Saturday, 19 April 2025

WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA WASHUHUDIA MAAJABU YA BUSTANI YA WANYAMA YA 'JAMBO ZOO' HAMASA YA UTALII TANZANIA

Na Kadama Malunde - Shinyanga

Waandishi wa habari katika Manispaa ya Shinyanga kupitia Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC) wametembelea bustani ya wanyama Jambo Zoo iliyopo katika eneo la Ibadakuli, Mjini Shinyanga, inayomilikiwa na Kampuni ya Jambo Group.

Ziara hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2025 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na kuwaunga mkono wawekezaji wazawa, ambapo imeratibiwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mhifadhi wa Jambo Zoo, Babuu Burhan Kajuna, alisema bustani hiyo ina wanyama wa aina mbalimbali ambao wamepewa mafunzo na kuzoea binadamu, hivyo kuwawezesha wageni kupiga nao picha kwa ukaribu.
"Tunawashukuru waandishi wa habari kwa kutembelea Jambo Zoo. Tunawakaribisha wananchi wote waje kufanya utalii wa ndani hapa Shinyanga. Bei zetu ni rafiki kabisa – watu wazima ni shilingi 20,000= na watoto shilingi 10,000/=," amesema Kajuna.

Ameongeza kuwa wageni wanaofika katika bustani hiyo hupata fursa ya kujifunza kuhusu tabia za wanyama, kupiga nao picha kwa ukaribu, na kuwalisha chakula kwa mikono yao.
Kwa upande wake, Msimamizi wa Chapa kutoka Jambo Group, Nickson George, amewataka wananchi kuitembelea bustani hiyo hasa katika kipindi hiki cha sikukuu ya Pasaka, wakiwa na familia zao, huku wakifurahia vinywaji vipya vya Jambo Lemon Lime na Jambo Power Boom.

Aidha, Mratibu wa ziara hiyo, Marco Maduhu, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya SPC na mfadhili wa safari hiyo, ameipongeza Kampuni ya Jambo Group kwa uwekezaji wa bustani hiyo ya wanyama, akisema umeunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kuhamasisha utalii wa kupitia filamu ya The Royal Tour.

Bustani ya Jambo Zoo inaendelea kuwa kivutio kikuu kwa wakazi wa Shinyanga na wageni, ikiwa ni sehemu ya utalii wa elimu, burudani na uhifadhi wa wanyama katika mazingira salama na rafiki kwa familia.

PICHA NA KADAMA MALUNDE NA MARCO MADUHU👇
Mhifadhi wa Jambo Zoo Babuu Burhan Kajuna, akizungumza na waandishi wa habari ambao wametembelea Bustani hiyo ya Wanyama.
Msimamizi wa Chapa Jambo Group Nickson George akizungumza na waandishi wa habari akiwa ameshika vinjwaji vipya ambavyo ni Jambo Lemon Lime na Jambo Power Boom, katika Tour hiyo ya Jambo Zoo.
Mjumbe wa Kamati Tendaji Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga Marco Maduhu akielezea Tour hiyo ya JAMBO ZOO na namna alivyo anzisha wazo hilo ili kuunga mkono Juhudi za Rais Samia Kuhamasisha Utalii wa ndani na kuwa "Support" wawekezaji wazawa.
Waandishi wa habari wakiwa TOUR JAMBO ZOO.



Picha za pamoja zikipigwa

PICHA NA KADAMA MALUNDE NA MARCO MADUHU
Share:

WATUMISHI BODI YA MFUKO WA BARABARA WATAKIWA KUZINGATIA MIONGOZO YA UANDISHI WA NYARAKA

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho, akifunga kikao kazi cha ndani cha Bodi ya Mfuko wa Barabara kilichofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro.

*************

Watumishi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara wametakiwa kuzingatia miongozo ya uandishi wa nyaraka mbalimbali za kiserikali ili kuboresha ubora na ufanisi wa mawasiliano ya kimaandishi ndani ya Serikali.

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho, wakati akifunga kikao cha ndani chaWafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara kilichofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika utumishi wa umma .

Mrisho amesema miongozo hiyo inatoa viwango vya uandishi wa nyaraka kama vile uandishi wa barua za Serikali na una dhumuni la kuweka muundo wa pamoja katika mawasiliano ya kiserikali.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo ametoa wito kwa watumishi wa Bodi hiyo kuboresha mahusiano na mawasiliano ndani ya Bodi ili kuongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga, ameeleza kuwa jumla ya watumishi 32 wameshiriki katika kikao hicho na kupata mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo na kuwaongezea ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kwamba watumishi hao pia wameapa na kutia saini viapo vya utunzaji siri za Serikali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Idara ya Mipango na Mapato kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara Godlove Stephen amesema watahakikisha wanayatekeleza vyema waliyojifunza hasa katika uandishi wa taarifa mbali mbali za Bodi kwa kuzingatia miongozo iliyopo pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya watumishi.

Naye, Afia Ndyamukama Mtumishi kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara ameiomba Bodi kutoa mafunzo kama hayo kwa watumishi mara kwa mara ili kuwajengea uwezo na kuwaongezea ufanisi zaidi katika utendaji kazi wao wa kila siku.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho (katikati), Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Utawala na Rasilimali Watu wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Aureus Mapunda, wakati wa hafla ufungaji kikao kazi cha ndani cha wafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara kilichofanyika mkoani Morogoro.
Viongozi na watumishi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara, wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho (hayupo pichani), wakati akifunga kikao kazi cha ndani cha Bodi hiyo kilichofanyika mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho, akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara mara baada ya kufunga kikao kazi cha ndani cha Bodi hiyo kilichofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 19,2025


Magazeti 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger