Monday, 26 May 2025

MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO


Na Mwandishi Wetu, OR- TAMISEMI

Mkuu wa Kitengo Cha Mawasilino Serikali na Msemaji Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI, John Mapepele ametoa wito kwa Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri zote nchini kutanguliza uzalendo na weledi wakati wa utoaji wa taarifa ili habari hizo ziwe na tija kwa taifa.

Mapepele ametoa wito huo mwisho wa juma wakati akiwasilisha maada kuhusu Mawasilino ya Kimkakati ya Kutangaza Nafanikio ya Sekta za Afya, Elimu na Miundombinu chini ya TAMISEMI kwa Maafisa Habari zaidi ya 200 wa Mikoa na Halmashauri zote nchini jijini Dodoma kwenye kikao kazi cha siku mbili kwa MaafisaHabari hao kilichoratibiwa na Wizara hiyo.
Kikao kazi hicho kilichofunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.Mohamed Omary Mchengerwa na kufungwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa kimejadili pamoja na mambo mengine, mikakati mbalimbali ya kutangaza mafanikio ya Serikali, pia kuwajengea uwezo Maafisa Habari hao kwa mada mbalimbali za kitaaluma hususan matumuzi ya mifumo ya kidigitali kwenye utoaji wa taarifa na kuja na maazimio kadhaa ya kuboresha utendaji kazi.

Aidha, Mapepele amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa katika mikoa na Halmashauri zote nchini ambayo haijatangazwa ipasavyo na Maafisa Habari katika maeneo hayo na kuwataka kuwa wabunifu wa kutoa taarifa hizo

"Ndugu zangu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanya mapinduzi makubwa kwenye sekta ya miundombinu ambapo tumeshuhudia mabarabara, madaraja, vituo vya mabasi na masoko yakitengenezwa kila uchao, ukiachia mbali madarasa, zahanati, vituo vya afya na vifaa tiba kwenye kila kona hivyo ni wajibu wetu sisi Maafisa Habari wa Halmashauri na Mikoa kuwa wazalendo na kuisemea Serikali yetu ili wananchi waweze kujua na kutumia huduma hizi kikamilifu". Amefafanua Mapepele

Akifungua kikao kazi hicho Mhe. Mchengerwa amewataka Maafisa Habari wote wa TAMISEMI kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi kwa wakati za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao ya kazi. 

"Mmebeba dhamana kubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi hivyo msiache watanzania walishwe habari potofu". Amesisitiza Mhe. waziri Mchengerwa

Akifunga kikao kazi hicho, Katibu Mkuu Msigwa ameipongeza Wizara ya TAMISEMI kwa kuratibu kikao kazi hiki ambapo ameshauri kiwe kinafanyika kila mwaka ili kufanya tathmini wa utendaji wa kazi na kujadiliana masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi wa kundi hili kubwa la Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri nchini katika kutoa taarifa za miradi ya maendeleo.



Share:

Sunday, 25 May 2025

TAASISI YA UDOPRESA YAZINDULIWA UDOM




Kamati ya Uzinduzi wa UDOPRESA ikikabidhi zawadi ya Picha kwa Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph katika Hafla ya Uzinduzi wa Taasisi hiyo.

.......

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu cha Dodoma, Bi. Rose Joseph katika Ukumbi wa LT2 (CHSS) UDOM amefanya Uzinduzi wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosomea Uandishi wa Habari na Uhusiano wa Umma Chuo Kikuu cha Dodoma - The University of Dodoma Public Relations Students Association (UDOPRESA) yenye jumla ya wanachama 250.

Taasisi hiyo imeanzishwa kwa dhamira kuu ya kuwaunganisha wanafunzi wanaosoma Taaluma ya Uhusiano na Umma na Uandishi wa Habari wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Kuimarisha Taaluma, Kushirikiana katika Tafiti na Mafunzo na kuwa chachu ya Maendeleo ya Taaluma hiyo Nchini.

Akizungumza wakati wa Hafla ya Uzinduzi; Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu cha Dodoma Bi. Rose Joseph ameahidi kuwapa ushirikiano wowote watakaohitaji huku akiwaasa kutumia Taasisi hiyo katika kulinda taswira ya Chuo na kuwataka watangulize uzalendo kwa Taifa mbele, kulinda na kuheshimu fani hiyo; pamoja na kuzingatia Sheria, Taratibu na Miongozo yote ya maafisa Uhusiano na Habari.

"Hili ni Jukwaa muhimu sana ambalo si tu kwamba linawaleta pamoja wanafunzi wanaosomea Uhusiano wa Umma UDOM, lakini naamini ni jukwaa zuri la kuwanoa, kuwaweka tayari kwa ajili ya kwenda kulitumikia Taifa, kutetea Tasnia na kwenda kuwa waandishi bora na maafisa bora wa umma" Aliongeza Bi. Rose.

Kwa Upande wake; Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari, Dkt. Deograsia Ndunguru amewapongeza Wanachama wote wa UDOPRESA huku akisisitiza kuwa Taasisi hiyo itawasaidia kuongeza ujuzi, Maarifa hasa katika kuwajenga kuwa maafisa Uhusiano Bora wa baadae.

Naye; Mlezi wa Taasisi hiyo Dkt. Mary Kafyome, amesema ulikuwa ni mchakato mkubwa kufanikisha jambo hilo huku akitoa pongezi kwa wote walihusika kufanikisha tukio hilo na ametoa wito kwa wanafunzi wanaobaki kuendeleza taasisi hiyo.

"UHUSIANO BORA, JAMII BORA!"
Mgeni Rasmi kwenye Hafla ya uzinduzi wa chama cha UDOPRESA, Bi. Rose Joseph akihutubia wakati wa uzinduzi.
Mlezi wa Taasisi ya UDOPRESA Dkt. Mary Kafyome akitoa neno la Shukurani wakati wa Uzinduzi wa Hafla ya UDOPRESA
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Chuo kikuu cha Dodoma Bi. Rose Joseph akikata keki kama ishara ya Uzinduzi wa Taasisi ya UDOPRESA kutoka kulia kwake ni Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari Dkt. Deograsia Ndunguru, akifuatiwa na Mlezi wa UDOPRESA Dkt. Mary Kafyome na Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa UDOPRESA Bw. Swerd Mwakage akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Huduma za Wanafunzi UDOM Bw. Gabriel Elia.
Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari Chuo Kikuu cha Dodoma Dkt. Deograsia Ndunguru akitoa neno wakati kwa Washiriki wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Wanachama wa UDOPRESA wakiwa katika hali ya furaha wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph akikabidhi Cheti cha Uongozi Bora kwa Mwenyekiti wa UDOPRESA Bw.Swerd Mwakage wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Kamati ya Uzinduzi wa UDOPRESA ikikabidhi zawadi ya Picha kwa Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph katika Hafla ya Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 25,2025

Magazeti




Share:

Saturday, 24 May 2025

MWENYEKITI ACT-WAZALENDO TAIFA MHE. OTHMAN AELEZA MKAKATI MZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025, "TUNALINDA DEMOKRASIA NA KUTHAMINI UKOMBOZI"


Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman akihutubia wananchi mkoani Shinyanga.

Na Mwandishi Wetu, Malunde 1 Blog Shinyanga

Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, amesema kuwa chama chake kiko tayari kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kwa dhamira thabiti ya kuendeleza harakati za mabadiliko ya kweli, haki kwa wananchi, na ukombozi wa Taifa.

Akihutubia wananchi katika viwanja vya shule ya Msingi Town iliyopo Manispaa ya Shinyanga Mei 24, 2025, Mheshimiwa Othman ameweka wazi kuwa dhamira ya kuasisi Taifa hili ilikuwa ni kuwapatia wananchi uhuru, sauti, na heshima katika kufanya maamuzi ya taifa lao – dhamira ambayo inazidi kudhoofishwa na mfumo wa sasa wa uongozi.

"Ndugu wananchi, lile ambalo tulilipambania sasa halipo tena, na wenzetu ndio ambao wamelipoteza," amesema kwa msisitizo, akirejea misingi ya uhuru na usawa wa wananchi.

Mheshimiwa Othman ameongeza kuwa kunyima wananchi haki ya kupaza sauti na kuchagua viongozi wanaowataka ni sawa na kuwafanya kuwa watumwa katika nchi yao wenyewe.

"Pale ambapo wananchi hawana sauti wala haki ya kuchagua wanaowaamini, Taifa hubaki dhaifu na tegemezi – hali ambayo siyo stahiki ya Watanzania," amesema Mheshimiwa Othman.

Mheshimiwa Othman pia ameeleza kuwa licha ya Mkoa wa Shinyanga, na maeneo ya jirani, kubarikiwa na rasilimali nyingi kama dhahabu na almasi bado, rasilimali hizo zimekuwa zikitumiwa vibaya, huku wananchi wa maeneo hayo wakibaki maskini.

"Shinyanga kama ingekuwa nchi inayojitegemea, ingeweza hata kuikopesha Tanzania nzima," aamesema Othuman.

Ameongeza kuwa wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakihadaiwa na kushawishiwa kila msimu wa uchaguzi, lakini hali halisi haibadiliki kwao.

Ziara ya Mheshimiwa Othman ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya ACT-Wazalendo inayoitwa Operesheni Linda Demokrasia, inayolenga kufufua matumaini ya wananchi na kuhakikisha kuwa sauti zao zinasikika kupitia sanduku la kura.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ndugu Ado Shaibu, amempongeza Mhe.Othman kwa kuwa kiongozi asiye na chembe ya kuyumba katika misingi ya haki huku akiwapokea wanachama 26 walio jiunga na chama hicho kutoka katika vyama vingine vya upinzani .

Mkutano huo wa kisiasa umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kanda ya ziwa, akiwemo Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Shinyanga, Ndugu Hassan Ibrahim, pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Chama.Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman akihutubia wananchi wa mkoa wa Shinyanga.Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.
Katibu mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo Taifa , Ndugu Ado Shaibu, aa cha ACT-Wazalendo Taifa Shangwe Ayo akizungumza na wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakati wa mkutano nakupokea wanachama wapya 26 waliohama vyama vyao na kujiunga na ACT Wazalendo.Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.Katibu Mwenezi wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa Shangwe Ayo akizungumza na wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakati wa mkutano.Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.
Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.
Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman wakati wa mkutano.

Share:

ELIMU YA KODI YAWAFIKIA WAFANYABIASHARA IRINGA KUPITIA RADIO NA MLANGO KWA MLANGO.


Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Mkumbwa akimuelimisha mlipakodi wa eneo la Miyomboni Iringa wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo akimpatia zawadi Meneja wa Radio ya Shamba FM ya Mkoani Iringa Bw. Laurian  Deogratius baada ya kumaliza kipindi kilichoangazia masuala ya haki na wajibu wa mlipakodi pamoja na umuhimu wa kulipa kodi ikiwa ni sehemu ya zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Shaga Gagunda  akimuelimisha mlipakodi wa eneo la Miyomboni Iringa wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Frola  Fulgence akimuelimisha mlipakodi wa eneo la Miyomboni Iringa wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo akizungumzia mada ya haki na wajibu wa Mlipakodi katika kipindi cha radio cha kivulini kinachorushwa na Shamba FM iliyoko mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Meneja Msaidizi wa Huduma kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Iringa Bw. Musa Haruni akizungumzia mada ya umuhimu wa kulipa kodi katika kipindi cha radio cha kivulini kinachorushwa na Shamba FM iliyoko mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Haika Mallya akimuelimisha mlipakodi wa eneo la Miyomboni Iringa wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya kodi mlango kwa mlango linaloendelea mkoani humo.
Share:

MADINI YA ALMASI YENYE THAMANI YA TSH 1.7 BILIONI YAKAMATWA YAKITOROSHWA UWANJA WA NDEGE MWANZA



▪️Waziri Mavunde awapongeza RC Mtanda,Kamati ya Usalama,Uwanja wa Ndege na Kikosi kazi Madini

▪️Aelekeza uchunguzi zaidi kubaini mtandao wote wa wahusika

▪️Atoa rai kwa wadau wa madini kuzingatia sheria ya biashara ya madini nchini

▪️Raia wa Kigeni mwenye asili ya India ashikiliwa 


Mwanza

Madini ya almasi yenye thamani ya zaidi ya Sh1.7 bilioni yamekamatwa yakitoroshwa kupitia Uwanja wa ndege wa Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari ljumaa usiku,Mei 23, 2025, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema madini hayo yalikamatwa Mei 18, 2025 kwa ushirikiano kati ya vyombo vya ulinzi na taasisi mbalimbali za Serikali na kutumia fursa hiyo kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Said Mtanda,Vyombo vya usalama,uongozi wa uwanja wa Ndege wa Mwanza na Kikosi Kazi cha Wizara ya Madini kwa kazi kubwa na ya kizalendo ambayo wameifanya.

“Mtu mmoja raia wa kigeni ambaye ana asili ya India , anashikiliwa kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo na anatarajiwa kufikishwa mahakamani uchunguzi na taratibu

Katika tukio hilo,almasi ghafi yenye uzito wa karati 2,729.82 na thamani ya takriban USD 635,887.66 (sawa na Shilingi za Kitanzania 1,715,434,129.67) yaligunduliwa yakiwa yamefichwa kwenye mabegi manne na raia mmoja mwenye asili ya India kwa lengo la kuyasafirisha bila vibali halali wala kufuata taratibu za kisheria.

Nitoe rai kwa wadau wote wa Sekta ya Madini nchini kuhakikisha wanafuata sheria ya biashara ya madini nchini Tanzania ili wasipate hasara kwa kupoteza madini hayo ambayo hutaifishwa na serikali” Alisema Mavunde

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Saidi Mtanda amesema Mkoa wa Mwanza unaendelea kuimarisha ulinzi na udhibiti wa biashara zote haramu ili kuhakikisha nchi yetu ya Tanzania inanufaika na rasilimali madini.

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger