Tuesday 2 July 2019

Picha : MDAU WA BLOG ZA KIJAMII MABULA KUTOKA NHIF TANGA AACHANA NA UKAPERA



Mdau wa Blog za Kijamii Peter Mabula kutoka ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) kushoto akiwa na Mkewe Jenipher Peter wakiingia kwenye Ukumbi wa Regail Naivera mara baada ya kufunga ndoa kwenye Kanisa Katoliki la St.Anthony Chumbageni Jijini Tanga
Mdau wa Blog za Kijamii Peter Mabula kutoka ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) wa pili kutoka kushoto akiwa na Mkewa Janipher Peter wakiwa na wasimamizi wao.
Mdau wa Blog za Kijamii Peter Mabula kutoka ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) wa pili kutoka kushoto akiwa na Mkewa Janipher Peter wakiwa na wazazi na ndugu.
Mdau wa Blog za Kijamii Peter Mabula kutoka ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) wa pili kutoka kushoto akiwa na Mkewa Janipher Peter wakiwa na wanafamilia.
Sehemu ya wageni waliokuwepo kwenye Sherehe hiyo ya harusi hiyo kulia ni Mhandisi Geofrey Hilly ambaye ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa).
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu katika aliyevaa suti akiwa na watumishi wa Mfuko huo wakati wa sherehe ya Harusi ya mtumishi mwenzao Peter Mabula.
Alawi Kupaza wa NHIF Tanga akitoka kumpongeza Bwana Harusi.
Wafanyakazi wanzake na Peter Mabula wakimpongeza.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akitoa nasaha kwa Bwana Harusi Peter Mabula kushoto ni Mhasibu wa NHIF Mkoa wa Tanga Hellena Manyanda.
Msimamizi wa NHIF Ofisi ya Tanga Dinna Mlwilo akizungumza wakati wa sherehe hiyo kulia ni Maneja wa NHIF Mkoa wa Tanga Ally Mwakababu 
Mhasibu wa NHIF Hellena Manyanga akiwa na watumishi wenzake
Share:

MAONESHO YA 43 YA BIASHARA YA KIMATAIFA KUFUNGULIWA

 Afisa Mwandamizi wa Malipo, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma,(PSSSF), Bi.Nyangi Masalu (kulia), akimuhudumia aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kuendeleza Biashahara Nchini (Tan Trade), ambaye sasa ni Mstaafu na Mwanachama wa PSSSF, Bi.Jacqueline Mneney Maleko (kushoto), alipofika kwenye banda namba 13 la PSSSF/NSSSF viwanja vya Sabasaba barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Maonesho hayo yamefunguliwa rasmi hii leo Julai 2, 2019.
Afisa Matekelezo Mwandamizi wa PSSSF, Bw. Donald Peter Maeda (kulia), akimsikiliza Mwanachama huyu aliyefika banda la Mfuko kupatiwa huduma.
 Mkurugenzi wa banda la PSSSF Bi.Eunice Chiume (kushoto), akimsikiliza Mwanachama wa Mfuko huo, aliyetembelea banda hilo kupatiwa huduma.
Muonekano wa banda namba 13 la PSSSF.
 Afisa Matekelezo PSSSF, Bi. Getrude Athanas (kulia), akimuhudumia Mwanachama wa Mfuko aliyefka yeye na familia yake kwenye banda la PSSSF ambalo linatumika kwa ushirikiano na NSSSF.
 Afisa Matekelezo PSSSF, Bi. Getrude Athanas (kulia), akimuhudumia Mwanachama wa Mfuko aliyefka yeye na familia yake kwenye banda la PSSSF ambalo linatumika kwa ushirikiano na NSSSF.
Afisa Uhusiano Mwandamizi PSSSF, Bw. Abdul Njaidi (aliyekaa), kwa kushirikiana na Afisa Mafao, wa Mfuko Bw. Salvatory Matemu kutafuta taarifa za michango ya Mwanachama (hayupo pichani).
Afisa Uhusiano Mwandamizi PSSSF, Bw. Abdul Njaidi (kushoto) na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Sebera Fulgence wakibadilishana mawazo wakati Bw. Sebera ambaye ni Mwanachama wa PSSSF alipotembelea banda la Mfuko kupata taarifa za michango yake.
Share:

MKUTANO WA 23 WA TAASISI ZA MAWASILIANO AFRIKA MASHARIKI (EACO) WAANZA JIJINI MWANZA


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye (wapili kushoto), akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasilkiano Tanzania (TCRA), Mhandisi James M. Kilaba (watatu kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya (TCRA), Dkt. Jones Killimbe (wanne kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa EACO Dtk. Ally Yahya Simba(wakwanza kulia) na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Mawasiliano Bw.Mulembwa Munaku. (wakzwanza kushoto), baada ya kufungua mkutano wa 23 wa Taasisi zinazosimamia Mawasiliano Afrika Mashariki (EACO), utakaofuatiwa na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa 26 wa EACO jijini Mwanza Julai 1, 2019
Muwakilishi wa Umoja wa Shirika la Posta Duniani (upu), Kusini mwa Afrika na Asia, Bi. Gladys Mutyavaviri ambaye
alimwakilisha Katibu Mkuu wa upu, akizungumza kwenye mkutano huo wakati wa ufunguzi.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James M. Kilaba, akizungumza na waandishi wa habari kufafanua baadhi ya mambo kuhusu mkutano huo.
Wajumbe kutoka Burundi, wakisikiliza hotuba ya Mhe. Naibu Waziri.
Wajumbe kutoka Kenya, wakisikilza hotuba ya Mhe. Naibu Waziri.
Wajumbe kutoka Rwanda, wakisikiliza hotuba ya Mhe. Naibu Waziri.
Wajumbe wenyeji Tanzania, wakimsikiliza Mhe. Naibu Waziri Mhandisi Nditiye wakati akifungua mkutano huo.
Wajumbe kutoka Uganda, wakisikilzia hotuba ya Mhe. Naibu Waziri.
Mhe. Naibu Waziri Mhandisi Nditiye na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka mataifa wanachama wa EACO. 
***
MKUTANO wa 23 wa Taasisi zinazosimamia Mawasiliano kwa Nchi za Afrika Mashariki, (EACO) umeanza leo Julai 1, 2019 jijini Mwanza.

Sambamba na mkutamno huo pia wajumbe watashiriki  Mkutano Mkuu wa 26 wa EACO ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kuiweka Afrika Mashariki katika eneo la Uchumi wa Kidijitali".Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi, Atashasta Nditiye, ndiye aliyefungua mkutano huo utakaodumu hadi Julai 5, wenyeji ni Tanzania, pamoja na mataifa mengine ya WAC, ambayo ni Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. 

Share:

KAMPUNI YA TIGO TANZANIA NA TECNO WAZINDUA SIMU MPYA



Meneja wa Bidhaa za intaneti wa Tigo, Mkumbo Myonga, (kushoto) akionyesha kwa waandishi wa habari simu mpya za Smartphone aina ya TECNO S3 na TECNO R7, wakati wa uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Saba Saba jijini Dar es Salaam. (kulia) ni Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Mobile, Eric Mkomoya.
Meneja wa Bidhaa za intaneti wa Tigo, Mkumbo Myonga, (kushoto) akimsikiliza Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Mobile, Eric Mkomoya (kulia) wakati akionyesha kwa waandishi wa habari simu mpya za Smartphone aina ya TECNO S3 na TECNO R7, wakati wa uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Saba Saba jijini Dar es Salaam leo
Meneja wa Bidhaa za intaneti wa Tigo,Mkumbo Myonga, (kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu aina ya TECNO S3 mmoja wa waandishi wa habari waliojishindia zawadi ya simu wakati wa uzinduzi simu hizo uliofanyika katika viwanja vya Saba Saba.jijini Dar es Salaam (kulia) ni Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Mobile, Eric Mkomoya.
Meneja wa Bidhaa za interneti wa Tigo, Mkumbo Myonga, (kushoto) akiwa na waandishi wa habari waliojishindia zawadi ya simu za TECNO s3 na TECNO S7 wakati wa uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Saba Saba. (kulia) ni Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Mobile, Eric Mkomoya.


*Kuwezesha mteja kupata Intaneti bure kwa mwaka mmoja

Kampuni inayoongoza kwa ubunifu wa kidigitali ya Tigo kwa kushirikiana na kampuni ya kimataifa ya kutengeneza simu za kisasa ya TECNO Mobile ,zimezindua aina mbili mpya ya simu janja za kisasa (smartphones) aina ya TECNO S3 na TECNO R7, katika soko la Tanzania,ambazo zitapatikana kwa bei nafuu na kuwawezesha wateja kufurahia matumizi ya Intaneti kupitia aina za vifurushi watavyochagua kujiunga nayo.

Akiongea wakati wa uzinduzi uliofanyika leo katika uwanja wa maonyesho ya Saba Saba,Meneja wa Bidhaa za Intaneti wa Tigo Tanzania,Mkumbo Myonga,alisema kuzinduliwa kwa simu mpya kwa ushirikiano na kampuni ya TECNO Mobile, kwa mara nyingine kunadhihirisha mkakati wa kampuni ya Tigo katika ubunifu wa kidigitali nchini na kufanikisha kuongeza watumiaji wa simu janja,watumiaji wa huduma za data na interneti ya kisasa ya 4G.

“Tunayo furaha kushirikiana na TECNO Mobile leo kuzingua aina mbili za simu janja za kisasa kwa mwaka huu wa 2019.Simu aina ya TECNO S3 na TECNO R7 ni simu zinazatikana katika mtandao wa Tigo pekee katika soko na zinapatikana kwa gharama nafuu ambazo wateja wengi wanamudu kuzinunua”,alisema Myonga.

Myonga alieleza kuwa Tigo inatoa MWAKA MMOJA WA BURE wa kutumia internet kwa wateja watakaozinunua ambapo watakaonunua simu aina ya TECNO R7 watapata (GB54) ambazo zinawezesha matumizi ya internet ya 4G na inauzwa kwa bei ya shilingi 124,900/-.

Kwa wateja watakaonunua simu aina ya TECNO S3,ambayo inawezesha matumizi ya internet ya 3G,watakuwa na uhuru wa kuchagua ofa wanayotaka, ya kwanza MWAKA MMOJA WA BURE wa kutumia internet kutokana na kupatiwa GB 48 na gharama ya kununua simu iyo ni shilingi 95,000/-.Ofa ya pili kwa kunua simu inayouzwa shilingi shilingi 74,900/- na kujipatia internet yenye GB3 ambayo inawezesha mteja kuitumia miezi mitatu bure.Simu hizi mpya katika soko la Tanzania zinapatikana katika maduka yote ya Tigo nchini na zitapatikana katika banda la maonyesho la Tigo lililopo katika uwanja wa maonyesho ya Saba Saba.

Kwa upande wake,Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Mobile, Eric Mkomoya, alisema kuzinduliwa kwa simu aina ya TECNO S3 na TECNO R7 kupitia mtandao wa Tigo umelenga kuwezesha wananchi wengi kutumia simu janja na kuweza kufurahia mapinduzi ya ubunifu wa kidigitali ya matumizi ya simu hizi.

“Simu aina ya TECNO R7 imetangenezwa ikiwa na kioo cha ukubwa wa inchi 5,ina scanner ya kisasa,kamera yenye uwezo wa mega 5 upande wa mbele na nyuma na flashi inayowezesha kuchua picha kwa kiwango cha ubora wa juu,imetengenezwa kwa ubunifu wa tekbolojia mbalimbali za kisasa zinazowezesha matmizi ya internet na kupiga picha.Simu ya aina ya TECNO S3 imetengenezwa kwa teknolojia za kisasa zinazowezesha matumizi ya teknolojia ya Android Go OS ,inao ukubwa wa kioo cha mbele cha inchi 4,inawezesha matumizi ya teknolojia za GPS na dual SIM,ambazo zimeongezwa katika simu za Tecno tolea la sasa hivi,”alisema Mkomoya.

Simu zote za TECNO S3 na TECNO R7 zina waranti ya miezi 13.
Share:

NSSF NA PSSSF WASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA SABASABA KWA PAMOJA

Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF Bi Lulu Mengele akitoa  elimu kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF katika banda la NSSF  na PSSSF katika maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika
viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.
Afisa Uhusiano wa NSSF Bi Aisha Sango akitoa ufafanuzi kwa mgeni alietembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya kimataifa ya  Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.
Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF Bi Lulu Mengele akitoa  elimu kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF katika banda la NSSF  na PSSSF katika maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika
viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.
Afisa matekelezo wa NSSF Ndugu Abdulaziz Abeid akitoa ufafanuzi kwa mgeni  alietembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya  kimataifa ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.
Maafisa Uhusiano wa NSSF (Aisha Sango, Kushoto na Amani Marcel, Katikati) na  wa PSSSF (Coleta Mnyamani) wakitoa elimu kwa wageni mbalimbali kuhusu  huduma mbalimbali zitolewazo na Mifuko hiyo katika maonesho ya  kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere  barabara ya Kilwa.
Afisa Uhusiano wa PSSSF ndugu Abdul Njaidi akitoa ufafanuzi kwa mgeni  aliyetembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya  kimataifa ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya 
Kilwa.
Share:

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 


Share:

Isikupite Hii! 👉Naitwa Chief Karim Wa Sultan.....Ni Bingwa Na Mtabiri Wa Nyota

Isikupite hii! 👉Naitwa CHIEF KARIM WA SULTAN Kutoka- TANGA - TANZANIA: Ni Bingwa, Mnajimu na Mtabiri wa Nyota na Matatizo yote ya ndoa/mahusiano.

Natabiri nyota yako, Kung'alisha nyota, Kufungua nyota zako za mafanikio zilizo fungwa  na kusababisha usifanikiwe katika maisha yako, au unajikuta unafanya kazi/biashara unapata hela lakini pesa yako haikai yaani inapita tu katika mikono yako.

Nawezesha  NYOTA, ni UTAJIRI usio na kafara yoyote na ni UTAJIRI unaoendana na nyota yako tu.

Hakika watu wengi wanazidi kufanikiwa na kutimiza ndoto zao , Kulipwa haraka haki zako unazodai, Mvuto wa mapenzi, kumrudisha mpenzi, mme au mke aliyekuacha/kukutelekeza.

 Je unapata wapenzi/wachumba lakini wanakuacha bila kujua sababu? Nitakusaidia!

Kufungua kizazi chako kilichofungwa na kusababisha usipate mimba/mtoto au unashika mimba zinatoka/kuharibika na maumivu makali ya tumbo/chango.

 ðŸ‘‰KWA TATIZO LOLOTE  LA KINYOTA WASILIANA NAMI 👉WhatsApp : 0763 103 527
au
👉PIGA SIMU  : 0716 681 318
👉 0688 745 790


Share:

Mambo Sasa Amjibu Zitto Kabwe Sakata la Kutekwa Raia wa Kenya

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam (SACP) Lazaro Mambosasa, amewataka watu wenye taarifa zitakazosaidia upatikanaji wa  Raphael Ongangi, waziwasilishe ofisini kwake ili zifanyiwe kazi.

Akizungumzia juu ya kauli zilizotolewa na kiongozi wa ACT Wazalendo,  Zitto Kabwe juu ya alipo Raphael,  kamanda amesema taarifa hizo  ni za mitandaoni, na kwamba wao hawafanyii kazi mambo ya mitandao.

“Hizo habari za mitandao kila mmoja anatoa anavyofikiria, cha msingi ambacho sisi tungeweza kukiona cha maana kama kuna jambo lolote lipelekwe kituo cha polisi, ofisi yangu ipo, kama kuna mtu ana taarifa alete". alisema Mambosasa.

Siku ya Julai Mosi, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, aliahidi kuwasilisha ushahidi wa eneo alilowekwa Raphael, kuanzia siku ya kwanza alipotekwa hadi siku ya Jumamosi.

Raia huyo wa Kenya ambaye ana mke na watoto wawili, alitekwa Juni 24 maeneo ya Oyserbay Dar es salaam ambapo hadi sasa bado hajapatikana.


Share:

PICHA: Muonekano wa jengo namba 3 (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere

Picha hizi ni za Muonekano wa jengo namba 3 (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam likiwa katika majaribio. 

Jengo hilo lina uwezo wa kuhifadhi ndege kubwa 24 kwa wakati mmoja, na litahudumia abiria milioni 6 kila mwaka.


Share:

Tundu Lissu Afunguka sababu ya kutomwandika barua spika wa Bunge, Job Ndugai

Aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameeleza sababu ya kutomwandika barua spika wa Bunge, Job Ndugai kumjuliusha kuwa yupo nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Wiki iliyopita Spika Ndugai alitangaza kumvua ubunge Lissu kwa kile alichoeleza kuwa kiongozi huyo hajulikana halipo zaidi ya kuonekana nchi za Ulaya na Marekani.

"Ni kweli sijawahi kumuandikia Spika Ndugai barua yoyote kuhusu mahali nilipo, na hali yangu ya kiafya. Sikumwandikia, sio kwa sababu nilisahau au nilipuuza, bali ni kwa sababu Spika Ndugai alikuwa anafahamu fika mahali nilipo, na sababu za mimi kuwa huko," amesema Tundu Lissu.

Ameendelea kwa kusema, "Kwa sheria na taratibu za Bunge, Spika na watendaji wake wanawajibika kufuatilia hali ya mbunge anayetibiwa nje ya nchi, na kutoa taarifa za maendeo yake. Sio wajibu wa mbunge mgonjwa kulitaarifu Bunge juu ya afya yake. Ndugai alipaswa kujua nilipo, na maendeleo yangu." Lissu,".

Aidha, Tundu Lissu amesema licha ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kudai hakujaza fomu za mali na madeni za viongozi wa Umma bado ana sifa za kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

"Ili upoteze sifa ya kugombea ubunge au urais sharti uwe na hatia, sasa mimi sijakutwa na hatia na mahakama au mahakama ya Sekretarieti ya maadili, Ndugai peke yake hawezi kunitia hatiani bila kunisikiliza."

"Kwa hiyo mimi naweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi iwe ubunge au urais. Kama wanataka nisigombee wanipeleke mahakamani au kwenye mahakama ya sekretarieti na wakiniuliza kwa nini sijajaza fomu nitawaambia nitawezaje kujaza nikiwa nje ya nchi," amesema Lissu

Amesema fomu hizo zinapaswa kujazwa na kuziwasilisha kwa njia ya mkono lakini zinapaswa kusainiwa na wakili wa Tanzania, "Sasa mimi niko hospitalini Ubelgiji, nawezaje kuzijaza, huku nampata wapi wakili, nawezaje kuzipeleka kwa mkono? Kwa hiyo walipaswa kuniuliza kwa nini sijajaza na si kuzungumza sijajaza bila kuwa na sababu."


Share:

NDUGAI AFURAHISHWA NA UCHAPAKAZI WA MKURUGENZI MKUU WA TMA


 Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ameonesha kufurahishwa na utendaji kazi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi.

‘Utendaji wako wa kazi ni wa kiwango cha juu, tunaona mafanikio ya TMA katika utoaji wa taarifa za hali ya hewa nchini kwa usahihi zaidi kulinganisha na huko nyuma ’ Alizungumza mhe. Ndugai

Mhe. Ndugai aliendelea kwa kumpongeza Dkt. Kijazi kwa kuchaguliwa kuwa makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwani imeonesha kazi kubwa inayofanywa na  TMA chini ya uongozi wake hivyo kumpa nafasi ya kushinda kwa kishindo na kuiletea sifa nchi katika nyanja za kimataifa.

Katika hatua nyingine, wabunge wa Bunge la JMT walimpongeza Dkt. Kijazi kwa shangwe kubwa mara alipotambulishwa ndani ya Bunge hilo na Mhe. Spika kama makamu wa tatu wa Rais wa WMO. 

Wabunge walionekana wakishangilia kwa furaha kuashiria kukubaliana na pongezi zilizokuwa zinawasilishwa na mhe. spika kwa niaba ya wabunge wote kabla ya kuahirisha rasmi vikao vya bunge la bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20

Naye, Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye alipata wasaa wa kuliambia Bunge jinsi mchakato wa uchaguzi ulivyoenda na umuhimu wa nafasi hiyo ya juu kwa TMA, Tanzania na Afrika, sambamba na kulishukuru Bunge kwa ushirikiano waliouonesha katika kampeni za awali wakiwakilishwa na Mhe. Mboni Mhita , mbunge wa Handeni Vijijini.

Dkt. Kijazi alikutana na Mhe. Spika na kuhudhuria Bunge kupitia mwaliko wa Mhe. Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano uliokuwa na lengo la kumtambulisha mteule wa nafasi ya makamu watatu  wa Rais wa WMO kutoka Tanzania na kutoa shukrani za ushirikiano wa Bunge hilo. 

Aidha, Dkt. Kijazi alimshukuru Mhe. Spika kwa pongezi na kuahidi kuongeza juhudi katika utekelezaji wa majukumu ya TMA na WMO ili kuendelea kuiletea heshima nchi katika sekta ya hali ya hewa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA (TMA)
(Picha kwa hisani ya Ofisi ya Bunge)


Share:

SAFARICOM YAMTEUA MICHAEL JOSEPH KUKAIMU NAFASI YA MTENDAJI MKUU ALIYEFARIKI JANA

Kampuni ya Safaricom imemteua ofisa mtendaji mkuu wake wa zamani, Michael Joseph kukaimu nafasi ya mtendaji mkuu iliyoachwa na Bob Collymore aliyefariki dunia jana Julai 1, 2019.
Kwenye mkutano maalumu wa wakurugenzi jana Jumatatu, bodi ya kampuni imeamua kumteua Michael Joseph kuongoza ambapo utekelezaji unaanza mara moja.
“Joseph atashikilia wadhifa huo hadi pale kampuni itakapotoa tangazo jingine kuhusu uteuzi wa kudumu,” Safaricom ilisema kwenye taarifa yake.
Joseph ni mjumbe katika bodi ya Safaricom na ni mwenyekiti wa sasa wa Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways.
Mwili wa Collymore aliyechukua wadhifa huo kutoka kwa Joseph Novemba 2010, utazikwa leo jijini Nairobi katika tukio litakalohusisha tu wanafamilia.
Share:

SERIKALI YAJIPANGA KUZUIA MBU WAAMBUKIZAO HOMA YA DENGUE


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka waganga wakuu wa mikoa kuchukua hatua za makusudi kuzuia mbu waambukizao homa ya dengue na kusisitiza mikoa iliyo mpakani kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa ebola.

Waziri Mwalimu ameagiza hayo jana jijini Dodoma wakati akifungua mkutano kikao kazi cha viongozi mbalimbali wa hospitali za rufaa za mikoa.

Alisema waganga wakuu ambao maeneo yao yamekumbwa na ugonjwa wa homa ya dengue na hata mikoa ambayo haijakumbwa na tatizo hilo kuhakikisha wanaangamiza mazalia kwa kutumia dawa ya viuadudu.

“Ninachotaka kusisitiza kwa waganga wakuu, najua wenzetu katika wilaya na halmashauri wanaweza wasituelewe, lakini lazima tuchukue hatua za kudhibiti mbu, hakuna maajabu mengine ambayo tutayafanya zaidi ya kudhibiti mbu.

“Kwa hiyo zile lita chache tunazowapa za dawa kuna wengine wanaona muda unaenda wanaenda katika mito wanazimwaga, hapana, lazima tukafanye kazi ya kunyunyuzia katika mazalia ya mbu,” alisema Ummy.

Alisema mashine hizo zitasambazwa katika baadhi ya mikoa ambayo ina mazalia na kuwataka waganga wakuu kuwabana wakurugenzi watenge bajeti kwa dawa hizo.

“Kipekee nimpokeze Mganga Mkuu wa Dar es Salaam amepambana sana na bahati nzuri Katibu Tawala wake amemshika vizuri, nasema kwamba ukipewa majukumu lazima ufanye kazi.

“Tanga sijaona jitihada zozote kukabiliana na dengue, nasema kweli kwa sababu mimi natoka Tanga ila watu wanaumwa, Pwani angalau kidogo,” alisema.

Kuhusu ugonjwa wa ebola, alisema Serikali inaendelea kuchukua hatua za kukabiliana nao kama utatokea huku akiupongeza Mkoa wa Mwanza kwa jinsi ulivyojiandaa kuukabili.

“Ebola bado ni tishio nchini, nilitoa taarifa kwa umma, lakini hakuna ‘case’ mpya zaidi ya zile zilizotokea. Habari mbaya ni kwamba WHO wamesitisha huduma DRC kwa sababu gari la watumishi limechomwa moto kule.

“Ina maana itazidi, kwa hiyo tuendelee kuchukua hatua Mwanza, Kigoma, Rukwa Songwe na Dar es Salaam, ila kipekee nimpongeze Mganga Mkuu wa Mwanza amefanya kazi nzuri kama mgonjwa atatokea jinsi ya kumhudumia,” alisema.

Ummy alisema wameagiza mashine 70 za X-ray ambazo zitafungwa katika hospitali za rufaa za mikoa pamoja na mnashine 20 za X-ray za meno ambazo nazo zitafungwa katika hospital hizo.


Share:

Iran Yasema Imezidisha Kiwango cha Madini ya Urani

Waziri wa Mambo ya Nchi za Kigeni wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema  kuwa Iran imezidisha  ukomo wa viwango vya madini yake ya urani katika hifadhi zake, uliowekwa chini ya mkataba wa 2015 wa nyuklia. 

Shirika la habari la Iran - ISNA limeripoti kuwa Iran ilipitisha kiwango cha ukomo wa kilo 300 kwenye mpango wake. 

Marekani ilijiondoa kwenye mpango huo wa nyuklia mwaka jana na ikaiwekea Iran vikwazo vikali kama sehemu ya kampeni ya kuiongezea mbinyo mkali. 

Kwa kulipiza kisasi, mnamo Mei 8, Iran ikatangaza kuwa haitaheshimu tena viwango vya mwisho vilivyowekwa vya hifadhi zake za madini ya urani yaliyorutubishwa. 

Ilitishia pia kwenda mbali zaidi na kuachana na ahadi zake za nyuklia kama washirika waliobaki katika mkataba huo, ambao ni pamoja na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani na Urusi, hawataisaidia nchi hiyo kutokana na vikwazo ilivyowekewa na hasa vya kuuza mafuta yake. 

Muda mfupi baada ya tangazo hilo la Iran kutolewa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti matumizi ya nishati ya nyuklia - IAEA limethibitisha kuwa Iran ilipindukia ukomo wa viwango vyake vya madini ya urani.


Share:

Daktari Atoa Ushahidi Kesi Ya Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA

Shahidi wa tano, Inspekta Msaidizi Dk. Juma Alfani (54) katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake, amedai mahakamani kwamba aliwapokea Koplo Rahim na Konstebo Fikiri wakiwa wanapiga kelele za kulalamika maumivu ya majeraha waliyopata kwenye maandamano.

Kadhalika, amedai kuwa Koplo Rahim alikuwa anaweweseka huku akilalamika maumivu shingoni kwa sababu alikuwa hajitambui na Konstebo Fikiri alikuwa anavuja damu nyingi kichwani.

Madai hayo aliyatoa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, wakati akisikiliza ushahidi wa Jamhuri dhidi ya vigogo tisa wa Chadema.

Jopo la Jamhuri liliongozwa na Mawakili wa Serikali Wakuu Faraja Nchimbi, Paul Kadushi, Dk. Zainabu Mango, Mawakili wa Serikali Jacqueline Nyantori, Wankyo Simon na Salimu Msemo.

Akiongozwa na Wakili Msemo, shahidi alidai kuwa Februari 16, mwaka jana, alikuwa kazini zamu ya usiku.

"Saa 5:40 usiku nikiwa wodi ya wazazi alikuja muuguzi wa zamu akaniarifu nahitajika kitengo cha dharura. Nilipokwenda niliwakuta wagonjwa wawili mmoja akivuja damu, huku akipiga kelele za maumivu na mwingine akiwa anaweweseka hana fahamu," alidai.

Aliongeza katika ushahidi wake kuwa: "Niliwaagiza wauguzi wawachome sindano za maumivu, nikamhoji aliyekuwa anatokwa damu kichwani, Fikiri kimetokea nini, akanieleza walikuwa wanatuliza maandamano ndipo wakajeruhiwa.

“Nilipojaribu kumhoji Rahim alikuwa anaweweseka na kuonyesha maumivu kwenye shingo upande wa kulia," alidai Dk. Alfani ni daktari wa Hospitali ya Polisi Barabara ya Kilwa ambayo ni ya rufani kwa zahanati zote za polisi.

Alidai kuwa baada ya kuwakagua majeruhi na kujiridhisha aliagiza wapelekwe wodini na walilazwa mpaka Februari 18, mwaka jana waliporuhusiwa. Pia alidai kuwa baada ya Rahimu kuendelea kulalamika maumivu aliagiza akafanyiwe kipimo cha CT Scan. Kesi hiyo inaendelea leo kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri.

Jopo la utetezi liliongozwa na Wakili Profesa Abdallah Safari, Peter Kibatala, John Mallya na Hekima Mwasipu.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya; Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko; Katibu Mkuu wa Chadema, Vicent Mashinji; Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika; Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Februari Mosi na Februari 16, mwaka huu Mbowe na wenzake wakiwa Kinondoni, Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama na wengine ambao hawapo mahakamani ya kutenda kosa la jinai ikiwamo kuendelea na mkusanyiko isivyo halali na kusababisha chuki na uchochezi wa uasi.

Ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana, Bulaya alishawishi kutenda kosa la jinai katika viwanja vya Buibui vilivyoko Kinondoni, Dar es Salaam kwa kuwataka wakazi wa eneo hilo kufanya maandamano yenye vurugu.

Pia ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana katika barabara ya Kawawa eneo la Konondoni Mkwajuni kwa pamoja washtakiwa na wenzao zaidi ya 12, walifanya mkusanyiko na kukaidi amri halali ya ofisa wa Jeshi la Polisi Gerald Ngiichi na kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na askari polisi wawili Konstebo Fikiri na Koplo Rahim Msangi kujeruhiwa.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger