya wananchi kushindwa kwenda na hivyo kupoteza haki zao.


Share:

Waziri Jafo Awataka Wakuu Wa Shule Kutojihusisha Na Udanganyifu Wa Mitihani.

Na  Faustine Gimu
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) SELEMANI JAFO  amewataka wakuu wa shule za msingi kutojihusisha na suala la udanganyifu wa mitihani kwa kuwa linaporomosha elimu ya Tanzania.
 
Waziri Jafo ametoa agizo hilo  jana jijini Dodoma wakati akifungua mkutano mkuu wa kwanza wa wenyeviti wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania Bara.
 
Amesema wao wanadhamana kubwa katika kusimamia sekta ya elimu nchini hivyo ikitokea uvujaji wa mitihani hauleti picha nzuri katika Taifa.

Akizungumzia suala la elimu bila ya malipo amesema matumizi ya fedha hizo yameimarika tofauti na ilivyokuwa mwanzo walipoanza ambapo kulijitokeza changamoto mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania bara(Tapsha), REHEMA RAMOLE ameipongeza serikali kwa uboreshaji wa miundombinu jambo ambalo limepunguza msongamano wa wanafunzi darasani.
 
Kauli mbiu ya mkutano huo inasema Uwajibikaji na Usimamizi makini wa Rasilimali katika elimu ndio Msingi wa Elimu Bora.



Share:

Rais Magufuli Kafanya Uteuzi wa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa na Wilaya




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne October 1




Share:

Monday 30 September 2019

Waziri Lugola Aagiza Askari Wote Kituo Cha Polisi Wahamishwe

Na Felix Mwagara, MOHA-Katavi
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Katavi, kuwahamisha askari wote wa Kituo cha Polisi Majimoto kutokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili askari hao.

Waziri Lugola alitoa agizo hilo jana kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi wa Mji wa Majimoto, Wilaya ya Mlele wakati akijibu kero mbalimbali za wananchi.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Lugola alisema kero zilizowasilishwa na wananchi hao, zinaonyesha askari wa kituo hicho wanajihusisha na vitendo mbalimbali vya rushwa, kupiga wananchi ovyo, kushindwa kudhibiti ulinzi na usalama pamoja na kushughulikia malalamiko ya wananchi.

“Natoa agizo hili liwe fundisho kwa askari wote wasiowaaminifu kote nchini, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huu natoa siku saba askari wote wa kituo hiki wahamishwe na waletwe wengine ili wajifunze,” alisema Lugola.

Baada ya agizo hilo, waendesha bodaboda na wananchi wengineo, walishangilia na kusema kuwa mji huo sasa utatulia kutokana na uwepo wa amani bila kuwa na manyanyaso.

Mmoja wa wananchi aliyetoa malalamiko dhidi ya polisi katika kituo hicho ni Malewe Maswe, alilalamikia kuwa baadhi ya askari hao walimpiga na kumsababishia maumivu makali ya miguu kutokana na kuhoji kosa lake la kuletwa kituoni hapo baada ya kugombana na mwalimu mmoja katika mji huo.

“Tulikuwepo na Mwalimu niliyegombana naye kituoni hapo, askari wakaniambia nendeni mkaelewane na mwalimu huyo, nikawaambia hatuwezi elewana maana zoezi hilo lilishindikana, askari wakasema unatufundisha kazi, yule pale dogo (askari ambaye alikuwa katika mkutano huo) simjui jina lake alinipiga kipigo sana, na askari mwingine bonge anachochea hii ndiyo Serikali ya Magufuli,” alisema Maswe.

Aidha, Waziri Lugola alijibu kero mbalimbali, ikiwemo ya Mkazi wa Mji huo, Malugu Mayombi ambaye ni mkulima maarufu wa mpunga wa eneo hilo, aliangua kilio kwa waziri akidai polisi wameshindwa kushughulikia kesi yake ya madai ya shilingi milioni sitini (6000,000/-) anazomdai mfanyabiashara Sali Kulwa maarufu TBS aliyemuuzia gunia 623 za mpunga.

“Waziri wangu, naomba unisaidie mimi maskini, ujiowako utaniokoa, nakuomba Waziri unisaidie nadai shilingi milioni 33 na laki 5 kati ya shilingi milioni 60 nimelipwa shilingi milioni 26 na laki 5 pekee, nimeshindwa kuendeleza kilimo naishi kwa shida, nilikuwa nalima ekari 100 kwasasa nalima ekari 30 tu nisaidie jamani, nateseka mimi,” alisema Mayombi.

Waziri Lugola alimuagiza Kamanda wa Polisi kushirikiana na Mkuu wa Polisi Wilaya kulitatua suala hilo kwa muda wa wiki moja wamkamate mtuhumiwa na aweze kumlipa fedha za Mayombi.

Waziri Lugola amemaliza ziara ya siku tano Mkoani Katavi, na ameelekea Mkoani Rukwa kuendelera na ziara ya kikazi akisikiliza kero za wananchi na kuzitatua katika mikutano mbalimbali ya hadhara mkoani humo.


Share:

WAMILIKI WA MAKANISA,BAA NA KUMBI ZA STAREHE WANAOPIGA 'MUZIKI MNENE' WAPEWA ONYO KAHAMA


Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha

Na Salvatory Ntandu - Malunde 1 blog
Serikali wilayani Kahama mkoani Shinyanga imetoa onyo kwa wamiliki wa baa na kumbi za starehe za usiku ambazo zipo katikati ya makazi ya watu ambazo zinapiga muziki kwa sauti ya juu sambamba na kuzifungia kwa kukiuka sheria na kusababisha kero kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa jana Septemba 29,2019 na Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na namna wanavyotekeza suala hilo la uchafuzi wa mazingira unaofanywa na upigaji kelele katika vilabu vya usiku.

Amesema wamebaini wengi wao wan aleseni ambazo haziwaruhusu kuendesha biashara ya usiku katika maeneo yao kutokana na kutokidhi vigezo ikiwa ni pamoja na kuwa na kumbi ambazo hazitoi kelele ya muziki nyakati za usiku.

“Zipo baa na klabu ambazo zinajinasibu kwa ni night club lakini hazina sifa hizo na zipo zimejengwa katikakati ya makazi ya watu nab ado zinaendelea kupiga muziki kwa sauti ya juu,hatutakubali kuona uchafuzi huu wa mazingira ukiendelea”alisema Macha.

Katika hatua nyingine Macha alisema serikali inaheshimu sana madhehebu ya dini lakini katika wilaya yake yapo baadhi ya makanisa yamejengwa katikakati ya makazi hali ambayo imekuwa ikisababisha malalamiko kwa baadhi ya wapangaji ambao sio waumini wa madhehebu hayo.

Alisema baadhi ya makanisa hayo yamekuwa yakifungua muziki wa sauti ya juu katika makanisa hayo nyakati za usiku na kusababisha usumbufu kwa watu wengine hususani wagonjwa.

“Kuna sehemu tumetembelea na kukuta vifaa vipo tu pekee na vikiendelea kupiga muziki tuu bila ya kuwepo kwa waumini wa madhehebu hayo katika nyumba hizo”,alisema Macha.

"Tunawashauri viongozi wa dini kujenga makanisa yao katika maeneo ambayo yametengwa na Halmashauri ili kuondoa migogoro kwa wananchi",alisema.
Share:

LUGOLA AAGIZA ASKARI WOTE WA KITUO CHA MAJIMOTO WAHAMISHWE.... WANANCHI WATAKA MKUU WA KITUO ABAKI

Na Adelina Ernest - Malunde 1 blog
Waziri wa mambo ya Ndani nchini Tanzania, Kangi Lugola ametoa siku saba kwa Polisi Mkoa wa Katavi kuwahamisha askari wote wa kituo cha Polisi Majimoto kwa madai kushindwa kushugulikia kutatua kero za wananchi pamoja na kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Lugola alitoa agizo hilo jana jioni Jumapili Septemba 29, 2019 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika stendi ya Majimoto Halmashauri ya Mlele mkoani Katavi wakati akijibu kero za wananchi ambao walieleza kuwepo kwa kero lukuki katika kituo cha polisi Majimoto hali iliyomlazimu kuagiza askari wote 15 wa kituo hicho kuondolewa.

Waziri Lugola alisema kupitia kero zilizowasilishwa na wananchi, zinaonyesha wazi askari hao 15 wanajihusisha na rushwa, kupiga wananchi ovyo wakiwemo bodaboda, kushindwa kudhibiti ulinzi na usalama na kutoshughulikia malalamiko ya wananchi.

"Nataka niseme haya kutoa mfano, ili iwe fundisho kwa wengine kote nchini, Kaimu kamanda, natoa siku saba askari wote wa kituo hiki wahamishwe na waletwe wengine ili wajifunze," alisema Lugola.

Baada ya agizo hilo, Waziri Lugola aliwauliza wananchi askari wote wanatakiwa kuhamishwa? ambapo walipinga mkuu wa kituo hicho Iddy Kombo asihamishwe badala yake wahamishwe askari wengine wote.

"Asihamishwe, asihamishwe, asihamishwe," walisema wananchi.

Awali mmoja wa wananchi wa Majimoto Malugu Mayombi ambaye ni mkulima wa zao la Mpunga alieleza kero yake ya kutapeliwa Mpunga gunia 600 zenye thamani ya Sh.Milioni 60 na Mfanyabiashara anayejulikana kwa jina la Sali Kulwa maarufu kama TBS lakini jeshi la Polisi limeshindwa kumpa msaada.

Hata hivyo amewataka kutimiza wajibu wao kama Jeshi la Polisi na kuhakikisha hali ya usalama unaimarika katika kata hiyo kwani maendeleo huambatana na ulinzi na usalama wa kutosha.
Share:

TMDA YAENDESHA MAFUNZO YA SIKU TANO KWA WAKAGUZI WA DAWA WA MKOA WA PWANI




Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) inaendesha mafunzo maalum ya siku tano kwa wakaguzi  wa dawa wa Halmashauri za Mkoa wa Pwani yanayoendana na kuzingatia maadili, uweledi pamoja na uelewa wa kanuni na sheria ikiwemo suala la usimamizi wa  dawa zenye asili ya kulevya  ili kuhakikisha kuwa zinatumika  kwa matumizi yanayotarajiwa na si vinginevyo katika kulinda Afya za Jamii.


Awali akifungua mafunzo hayo yanayoendelea katika ukumbi wa Baraza la Wauguzi na Ukunga (TNMC) Kibaha Mkoani Pwani,   mgeni rasmi ambaye ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dkt. Gunini Kamba amewapongeza TMDA kwa hatua hiyo kwani imekuja kipindi muafaka kwa watalaam hao  kwani mkoa huo umejipanga kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa tiba pamoja na viwanda vingine.

“Mkoa wa Pwani unaendelea kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vikiwemo vya kawaida na vya dawa. Wataalam wetu wekitoka hapa watakuwa msaada na kuongeza chachu ya kuwezesha ukaguzi na ufuatiliaji  na kutimiza wajibu wao.

"Pia naamini  mtajifunza mbinu za kukabiliana na dawa na vifaa tiba duni na bandia  na utoaji wa taarifa kuhusiana na madhara yatokanayo na madhara ya matumizi ya bidhaa za dawa.” Alieleza Dk.Kamba

Aidha, Dk. Kamba alisema kuwa, katika dhana ya viwanda, Mkoa wa Pwani umekuwa mstari wa mbele katika kuvutia wawekezaji wa viwanda hususani vya dawa na vifaa tiba.

“Mpaka sasa tuna viwanda sita ambavyo vimeanza kujengwa tangu serikali ya awamu ya tano imeingia madarakani. Viwanda hivi vitaongeza ajira kwa wananchi wa Mkoa wetu lakini pia kuzuia fedha zetu kwenda nje kufuata dawa ..naamini tutapiga hatua na tutaendelea kutimiza wajibu wetu” alimalizia Dk. Gunini.

Kwa upande wake Meneja wa Kanda ya Mashariki  wa TMDA,  Adonis Bitegeko ameeleza kuwa mafunzo hayo yatalenga kwenye utendaji sahihi na uelewa kama taratibu za Mamlaka zinavyolenga.

“Katika uzoefu wa kufanya ukaguzi imeonekana mapungufu kwa baadhi ya wakaguzi wetu hivyo katika mafunzo haya tutajitahidi wakaguzi waelewe na watambue namna ya kubaini dawa duni na  bandia pia washiriki watapatiwa mafunzo ya kuzingatia miongozo katika ukaguzi wa viwanda vinavyozalisha na dawa na vifaatiba ili kuwezesha uzalishaji wa dawa bora, salama na fanisi alisema Adonis Bitegeko.

Nae Mratibu wa ofisi za Kanda  na Halmashauri za TMDA, Dkt. Henry Irunde akisoma taarifa ya utangulizi ya mafunzo hayo, akimwakilisha Mkurugenzi wa TMDA, alibainisha kuwa, jukumu kubwa la watalaam hao kuhakikisha wanazingatia maadili ya kazi zao katika kulinda afya ya jamii kwa kudhibiti ubora, usalama na ufanisi katika dawa na vifaa tiba nchini.

“ufanisi wa dawa na vifaa tiba ni jambo muhimu sana  katika kuboresha afya ya jamii. Hadi sasa zaidi ya asilimia 80 ya dawa zinazotumika nchini zinatoka nje ya nchi. Pamoja na kwamba udhibiti katika vituo vya forodha na katika soko umeimarishwa, bado kuna changamoto ya uwepo wa dawa duni, bandia na ambazo hazijasajiliwa hivyo dawa hizi hazina  budi kufuatiliwa na kuondolewa  kwenye soko hivyo mafunzo haya tutapata wakaguzi wenye weledi katika kutambua dawa na vifaa tiba visivyofaa kwa matumizi pamoja na kuhamasisha uwekezaji na ukuaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini” Alisema Dkt. Irunde.


 Mafunzo hayo ya siku tano  yaliyoanza Septemba 30, yanatarajiwa kufikia tamati Oktoba 4, mwaka huu huku yakizingatia masuala muhimu  kwa wakaguzi hao ni pamoja na kuwakumbusha maadili na taratibu za kazi katika kutumiza majukumu yao. Pia uwelewa wa kanuni za uzalishaji pamoja na miongozo ya usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi nchini.
Share:

RAIS MAGUFULI : NIMEONGEZA SIKU 7 TENA ZA KUOMBA MSAMAHA KWA WAHUJUMU UCHUMI..SIFANYI KAZI YA KITOTO WASIDANGANYWE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, ameongeza siku 7 zingine kwa watuhumiwa wa makosa ya Uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha, kuendelea kuwasilisha maombi ya kuomba radhi kwa Mkurugenzi wa mashtaka (DPP),ili waweze kusamehewa na kuachiwa huru.

Maamuzi hayo ameyatoa leo Septemba 30, 2019, Ikulu jijini Dar es salaam, wakati akipokea taarifa ya maombi ya Watuhumiwa wa Uhujumu Uchumi kutoka kwa DPP,ambapo hadi sasa jumla ya maombi 467 yamekwishawasilishwa.

"Najua una barua nyingine zimekwama kwenye Ofisi za Mkoa, na kama kweli wapo waliokwamishwa kwa sababu ya umbali, nimeongeza tena siku 7 ili usije ukaniomba tena, katika siku 7 wapo ambao walizuiliwa na Maofisa na Magereza akitaka hongo kidogo, Kamishina wa Magereza upo hapo mkafuatilie walioomba msamaha kwa DPP ili msiwakwamishe'' amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa "natoa wito kwa Watanzania wenye tuhuma za uhujumu uchumi, wasiwe na wasiwasi ukishakiri basi kesho ndiyo ushahidi huo, siwezi nikafanya kazi ya kitoto ya namna hiyo nimeshasema nimetoa msamaha ni msamaha kweli, kwa hiyo wasidanganywe''

Mapema wiki iliyopita wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua, Rais Magufuli alishauri na kutoa siku 7 kwa DPP, kukutana na watuhumiwa wa uhujumu uchumi na kwa wale ambao watakuwa tayari kukiri makosa yao na kukubali kuzirudisha fedha hizo basi waachiwe huru.

TAZAMA HOTUBA YA RAIS MAGUFULI HAPA

Share:

Waziri Mkuu Kuanza Ziara Ya Kikazi Ya Siku Tatu Mkoani Singida

Na Dotto Mwaibale, Singida
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Singida na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi alisema ziara hiyo ataianza Oktoba 4, 2019 na Oktoba 7 atafungua rasmi maonesho ya pili ya viwanda vidogo vidogo (SIDO) yatakayofanyika kitaifa mkoani humo.

NCHI sita za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika (SADC) zinatarajiwa kushiriki maonesho hayo ambazo ni Kenya, Burundi, Ruanda, Uganda, China, India na Afrika kusini.

Dkt.Nchimbi alisema maonesho hayo yataanza kufanyika Oktoba 4 hadi 9 mwaka huu,na yatafunguliwa rasmi oktoba 7 na waziri mkuu Kassimu Majaliwa.

” Maonesho haya yatafanyika sanjari na maadhimisho ya wiki ya chakula duniani ambayo yatafanyika kuanzia Oktoba 10 hadi 16 mwaka huu katika Viwanja vya Bombadier zamani Peoples” alisema Nchimbi.

Alisema kufanyika maonesho hayo mkoani Singida ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo ambao unakuwa kiuchumi kutokana na shughuli za kilimo, ufugaji, biashara na viwanda.

Pia alisema mkoa wa Singida wanajivunia kuchaguliwa kufanyika kwa maonesho hayo kitaifa na hii itawapa hamasa kubwa wananchi katika kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya usindikaji kutokana na mazao yanayolimwa mkoani hapa.

Dkt. Nchimbi alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wananchi wote wa mkoa huo na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kupokea ugeni huo na kushiriki katika maonesho hayo.

Aidha mkuu wa mkoa alisema kabla ya kufungua maonesho hayo waziri mkuu Kassim Majaliwa atafanya ziara ya kikazi kila wilaya na halmashauri zote za mkoa huo na kuzungumza na wananchi pamoja na watumishi katika mkutano wa hadhara.

Katika ziara hiyo Majaliwa atatembelea miradi mbalimbali ya kimkoa na miradi mikubwa ya kitaifa, ambapo miradi ya kitaifa ni mradi wa kupokea na kupozea umeme uliopo katika halmashauri ya manispaa ya Singida pamoja na mradi wa daraja Sibiti linalounganisha mkoa wa Singida na Simiyu lililopo wilayani
Mkalama.


Share:

HOTUBA YA DPP BISWALO MGANGA ALIPOKABIDHI KWA MHE RAIS UTEKELEZAJI WA MSAMAHA WAHUJUMU UCHUMI NCHINI

Share:

HOTUBA YA RAIS DKT. MAGUFULI MARA BAADA YA KUKABIDHIWA UTEKELEZAJI WA MSAMAHA WA WAHUJUMU UCHUM

Share:

SCHOLARSHIP TENABLE IN KOREA AT THE ACADEMY OF KOREAN STUDIES STARTING FROM MARCH 2020

1.0 Call for Application The General Public is hereby informed that, the Academy of Korean Studies has granted a Scholarship programme to eligible Tanzanian Nationals to pursue Masters and Doctoral Degree programs at the Academy of Korean in the Republic of South Korea in the academic year 2019/2020. For further information visit the following link htt://intl.aks.ac.kr/english (AKS in… Read More »

The post SCHOLARSHIP TENABLE IN KOREA AT THE ACADEMY OF KOREAN STUDIES STARTING FROM MARCH 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP FOR 2020 GLOBAL KOREA SCHOLARSHIP (GKS) FOR UNDERGRADUATE DEGREE

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP FOR 2020 GLOBAL KOREA SCHOLARSHIP (GKS) FOR UNDERGRADUATE DEGREE 1.0 Call for Application The general public is hereby informed that, the National Institute for International Education (NIIED) under the Ministry of Education of the Republic of Korea is offering undergraduate study opportunity to a Tanzanian citizen for 2020 Undergraduate Global Korea Scholarship (GKS). 2.0… Read More »

The post WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP FOR 2020 GLOBAL KOREA SCHOLARSHIP (GKS) FOR UNDERGRADUATE DEGREE appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Maji




Share:

Rais Magufuli Atoa Tahadhari Kwa Watuhumiwa Wa Uhujumu Uchumi

Rais John Magufuli amewataka watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi walioagizwa kuwasilisha barua zao za kuomba msamaha katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuepukana na dhana ya kuwa msamaha huo ni wa uongo kwakuwa yeye ameutoa kwa dhati na kwamba hawezi kufanya hivyo kwa lengo la kuwatega.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Septemba 30, alipokuwa akipokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kusamehe watuhumiwa hao wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali.

“Hizi siku saba ni kwaajili ya wale ambao wamekwama inawezekana mwingine akawa amejifikiria zaidi katika siku ya leo hadi ya saba akatoa maamuzi yake ninafahamu wapo wanaodanganywa huu msamaha ni wa uongo,”

“Huwa hakuna msamaha wa uongo hauwezi ukatoa msamaha wa majaribio au wa kumtega mtu, msamaha ukishautoa ni msamaha la sivyo wewe uliyetoa utaibeba hiyo dhambi kwa Mungu.

"Ninafahamu wapo wanaodanganywa na mawakili wao ili waendelee kuwachomoa pesa wanaawambia ukiomba msamaha maana yake unakuwa umeshajishtaki mwenyewe sasa hiyo ni shauri yao waamue wanamsikiliza nani,” amesema Magufuli.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger