Tuesday 24 January 2017

WALIMU WATATU WAKAMATWA KWA KUPIGA DILI LA KUPOKEA MISHAHARA PRIVATE NA SERKALINI

Walimu watatu mkoani Mwanza wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la  kukimbia vituo vyao vya kazi na kufanya kazi shule binafsi huku wakiendelea kupokea mishahara ya serikali

Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Mwanza imewataja walimu hao waliokamatwa jana asubuhi katika mtaa wa Buhongwa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza,kuwa ni pamoja na Richard Mgendi (30), Rwiza Ntare (27) na Gilbert Makwaya (33).

Walimu hao kila mmoja ana story yake kama ifuatavyo:-

Mwalimu Richard Mgendi alikuwa akifundisha shule ya sekondari ya Misasi wilayani Misungwi, mwaka 2012 alimuaga mkurugenzi wa wilaya hiyo kuwa anakwenda kusoma Masters ya lugha (Linguistic) katika chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino, kwa kipindi chote hicho inadaiwa mwalimu huyo alikwenda kusoma na alipomaliza hakurudi katika shule yake ya awali bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara kutoka serikalini.

Mwalimu Rwiza Ntare alikuwa akifundisha shule ya sekondari iitwayo Kigongo sekondari iliyopo wilaya ya Chato mkoani Geita ambapo mwaka 2015, alimuaga mkurugenzi wake kuwa anakwenda hospitali ya rufaa ya Bugando kupatiwa matibabu ya macho na vidonda vya tumbo lakini hakurudi tena bali inadaiwa alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara na serikali.

Mwalimu Gilbert Makwaya alikuwa akifundisha Runima sekondari iliyopo maeneo ya Buhongwa na alimuaga mkurugenzi wa wilaya ya Nyamagana tarehe 27/09/2015 kuwa anakwenda kusoma Masters ya Hesabu katika chuo kikuu cha Mwenge kilichpo mjini Moshi lakini hakwenda bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kupokea mshahara kutoka serikalini.

Walimu wote watatu wapo katika mahojiano na jeshi la polisi na pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Jeshi la polisi linaendelea kuwatafuta baadhi ya walimu ambao wametoroka lakini inadaiwa wapo katika shule hiyo binafsi ya Musabe huku wakiendelea kulipwa mshahara na serikali pamoja na mkurugenzi wa shule hiyo.
Share:

MAJAMBAZI WAWILI 2 WAUAWA JIJINI MWANZA

Watu wawili waliokuwa wakituhumiwa kwa ujambazi wameuawa wakati wakitaka kujaribu kuwatoroka askari polisi wilayani Ilemela mkoani Mwanza

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amesema kwamba tukio hilo lilitokea  tarehe 20.01.2016 majira ya saa 2:30  usiku, katika mtaa wa kiloleli “A” kata ya Nyasaka mkoa wa Mwanza na kuwataja majambazi waliouawa kuwa ni Eric Magese miaka 22, na aliyejulikana kwa jina moja la Peter miaka kati 25 hadi 27 wote wakazi wa Mecco jijini Mwanza.

Amesema majambazi hao waliuawa wakati wakijaribu kutoroka askari polisi pindi wakiwapeleka mahali ambapo wenzao wamejificha ili waweze kufanya uvamizi.

Amesema kuwa katika tukio hilo pia ilipatikana silaha moja aina ya short gun yenye namba TZ CAR 103283 ikiwa na risasi tatu ambayo inadaiwa walipora kwenye kampuni ya ulinzi iitwayo Malika Security Service Limited

Msangi amesema majambazi hao walikuwa wakitafutwa na polisi baada ya kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali jijini Mwanza ilikiwemo tukio la Kitangiri mnamo tarehe 19.12.2016 na tukio la tarehe 02.01.2016 katika mtaa wa Nyasaka.

Jinsi walivyouawa
Msangi amesema baada ya upelelezi uliofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao, walikubali kuwapeleka askari katika eneo ambalo walikuwa wamepanga pamoja na wenzao wawili kwa ajili ya kufanya matukio zaidi ya ujambazi.

Amesema walipofika katika eneo hilo, watuhumiwa hao walipiga kelele kama ishara ya kuwatorosha wenzao na kuanza kuwakimbia askari.

Askari walifyatua risasi kadhaa hewani wakiwaamuru wasimame lakini waligoma ndipo waliwafyatulia risasi za mguuni kwa bahati mbaya ziliwalenga maeneo ya juu ambapo walifariki dunia wakati wakipelekwa hospitali.
Share:

WARAKA WA ZITTO KABWE KUHUSU UCHAGUZI WA MARUDIO

Share:

TUNDU LISSU AFUNGUKA KUHUSU UPINZANI KUBURUZWA NA CCM UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

KAULI YA MTATAIRO BAADA YA UPINZANI KUANGUKIA PUA UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

KAULI YA RAIS MAGUFULI BAADA YA CCM KUSHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARY TAREHE 24.1.2017

Share:

Monday 23 January 2017

Bulembo amtaka Lowassa Aachane na Siasa

Share:

Hatimaye Jecha Afunguka Kuhusu Kufuta Uchaguzi Zanzibar...

Share:

Bibi Akutwa amekufa Huku akiwa na vibuyu 5 na kuku mweupe

Bibi  mwenye umri wa miaka 60 amekutwa amekufa mkoani Tabora huku amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki, akiwa na vibuyu vitano na kuku mweupe, katika mazingira yanayoashiria kushiriki vitendo vya kishirikina.

Aidha, mwili wa mtu mwingine umekutwa pembeni ya mti aliokuwa akichimba dawa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamis Selemani iliwataja waliokutwa wamekufa kuwa ni Nsoma Dotto (60) mkazi wa Kijiji cha Zugimlole Wilaya ya Kaliua na Mayara Marashi (50) ambaye ni mkazi wa Igunga.

Kamanda Selemani alisema Nsoma alikutwa akiwa amekufa umbali wa mita 200 kutoka nyumbani kwake juzi.

Alisema bibi huyo alikutwa amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki akiwa na vibuyu vitano huku pembeni yake kukiwa na kuku mweupe. Uchunguzi wa awali wa jeshi hilo, unaonesha kuwa huenda ni imani za kishirikina.

Aidha, alisema Marashi ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mwakapinga, Kata ya Nanga, aliyekuwa mganga wa kienyeji, mwili wake uliokotwa Januari 16, mwaka huu ukiwa umeanza kuharibika.

Kwa mujibu wa Kamanda Selemani, mganga huyo wa kienyeji aliondoka nyumbani kwake Januari 8, mwaka huu kwenda porini kuchimba dawa, lakini hakurudi kijijini hadi maiti yake ilipookotwa akiwa amekufa.

Alisema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho. Aliwaomba wananchi wanaoenda porini kwa ajili ya shughuli zozote zile, wawe wanatoa taarifa kwa ndugu zao ili iwe rahisi tatizo linapotokea.
Share:

Rais wa Uturuki Awasili Nchini Kwa Ziara ya Kikazi

RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini jana jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na niaba ya Mheshimiwa Rais. Dkt. John Magufuli.

Rais huyo ameambatana na mkewe Mama Emine Erdogan pamoja na Mawaziri watatu ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mevlüt ÇavuÅŸoÄŸlu, Waziri wa Uchumi Mheshimiwa Nihat  Zeybekekci na Waziri wa Nishati na Maliasili Mheshimiwa Berat Albayrak

Pia Rais huyo ameambatana na wafanyabiashara wapatao 85 wa nchi hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   na Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan  aliyefuatana na  mkewe, Mheshimiwa Emine Erdogan (kulia) wakifuhia ngoma kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage jijini Dar es salaam baada ya Rais huyo  kuwasili kwa ziara rasmi nchini Januari 22, 2017. Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Share:

Zitto Kabwe Asakwa na Jeshi la Polisi kwa Uchochezi,ACT Wazalendo Wadai Yuko Salama, Wataka Polisi Wafuate Utaratibu

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARY TAREHE 23.1.2017

Share:

Sunday 22 January 2017

MH RAIS MAGUFULI AMTEUA ANNE KILANGO MALECELA KUWA MBUNGE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,  tarehe 21 Januari, 2017 amemteua Anne Kilango Malecela kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Anne Kilango Malecela ataapishwa kwa mujibu wa taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

21 Januari, 2017
Share:

Saturday 21 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARY TAREHE 21.1.2017

Share:

Friday 20 January 2017

Donald Trump Kukabidhiwa Leo IKULU Ya Marekani


Mshindi wa uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba Donald Trump leo anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani.

Bw Trump wa Chama cha Republican anatarajiwa kuapishwa mbele ya watu 750,000 mbele ya majengo makuu ya bunge la Marekani, Capitol Building, Washington D.C.

Kisheria, rais anafaa kuapishwa kabla ya saa sita mchana saa za Amerika Mashariki ambazo Afrika Mashariki ni saa mbili usiku.

Hii hapa ni ratiba fupi ya matukio yanayotarajiwa siku hiyo.
Saa 17:30 (Saa za Afrika Mashariki) Wanamuziki walioalikwa wataanza kutumbuiza.

19:30 Hotuba za kufungua sherehe zitaanza kutolewa.

20:00 Muda mfupi kabla ya saa Mbili Afrika Mashariki Donald Trump atalishwa kiapo cha kuwa rais wa Marekani na Jaji wa Mahakama ya Juu John Roberts.

Baadaye, kutakuwa na msafara baada ya sherehe ya kuapishwa ambao utaanza katika vidato vya jumba la Capitol Building kuelekea ikulu ya White House kupitia barabara maarufu ya Pennsylvania Avenue.

Bw Trump na mkewe Melania baadaye watacheza dansi katika matamasha matatu, mawili katika ukumbi wa mikutano wa Walter E Washington na jingine katika ukumbi wa Jengo la Makumbusho ya Taifa.

Miaka minane iliyopita, Rais Obama alipokuwa anaapishwa kura rais, waliohudhuria walikuwa watu 1.8 milioni.
 
Siku moja baada ya kuapishwa kwa Bw Trump, wanawake takriban 200,000 wanatarajiwa kuandamana Washington DC na miji mingine kumpinga Bw Donald Trump.

Hillary Clinton na mumewe Bill wamethibitisha kwamba watahudhuria sherehe hiyo, sawa na George W Bush na mkewe Laura.

Wamesema wanataka “kushuhudia kukabidhiwa madaraka kwa rasi mwingine kwa njia ya amani.”

Rais mwingine wa zamani Jimmy Carter atahudhuria pia, lakini George HW Bush, 92, na mkewe Barbara hawataweza kwa sababu za kiafya.

Chanzo: bbcswahili
Share:

TAARIFA KWA UMMA: MAOMBI YA NAFASI 1000 ZA MAFUNZO YA STADI ZA KUTENGENEZA VIATU


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU

Image result for SERIKALI YA TANZANIA
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger