Monday, 17 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 17,2025



Magazeti












Share:

Sunday, 16 November 2025

MIRADI YA CSR YA MIGODI YAWANUFAISHA WANANCHI SIMIYU


📍Simiyu

Serikali imesema itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) inayotekelezwa na kampuni za uchimbaji madini nchini, ili kuhakikisha wananchi wanaoishi jirani na migodi wananufaika moja kwa moja na shughuli za uchimbaji madini.

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Simiyu, Mayigi Makolobela, alisema hayo hivi karibuni alipokagua utekelezaji wa miradi ya CSR inayofanywa na kampuni za uchimbaji madini katika mkoa huo, akibainisha kuwa miradi hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na miundombinu ya umeme.

“Serikali inatambua mchango mkubwa wa sekta ya madini katika kukuza uchumi wa nchi na kuboresha maisha ya wananchi. Ndiyo maana tunasisitiza kampuni zote za uchimbaji, zikiwemo zinazomilikiwa na wachimbaji wadogo, kutekeleza wajibu wao wa kijamii kupitia miradi ya CSR ili jamii inayoishi jirani na migodi inufaike moja kwa moja na rasilimali hizo,” alisema Makolobela.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya EMJ Mining iliyopo eneo la Dutwa mkoani Simiyu, Masanga Silanga, alisema kampuni hiyo inajihusisha na uchimbaji wa dhahabu kwa ushirikiano na wawekezaji kutoka China, jambo lililoongeza ufanisi na teknolojia katika shughuli zao za uchimbaji.

Alisema kampuni hiyo huzalisha wastani wa kilo 10 za dhahabu kwa mwezi endapo kuna upatikanaji mzuri wa mwamba wenye madini (mbale), ingawa wakati mwingine hukumbwa na changamoto ya upatikanaji wa mwamba kutokana na baadhi ya maeneo kuwa na mishororo midogo ya dhahabu (narrow vein).

Silanga alibainisha kuwa kampuni yake imetekeleza miradi kadhaa ya CSR ikiwemo kutoa madawati 50 na matofali 2,000 kwa Shule ya Msingi Dutwa, mashine za kuchapisha (printer) na nakala (photocopy) kwa taasisi za elimu, pamoja na mchango wa matofali 2,000 kwa Hospitali ya Nguno.

“Tayari tumewekeza zaidi ya Dola 50,000 katika miradi ya CSR, ikiwemo mradi wa kuvuta umeme kutoka Dutwa hadi vijiji vya jirani ambavyo awali havikuwa na huduma ya umeme,” alisema Silanga.

Naye Meneja wa Mgodi huo, Noah Wang, alisema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo kwa sasa ni upungufu wa mwamba wenye madini (mbale), hali inayosababisha baadhi ya mitambo kusimama na kupunguza uzalishaji.

“Mitambo yetu ina uwezo wa kuchakata hadi tani 500 za mwamba kwa siku, lakini kwa sasa hatupati kiwango hicho, jambo linalolazimisha baadhi ya mitambo kuzimwa mara kwa mara. Kwa sasa shaft moja pekee ndiyo inaendelea na kazi, hivyo uzalishaji umeshuka kwa kiasi kikubwa,” alisema Wang.

Aliongeza kuwa kampuni hiyo imeajiri jumla ya wafanyakazi 48, wakiwemo 30 wazawa na 18 raia wa China, wanaofanya kazi kwa mfumo wa kupokezana (shift system).

Share:

Saturday, 15 November 2025

WITO WA KITAIFA WA AMANI – KUTOKA ARUSHA HADI SONGWE, WATANZANIA WASEMA ‘SOMO TUMEJIFUNZA’


Wiki chache baada ya ghasia na vurugu zilizofuatana na uchaguzi, Watanzania kutoka maeneo mbalimbali wamejitokeza kwa umoja kutoa tamko la dhati la kuahidi kuilinda amani, wakibainisha kuwa matukio hayo yaliwaacha na somo la maumivu.

Kauli za wananchi zilizosambaa mitandaoni zinaonyesha mwafaka wa kitaifa unaopita mipaka ya kijiografia: "Kutoka Arusha hadi Mbeya, kutoka Mwanza hadi Songwe, Watanzania wanasema kwa sauti moja: Amani ndiyo njia, na sisi ndio walinzi wake."

Miongoni mwa walioeleza athari za vurugu hizo ni Bi. Witness Rabson Nkini, mkazi wa Mvuti, Dar es Salaam, ambaye biashara yake iliathirika moja kwa moja. Witness alieleza jinsi uchafuzi wa amani ulivyosimamisha maisha yao na kuwalazimu kutumia fedha nyingi katika kununua vyakula.

"Kipindi cha uchaguzi kulikuwa na mtafaruku, kulikuwa na maandamano, ikatupelekea kufunga ofisi zetu. Kama mimi hapa nafanya saluni, tumekosa fedha. Tukikosa fedha tukalamzika kutumia fedha nyingi kununua vyakula," alieleza Witness.

Alisisitiza kuwa matukio hayo yamepelekea kupungua kwa amani si tu kwa watu wazima, bali pia kwa watoto wao, akitoa wito: "Tunaomba tuwe na amani na upendo. Wengine tunawatoto wanakosa amani."

Ushuhuda wa Witness na wengine unaakisi hali halisi ya Watanzania wengi ambao sasa wanaeleza kwamba, "Tumepitia maumivu, tumejifunza somo. Leo tunachagua amani, kwa ajili ya familia zetu, kazi zetu na mustakabali wa Tanzania."

Kauli hizi zimeungwa mkono na jumbe mbalimbali zinazosisitiza:

"Watanzania hili Ni somo tumejifunza tuilinde amani. Amani ni tunu yetu."

"Uchafuzi wa amani hauna faida. Tuungane kuilinda nchi yetu."

"Maandamano ni biashara, wachache inawalipa na kuwanufaisha zaidi huku wengi tukiumia kwa kupoteza kazi, biashara zetu na madhara mengine mengi."

Wananchi wengi wameahidi kuendelea kuienzi amani kama msingi wa maendeleo, huku wakihimiza: "Kesho bora ya Tanzania itajengwa kwa kuendelea kuenzi amani, kuvumiliana na kushirikiana."

Katika kuimarisha azma ya kudumu ya amani, kuna wito wa dhati wa kuwaepuka wale wote wanaoweza kuvuruga utulivu wa taifa. Ujumbe ulioenea unasema: "Tusitoe nafasi kwa watovu wa amani nchini mwetu kuja kuvuruga amani, upendo na mshikamano tulionao."

Wengi wamekubaliana kuwa "Amani si tukio, ni maamuzi ya kila siku. Tuanze leo, kwa maneno yetu, matendo yetu, na mioyo yetu."  

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 15,2025



Magazeti



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger