Monday 6 February 2017

Kulala chali kwa mjazito ni hatari kwa mtoto


Wanawake wajawazito wanaopenda kulala chali  wapo kwenye hatari  ya kuzaa mtoto mfu(stillbirth),kulingana na wanasayansi.

Katika utafiti  uliofanyika nchini Ghana, wanawake wajawazito ambao walipenda kulala chali wakati wa ujauzito  walikuwa  kwenye hatari mara tano zaidi ya kuzaa watoto wenye uzito mdogo na  kwa wanawake wengine walizaa watoto wafu.

Utafiti huu ulifanyika nchini Ghana kutokana na kuwa kati ya watoto 1000 wanaozaliwa 20 hadi 50 kati yao huwa ni watoto wafu.Hata hivyo, utafiti mpya uliofanyika nchini New Zealand pia umehusisha kulala chali kwa mwanamke mjamzito na idadi kubwa ya  watoto wafu wanaozaliwa  katika nchi zenye raia wenye kipato kikubwa.

Mkuu wa utafiti huu,Louise O'Brien  kutoka chuo kikuu cha Michigan, nchini Marekani amesema kama kutokulala chali wakati wa ujauzito hupunguza uwezekano wa kuzaa mtoto mfu basi ni vizuri kuhamasisha kina mama wajawazito kutolala chali kwani hii ni njia rahisi na isiyokuwa na gharama yoyote ile.

Tabia hii ya kulala chali wakati wa ujauzito inaweza kuepukika kwa kuwashauri  kina mama wajawazito madhara yanayopatikana kwa kulala chali.

Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha ya kwamba zaidi ya robo ya idadi ya watoto wanaozaliwa wafu inaweza kuepukika kwa kubadilisha staili ya kulala tu kwa wanawake wajawazito.

Siku zote madaktari wanashauri kina mama wajawazito kulala ubavu mmoja hasa upande wa kushoto ili kuepuka kuzaa mtoto mfu au mtoto mwenye uzito mdogo kwa sababu mwanamke mjazito anapolalia ubavu wake wa kushoto huongeza mzunguko wa damu kwa kiumbe kilichomo ndani yake.

Utafiti huu uliofanyika nchini Ghana unaunga mkono utafiti uliofanyika hivi karibuni nchini Australia unaojulikana kama Sydney Stillbirth Study ambao ulisema ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito wako kwenye hatari ya mara sita zaidi ya kuzaa watoto wafu.Utafiti huu wa Australia ulifanyika kwa miaka mitano na ulihusisha wanawake wajawazito 295 kutoka katika hospitali nane nchini Australia.

Naye mtafiti mkuu katika utafiti huu Dr. Adrienne Gordon, kutoka Sydney's Royal Prince Alfred Hospital amesema “Tafiti za awali zilionyesha ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito, hupunguza mzunguko wa damu unaotakiwa kwenda kwa mtoto.Lakini  pia ni vizuri kwa wanawake ambao ni wajawazito  kutotaharuki kama wakati mwingine watalala chali.’’Kutokana na idadi ndogo ya wanawake wajawazito waliohusishwa kwenye utafiti huu sisi wana Tanzmed tunachelea kusema ya kwamba ni vigumu kusema utafiti huu umetoa mapendekezo sahihi ya  namna ya kulala kwa wanawake wajawazito.

Pia kutokana na kutoangalia muda ambao wanawake hao walilala wakiwa chali (mfano kama walilala masaa 4,6 au 8 kwa siku na kwa siku ngapi) na tofauti ya hatari kati ya wanawake wajawazito waliolala muda mfupi na mrefu, hivyo tunawaambia wanawake wajawazito kutohofu kama watalala chali lakini ni bora kuchukua tahadhari mapema.Tafiti hii inatoa changamoto kwa watafiti wetu wa afya kuangalia jinsi ya kufanya tafiti kama hizi katika mazingira ya kwetu.
Share:

Ukata kuchelewesha utoaji wa haki

Bukoba.  Ukata katika Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba umesababisha majaji kutoendeleza vikao vya kusikiliza mashauri 24 ya kesi za mauaji, hali itakayosababisha haki kutokutolewa kwa wakati.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salvatory Bongole akizungumza wakati wa kilele cha siku ya sheria nchini, alisema hadi Desemba mwaka jana hakuna kesi iliyokuwa imezidi miezi sita katika mahakama zote za mwanzo.

Alisema wamejitahidi kumaliza mashauri mengi kwa wakati pamoja na kupunguza malalamiko,  huku kesi 81 zikizidi mwaka mmoja katika mahakama za wilaya kwa kuwa korti hizo hazikuwa na uwezo nazo.

Oktoba 27 mwaka jana katika kesi ya jinai namba 67/2015, Mahakama Kuu chini ya Jaji Firmini Matogolo ilitoa uamuzi baada ya  miaka minane kwa  kuwatia hatiani wanandoa Lameck Bazil na Pancras Minago kwa mauaji ya mlemavu wa ngozi, Magdalena  Andrea yaliyotokea mwaka 2008 wilayani Biharamulo mkoani Kagera.
Share:

Uporaji kwenye maduka, bodaboda wazua hofu

Mbeya. Wamiliki wa maduka, bodaboda na glosari jijini hapa wameingiwa hofu baada ya kuibuka kundi la watu wanaodaiwa kuwa majambazi wanaopora fedha na pikipiki tangu mwishoni mwa Januari.

Mitaa iliyoonja adha ya wavamizi hao ni ya Mafiati, Mwanjelwa, Mabatini, Soweto na Mabanzini ambako vikundi hicho vilivunja maduka matano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari alisema  wanawashikilia watu watatu wakituhumiwa kuhusika na matukio hayo.

Kidavashari alisema upelelezi wa awali unaonyesha kundi hilo la watu hutoka Tunduma mkoani Songwe na hupokewa na wenyeji ambao huwaongoza katika uporaji.

 Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Bodaboda Kanda ya Soweto, Joseph Patrick alisema hivi karibuni kuna watu waliofika eneo hilo saa 3:00 usiku waliowavamia madereva na kuwapora fedha na baadaye walivamia Mtaa wa Block Q walikopora pikipiki mbili.
Share:

Serikali yashauriwa kupiga marufuku viroba


Mbulu. Serikali imetakiwa kupiga marufuku pombe kali zinazofungwa kwenye pakiti maarufu viroba, ili kuwanusuru vijana na ulevi unaosababisha Taifa kupoteza nguvu kazi.

Mkurugenzi wa kituo cha wagonjwa wasiojiweza cha Bashay wilayani Mbulu, Mkoa wa Manyara, Padri James Amnaay alitoa rai hiyo juzi alipopokea msaada wa vyakula, nguo na sabuni kutoka  Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wilayani hapa.

Padri Amnaay alisema iwapo Serikali itapiga marufuku pombe hizo, itasaidia vijana kutojiingiza kwenye ulevi ambao umekithiri na kusababisha baadhi yao kuwa vichaa.

Alisema kutokana na urahisi wa kubeba na bei nafuu, pombe hizo zimewaathiri vijana wengi wanaokunywa na kulewa hatimaye kujiingiza kwenye dawa za kulevya.
Share:

Vyakula Muhimu Kwa Waja Wazito

Wiki iliyopita tuliona orodha ya vyakula hatari kwa wajawazito. Orodha hiyo imekatazwa kuliwa na wajawazito kwa sababu ina madhara kwa afya ya mtoto. Darasa hili ni muhimu kama mama anahitaji kuzaa mtoto mwenye afya na akili timamu.

Baada ya kujua orodha ya vyakula visivyofaa kwa wajawazito, wiki hii tujifunze vyakula vinavyofaa kuliwa zaidi na wajawazito.

Kumbuka kwamba vyakula vyote vinaweza kuwa ni muhimu mwilini lakini huzidiana kulingana na mahitaji na hali ya mtu kwa wakati maalumu.

Mahitaji ya madini na vitamini mwilini wakati wa ujauzito huwa ni makubwa, hususani madini ya kashiamu, chuma na Vitamin B9 (folic acid).

MADINI YA KALISI (Calcium)
Wakati wa ujauzito, madini mengi ya kalisi husafirishwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa ajili ya kuimarisha mifupa na meno. Katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo, mama huhifadhi madini hayo mwilini mwake. Kiumbe kinapokamilisha umbo lake katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho, hifadhi hiyo huanza kutumiwa na kiumbe hicho, hivyo mahitaji yake kuongezeka.

Katika kipindi hiki, mjamzito anatakiwa kula kwa wingi vyakula vinavyoongeza madini ya kalisi kama vile maziwa na vyakula vitokanavyo na maziwa. Kukiwa na upungufu wa madini hayo, meno ya mama na mifupa huathirika pia.

MADINI YA CHUMA (Iron)
Mahitaji ya madini ya chuma nayo huwa makubwa kwa wajawazito. Madini hayo ni muhimu kwa utengenezaji wa damu ambayo huhitajika kwa wingi na mama pamoja na mtoto.

Madini joto hupatikana kwa kula kwa wingi vyakula kama vile nyama, samaki, mayai, vyakula vilivyopikwa kwa nafaka zisizokobolewa (ugali wa dona, mkate mweusi, n.k) na mboga za majani kama vile spinachi na brokoli. Ili kupata madini hayo ya kutosha kutokana na vyakula hivyo, inashauriwa mjamzito kutumia pia vidonge vya Vitamin C (Vitamin C food supplements).

VITAMIN B9 (Folic Acid)
Vitamini hii ni muhimu sana kwa mjamzito, ni kosa kubwa sana la kiafya kwa mjamzito kuwa na upungufu wa vitamin hii. Vitamin B9 ndiyo inayohusika na ukuzaji na uimarishaji wa mfumo wa fahamu wa kiumbe tumboni.

Aidha, Vitamin hii ndiyo inayotoa kinga ili viungo vya mtoto visiathirike na kuepusha uzaaji wa watoto walemavu au wenye kasoro za viungo kama ‘midomo ya sungura’ na kadhalika.

Vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Vitamin B9 ni pamoja na mboga za majani, juisi ya machungwa, mapeasi, vyakula vilivyopikwa kwa ngano na mchele (hasa brown rice) na mayai.

Hata hivyo, kutokana na hali ya vyakula vyetu, mjamzito hawezi kupata kiwango kinachotakiwa cha vitamin hiyo kwa kula vyakula peke yake.

Ili kupata kiwango cha vitamin hiyo kinachotakiwa, mjamzito atatakiwa kutumia pamoja na vidonge vya lishe vya Vitamin B9 ili kuepuka upungufu huo. Inashauriwa kutumia vidonge hivyo miezi michache kabla ya kushika mimba na katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho ya ujauzito, kipindi ambacho vitamin hiyo huhitajika kwa wingi.

Kwa ujumla, lishe bora ni muhimu kwa mjamzito katika kipindi chote cha ujauzito wake. Matatizo mengi ya kuzaa watoto wenye ulemavu wa aina mbalimbali, hutokana na upungufu wa madini na vitamin muhimu mwilini katika kipindi cha ujauzito.
Share:

Cameroon yatawazwa mabingwa wa Afcon 2017

Timu ya Taifa ya Soka ya Cameroon imetawazwa kuwa mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka 2017 baada ya kuilaza timu ya Taifa ya Misri kwa mabao 2-1,  yaliyofungwa na Nicolas N'Koulou na Vincent Aboubakar.
Share:

Mbowe awakutanisha mameya sakata la UDA


MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amekutana kwa dharura na mameya, manaibu meya na viongozi waandamizi kutoka vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wa Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili suala la Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA).
Hivi karibuni, Rais John Magufuli wakati akizindua Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam (DART) alitoa siku tano kwa uongozi wa Jiji kuhakikisha Sh bilioni 5.8 zilizolipwa na Kampuni ya Simon Group zinapangiwa matumizi baada ya kuuzwa hisa asilimia 51 kati ya 100 kwa kampuni hiyo.
Jiji la Dar es Salaam kwa sasa linaongozwa na Ukawa chini ya Meya kutoka Chadema, Isaya Mwita. Katika kikao cha baraza Halmashauri ya Jiji hilo chini ya Meya Mwita kilichofanyika wiki iliyopita, kilishindwa kufikia mwafaka wa kuzipangia matumizi fedha hizo kutokana na madai ya wajumbe wa baraza hilo kuwa kitendo hicho ni kubariki ufisadi wa kuuza hisa kwa Simon Group.
Kikao hicho cha Baraza kilifanyika ili kuitikia agizo hilo la Rais Magufuli alilolitoa wakati wa uzinduzi wa mradi wa Dart.
Hata hivyo, pamoja na siku tano alizotoa kuisha bado halijapatiwa ufumbuzi. Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alipozungumzia suala hilo nje ya ukumbi wa Bunge, alikiri kuwaita viongozi hao wa jiji la Dar es Salaam ili kuzungumzia suala hilo la UDA.
“Nimewaita ili tuzungumze sintofahamu ya suala hili ili tupate msimamo wa pamoja.Tunahitaji kupata suluhisho la suala hili ili wakazi wa Dar es Salaam wanufaike na Uda,” alisisitiza.
Katika jiji la Dar es Salaam lenye halmashauri sita, Ukawa ilishinda halmashauri tatu ikiwemo halmashauri ya jiji hilo inayoongozwa na Mwita, Ubungo ikiongozwa na Boniface Jacob na Ilala chini ya Charles Kuyeko.
Baadhi ya viongozi hao wa Ukawa wa Dar es Salaam walionekana wakirandaranda katika viwanja vya Bunge jana na baadhi yao walikiri kuitwa na mwenyekiti huyo wa Chadema huku wakidai kuwa hawafahamu wameitiwa nini.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene akizungumzia kushindwa kugawanywa kwa fedha hizo alitaka watendaji wa jiji hilo wapewe muda ili waweze kuja na suluhisho la suala hilo.
Alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia maagizo ya Rais Magufuli kuhusu matumizi ya fedha hizo, lakini endapo atapewa maelekezo kuhusu fedha atayatekeleza.
Share:

Watoto wote wanaweza kupatiwa vyeti vya kuzaliwa -Mwakyembe

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema inawezekana kuwasajili watoto wote nchini na kuwapatia vyeti vya kuzaliwa.
Mwakyembe aliyasema hayo katika hafla ya kukabidhi tuzo zilizotolewa na Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa viongozi wa mikoa ya Iringa na Njombe.
Ilikuwa ni hatua ya kuwapongeza na kutambua mchango wao katika kufanikisha utekelezaji wa mpango wa kuwasajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa watoto wa umri chini ya miaka mitano katika mikoa yao.
“Iringa na Njombe wameweza kusajili watoto kwa asilimia 100 kwa kipindi cha miezi minne, hivyo kama mikoa mingine itaiga mfano kwa mikoa hii basi serikali itaweza kukamilisha, ndani ya muda mfupi, kuwasajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa watoto wote walio na umri chini ya miaka mitano,” alisema.
Alieleza kwamba mikoa ya Mwanza, Mbeya na Songwe imekuwa ikitekeleza mpango huu kwa zaidi miaka mitatu lakini mpaka sasa hawajafikia kusajili watoto kwa asilimia 80, hivyo akakasisitiza viongozi wahakikishe suala hilo linafanikiwa.
Kwa mujibu wa maelezo ya awali yaliyotolewa na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Emmy Hudson, hali ya usajili katika mikoa ya Iringa na Njombe ilikuwa sio ya kuridhisha kwani ni watoto asilimia 11.7 katika mkoa wa Iringa na asilimia 8.5 katika mkoa wa Njombe ndio walikuwa wamesajiliwa.
“Hivi karibuni tutaanza utekelezaji wa mpango huu katika mikoa ya Shinyanga na Geita na tutatumia uzoefu tulioupata katika mikoa ya Iringa na Njombe ili kuhakikisha na huko tunapata mafanikio makubwa kwa kipindi kifupi” alissema Hudson.
Katika hafla hiyo Mwakyembe alikabidhi tuzo na hati za pongezi kwa halmashauri 11, Ofisi zote za wakuu wa wilaya za mikoa ya Njombe na Iringa na kwa ofisi za za wakuu wa mikoa hiyo.
Share:

VIDEO | MAdada Sita - Matobo | Watch/Download


Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI TAREHE 6.2.2017

Share:

Serikali yatangaza ‘Diploma’ ndiyo kigezo cha chini cha elimu kwa waandishi wa habari


Share:

Sunday 5 February 2017

Tunda Man adai amepokea simu nyingi baada ya jina Tunda kutajwa kwenye list mpya ya Mtandao wa Madawa ya Kulevya

Msanii wa muziki Tunda Man amedai jana alipokea simu nyingi baada ya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutangaza list mpya ya majina ya watu wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya Madawa ya kulevya ilikiwemo jina la Tunda ambaye ni video queen.

Baadhi ya waandishi kwenye mitandao ya kijamii waliandika jina Tunda bila kutolea ufafanuzi ni Tunda gani, hali ambayo iliwafanya wasiohusika kupigiwa simu nyingi akiwemo msanii wa muziki Tunda Man.

Tunda Man amedai wengi ambao ulikuwa wanampigia simu walitaka kujua kama kweli ni yeye ndiye aliyetajwa au ni Tunda mwingine.

“Jaman Tunda alietajwa na Mh Paul Makonda ni huyu sio mie maaana simu zimekuwa nyingi @soudybrown na wewe hujui au umeamua tu kunipigia,” aliandika Tunda Man Instagram huku akiwa amempost dada huyo.

Pia kwenye list hiyo mpya alitajwa mwanadada Vanessa Mdee ambaye pia anatakiwa kuripoti makao makuu polisi Jumatatu.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya February 5

Share:

CCM YABADILI GIA ANGANI

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema chama hicho siku ya kesho tarehe 5 mwezi wa pili kitakuwa kikitimiza miaka 40
Share:

Mawaziri: Mageuzi ya Rais Magufuli Yanazaa Matunda

Share:

Friday 3 February 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY TAREHE 3.2.2017

Share:

Wednesday 1 February 2017

NECTA:CSEE RESLUTS/ MATOKEO KIDATO CHA NNE/FORM 4 2016




 



NECTA yaachia matokeo ya wanafunzi ambaowamemaliza kidato cha nne 2016 ,Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG tunaendelea kutoa huduma ya kuangalizia majina endapo unahitaji kujua matokeo yako;

ILI KUANGALIZIWA FANYA YAFUATAYO;

TAFADHALI FANYA YAFUTAYO KAMA UNATAKA KUANGALIZIWA;
1.TUMA  EXAM NAMBA ya form 4  KWENDA NAMBA 0652740927 mfano:s0710/0119/2016

2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 AMBAYO UTAITUMA 

KWA MPESA KWENDA NAMBA 0742289379

AU TIGO PESA KWENDA NAMBA 0652740927

UTAJIBIWA BAADA YA DK 1 TU.

TUMA PESA KWANZA NDIO UJIBIWE.

Matokeo yote yapo hapa > BONYEZA HAPA
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger