Sunday, 9 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 9,2025


Magazeti
Share:

Saturday, 8 November 2025

MKUTANO WA SADC WAMPONGEZA RAIS DKT. SAMIA KWA USHINDI KATIKA UCHAGUZI MKUU 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imechukua hatua za kurejesha utengamano katika nchi na kuhakikisha wananchi wanaishi katika utawala wa sheria.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC), uliyofanyika kwa njia ya mtandao, akiwa mkoani Dodoma.

Amesema dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha mchakato wa mazungumzo ya maridhiano unafanikiwa ili kuwa na Taifa lenye amani na umoja na kuendelea kuwa mfano wa utulivu katika Afrika na Dunia kwa ujumla.

Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema Tanzania ni salama na tulivu na ipo tayari kuendelea kupokea wageni kutoka duniani kote kwa manufaa ya nchi zote. 

Aidha, Makamu wa Rais, amewashukuru viongozi wa SADC walioshiriki uapisho wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wote waliotoa pongezi za dhati. Amesema jitihada zote zitatumika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo na amani kuendelezwa. 

Mkutano huo umempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi aliyoupata na uchaguzi wenye mafanikio.

Mkutano huo ulilenga kujadili kujiondoa kwa nchi ya Madagascar kama nchi Mwenyekiti wa SADC, ambapo nchi ya Afrika Kusini imependekezwa kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha mpito mpaka kufikia mwezi Agosti 2026.

Mkutano huo umekubaliana kuendelea kutumia kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa SADC uliyofanyika nchini Madagascar ambayo ni “Kuimarisha Viwanda, Mapinduzi ya Kilimo, Mabadiliko ya Nishati kwa SADC yenye Uhimilivu”


Imetolewa na 
Ofisi ya Makamu wa Rais
08 Novemba 2025
Dodoma.






Share:

MALI ZA UMMA NA BINAFSI ZIMECHOMWA, HAYAKUWA MAANDAMANO—ZILIKUWA VURUGU




Na Mwandishi wetu, DAR

Samwel Salum, mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam, amelaani vikali matukio ya Oktoba 29 akieleza kuwa hayakuwa maandamano halali bali vurugu zilizoleta uharibifu mkubwa wa mali za umma na watu binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Samwel amesema vitendo hivyo havikuwa na lengo la kutoa ujumbe kwa Serikali bali vilichochewa na nia ovu ya kuharibu, kujeruhi, na kuathiri uchumi wa Taifa.

“Maandamano ya kweli huwa na hoja au ujumbe unaoeleweka kwa mamlaka husika, lakini haya ya Oktoba 29 yalikuwa vurugu tupu. Watu wamepoteza mali zao, maduka yamechomwa, na shughuli za kiuchumi zimesimama,” amesema Samwel kwa masikitiko.

Ameongeza kuwa vitendo vya namna hiyo vinapaswa kulaaniwa na Watanzania wote wanaopenda amani, akisisitiza kuwa hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana katika mazingira ya machafuko.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 8,2025


Magazeti

Share:

Friday, 7 November 2025

VIJANA WASHAURIWA KUACHA MIHEMKO NA KUILINDA AMANI



Wananchi wa Mkoa wa Dar Es salaam wameeleza kuwa mfumuko wa bei kwa bidhaa mbalimbali nchini pamoja na ukosefu wa huduma na bidhaa muhimu kulikotokana na ghasia na vurugu za Oktoba 29, 2025 kumewaathiri kiuchumi, wakiwataka Vijana kuacha mihemko na kutokubali kurubuniwa katika kuharibu amani na utulivu uliopo nchini.

Wananchi hao kwa nyakati tofauti wakizungumza na waandishi wa habari akiwemo Bw. Rahim Hassan Bakari, Mfanyabiashara wa soko la Kariakoo amesema kwa siku sita za ghasia hizo na zuio la kutofanya biashara kwa saa 24 kama walivyozoea limesababisha mfumuko huo ikiwemo katika bidhaa za vyakula ambapo nyanya moja kwasasa inauzwa shilingi 1, 000 kutoka Shilingi 100 huku Mchele ukiuzwa Kilo moja Shilingi 4,000 badala ya 2500.

"Vijana wenzangu nawashauri tuache mihemko, kilichotokea juzi kilikuwa mihemko tu kwasababu leo ukimuuliza aliyeandamana kwamba kwanini aliandamana atakuambia hana majibu. Mimi niombe tu kuwa tuache mihemko na kama tuna madai mbalimbali tufuate njia sahihi za kushughulikia changamoto zetu." Amesisitiza Bw. Bakari.

Kwa upande wake Bi. Faizat Peter, Mkazi wa Mbagala Jijini Dar Es Salaam ameeleza namna ambavyo maandamano hayo yamemuathiri kiuchumi na kijamii, akitoa wito wa amani nchini Tanzania na Watanzania wote kufanya tafakuri na kujifunza kutokana na athari zilizojitokeza Oktoba 29 kutokana na vurugu na ghasia zilizotokea Mkoani Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha, Songwe na Mbeya.


Share:

Thursday, 6 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 7, 2025

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger