Monday 28 November 2016

RAIS Magufuli Ampongeza Paul Makonda

RAIS John Magufuli amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa juhudi za kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Magufuli ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na Mkuu huyo wa Mkoa huo kwa njia ya simu wakati Makonda akiendelea na mkutano wa hadhara katika eneo la Mbezi Maramba Mawili jijini humo.

Amesema, juhudi anazozifanya Makonda ni za kuigwa na viongozi wengine katika mikoa yao kwani anasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

“Wananchi wana kero nyingi sana, lakini viongozi wao wangekuwa wanawasikiliza hata maswali wanayouliza hapo yasingeulizwa, nakupongeza sana Mkuu wa Mkoa natamani na viongozi wengine wangeiga mfano wako,”amesema Magufuli.

Rais alipigiwa simu na Makonda ili asaidie kutoa ufafanuzi kuhusu upana wa barabara zilizopo chini ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads) baada ya wananchi kulalamikia kuvunjiwa maeneo yao ili kupisha ujenzi.

Katika ufafanuzi wake, Rais Magufuli alisema suala la barabara kutoka Ubungo hadi Ruvu tayari wameshalitolea ufafanuzi mara nyingi.

Amesema akiwa Waziri wa Ujenzi wakati serikali inataka kupanua barabara ya kutoka Ubungo kwenda Kibaha kulitokea malalamiko ya aina hiyo na kesi kuhusu suala hilo namba 137 ilifikishwa mahakamani ambapo serikali ilishinda na baadaye yalitolewa maelekezo kuhusu maeneo yaliyopo katika hifadhi ya barabara.

Amesema baada ya ushindi huo kutoka Mahakama Kuu walichukua hatua ya kubomoa nyumba zote zilizokuwa katika hifadhi ya barabara kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1932 ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 1949 ikafanyiwa tena marekebisho mwaka 1954 na mwaka 1965.

Amesema Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Vijiji namba tano ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji na Matumizi ya Ardhi ya mwaka 2007 zote zinatambua hifadhi ya barabara na kwa barabara ya Dar es Salaam kwenda Kibaha iliachwa kwa upana uliopo kama filta ya Jiji la Dar es Salaam.

“Mwito wangu kwa wananchi wazingatie sheria na sheria ni msumeno, tulitunga sheria sisi wenyewe hivyo ni wajibu wetu sisi serikali kusimamia sheria, lakini kama wanaona sheria haifai ni kiasi cha kwenda kulishauri Bunge libadilishe sheria ili barabara ya Ubungo iwe sentimita tano zipite bajaji tu, lakini ukweli unabaki palepale kwamba sheria ipo na haijawahi kubadilishwa,”amesema Rais Magufuli.

Aidha Magufuli aliipongeza Tanroads kwa kusimamia sheria kwani alisema itafika kipindi kutakuwa hakuna barabara nchini.

Rais Magufuli amesema pia kazi ya kuvunja nyumba zilizopo katika hifadhi ya barabara ipo pale pale kwa vile serikali imepata kiasi cha Sh bilioni 67 za kujenga barabara zinazobadilishana (interchange) katika eneo la Ubungo ambayo itakuwa ya ghorofa mbili au tatu ili kurahisisha usafiri.

“Ghorofa zote na majengo yatavunjwa bila fidia hata kama litakuwa jengo la Tanesco kwa sababu lazima tuzingatie sheria, lakini kama wananchi wataona wameonewa basi waende mahakamani,” alisema.
Share:

MTOTO WA MIAKA 11 ATUNUKIWA PHD TANZANIA

WAHITIMU, viongozi na wageni waliohudhuria Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mkoani Morogoro, waliingiwa na simanzi wakati mtoto, Tamar Aaron Mbogho (11), alipojitokeza na kupokea Shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD), akimwakilisha mama yake Swai Sophia Faustin ambaye alifariki dunia miezi sita kabla ya kufika siku ya mahafali.
Tamar, mtoto pekee wa marehemu, ambaye baba yake mzazi ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, Aaron Mbogho alifika katika hafla hiyo akiwa ameambatana na ndugu zake kadhaa, tayari kwa ajili ya kupokea heshima hiyo kwa niaba ya mama yake.
Gazeti hili liliweza kuwasiliana kwa njia ya simu na Mbogho akiwa katika kituo chake cha kazi Mwanga ambapo alisema Tamar alifika katika hafla hiyo kupokea shahada hiyo kwa niaba ya mama yake.
Kwa mujibu wa Mbogho, mkewe Dk Sophia alifariki dunia Mei 21, 2016, wakati huo akiwa ameshahitimu masomo yake kikamilifu na alisema Tamar ni mtoto wa pekee wa Sophia.
"Alikuwa ni mmoja wa wahitimu waliopaswa kutunukiwa shahada hiyo kwa sababu tayari alishahitimu na kubakia muda wa mahafali, lakini bahati mbaya akafariki dunia kabla ya muda kuwadia,” alisema na kuongeza.
"Binti yetu alipenda kwenda kuchukua shahada ya mama yake na alisindikizwa na ndugu zake wa familia. Ameniambia malengo yake ni kusoma kwa bidii ili aweze kupata Shahada ya Udaktari wa Falsafa kama mama yake, " alisema Mbogho.
Katika mahafali hayo yaliyofanyika juzi katika Kampasi ya Solomon Mahlangu, Mazimbu, wahitimu 61 walifuzu na kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
Naibu Makamu Mkuu Taaluma wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Peter Gilla, alisoma orodha ya watunukiwa ambapo pia alitaja jina la mwanafunzi asiyekuwapo ambaye alifariki dunia, lakini akiwa amefuzu na anastahili kupata Shahada ya PhD ya Chuo Kikuu hicho ambaye ni Sophia.
Hivyo, Mwenyekiti wa Mahafali hayo, Dk Benno Mrembuka, alimwongoza mtoto Tamar kwenda kupokea shahada hiyo kutoka kwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Fedha na Utawala, Profesa Yonika Ngaga, hali iliyoleta simanzi na huzuni kwa washiriki waliokuwepo katika mahafali hiyo.
Baadaye Tamar alielekezwa kufika mbele ya meza kuu ili kuwapa mkono wageni mbalimbali ambao walitumia nafasi hiyo kumfariji kutokana na kumpoteza mama yake mzazi ambaye alikuwa ni mhitimu.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Gerald Monela, alisema SUA imeendelea kutoa wahitimu wa Shahada ya Sayansi na Ualimu katika masomo ya sayansi kwa ajili ya kukidhi mahitaji makubwa ya walimu wa kufundisha shule za sekondari nchini.
Share:

KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOV 28 2016

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBER TAREHE 28.11.2016

Share:

Sunday 27 November 2016

SERIKALI KUNUNUA NDEGE ZA KISASA KUIMARISHA ULINZI HIFADHI ZA TAIFA



SERIKALI imepanga kununua ndege za kisasa ili kuimarisha ulinzi katika Hifadhi za Taifa nchini.
Hayo yamesemwa jana na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi wakati akihojiwa na kipindi maalumu cha TUNATEKELEZA kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC1).
Meja Jenerali Milanzi anasema Serikali imeweka mfumo maalumkatika  kulinda hifadhi zilizopo na ili kuweza kukabiliana na ujangili unaojitokeza katika hifadhi mbalimbali nchini.
“Sekta ya Utalii nchini inachangia pato la taifa kwa takribani asilimia 17.5 na kutoa ajira kwa zaidi ya watumishi milioni 3 katika sekta mbali mbali ya utalii nchini, hivyo ni vyema tukaweka mikakati madhubuti katika kulinda vyanzo vilivyopo” alisema Meja Milanzi.
Aidha, alisema kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wote watakaobainika kujihusisha na ujangili pamoja na biashara ya magogo ili kulinda hifadhi za Taifa na kuweza kuvutia watalii nchini.
Aidha Meja Jenerali Milanzi aliitaka jamii kwa ujumla kuona umuhimu wa kutumia nishati mbadala ili kulinda misitu iliyopo kwa kutunza mazingira na hifadhi za taifa.
Mbali na hayo Meja Jenerali Milanzi alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazovutia watalii wengi kutoka Marekani na Uingereza hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria na kanuni zinazosimamimia Hifadhi za Taifa ili kuzudi kuvutia watalii nchini.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOV 27 2016

Share:

MADEREVA WA SERIKALI NA TAASISI ZA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI



KAMANDA wa Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga ametoa wito kwa madereva wote ikiwemo madereva wa Serikali na Mashirika ya Umma kuzingatia sheria za Usalama Barabarani.
Kamanda Mpinga ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya “Abiria paza sauti” inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 28 Novemba, mwaka huu.
Kamanda Mpinga alisema kumekuwa tabia ya baadhi ya madereva hususani wa Serikali na mashirika ya umma ya kutofuata sheria za usalama barabarani kwa kuendesha magari kwa mwendokasi, na kuwaonya kuwa sheria ni msumeno na inapaswa kufuatwa na kila mtu.
“Kumekuwa na madereva hasa wa magari madogo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ya nchi huku wakiwa hawana uzoefu wa kuendesha umbali mrefu na hivyo kupelekea uvunjifu wa sheria za barabarani kwa kuendesha kwa mwendokasi na kusababisha ajali” alifafanua Kamanda Mpinga.
Akifafanua zaidi Kamanda alisema uzoefu unaonyesha kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka kumekuwa na ongezeko kubwa la magari barabarani, na hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria za barabarani ili kuweza kupunguza ajali za barabarani.
Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani, Jackson Kalikumtima alisema lengo la kampeni ya Paza Sauti ni kuhamasisha ushiriki kamilifu wa wananchi katika kukabiliana na ajali kwa kuchukua hatua stahiki bila ya uwepo wa askari.
Pia alisema kuwa kampeni hiyo imelenga kubadili tabia na mtazamo wa madereva kuhusu usalama barabarani ili waendeshe kwa kuzingatia sheria bila shuruti na kubadili mtazamo wa wananchi kuhusu usalama barabarani ili watambue kuwa usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja.
Naye Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, (ASP), Deus Sokoni alisema mkakati wa kupunguza ajali barabarani katika kampeni hiyo  umelenga katika kutoa elimu kwa jamii ili kuona suala la usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja na si jukumu la Polisi pekee.
“hakuna asiyetumia barabara duniani, hatutaki ajali tunataka kuishi salama, hivyo kila abiria anawajibu wa kutunza na kutii sheria za barabarani “ aliongeza Mwanasheria huyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA), Hassan Mhanjama aliwataka abiria wote nchini hususani wanaotajaria kusafiri mwishoni mwa mwaka kuwasiliana na Mamlaka ya Usafirishaji SUMATRA pindi watakapopandishiwa nauli mbali na taratibu zilizopo
Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBER TAREHE 27.11.2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO


TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Saturday 26 November 2016

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VYA VETA 2017

Image result for VETA.GO.TZ
Share:

MH.UMMY MWALIMU :TAHADHARI KUHUSU UTAPELI HUU

 MoHCDGEC
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOFANIKIWA KUHAMIA CHUO KIKUU UDOM 2016/2017

 Image result for UDOM.AC.TZ
Share:

Muuguzi anayedaiwa kumwambia mama wa mgonjwa ‘ataisoma namba kumchagua Magufuli’ atambuliwa

Mbeya. Muuguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya anayedaiwa kumkamshifu Junes Elias, mkazi wa Mbozi mkoani Songwe na Rais John Magufuli ametambuliwa.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Dk Gloria Mbwille alisema muuguzi huyo ametambuliwa na kwamba tume imeundwa kuchunguza tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kuhusu muuguzi huyo wala kumtaja jina akisema taarifa zaidi zitatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya tume kukamilisha uchunguzi huo. Juzi mchana, Junes alimueleza Makalla kwamba alifika hospitalini hapo Novemba 22 asubuhi akitokea wilayani Mbozi.

Alisema baada alifuata taratibu za kufungua kadi kwa gharama ya Sh5,000 kwa ajili ya kutaka matibabu ya mtoto wake, Joyce Asifiwe (9), lakini alikashfiwa kwenye dirisha la dawa akiambiwa ataisoma namba kwa kumchagua Rais Magufuli.

Alisema baada ya kumuona daktari aliandikiwa dawa za kwenda kuchukua kwenye dirisha ambako ndiko alikotolewa maneno ya kashfa.

“Kwenye dirisha hilo nilimkuta muuguzi mmoja ambaye aliniambia kwamba dawa zote zinauzwa. Hapa hakuna dawa za bure, si mlimchagua Magufuli, sasa mtaisoma namba,’’ alisema akidai kumnukuu aliyemtaja kuwa ni muuguzi.


Baada ya kumsikiliza malalamiko hayo, Makalla aliagiza mganga mkuu aitwe, lakini ilielezwa alikuwa safarini, hivyo kaimu wake, Dk Ismail Macha alifika.

Makalla alimueleza Dk Macha kwa kifupi yaliyojiri kutoka kwa mlalamikaji huyo na kumtaka waongozane hadi hospitalini na kuwaita wauguzi waliokuwa zamu Novemba 22 dirisha la dawa ili amtambue mhusika na achukuliwe hatua jambo ambalo limefanyika.
Share:

Rais wa Zamani wa Cuba, Fidel Castro Afariki Dunia

CUBA: Rais wa zamani wa Cuba, na kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha nchini humo, Fidel Alejandro Castro Ruz amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 90.
Share:

Magazeti ya Leo Jumamosi november tarehe 26.11.2016

Share:

Friday 25 November 2016

official VIDEO | MwanaFA Ft. Vanessa Mdee – Dume Suruali | Watch/Download


dume
Share:

Rais Magufuli amualika Rais wa Zambia kwa ziara ya siku 3

Share:

Ripoti ya uchunguzi wa mali za BAKWATA yakabidhiwa

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber  jana amekabidhiwa ripoti ya awali iliyoandaliwa na tume ambayo ameiunda  kwa ajili ya kufanya uchunguzi  na kuzibainisha  mali zote za  Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Akizungumza wakati wa kumkabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa tume hiyo Sheikh Abubakari Khalid Hajj alisema kuwa  ripoti hiyo imefanyika kwa muda wa miezi mitatu licha ya kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa muda.

Aidha aliwambia wanahabari kuwa uchunguzi huo umehusisha ufuatiliaji wa mali za Bakwata katika Mkoa wa Dar es salaam pekee,ikiwemo majengo,viwanja, pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ili  kujiridhisha kama imefuata taratibu za kisheria.

Akizungumza mbele ya wanahabari mara baadi ya kupokea ripoti hiyo Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber alisema kuwa ataipitia ripoti hiyo  ili kujua yale yaliyobainishwa na tume yake, na kuahidi kuyafanyia kazi mapema iwezekanavyo.

Hata hivyo Mufti huyo ameiongezea muda wa miezi mitatu tume hiyo ambayo ina jumla ya  wajumbe wanane kwa ajili ya kukamilisha kuandaa ripoti ya mkoa wa Dar es salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine kwani zoezi hilo litafanyika nchi nzima.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger