Sunday 3 July 2016

magazeti ya leo jumamosi july tarehe 2.7.2016

IMG_20160702_045007
IMG_20160702_045030
IMG_20160702_045053
IMG_20160702_045110
IMG_20160702_045132
IMG_20160702_045155
IMG_20160702_045220
IMG_20160702_045240
IMG_20160702_045305
IMG_20160702_045323
IMG_20160702_045347
IMG_20160702_045409
IMG_20160702_045431
IMG_20160702_045455
IMG_20160702_045517
IMG_20160702_045539
IMG_20160702_045602
IMG_20160702_045624
IMG_20160702_045646
IMG_20160702_045715
IMG_20160702_045741
IMG_20160702_045804
IMG_20160702_045826
IMG_20160702_045845
IMG_20160702_045903
IMG_20160702_045919
IMG_20160702_045939
IMG_20160702_045956
IMG_20160702_050014
IMG_20160702_050032
IMG_20160702_050047
IMG_20160702_050104
IMG_20160702_050122
IMG_20160702_050140
Share:

Share:

Friday 1 July 2016

MAJINA YA WANAFUNZI(DIPLOMA NA CHETI) WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU CHA MUCCOBS-MOCU 2016/2017

Share:

Mtumishi wa umma atakayekwenda kusomea 'first degree' sasa kuchukua likizo isiyo na malipo

Mtumishi atakayekwenda kusomea FIRST DEGREE anatakiwa achukue LIKIZO ISIYO NA MALIPO na hastahili kulipwa chochote na Mwajiri wake ikiwa ni pamoja na kutolipwa Mshahara kwakuwa HAYUPO KAZINI.
Hakuna malipo yoyote ya UHAMISHO kwa Mtumishi atakayehamishwa umbali usiozidi kilometa 10.

1467384890217.jpg
Share:

MPYA: Serikali imezuia Benki kupandisha viwango vya tozo katika miamala yake

Image result for TANZANIA
Mamlaka ya mapato Tanzania 'TRA' imetoa ufafanuzi kuhusu kodi ya ongezeko la thamani kwenye huduma za kifedha kuwa marekebisho ya sheria ya mwaka 2014 yaliyopitishwa na bunge yanayolenga kutoza kodi la ongezeko la thamani kwa kiwango cha 18% kwenye ada ambazo benki inatoza wateja wake kwenye huduma mbalimbali zitolewazo na benki au taasisi za fedha.

TRA wamesema taasisi za fedha wanapoongeza makato ya miamala ya fedha wanakosea kwa kupandishia wananchi kwa kuwa sheria hiyo inahusu fedha ambayo mwanachi alikuwa anakatwa na taasisi hizo ambayo hapo mwanzoni zilikuwa azilipiwi kodi kwa hiyo hizo ndizo zitakazokatwa 18%.

Mfano kama umetoa fedha ukakatwa 1000 na taasisi ya fedha ilikuwa haikatwi kodi lakini kwa sheria hiyo ada hiyo ndio itakatwa 18% na sio mwananchi kuongezewa makato kama ilivyofanyika kwa baadhi ya taasisi za fedha.
Share:

PICHA :Ajali Ya basi iliyotokea Mkoani Morogoro -imeua 11






Habari iliyoripotiwa hivi punde na kituo cha ITV ni kuhusu ajali ambayo imetokea eneo la Veta Dakawa mkoani Morogoro ikihusisha magari matatu ambayo ni lori la mafuta, kontena lililobeba mchele pamoja na basi.

Taarifa hiyo inasema kuwa watu 11 wamefariki dunia na wengine ambao idadi yao bado haijajulikana wamejeruhiwa.

Tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi kuhusu ajali hiyo.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya July 1

Share:

NECTA: TANGAZO LA USAJILI ACSEE 2017

TANGAZO LA USAJILI ACSEE 2017

Share:

Waziri Mkuu: Serikali Itatoa Waraka Juu Ya Ukusanyaji Mapato Kupitia Mawakala

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Halmashauri zitaelekezwa kwa waraka ni vyanzo vipi vitahitaji kutumia wawakala wa ukusanyaji mapato kwani siyo kila chanzo cha mapato ya Halmashauri kitakusanywa kwa ufanisi kwa kutumia au kwa kutotumia mawakala.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana mchana (Alhamisi, Juni 30, 2016) wakati akitoa hoja ya kuhitimisha mkutano wa tatu wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

Alisema katika ukusanyaji wa mapato, baadhi ya vyanzo vitapaswa kukusanywa na Halmashauri zenyewe kwa kuzingatia miongozo iliyotolewa na Serikali. 
“Moja ya miongozo hiyo ni kwamba kuanzia sasa, iwe kwa kutumia mawakala au Halmashauri zenyewe ni lazima fedha zinazokusanywa ziwekwe kwenye akaunti ya Halmashauri na kutumia mifumo ya kielektroniki ili kupunguza au kumaliza kabisa masuala ya kutumia malipo kwa fedha taslimu (cash transactions),” alisema.

Alisema katika kutekeleza agizo hilo, Halmashauri itabidi zikubaliane na wakala ni kiasi gani cha asilimia ya makusanyo kitalipwa kwa wakala na malipo yafanyike baada ya kukusanya na kuingizwa kwenye akaunti ya Halmashauri.

Alisema Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa Sura ya 290, inazipa uwezo Mamlaka za Serikali za Serikali za Mitaa kutoza na kukusanya kodi, ushuru na ada mbalimbali kama vyanzo vya mapato vya Mamlaka za Serikali za Mitaa.

“Sheria hiyo pia inazipa mamlaka hizo kuteua mawakala wa kukusanya mapato hayo kwa niaba ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu. Lakini Serikali imebaini changamoto za kiufundi katika kufanya tathmini ya vyanzo vya mapato; ugumu katika kupata mawakala wenye weledi katika ukusanyaji mapato na kubuni vyanzo vipya vya mapato, na wakati mwingine watumishi wenyewe kujipa uwakala kinyume na taratibu zinazomzuia mtumishi kufanya biashara na taasisi yake,” alisema.

Alisema hatua ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kutumia mawakala ni miongoni mwa mikakati ya kuboresha ukusanyaji mapato na pia kutoa muda mwingi zaidi kwa watumishi wa mamlaka hizo kushughulika na majukumu ya msingi ya Halmashauri na hasa utoaji wa huduma kwa wananchi na usimamizi wa miradi ya maendeleo.

“Pamoja na dhamira nzuri ya hatua hizo, tunayo mifano ya baadhi ya Halmashauri kama vile Nzega ambayo baadhi ya wahusika wameshinikiza wakitaka zabuni zote wapewe madiwani. Jambo hili halikubaliki na tena ni kinyume cha maadili ya utumishi,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza Halmashauri zote nchini kwamba kuanzia Julai Mosi, 2016 zihakikishe zinatumia mifumo ya kielektroniki katika kukusanya mapato, katika kulipa, kuweka na kutekeleza kikamilifu mikakati madhubuti ya kuboresha makusanyo iwe yanakusanywa na Halmashauri au na wakala.

Alisema Mamlaka za Serikali za Mitaa zina wajibu wa kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu mapato na matumizi ya Serikali pamoja na michango ya wananchi licha ya kuwa uzoefu unaonesha kuwa mamlaka hizo zina tatizo la kukaa na fedha kwa muda mrefu kabla ya kuzielekeza kwenye matumizi yaliyokusudiwa.

“Kuchelewesha kutoa fedha zilizotengwa kwa shughuli zilizopangwa ni kuchelewesha kufikisha huduma muhimu kwa wananchi. Napenda kuhimiza uzingatiaji wa utaratibu wa kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu mapato na matumizi ya fedha za Serikali katika ngazi zote ili kuongeza uwazi na uwajibikaji katika sekta ya umma,” aliongeza.

Mkutano huo wa tatu wa Bunge ulioanza Aprili 19, 2016 ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kujadili na kupitisha bajeti ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Bunge limeahirishwa hadi Septemba 6, mwaka huu litakapokutana tena mjini Dodoma.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S.L. P. 980,
DODOMA.
ALHAMISI, JUNI 30, 2016
Share:

Thursday 30 June 2016

MPYA:MKURUGENZI WA TBS ATUMBULIWA JIPU,PIA MENEJA WA FEDHA APIGWA CHINI


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage leo amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa shirika la Viwango Tanzania TBS Bwana Joseph B. Masikitiko ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Pia Waziri Mwijage ameagiza Bwana Emmanuel M. Ntelya Meneja wa Fedha, Mipango na Utawala wa TBS, asimamishwe kazi mara moja kwa kipindi chote ambacho uchunguzi utakuwa unaendelea. Aidha waziri amemteua Dkt Egid B. Mubofu, Mkuu wa Idara ya Kemia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania.

index.jpeg
Share:

KESI YA UCHOCHEZI:TUNDU LISSU APEWA DHAMANA,YAHAIRISHWA HADI AGOSTI 12 2016

 Image result for TUNDU LISSU
Mh Tundu Lissu apandishwa kizimbani Muda huu mahakama ya kisutu kwa zile tuhuma za maneno ya kuudhi, nunachokisubiri hapa ni maneno mengine yenye tafsiri nyingine kwa watu wengine atakayoitoa leo baada ya kupata dhamana panapo majaliwa. Ndio kwanza kumekucha mapambano yataendelea.
UPDATES:

Lissu anatetewa na wanasheria 17 wakiongozwa na John Mallya Peter Kibatala na timu nyingine toka makao makao makuu ya Chama.

Viongozi wote wa makao makuu wameshawasili,

Tunasubiri Hakimu tu aingie kwenye ukumbi wa mahakama...

UPDATES,

Tayari Hakimu anayesikiliza shauri ameshawasili, sasa ni utambulisho wa mawakili wa pande zote,

Kesi inaanza kusomwa,

Mwendesha mashitaka: Tundu Lisu anashitakiwa kwa makosa ya uchochezi, mnamo tarehe 28/06/2016 akiwa eneo la mahakama kwania ya kudhalau umma dhidi ya mamlaka yao walioyoichagua kihalali, alisema huyu dikteta uchwara lazima tumpinge kila kona"

Hakimu: Mshitakiwa, unakubali au unakataa?

Lissu: nakataa yote

Mwendesha mashitaka: Mh Hakimu ushahidi wa shauri hili umekamilika, tunaomba tarehe ya kuanza usikilizwa,

Hakimu: Mawakili wa utete mnalololote la kusema?

Wakili: Mheshimiwa kwamjibu wa kifungu cha sheria na.... Mshitakiwa kosa aliloshitakiwa linadhaminika, hapa tunao wadhamini na zaidi mshitakiwa ni mbunge na mwanasheria wa chama, hivyo anadhaminika, na zaidi mshitakiwa aliliripoti mwenyewe mbele ya polisi baada ya kuitwa tu kwa simu. Ni hayo tu mh

Mwendesha mashitaka: Mshitakiwa aliyembele yako, mnamo tarehe 28 mwenzi huuhuu alifikishwa mahakamani kwa kosa...... Aaah nimesahau sina nakala ya mashitaka, na wenzake watatu na kudhaminiwa. Hivyo akatenda kosa hili, huyu ana nidhamu mbovu, ameona kutenda kosa ni kawaida,

Hakimu: Kwanini unamhukumu kwa kosa ambalo mahakama hii haikumtia hatiani...na siajabu akitoka hapa atatenda kosa tena....

Wakili: Mh hakimu nashindwa kujua huyu wakili wa serikali anajipa kazi ya hukumu kwa kesi iliyopo mahakamani, nimshauri arudi kwenye kesi iliyopo mezani kwakuwa kesi ya nyuma ni tuhuma tu na sio hukumu inayoweza kutumika kama kielekezo hapa.

Mwanasheria: Mh huyu mtuhumiwa ni mzoefu wa kutenda makosa...... Watu wanaangua kicheko kwa kwa kwa...

Hakimu..... Wakili

Wakili: Kwanza Mh hakimu naomba ifahamike kwamba upande wa serikali wamekubali kuwa suala la dhamani liko wazi, hili liweke katika kumbukumbu... Haya anayoyaleta sasa huyu mwanasheria hayana msingi, kwani kwa mjibu wa vifungu vya sheria na.....na... Vinampa haki yakupata dhamana, izingatiwe kuwa katika dhamana ya kesi ya mwanzo hakukuwa na mashariti ya mtuhumiwa kutotoa maoni ama kutenda kosa nje ya lile.. Izingatiwe kuwa sababu za kukidhi dhamana tumeshazitoa

Hakimu: Mahakama inaamua kuwa mtuhumiwa apewe dhamana, wadhamini wa mtyhumiwa waje mbele...kuhakiki nyaraka zao

Mwanasheria: Anainuka... Mh Hakimu...

Hakimu anasema Jamhuri haijajenga hoja za kutosha kuzuia dhamana.Kwahiyo hakuna Pingamizi la Dhamana

Anawaita Wadhamini

Wamejitokeza Mbunge Susan Lyimo, Madiwani Humphrey Sambo na Rose Moshi Kwa ajili ya kudhamini

Amepewa dhamana.Asanteni
Share:

UFAFANUZI KUHUSU SIFA, VIGEZO NA MASHARTI YA KUPATA MKOPO 2016/2017

 Tokeo la picha la HESLB
Habari zenu;
Kwanza natumaini mu wazima wa afya,pia kwa upande wangu namshukuru Mungu nipo fresh kabisa.

Leo nimeamua kufafanua kwa kina vigezo na masharti ya Kupata mkopo mwaka wa masomo 2016/2017.

NANI ANAFAA KUPATA MKOPO?

mwanafunzi anaehitaji mkopo lazima akidhi vigezo vifuatavyo;
1.yatima aliepoteza mzazi/wazazi asiezidi miaka 30
2. Mwanafunzi mwenye disiability au mzazi wake hajiwezi asiezidi
     miaka 30 pia awe na cheti
    kinachotambuliwa na doctor wa wilaya.

3.Mwanafunzi anaetoka ktk familia maskini na awe anatambuliwa 
    na jamii.

4.Mwanafunzi ambae alikuwa akisomeshwa na wafadhili kutokana
   na kutokujiweza.


VIGEZO VITAKAVYOKUFANYA UPATE MKOPO 2016/2017.

1.Lazima uwe mtanzania
2.Lazima uombe mkopo thru online system.
3.Lazima uwe umechaguliwa na chuo chochote kikuu either thru TCU au NACTE.
4.lazima awe mwanafunzi aliefaulu na anaendelea na masomo(hii inawahusu waliopo chuoni)
5.Asiwe mwanafunzi anaedhaminiwa na mtu yeyote au organization.

SIFA ZA NYONGEZA ZITAKAZOKUFANYA UPATE MKOPO 2016/2017

1.Kwa form 6 ,Uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016-DIRECT
2.Kwa  diploma uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016-INDIRECT

KOZI KIPAUMBELE MWAKA 2016/2017

Zifuatazo ni kozi ambazo ni kipaumbele kwa mwaka wa masomo 2016/2017 ktk kupewa mkopo,kozi hizi zimegawanyika mara mbili Kuna PART A NA PART B

PART A
Priority courses  include: -

i)   Education (Science) and Education (Mathematics);
ii)  Health Sciences (Doctor of Medicine, Dental Surgery,
     Veterinary Medicine, Pharmacy, Nursing, Midwifery, BSc in
     Prosthetics and Orthotics, BSc in  Physiotherapy, BSc in Health
      Laboratory Sciences, BSc in Medical Laboratory Sciences and
     BSc in Radiotherapy Technology) and other Health Sciences;
iii)  All Civil and IrrigationEngineering;
iv)  All Petroleum and Gas Engineering;
 

NOTE:wanafunzi wote mtakaochaguliwa katika kozi hizi za PART A mtapewa mkopo wote bila kuangalia kigezo cha MWAKA ULIOMALIZA SHULE.

 PART B:
wanafunzi hawa wote wanasifa za kupata mkopo,hivyo basi watapewa mkopo kulingana na mahitaji yao waliyonayo tofauti na PART A ambapo wote watapata mkopo bila kuangalia kigezo chochote.

 

Priority courses cluster II include:

i) Engineering Programmes (Civil, Mechanical, Electrical, Mining, Mineral and Processing, Textile, Chemical and Processing, Agriculture, Food and Processing, Automobile, Industrial, Electrical and Electronics, Legal and Industrial Metrology, Maritime Transportation, Marine Engineering Technology, Electronics and Telecommunication, Computer, Computer Science Software, Information Systems and Network, Environmental, Municipal and Industrial Services, and Bio-Processing and Post-Harvest)


iii) Agricultural and Forestry Sciences Programmes (Agriculture, Agronomy, Horticulture, Agricultural Economics and Agribusiness,
Forestry, Aquaculture, Wildlife Management, Life Sciences, and Food Science and Technology)


iv) Animal Sciences and Production


v) Science Programmes (BSc General, BSc in/with Applied Zoology, Botanical, Chemistry, Physics, Biology, Microbiology, Molecular Biology and Biotechnology, Fisheries and Aquaculture, Aquatic Environmental Sciences and Conservation, Geology, Petroleum Geology, Petroleum Chemistry, Mathematics, Mathematics and Statistics, Environmental Science and Management, Environmental Health, Biotechnology and Laboratory, Wildlife and Conservation and Computer)
vi) Land Sciences Programmes (Architecture, Landscape and Architecture, Interior Design, Building Survey, Building Economics, Urban and Regional Planning, Land Management and Valuation, and Geospatial Sciences).


NOTE:wanafunzi wote mtakaochaguliwa kozi hizi ili upate mkopo lazima uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016


KWA KOZI ZOTE ZA ARTS NA BIASHARA AMBAZO HAZIJAORODHESWA HAPO JUU KTK PART A NA B 

Wanafunzi watakaochagua kozi hizi wanahesabiwa kama wapo katika kozi ambazo ni NON PRIORITY ,hivyo basi WATAPATA MKOPO TU endapo wote waliochagua kozi PRIORITY PART A na B kuwa wamepata.

KAMA UTACHAGULIWA OPEN UNIVERSITY

*wanafunzi wote waliochaguliwa open univeristy watapewa MKOPO wa BOOKS AND STATIONARY ONLY 

ENDAPO UTAPATA MKOPO,HUU NDIO MCHANGANUO

i. Meals and Accommodation charges
ii. Books and Stationery expenses
iii. Special Faculty Requirements expenses
iv. Field Practical Training expenses
v. Research expenses
vi. Tuition Fees


KUHUSU DIVISION I AND II AU UPPER SECOND CLASS KUPEWA MKOPO

Jamani kwa ambao hamuelewi swala hili ni kwamba,hii inawahusu wanafunzi watakaodahiliwa katika kozi za MEDICINE,VETERNARY MEDICINE NA LABORATORY ndio watapewa GRANT,means hawatarudisha pesa yoyote hivyo basi wakimaliza chuo inabidi waifanyie serikali kazi si chini ya miaka 5 kwanza.

JINSI YA KUOMBA MKOPO

A:LIPIA MPESA

1. To get MPESA Menu dial *150*00# (Piga *150*00#)

2. Choose option 4 for Pay by MPESA (Lipa kwa MPESA)
3. Choose option 3 for Choose Business (Chagua aina ya Biashara unayolipa)
4. Enter 8 for Education Services(Ingiza 8 kwa Huduma za Elimu)
5. Enter 2 for HESLB(Ingiza 2 kwa HESLB)
6. Enter 1 for Reference Number (Ingiza 1 kwa namba ya kumbukumbu)
7. Enter Account Number (Ingiza namba yako ya kumbukumbu), which is your formatted 15 character form 4 index number e.g. S0143.0012.2009
8. Enter the amount in Tshs to pay either 30,000 or 10,000 based on your application category
9. Enter your 4 digit PIN
10. Enter 1 to confirm
11. A confirmation Message will be displayed. N.B: Please keep this message privately

B:BONYEZA HAPA KUOMBA>>>>>>>>>>http://olas.heslb.go.tz/index.php/olas/olas/trans_add

MWISHO

Napenda kumaliza kwa kuwapa wito kwamba muombe mkopo kwani deadline ni 31 july 2016,Hivyo basi mtu asikutishe kuhusu kutopewa mkopo ,kikubwa muombe MUNGU akuongoze katika kujaza form,USIDANGANYE wala kusema uongo,kama baba ako ni MKUU WA MKOA,we andika ukweli.kwani hata mwaka hata miaka iliyopita kulikuwa na non priority course na mkopo walipata.

siku zote UKWELI UMUWEKA MTU FREE! 

NAKUTAKIA MAOMBI MEMA,ILA ENDAPO UTAHITAJI USHAURI /MSAADA NITAKUSAIDIA BE FREE!

NADHANI NIMEJIBU MASWALI YALIYOKUWA YANAWAUMIZA WENGI.

SHARE NA MWENZAKO

wako;
BLOGGER BOY
MASWAYETU BLOG TEAM!
Share:

Breaking news:Wabunge wa CHADEMA Joseph Mbilinyi, Kubenea na James Millya wasimamisha kuhudhuria vikao vya Bunge

Wanajamvi wasalaam!
Leo hii kamati ya haki,maadili na madaraka ya bunge leo inataraji kusoma taarifa ya shauri la Mbunge Joseph Mbilinyi baada ya kutoa ishara ya matusi bungeni na kunaswa na kamera za bunge!

Tunataraji Mbunge Mbilinyi kupewa adhabu kali ili iwe fundisho kwa vizazi na wabunge wa aina yake ndani na nje ya bunge!

Kwakuwa Joseph Mbilinyi alitoa ishara ya matusi kwa bunge na wabunge tulitegemea chama chake cha CHADEMA kingempa adhabu lakini wamenyamaza kimya!


Joseph Mbilinyi (Mb) amekiri kunyoosha kidole cha kati juu wakati akitoka bungeni baada ya kusika mbunge amemtusi mama yake. Mh. Mbilinyi amejitetea kuwa ni kweli alinyoosha kidole cha kati juu baada ya kumsikia mbunge wa CCM akimtusi mama yake mzazi hivyo kupata short temper na kujikuta akitenda kosa hilo.

Pia Joseph Mbilinyi amesema kuwa alinyoosha kidole cha kati juu kama kupinga kile kilichokuwa kinafanyika na mbunge huyo wa CCM, alipoulizwa na Kamati ya Maadili inayoongozwa na Mh. Mkuchika, Mh. Mbilinyi alisema kuwa kunyoosha kidole cha kati juu hakina maana ya moja kwa moja hivyo kwa uelewa wake yeye alikuwa anapinga kitendo cha mbunge wa CCM.

Kamati ya maadili imeridhika kuwa kitendo cha Joseph Mbilinyi (Mb) kuonesha kidole cha kati juu ni kosa na kutoheshimu mamlaka ya Spika wa bunge baada ya kupitia matoleo ya maana mbalimbali ya (Kuonesha kidole cha kati juu) nchi tofauti tofauti.

Maazimio ya Kamati Maadili
Bunge limeazimia kuwa mbunge wa Mbeya Mh. Joseph Osmond Mbilinyi asimamishwe kuhudhuria vikao 10 vya bunge la 11 kuanzia kikao cha leo Juni 30 mpaka hapo adhabu itakapokuwa imekamilika. Bunge limepitisha kwa kauli moja adhabu hiyo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger