








Na Mwandishi wetu, Mtwara
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu)Joyce Ndalichako ametoa rai kwa wananchi wa Mtwara kuzichangamkia fursa za kibiashara zilizopo mkoani humo ili kukuza uchumi.
Ndalichako amesema hayo Mkoani Mtwara wakati akifungua maonesho ya biashara,Uwekezaji na fursa yanayofanyika katika viwanja vya mashujaa kuanzia Machi 19 hadi Machi 31,mwaka huu.
Amesema kuwa Mkoa huo unakuwa kwa kasi kiuchumi hivyo ni vyema kila mwananchi akatambua kuwa hiyo ni fursa katika kukuza uchumi kibiashara.
"Maonesho haya ya Biashara, Uwekezaji na Fursa ni maonesho ya Kwanza kufanyika Mkoani Mtwara yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza biashara na uwekezaji wa kisasa pamoja na fursa zilizopo katika sekta hiyo na Mkoa wa Mtwara kwa ujumla,"amesema Ndalichako.
Aidha Ndalichako alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi katika uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru utakaowashwa Aprili 1 mwaka huu katika kiwanja cha Nangwanda sijaona,Mkoani hapo.
Akizungumza na Vyombo ya habari Kaimu Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa wa Mtwara katika maonesho hayo Mha. Joseph Myaka amesema kuwa katika kutekeleza majukumu yao Shirika hilo limejikita katika kutoa elimu kwa wananchi kufahamu shirika hilo linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.
Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo pia TASAC imeshiriki maonesho hayo ili kuwapa elimu wananchi kuhusu fursa za biashara zilizopo katika Sekta ya Usafiri kwa njia ya Maji sambamba na elimu kuhusu Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa mazingira majini jukumu linalotekelezwa na Shirika hilo.
“TASAC tunashiriki maonesho haya ya Biashara Uwekezaji na Fursa mkoani Mtwara ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yanayotekezwa Kisheria kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba majini,
“Pia tunatoa elimu kwa wananchi wa Mtwara na wadau wa usafiri kwa njia ya maji katika jukumu letu la Udhibiti wa Safari kwa njia ya Maji na udhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira majini, wanaweza kufanya shughuli zao kwa usalama na kupata maendeleo na kuongeza pato la Taifa,"ameeleza Myaka.
Aidha ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.


Jisajili Meridianbet upate mizunguko 50 bure ya kucheza moja ya mchezo wa kasino ya mtandaoni utakaopenda! Kujisajili bonyeza hapa https://a.meridianbet.co.tz/c/RGCCr7
Jinsi ya kucheza mchezo huu wa kasino ya mtandaoni ni rahisi sana. Unachotakiwa kuwafanya ni kubofya kitufe chenye neno *Spin kuanzisha mzunguko ambapo Sloti ya Pumpkin Patch ina alama kuu mbili.
Alama ya Boga linalo cheza likiwa kwenye kifukuzia kunguru na alama ya Wild. Ikiwa alama ya Kunguru ikaangukia pembeni ya Boga, itasababisha boga hilo kusambaa kwenye kolamu ya sloti na kutengeneza alama ya ushindi yenye kukuletea malipo ya kiwango kikubwa iitwayo Complex Wild.
Kama Kindi (Squirrel) akiangukia pembeni ya Boga, basi Boga hilo litabadilika na kuwa alama ya ushindi ambayo itakutea malipo mara mbili ya mwanzo iitwayo Wild.
Ndio! Ni Meridianbet pekee ndio inayo kuhakishia ushindi kwa kukupa Bonasi, Odds kubwa na Promosheni za kipekee. Sio hivyo tu, Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet ya sloti ya Pumpkin Patch inakupa nafasi ya kushinda mizunguko kibao ya bure. Jiunge sasa kupitia https://www.meridianbet.co.tz na upate bonasi ya bure ya kuanzia.
Meneja wa Fedha na Utawala wa Taasisi ya WAJIBU, Jackson Mmary akizungumza mbele ya Wanahabari na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini wakati wa ufunguzi wa Mafunzo siku mbili yanayoendelea jijini Dodoma yaliyohusu namna ya kufanya uchambuzi wa masuala ya uwajibikaji na usimamizi wa fedha za umma,lengo mojawapo ikiwa ni kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.
Baadhi ya Wanahabari na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo wakati mafunzo yakiendelea.
Mmoja wa Wandishi wa habari akichangia jambo katika suala zima la kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.
Wakifuatilia baadhi ya vitabu vinavyohusu Ripoti ya uwajibikaji vinavyoandaliwa na Taasisi ya WAJIBU ikiwa ni sehemu ya kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.