Wednesday, 11 March 2026
Tuesday, 10 March 2026
Monday, 9 March 2026
DAWA ZA UHAKIKA ZA ULINZI WA MWILI NA NYUMBA 'ZINDIKO ZITO'

Je, unahisi kuna nguvu zisizoeleweka zinakufuata?
Je, nyumba yako inakosa amani au biashara haikui?
Dr. Sudai “Ng’wana Gama” anatoa dawa za kienyeji zenye nguvu za ulinzi wa mwili na nyumba, kupitia zindiko la asili lenye nguvu kubwa za kiroho.
Huduma zinazopatikana:
✔ Ulinzi wa mwili dhidi ya nguvu hasi
✔ Kufunga njia za wachawi na majambazi
✔ Kuweka kinga ya kiroho kwenye nyumba au biashara
✔ Kuondoa mikosi na mapepo
✔ Kuvutia mafanikio na baraka
📍 Huduma zinapatikana Maswa – Simiyu
📞 Wasiliana: +255 676 444 408 au 0624333380
WANAZUONI WAHIMIZA WAISLAMU KUTOA ZAKA KUPAMBANA NA UMASKINI
***
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga, amewahimiza Waislamu kutekeleza ipasavyo ibada ya Zaka ili kusaidia kupunguza umasikini katika jamii.
Akizungumza katika kongamano la wanazuoni wa Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Dar es Salaam Youth Centre (DYCC) jijini Dar es Salaam, Sheikh Ndauga alisema Zaka ni moja ya ibada muhimu inayolenga kuwasaidia watu wenye uhitaji katika jamii.
Alisema kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu, Zaka imewekwa mahsusi ili kuwainua watu wasiojiweza pamoja na kuimarisha mshikamano wa kijamii miongoni mwa waumini wa dini hiyo.
Sheikh Ndauga alieleza kuwa Waislamu wakitekeleza ibada hiyo kwa uaminifu na kwa kuzingatia maelekezo ya dini, inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu wengi.
Kwa upande wake, Sheikh Ally Zuberi akichangia mada katika kongamano hilo, alisema kumekuwepo na dhana potofu miongoni mwa baadhi ya Waislamu kuhusu walengwa wa Zaka.
Alisema baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Zaka inapaswa kutolewa kwa yatima pekee bila kuzingatia mafundisho sahihi ya Kiislamu kuhusu makundi yanayostahili kupewa Zaka.
Sheikh Zuberi alifafanua kuwa katika mafundisho ya Kiislamu, yatima hawakutajwa moja kwa moja miongoni mwa makundi ya wanaostahili kupewa Zaka isipokuwa pale wanapokuwa katika hali ya umasikini.
Wanazuoni hao walisisitiza umuhimu kwa Waislamu kujifunza na kuelewa kwa usahihi mafundisho ya dini kuhusu utoaji wa Zaka ili kuhakikisha ibada hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa.









































