Thursday 29 August 2019

MAKONDA AIBUKA NA MKAKATI MWINGINE ...."PEKENYUA TUKUFUKUNYUE"

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo Agosti 29,2019 amezindua Mpango Mkakati wa Kutokomeza  Wahamihaji haramu Mkoa wa Dar es salaam alioubatiza jina la  "PEKENYUA TUKUFUKUNYUE" na  kuwaagiza Watendaji wa Mitaa kurejesha Daftari la Mkazi ili Kila Mkazi kuanzia ngazi ya Mtaa afahamike anapoishi na kazi anayofanya jambo litakalosaidia pia kuondoa uhalifu.


Makonda amesema mpango huo ni Mwarobaini tosha wa kupambana na Wageni wanaoishi Nchini kinyume na Sheria na utahusisha Watendaji wa Kata, Mitaa na Wananchi ambao watakuwa na jukumu la kutoa taarifa pindi wanapobaini uwepo wa mgeni au mtu wanaemtilia mashaka kwenye Makazi wanayoishi.

Aidha Makonda amesema uwepo wa Wahamihaji Haramu Nchini ni jambo la hatari kiusalama kwakuwa baadhi yao wanafanya uhalifu wa Wizi, Ubakaji, Uporaji, wanatumia rasilimali za nchi, wanatumia fursa ambazo zilipaswa kuwanufaisha wazawa ikiwemo Afya, Elimu na Ajira, kusababisha msogamano wa watu magerezani pamoja na kuwa Chanzo cha Migogo ikiwemo ya Ardhi.

Kutokana na hilo Makonda ameviagiza Vyombo Vyote vya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Viongozi wa Kata na Mitaa kuhakikisha Mpango huo unafanikiwa kwa 100%.

Kwa upande wake Kamishina wa Uhamihaji Mkoa wa Dar es salaam amesema wamebaini idadi kubwa ya wahamihaji haramu wanatoka mataifa ya Burundi, DRC, Somalia na Ethiopia na wamekuwa wakipendelea kuishi Mkoa wa Dar es salaam kwakuwa umekuwa jiji lenye fursa nyingi za kibiashara.
Share:

Waganga Wakuu Wa Mikoa Watakiwa Kushirikiana Na Viongozi Wa Vijiji Kuhakikisha Kila Mwezi Wanaingiza Kaya Mpya 31 Katika CHF

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
NAIBU katibu mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya dokta DOROTHY GWAJIMA amewataka waganga wakuu wa mikoa kushirikiana na viongozi wa serikali za vijiji nchini kuhakikisha kila mwezi wanaingiza kaya mpya 31 za mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa(CHF).
 
Dokta GWAJIMA amesema hayo alipotembelea Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma kushuhudia namna ambavyo Zahanati hiyo imeweza kuandikisha idadi kubwa ya kaya katika mfumo huo.
 
Amesema zahanati hiyo ipo kijijini umbali wa km 90 lakini imeweza kuandikisha kaya 315 sawa na asilimia 63.
 
Azma ya serikali ni  kutengeneza mfumo wa bima ambao mwananchi atatambuliwa na pesa anayochangia itarudi kwenye kituo kama anavyoeleza meneja mradi wa HPSS Tuimarishe afya ALLY KEBBY.
 
Kwa upande wake mratibu wa CHF iliyoboreshwa mkoa FRANCIS LUTALALA amesema ili kupata mafanikio ni lazima uwepo ushirikiano baina ya viongozi.
 
Naye Muuguzi wa Zahanati hiyo SHIJA MAKEJA anaeleza siri kubwa ya mafanikio waliyoyapata kuwa  ni ushirikiano waliouweka baina yao na viongozi wa serikali ya kijiji.
 
Hadi kufikia agosti mwaka huu jumla ya kaya elfu 23,114 kati ya kaya laki 447,773 za mkoani hapa zimejiunga na CHF iliyoboreshwa huku uhamasishaji Zaidi ukiendelea kutolewa kwa kaya zote kuona umuhimu wa kujiunga na CHF iliyoboreshwa.


Share:

22 WATUPWA JELA KWA KUFANYA BIASHARA YA NGONO 'UZEMBE NA UZURURAJI'

 Mahakama ya Mwanzo Nunge manispaa ya Morogoro imewahukumu watu 22 kifungo cha miezi sita jela baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la uzembe na uzururaji.

Baada ya hakimu Emelia Mwambagi kusoma hukumu hiyo, washtakiwa hao ambao wengi ni wanawake waliangua kilio mahakamani, kuomba kusamehewa.

Kesi hiyo ilisikilizwa jana Jumatano Agosti 28, 2019 kwa zaidi ya saa tano dhidi ya wasichana wanaodaiwa kufanya biashara ya ngono pamoja na wanaume wanaodaiwa kujihusisha na ushoga.

Washtakiwa hao walikamatwa usiku wa Agosti 16, 2019 eneo la Kahumba manispaa ya Morogoro.

Hakimu Mwambagi aliieleza mahakama hiyo kuwa adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa washtakiwa hao na wengine wanaotumia miili yao kujidhalilisha na kuwadhalilisha wazazi, ndugu na jamaa kwenye maeneo wanayotoka.

Na Hamida Shariff, Mwananchi 
Share:

Wizara Ya Uchukuzi Yaanza Kukusanya Maoni Ya Wadau Kujadili Rasimu 8 Za Kanuni Za Usafirishaji.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wizara ya ujenzi , uchukuzi na mawasiliano imeanza kukusanya maoni kutoka kwa wadau wa usafirishaji  wa Ardhini nchini,  maoni yatakayosaidia kuboresha rasimu nane za kanuni  zilizoandaliwa na wizara hiyo zitakazo saidia kuondoa baadhi ya vikwazo vya usafiri wa Ardhini.
 
Akizungumza jijini Dodoma Agosti 28,2019   wakati akifungua kikao hicho kilichowahusisha wadau wa uasafirishaji pamoja na mamlaka ya uasafiri wa ardhini LATRA ,katibu mkuu wa  uchukuzi Dkta Leonard Chamriho amewataka wadau hao kuwa huru katika kutoa maoni yao yatakayosaidia kuleta matokeo chanya katika sekta ya usafirishaji wa Ardhini.

Mkurugenzi wa mamlaka ya udhibiti usafirishaji ardhini (LATRA) Gerald Ngewe amesema kuwa  maoni ya wadau ni muhimu katika urekebishaji wa sera na sheria katika sekta hiyo.
 
Hata,hivyo amezungumzia  kifungu cha kanuni ya 10 juu ya Masharti ,ambapo yanamtaka mtumiaji wa vyombo vya usafiri kutotumia vilevi,kuvaa sare safi,kutoruhusu watu kufanya biashara ndani ya basi ,kutozidisha abiria pamoja na kuzingatia ukomo wa mwendo kasi.
 
Nao baadhi ya Wadau wa Usafiri hapa nchini wamesema ni vyema LATRA ikajikita zaidi katika utoaji wa elimu kwa wadau.


Share:

Waziri wa viwanda: Serikali imeondoa kodi kero 54 kwa wafanyabiashara

Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa viwanda na biashara Innocent Bashungwa amesema serikali imefuta kodi kero  54 kwa wafanyabiashara pamoja na kupunguza mamlaka za kutoa leseni za biashara .

Bashungwa ameyasema hayo mjini Makambako mkoani Njombe wakati akizungumza na wafanyabiashara kutoka mikoa zaidi ya 7 nchini waliokutana  mjini hapo kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya biashara na kuja na maazimio ya kuiomba serikali kupunguza utitili wa kodi,tozo na leseni kwa wafanyabiashara ili kunusuru sekta hiyo ambayo imetajwa kuwa katika hali mbaya kimaendeleo kwa sasa.

“Kuna kodi 54 zimeishaondolewa na ili nisiseme tu 54 mheshimiwa mwenyekiti wenu nimeisha mkabidhi hizo kodi kero 5”alisema Bashungwa

Awali wakizungumzia changamoto hizo wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka mikoa ya Tanga, Dar es salaamu,Mbeya,Songwe, Ruvuma, Iringa,Njombe na Katavi wamesema hali ya biashara nchini imezidi kuwa ngumu kwasababu kumekuwa na mrundikano wa tozo na ushuru kutoka mamlaka mbalimbali ikiwemo TRA,Halmashauri na nyinginezo hatua ambayo inawafanya watu wengi kufunga biashara zao.

Amani Mahellah,Sifael Msigala na Ismail Masoud ni baadhi ya wawakilishi walitoa maoni yao katika mkutano huo mkubwa wa wafanyabiashara nchini ambapo wamemuomba waziri wa viwanda na biashara Innocent Bashungwa kuhakikisha anakutana na wizara zote zinazomgusa mfanyabiashara katika majukumu yake ili kuzitafutia ufumbuzi changomoto hizo kwa ustawi wa sekta ya biashara na taifa kwa ujumla.

“Hizi taasisi zinazokusanya kodi za serikali zikutane kwa pamoja na wafanyabiashara ili kila mtu ajue kwa mfanya biashara yule anachukua shilingi ngapi”alisema Amani Mahellah mmoja wa wafanyabiashara

Akifafanua kiini cha kusuasua kwa sekta ya biashara nchini katibu mkuu wa jumuiya ya wafanyabiashara JWT Abdallah Mwinyi amesema kuwepo kwa urasimu mkubwa bandarini kunawafanya kutengeneza mianya ya rushwa huku  kamishna wa TRA nchini Edwin Mhede akimtaka kila mfanyabiashara kuviripoti vitendo vyote vya rushwa kwani vinaikosesha nchini Mapato.

“Forodha aangaliwe kwa makini nap engine sheria zibadilishwe kwenye udhaminishaji na uondoshaji mizigo bandalini” alisema Abdallah Mwinyi

Katika mkutano huo wizara nne zenye mahusiano ya karibu na wafanyabiashara zimealikwa ikiwemo ya viwanda na biashara ,tamisemi, fedha na uwekezaji.


Share:

VIDEO: Rais Magufuli apokea hati za utambulisho wa balozi wa zimbabwe nchini tanzania

Balozi mteule wa Zimbabwe nchini Tanzania, Meja Jenerali Anselem Nhamo Sanyatwe, amekabidhi hati za utambulisho kwa Rais Magufuli leo Agosti 29 Ikulu Jijini Dar es Salaam


Share:

World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC)

World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC) Applications are open for the World Bank Youth Summit 2019 Competition. The Competition challenges young social entrepreneurs to submit innovative proposals for scalable enterprises that leverage smart technology to build sustainable and inclusive cities that will serve the needs of… Read More »

The post World Bank Youth Summit 2019 Competition for Young Social Entrepreneurs (Win funded trip to Youth Summit in Washington, DC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Commonwealth Youth Awards 2020 for excellence in development work (Win cash prizes and trip to London)

Deadline: October 31, 2019 Nominations for the 2020 Commonwealth Youth Awards are now open. The Commonwealth Youth Awards for Excellence in Development Work 2020 will recognise the contribution of young people towards achieving the Sustainable Development Goals. The Commonwealth Youth Awards recognise the exemplary work undertaken by young people across the 53 member countries. The awards will see winners awarded a cash grant… Read More »

The post Commonwealth Youth Awards 2020 for excellence in development work (Win cash prizes and trip to London) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded)

Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded): commonwealth scholarship 2019/2020, commonwealth scholarship 2020, commonwealth masters scholarship 2019, commonwealth scholarship application portal, how to apply for commonwealth scholarship, how to apply for commonwealth scholarship 2019, commonwealth scholarships 2020, commonwealth phd scholarship 2019 Commonwealth Master’s Scholarships are for candidates from low and middle income… Read More »

The post Commonwealth Master’s Scholarships 2020 for full-time Master’s study at a UK university (Fully Funded) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana

Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana


Share:

Nafasi za Internships- (Mechanism Archives and Records Section)

Posting Title: INTERN – Mechanism Archives and Records Section, Arusha, I (Temporary Job Opening) Job Code Title: INTERN – INFORMATION MANAGEMENT Department/Office: International Residual Mechanism for Criminal Tribunals Duty Station: ARUSHA Posting Period: 28 August 2019 – 26 August 2020 Job Opening Number: 19-Documentation and Information -RMT-117032-J-Arusha (O) Staffing Exercise N/A Org. Setting and Reporting The International Residual… Read More »

The post Nafasi za Internships- (Mechanism Archives and Records Section) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Video Mpya ya Maua Sama – Niteke

Video Mpya  ya  Maua Sama – Niteke


Share:

TENDER: Provision of Transport Services to Tanzania Youth Alliance (TAYOA) under the Global Fund Project

INVITATION OF TENDERS Tanzania Youth Alliance (TAYOA) is locally registered non-profit organization dedicated to improving the health of youth and adult people in Tanzania, with a focus on HIV/AIDS prevention ,reproductive health, entrepreneurship and employ-ability. TAYOA is implementing Global Fund project on HIV Prevention Programs for Adolescent Girls and Young Women -in Morogoro and Dodoma Regions. The organization invites eligible suppliers… Read More »

The post TENDER: Provision of Transport Services to Tanzania Youth Alliance (TAYOA) under the Global Fund Project appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

AJIUA KWA KUNYWA SUMU BAADA YA KUMUUA MKEWE KISHA KUMLAZA KITANDANI KAGONGWA

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard  Abwao
Na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mwanaume aitwaye Paschal Clement Mahona (32) mkazi wa Iponya kata ya Kagongwa wilaya ya Kahama amejiua kwa kunywa sumu baada ya kumuua mkewe Ashura Paschal (30) kwa kumnyonga shingo kisha kumlaza kitandani.


Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard  Abwao tukio hilo limetokea Agosti 28,2019 majira ya saa moja usiku.

"Ashura Paschal ambaye ni mkazi wa Iponya alikutwa akiwa ameuawa kwa kunyongwa shingo na kulazwa kitandani na mmewe aitwaye Paschal Clement Mahona mbaye naye baada ya kufanya mauaji hayo alijiua kwa kunywa sumu ambayo aina yake bado kujulikana na kukutwa chumbani akiwa amelala sakafuni, akitoa povu mdomoni",amesema Kamanda Abwao.

"Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kwani  kabla ya tukio hilo wanandoa hao walikuwa wakigombana huku mume akimtuhumu mkewe kukosa uaminifu katika ndoa yao",ameongeza Kamanda Abwao.

Share:

WAZIRI LUKUVI AOKOA ARDHI YA AJUZA NA KUAMURU ALIPWE FIDIA YA SH. MILIONI 500 NDANI YA MIEZI MITATU


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi, ametoa miezi mitatu kwa wavamizi 110 waliovamia eneo la Ajuza Nasi Murio, mwenye umri wa miaka 98, lenye ukubwa wa hekari nane kumlipa kiasi cha sh. milioni 500 kama fidia.

Lukuvi ametoa agizo hilo Jijini Arusha leo Agosti 28, katika kata ya ya Sinoni ambapo amesema kila mtu atalipa fedha kulingana na ukubwa wa eneo alilopora.

Amesema serikali imewaonea huruma na kwamba watalipa shilingi 20,000 kwa kila mita moja za eneo.

Waziri amesema ili wavamizi hao waweze kurasimishwa na kuwa wamiliki halali watalazimika kulipa gharama za upimaji pamoja na gharama za kupata hati miliki pamoja na kodi ya ardhi.


Share:

73 Jobs at Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC)

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA  PRESIDENT’S OFFICE  PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT  Ref.No.EA.7/96/01/J/68 28th August, 2019  VACANCIES ANNOUNCEMENT  On behalf of Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC); Public Service  Recruitment Secretariat invites dynamic and suitably qualified Tanzanians to fill 73 vacant posts.  1.0 TANZANIA SHIPPING AGENCIES CORPORATION (TASAC) Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) is a Public Institution established under the Tanzania Shipping… Read More »

The post 73 Jobs at Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DKT.GWAJIMA ATAKA VIONGOZI WA VIJIJI KUHAMASISHA WANANCHI KUJIUNGA BIMA YA AFYA CHF ILIYOBORESHWA


Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima,akizungumza na viongozi akiwataka wasaidie kuwahamasisha wananchi kujiunga na bima ya afya ya jamii ya CHF iliyoboreshwa alipotembelea Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma kushuhudia utekelezaji wa kuandikisha Kaya katika mfumo huo.
Muuguzi wa Zahanati ya kijiji cha Chiboli ,Shija Makeja,akielezea jinsi wanavyoshirikiana na uongozi uliopo katika kuhamasisha wananchi kujiunga na bima ya afya ya jamii ya CHF iliyoboreshwa kushoto ni katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima,akimsikiliza.
Meneja mradi wa HPSS Tuimarishe afya, Ally Kebby Abdallah,akizungumzia Azma ya Serikali ni kutengeneza mfumo wa bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa ni kuona mwananchi anatambuliwa lakini pesa anayochangia irudi kwenye kituo.
Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima,akiangalia kibao kinachoonesha ratiba ya kazi katika Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma alipotembelea kushuhudia utekelezaji wa kuandikisha Kaya katika mfumo wa bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa.
Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima,akiwahamasisha wananchi wa kijiji cha Chiboli wajiunge na bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa ili wafurahie huduma bora alipotembelea Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma kushuhudia utekelezaji wa kuandikisha Kaya katika mfumo wa bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa.
Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima,mkazi wa kijiji cha Chiboli anayetumia bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa jinsi inavyookoa maisha ya familia yake pindi anapopata na tatizo
***
Serikali imewataka viongozi wa serikali za Mitaa a vijiji nchini kusaidia kuhamasisha wanachi kujiunga na bima ya afya ya jamii ya CHF iliyoboreshwa ili waondokane na adha pindi wanapokuwa hawana fedha za mkononi kulipia matibabu.

Haya yamebainishwa na katibu mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)anayeshughulikia Afya Dk.Doroth Gwajima alipotembelea Zahanati ya kijiji cha Chiboli wilayani Chamwino mkoani Dodoma kushuhudia utekelezaji wa kuandikisha Kaya katika mfumo huo.

Amesema suala la kuhamasisha wanachi kujiunga na bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa siyo jukumu la wataalam wa afya peke yao kwani wanaotakiwa kulisimamia ni viongozi wa vijiji ambao ndiyo waliokaribu na watu.

"Hili suala la watu kujiunga na bima hii ya afya ya jamii ya CHF iliyoboreshwa ni suala la kushirikishana hawa viongozi wa vijiji kama mwenyekiti wa kijiji na afisa mtendaji wa kijiji ndiyo wenye watu na wenye mikutano ya hadhara ambayo ajenda hii wataifikisha kwa njia rahisi"amesema Dk. Gwajima.

Pia Dk. Gwajima amesema kuwa kama viongozi wa serikali za vijiji watakuwa na ushirikiano na wataalamu wa vituo vya afya nchini wataweza kuibeba ajenga hiyo kwa kuifikisha kwa wanachi na kuweza kuziandikisha kaya zote nchini katika mfumo huo wa CHF iliyoboreshwa.

Kwa upande wake Muuguzi wa Zahanati hiyo Shija Makeja,amesema kuwa kupata mafanikio ya kuwa na idadi kubwa ya wanachama wa bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa kumetoka na kushirikiana kwa karibu na viongozi wa serikali ya kijiji.

Amesema kutokana na kuhudumia idadi kubwa ya watu wanaotumia CHF iliyoboreshwa wameweza kupata fedha za kujiendesha na kuondokana na changamoto za ukosefu wa madawa ambao awali ulikuwa kikwazo.

Nae Meneja mradi wa HPSS Tuimarishe afya, Ally Kebby, amesema kuwa azma ya serikali ni kutengeneza mfumo wa bima ambao mwanachi atatambuliwa na pesa anayochangia itarudi kwenye kituo.

Mradi wa HPSS Tuimarishe afya unafadhiriwa na shirika la maendeleo na ushirikiano la Uswisi kwa kushirikana na serikali ya Tanzania ambao umechangia katika kuunda mfumo wa kutendea kazi wa IMIS na kutoa mafunzo kwa waandikishaji waratibu na wasimazi wa CHF iliyoboreshwa nchini.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger