Saturday, 22 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 23,2025




Magazeti
Share:

WITO KWA WATANZANIA KUTUMIA FIKRA CHANYA KULINDA AMANI

 

Viongozi, wachambuzi wa kijamii, na wadau wameungana kutoa wito kwa Watanzania wote kudumisha amani na umoja wa nchi, huku wakitahadharisha dhidi ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yanayolenga kuleta vurugu, hususan kuelekea mwezi wa Desemba. Kauli za wadau zinabainisha wazi kuwa, bila amani, hakuna mustakabali wa maendeleo, hasa kwa vijana.

Akizungumza kwa hisia, Bwana Shamte Mkali, alipongeza jitihada za uongozi wa nchi katika kuimarisha utulivu.

"Napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais ,Dkt. Samia Suluhu Hassan,kwani wakati ule hali ilipokuwa ngumu, wananchi wapo ndani wanasikilizia, Rais akasema neno, neno lile likatoa faraja nchi nzima. Kuanzia siku hiyo hali imekwenda vyema hadi leo," alisema Bwana Mkali, akisisitiza umuhimu wa kauli za kiongozi mkuu wa nchi.

Bwana Mkali pia alisisitiza umuhimu wa maridhiano kama msingi bora wa kutafuta amani na si vinginevyo.

 "Nchi hii ni yetu sote, ni lazima tuwe katika mshikamano... watu wakae wafanye mazungumzo, kwani shida ni nini? Taifa linaendelea na si kufanya fujo... vurugu hizo madhara sio kwa serikali tu, bali hata kwa wananchi na wale wanaoingia kuzifanya," alionya.

Wakati kukiwa na taarifa za uchochezi zikizunguka mitandaoni zikilenga kuleta vurugu Desemba 9, wadau wameonya umuhimu wa kuwa na fikra chanya na kukataa waziwazi wachochezi wanaojificha nyuma ya skrini.

Amani ni Tunu: "Amani tuliyonayo ni tunu na alama ya taifa letu maana mataifa mengine yamekosa hii sifa na wanakuja kwetu," alisema mdau mmoja katika mijadala ya kijamii, akitaka Watanzania kudumisha sifa hiyo.

Amani ni Ngao: Mdau mwingine alibainisha kuwa, "Amani ni ngao ya taifam,ikipotea kila mmoja huwa dhaifu. Vurugu huharibu utulivu wa taifa, biashara husimama, shule hufungwa na jamii hupoteza mwelekeo."

Katika mitandao imeoneshwa na taswira mbalimbali za uvunjifu wa amani ambao ndio adui mkubwa wa maendeleo ya vijana. Wakati amani ikivunjika na serikali inapambana na kuirejesha mara zote biashara na wawekezaji huondoka, ajira hupungua,elimu husimama: Shule hufungwa na vijana hukosa msingi wa kupata maarifa na badala ya kufanyakazi za maendeleo jamii huishi kwa wasiwasi.

"Hatuwezi kufurahia matunda ya maisha bila mbegu ya amani. Tupande mbegu hiyo leo," ni kauli inayotolewa kama ujumbe wa kuamsha Watanzania kuchukua hatua chanya.


Share:

4, 826 WAHITIMU MAFUNZO YA POLISI MOSHI, IGP AKIONYA KUHUSU UGAIDI NA DAWA ZA KULEVYA


Na Mwandishi wetu, Arusha
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Tanzania IGP Camillus Wambura amesema miongoni mwa changamoto watakazokutana nazo wahitimu wapya wa mafunzo ya awali ya Polisi ni pamoja na matishio ya ugaidi wa dunia, uwepo wa dawa za kulevya, usafirishaji haramu wa binadamu na uhamiaji haramu.

IGP Wambura amebainisha hayo Moshi Mkoani Kilimanjaro alipokuwa akifunga mafunzo ya awali ya Polisi kwa Kozi namba moja ya mwaka 2024/25, akisema kazi za Polisi zinahitaji ushirikiano wa dhati na wa karibu ili kuweza kuzuia na kupambana na changamoto hizo.

IGP Wambura pia akisisitiza kuhusu umuhimu wa usalama kama nyenzo ya maendeleo na ustawi wa Binadamu, ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kuweza kudhibiti uhalifu na wahalifu kote nchini Tanzania.

" Tusikubali pia kugawanyika kutokana na sababu yeyote ile iwe ya kisiasa, kidini au rasilimali. Tuendelee kutunza tunu yetu ya usalama na amani ya nchi yetu iliyodumu takribani kwa miongo mingi sasa. Tushirikiane popote kuhakikisha tunakuwa salama." Amesisitiza IGP Wambura.

Awali wakati wa maelezo yake, Mkuu wa Chuo hicho Ramadhan Mungi amesema askari wapya 4, 826 wakiwemo wanaume 3, 436 na wanawake 1, 390 wamehitimu mafunzo hayo, huku wanafunzi 217 wakiondolewa chuoni hapo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa nidhamu na uwezo mdogo katika kujifunza.


Share:

BODI YA TANAPA YATEMBELEA OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI


Bodi ya wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Novemba 21, 2025 imefanya ziara Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza namna Mamlaka hiyo inavyofanya kazi kama wadau muhimu katika masuala ya uchunguzi wa kisayansi kwa wanyamapori.

Wajumbe wa Bodi hiyo walipokelewa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, na kupewa maelezo kuhusu majukumu yanayofanywa na Mamlaka hiyo yenye jumla ya maabara 7 za vipimo, uchambuzi na utafiti.

Ziara hiyo iliambatana na kutembelea Maabara ya Vinasaba vya Wanyamapori “Wildlife DNA Laboratory” ambapo maabara hiyo ina jukumu la uchunguzi wa vinasaba “DNA” vya wanyamapori, kutoa ushahidi wa kisayansi kwa kesi za ujangili, kutoa mafunzo juu ya ukusanyaji na uhifadhi wa sampuli, kuhifadhi na kusaidia ushirikiano kati ya taasisi hiyo na wadau mbalimbali katika kukabiliana na ujangili.

Share:

TBS WATOA WITO USALAMA WA CHAKULA


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wananchi kuzingatia matumizi ya chakula salama pamoja na kuimarisha usafi katika maandalizi ya chakula ili kulinda afya ya mlaji na kupunguza madhara yanayotokana na vyakula visivyo salama.

Akizungumza leo Novemba 21, 2025 Jijini Dar es Salaam, Afisa Udhibiti Ubora Mkuu wa TBS, Bw. Moses Mbambe, amesema usalama wa chakula unategemea kwa kiasi kikubwa maandalizi yanayozingatia usafi na matumizi ya maji salama.

“Chakula salama ni kile kilichoandaliwa katika mazingira safi, kisichokuwa na bakteria au vimelea vinavyoweza kusababisha maradhi kwa mlaji,” amesema Mbambe.

Mbambe amesema matumizi ya maji machafu katika maandalizi ya chakula, pamoja na kupikia katika mazingira yasiyo safi au vyenye maandalizi hafifu, huathiri kwa kiasi kikubwa usalama wa chakula kinachotumika majumbani, kwenye migahawa na katika maeneo ya biashara.

Katika kuongeza usalama wa chakula, TBS imehimiza uhifadhi sahihi wa vyakula hususan nafaka kwa kuzihifadhi kwenye madumu yenye mfuniko ili kuzuia mashambulizi ya sumukuvu, ambayo yana madhara makubwa kiafya.

Vilevile, Mbambe amesisitiza umuhimu wa kutenganisha chakula kilichopikwa na kisichopikwa, pamoja na kupika vyakula kama nyama kwa muda sahihi ili kuua vimelea vya magonjwa.

TBS imeonya pia juu ya matumizi ya vyombo visivyo safi na usambazaji wa chakula kwenye vifungashio visivyo salama ikiwemo chupa zilizotumika awali kuhifadhia juisi, mafuta au bidhaa nyingine.

“Chakula kinapobaki lazima kipashwe angalau nyuzi joto 60°C ili kuua vimelea vinavyoweza kuleta athari kwa afya ya binadamu,” amesema Mbambe.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Tathmini ya Hatari za Chakula TBS, Bi. Immaculatha Justine, amesema vyakula vinavyotokana na mifugo ni muhimu kwa afya ya binadamu lakini vinaweza kuwa hatarishi endapo kanuni bora hazitazingatiwa kuanzia ufugaji, uchinjaji hadi usambazaji.

Ametaja vihatarishi vya kibailojia kama vile virusi vya homa ya manjano, bonde la ufa na minyoo kuwa miongoni mwa vimelea vinavyoweza kusababisha madhara ya kudumu kwa walaji.

Ameongeza kuwa matumizi holela ya dawa za mifugo bila kufuata ushauri wa wataalamu yanaweza kusababisha mabaki ya kemikali hatarishi kubaki katika mazao ya wanyama.

Kwa upande wa samaki wanaofugwa, Bi. Immaculatha ameainisha uwezekano wa kuwepo kwa mabaki ya madini tembo, ambayo husababisha athari za kiafya endapo yataliwa bila kudhibitiwa.

Bi. Immaculatha amehimiza kufuatwa kwa kanuni za usafi katika hatua zote za mnyororo wa thamani wa chakula cha mifugo, na amewataka wananchi kununua bidhaa za mifugo katika maeneo yaliyoidhinishwa na kukaguliwa na mamlaka husika.
Share:

Friday, 21 November 2025

WATANZANIA KATAENI KUVURUGWA DESEMBA 9 – AMANI NDIO RIZIKI YETU!

Katika hali inayoonyesha wasiwasi wa baadhi ya wananchi kuhusu mipango ya uvunjifu wa amani, inayosambazwa mitandaoni hasa ile inayoelezwa kulenga Desemba 9, wito umetolewa kwa Watanzania wote kusimama imara na kukataa ushawishi wa wale wanaotaka kuingiza taifa kwenye machafuko.

Wananchi wamesema amani ni msingi mkuu wa maisha yao ya kila siku, huku wakisisitiza kwamba hakuna kazi wala maendeleo yanayoweza kupatikana bila utulivu.

Amani Huratibu Kazi, Huzima Vurugu

Malugu Nkwabi  mkazi wa Bariadi ambaye ni Afisa Usafirishaji, alitoa msisitizo mkubwa kwa umuhimu wa amani katika ufanisi wake wa kazi.

"Ni lazima Watanzania tushikane kuhakikisha amani ndiyo kila kitu. Amani ndiyo kitu cha muhimu sana kwenye taifa. Maisha yote yanategemea kuwepo kwa amani. Ukiangalia kuanzia saa 12:00 jioni ukifika ni lazima nifanye kazi ili niweze kurudi nyumbani na maisha yangu kuendelea. Huwezi kufanya kazi pasipo kuwepo amani.."

Kauli hii inalenga moja kwa moja wale wanaofikiria kuandamana au kufanya vurugu, ikiwakumbusha kwamba uvunjifu wa amani kwanza unakwenda kuathiri shughuli zao za kujipatia riziki.

Kwa upande wake, Bwana Marco Mahega,kutoka mkoani Simiyu , alieleza masikitiko yake kwa jinsi Watanzania wanavyotaka kuichoma nchi yao na kukumbusha  nchi  zenye migogoro, akisisitiza kuwa amani inalinda hata viwango vya chini vya jamii.

"Sisi wenye familia zetu tukikuta nchi haina amani hatuna kwa kuikimbilia... Tunashukuru Mwenyezi Mungu, tumepewa amani. Naomba tuendelee kuihifadhi. Ukiona nchi haina amani maana yake haina amani hata kwenye familia yako. Tunaangalia nchi nyingi ambazo hazina amani wanatumia muda wao mwingi kuendelea kwenye migogoro. Sisi amani ndiyo kila kitu. Nawaomba Watanzania wenzangu tuendelee kudumisha amani."

Wakati wakikataa vurugu, wananchi pia wanatoa wito kwa viongozi kuwajibika. Bwana Paul Mboyi,alielekeza wito wake kwa viongozi waliochaguliwa hivi karibuni, akisisitiza umuhimu wa kufanya kazi badala ya kuendeleza siasa.

"Kila mtu atimize wajibu wake... Naomba viongozi ambao kwanza wamechaguliwa waanze kufanya yale mambo waliyoahidi.  Tusiishie tu kwenye siasa. Tunaomba viongozi kuwafuata wananchi, wasikae ofisini tu. Mkutano wa mkoa tulinde kwanza kauli ya amani. Kusiwe na makundi."

Wito wa Bwana Mboyi unaonesha kuwa wananchi wanataka kuona uongozi unajikita katika maendeleo, lakini wanakiri kwamba amani lazima ilindwe kwanza kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi.

Share:

TUYAKATAE MAKUNDI YASIYOFAA, YATATUGHARIMU




Na Mwandishi wetu, Dar

Wito umetolewa kwa Vijana kujiepusha na makundi yasiyofaa pamoja na kutofuata kila wanachoambiwa kwenye Mitandao ya Kijamii nchini katika kuhakikisha amani na utulivu unaendelea kuwepo.

Wito huo umetolewa na Mzee Ally Bomba Omar, Mkazi wa Tandika Mabatini Mkoani Dar Es Salaam, akieleza kuwa tangu kuzaliwa kwake Mwaka 1949 hakuwa kushuhudia vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

"Tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere tulikuwa tunaishi kwa amani, matatizo haya yaliyotokea hapa yamenishangaza na watu hawa sijui wametokea wapi. Sisi tusiokuwa nacho na tuliozoea kununua unga nusu kilo nusu kilo tuliteseka sana na bahati mbaya hata ukiwa na visenti unanunua wapi vitu? Maduka yote yalikuwa yamefungwa." Amesema Mzee Bomba.

Mzee huyo amefahamisha kuwa ana amini kwamba kila mmoja ana akili timamu, akisema makundi mabaya yatawapoteza, akisema maandamano yasiyo rasmi yanaleta matatizo mengi ikiwemo vifo, majeraha na uharibifu wa mali na maisha.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 21,2025

Magazeti
 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger