INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
BARAZA LA MITIHANI LA
TANZANIA
|
Baadhi
ya wadau wamekuwa wakitaka kujua utaratibu uliotumika kukokotoa pointi za
madaraja katika matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) 2014. Hii
imetokana na kuona kuwa kuna baadhi ya masomo hayakujumuishwa katika kupata
idadi ya pointi kwa watahiniwa wa Tanzania Bara na wale wa Zanzibar.
Baraza
la Mitihani la Tanzania linapenda kuwajulisha wadau wote kuwa ukokotoaji wa
pointi za madaraja kwa watahiniwa wa Mtihani wa Kidato cha Sita huzingatia
masomo ya Tahasusi (Subject Combinations) aliyoyasoma mtahiniwa kama
ilivyobainishwa katika Kanuni za Mitihani (The Examinations Regulations) Toleo
la mwaka 2013 kifungu cha 23(1) kinachosomeka: