Thursday, 29 May 2025
Wednesday, 28 May 2025
DIWANI AWAWASHIA MOTO WANAOMKASHIFU NA KUMTUKANA RAIS SAMIA,
Na Woinde Shizza ,moshi
Diwani wa kata ya Boma Mbuzi Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Juma Rahibu, amewajia juu baadhi ya Watanzania wanaomkashifu na kumtukana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akisema ni ishara ya kuporomoka kwa maadili katika jamii na kudhalilisha heshima ya taifa.
Akizungumza kwa hisia kali katika sherehe za uzinduzi wa kikundi cha mtetezi wa mama , Rahibu alisema ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya watu wakitumia majukwaa ya mitandao ya kijamii na mikusanyiko ya watu kumvunjia heshima kiongozi mkuu wa nchi ambaye, kwa mujibu wake, amekuwa akitekeleza majukumu yake kwa bidii na mafanikio makubwa.
“Huu si ustaarabu Rais Samia anajitahidi kutuletea maendeleo kama barabara, afya, elimu halafu mtu anajitokeza tu na kuanza kumtukana? Tunataka vyombo vya dola viwajibike,” alisema Rahibu.
Diwani huyo alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuenzi maadili ya taifa, hasa heshima kwa viongozi walioko madarakani, huku akionya kuwa uhuru wa kutoa maoni haupaswi kuwa kisingizio cha matusi, kashfa na propaganda zisizojengwa kwenye hoja za msingi.
Katika hatua nyingine, Rahibu alielekeza lawama kwa baadhi ya raia kutoka mataifa jirani ya Kenya na Uganda kwa kile alichokieleza kuwa ni tabia ya kudhalilisha na kumsema vibaya Rais Samia kwenye mitandao ya kijamii.
“Sasa imefika hatua hata baadhi ya Wakenya na Waganda wanathubutu kumtukana Rais wetu? Hii ni dharau ya hali ya juu ,Tanzania si uwanja wa mazoezi wa siasa za kejeli,” alisema kwa msisitizo.
Alisema Tanzania imekuwa nchi ya mfano wa heshima na ustaarabu kwa viongozi wa mataifa jirani, hivyo si haki kuona baadhi ya watu kutoka nje ya nchi wakitumia vibaya uhuru wa mitandao kwa maneno ya matusi dhidi ya kiongozi wa Tanzania.
“Tunawaheshimu viongozi wao, hatujawahi kusikia Watanzania wakimtukana Rais wa Kenya au wa Uganda ,Na wao wajifunze kutufanyia heshima hiyo hiyo,” aliongeza.
Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya wakazi wa Moshi wameonyesha kuguswa na kauli hiyo, wakisema kuwa ni kweli kuwa maadili yanaporomoka na watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya.
Esther Kilave, mkazi wa Pasua, alisema:
“Mitandao inatumika kama sehemu ya matusi sasa huu si utamaduni wetu ,Rais Samia anastahili kuheshimiwa kwa kazi anayoifanya.”
John Mlay, fundi umeme mjini Moshi, alisema:
“Tunaona mabadiliko mengi nchini Watu wanapaswa kutoa hoja za maana, si kejeli na matusi na niseme Wanapotukana Rais, wanatudhalilisha sisi sote. Acheni siasa za matusi.”
Rais Samia ameendelea kupokea pongezi kutoka kwa wananchi wa makundi mbalimbali nchini, kufuatia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na msimamo wake wa kudumisha amani, umoja wa kitaifa na usawa wa kijinsia.
JUMUIYA YA WANADIPLOMASIA YAKARIBISHWA NCHINI
WAZIRI DKT. GWAJIMA AANISHA VIPAUMBELE VITANO WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII 2025/2026


Na WMJJWM, Dodoma
Waziri wa Maendeleo ya Jamii. Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameainisha vipaumbele vya Wizara vikubwa vitano katika utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Mhe. Dkt. Gwajima ameainisha hayo wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka husika wa Fedha leo Mei 27, 2025 Bungeni jijini Dodoma.
Ameeleza kuwa Wizara kupitia Idara na Taasisi zilizo chini yake zitatekeleza vipaumbele hivyo ambavyo ni kukuza ari ya Jamii kushiriki katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ngazi ya msingi, kuratibu na kuimarisha utoaji wa huduma za ustawi wa maendeleo ya jamii, kutambua pamoja na kuratibu maendeleo ya ustawi kwa Makundi Maalum.
Mhe. Dkt. Gwajima ameongeza kuwa vipaumbele vingine ni pamoja kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia katika Taasisi na Vyuo vya Ustawi na Maendeleo ya Jamii na kuimarisha mazingira ya ushiriki na mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Maendeleo ya Taifa.
Amesema Wizara imeendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kuhamasisha na Kusimamia Maendeleo katika Ngazi ya Msingi (2022/23 – 2025/26) ambao unalenga kuwawezesha wananchi kuwa kitovu cha maendeleo na kuchochea mageuzi ya kifikra, mtazamo na kiutendaji kwa timu ya wataalam ngazi ya msingi ili kuboresha utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika kuhakikisha Watoto wanalindwa na ukatili Waziri Dkt. Gwajima amesema Wizara imeratibu na kusimamia Kampeni ya Taifa ya Usalama wa Mtoto Mtandaoni (Child Online Protection - COP) katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Kampeni ilikuwa na lengo la kuelimisha Wazazi au Walezi na Watoto wenyewe kuhusu Usalama wa Mtoto anapokuwa anatumia mitandao.
Aidha Mhe. Dkt. Gwajima amefafanua kuwa Wafanyabiashara ndogondogo 601 (Me 274; Ke 327) wamekopeshwa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,101,650,000 na zoezi hilo linaendelea. Vilevile maombi 2,092 yanaendelea kuchakatwa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 3,590,477,000.
"Wizara kwa kushirikiana na OR - TAMISEMI imeendelea kuratibu na kufuatilia maendeleo ya ya Ujenzi wa Ofisi za wafanyabiashara ndogondogo katika ngazi ya mikoa ambapo hadi kufikia Aprili 2025 mikoa 17 kati ya mikoa 26 imekamilisha ujenzi wa Ofisi hizo" ameeleza Mhe. Dkt Gwajima.
Akichangia hoja, Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Dkt. Thea Ntara amesizitiza Serikali kuchukua hatua na kusimamia maadili nchini, kutokana na kuwepo kwa matukio mengi ya uvunjifu wa maadili.
Naye Mbunge wa kuteuliwa Dkt. Shukurani Manya ameshauri kuongezeka kwa juhudi za kuelimisha Jamii kuhusu elimu ya malezi ili kuepusha kutelekezwa kwa watoto ili waweze kupata malezi ya baba na mama.
MWENYEKITI WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE KAHAMA AWAKARIBISHA WANANCHI KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI
Tuesday, 27 May 2025
ALIYENIFUKUZA KISA NILIKATAA KULALA NAYE, AKUMBWA NA MAZITO!

SERIKALI YAMWAGA MILIONI 815 KUBORESHA HUDUMA YA MAJI KWA VIJIJI VINNE MTWARA

Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Mkoani Mtwara Mhandisi Hamis Mashindike aliyeshika fimbo,akimuonyesha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi miundombinu ya mradi wa maji Dihimba uliofanyiwa ukarabati mkubwa ili kuboresha hduma ya majisafi na salama kwa Wananchi wa Vijiji vinne vya Dihimba,Mpondomo, Kinyamu na Ndumbwe.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi,akiangalia kisima cha maji katika kilichofanyiwa ukarabati mkubwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji kwa Wananchi wa Vijiji vya Ndumbwe,Dihimba,Mpondomo na Kinyamu Wilayani Mtwara,kushoto Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Hamis Mashindike na kulia Mkuu wa Wilaya
TAKUKURU YADHIBITI UBADHIRIFU WA MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU USHETU, SHINYANGA

Na Kadama Malunde – Malunde 1 Blog
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga imefanikiwa kudhibiti ubadhirifu wa kiasi cha shilingi milioni 92.16 zilizotengwa kwa ajili ya kuwafidia wakulima wa tumbaku wa Chama cha Msingi cha Ushirika (AMCOS) Ibambala, kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu mkoani humo.
Taarifa hiyo imetolewa leo Mei 27, 2025 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Shinyanga.
Kwa mujibu wa Kessy, fedha hizo zilitolewa kwa wakulima waliopata hasara kutokana na mafuriko yaliyoathiri uzalishaji wa tumbaku katika msimu wa kilimo wa mwaka 2023/2024, lakini hazikufika kwa walengwa kama ilivyokusudiwa.
“TAKUKURU ilibaini kuwa shilingi milioni 11.62 zilichukuliwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho kwa matumizi yao binafsi, akiwemo Katibu Meneja Bw. Charles Alex Shiyengo na Mwenyekiti Bi. Faida Paulo Deda,” amesema Kessy.
Aidha, TAKUKURU imebaini kuwa kiasi kikubwa cha fedha—shilingi milioni 151.53—kiligawiwa kwa watu wasiostahili, wakiwemo ndugu wa viongozi hao. Miongoni mwa waliopokea fedha hizo ni Bi. Lucy Masanja Dglibata, mke wa Katibu Meneja, ambaye alipokea shilingi milioni 34.58, pamoja na Bw. Charles Charles Masanja aliyelipwa shilingi milioni 5.58.
Hatua za awali za kurejesha fedha hizo zimeanza kuchukuliwa huku wahusika wakikabiliwa na hatua za kisheria.
Katika kipindi cha Januari hadi Machi 2025, TAKUKURU Shinyanga pia imepokea jumla ya taarifa 57 za tuhuma za rushwa, ambapo 52 zilifanyiwa uchunguzi na 13 kati yake zimefikishwa mahakamani.
Kwa upande wa elimu kwa umma, taasisi hiyo imeendesha mikutano ya hadhara 61, semina 30, na vipindi vya redio na runinga 13 kupitia programu yao ya Takukuru Rafiki, lengo likiwa ni kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa.
Kessy amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na TAKUKURU kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa njia ya simu ya bure 113 au kupitia tovuti yao ya www.pccb.go.tz.
Monday, 26 May 2025
SERIKALI ,WANAZUONI KUJADILI PPP, UCHUMI NA DIRA 2050

Mei 26, 2025
Na Mwandishi Wetu _ Dar es Salaam
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia (PPPC) David Kafulila, mjadala huo wa wazi utafanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Kituo cha PPPC kitafanya kongamano kwa kushirikiana na Taasisi ya Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia (REDET) ambayo iko chini ya UDSM.
Mada kuu ya kongamano ni: Dola, Masoko na Uhamasishaji wa Mitaji: Nafasi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi Kufikia Malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.
Kafulila atafanya wasilisho kuhusu Dhana ya PPP na Nafasi yake Kuelekea Dira ya Taifa 2050 na Mwenyekiti wa REDET, Prof. Rwekaza Mukandala, ataongoza kongamano kama moderator.
Kongamano litafanyika katika Ukumbi wa Maktaba Mpya, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumanne tarehe 27 Mei 2025 kuanzia saa 3:00 asubuhi mpaka saa 6:00 mchana.
Maafisa waandamizi wa serikali, wakuu wa makampuni ya sekta binafsi, wanazuoni na wawakilishi wa kada nyingine mbalimbali wanatarajiwa kushiriki kwenye mjadala wa wazi utakaorushwa mubashara na vituo kadhaa vya televisheni.
"Wananchi wote wanakaribishwa kuhudhuria kongamano hili la wazi ili waweze kushiriki kwenye mjadala kuhusu dhana ya PPP na nafasi yake kwenye kutekeleza Dira ya Taifa 2050," Kafulila amesema.
"Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) una nafasi kubwa kwenye mwelekeo mpya wa uchumi na maendeleo ya Tanzania."
Kituo cha PPPC kinasimamia jumla ya miradi 84 ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ambayo iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
Miradi hiyo ipo kwenye sekta za usafirishaji, nishati, miundombinu na maeneo mengine.
Baadhi ya miradi hiyo ni Barabara ya waendao haraka (Express way) ya Kibaha–Chalinze -Morogoro (205km), na ile ya Isongole-Tunduma (210km) ambazo zikijengwa njia nne za barabara (epxress way), zinaweza kugharimu karibu dola za Marekani Bilioni 1.6.
Mradi wa barabara kwa ajili ya kupunguza foleni katikati ya Jiji la Dar es Salaam (Outer ring roads) nao ni miongoni mwa miradi ya kutekelezwa kwa ubia wa PPP.
MWENGE WA UHURU WAZINDUA VISIMA TANDAHIMBA, WANANCHI WAPATA MAJI YA BOMBA KWA MARA YA KWANZA TANGU UHURU

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara Falaura Kikusa,akimuonyesha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi ,mchoro wa mradi wa Kisima cha maji uliotekelezwa katika Kijiji cha Mivanga.




















