Friday 30 August 2019

JUMUIYA YA MADAKTARI WATANZANIA WALIOSOMA CHINA (DCAT) YATOA HUDUMA YA AFYA BURE KISARAWE, PWANI


WAKAZI wa Kisarawe wamenufaika na kambi ya kwanza ya kampeni ya uchunguzi na matibabu dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza inayotolewa na madaktari bingwa wa Jumuiya ya Madaktari  Watanzania waliosoma China (DCAT).

Awali akifungua kambi hiyo wiki hii katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jafo amewahamasisha kujitokeza kwa wingi ili kujua hali zao.

Jafo ambaye pia ni Mbunge wa Kisarawe ametumia fursa hiyo kuwasilisha ombi lake kwa Mwambata wa Ubalozi wa China, anayeshughulikia masuala ya utamaduni na elimu, Gao Wei, ambaye alimwakilisha Balozi wa China, kwamba waijengee Hospitali hiyo jengo la kisasa la matibabu.

"Tunashukuru wataalamu wetu wameona katika kampeni hii, Kisarawe iwe ya kwanza kisha watakwenda maeneo mengine ya nchi, Rais Dk. John Magufuli anatujengea jengo la kisasa la OPD (wagonjwa wa nje) hapa Kisarawe.

"Nitumie fursa hii kuuomba ubalozi wa China, ikizingatiwa pia kwamba Wilaya hii ina historia hasa katika ujenzi wa reli ya Tazara, Wachina walikaa hapa na wakazi wa Kisarawe walishiriki kuijenga.

"Ukiacha mahusiano yale ya ujenzi wa reli ya Tazara, leo hii wigo umepanuka mpaka kwenye elimu, afya na sekta nyinginezo," amesema.

Ameongeza "Nawasihi wakazi wa Kisarawe kuitumia fursa hii ya uchunguzi vizuri, hata yule mwenye mgonjwa aliyepo nyumbani amlete, hapa Wapo madaktari wabobezi watachunguzwa na watagundua tatizo linalomsumbua.

Kuhusu ombi hilo la Waziri Jafo, Mwambata huyo wa Ubalozi amesema amelipokea na kuridhia kwamba wapo tayari kujenga jengo la kisasa kwa Hospitali hiyo.

Awali, amesema ushirikiano wa China na Tanzania ni wa miaka mingi na imekuwa ikitoa ufadhili kwa watanzania kwenda kusoma nchini humo elimu mbalimbali .

Amesema wanafurahi kuona kwamba wataalamu waliopata ufadhili wa masomo China sasa wanasaidia nchi katika mambo mbalimbali.

Mwenyekiti wa DCAT, Dk. Liggyle Vumilia amesema katika siku hizo tatu wanatarajia kuwachunguza afya watu kati ya 600 hadi 1000 ambapo watachunguzwa magonjwa ya saratani, moyo, kisukari na mengineyo.

"Kampeni yetu ina kauli mbiu 'Jali Afya yako, Fanya uchunguzi mapema', tunalenga wananchi wa kawaida kabisa, kuwahamasisha wajenge tabia ya kuchunguza afya zao, itawasaidia kujua mapema kama wanakabiliwa na matatizo au la!

"Wale tutakaowakuta na matatizo madogo tutawatibu kupitia mfuko tulioandaa, tunawapa na elimu ya kujikinga dhidi ya magonjwa haya," amesema.

Amesema wanatarajia pia kwenda hivi karibuni mkoani Tanga ambako watafanya kampeni hiyo na baadae nchi nzima.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Jokate Mwegelo amesema utoaji wa huduma bora za afya ni miongoni kwa vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Magufuli na kwamba msisitizo zaidi ni katika utoaji wa huduma za kinga.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jafo  akiwashukuru wanajumuiya ya Watanzania walioishi nchini China (DCAT) kwa kujitolea kuwapa huduma ya afya bure kwa wakazi wa wila ya Kisarawe, Pwani. 
Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo (kushoto) akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jafo  kutoa hotuba yake.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amesema utoaji wa huduma bora za afya ni miongoni kwa vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Magufuli na kwamba msisitizo zaidi ni katika utoaji wa huduma za kinga.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Watanzania waliosoma nchini China Dkt. Liggyle Vumilia akielezea kwa ufasaha huduma hiyo ya afya bure.
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Utamaduni wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Bwana Gao Wei akisoma hotuba yake.
Mtaalam wa Tiba ya jadi ya Kichina Dkt Paul Mhame akitoa ushauri kwa jamii.


Wananchi wa wilaya ya Kisarawe, Pwani na vitongoji vyake wakipima uzito na urefu ili kuweza kupatiwa matibabu ya bure kutoka kwa Jumuiya ya Madaktari  Bingwa Watanzania waliosoma nchini China (DCAT) waliopiga kambi kwa muda wa siku tatu. Jumuiya hiyo imejipanga kuendelea na zoezi la kutoa huduma katika mkoa wa Tanga na maeneo mengine ya Tanzania. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Dokta Bingwa wa Magonjwa ya Saratani, Dkt Heri Tungaraza akitoa maelekezo kwa wagonjwa.

Wagonjwa wakipimwa presha.
Wagonjwa wakipimwa ugonjwa wa Kisukari.
Mtatibu wa zoezi la upimaji wa Afya Bure, Bi. Linas akigawa maji kwa wagonjwa.

Wananchi wakisubiri huduma.
Wazee wakipatiwa ushauri kabla ya kuingia kuwaona Madaktari bingwa waliojitolea kufanya zoezi la kutoa huduma ya Afya Bure kwa wananchi wa Jumuiya ya Madaktari  Bingwa Watanzania waliosoma nchini China (DCAT).
Kila mmoja alijitahidi kumleta mgonjwa wake ili apatiwe huduma ya afya bure.
Wananchi wa wilaya ya Kisarawe, Pwani na vitongoji vyake wakipimwa presha ili kuweza kupatiwa matibabu ya bure kutoka kwa Jumuiya ya Madaktari  Bingwa Watanzania waliosoma nchini China (DCAT) waliopiga kambi kwa muda wa siku tatu.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Watanzania waliosoma nchini China Dkt. Liggyle Vumilia (aliyevaa tai) akitoa ushari kwa wagonjwa walifika kupatiwa huduma ya Afya bure iliyofannyika wilaya ya Kisarawe, Pwani.

Wananchi wa wilaya ya Kisarawe wakiwa wamepanga foleni kuoatiwa huduma ya Afya Bure.
Watoa huduma wakiendelea kutoa ushari kwa wagonjwa waliofika kupatiwa huduma ya Afya bure.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Watanzania waliosoma nchini China Dkt. Liggyle Vumilia akigawa maji kwa wagonjwa aliojitokeza kupatiwa huduma ya Afya Bure.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 30 August




Share:

Thursday 29 August 2019

MAKONDA AIBUKA NA MKAKATI MWINGINE ...."PEKENYUA TUKUFUKUNYUE"

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo Agosti 29,2019 amezindua Mpango Mkakati wa Kutokomeza  Wahamihaji haramu Mkoa wa Dar es salaam alioubatiza jina la  "PEKENYUA TUKUFUKUNYUE" na  kuwaagiza Watendaji wa Mitaa kurejesha Daftari la Mkazi ili Kila Mkazi kuanzia ngazi ya Mtaa afahamike anapoishi na kazi anayofanya jambo litakalosaidia pia kuondoa uhalifu.


Makonda amesema mpango huo ni Mwarobaini tosha wa kupambana na Wageni wanaoishi Nchini kinyume na Sheria na utahusisha Watendaji wa Kata, Mitaa na Wananchi ambao watakuwa na jukumu la kutoa taarifa pindi wanapobaini uwepo wa mgeni au mtu wanaemtilia mashaka kwenye Makazi wanayoishi.

Aidha Makonda amesema uwepo wa Wahamihaji Haramu Nchini ni jambo la hatari kiusalama kwakuwa baadhi yao wanafanya uhalifu wa Wizi, Ubakaji, Uporaji, wanatumia rasilimali za nchi, wanatumia fursa ambazo zilipaswa kuwanufaisha wazawa ikiwemo Afya, Elimu na Ajira, kusababisha msogamano wa watu magerezani pamoja na kuwa Chanzo cha Migogo ikiwemo ya Ardhi.

Kutokana na hilo Makonda ameviagiza Vyombo Vyote vya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Viongozi wa Kata na Mitaa kuhakikisha Mpango huo unafanikiwa kwa 100%.

Kwa upande wake Kamishina wa Uhamihaji Mkoa wa Dar es salaam amesema wamebaini idadi kubwa ya wahamihaji haramu wanatoka mataifa ya Burundi, DRC, Somalia na Ethiopia na wamekuwa wakipendelea kuishi Mkoa wa Dar es salaam kwakuwa umekuwa jiji lenye fursa nyingi za kibiashara.
Share:

Waganga Wakuu Wa Mikoa Watakiwa Kushirikiana Na Viongozi Wa Vijiji Kuhakikisha Kila Mwezi Wanaingiza Kaya Mpya 31 Katika CHF

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
NAIBU katibu mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya dokta DOROTHY GWAJIMA amewataka waganga wakuu wa mikoa kushirikiana na viongozi wa serikali za vijiji nchini kuhakikisha kila mwezi wanaingiza kaya mpya 31 za mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa(CHF).
 
Dokta GWAJIMA amesema hayo alipotembelea Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma kushuhudia namna ambavyo Zahanati hiyo imeweza kuandikisha idadi kubwa ya kaya katika mfumo huo.
 
Amesema zahanati hiyo ipo kijijini umbali wa km 90 lakini imeweza kuandikisha kaya 315 sawa na asilimia 63.
 
Azma ya serikali ni  kutengeneza mfumo wa bima ambao mwananchi atatambuliwa na pesa anayochangia itarudi kwenye kituo kama anavyoeleza meneja mradi wa HPSS Tuimarishe afya ALLY KEBBY.
 
Kwa upande wake mratibu wa CHF iliyoboreshwa mkoa FRANCIS LUTALALA amesema ili kupata mafanikio ni lazima uwepo ushirikiano baina ya viongozi.
 
Naye Muuguzi wa Zahanati hiyo SHIJA MAKEJA anaeleza siri kubwa ya mafanikio waliyoyapata kuwa  ni ushirikiano waliouweka baina yao na viongozi wa serikali ya kijiji.
 
Hadi kufikia agosti mwaka huu jumla ya kaya elfu 23,114 kati ya kaya laki 447,773 za mkoani hapa zimejiunga na CHF iliyoboreshwa huku uhamasishaji Zaidi ukiendelea kutolewa kwa kaya zote kuona umuhimu wa kujiunga na CHF iliyoboreshwa.


Share:

22 WATUPWA JELA KWA KUFANYA BIASHARA YA NGONO 'UZEMBE NA UZURURAJI'

 Mahakama ya Mwanzo Nunge manispaa ya Morogoro imewahukumu watu 22 kifungo cha miezi sita jela baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la uzembe na uzururaji.

Baada ya hakimu Emelia Mwambagi kusoma hukumu hiyo, washtakiwa hao ambao wengi ni wanawake waliangua kilio mahakamani, kuomba kusamehewa.

Kesi hiyo ilisikilizwa jana Jumatano Agosti 28, 2019 kwa zaidi ya saa tano dhidi ya wasichana wanaodaiwa kufanya biashara ya ngono pamoja na wanaume wanaodaiwa kujihusisha na ushoga.

Washtakiwa hao walikamatwa usiku wa Agosti 16, 2019 eneo la Kahumba manispaa ya Morogoro.

Hakimu Mwambagi aliieleza mahakama hiyo kuwa adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa washtakiwa hao na wengine wanaotumia miili yao kujidhalilisha na kuwadhalilisha wazazi, ndugu na jamaa kwenye maeneo wanayotoka.

Na Hamida Shariff, Mwananchi 
Share:

Wizara Ya Uchukuzi Yaanza Kukusanya Maoni Ya Wadau Kujadili Rasimu 8 Za Kanuni Za Usafirishaji.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wizara ya ujenzi , uchukuzi na mawasiliano imeanza kukusanya maoni kutoka kwa wadau wa usafirishaji  wa Ardhini nchini,  maoni yatakayosaidia kuboresha rasimu nane za kanuni  zilizoandaliwa na wizara hiyo zitakazo saidia kuondoa baadhi ya vikwazo vya usafiri wa Ardhini.
 
Akizungumza jijini Dodoma Agosti 28,2019   wakati akifungua kikao hicho kilichowahusisha wadau wa uasafirishaji pamoja na mamlaka ya uasafiri wa ardhini LATRA ,katibu mkuu wa  uchukuzi Dkta Leonard Chamriho amewataka wadau hao kuwa huru katika kutoa maoni yao yatakayosaidia kuleta matokeo chanya katika sekta ya usafirishaji wa Ardhini.

Mkurugenzi wa mamlaka ya udhibiti usafirishaji ardhini (LATRA) Gerald Ngewe amesema kuwa  maoni ya wadau ni muhimu katika urekebishaji wa sera na sheria katika sekta hiyo.
 
Hata,hivyo amezungumzia  kifungu cha kanuni ya 10 juu ya Masharti ,ambapo yanamtaka mtumiaji wa vyombo vya usafiri kutotumia vilevi,kuvaa sare safi,kutoruhusu watu kufanya biashara ndani ya basi ,kutozidisha abiria pamoja na kuzingatia ukomo wa mwendo kasi.
 
Nao baadhi ya Wadau wa Usafiri hapa nchini wamesema ni vyema LATRA ikajikita zaidi katika utoaji wa elimu kwa wadau.


Share:

Waziri wa viwanda: Serikali imeondoa kodi kero 54 kwa wafanyabiashara

Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa viwanda na biashara Innocent Bashungwa amesema serikali imefuta kodi kero  54 kwa wafanyabiashara pamoja na kupunguza mamlaka za kutoa leseni za biashara .

Bashungwa ameyasema hayo mjini Makambako mkoani Njombe wakati akizungumza na wafanyabiashara kutoka mikoa zaidi ya 7 nchini waliokutana  mjini hapo kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya biashara na kuja na maazimio ya kuiomba serikali kupunguza utitili wa kodi,tozo na leseni kwa wafanyabiashara ili kunusuru sekta hiyo ambayo imetajwa kuwa katika hali mbaya kimaendeleo kwa sasa.

“Kuna kodi 54 zimeishaondolewa na ili nisiseme tu 54 mheshimiwa mwenyekiti wenu nimeisha mkabidhi hizo kodi kero 5”alisema Bashungwa

Awali wakizungumzia changamoto hizo wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka mikoa ya Tanga, Dar es salaamu,Mbeya,Songwe, Ruvuma, Iringa,Njombe na Katavi wamesema hali ya biashara nchini imezidi kuwa ngumu kwasababu kumekuwa na mrundikano wa tozo na ushuru kutoka mamlaka mbalimbali ikiwemo TRA,Halmashauri na nyinginezo hatua ambayo inawafanya watu wengi kufunga biashara zao.

Amani Mahellah,Sifael Msigala na Ismail Masoud ni baadhi ya wawakilishi walitoa maoni yao katika mkutano huo mkubwa wa wafanyabiashara nchini ambapo wamemuomba waziri wa viwanda na biashara Innocent Bashungwa kuhakikisha anakutana na wizara zote zinazomgusa mfanyabiashara katika majukumu yake ili kuzitafutia ufumbuzi changomoto hizo kwa ustawi wa sekta ya biashara na taifa kwa ujumla.

“Hizi taasisi zinazokusanya kodi za serikali zikutane kwa pamoja na wafanyabiashara ili kila mtu ajue kwa mfanya biashara yule anachukua shilingi ngapi”alisema Amani Mahellah mmoja wa wafanyabiashara

Akifafanua kiini cha kusuasua kwa sekta ya biashara nchini katibu mkuu wa jumuiya ya wafanyabiashara JWT Abdallah Mwinyi amesema kuwepo kwa urasimu mkubwa bandarini kunawafanya kutengeneza mianya ya rushwa huku  kamishna wa TRA nchini Edwin Mhede akimtaka kila mfanyabiashara kuviripoti vitendo vyote vya rushwa kwani vinaikosesha nchini Mapato.

“Forodha aangaliwe kwa makini nap engine sheria zibadilishwe kwenye udhaminishaji na uondoshaji mizigo bandalini” alisema Abdallah Mwinyi

Katika mkutano huo wizara nne zenye mahusiano ya karibu na wafanyabiashara zimealikwa ikiwemo ya viwanda na biashara ,tamisemi, fedha na uwekezaji.


Share:

VIDEO: Rais Magufuli apokea hati za utambulisho wa balozi wa zimbabwe nchini tanzania

Balozi mteule wa Zimbabwe nchini Tanzania, Meja Jenerali Anselem Nhamo Sanyatwe, amekabidhi hati za utambulisho kwa Rais Magufuli leo Agosti 29 Ikulu Jijini Dar es Salaam


Share:

World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC)

World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC) Applications are open for the World Bank Youth Summit 2019 Competition. The Competition challenges young social entrepreneurs to submit innovative proposals for scalable enterprises that leverage smart technology to build sustainable and inclusive cities that will serve the needs of… Read More »

The post World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Commonwealth Youth Awards 2020 for excellence in development work (Win cash prizes and trip to London)

Deadline: October 31, 2019 Nominations for the 2020 Commonwealth Youth Awards are now open. The Commonwealth Youth Awards for Excellence in Development Work 2020 will recognise the contribution of young people towards achieving the Sustainable Development Goals. The Commonwealth Youth Awards recognise the exemplary work undertaken by young people across the 53 member countries. The awards will see winners awarded a cash grant… Read More »

The post Commonwealth Youth Awards 2020 for excellence in development work (Win cash prizes and trip to London) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded)

Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded): commonwealth scholarship 2019/2020, commonwealth scholarship 2020, commonwealth masters scholarship 2019, commonwealth scholarship application portal, how to apply for commonwealth scholarship, how to apply for commonwealth scholarship 2019, commonwealth scholarships 2020, commonwealth phd scholarship 2019 Commonwealth Master’s Scholarships are for candidates from low and middle income… Read More »

The post Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana

Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana


Share:

Nafasi za Internships- (Mechanism Archives and Records Section)

Posting Title: INTERN – Mechanism Archives and Records Section, Arusha, I (Temporary Job Opening) Job Code Title: INTERN – INFORMATION MANAGEMENT Department/Office: International Residual Mechanism for Criminal Tribunals Duty Station: ARUSHA Posting Period: 28 August 2019 – 26 August 2020 Job Opening Number: 19-Documentation and Information -RMT-117032-J-Arusha (O) Staffing Exercise N/A Org. Setting and Reporting The International Residual… Read More »

The post Nafasi za Internships- (Mechanism Archives and Records Section) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Video Mpya ya Maua Sama – Niteke

Video Mpya  ya  Maua Sama – Niteke


Share:

TENDER: Provision of Transport Services to Tanzania Youth Alliance (TAYOA) under the Global Fund Project

INVITATION OF TENDERS Tanzania Youth Alliance (TAYOA) is locally registered non-profit organization dedicated to improving the health of youth and adult people in Tanzania, with a focus on HIV/AIDS prevention ,reproductive health, entrepreneurship and employ-ability. TAYOA is implementing Global Fund project on HIV Prevention Programs for Adolescent Girls and Young Women -in Morogoro and Dodoma Regions. The organization invites eligible suppliers… Read More »

The post TENDER: Provision of Transport Services to Tanzania Youth Alliance (TAYOA) under the Global Fund Project appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

AJIUA KWA KUNYWA SUMU BAADA YA KUMUUA MKEWE KISHA KUMLAZA KITANDANI KAGONGWA

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard  Abwao
Na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mwanaume aitwaye Paschal Clement Mahona (32) mkazi wa Iponya kata ya Kagongwa wilaya ya Kahama amejiua kwa kunywa sumu baada ya kumuua mkewe Ashura Paschal (30) kwa kumnyonga shingo kisha kumlaza kitandani.


Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard  Abwao tukio hilo limetokea Agosti 28,2019 majira ya saa moja usiku.

"Ashura Paschal ambaye ni mkazi wa Iponya alikutwa akiwa ameuawa kwa kunyongwa shingo na kulazwa kitandani na mmewe aitwaye Paschal Clement Mahona mbaye naye baada ya kufanya mauaji hayo alijiua kwa kunywa sumu ambayo aina yake bado kujulikana na kukutwa chumbani akiwa amelala sakafuni, akitoa povu mdomoni",amesema Kamanda Abwao.

"Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kwani  kabla ya tukio hilo wanandoa hao walikuwa wakigombana huku mume akimtuhumu mkewe kukosa uaminifu katika ndoa yao",ameongeza Kamanda Abwao.

Share:

WAZIRI LUKUVI AOKOA ARDHI YA AJUZA NA KUAMURU ALIPWE FIDIA YA SH. MILIONI 500 NDANI YA MIEZI MITATU


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi, ametoa miezi mitatu kwa wavamizi 110 waliovamia eneo la Ajuza Nasi Murio, mwenye umri wa miaka 98, lenye ukubwa wa hekari nane kumlipa kiasi cha sh. milioni 500 kama fidia.

Lukuvi ametoa agizo hilo Jijini Arusha leo Agosti 28, katika kata ya ya Sinoni ambapo amesema kila mtu atalipa fedha kulingana na ukubwa wa eneo alilopora.

Amesema serikali imewaonea huruma na kwamba watalipa shilingi 20,000 kwa kila mita moja za eneo.

Waziri amesema ili wavamizi hao waweze kurasimishwa na kuwa wamiliki halali watalazimika kulipa gharama za upimaji pamoja na gharama za kupata hati miliki pamoja na kodi ya ardhi.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger