Saturday, 15 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 15,2025



Magazeti



Share:

Friday, 14 November 2025

SAUTI YA WAZEE : AMANI HUANZIA MOYONI, SIYO SERIKALINI

WACHAMBUZI wa masuala ya kisiasa na jamii wamesema mchango wa wazee katika kudumisha utulivu baada ya taharuki za kisiasa ni wa muhimu na wa kutilia mkazo.

Mwandishi mmoja wa makala ya kijamii aliandika, 'Sauti yao ni ngome ya busara na heshima ambayo inaweza kubadilisha jamii kuliko mamlaka yoyote.' Kauli hii inaonyesha umuhimu wa kuwasikiliza na kuwawezesha wazee kushiriki kikamilifu katika malezi ya kijamii.

Aidha inafaa ikumbukwe kuwa kila jamii imara imejengwa juu ya msingi wa hekima, na hekima hiyo mara nyingi hutoka kwa wazee. Wazee ni hazina ya taifa, walinzi wa maadili, na walimu wa vizazi vipya. Tanzania, taifa linalojivunia mila za heshima na utu, lina wajibu wa kuendelea kuthamini sauti zao, hasa katika kipindi hiki cha kujenga upya amani na maridhiano baada ya changamoto za kisiasa.

Wazee wanahimizwa kukaa na vijana, wazungumze nao kwa upendo na subira kuhusu thamani ya kulinda mali za umma na binafsi.

"Wazee wa taifa hili wametumia maisha yao kulinda amani, wakijitolea katika vita, kazi, na ujenzi wa uchumi. Ni haki yetu kusikiliza ushauri wao, kwa sababu wameona mengi kuliko sisi," inasema sehemu ya makala hiyo.

" Amani haianzi serikalini, bali inaanzia mioyoni mwa watu. Kama wazazi na walezi, tuna jukumu la kujenga kizazi kinachoamini katika busara badala ya hasira, mazungumzo badala ya makabiliano, na heshima badala ya chuki" anasema Franklin Leonard wa Morogoro.

Mama Mary Nyerere, mwalimu mstaafu, anaeleza: “Elimu ya amani inaanzia nyumbani. Mtoto akiona wazazi wanaheshimiana, atajifunza heshima. Akiona upendo, atajifunza upendo.”

Wazee wanapaswa kuwakumbusha vijana kuwa mali ya umma kama barabara, shule, hospitali, na ofisi za Serikali si mali ya chama, bali ni mali ya wananchi wote. Uharibifu wake ni sawa na kuchoma nyumba ya familia nzima.

Kwa mujibu wa wataalamu wa jamii, mabadiliko ya kimaadili yanapaswa kuanza katika familia. Mtoto anayejifunza thamani ya maisha ya wengine hawezi kushiriki katika kuharibu mali za umma au binafsi.

Katika tamaduni nyingi za Kiafrika, wazee wamekuwa walinzi wa mila na desturi, wapatanishi, na washauri wa uongozi. Heshima kwa wazee ni heshima kwa taifa. Tukianza kuwapuuza, tunapoteza dira ya maadili.

Leo, wazee wanahimizwa kutumia nafasi zao za kijamii kuwa walimu wa maadili, wakiwakumbusha vijana kwamba: “Kuhifadhi mali za umma na binafsi si kazi ya Serikali pekee, ni jukumu la kimaadili linalotufanya sisi wote kuwa walinzi wa maendeleo yetu.”

mwisho

Share:

TULILINDWA NA MUNGU, SASA TUISHI KWA KUWAJIBIKA, TUSIKUBALI TENA KUCHOCHEWA

Kwa viongozi wa dini na wananchi wengi, ukweli kwamba amani ilirejea haraka si jambo la kawaida. Ni ushahidi wa wazi kwamba Mungu amelilinda taifa hili, na sasa anatuita tuishi kwa busara, toba, na uwajibikaji.

Katika kipindi cha taharuki na majeraha ya kitaifa yaliyofuata baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, Watanzania walishuhudia vurugu, uharibifu, na hofu iliyotishia misingi ya utulivu tuliyoizoea kwa miongo mingi. Hata hivyo, pamoja na maumivu hayo, taifa letu lilipita salama. Amani ilirejea, shughuli za kawaida zilianza, na matumaini yakachipuka upya.

Askofu Nyaisonga alizungumza kwa uzito mkubwa, akiwakumbusha Watanzania kuwa taifa letu limesimama kwa sababu msingi wake ni imara: amani, ambayo ni zawadi kutoka kwa Mungu.

"Tanzania imepitia vipindi vigumu lakini Mungu ametuvusha. Sasa ni wakati wa kuacha chuki na kuchagua maelewano," alisema Askofu Nyaisonga. Kauli hii imekuwa mwanga wa faraja kwa mamilioni ya wananchi waliotafuta majibu baada ya machafuko.

Kanisa la KKKT (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) kupitia viongozi wake lilionyesha masikitiko makubwa kuhusu uharibifu wa mali uliotokea. Walieleza wazi kwamba kuchoma na kuharibu ofisi za umma, na kupora mali za watu hakustahili kuungwa mkono chini ya sababu yoyote. Walisisitiza kuwa uharibifu huo si tu kosa la kisheria, bali ni pigo kwa utakatifu wa jamii inayomcha Mungu na kuheshimu maisha ya watu.

Viongozi wa KKKT waliwataka wanaohusika kutafakari na kutubu, wakikumbusha kwamba haki haitafutwi kwa kuumiza wengine au kuchoma mali ya umma.

Maombi, Msamaha na Utiifu

Katika ibada na sala mbalimbali za kitaifa zilizofanyika baada ya vurugu, viongozi wa dini kutoka madhehebu yote walisisitiza kwamba maridhiano, msamaha na maombi ndiyo yatakayoijenga Tanzania upya.

Waliwaomba wananchi kuchagua upendo badala ya hasira, busara badala ya jazba, na ukweli badala ya uzushi. Wakiwakumbusha vijana kuwa kila hatua ya vurugu inaumiza familia zisizo na hatia, inapunguza ajira, na inafanya taifa kupoteza heshima kimataifa.

Askofu mmoja wa KKKT alisisitiza kwamba amani inahitaji utiifu kwa sheria: “Amani haiishi mahali ambapo watu hawaheshimu sheria. Sheria ndiyo nguzo ya ulinzi wa maisha yetu.”

Jukumu la Kila Kaya

Wale waliogusa uharibifu wa miundombinu, mali, au maisha wamebeba majeraha ambayo yatahitaji muda kupona. Katika kaya na familia mbalimbali, wazazi kwa sasa wanazungumza na vijana kuhusu umuhimu wa kutotumiwa na uchochezi wa mitandaoni, wakikumbusha kuwa uharibifu wa mali ya umma ni sawa na kuharibu maisha ya watu wa kawaida na mustakabali wa taifa.

Katika kipindi hiki cha uponyaji, wajibu wa kila raia ni mkubwa kuliko hapo awali. Amani si jukumu la Serikali pekee. Ni kazi ya kila mmoja. Kila Kanisa, kila Msikiti, kila nyumba ya ibada, na kila kaya inapaswa kuwa sehemu ya maombi na mazungumzo ya kujenga taifa lenye upendo na uthabiti.

Ujumbe wa pamoja unagusa mioyo ya wengi: Tulilindwa na Mungu, sasa tuishi kwa kuwajibika. Tusikubali tena kuchochewa, kutumiwa, au kurubuniwa na hisia za hasira na chuki.

Tuchague amani, tuchague ukweli, tuchague Tanzania. Amani ni urithi, uwajibikaji ni wajibu, na Tanzania ni nyumba yetu sote. Tuihifadhi, tuijenge, na tuirithishe kwa vizazi vijavyo.
Share:

Thursday, 13 November 2025

WITO WA AMANI NA UMOJA: VIONGOZI WA DINI WAIMARISHA MSINGI WA TAIFA

Kufuatia matukio ya vurugu na misukosuko ya kisiasa iliyolikumba taifa mwishoni mwa mwaka 2025, viongozi wa dini nchini Tanzania wameendelea kuwa chachu na sauti ya busara na faraja. 

Wamehimiza wananchi wote kurejea katika misingi imara ya imani, heshima, na maelewano ili kulinda na kuendeleza amani na umoja uliokuwa nguzo ya taifa kwa zaidi ya miongo sita.

Askofu Israel Maasa, Katibu wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), amesisitiza umuhimu wa kuitekeleza kwa vitendo falsafa ya 4R iliyoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya Maridhiano (Reconciliation),Ustahimilivu (Resilience),Mageuzi (Reforms) na Kujenga Upya (Rebuilding).

Askofu Maasa ameeleza kuwa falsafa hii ni tiba muafaka kwa majeraha ya kisiasa na kijamii yaliyotokana na uchaguzi. “Si lazima tukubaliane katika kila jambo, lakini tunaweza kukubaliana katika kutokukubaliana kwa amani. Tunahitaji diplomasia zaidi,” aliongeza Askofu Maasa.

Kwa waamini wa dini tofauti, kauli hii imekuwa mwanga wa matumaini. Hekima ya kuketi meza moja, kusikilizana, na kusamehe inajenga imani ya kitaifa.

Viongozi wa dini wanaamini kwamba maombi na msamaha ni dawa sahihi ya kuponya majeraha ya mioyo ambayo siasa peke yake haiwezi kuyaponya.

Akisisitiza umuhimu wa amani, mwanasiasa mkongwe kutoka mkoani Arusha, Modesti Meikoki, alieleza kuwa hakuna sababu ya kuruhusu maandamano au hasira za kisiasa kugawanya taifa. Alisema, “Matukio yaliyotokea yameleta taharuki kwa wapenda amani duniani. Tuna wajibu wa kurejea katika maadili ya Kikristo na Kiislamu yanayohimiza amani, mshikamano, na utii kwa sheria.”

Viongozi wa dini wametoa wito kwa wananchi kurejelea utu na busara katika maamuzi yao ya kila siku. Wamehimiza kuepuka chuki, kulinda lugha yetu mtandaoni, na kuchagua mazungumzo badala ya mabishano. Katika maombi ya kitaifa yaliyofanyika Dodoma mwezi Novemba 2025, kiongozi mmoja wa dini aliwakumbusha waumini kwamba amani haiwezi kujengwa kwa matusi, bali kwa huruma na heshima.

Kama viongozi wa dini wanavyokumbusha, tuendelee kuomba na kufanya kazi kwa amani. Tuendelee kujenga madaraja ya maelewano badala ya kuta za mabishano. Kwa upendo, kwa huruma, na kwa imani, Tanzania itaendelea kusimama kama mfano wa amani barani Afrika.
Share:

Wednesday, 12 November 2025

WEWE NI NGUVU YANGU WIMBO KUTOKA KWA GRACE OF AFRICA



Grace of Africa rasmi wameachia wimbo mpya wa injili,
“Wewe ni Nguvu Yangu (You’re My Strength)”, unaohamasisha imani, tumaini, na nguvu ya ndani.

Wimbo huu, uliotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya AI, unachanganya sauti za kisasa na ujumbe wa kiroho, ukikumbusha wasikilizaji kwamba nguvu na ujasiri hutoka kwa Mungu.

“Nguvu Yangu’ si wimbo tu — ni ujumbe wa shukrani na uvumilivu,”

“Wewe ni Nguvu Yangu (You’re My Strength)” sasa inapatikana kwenye majukwaa yote makuu ya muziki mtandaoni.
Share:

WANANCHI WAHIMIZA UVUMILIVU, MCHAKATO WA MARIDHIANO YA KITAIFA


Na mwandishi wetu, Dar

Kama ilivyoahidiwa na Rais wa Tanzania kwamba moja ya ahadi zake ni pamoja na kutafuta maridhiano ya Kitaifa na kuanzisha mchakato wa Katiba mpya ili kulileta Taifa pamoja na kushughulikia changamoto za wadau mbalimbali, wananchi wa Mkoa wa Dar Es Salaam wamewashauri makundi mbalimbali ya kijamii kuacha mihemko na kuisikiliza serikali, huku serikali pia ikitakiwa kuusikiliza upande wa wananchi kujua kile wanachokitaka.

Kauli za wananchi zinakuja siku chache pia mara baada ya Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kusisitiza dhamira hiyo ya Rais Samia kuhusu maridhiano ya Kitaifa ili kusikiliza wananchi na kuendelea kuifanya Tanzania kuwa yenye amani na utulivu.

"Ni dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha tunaanzisha mazungumzo ya maridhiano ili kuhakikisha hata hao wachache wanapata nafasi ya kusikilizwa ili kuwa na taifa lenye amani na umoja na kuendelea kuwa mfano wa utulivu katika Afrika na dunia.”Alisema Dkt. Nchimbi kwenye Mkutano wa Kimataifa uliofanyika siku mbili zilizopita.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wanaoishi Chanika, Jijini Dar Es salaam wamesisitiza umuhimu wa maridhiano hayo ili kujenga jamii yenye amani na ustawi, wakirejea athari kubwa zilizotokea wakati wa ghasia na vurugu za Oktova 29, 2025.

Wamelaani pia utafutaji wa haki kwa kuhamasisha na kutenda vitendo vyenye kuhatarisha amani ya Tanzania, wito zaidi ukitolewa kwa vijana kuachana na mihemko na ushawishi wa kufanya vurugu na badala yake kupendelea zaidi njia ya mazungumzo na masikilizano katika kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maeneo mbalimbali.

Share:

Tuesday, 11 November 2025

AMANI NDIYO MTAJI: FAMILIA ZALIA NA MADENI KUFUATIA TAHARUKI


Hasara kubwa ya kiuchumi imeripotiwa kufuatia vurugu, huku wananchi wa hali ya chini wakikosa hata riziki ya siku na kuingia kwenye madeni, jambo linaloonesha wazi umuhimu wa amani kama msingi wa maisha. Kipindi cha Lockdown kimeacha maumivu ya muda mrefu.

kijana mmoja ambaye hakupoenda kutaja jina lake anaeleza athari za moja kwa moja za kukosekana kwa amani na maandalizi hafifu ya kukabiliana na majanga ambayo yanatokea kwa kushtukiza.

"Ile lockdown imetusababishia madeni manake hatukuwa na chochote, kwanza tulikuwa hatuitarajii kutokea yale yaliyotokea. Pili, tunakuwaga hatuna akiba familia zetu nyingi. Wengine ndio tumetoka jana; sio siku tano, wengine tuna siku sita na wengine saba. Tudumishe amani, amani ndio kila kitu."

Faizat Peter, mkazi na mfanyabiashara wa Mbagala, anaeleza athari za kijamii na kiuchumi: "Kiufupi maandamano yalituathiri kiuchumi na kifamilia kiujumla. Maisha ya Mtanzania asilimia kubwa ni utoke ili upate kuishi. Watu wamepata taabu, familia zimeathirika, kulingana na kipato imekuwa taabu sana."

Mtaalamu wa Uchumi wa Familia  anasema, "Familia nyingi za Watanzania huishi kwa mapato ya siku. Kukaa ndani kwa siku tano hadi saba kunamaanisha wamepoteza mapato yote. Tunapaswa kujifunza kutokana na hili, tutaweza kudumisha utulivu wa kiuchumi kwa kuwa katika utaratibu, tusigeuze utaratibu" alisema.
Share:

TUWAKATAE WACHOCHEZI, GHASIA, VURUGU VINATURUDISHA NYUMA KIMAENDELEO



Na Mwandishi wetu, Dar

Mjasiriamali Kijana Bw. Peter Shaaban Gerald, Mkazi wa Kimara Dar Es Salaam amewasihi Vijana wenzake kujiepusha na uratibu na ufanyaji wa matukio ya ghasia na vurugu, yenye kuhatarisha amani ya Tanzania kwani athari za Kijamii na kiuchumi ni nyingi kutokana na mtindo wa maisha na namna ya kujipatia Kipato kwa Watanzania wengi hususan Vijana.

Ameyaeleza hayo wakati akizungumzia uzoefu alioupata kwa takribani siku saba zilizopita, zikitokana na uharibifu na ghasia za Oktoba 29, 2025 kwenye Majiji na Miji ya Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Songwe, akisema uchumi wake umetetereka pakubwa kutokana na kukosa kipato kulingana na kazi yake ya kumtaka kuwa barabarani kila wakati ili kuwafuata na kuwatafuta wateja.

"Sisi tumezoea kutembea barabarani kujitafutia chochote, na unajua maisha ya Vijana ni gheto (Vyumba vya kuishi) sasa si sahihi kuandamana kwasababu sisi Vijana wengi tuliumia, wengine walizipoteza pia familia zao na tumezoea Tanzania ni nchi ya amani hivyo ni muhimu kuilinda amani yetu sisi kama Vijana." Amesisitiza Bw. Peter.

Peter amekumbusha pia wajibu wa Vijana katika kulinda amani ya Tanzania kwa msingi wa kuliandaa Taifa la kesho kutokana na nguvu kazi yao, akiishukuru serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama kwa kurejesha amani katika maeneo yote nchini na hivyo kuruhusu shughuli za kiuchumi na kijamii kuweza kuendelea kama kawaida.



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 11,2025



Magazeti

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger