Friday, 26 December 2025

DC NKINDA AKUTANA NA VIJANA KAHAMA KUSHEREHEKEA SIKUKUU YA XMAS, ASIKILIZA KERO NA KUWAHIMIZA KULINDA AMANI

 



Na Neema Nkumbi, Kahama



MKUU wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Frank Nkinda, amekutana na makundi mbalimbali ya vijana wilayani humo katika hafla ya pamoja ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi, iliyolenga kuimarisha mshikamano kwa kula chakula cha pamoja sambamba na kusikiliza changamoto zinazowakabili vijana wa Kahama.

Akizungumza katika mkutano huo, Mchungaji wa Kanisa la Kalvari Lango la Ushindi, Mchungaji Flora Mwanri, amempongeza Mhe. Nkinda pamoja na Katibu Tawala wa Wilaya Glory Absalum kwa hatua ya kuwakutanisha wananchi wa Kahama bila kujali dini au itikadi za kisiasa kwani tukio hilo limeonesha mfano wa uongozi unaojali umoja na mshikamano wa jamii, akibainisha kuwa kiongozi huyo amewaunganisha wananchi wote kwa pamoja.

Kwa upande wake, kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo wilayani Kahama, Abas Omari, amewasilisha kero kadhaa ikiwemo ombi la kuwekwa taa za barabarani katika eneo la Shunu ili kuwawezesha wananchi kufanya shughuli za kibiashara nyakati za usiku, Pia ameeleza changamoto ya barabara ya kuelekea makaburini ya Shunu ambayo huwa haipitiki wakati wa mvua kutokana na tope, hali inayowalazimu baadhi ya wananchi, wakiwemo waliovaa kanzu, kuzikunja ili kupita.

Aidha, ameeleza kuwa barabara ya eneo la Msikiti wa Shunu Lugela imekatika kabisa, jambo linalowalazimu watoto wanaotoka upande wa pili kuzunguka milimani kufika Shule ya Msingi Shunu.

Akitoa nasaha zake, Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Kahama (OCD), Mtaju, amewataka wananchi na vijana kutokuwa na hofu ya kufikisha changamoto zao polisi wakati wowote amesema ofisi yake iko wazi muda wote na endapo changamoto itahitaji utatuzi wa ngazi za juu, atalifikisha kwa mamlaka husika.

Pia, amewahimiza vijana kutumia hekima katika kutatua changamoto, akisisitiza kuwa vijana ni nguvu kazi na tegemeo la taifa, hivyo wanapaswa kuepuka kujihusisha na shughuli zisizo halali zinazoweza kukatiza ndoto zao.

Akijibu hoja na kero zilizowasilishwa, Mhe. Nkinda amesema kuhusu barabara ya makaburini Shunu, amemtaka aliyetoa changamoto hiyo kufika ofisini kwake kufikia Jumatatu ili yeye na timu ya wataalamu wa wilaya waende eneo husika kujionea ukubwa wa tatizo na kulifanyia kazi kwa haraka.

Kutokana na vijana wengi kuwa na changamoto amesema wataandaa kongamano maalum la vijana, litakalowapa fursa ya kuwasilisha changamoto zao kwa kina ili zipatiwe ufumbuzi.

Mhe. Nkinda amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ina utaratibu wa kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi, iwe ni kwa makundi au mtu mmoja mmoja, akibainisha kuwa milango ya ofisi yake iko wazi kwa wananchi wote.

Katika hitimisho lake, Mkuu wa Wilaya aliwataka vijana wa Kahama kuendelea kuwa watulivu, kulinda amani na mshikamano, akisisitiza kuwa uongozi wa wilaya uko pamoja nao katika kuhakikisha maendeleo na ustawi wa wananchi wa Kahama yanaendelea kupatikana.

 
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 26,2025

Magazeti








Share:

Thursday, 25 December 2025

JESHI LA POLISI LAWASHUKURU WATANZANIA KWA KUDUMISHA AMANI SIKU YA KRISMASI



Na Mwandishi wetu,Dodoma

Jeshi la Polisi Tanzania limetoa shukrani kwa wananchi wote nchini kwa ushirikiano waliouonyesha katika kulinda na kudumisha amani kipindi chote cha Sikukuu ya Krismasi, iliyoadhimishwa 25 Desemba 2025.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Dodoma DCP David Misime
,amesema hatua hiyo imewezesha sherehe za mwaka huu kufanyika kwa utulivu na bila changamoto za kiusalama.

Amesema hali ya usalama imeendelea kuwa shwari katika maeneo yote ya nchi, huku wananchi wakiendelea kusherehekea sikukuu kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi bila wasiwasi wala hofu.

" Jeshi la Polisi limeeleza kuwa ushirikiano baina ya wananchi na vyombo vya ulinzi umekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha dhamira ya kulinda amani na kutengeneza mazingira mazuri ya kusherehekea, "amesema

Akitoa wito kwa umma, Msemaji wa Jeshi hilo amewataka Watanzania kuendelea kuilinda amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.

“Tunaendelea kuwasihi wananchi kudumisha amani kwani ndiyo inatupa fursa ya kusherehekea bila hofu tukiwa na marafiki na jamaa,” amesema.

Ameongeza kuwa bila amani hakuna shughuli za kijamii na kiuchumi zinazoendelea kwa ufanisi.

Kupitia taarifa hiyo amebainisha kuwa shughuli za kiuchumi, ikiwemo biashara, usafirishaji, huduma za kijamii na kazi za utumishi wa umma zinaendelea kama kawaida bila wasiwasi wowote.

Aidha Jeshi hilo linasisitiza wananchi kuendelea ushirikiano na utulivu huku likiahidi kuendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yo te na , kuhakikisha kila raia anabaki salama wakati wote.

Pia limewataka wananchi kuendelea kutoa taarifa mapema pale wanapotilia shaka viashiria vya uvunjifu wa amani, ili kuchukua hatua za haraka na kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza.






Share:

MHANDISI JAMES JUMBE AWAPA TABASAMU LA KRISMASI WATOTO YATIMA SHINYANGA

Na Mwandishi wetu- Malunde 1 blog

Mdau wa maendeleo, Mhandisi James Jumbe, amewasha mishumaa ya furaha na matumaini kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha Shinyanga Society Orphanage Centre baada ya kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi leo.

Msaada huo uliolenga kuongeza furaha kwa watoto hao katika Manispaa ya Shinyanga, umekabidhiwa kwa niaba yake na Ndg. Masuka Jumbe, ambaye amesisitiza umuhimu wa jamii kuyakumbuka na kuyajali makundi maalum, hasa katika msimu huu wa upendo na kutoa.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Masuka Jumbe ameeleza kuwa Mhandisi Jumbe ameona ni vyema kusherehekea siku hii ya leo kwa vitendo kwa kugusa maisha ya watoto hao.

"Katika kusherehekea Sikukuu hii ya Krismasi, Mhandisi ameona asiyaache nyuma makundi maalum. Tumefika hapa ili kusherehekea nao kwa pamoja, kwani ni muhimu kuwafariji na kuwapatia mahitaji yanayotakiwa," amesema Masuka Jumbe.

Aidha, Masuka ameongeza kuwa kitendo hicho si cha mara moja, bali ni mwendelezo wa moyo wa kutoa wa Mhandisi Jumbe kwa jamii ya Shinyanga.

 "Hii siyo mara ya kwanza; mwaka uliopita tulileta mahitaji, na safari hii pia siyo ya mwisho. Tutaendelea kutoa misaada na kuwatia moyo hawa watoto ili wajione kuwa ni sehemu ya jamii yetu", amesema.







Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DISEMBA 25,2025


Magazeti



















Share:

Wednesday, 24 December 2025

UZALENDO KWANZA: ALIYEKUWA MGOMBEA BAVICHA AWATAKA WATANZANIA KUPUUZA CHOKOCHOKO NA KULINDA AMANI YA TAIFA

Katika hali inayoonyesha kuimarika kwa umoja wa kitaifa na kupaa kwa sauti ya uzalendo, aliyekuwa mgombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Taifa, Masoud Mambo, ametoa mwongozo mzito kwa Watanzania akisisitiza kuwa amani ndiyo msingi mkuu wa haki na maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mambo ameweka wazi kuwa watu wote wanaohamasisha machafuko, vurugu, au migawanyiko ya kisiasa wanapaswa kukataliwa kwa nguvu zote. Amesema kuwa harakati zinazolenga kuvuruga utulivu wa nchi hazina maslahi na mustakabali wa maendeleo ya wananchi.

"Bila amani hakuna haki, na bila utulivu hakuna maendeleo. Tanzania imekuwa kimbilio la wengine kutokana na utulivu wetu, hivyo tusikubali historia hii tukufu ibadilishwe kwa matakwa ya kisiasa ya muda mfupi," alisisitiza Mambo.

Kauli ya Mambo inakuja wakati ambapo Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, iko katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuondoa kero za wananchi. Mifano ya miradi hiyo ni pamoja na:Uimarishaji wa Sekta ya Majini: Uingizaji wa meli mpya za mizigo katika Bandari ya Karema, Ziwa Tanganyika, hatua inayofungua fursa za ajira na biashara ya kimataifa.

Ujumbe huu unaendana na msimamo wa wadau wengine wa maendeleo na viongozi wa kijamii wanaokemea kuingiza uanaharakati uliopitiliza katika mambo yanayogusa ustawi wa nchi. Wananchi wamehimizwa kutambua kuwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika miradi kama ya TASAC huko Karema ni sehemu ya uzalendo unaopaswa kupewa kipaumbele kuliko maandamano.

Msimamo wa Wananchi: #NchiKwanza

Sehemu kubwa ya wananchi wameendelea kusisitiza msimamo wa #Hatuandamani, wakiamini kuwa njia sahihi ya kupata haki na maendeleo ni kupitia mazungumzo, amani, na kuunga mkono kazi zinazofanyika kwa vitendo. Wananchi wametakiwa kuwa na imani na Serikali kwani usambazaji wa taarifa sahihi unalinda jamii dhidi ya uvumi na hofu.

 Wito wa Masoud Mambo ni kengele ya kuamsha uzalendo kwa kila Mtanzania. Ni ukumbusho kuwa maendeleo ya kweli, kama yanayoshuhudiwa katika bandari zetu na miundombinu mingine, yanategemea utulivu wa Taifa na mshikamano wa dhati kati ya wananchi na viongozi wao.

Share:

KRISMASI NI SIKUKUU YA AMANI: MCHUNGAJI HANANJA NA WANANCHI WALAANI KUINGIZA UANAHARAKATI KWENYE IBADA

Kuelekea maadhimisho ya Sikukuu ya Krismasi, Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Richard Hananja, ametoa wito mzito kwa Watanzania akisisitiza kuwa sikukuu hii ni mahususi kwa ajili ya kumtukuza Mungu na kuhubiri amani, na si jukwaa la harakati za kisiasa.

Mchungaji Hananja ameeleza kuwa jaribio lolote la kuingiza uanaharakati au maandamano ndani ya misingi ya kidini wakati wa msimu huu wa sikukuu ni sawa na kufuru. Akirejea maandiko matakatifu, amekumbusha kuwa ujumbe wa kwanza wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo ulikuwa ni amani kwa wanadamu.

"Krismasi ni sikukuu ya kumtukuza Mungu. Malaika walitangaza amani, na Luka 2:12 inatupa ishara ya mwokozi aliyeleta amani duniani. Kugeuza madhabahu au siku hii kuwa sehemu ya harakati ni kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu," alisema Mchungaji Hananja.

Kauli hiyo ya Mchungaji imeungwa mkono na sehemu kubwa ya wananchi ambao wamejitokeza kusisitiza umuhimu wa utulivu. Kupitia mijadala mbalimbali, wananchi wameonya dhidi ya vikundi vinavyojaribu kuchochea machafuko au maandamano wakati wa msimu wa sikukuu.

Wananchi wamehimiza kuwa Tanzania ni nchi ya amani na mshikamano wa kitaifa ni tunu inayopaswa kulindwa kwa gharama yoyote.

Kutokana na msimamo huo  wananchi wamekuwa mtandaoni  wakionesha msimamo dhidi ya maandamano kwa kauli mbiu za #Hatuandamani  huku wengi wakisema  kuwa wanaochochea vurugu wana ajenda za siri ambazo hazina maslahi kwa Taifa.

Wananchi wametoa tahadhari kwa vijana kutokubali kutumiwa na watu "waliohongwa" ili kuharibu utulivu wa nchi.

Mchungaji Hananja amewataka Watanzania kusherehekea kwa furaha na utulivu majumbani mwao na katika nyumba za ibada, akisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo ya nchi yoyote.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger