Saturday 30 July 2016

New AUDIO | Cannibal Ft. Juma Nature - Buti Na Shati | Download

Share:

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Julai, 2016 ameanza ziara ya siku nne katika mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita akitokea mkoani Dodoma

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Julai, 2016 ameanza ziara ya siku nne katika mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita akitokea mkoani Dodoma, ambapo amezungumza na wananchi kwa lengo la kuwashukuru kwa kumpigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana  na kueleza juhudi zinazofanywa na serikali katika kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo.
Akiwa Mkoani Singida, Rais Magufuli aliyeongozana na mkewe Mama Janeth Magufuli amewasihi watanzania kufanya kazi kwa juhudi na kujiepusha na vitendo vya vurugu vinavyohamasishwa na baadhi ya wanasiasa huku akionya kuwa serikali yake haitamvumilia mtu yeyote ambaye atathubutu kuchochea vurugu ikiwemo maandamano kinyume cha sheria.
"Sitaki nchi hii iwe ya vurugu, watakaoleta vurugu mimi nitawashughulikia kikamilifu bila huruma, na wasije wakanijaribu, mimi ni tofauti sana na kama wapo watu wanaowatumia wakawaeleze vizuri, mimi sijaribiwi na wala sitajaribiwa.
"Wananchi hawa wana shida, na siasa nzuri ni wananchi washibe, siasa nzuri ni wananchi wetu wapate dawa" Amesema Rais Magufuli.
Kuhusu hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali yake ya awamu ya tano tangu aingie madarakani Rais Magufuli ametaja baadhi ya  hatua hizo kuwa ni kufuta ada kwa shule za msingi na sekondari, kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu zaidi ya laki moja na kuongeza fedha za miradi ya maendeleo katika bajeti ya serikali kutoka asilimia 26 ya mwaka 2015/2016 hadi kufikia asilimia 40 katika bajeti ya mwaka huu 2016/2017.
Hatua nyingine ni kuondoa wafanyakazi hewa 12,500 katika orodha ya waliokuwa wanalipwa mshahara na serikali, kudhibiti upotevu wa mapato serikalini, kutenga shilingi Trilioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Reli ya kati kwa kiwango cha kisasa yaani Standard gauge na pia akazungumzia hatua zilizochukuliwa dhidi ya wala rushwa na wanaojihusisha na ufisadi kwa kuunda mahakama ya mafisadi huku akiapa kuwa katika kipindi chake hakuna fisadi atakayeendelea kutamba.
Akiwa njiani Rais Magufuli amewasalimu wananchi wa Ikungi na baadaye amefanya mkutano wa hadhara Singida Mjini ambako amesisitiza kuwa serikali yake haiko tayari kumvumilia mtu yeyote atakayekwamisha utekelezaji wa Ahadi na Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Singida
29 Julai, 2016
Share:

VIDEO:RAIS MAGUFULI AWAONYA UKAWA/UKUTA KUHUSU MAANDAMANO


Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULY TAREHE 30.7.2016








Share:

Audio: Msikilize Rais Magufuli Akizungumzia Jinsi Atakavyoyapiga Mnada Majengo ya Serikali Dar na Atakachofanya Kwa Watumishi Watakaokataa Kuhama


Rais John Magufuli amesema azma ya Serikali yake kuhamia Dodoma haraka iwezekanavyo ipo pale pale huku akiwaonya wale wataong'ang'ania kubaki Dar es Salaaam kuwa watakuwa wamejifukuzisha kazi wenyewe.

Alitoa msimamo huo mjini Singida jana kwenye mkutano wake wa kwanza wa hadhara  tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka jana.

Alisema kuwa licha ya kuhamia Dodoma atahakikisha anauza majengo ya wizara mbalimbali yaliyopo Dar es Salaam kwa mnada ili wale wasiotaka kuhama,wahame kwa lazima.

Bonyeza Audio ya kwanza  na  ya Pili Kumsikiliza akiongea

DOWNLOAD HAPA>>>>>http://music.audiomack.com/tracks/mpekuzi-blog/kauli-ya-rais-magufuli-kuhusu-watumishi-watakaokataa-kuhamia-dodoma.mp3?Expires=1469860388&Signature=Tkt1fHvqeGAnYia4-kHzhc1T-R8eNf0nlhlMBBcBJi1Ggz87PO18Q7gLHu5ceVeTdixLL67tIxDVhe1Mo9gTweZkfczrehg~VHg9zkterVlLJU0fwv7ODqwpx1dO~~EjgaoPNi9S7JHKDZQk9S0EYS97TueHMQV3TqLKhl4FXE4_&Key-Pair-Id=APKAIKAIRXBA2H7FXITA  

 DOWNLOAD HAPA>>>>>>http://music.audiomack.com/tracks/mpekuzi-blog/kauli-ya-rais-magufuli-kuhusu-watumishi-watakaokataa-kuhamia-dodoma-1.mp3?Expires=1469860577&Signature=elpI6pFvDo~PaFI-Bsi4neQOUsQkqJmL4nIPRbUc-ROSODHG1gcPNsQFF-GZGEDEp5K8se5BgfXuw4w87-TKm4ZPBDF8JffkXswzOo9otcmqG-xC-t6ftiVKEuqwgHyimSN35bQlAuvefxQtjIVSlomaSHXpgdnSTvWgULhNlhM_&Key-Pair-Id=APKAIKAIRXBA2H7FXITA
Share:

Friday 29 July 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU SABABU ZA KUTOKUCHAGULIWA KWA BAADHI YA WALIOOMBA KUDAHILIWA KATIKA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU SABABU ZA KUTOKUCHAGULIWA KWA BAADHI YA WALIOOMBA KUDAHILIWA
KATIKA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
Baraza linapenda kuwaarifu wote walioomba kudahiliwa katika kozi za cheti na diploma na umma kwa ujumla kuwa kuna baadhi ya waombaji ambao hawakuchaguliwa kwenye uteuzi wa kwanza ambao ulitolewa tarehe 22 Julai 2016.  

Mwombaji ambae hakuchaguliwa hupaswa kuangalia kwenye kurasa yake binafsi (profile) ili kupata sababu za kutokuchaguliwa. Sababu za kutokuchaguliwa zinaweza zikawa kama ifuatavyo:
1. Sifa za muombaji kuwa pungufu kulinganisha na sifa za chini za kozi;
2. Nafasi za mafunzo katika chuo na kozi husika kujaa kutokana na ushindani wa waombaji wenye sifa za juu zaidi.
3. Kutokamilisha ujazaji wa maombi kwenye mfumo;
4. Kutoambatanisha vyeti vya masomo kwa baadhi ya waombaji; na
Waombaji wanashauriwa kusoma kwa makini sababu hizo na kufuata ushauri unaotolewa ili kuweza kuchaguliwa katika uteuzi unaofuata.

Baraza linaomba ifahamike kuwa vyuo na kozi zilizojaa hazitaonekana tena wakati wa maombi bali kozi zitakazoonekana ni zile zenye nafasi tu. Orodha ya kozi zilizojaa zimeainishwa hapa
.
Baraza pia linapenda kuwaarifu waombaji waliofanya maombi kwenye vyuo vya Ualimu vya Serikali kuwa uteuzi kwenye vyuo hivyo unasubiri mwongozo wa Serikali na hivyo watafahamishwa punde uteuzi utakapokamilika. Waombaji wa vyuo hivi wanashauriwa kusubiri na kutokubadili machaguo yao hadi kutangazwa kwa uteuzi kwa vyuo vya Ualimu vya Serikali.

Aidha Baraza linapenda kuwafahamisha waombaji wa Shahada ya Kwanza waliofanya maombi kupitia mfumo wa pamoja wa udahili wa Baraza kuwa utaratibu wa kukamilisha maombi yao utatolewa baada ya mashauriano kati ya Baraza na Tume ya Vyuo Vikuu yatakapokamilika.

Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 28 Julai, 2016
Share:

Taarifa kwa Wanafunzi Wote Kuhusu tarehe ya Kufungua Chuo sekta ya uvuvi Tanzania bara 2016/2017

 Fisheries Education and Training Agency

Taarifa kwa Wanafunzi Wote Kuhusu Kufungua Chuo

Kurugenzi ya Mafunzo na Utafiti Inapenda Kuwatangazia Wanafunzi Wote wa Wakala Wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwamba, Tarehe ya Kufungua Chuo Imebadilishwa tena na Hivyo kwa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza (New Comers) Pamoja na Wale Wanaotarajia Kufanya Mitihani ya Supplementary na Mitihani Maalum (Special Exams) Wataripoti Kuanzia Siku ya Jumatatu ya Tarehe 29 Mwezi Agosti. Aidha Wanafunzi Wanaoendelea Wao wataripoti chuo Kuanzia Jumatatu ya Tarehe 5 Mwezi wa Septemba. Tunaomba Radhi sana Kwa Usumbufu Wote Ambao utajitokeza.
Imetolewa na
Kurugenzi ya Mafunzo na Utafiti
28/07/2016
 
 
 
Share:

MPYA:NAFASI ZA MASOMO KWA FORM SIX 2016 ,WALIOKOSA SIFA ZA KUNDELEA NA CHUO KIKUU 2016/2017


Share:

UDOM:CALL FOR APPLICATIONS INTO POSTGRADUATE PROGRAMMES FOR 2016-2017ACADEMIC YEAR

Share:

MPYA:NAFASI ZA KAZI SUA-FRESH GRADUATE FROM SUA WANAHITAJIKA HARAKA SANA

Fresh graduates required

Tokeo la picha la suanet.ac.tz

The School of Agricultural Economics and Business Studies (SAEBS) at the Sokoine University of Agriculture (SUA) is looking for fresh graduates in BSc Agricultural Economics, Agri-business Management or any other Agriculture-related disciplines with some experience in rural households’ data collection to be engaged for a short-term data collection assignment.

Qualified candidates should send in their application to the email address saebs@suanet.ac.tz copied to amakyoo@yahoo.co.uk ; zekenya@yahoo.com and indicate “ENUMERATOR” in the subject line. Applications can also be dropped at the School’s offices at the New Agribusiness Incubator building off Morogoro – Iringa Highway Road in the main campus, Morogoro Municipality. Applicants must include a cover letter, CV and academic and professional certificates. Application must be received by Friday, 5th
Share:

Taarifa muhimu kwa wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu walioko Dar es Salaam

Share:

Bingwa wa kubikiri Wasichana Nchini Malawi abainika ana UKIMWI........Rais Aamuru Akamatwe Haraka


Rais wa Malawi, Peter Mutharika juzi alitoa amri ya kukamatwa kwa Eric Aniva ambaye hivi karibuni alibainika kufanya kibarua cha kuwabikiri mabinti wa chini ya umri wa miaka 13 zaidi ya 100.

Amri hiyo ya Rais imekuja baada ya kubainika kuwa mwanamume huyo maarufu kwa jina la ‘Fisi’ anaishi na Virusi vya Ukimwi (VVU). 

Mutharika alisema lazima mwanamume huyo akamatwe na hatua kali zichukuliwe dhidi yake kwa kuwa, kwa makusudi alifanya vitendo viovu akijua anaishi na VVU na lengo lake lilikuwa kuwaambukiza mabinti hao.

Aniva aliingia matatani baada ya kukiri katika mahojiano akijinasibu kuwa anaendesha maisha kwa kuwabikiri mabinti na kwamba hulipwa kuanzia dola nne za Marekani mpaka saba ambayo ni wastani wa Sh10,000 kwa kila mtu.

Mwanamume huyo alisema wazazi wa mabinti huwa wanampa kibarua cha kuwavusha kutoka utoto kuingia katika utu uzima na kwamba hatua hiyo ni sawa na tambiko. 
Share:

Waombaji wa Mikopo Elimu ya juu Wafikia 69,820 Mpaka Sasa


JUMLA ya wanafunzi 69,820 wameomba mikopo kwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) hadi sasa ikiwa zimebaki siku tatu kufikia mwisho wa kupokea maombi hayo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa bodi hiyo, Cosmas Mwaisoga, alisema mwaka jana walioomba kupewa mikopo walikuwa 65,000, hivyo waombaji wa mwaka huu wameongezeka.

Mwaisoga alisema tofauti na awali, mchakato wa sasa wa kuomba unafanyika kwa njia ya mtandao na baada ya kutumwa kwao, watayapitia na kwa yale yenye kasoro, wahusika wataitwa ili wayarekebishe.

Alisema dirisha la uombaji wa mikopo linatarajia kufungwa Jumapili hii.

Katika hatua nyingine, alisema idadi ya wanaorejesha mikopo imeongezeka maradufu baada ya kutakiwa kufanya hivyo.

“Kwa sasa ni vigumu kutaja idadi yao kwa sababu huwa tunaitoa mwishoni mwa mwezi kwa hiyo kesho tutakuwa na idadi kamili ya waliorejesha, lakini ikilinganishwa na huko nyuma, sasa hivi mwitiko wa wanaorejesha umeongezeka,” alisema.

Mwaisoga alisema sheria inamtaka aliyekopa aanze kurejesha baada ya mwaka mmoja wa kuhitimu masomo yake, lakini anapochelewesha, kila mwaka kunakuwa na penati ya ongezeko la asilimia sita.
Share:

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULY TAREHE 29.7.2016


Share:

Mkapa ahimiza sera zinazotekelezeka


RAIS mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, amezitaka nchi za Afrika kuhakikisha zinatoa kipaumbele katika uongozi unaojali masuala ya utawala bora, uzalendo na sera zinazotekelezeka ili kuweza kupata maendeleo endelevu.
Kwa mujibu wa Mkapa pamoja na marais wengine wastaafu wa nchi za Afrika, endapo nchi hizo zitashindwa kutumia njia sahihi kufikia malengo yake ya maendeleo zitajisababishia kuwa nchi zisizo na usawa katika mgawanyo wa mali na migogoro.
Akizungumza katika Kongamano la Viongozi wa Afrika lililofanyika jijini Dar es Salaam jana, Rais Mkapa alisema ni lazima Waafrika wajitume na kujiletea maendeleo yao wao wenyewe na kusisitiza kuwa hakuna mtu yeyote wa mataifa ya nje atakayewasaidia.
Alisema ni wakati muafaka sasa kwa Waafrika kuungana na kutumia uwezo walionao kuhakikisha ajenda ya Umoja wa Afrika (AU) ya kutafuta na kutumia rasilimali zinazopatikana Afrika ifikapo mwaka 2063 inafanikiwa.
“Kaulimbiu ya mwaka huu, inasema namna Sekta ya Biashara inavyoweza kuleta mageuzi Afrika kwa haraka. Kama mnavyojua katika ajenda yetu ya 2063 tumejiwekea malengo ya kuhakikisha nchi za Afrika zinakua kiuchumi na kuwa na maendeleo endelevu…lakini ili haya tuyafanikishe ni lazima tutegemee zaidi ushiriki wa Waafrika,” alifafanua.
Alitolea mfano kipindi cha uongozi wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere kwamba aliweka msisitizo katika masuala ya watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora ili kuwapatia maendeleo Watanzania.
“Ardhi tuliyonayo inaweza kutumika kwa manufaa yetu, watu tulionao tunaweza kuwahamasisha kuwajibika, sera nzuri zinaweza kusaidia kusukuma watu kuleta maendeleo lakini pia utawala bora unatengeneza njia kwa maendeleo endelevu,” alisema Mkapa.
Naye Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Wachimba Madini cha Afrika Kusini na mtoa mada mkuu katika mkutano huo, Sipho Nkosi, alisema Afrika imekuwa na maendeleo mazuri ya kibiashara kwa muda mrefu na kusisitiza kuwa kwa mwenendo uliopo, bara hilo litaleta mageuzi makubwa duniani.
Nkosi ambaye ni bilionea wa tatu kwa utajiri Afrika Kusini, alisema kila nchi ya Afrika ina wajibu kutengeneza mazingira mazuri na fursa kwa wafanyabiashara Waafrika ili kuwajengea uwezo na kuwapa nafasi ya kuwa sehemu ya mafanikio ya nchi yao.
Kwa upande wake, Rais mstaafu wa Msumbiji Joaquim Chissano, alisisitiza umuhimu wa kutafuta mbinu bora za kisasa za kutumia ardhi ili iweze kuleta maendeleo katika nchi hizo za Afrika badala ya kutegemea zaidi mikakati na mbinu za nchi za Magharibi.
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika, Frannie Leautier, alisema nchi nyingi za Afrika zinakabiliwa na ukosefu wa viongozi wenye mikakati na uwezo wa kuziletea mabadiliko ya kiuchumi hali inayosababisha nchi hizo uchumi wake kukua taratibu.
Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki, alisema viongozi wanaochukia ubinafsi ndio chachu katika kuwawezesha Waafrika kukua kimaendeleo.
Share:

Asilimia 60 ya waajiriwa hawana mikataba ya kazi


KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimezindua Ripoti ya Haki za Binadamu na Biashara kwa Mwaka 2015 ambacho kimebainisha kuwa asilimia 60 ya wafanyakazi nchini hawana Mikataba stahiki ya kazi, jambo linalosababisha serikali kupoteza mapato ya kodi.
Aidha ripoti imebainisha Mikataba mingine iliyopo kuwa na upungufu mwingi ikiwa ni pamoja na miongoni mwao kuandikwa kwa lugha isiyoeleweka na mingine kuandikwa kwa ufupi na kushindwa kujumuisha mambo ya msingi.
Nalo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), limekiri kuwepo kwa matatizo hayo kwa wafanyakazi lakini likafafanua kuwa wengi ni waoga kufukuzwa kazi, hivyo wanashindwa kujitokeza hadharani na kueleza yanayowasibu.
Akizungumzia ripoti hiyo wakati wa uzinduzi jijini Dar es Salaam jana, Mtafiti wa Taarifa wa LHRC Clarence Kipobota alisema miongoni mwa wafanyakazi ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa kukosa Mikataba halali ya kazi ni pamoja na waandishi wa habari pamoja na madereva.
Alisema kutokuwepo pia kwa vyama vya wafanyakazi katika maeneo ya kazi, kumekuwa kukichangia wengi wao kukosa makubaliano ya pamoja.
“Hali ya ajira na mahusiano kazini inakabiliwa na changamoto kubwa, wengi hawana Mikataba na matokeo yake Serikali inakosa kodi ambayo ingekatwa katika Mishahara inayofahamika kama PAYEE,” alisema Kipobota huku akiitaka Tucta kusaidia kumalizwa kwa tatizo hilo.
Aidha alisema utatuzi wa masuala ya kazi unaofanywa na Tume ya Usuluhishi wa Migogoro sehemu ya Kazi (CMA) umekuwa hauna kasi kama inavyotakiwa kumalizika ndani ya siku 60 ambapo mashauri mengi huchukua muda mrefu.
Alisema asilimia 57.5 ambayo ni sawa na mashauri 30,095 ndio ambayo yamesikilizwa tangu mwaka 2006 hadi 2015.
Kuhusu suala la ardhi alisema ardhi za vijiji zinaendelea kuchukuliwa ambapo wawekezaji wa ardhi wamekuwa wakichukua eneo kubwa na kuliacha bila kuendelezwa huku wananchi wakiendelea kuhangaika jambo linalozalisha migogoro ya wakulima na wafugaji.
Share:

Chadema yakosa pa kushika


SIKU moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza nia ya kufanya mikutano ya hadharani nchini kote kuanzia Septemba Mosi kutokana na sababu mbalimbali, taasisi na wadau mbalimbali wamelaani mpango huo.
Akizungumzia hilo, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema amepokea kwa masikitiko makubwa tamko hilo, huku Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikijitokeza na kulaani mpango huo.
Wengine waliopinga mpango huo ni wasomi wakiwemo Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anayejipambanua katika siasa za upinzani, aliyewahi kuwa mwanachama wa Chadema, Dk Kitila Mkumbo na wachambuzi wa Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk Benson Bana na Dk Bashiru Ally.
Msajili vyama vya siasa alaani
Akizungumzia tamko hilo la Chadema, Jaji Mutungi alisema limejaa lugha ya uchochezi, kashfa, kuudhi na lenye kuhamasisha uvunjifu wa amani.
Alisema kimsingi Sheria ya Vyama vya Siasa namba 5 ya mwaka 1992 kifungu (2) (c) inakataza chama cha siasa kutumia au kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu kama njia ya kufikia malengo yake kisiasa.
Alisema aidha kifungu cha 9 (2) (f) kinakataza chama cha siasa kuruhusu wanachama au viongozi wake kutumia lugha ya matusi, kashfa na uchochezi ambayo inaweza kusababisha au kupelekea kutokea uvunjifu wa amani.
Alisema pia kanuni ya Maadili ya Vyama vya Siasa, Tangazo la Serikali namba 215, linakataza chama cha siasa kutumia lugha za matusi, kashfa, uongo na uchochezi.
Alisema Kanuni ya 5 (1) (d) inakitaka chama cha siasa kutotoa maneno yoyote au maandishi ambayo ni uongo, kuhusu mtu yeyote au chama cha siasa chochote. “Hivyo tamko la Chadema ni ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa.
Aidha, hii si mara ya kwanza kwa Chadema kutumia lugha za namna hii za kuhamasisha uvunjifu wa amani.
“Natumia fursa hii kukemea tamko hilo hadharani, kwa mujibu wa kanuni ya 6 (2) ya Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa, pia nawaasa Chadema wasiendeleze tabia hii,” alisema Jaji Mutungi.
Alisema dhamana aliyopewa kama Msimamizi wa Sheria ya Vyama vya Siasa kazi yake ni kuviasa vyama vyote vya siasa vitimize wajibu wao kwa weledi kama taasisi za kisiasa.
“Ni vyema viongozi wa vyama vya siasa wakaonesha taswira stahiki ya wanasiasa wakomavu, au vyama vya siasa vya kutolea mfano ndani na nje ya mipaka yetu, kwa kuzingatia sheria za nchi katika kuendesha shughuli za kisiasa. “Vyama vya siasa viepuke vitendo, kauli au matamshi yenye mlengo wa kusababisha uchochezi au kufarakanisha umma na serikali yao. Navisihi kuzingatia utaratibu wa mawasiliano kwa mujibu wa sheria zilizopo, aidha uvumilivu wa kisiasa katika azma za kudumisha ukuaji wa kidemokrasia nchini haukwepeki,” alisema Jaji Mutungi.
CCM wajibu mapigo
Katika hatua nyingine CCM imeionya Chadema kuacha kupotosha umma na kutaka kuwaaminisha wananchi uongo wanaoutunga ili kujaribu kupata wafuasi.
Aidha, imewataka Watanzania kupuuza maandamano yaliyopangwa kufanywa na Chadema kwa kuwa ni ishara ya kuchochea uvunjifu wa amani, huku ikiwataka viongozi hao wanaoshinikiza maandamano kuandamana na familia zao.
Msemaji wa CCM, Christopher ole Sendeka alisema Dar es Salaam jana kuwa tamko lililotolewa na Chadema la kupanga kufanya mikutano ya hadhara nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu, limejaa uongo na ubabaishaji na linaonesha kuwa wapinzani wamekosa ajenda na njia pekee wanayoona inafaa ni kutunga utapeli, uongo na uzushi.
Alisema kimsingi hoja walizotumia kufikia uamuzi wao bila kuzirudia zimejaa upotoshaji na uongo uliokithiri.
Alisema kwa mfano chama hicho kimekuwa kikidai serikali imezuia mikutano yote ya vyama vya siasa huku wakijua jambo hilo si kweli. “…Wamekuwa wakisema hivyo huku wakijua kuwa ni uongo kwani serikali haijazuia mikutano. Kwenye majimbo wabunge wao wako huru kufanya shughuli zao, tumeona wabunge wakifanya mikutano kwenye majimbo ikiwemo wa upinzani,” alisema Ole Sendeka.
Alisema vyama vya siasa kufanya shughuli zao kwa mujibu wa Katiba si kosa na wala si jambo ambalo limezuiliwa na ndio maana imeshuhudiwa vyama vya siasa vikifanya mikutano yao ya kikatiba bila tabu.
Ole Sendeka alisema jambo lingine ambalo ni hoja za uongo na uzushi ni kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ni ya kidikteta, na alihoji udikteta wanaousema Chadema ni upi? “Ni huu wa kushughulikia watumishi hewa, ni huu wa kuwabana wakwepa kodi, ni huu wa kupunguza na kudhibiti safari za nje, ni huu wa kubana matumizi ya serikali, ni huu wa kufukuza wazembe na wabadhirifu kazini? “Hivi udikteta huo ni huu wa kushughulikia mafisadi na mpaka kuanzisha Mahakama yao?” Alihoji Msemaji huyo wa CCM.
Alisema CCM inaamini Watanzania wengi wanaunga mkono hatua zinazochukuliwa na Rais John Magufuli na serikali yake, lakini kama hatua hizo Chadema inaona ni udikteta bila shaka wao ni sehemu ya mfumo mbovu na ndio maana wako tayari kuleta vurugu.
Wasomi UDSM wafunguka
Wakitoa maoni wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mkumbo, Dk Bashiru na Bana walikosoa mpango huo wa Chadema. Profesa Mkumbo alisema vyama vya siasa vina wajibu wa kulinda misingi ya demokrasia lakini pia vina haki ya kupigania kufanya shughuli za siasa ingawa si kwa mapambano.
Alisema ni muhimu vyama vya siasa kujenga amani ya nchi lakini akasema ni muhimu pia kwa Jeshi la Polisi kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu kupinga mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa.
“Pande zote mbili yaani Jeshi la Polisi na vyama vya siasa vipeane nafasi kila mmoja, bila kuvuruga shughuli za maendeleo, kulindwa kwa demokrasia na kuiendeleza,” alisema Profesa Mkumbo.
Naye Dk Bashiru alisema kauli ya kufanya mikutano nchi nzima ni vyema ikafafanuliwa, kuhojiwa au kutafsiriwa na taasisi za kidemokrasia ikiwemo Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo inasiamamia sheria za vyama vya siasa.
Alisema taasisi hiyo itoe ufafanuzi kwa kuzingatia sheria ili kuongoza kauli na vitendo vitolewavyo na vyama vya siasa katika kukuza demokrasia, pamoja na kuangalia matakwa ya wanasiasa ili isiwe ni kuvuruga misingi ya mamlaka.
Alisema hakuna mahali utaratibu, sheria na kanuni zinafuatwa kiholela, na kwamba uholela haujengi demokrasia bali ni chanzo cha chuki na hata kuumiza, hivyo yawepo mazungumzo ili kufikia muafaka na kama yupo asiyeridhika aende Mahakamani.
Kwa upande wake Dk Bana alisema kukaidi agizo linalotolewa na vyombo vya dola sio jambo jema na kwamba ni vyema kuheshimu ikiwa ndio njia ya kukuza demokrasia. Alisema kama chama hicho kinaona hakiridhiki na maagizo hayo wanaweza kutafuta ufumbuzi wake kwa kwenda Mahakamani ili kuitafuta huko.
Akizungumzia sakata hilo, Dk Bana alisema mpango huo si suluhisho la maridhiano ya kisiasa na badala yake utaleta vurugu na kuchochea uvunjifu wa amani.
Alisema Chadema wanapaswa kuachana na mpango huo na badala yake waombe kuonana na Rais Magufuli na viongozi wengine wa Serikali ili kuwasilisha hoja zao kuhusu mambo wanayoona hayaendi sawa, akisema Rais Magufuli ni msikivu.
‘Kutumia ubabe hakuwezi kuzaa mwisho mwema kwao, wangeweza pia kulitumia Bunge lakini walilikwepa, hivyo si njia za kiungwana kufanya mikutano hiyo kwa nchi nzima na watambue kuwa hawatoungwa mkono,” alisema Dk Bana.
Kuhusu kumwita kiongozi wa nchi dikteta, Dk Bana alihoji kama kitendo cha kutumbuliwa kwa majipu na mafisadi kimewaudhi au walitaka atumie sindano kubwa ama ndogo ili aweze kutimiza azma hiyo na wao waweze kufurahia.
Alisema Watanzania wameshaona mwanga wakitambua kuwa Rais Magufuli ndiye kiongozi wamtakaye na anaongoza serikali waitakayo na hivyo ni vigumu kuwaaminisha vinginevyo kama wanavyotaka kufanya Chadema.
Habari hii imeandikwa na Oscar Mbuza, Lucy Lyatuu na Katuma Masamba
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger