Sunday 30 June 2019

Donald Trump Kawa Rais wa Kwanza wa Marekani Kukanyaga Ardhi ya Korea Kaskazini Leo....Tazama Picha

Rais Donald Trump amekuwa rais wa kwanza wa Marekani kukanyaga ardhi ya Korea Kaskazini.

Trump amekutana leo na Kim Jong-un, kiongozi wa Korea Kaskazini katika mpaka usiokuwa wa kijeshi wa Korea Kaskazini na Korea Kusini, ambapo Trump amevuka mstari wa mpaka huo na kukanyaga ardhi ya Korea Kaskazini.

Baada ya kuvuka mstari unaoashiria mpaka wa nchi mbili hizo jirani, Trump amesema, "Hii ni fahari kubwa kwangu, Sikutaraji. Kuuvuka mstari huu ni jambo kubwa kwangu."

Trump ameambatana na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in katika safari yake hiyo. Hii ni katika hali ambayo Trump awali alikuwa ametangaza kwamba hatokutana na Kim Jong-un katika safari yake ya Peninsula ya Korea.
 
Kiongozi wa Korea Kaskazini kwa upande wake amesema, "Trump amekuwa rais wa kwanza wa Marekani kuingia katika nchi yetu. Hatua hii inaashiria azma ya kufuta uhasama wa nyuma, na kufungua ukurasa mpya."

Rais wa Marekani na kiongozi wa Korea Kaskazini wamekutana mara mbili nchini Singapore na Vietnam, lakini vikao hivyo havijakuwa na tija, kwani Washington imeendelea kuiwekea Pyongyanga vikwazo, huku Pyongyanga nayo ikiendelea kufanyia majaribio makombora yake.


Share:

Trump na Xi wa China wakubaliana kusitisha uhasama wao kibiashara

Rais wa Marekani Donald Trump, leo amesifia mazungumzo kati yake na rais wa China Xi Jinping na kuyataja kuwa mazuri kuliko yalivyotarajiwa, na ameahidi kusitisha kuongeza ushuru kwa bidhaa za China wakati mazungumzo kati yao yakiendelea.

 Siku moja tu baada ya mazungumzo yao mjini Osaka Japan, pembezoni mwa mkutano wa kilele wa nchi wanachama wa G20, Trump ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa ubora wa mazungumzo ni muhimu zaidi kwake kuliko kasi. 

Kwa hivyo hana haraka, lakini mambo yanaonekana kuwa mazuri. 

Trump na Xi walikubaliana kufanya mazungumzo ya kusitisha uhasama wa kibiashara kati ya nchi zao. Trump alithibitisha kuwa Marekani imejitolea kutoongeza ushuru mpya kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka China. 

Marekani na China zimekuwa kwenye mzozo wa kibiashara huku pande zote zikiongeza ushuru kwa bidhaa.


Share:

Wadau mkoani Njombe watoa msaada kwa mahabusu na wafungwa

Na Amiri kilagalila-Njombe
Shirika lisilo la kiserikali la Njombe youth development organization (NJOYODEO) kwa kushirikiana na umoja wa vijana chama cha mapinduzi (CCM) mkoani Njombe wamewatembelea wafungwa na mahabusu katika gereza la mkoa mpechi  na kutoa msaada  ikiwemo mashuka na mablanketi  ili kuwaondolea dhana ya kwamba kundi hilo limesahaulika katika jamii.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo mkuu wa gereza la mkoa wa Njombe SP Charles Myinga amesema idadi kubwa ya wafungwa na mahabusu gerezani hapo wanakabiliwa na kesi za mauaji ambazo chanzo chake ni migogoro ya ardhi, ushirikina na tamaa ya utajiri na kuendelea kuisisitiza serikali na mahakama kuongeza nguvu katika usikilizaji wa kesi za mauaji

Aidha Myinga amesema gereza linakabiliwa na changamoto nyingi hivyo msaada uliotolewa na wadau hao utasaidia kupunguza changamoto licha ya kuwa na uhitaji mkubwa kwa mahabusu,huku jeshi hilo pia likiwa na uhaba wa makazi ya askari.

“Sisi tunatoa shukrani lakini bado uhitaji ni mkubwa na sasa hivi jeshi tunauhaba wa makazi ya askari,na kwa sasa tunafyatua matofari ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari kwa hiyo kama kuna wadau wanaoweza kujitolea mabati,misumari,mbao  sisi vyote tunapokea lengo letu askari wapate makazi”alisema Myinga

Hamis Kasapa ni mkurugenzi wa NJOYODEO na Nehemia tweve ni mwenyekiti  wa umoja wa vijana UVCCM mkoa wa Njombe, wamesema  sababu  zilizowagusa kutembelea  katika gereza hilo ni uwepo wa idadi kubwa ya vijana waliofungwa pamoja na mahabusu jambo ambalo linaonyesha kundi la vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa lakini idadi kubwa wako hatarini kuishia gerezani .

“Yapo malengo mengi yaliyotufanya kufika hapa kwa  wenzetu waliopo magereza,lakini tumebaini changamoto ambazo wenzetu wanakumbana nazo kuna zingine ni za kawaida ambazo zipo ndani ya uwezo wetu na tunazimuda katika kuzifanyia kazi,lakini kwa changamoto kubwa moja mlundikano wa kesi au kulimbikizwa kwa kesi na muda wa vikao vya mahakama,tutajitahidi kwa nafasi zetu kuona namna gani wanaohusika wanaweza kutusaidiaje ili jambo hili liweze kufanyika kwa wakati”alisema Nehemia Tweve

Kwa upande wake Hamisi Hassan Kasapa amesema kuwa  wameahidi  Jully 2 kufikisha screen kwa ajili ya akina baba na akina mama pamoja na radio zitakazoweza kugawanywa spika katika vyumba vya kulala kwa kufuata utaratibu  ili  kuweza kujua nini kinachoendelea katika nchi yao.

Aidha amesema wao kama vijana hawatoi misaada kwa ajili ya kuwadekeza wafungwa isipokuwa ni kufikisha baadhi ya huduma za msingi ambazo wafungwa wanazikosa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa gerezani  hapo zaidi ya asilimia 70  ya wafungwa wake na mahabusu ni vijana na wana kabiliwa na kesi za za mauaji.


Share:

Katibu Mkuu Wizara Ya Afya Azindua Baraza La Wafanyakazi Hospital Ya Benjamin

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Taasisi ya Hospitali ya Rufaa ya  Benjamin mkapa imefungua na kuzindua Baraza jipya la wafanyakazi  tangu hospitali ianzishwe  ambayo ni miongoni mwa hospitali kubwa hapa nchini. 

Akizungumza katika uzinduzi  huo,na wafanyakazi  wa Baraza la wafanyakazi Hospitali ya Rufaa Benjamin Mkapa iliyopo jijini Dodoma,katibu mkuu Wizara  ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dokta.Zainab Chaula ametoa rai kwa Wafanyakazi  wa baraza hilo kuwajibika katika Kazi zao na kufanya kazi kwa kujituma zaidi na kuonesha uzalendo kwa Wagonjwa. 

Dokta Chaula amesema kazi ya Utabibu na Udaktari ni ya  neema  na Rehema kutoka  kwa Mwenyezi Mungu na inayohitaji kuwa na uvumilivu , huruma na maneno ya Faraja kwa Wagonjwa hivyo kila  Mmoja anatakiwa kuguswa pindi anapotoa huduma kwa mgonjwa. 

“Tunajifunza kila siku,kwa hiyo nyie mlioteuliwa mtuwezeshe,haki haipo bila wajibu,na kila mmoja akijituma atatimiza wajibu  wake,mimi sikumbuki kutumwa na napata shida kum-push  mtu,na lazima tutengeneze Mechanism ya watu kufanyakazi bila kutumwa.Hakuna kazi  ya   neema na ibaada tunayo fanya kama hii,Mtu ana Stress zake,ana shida,hana hela lakini unamfariji,unamtibu,mwisho wa kazi saa 9 ukifanya kazi mpaka saa 11 au saa 1 jioni una dhambi gani.”Alisema. 

Aidha ,Dokta Chaula amewataka wafanyakazi kuwa Wepesi katika kutekeleza Majukumu yao na kutowakwaza wagonjwa na wananchi kwa ujumla hivyo ni jambo la busara kupeana Moyo katika kazi ngumu na yenye wito ya  utabibu na kumtegemea Mungu katika changamoto wanazokumbana nazo . 

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Afya  Dokta Chaula amesema upendo na huruma ni jambo la Muhimu kwa Maisha ya Binadamu kwani ni Moja ya Kujenga Marafiki wengi  na kusema kuwa hakuna mtu mdogo katika maisha kila mtu ana  mchango wake na kinachotofautisha ni Madaraka na Mamlaka tu ila  binadamu wote ni sawa.. 

“Kwa makusudi tu mtu anakuja  halafu anatoka analia  ofisini kwako unajisikiaje,lazima tupendane tuhurumiane tukitengeneza system ya namna hii katika maisha yetu tutakuwa na marafiki wengi kuliko maadui,tusameheane”Alisema. 

Kwa upande wake Katibu wa Baraza la wafanyakazi mkoa wa Dodoma,ambaye pia Mjumbe Taifa wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali kanisa  la Waadventista Wasabato ,[ATAPE] Bw.Mchenya John  amesema amesema wataendelea kuyafanyia kazi maelekezo yote  muhimu yaliyotolewa huku akizungumzia namna  walivyofanya mchakato wa   uanzishaji wa Chuo wa Chuo kikuu cha Dodoma pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa akitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa awamu ya nne Dokta.Jakaya Mrisho Kikwete kwa kufanikisha uanzishaji  wa Hospitali hiyo. 

Naye Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi  Taasisi ya Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa ambaye pia mkurugenzi mtendaji wa Hospitali hiyo Dokta Alphonce Chandika  amesema taasisi hiyo ina takriban  miaka mitatu tangu ianzishwe na walikuwa hawajaunda Baraza la Wafanyakazi kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na wafanyakazi lakini kwa sasa idadi imejitosheleza na wameona kuwa na umuhimu wa kuwa na Baraza ambapo tayari na  katiba na mkataba wa Baraza hilo ilishatengenezwa.


Share:

Waziri Kairuki Autaka Uongozi Wa KNAUF Kuendelea Kushirikiana Na Jamii Inayowazunguka.

NA.MWANDISHI WETU – OWM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuka ameutaka uongozi wa kiwanda kinachotengeneza bidhaa za cha za jasi (Gypsumboard) cha KNAUF kuendelea kushirikiana na jamii inayowazunguka katika kujiletee maendeleo.

Ametoa kauli hiyo mapema mwishoni mwa wiki hii alipotembelea kiwanda hicho kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani ili kukagua shughuli za uzalishaji zinazoendela pamoja na kusikiliza changamoto za wawekezaji hao na kuweza kujadili masuala ya kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Waziri Kairuki aliwataka kuona umuhimu wa kuchangia katika shughuli za kimaendeleo katika maeneo yanayozunguka kiwanda hicho hususan katika uboreshaji wa miundombinu na utoaji wa misaada itakayofikia jamii kwa sehemu kubwa na si mtu mmoja mmoja ili kuleta maendeleo katika eneo kubwa na kuondoa tofauti kubwa za kimaendeleo zisizoendana na maendeleo ya maeneo kiwanda hicho.

“Ni muhimu sana, na ni busara kuona ni kwa  namna gani mnashirikiana na wananchi wanaozunguka eneo hili katika kuleta maendeleo ili kuhakikisha mnakubalika , na kuleta maendeleo ya eneo husika na kuondoa tofauti za kimaendeleo kati ya ustawi wa kiwanda na jamii inayowazunguka”alieleza Waziri Kairuki

Waziri aliutaka uongozi huo kushiriki kimalilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo kuchangia kuboresha miundombinu inayozunguka mazingira ya kiwanda ili kuendelea kushiriki kwa vitendo na kuunga mkono jitihada za kuendelea eneo hilo.

Sambamba na hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Jumaa Abeld aliomba uongozi wa kiwanda kuona namna ya kuchangia katika maendeleo ya eneo lao kwa kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa sita katika shule ya msingi ya Kitangwi pamoja na madarasa manne  katika shule ya msingi ya Kisemvule zilizopo Wialya ya Mkuranga katika mkoa huo.

“Ombi letu ni kuona namna kiwanda hiki kinavyoweza kuchangia katika maendeleo kwa kutujengea vyumba sita vya madarasa katika shule zinazotuzunguka ili kusaidia uhaba uliopo na kusaidi watoto wetu kujifunza katika mazingira mazuri,”alisema Jumaa.

Aidha Meneja Masoko wa Kiwanda hicho Bi. Zainab Mwasara aliahidi ifikapo Julai 05 mwaka huu uongozi wa kiwanda utatoa taarifa za utekelezaji wa maombi hayo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 6.

“Tunaahidi kukutana kama uongozi wa kiwanda ili kujadili na kutekeleza masuala ya msingi ikiwemo hili la ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuendelea kuleta tija kwa uwepo wa kiwanda katika eneo hili,”alisema Mwasara.

Naye, Meneja Fedha wa kiwanda hicho Bi. Wema Mboga alishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya wawekezaji nchini na kumpongeza ziara ya Waziri katika kutatua na kuahidi kufanyia kazi masuala yaliyoelezwa kuwa ni changamoto kiwandani hapo ikiwemo uhaba wa upatikanaji wa nishati ya umeme ya uhakika, kutokamili kwa leseni za uchimbaji kwa wakati, tozo kubwa za malighafi na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji kiwandani hapo.

AWALI

Kiwanda cha KNAUF kilianzishwa mwezi Novemba mwaka 2015 kwa lengo la kuzalisha bidhaa za jasi (Gypsum board), gundi za jasi, pamoja na chuma za jasi (metal profile) kufanya kazi na usambazaj.Kiwanda kinafanya kazi katika nchi zaidi ya 80 ambapo katika nchi za kusini mwa Janga la Sahara, Tanzania ni nchi pekee ambayo ina uwekezaji huo kutokana na sababu za mazingira mazuri ya kibiashara na uwekezaji pamoja na sababu za kijiografia.Kampuni imeajiri wazawa 150 katika Nyanja zote kwa kulenga ifikapo 2020 kiwanda kiweze kuendeshwa na wazawa pasipo kutegemea wataalam kutoka nje.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 30 June















Share:

DPP Akabidhi Madini, Vito Na Fedha Benki Kuu (BOT ) Zilizotokana Na Kesi Za Uhujumu Uchumi.

Jumla ya madini yenye thamani ya Sh.3,125, 704,456.12 yamekabidhiwa kwa Serikali kupitia Hazina baada ya kutaifishwa kutokana na kubainika yalikuwa yanatoroshwa nchini.

Mbali na kukabidhiwa madini na vito, pia Serikali imekabidhiwa fedha za kigeni ambazo nazo zimetaifishwa.

Akizungumza wakati wa kukabidhi madini, vito na fedha hizo kwa Katibu Mkuu Hazina Dotto James, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) Biswalo Mganga amefananua kuwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS) katika vipindi tofauti kati ya mwaka 2017 na mwaka 2018 imeendesha kesi mbalimbali.

Amesema kesi hizo zilikuwa zinahusiasana na utoroshaji au kukutwa na madini bila kuwa na kibali na katika uendeshaji wa kesi hizo washtakwa walitiwa hatiani na kuamriwa kulipa faini au kutumikia kifungo gerezani pamoja na amri ya kutaifishwa madini na fedha walizokutwa nazo wakati wakisafirisha madini hayo.

"Madini yaliyotaifishwa ni kilo 25.546 za dhahabu ,zaidi ya kilo 76,020.20(tani 76) za Colored gemstone, Tanzanite pamoja na fedha za kigeni za mataifa mbalimbali 15 zenye thamani ya Sh.1,023,608, 515.12.

"Kwa kuwa madini hayo yametunzwa sehemu mbalimbali kiasi kwamba uwezekano wa kupotea au kumbukumbu zake kupotea na kwa kuwa mali zote zinazotaifishwa zinakuwa mali za Serikali na Katibu Mkuu Hazina ndiye msimamizi wa mali hizo" ameeleza.

"Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) anakabidhi kilo 25.5 za dhahabu zenye thamani ya Dola za Marekani 913,954.72 sawa na Sh.bilioni 2,102,095,941,"amesema Mganga.

Akifafanua madini na vito, amesema kuna tani 76 na Carrats 2849 zenye thamani ya Dola za Marekani 2,638,349.95 sawa na Sh.bilioni 6,068,204.885 na Carrats 2,849 zenye thamani ya Dola za Marekani 3,803.32 sawa na Sh. milioni 888,409,000.

Pia Tanzanite gramu 888 zenye thamani ya Dola 3,197 sawa na Sh.bilioni 7,353,348 na fedha za kigeni za mataifa 15 ambazo ni sawa na Sh.1,023,608,515.12.


Share:

Rais Mstaafu Mkapa Mgeni Rasmi Uzinduzi Maadhimisho Ya Miaka 20 Kuelekea Miaka 25 Tangu Kuanzishwa Kwa Chuo Kikuu SAUT

Na Eleuteri Mangi- SAUT
Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin Mkapa anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 20 kuelekea miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mt. Augustino Tanzania (SAUT).

Kwa mujibu wa Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho Balozi Prof. Costa Ricky Mahalu amesema kuwa chuo kimemualika Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa kwa kutambua na kuthamini mchango wake katika elimu ya juu ambapo uzinduzi wa maadhimisho hayo unatarajiwa kufanyika chuoni hapo Julai, 2 mwaka huu jijini Mwanza.

Akiongea na waandishi wa habari leo chuoni hapo makamu wa Mkuu wa Chuo hicho Balozi Prof. Mahalu amesema kuwa yapo mafanikio mengi ambayo chuo kinajivunia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1998. Miongoni mwa mafanikio hayo ni pamoja na kuongezeka udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 204 hadi wanafunzi 11400 kwa mwaka wa masomo 2018/2019 licha ya kwamba katika mwaka wa masomo 2012/2013 udahili uliwahi kufikia wanafunzi 13121 kabla ya kuongezeka kwa matawi 13 ya chuo hicho.

“Katika mtaala wa chuo, wanafunzi wanapata fursa ya kusoma masomo ya ujasiriamali na kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao na hivyo kuondokana na dhana ya kungoja kuajiriwa. Chuo kimeboresha kiwango cha elimu inayotolewa kuhakikisha wahitimu wanahimili soko la ushindani Afrika Mashariki na duniani kote pia kutokana na elimu ya dini na maadili kwa wanafunzi wote.” Amesema Balozi Prof. Mahalu 

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, Balozi Prof. Mahalu amesema kuwa chuo kimefanikiwa kuanzisha kituo cha kuzalisha na kuwawezesha wajasiriamali ambapo wanafunzi wanaohitimu masomo yao wanapata fursa ya kuandika mawazo ya biashara na baada ya mawazo yao kukubalika hupatiwa mafunzo maalumu juu ya mawazo hayo na kisha wanapatiwa mtaji kati ya shilingi milioni 25 hadi 30 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali.

Aidha, chuo hicho kimefanikiwa kuongeza vitivo vingine vinne (4) kutoka kitivo kimoja ambacho kilikuwa cha Sayansi ya Jamii na Mawasiliano kilichokuwa na shahada moja ya Mawasiliano ya Umma na kuongezeka kwa Kitivo cha Biashara na Utawala, Kitivo cha Ualimu, Kitivo cha Sheria na Kitivo cha Uhandisi.

Zaidi ya hayo Balozi Prof. Mahalu amesema chuo cha SAUT kina mchango mkubwa katika kutoa wanataaluma na wataalam katika fani mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wahadhiri, Wanahabari, Wanasheria, Wasimamizi katika taasisi za Fedha na Wakaguzi wa Fedha, Walimu, Wahandisi, Wafanyabiashara, Watunza amani katika majeshi ya Ulinzi na Usalama pamoja na Wanasiasa. Miongoni mwa wahitimu hao ni Mhe. Dotto Biteko Waziri wa Madini, Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi, Zawadi Machibya na Sammy Awami ambao ni watangazaji wa BBC, pamoja na wataalamu mbalimbali wanaofanya kazi ndani na nje ya nchi.

Chuo cha SAUT nje ya taaluma pia kinatoa huduma kwa jamii ambapo kimefanikiwa kuanzisha mradi mkuwa wa umeme wa kutumia nishati ya jua kwa kushirikiana na nchi ya Ujerumani ambapo mradi huo unatekelezwa katika vijiji mbalimbali katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Geita. 

Naye Mratibu wa Kamati ya Habari-Maandalizi ya kuelekea miaka 20/25 ya chuo cha SAUT Padre Titus Ngapemba amesema kuwa Rais Mtaafu Benjamin Mkapa amekuwa mdau muhimu katika sekta ya Elimu nchini katika ngazi mbalimbali za uongozi.

Padre Ngapemba amesema kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa amekuwa mdau muhimu katika sekta ya elimu nchini na kwa namna ya pekee katika chuo cha SAUT, akiwa madarakani alifanikisha ujenzi wa barabara ya kutoka jijini Mwanza kuingia chuoni hapo ambapo ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ulianza mwaka 2002 na kuzinduliwa mwaka 2004.”

“Mzee Mkapa anakumbukwa sana kwa kuwa mwasisi wa utoaji wa mikopo ya elimu ya juu kwa wanafunzi wa vyuo vyote vya umma na binafsi. Uamuzi huu wa Mzee Mkapa wa kuwapatia mikopo wanafunzi wa vyuo vikuu binafsi umesaidia Watanzania wengi kusoma elimu ya juu. Kwa hili utakumbukwa Mzee Mkapa” alisisitiza Padre Ngapemba.

Padre Ngapemba aliendelea kusema “Kwa mara ya kwanza mwaka 2005 Serikali ya Awamu ya Tatu ilibadilisha Sera ya mikopo ya elimu ya juu na kuanza kutoa mikopo kwa vyuo vikuu binafsi ikiwemo SAUT baada Makamu wa Mkuu wa chuo wa wakati huo Padre Deogratius Rweyengeza kutoa ombi hilo wakati wa mahafali ya kwanza mwaka 2001 tangu kipandishwe hadhi.”

Chuo Kikuu cha SAUT kinamilikiwa na kusimamiwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kimeanzishwa kwa mujibu wa sheria za nchi na kinafanya kazi chini ya Tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU) kwa mujibu wa masharti ya vyuo vikuu sheria namba 7 ya mwaka 2005 ambapo awali kilikuwa kinajulikana kama Chuo cha Maendeleo ya Jamii Nyegezi (NSTI) kilichoanzishwa tangu mwaka 1960 na wamisionari wa kanisa katoliki ambao kwa sasa wanajulikana kama Wamisionari wa Afrika wakiwa chini ya Askofu Mkuu Joseph Blomjous wa Jimbo Kuu la Mwanza.


Share:

Saturday 29 June 2019

TASAC: TUNAFANYA UKAGUZI WA MELI KUHAKIKI UBORA NA KUVIONDOSHA VISIVYOKUWA NAVYO MAJINI

Meneja wa Usajili,Ukaguzi na Udhibiti wa Usalama wa Vyombo vya maji Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Afred Waryana akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa warsha hiyo

Meneja wa Usajili,Ukaguzi na Udhibiti wa Usalama wa Vyombo vya maji Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Afred Waryana wa pili kushoto akimueleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella alipotembelea banda lao wakati wa maadhimisho ya wiki ya mabaharia kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi
Sehemu ya mabaharia wakiwa kwenye warsha hiyo
Sehemu ya mabaharia wakiwa kwenye warsha hiyo
Sehemu ya wanafunzi wa shule za Sekondari wakiwa kwenye warsha hiyo


UKAGUZI wa kushtukiza mara kwa mara kwenye vyombo vya majini umeelezwa kwamba unaweza kusaidia kuondosha vyombo vya majini visivyokuwa na ubora na hivyo kusaidia kupunguza majanga yanayoweza kujitokeza wakati wakiendelea kutoka huduma hizo ikiwemo meli

Hayo yalisemwa na Meneja wa Usajili,Ukaguzi na Udhibiti wa Usalama wa Vyombo vya maji Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Afred Waryana wakati wa warsha ya kuwajengea uwezo mabaharia na wadau wa masuala ya usafirishaji wa majini iliyoandaliwa na shirika la hilo kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi.

Alisema kwamba wanafanya hivyo ili kuhakikisha meli zinazofanya kazi na kutoa huduma majini wamiliki wake wanafuata taratibu na viwango vinavyostahili ikiwemo kuwa na ubora ili kuweza kuepusha majanga ambayo yanaweza kujitokeza wakiwa wanaendelea na shughuli hizo.

“Tumekuwa tukifanya kaguzi mbalimbali kwa lengo la kujirihidhisha na ubora wa meli husika na hili hufanyika wakati wa meli inajengwa kabla ya kuingizwa majini, ukaguzi wa kila mwaka kuhakikiwa kwamba ina ubora”Alisema

Aidha alisema pia wamekuwa wakifanya ukaguzi wa kila baada ya miaka miwili na nusu kwa meli kutolewa kwenye maji na kuangaliwa kama bado ina viwango hiyo yote ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha vyombo vya majini vinavyotoa huduma majini vinakuwa na ubora unaotakiwa.

Mkurugenzi hiyo alisema kwamba kaguzi hizo zipo kwa mujibu wa sheria lengo likiwa ni kuhakikisha meli hazitoi huduma bila kukaguliwa huku akieleza wanafanya za kushtukiza kuzuia watu kufanya shughuli za meli bila kukaguliwa.

Alisema kwa sasa wanafanya ukaguzi kwa vyombo 6000 vya majini nchi nzima kwa kila mwaka huku vyombo vikubwa meli kubwa na ndogo vilivyo zaidi ya tano 50 kwenda juu wanakagua zaidi ya kaguzi 230.

Awali akizungumza wakati akiwasilisha mada kwenye warsha hiyo Captain Hilaly Salum kutoka Chuo cha Mabaharia (DMI) Dar es Salaam akiwasilisha mada ya tatu katika Warsha hiyo alikieleza chuo hicho pekee Afrika Mashariki kilichoanzishwa miaka 42 iliyopita kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya kiteknolojia na hali ya kiuchumi.

Alitumia nafasi hiyo kuiomba serikali na taasisi kukisaidia chuo hicho kupata vyombo kwa ajiri ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi ambavyo vitawawezesha kufanya majaribio wasifu pamoja na kutoa ufadhili kwa wanafunzi wa ngazi ya chini ambao hawana uwezo kugharamia masomo hayo.

“Endapo serikali itagharamia elimu hiyo kwa wanafunzi wa chini wasiyo na uwezo kifedha wa kulipa ada licha ya kuwafanya kupata ajira lakini pia watailipa serikali kodi na hivyo kuchangia uchumi wa taifa”alieleza Salimu.

Awali wakichangia mjadala baadhi ya washiriki wa warsha hiyo waliiomba serikali kufanya uwekezaji katikamazao ya baharini kama inavyofanya kwenye sekta mbalimbali nchini na kwamba kufanya hivyo kutaongeza pato la taifa kwa madai kuwa bahari ndiyo eneo pekee lenye uwezo mkubwa wa kufanya uwekezaji Duniani.

Share:

MKUU WA MKOA AMTAKA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MBULU NA TIMU YAKE WAJITAFAKARI

Share:

MNYETI: SINA NIA YA KUMDONDOSHA YEYOTE

Share:

Waziri Mkuu: Ujenzi Wa Nyumba Bora Waongezeka

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kaya zinazoishi kwenye makazi bora zimeongezeka kwa asilimia 16 katika kipindi cha miaka sita ikilinganishwa na hali ilivyokuwa mwaka 2011/2012.

“Kaya zinazoishi kwenye nyumba zenye paa la kisasa zilizoezekwa kwa bati zimeongezeka kutoka asilimia 68 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 84 mwaka 2017/2018 wakati kuta za kudumu zimeongezeka kutoka asilimia 46 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 79 mwaka 2017/2018,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo jioni (Jumamosi, Juni 29, 2019) wakati akizungumza na viongozi na wananchi mara baada ya kuzindua Jengo la Ofisi ya Taifa ya Takwimu lililoko Makulu, Manispaa ya Jiji la Dodoma.

Waziri Mkuu ambaye alimwakilisha Dkt. John Pombe Magufuli, pia alizindua ripoti ya matokeo ya viashiria muhimu vya utafiti wa mapato na matumizi ya kaya binafsi Tanzania Bara ya mwaka 2017/18.

Waziri Mkuu alisema takwimu hizo ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na zinaonyesha jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano za kujenga Tanzania ya Viwanda zinaendelea kuwanufaisha wananchi kwa zinagusa moja kwa moja katika sekta ya ujenzi kama vile viwanda vya saruji, mabati, nondo, na vinginevyo.

Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali ni kuona kila Mtanzania anaishi kwenye makazi bora kwani makazi bora huimarisha afya za wakazi na afya bora ni mtaji wa msingi kwa kila mwanadamu kwa kufanya kazi na hivyo kukuza uchumi.

“Tuendelee kuunga mkono jitihada za Serikali kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje waje wawekeze kwenye viwanda vya saruji, mabati, na marumaru ili kuongeza uzalishaji na kuleta ushindani wa bei ambao utawanufaisha watu wengi na kuwapatia fursa za kujenga makazi bora ya kuishi,” alisema.

Waziri Mkuu alisema mbali na makazi bora, utafiti huo umebainisha uwepo wa ongezeko la kaya zilizounganishwa kwenye umeme wa Gridi ya Taifa kutoka asilimia 18 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 29.1 mwaka 2017/2018.

 “Jitihada za Serikali chini ya Mpango wa Umeme Vijijini (REA), zinaendelea na utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Awamu ya Tatu wa kusambaza nishati vijijini unaojumuisha vijiji 7,873 katika wilaya na mikoa yote ya Tanzania Bara ambao unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano ulioanza mwaka wa fedha 2016/17 na unategemewa kukamilika mwaka 2020/2021,” alisema.

Akizungumzia hali ya umaskini barani Afrika, Waziri Mkuu alisema kiwango cha umaskini wa kipato cha Watanzania hakitofautiani sana na nchi nyingine ndani ya bara hilo.

 “Tukiangalia hali ya umaskini katika nchi nyingine za Bara la Afrika kwa miaka ya hivi karibuni, nikianza na Kenya kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi ni asilimia 36.8 (mwaka 2015), Afrika ya Kusini asilimia 55.5 (mwaka 2015), Rwanda asilimia 38.2 (mwaka 2016), Zambia asilimia 54.4 (mwaka 2015), Ethiopia asilimia 23.5 (mwaka 2015) na Zimbabwe asilimia 72.3,” alisema.

Alisema kupunguza umaskini kwa nchi yoyote ile kunapaswa kuhusishwa na uwekezaji kwenye sekta nyingine za kiuchumi ambazo hugusa na kuwanufaisha wananchi walio wengi. “Nitumie fursa hii kusisitiza kuwa umaskini ni changamoto kwa dunia nzima na hasa kwa nchi zinazoendelea. Nchi zilizo na hali mbaya zaidi ni zile zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara kama takwimu rasmi zinavyoonesha.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema ni lazima Serikali iimarishe upatikanaji wa takwimu kwa kuajiri maafisa takwimu wanaowajibika moja kwa moja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu badala ya kumtegemea mtu anayewajibika kwa Mkurugenzi wa Halmashauri.

“Leo hii hatuna Afisa Takwimu katika kila Halmashauri, na matokeo yake hatuna mfumo mzuri wa kupata taarifa kuanzia ngazi ya chini. Tuweke utaratibu ili hawa watu wawepo na kila Afisa takwimu awajibike kupeleka taarifa yake kwa Mtakwimu Mkuu kila wakati.”

“Nilipokuwa Naibu Waziri TAMISEMI ninayeshughulikia elimu, nikiagiza takwimu fulani, kuzipata ilikuwa inachukua zaidi ya wiki mbili, na hiyo ni kwa Halmshauri moja tu. Na wakati mwingine, taarifa inakujia wakati umeshasahau kuwa ulitoa agizo uletewe.”

Mapema, akitoa taarifa juu ya utafiti huo, Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi duniani ambazo kiwango cha umaskini kimeendelea kushuka na kufikia tarakimu moja.

Alisema utafiti huo uliofanywa na ofisi yake kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, baadhi ya balozi na mashirika ya Umoja wa Mataifa ulilenga kupata makadirio ya viwango vya umaskini ili kufuatilia, kupima na kutathmini mipango mbalimbali ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Alisema katika utafiti huo, walitumia teknolojia ya kisasa iitwayo survey solution ambayo imesaidia kupunguza gharama za utafiti za kupeleka madodoso na magari. “Tulitumia vishkwambi (tablets) na kupunguza mzigo wa kubeba na makaratasi au kukaa kujumlisha taarifa,” alisema,

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Serikali Yadhamiria Kuimarisha Huduma Kwa Watu Wenye Ulemavu

Na; Mwandishi Wetu
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa kushirikiana na wadau imedhamiria kuboresha huduma na upatikanaji wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa hafla ya kupokea vifaa saidizi kwa ajili ya watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC Plc), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa kundi la Watu wenye Ulemavu lilikosa baadhi ya fursa hapo awali kutokana na changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo.

“Tunafahamu watu wenye ulemavu wanauhitaji wa huduma bora na vifaa saidizi vitakavyo wawezesha kumudu mazingira ili nao waweze kujumuika katika nyanja zote,” alisema Mhagama

Alifafanua kuwa takwimu na Sensa ya Taifa ya Watu wenye na Makazi ya mwaka 2012, imekadiria idadi ya watu Tanzania ni zaidi ya milioni 44 ambapo milioni 2.5 ni Watu wenye Ulemavu.

Waziri Mhagama alisema, Serikali imeazima kuboresha huduma kwa Watu wenye ulemavu ikimemo kutoa elimu bure na kuimarisha elimu jumuishi, kujenga vituo vya afya na hospitali pamoja na utoaji wa matibabu bure kwa watu wenye ulemavu wasio na uwezo.

Mbali na hayo, alihimiza wadau pamoja na makampuni kuona umuhimu wa kuhudumia kundi la watu wenye ulemavu wakiwa wanatoa huduma mbalimbali za kijamii.

Aidha, alipongeza Kampuni ya Singara Tanzania (TCC) kwa msaada huo na kuwashauri waendelee kukumbuka kundi hilo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa TCC, Bw. Godson Killiza alisema kuwa watu wenye ulemavu wana uwezo mkubwa na nijukumu kama wadau kuwasaidia na kuwaunga mkono kwenye masuala mbalimbali.

Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bi. Ummy Nderiananga alieleza kuwa juhudi za Serikali katika kushirikiana na wadau itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa changamoto za Watu wenye Ulemavu katika kufanikisha masuala yao.


Share:

PICHA: Zijue Alama za barabarani pamoja na matumizi yake


Credit: Jamii Forums


Share:

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia: Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR) – Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia:  Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.


Share:

Fahamu Chanzo Halisi cha Kupungukiwa Nguvu za Kiume

Unafahamu kwa kina tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na  maumbile ya kiume kusinyaa?

Wanaume wengi kwa sasa wanasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile  kuwa mafupi na wengi wao huamua kutafuta tiba ili waweze kujilejeshea nguvu zao za asili bila kujua ni nini chazo cha hilo tatizo 

Tambua kuwa hakuna dawa ya kuongeza maumbile ya kiume  kama  ulikuwa mdogo  tangu unazaliwa, labda kama tatizo limeazia ukubwani kwa kujichua ( kupiga punyeto)  au kutokana na magonjwa 

Pia hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume kama tatizo umezaliwa nalo bali zipo tiba za kutibu na ukapona matatizo hayo kama yameanzia  ukubwani kutokana na sababu zifatazo ;
1,Unene kupita kiasi 
2.Kuvaa nguo za kubana 
3.Magonjwa ya moyo,kisukar,presha,vidonda vya tumbo,ngiri,tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kupiga punyeto,Msongo wa mawazo.

Haya ndo mambo makuu yanayosababisha tatizo hilo. kwa ushauri zaidi , piga simu 0683645920


Share:

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger