Friday, 16 May 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 16,2025


Magazeti



Share:

Thursday, 15 May 2025

MAGEUZI MAPYA KATIKA SEKTA YA MILIKI YALENGA KUIMARISHA MAKAZI NA BIASHARA



Na Woinde Shizza, Arusha

Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi iko mbioni kuandaa sera mpya pamoja na kupitia sheria mbalimbali zitakazotambua kada ya Miliki, Wathamini na Madalali nchini.

Akizungumza jijini Arusha katika mkutano wa tano wa mwaka wa wadau wa Miliki Kuu, Waziri wa wizara hiyo, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa serikali imelenga kuimarisha sekta ya makazi na kupanua wigo wa biashara.

Amesema mchango wa wataalamu wa miliki ni mkubwa katika kukuza na kuimarisha miundombinu ya nchi, jambo linalokwenda sambamba na dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
“Mageuzi haya yanaendana na maboresho ya miundombinu kama Reli ya Kisasa, barabara, usafiri wa anga na maji,” amesema Ndejembi, huku akiahidi ushirikiano wa karibu kati ya serikali na wataalamu wa sekta hiyo.

Rais wa Chama cha Wataalamu wa Miliki Kuu nchini, Andrew Kato, amesema kutokuwepo kwa sera maalumu ya makazi kumechangia changamoto nyingi katika sekta hiyo na kuathiri utekelezaji wa miradi.
Amesema sera na sheria mahususi zitasaidia kuweka mipaka ya majukumu, kurahisisha huduma kwa wananchi, na kuhakikisha kuwa miradi inakamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.

Makamu wa Rais wa Miliki Afrika Mashariki, Prof. Nicky Nzioki, ameshauri serikali kuiga mifumo ya nchi kama Kenya na Rwanda katika usimamizi wa sekta ya makazi, akibainisha kuwa sera hiyo ikiwekwa itasaidia pia kuongeza ajira kwa vijana.

Mkutano huo umehudhuriwa na zaidi ya washiriki 180 kutoka kada mbalimbali ikiwemo Maafisa Ardhi, Wathamini, Wasimamizi wa Majengo, Wawekezaji na Wataalamu wa sekta ya miliki kutoka nchi za Afrika Mashariki
Share:

Video Mpya : MAMA USHAURI - MAWAZO GANE

 

Share:

WANANCHI WA MSISIMA NA MNALAWI WAMEIPONGEZA SERIKALI KWA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA

Tanki la Maji katika kijiji cha Msisima na Mnalawi halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma uliopo chini ya Mradi wa maji safi na salama vijijini (RUWASA)
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Ismail Ussi akizungumza na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa maji kijiji cha Msisima na Mnalawi Wilayani Namtumbo
Na Regina Ndumbaro Namtumbo-Ruvuma




Wananchi wa kata ya Msisima na Mnalawi, Wilaya ya Namtumbo, wameeleza furaha yao kubwa  kuuona mwenge wa Uhuru kwa mara ya kwanza tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961,baada ya mwenge wa uhuru kufika kijijini kwao. 

Wakiwa katika uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama chini ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wananchi hao wametoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea maendeleo na kuonesha dhamira ya kweli ya kuwahudumia Watanzania wote bila ubaguzi.

Yasin Dauda na Zainabu Mjomba, wakazi wa vijiji hivyo, wameeleza kuwa mradi huo wa maji utasaidia kuondoa adha waliyozoea ya kutumia maji yasiyo salama, kupunguza umbali wa kutafuta maji na kuimarisha afya za familia zao. 

Wamesema kuwa huduma hii muhimu ni ya kihistoria na kielelezo cha utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita. 

Kwa heshima na kuthamini mchango wa Rais Samia, wameahidi kumpa kura zote katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Oktoba, wamesisitiza kuwa hawatamwangusha kiongozi huyo aliyeonesha kuwajali kwa vitendo.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo, Ndugu David Mkondya, Ameeleza kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60. 

Mradi huo una thamani ya shilingi bilioni 1.1, na unatarajiwa kunufaisha wakazi 481 kutoka vijiji viwili kwa kutumia chanzo cha maji kutoka Mto Msokambale. 

Mradi unahusisha ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi lita 200,000, mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita saba, huku chanzo hicho kikiwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya lita milioni nne kwa siku ikilinganishwa na mahitaji ya lita 242,000 kwa siku. 

Mradi huo wa maji ulianza tarehe 17 Oktoba 2023 na unatarajiwa kukamilika tarehe 13 Juni 2025.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ussi, amesisitiza kuwa mwenge wa uhuru umebeba ujumbe wa matumaini, amani, upendo na mshikamano kwa Watanzania. 

Ameeleza kuwa asilimia mia moja ya wakazi wa maeneo hayo watanufaika moja kwa moja na mradi huo wa maji. 

Pia amewahimiza wananchi kudumisha mshikamano, umoja na amani ili mradi huo uwe endelevu na kuleta mafanikio ya muda mrefu kwa jamii.

Kwa ujumla, ujio wa mwenge wa uhuru katika kata ya Msisima na Mnalawi umetajwa kuwa chachu ya maendeleo na ukombozi wa kweli kwa wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji kwa muda mrefu. 

Serikali imeendelea kuonesha kwa vitendo kuwa dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo si ya maneno bali ni ya vitendo, jambo ambalo limepongezwa kwa nguvu na wananchi wa maeneo hayo.

Share:

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AHIMIZA ELIMU KWA WATOTO


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi akizindua jiwe la msingi katika shule ya msingi Mtakanini Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Shule ya msingi Mtakanini iliyozinduliwa leo na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Mwenge wa uhuru ulipowasili katika halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma ukitoka katika Manispaa ya Songea
Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Ngolo Malenya katika makabidhiano yaliyofanyika katika kijiji cha Lumecha Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Na Regina Ndumbaro Namtumbo-Ruvuma. 

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Ndugu Ismail Ussi, ametoa wito kwa wazazi na jamii kuhakikisha watoto wote wanapelekwa shule ili wapate elimu bora. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi kuweka jiwe la msingi katika Shule ya Msingi Mtakanini iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, Ussi ameeleza kuwa shule hiyo imeboreshwa na sasa ina miundombinu ya kisasa yenye ubora wa hali ya juu.

Shule ya Msingi Mtakanini ambayo imezinduliwa rasmi leo, ina jumla ya madarasa manne na matundu ya choo sita. 

Uboreshaji huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia kwa wanafunzi. 

Kiongozi huyo amesisitiza kuwa jitihada hizi zinaonesha dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais katika kuhakikisha kila mtoto nchini anapata elimu bora.

Katika hatua nyingine, makabidhiano ya mbio za mwenge yamefanyika leo katika kijiji cha Lumecha, Kata ya Msindo, katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma.

 Makabidhiano hayo yamefanyika kati ya Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngolo Malenya.

Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kwa jumla ya kilomita 147 katika Wilaya ya Namtumbo, ukitembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngolo Malenya, amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya awamu ya sita chini ya Daktari Samia Suluhu Hassan walipatiwa kiasi cha fedha wilayni humo  katika  utekelezaji wa miradi kiasi cha shilingi bilioni 89 .

Kupitia tukio hili, viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya serikali na wananchi katika kuendeleza maendeleo ya elimu na miundombinu kwa ujumla. 

Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo muhimu katika kuhamasisha maendeleo na uzalendo nchini.

Share:

BENKI YA CRDB YAWAKARIBISHA WANAHISA KWENYE MKUTANO MKUU WA 30

 

Arusha 14 Mei 2025 - Benki ya CRDB imewataka wanahisa wake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa, unaotarajiwa kufanyika Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya mafanikio tangu kuanzishwa kwa benki hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye hoteli ya Gran Meliá, jijini Arusha, ambapo Benki ya CRDB pia ilizindua Ripoti yake ya Mwaka 2024, inayoonyesha maendeleo makubwa ya kifedha, kiutendaji na kijamii yaliyopatikana katika kipindi hicho.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, amesema kuwa Mkutano Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa kipekee kwani utatanguliwa na semina maalum kwa wanahisa na umma, itakayofanyika Ijumaa, tarehe 16 Mei 2025, katika ukumbi wa Simba, AICC. “Semina hii ya kihistoria itakuwa chini ya kaulimbiu yetu ya mwaka huu: ‘Miaka 30 ya Ukuaji wa Pamoja,’ na itafunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio yetu ya pamoja, changamoto tulizozishinda, na mwelekeo wetu wa miaka ijayo,” amesema Dkt. Laay.

Ajenda mbalimbali zitajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB ni pamoja na uchaguzi wa wajumbe wa bodi, kuteua wakaguzi wa hesabu, kujadili mapendekezo ya maboresho ya Katiba ya Benki, kujadili na kupokea Taarifa ya Bodi ya Wakurugenzi, na Taarifa ya Hesabu zilizokaguliwa, pamoja na gawio kwa mwaka 2024 ambapo pendekezo la gawio la Sh 65 kwa hisa litawasilishwa sawa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa yamekamilika kwa asilimia 100. Nsekela amesema mkutano huo utafanyika kwa njia mseto “Hybrid Meeting” ili kutoa fursa kwa wanahisa wengi zaidi kushiriki moja kwa moja na kwa njia ya kidijitali. “Tumeweka muongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yetu ya www.crdbbank.co.tz, mitandao yetu ya kijamii, lakini pia maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa Wanahisa,” amesema Nsekela huku akiwahakikishia kuwa Benki hiyo vizuri katika kuhakikisha wanashiriki bila chanagamoto yoyote.
Nsekela amewahamasisha wanahisa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu huo wa kihistoria, akisisitiza kuwa uwepo wao ni muhimu kwa ajili ya kushuhudia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika miaka 30. “Tumejenga taasisi imara inayotoa huduma bora, tumeongeza thamani kwa wanahisa, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa letu. Hii ni fursa adhimu kwa kila mwanahisa kujivunia sehemu yake katika mafanikio haya na kushiriki kuamua mustakabali wa benki yetu katika miaka ijayo,” amesisistiza.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger