Sunday, 1 March 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MACHI MOSI 2026


Magazeti
 
Share:

SHIRECU YAANDIKA HISTORIA MPYA YA USHIRIKA, MKUTANO MKUU WAPITISHA BAJETI ZAIDI YA SH BILIONI 2.8

 

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU

Meneja  wa Chama cha Ushirika SHIRECU Alphonce Makasi  akisoma  rasimu  ya  bajeti  kwenye mkutano Mkuu wa 31 

                   Chama Kikuu Cha Ushirika Mkoani Shinyanga (SHIRECU)  kimepitisha rasimu ya  bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 2.8  kwa mwaka wa fedha 2026/2027 huku ikijizatiti kuanza  kukopesheka  kwenye taasisi za kifedha.

Bajeti hiyo limepitishwa leo  April 28, 2026   baada ya Meneja  wa chama cha ushirika Shirecu Alphonce Makasi  kuwasomea  taarifa na rasimu  ya  bajeti  kwenye mkutano Mkuu wa 31  uliowakutanisha  wajumbe  202 kati ya wajumbe 214  waliokuwa wakitakiwa kuhudhuria kwenye mkutano huo.

Akisoma taarifa hiyo Meneja Makasi amesema wajumbe wakiridhia kupitishwa kwa bajeti zaidi ya shilingi bilioni 2.8  na kukopa kwenye taasisi za kifedha wataweza kutimiza adhima ya mipango ya kuendeleza biashara ya ununuzi wa mazao.

Pia mazao hayo yatakuwa Mchanganyiko,uanzishwaji na kufufua kiwanda kipya cha kukamua mafuta ya alizeti na kuendeleza duka la pembejeo.

“Awali taasisi za kifedha zilikataa kabisa kutukopesha kutokana na kuwepo kwa vikwazo vya deni kutoka benki ya Uwekezaji ya (TIB) lakini sasa tumeanza kuonyesha uaminifu wa kulipa na kupata ruhusa ya kuendelea kukopesheka kwenye taasisi za kifedha zozote nchini”amesema Makasi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Shirecu Naomi Chaba amesema  kuna vyama vya ushirika (Amco’s) 107 na wanachama 7413, ambapo mpango ulioanza mwaka 2025 hadi  Februari  2026  wamefanikiwa kununua mazao Mchanganyiko kama choroko na dengu,kugawa kompyuta mpakato 50 nakutoa mafunzo

"Pia ,tumefanikiwa kukarabati shule ya sekondari Buluba  na kusomesha wanafunzi 28  wa kidato cha tano kwa awamu,  kwa gharama ya shilingi Milioni 45."    pia  Chama kinatarajia kujenga kiwanda cha dengu kufanya biashara ya pamba ukarabati wa magala ,  amesema Chaba

Naye  Mrajis msaidizi  wa Ushirika mkoa wa Shinyanga Ibrahim  Kakozi amesema taasisi za kifedha   sasa zikae sawa kuwakopesha shirecu  huku akiwataka wajumbe waeleze yale ambayo wanataka yatekelezwe na yakikwama waihoji bodi  nakutoa ushauri zaidi nini kifanyike ili kuboresha zaidi.

"Niombe kila Amcos iripoti kila tatizo lililopo ili chama kiweze kufuatilia na kujua tatizo nini, kwani mkileta kwa barua itakuwa ni rahisi kufuatiliwa kwa haraka zaidi"amesema Kakozi.

        Mwakilishi wa COASCO Rodrick Kilemile 
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Lucy Mayenga akizungumza kwenye mkutano wa SHIRECU

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU
Wajumbe wa mkutano wa SHIRECU

Mkutano unaendelea

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU




Share:

Saturday, 28 February 2026

BARRICK YAPONGEZWA KWA KUWEKA MIUNDOMBINU YA KITUO CHA MICHEZO BUZWAGI

 
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi akitoa maelezo kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake walipotembelea kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa shirikisho hilo Wallace Karia na Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi.

**


Mgodi wa Barrick Buzwagi ambao uko katika mchakato wa kufungwa kwa kushirikiana na Serikali umepongezwa kwa kuweka miundombinu ya kituo cha michezo ambacho kitasaidia kukuza mchezo wa soka na michezo mingineyo nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia, alipoongoza wajumbe wa Mkutano Mkuu wa taifa wa shirikisho hilo kutembelea eneo hilo ambapo amesema miundombinu iliyopo inaridhisha.

Amesema miundombinu hiyo kuanzia nyumba za malazi kwa wanamichezo, viwanja vya michezo, usalama, pamoja na mazingira yake kwa ujumla ipo katika hali nzuri na inakidhi mahitaji ya kuanzishwa kwa kituo hicho.

“Natoa shukrani kwa kampuni ya Barrick na Serikali kwa kukubali ombi la kuanzishwa kituo cha michezo katika eneo la mgodi uliofungwa, tunafurahi kuona kituo kiko katika hali nzuri na kina viwango vikubwa kwa ajili ya kuhudumia wanamichezo, hii ni fursa muhimu kwa maendeleo ya michezo yetu”, amesema.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Taifa ya TFF, Azan Mufti, amesema kutengwa kwa eneo hilo kwa ajili ya wanamichezo kunadhihirisha ushirikiano mzuri uliopo kati ya sekta binafsi na wadau wa sekta ya michezo katika kufanikisha ajenda ya Serikali ya kukuza vipaji na kuendeleza michezo nchini.

Naye Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi, amesema kutengwa kwa eneo la kujengwa kituo cha michezo katika eneo hilo la mgodi uliofungwa kumezingatia dhamira ya kampuni ya kusaidia jamii sambamba na kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza vipaji na kuchochea maendeleo ya michezo nchini.
Share:

ROCK BLOCK YACHOCHEA MAPINDUZI YA UJENZI KILIMANJARO



- Ajira 122 zatengenezwa, Serikali yavuna Shilingi Milioni 400/-

📍Rombo, Februari 28, 2026

MGODI wa Rock Block uliopo Wilayani Rombo, mkoani Kilimanjaro, umeendelea kuwa kichocheo cha mageuzi katika Sekta ya Madini ya Ujenzi kwa kuzalisha ajira 122 na kuiingizia Serikali zaidi ya Shilingi milioni 400 katika kipindi cha miaka mitatu ya uendeshaji wake.

Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Abel Madaha, amesema hayo kupitia mahojiano maalum Wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro na kuongeza kuwa uchimbaji na uchongaji wa miamba kwa ajili ya kutengeneza matofali na bidhaa nyingine za ujenzi ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kusimamia na kuendeleza madini ya ujenzi ili kuongeza thamani na mapato ya taifa.

Amesema mgodi huo umeendelea kuchangia mapato ya Serikali kupitia ada, mrabaha na kodi mbalimbali zinazolipwa kwa taasisi ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Halmashauri ya Wilaya, hali inayochochea maendeleo ya kiuchumi katika eneo la Rombo na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla.

Mhandisi Madaha amefafanua kuwa miamba inayochimbwa katika eneo la Holili ilitokana na milipuko ya lava kutoka Mlima Kilimanjaro, jambo linalolifanya eneo hilo kuwa na malighafi adimu na ya kipekee inayopatikana Rombo pekee nchini.

Amesema bidhaa zinazozalishwa na mgodi huo ni pamoja na matofali ya miamba, paving blocks, vigae, coblestone, wall cladding, kerbstone zinazotumika katika utengenezaji wa kingo za barabara, pozolana — mchanga maalum mweusi unaotumika katika uzalishaji wa Saruji na kazi nyingine za ujenzi.

Kwa mujibu wa Mhandisi Madaha, matofali ya miamba yana uimara mara tatu zaidi ya matofali ya kawaida, hayaathiriwi na fangasi wala ukungu na hudumu kwa muda mrefu, jambo linaloyafanya kuwa chaguo sahihi kwa miradi ya kisasa ya ujenzi. 

Amewahimiza wawekezaji kujitokeza kuwekeza katika Sekta ya Madini ya ujenzi kwa kuwa ina fursa kubwa ya kukuza uchumi na ajira.

Naye Mkurugenzi wa Rock Block Limited, Fabian Woisso, amesema kampuni hiyo imeajiri wafanyakazi 72 wa kudumu na vibarua 50, hatua inayochangia kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana katika eneo hilo.

Amesema soko la bidhaa zao ni la ndani ya nchi, hususan katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Dodoma na Dar es Salaam, ambapo mahitaji ya vifaa vya ujenzi yamekuwa yakiongezeka kufuatia kukua kwa miradi ya miundombinu na makazi.

Aidha, Woisso amesema kampuni imewekeza katika miradi ya uwajibikaji kwa jamii (CSR), ikiwemo ujenzi wa barabara ya kilomita tisa kutoka Holili hadi Kidondoni, ujenzi wa darasa katika Shule ya Msingi Kidondoni na uchangiaji wa matofali kwa shule na vituo vya polisi.

Amehitimisha kwa kuwataka vijana kuchangamkia fursa zilizopo katika Sekta ya Madini ya Ujenzi, akisisitiza kuwa sekta hiyo ina uwezo wa kuongeza ajira, mapato ya taifa na kuimarisha maendeleo ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.












Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger