Sunday, 16 February 2025

WABUNGE WAPONGEZA MIGODI YA BARRICK-TWIGA KWA UTUNZAJI MAZINGIRA, UTEKELEZAJI WA MAUDHUI YA NDANI ‘LOCAL CONTENT’


Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa akizungumza wakati wa ziara hiyo
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick -Twiga Bulyanhulu, Victor Lule akizungumza. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa  akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Kilumbe Ng’enda
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakiwa katika sehemu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakiwa katika sehemu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakiwa katika sehemu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu

***

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Migodi wa Barrick naTwiga kwa kuendelea kufuata viwango vya kimataifa na vinavyokubalika vya uchimbaji wa madini vinavyoimarisha utunzaji wa mazingira, usalama mahala pa kazi kwa maslahi mapana ya wafanyakazi na wananchi wanaozunguka mgodi.

Akizungumza kwenye ziara ya siku ya pili ya kamati hiyo mwishoni mwa wiki migodi ya Barrick Twiga ya Bulyanhulu na Buzwagi ambao upo kwenye hatua za mwisho za ufungaji na kuwa kongani maalumu , Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kilumbe Ng’enda alisema kwamba migodi ya Barrick yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga iko mstari wa mbele katika kuwasaidia watanzania kupitia kanuni ya maudhui ya ndani (Local Content) na Uwajibikaji wa Jamii (CSR).

“Hii ni mara ya pili tunazuru Mgodi wa Barrick Twiga kuona maendeleo ya uchimbaji na upanuzi wa shughuli hizo za hasa utafiti, usindikaji na shughuli zingine za kila siku ambazo zina matokeo Chanya kwa jamii inayozunguka mgodi husika,” alibainisha.

Alisisitiza kwamba Mgodi wa Barrick -Twiga umetilia mkazo sekta zote muhimu zinazohitajika kwa matumizi ya binadamu kama vile elimu, uchimbaji wa visima maji, vituo vya afya, na programu mbalimbali zinazolenga kusaidia wananchi wa eneo linalozunguka mgodi.

“Tumeambiwa na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu kwamba muda wa maisha ya mgodi wa Bulyanhulu ni miaka 25 ijayo, hivyo bado Bunge, Serikali na mgodi wenyewe tunapaswa kuendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha faida za uwepo wa mgodi zinasambaa kwa wananchi wa kawaida na nchini kwa ujumla pamoja wakati wa kipindi chote hiki,” alibainisha.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa amewataka makampuni mengine ya madini nchini kuiga mwenendo wa mgodi wa Barrick-Twiga katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku katika sekta ya uchimbaji madini.

Alisema kuwa serikali kupitia wizara ya madini imeona mafanikio makubwa katika utekelezaji wa kanuni za maudhui ya ndani (Local content) na uwajibikaji wa jamii (CSR) ambazo zinakusudia kuwaondoa watanzania wa kawaida katika umaskini.

Alibainisha kuwa lengo la serikali kuanzisha kanuni hizi mbili ni kuhamasisha ushirikishwaji na kukuza uhusiano wa kijamii kati ya mgodi na wananchi wa eneo hilo lakini pia kuona Watanzania wakishiriki katika uwekezaji wa biashara ya madini nchini.

Naibu Waziri alieleza zaidi kufuata na kufanya kwa ufanisi maudhui ya ndani na uwajibikaji kwa jamii na kufungua milango kwa watanzania kushiriki katika biashara ya uchimbaji madini ni mafanikio yanayoleta ustawi wa jamii.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick -Twiga Bulyanhulu, Victor Lule alisema kampuni inashukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa ziara rasmi kwenye mgodi huo ambayo inawawezesha kuelewa shughuli za mgodi na utendaji kazi wake wa kila siku kuanzia utafiti , uchakataji na taratibu zingine ndani ya mgodi.


Alisema mgodi unatekeleza kikamilifu kanuni za uwajibikaji wa jamii (CSR) na sheria za CSR na maudhui ya ndani kwani unalenga hasa kuhamasisha na kujenga uwezo wa Watanzania.


“Tunaendelea kuwafundisha na kuwajengea uwezo wafanyakazi wetu kuhusu matumizi ya mashine za kisasa za uchimbaji madini, teknolojia na ujuzi wa kiufundi ili kuhakikisha kuwa tuna rasiliamali watu wenye uelewa wa kutosha wa teknolojia kwa sababu pia tuna watalaamu wachache kutoka nje na ni muhimu ujuzi wao unabaki hapa nyumbani ,” alibainisha.

“Hadi sasa, tuna asilimia 11 ya wanawake katika nafasi mbalimbali hapa Bulyanhulu, tunatekeleza tunachosema tunapohamasisha wanawake katika sekta ya uchimbaji madini hapa nchini,” alieleza.


Alisisitiza kuwa kampuni ya hiyo ya uchimbaji madini itaendelea kuelimisha wajasiriamali na wasambazaji wa ndani jinsi ya kufanya biashara na makampuni ya madini, jinsi ya kusajili makampuni yao na kushiriki katika warsha za mafunzo, semina na mikutano ili kujenga uhusiano wa kudumu na wenye manufaa kwa nchini nzima.

Bwana Lule alieleza kuwa kampuni ya madini ina asilimia 96 ya wafanyakazi wake ambao ni Watanzania, baadhi yao wakiwa kwenye ngazi za usimamizi, jambo linalothibitisha wazi kuwa Barrick -Twiga inakuza dhana ya maudhui ya ndani.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakiwa katika sehemu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu
Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa akizungumza wakati wa ziara hiyo
Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa

Share:

KIJANA ASHANGAA MAPENZI YA MAMA YAKE MZAZI!

Kuna siku kulijitokeza kisa cha kushangaza mtandaoni baada ya kijana mmoja, Moses, 19, kudai kuwa mama yake bado anamchukulia kama mtoto mdogo, anasema kutokana na kuwa mtoto pekee na wa kiume analizimika kukubaliana na jambo hilo. 

Moses anadai kuwa mama yake bado anataka kumnyonyesha angali tayari ni mtu mzima, mama yake hukasirika anapomkataa kila anapomvuta karibu ili kumpa titi zake laini.

Anafichua kwamba mama yake, mwanamke wa makamo katikati ya miaka 49 hivi anaendelea kuvuka mipaka yake, mara nyingi humuomba kulala naye kitandani. 

Baba yake aliondoka nyumbani wakati Moses akiwa na umri wa miaka minne tu, na tangu wakati huo mama yake ndiye aliyekuwa akimtunza na hadi sasa amekuwa mtu mzima ambaye siku sio nyingie naye atakuwa na familia yake. 

Kijana huyo anahisi kuna kitu hakipo sawa kwa mama yake kwani kuna wakati anamuomba asitongoza wasichana akisema kwamba yey anamtosha na atampa chochote anachotaka kama mwanaume. 

"Ananiambia 'nakupenda' kila siku na hata akanibusu kwenye midomo, ninaogopa nimkimbia najua ataweza atajiua, kama mtoto wake wa pekee na nilitaka kutafuta suluhisho ili tuweze kuishi katika nyumba moja bila kufanya chochote kile," alisema Moses. 

Moses anasimulia matukio kadhaa ambapo mama yake alimtaka alale chumbani kwake na kumwambia asiogope kufanya hivyo, lakini bado alikuwa na wasiwasi kutokana na kuongezeka kwa visa vya unyanyasaji wa kingono. 

Hatimaye mjomba wake Moses alilazimika kuingilia kati suala hilo na kumuagiza mama huyo kwenda kwa Kiwanga Doctors kupata tiba ili kuondoka na tabia hiyo ambayo ni laana kama mama kutembea na mtoto wake wa kiume. 

Moses anasema tangu mama yake kupatiwa tiba na Kiwanga Doctors tabia yake ilibadilika kabisa, wakaweza kuisha kwa kuheshimiana ndani ya nyumba kama mtoto na mzazi wake. 

"Kiwanga Doctors alinisaidia sana mimi na mama yangu kukubaliana na ukweli kuwa uhusiano wetu ulipaswa kuwa kama mtoto na mzazi na sio mtu na mpenzi wake kama alivyokuwa anataka". 

"Nashauri yeyote mwenye shida kama niliyokuwa nayo basi awasiliane na Kiwanga Doctors kwa namba +254 769 404965 kwa maelezo zaidi," alisema Moses. 

Anasema ana mamlaka ya kufanya kazi ndani ya saa 24 kwa kutumia matambiko, uchawi na hirizi zake, Kiwanga Doctors anashughulikia matatizo kama kushinda kesi mahakamani, kushinda bahati nasibu, ulinzi wa familia na mali pamoja na kukutabiria nyota ya maisha yako. 

Mwisho. 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 16,2025

 

magazeti leo










Share:

Saturday, 15 February 2025

MAMA MKWE AWEKA UCHAWI CHUMBANI KWETU!

Jina langu ni Sarah mkazi wa Kandara huko Muranga nchini Kenya. Nimekuwa nikiishi katika hali ya misukosuko ya mara kwa mara, nikijiuliza kwa nini mimi na mume wangu tumekuwa na migogoro ya ndoa. 

Jibu la tatizo langu lilikuja kwa namna ambayo sikuitarajia ambapo rafiki yangu mmoja alinielekeza kwa Kiwanga Doctors ambao ni 

waganga wa kienyeji wanaojulikana kwa uhodari wao wa kutatua changamoto mbalimbali za maisha. 

Kwa moyo mzito na hitaji la kupata majibu, niliamua kuwatembelea. Sikujua kwamba uamuzi huo ungefanya kazi na kufichua mambo ambayo nilikuwa siyajui na ndio hasa yalikuwa yakileta migogoro katika ndoa yangu. 

Baada ya kufanyiwa dawa na Kiwanga Doctors, niligundua kuwa mama mkwe wangu alikuwa akitumia hirizi kuleta fujo katika ndoa yangu.

Kusudi lake lilikuwa kuzidisha migogoro ili mimi na mume wangu tupeane talaka. 

Ufunuo huo uliniacha na butwaa. Mwanamke niliyemheshimu na kumchukulia kama mama yangu mzazi ndiye aliyesababisha misukosuko katika ndoa yangu.

Nikiwa nimeazimia kuokoa ndoa yangu, niliamua kupambana na moto kwa moto. 

Nililipa Ksh3000 kwa  Kiwanga Doctors ambao walinihakikishia kwamba matambiko yao yatakabiliana na athari za hirizi ambazo mama mkwe alikuwa akitumia.

Siku tatu baadaye, nilimkamata mama mkwe wangu akicheza mbele ya chumba chetu cha kulala.

Alishtuka kuniona na kwa mshangao wake akakubali kile alichokuwa akifanya. Kuonekana kwa dansi yake na kukiri maovu yake ilikuwa dalili ya wazi kwamba dawa za kuikinga ndoa yangu zilikuwa zikifanya kazi. 

Aliomba msamaha na kuahidi kutoingilia ndoa yetu. Leo, mimi na mume wangu katika ndoa tuna furaha. Tumefanikiwa kuondokana na changamoto zilizokuwa zikitishia kutuachanisha. 

Upendo wetu kwa kila mmoja wetu umeimarika, na tumeungana zaidi kuliko hapo awali. Jambo hili limenifunza umuhimu wa kuwa karibu na waganga wa kienyeji katika kutatua migogoro ya ndoa. Basi wasiliana na Kiwanga Doctors kwa namba +254 769404965 ili kupata huduma. 


Share:

ANDENGENYE AWAONYA WAFANYABIASHARA WANAOINGIZA MAGENDO NCHINI

Mkuu wa wilaya ya Kigoma Rashid Chuachua akizungumza wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa wafanyabiashara wa mkoa Kigoma iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Naibu Kamishna wa forodha na ushuru wa bidhaa TRA Makao Makuu, Julieth Nyomolelo
Naibu Kamishna wa forodha na ushuru wa bidhaa TRA Makao makuu Julieth Nyomolelo (kulia) akikabidhi tuzo kwa mfanyabiashara wa mkoa Kigoma Kilahumba Kivumo (kushoto) ambaye amekuwa mmoja wa wafanyabiashara waliofanya vizuri mkoani Kigoma
Sehemu ya wafanyabiashara na wageni waliohudhuria utoaji tuzo kwa wafanyabiashara wa mkoa Kigoma waliofanya vizuri katika ulipaji kodi

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

MKUU wa mkoa Kigoma Thobias Andengenye amekemea wafanyabiashara wa mkoa huo wanaoingiza bidhaa nchini kupitia ziwa Tanganyika  bila kufuata taratibu wa kulipa ushuru (Magendo) wamekuwa wakiikosesha serikali mapato na hivyo kutoa onyo kwamba adhabu kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.


Andengenye alisema hayo katika hafla ya utoaji tuzo kwa wafanyabiashara wa mkoa Kigoma iliyoandaliwa na Mamlaka ya mapato kutambua mchango mkubwa wa wafanyabiashara hao katika kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati hivyo kuifanya mamlaka hiyo kufikia lengo la ukusanyai.


Pamoja na kutoa onyo hilo  Mkuu wa wilaya Kigoma, Dk.Rashid Chuachua ambaye alimwakilisha Mkuu wa mkoa Kigoma alisema kuwa anaipongeza TRA kwa kazi kubwa ya kukusanya kodi na kufikia malengo ya ukusanyaji yaliyowekwa jambo ambalo linaifanya serikali kuweka mazingira wezeshi ya kuifanya mamlaka hiyo kutimiza malengo yake kwa ufanisi.


Katika hotuba iliyotolewa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya Kigoma Rashid Chuachua alisema kuwa ukwepaji kodi sambamba na wafanyabiashara wasiotumia mashine za kielektroniki kumesababisha serikali kupoteza mapato hivyo amepota onyo kwa wafanyabiashara wanaofanya hivyo kuacha mara moja huku akiipongeza TRA kuongeza ukusanyaji mapato ambako kumeifanya serikali kutekeleza miradi mikubwa Kwenda kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla hiyo Naibu Kamishna wa forodha na ushuru wa bidhaa TRA Makao Makuu, Julieth Nyomolelo amesema kuwa uingizaji wa bidhaa nchini bila kulipiwa kodi kwa njia ya magendo  imekuwa changamoto kubwa ambayo inavuruga malengo ya mamlaka hiyo katika kufikia lengo la ukusanyaji mapato nchini.

Naibu Kamishna wa forodha na ushuru wa bidhaa alisema kuwa ulipaji kodi kwa hiari kwa kufuata taratibu za kisheria kulingana na biashara iliyofanyika inatija kubwa katika kuongeza makusanyo ya mamlaka hiyo sambamba na kufikia au kuvuka lengo lililoweka hivyo ametoa wito kwa watu wote kufuata taratibu na kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati.

Mmoja wa wafanyabiashara waliopewa tuzo kwenye hafla hiyo, Kilahumba Kivumo alisema kuwa mabadiliko ya utendaji ya maafisa wa TRA ambayo yametokana na vikao vya mara kwa mara wanavyofanya imekuwa chachu kwa wafanyabishara kulipa kodi kwa hiari na kuwaita maafisa hao kuwapa ushauri badala ya kuwakimbia.


Share:

MSAJILI WA MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA NCHINI ASISITIZA MASHAURI KUISHA KWA WAKATI NA KWA HAKI




Dar-es-Salaam 

Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya nchini, Bi. Stella Tullo amesisitiza umuhimu wa mashauri kumalizika kwa wakati na kwa Haki ili kuhakikisha wananchi wanapata haki za 
umiliki wa ardhi zao kwa haraka kwani ardhi ni rasilimali muhimu ya kuwawezesha kuendesha 
shughulli za kujipatia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. 

Bi. Tullo ameyasema hayo Februari 12, 2025, alipokutana na mawakili wa kujitegemea katika 
kikao kazi kilichofanyika kwenye ofisi za ndogo za Wizara ya Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, jijini Dar es Salaam. 

Katika kikao hicho, Bi.Tullo amewataka mawakili na wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi jijini Dar es Salaam kufanya kazi kwa weledi, uwajibikaji na kuzingatia muda wa mashauri ili kuharakisha  uamuzi wa kesi.

Ameeleza kuwa lengo ni kuhakikisha mashauri yote yanamalizika ndani ya muda mfupi, huku akisisitiza kuwa mashauri yaliyodumu Barazani zaidi ya miaka miwili  yanapaswa kupewa kipaumbele zaidi yamalizike kwa haki na kwa haraka ili kupunguza msongamano wa kesi. 


Aidha, Bi.Tullo amewapongeza wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi jijini Dar es Salaam kwa  ushirikiano wao mzuri na wadau wa utoaji haki.

Msajili ameridhishwa na juhudi zao za kutoa elimu kwa wananchi kuhusu taratibu za mashauri ya ardhi, pamoja na ushiriki wao wa dhati katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini. 

"Tumeona maendeleo chanya kutokana na ushirikiano wenu na mihimili mingine ya utoaji haki. Ni muhimu tuendelee kushirikiana ili kuhakikisha haki inatendeka kwa wakati," alisema Bi. Tullo. 


Kwa upande wake Wakili Geofrey akizungumza kwa niaba ya mawakili wa kujitegemea, amemshukuru Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kwa kuitisha kikao hicho na kusema wamepa fursa ya kujadili changamoto na kupata suluhisho la pamoja kwa 
ajili ya kuboresha utendaji kazi. 

"Tunamshukuru Bi.Tullo kwa kutupa nafasi ya kushiriki kwenye kikao hiki muhimu.Tumepata 
fursa ya kujadili masuala muhimu ambayo yameimarisha mahusiano yetu na kutukumbusha 
wajibu wetu wa kuhakikisha mashauri yote yanamalizika kwa wakati," alisema Wakili Geofrey. 


Mabaraza ya Ardhi na Nyumba nchini yamekuwa na jukumu muhimu katika kuhakikisha 
migogoro ya ardhi inatatuliwa kwa wakati na kwa haki. Hatua hii ya Msajili wa Mabaraza ya 
Ardhi inatarajiwa kuongeza ufanisi na kurahisisha utoaji wa haki kwa wananchi nchini kote.

Share:

Ngoma Mpya ya Moto !! KISIMA MAJABALA - KAKA JAMBAZI

Share:

Friday, 14 February 2025

KAPINGA ASHIRIKI KIKAO CHA MAWAZIRI WA KISEKTA ARUSHA

📌 Tanzania, Rwanda, Uganga kusaini MOU kuendeleza mradi wa kufua umeme wa pamoja wa Nsongezi

📌 Baraza kusimamia Kongamano na Maonesho ya 11 ya Petroli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Machi 5 hadi 7 2025 Jijini, Dar es Salaam.

**
Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga leo Februari 14, 2025 amemuwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko kwenye Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la kisekta la Nishati, Petroli na Madini la Jumuia ya Afrika Mashariki Jijini Arusha.

Baraza la kisekta limekutana kujadili miradi ambayo inatekelezwa ambayo ni pamoja na mradi wa kufua umeme wa Nsongezi utakaotekelezwa na Nchi za Tanzania, Rwanda na Uganda ambapo Mawaziri husika watasaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya utekelezaji wa Mradi huu.

Aidha, Baraza hili linasimamia Kongamano na Maonesho ya 11 ya Petroli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambalo litafanyika tarehe 5 hadi 7 Machi 2025 Jijini, Dar es Salaam.

Uenyeji wa Tanzania katika kongamano hilo unatokana na maamuzi ya mkutano wa 16 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta lililofanyika Mwezi Februari 2024 ambalo liliamua Tanzania kuwa Mwenyeji wa Kongamano hilo.

Share:

WANACHAMA WA CCM MASASI WAONYWA KUENDEKEZA MAKUNDI NDANI YA CHAMA

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mtwara ndg Mobutu Malima akizungumza na wajumbe wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Masasi Mohamed Lawa
Bi Mariam Kasembe Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya Masasi



Na Regina Ndumbaro - Masasi. 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mtwara, Ndg. Mobutu Malima, amewataka wanachama wa CCM wilaya ya Masasi kuepuka siasa za makundi ndani ya chama, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Masasi, Malima amesisitiza umuhimu wa mshikamano na umoja ndani ya chama ili kuhakikisha ushindi wa CCM katika uchaguzi ujao. 


Ameonya kuwa siasa za makundi zinaweza kudhoofisha chama na kuhatarisha mafanikio yake.


Katika hotuba yake, Malima pia amewataka wanachama kuwa waangalifu na wale wanaotangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwa ni pamoja na ubunge na udiwani akisemavbaadhi ya watia nia wamekuwa wakizunguka majimboni na kuwalaghai wanachama, jambo ambalo halikubaliki.


Amewatahadharisha watia nia hao kuacha mara moja tabia hizo, kwani tayari wamebainika na chama hakitasita kuchukua hatua kali dhidi yao. 


Amesema CCM ina taratibu zake za kupata viongozi na hakuna haja ya kufanya kampeni za chinichini kabla ya wakati rasmi.


Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Masasi, Bi Mariam Kasembe, amemshukuru Katibu wa Mkoa kwa hotuba yake yenye maelekezo mazuri kwa wanachama akisema lengo ni kujenga chama.

Bi Kasembe amewataka wanachama wa CCM wilayani Masasi kuwa waaminifu kwa Chama na kufuata taratibu zilizowekwa ili kudumisha mshikamano. 

Amesema chama hakiwezi kuvumilia vitendo vinavyoweza kusababisha migawanyiko.


Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama katika ngazi ya wilaya na kata, ambapo walionesha mshikamano na kueleza dhamira yao ya kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.


Wanachama wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliopata nafasi ya kuzungumza wameonyesha kuridhishwa na hotuba ya Malima na kuahidi kushirikiana kwa karibu na uongozi wa chama ili kuhakikisha wanatekeleza maagizo yaliyotolewa kwa manufaa ya chama na jamii kwa ujumla.
Share:

Thursday, 13 February 2025

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA UONGOZI WA KISIASA


Waandishi wa habari wametakiwa kuendelea kuwaelimisha wanawake kuhusu umuhimu wa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania upande wa Zanzibar TAMWA-ZNZ, Dkt. Mzuri Issa, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliyofanyika huko Tunguu.

Dkt. Mzuri amesema kuwa licha ya waandishi wa habari kufanya kazi kubwa ya kuelezea changamoto zinazowakumba wanawake kwenye kuwania nafasi za uongozi pamona na kueleza umuhimu wa kuwa na uwiano sawa katika nafasi za uongozi, bado kuna kazi ya ziada ya kuwaelimisha wanawake ili waongeze ujasiri wa kujitokeza kugombea nafasi za uongozi katika vyama vya siasa.

"Wanawake wengi wana uwezo wa kuongoza, lakini tatizo kubwa ni ukosefu wa kujiamini. Hili ni jambo ambalo waandishi wa habari wanapaswa kulifanyia kazi kwa kuandaa vipindi vinavyoelimisha na kuwahamasisha wanawake," alisema Dkt. Mzuri.

Ameongeza kuwa redio zimekuwa zikiifanya kazi kubwa katika kutangaza mambo yanayohusu jamii, hivyo waandishi wanapaswa kuendelea kuandaa vipindi vyenye tija vinavyohamasisha ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.

Aidha, akizungumzia kaulimbiu ya Siku ya Redio Duniani kwa mwaka huu inayosema “Redio na Mabadiliko ya Tabianchi”, Dkt. Mzuri amebainiaha kuwa vyombo vya habari vina jukumu muhimu katika kuelimisha jamii kuhusu athari za uharibifu wa mazingira na jinsi ya kupambana na ongezeko la joto duniani.

Kwa upande wao, waandishi wa habari waliohudhuria maadhimisho hayo wamesema kuwa redio nyingi kwa sasa zimejikita zaidi kwenye masuala ya kibiashara badala ya kutoa maudhui yanayolenga maendeleo ya jamii.

Wameeleza kuwa baadhi ya vipindi vya redio vimegeuka kuwa sehemu za ushabiki, hasa kwenye michezo, ambapo mijadala mingi inajikita kwenye timu za Simba na Yanga badala ya kuzungumzia changamoto za msingi zinazoikumba jamii.

Waandishi hao wamependekeza kuwa redio zirudi kwenye misingi yake ya awali kwa kuhakikisha zinatoa vipindi vinavyolenga maendeleo ya jamii, hususan katika kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika siasa na uongozi.

Waandishi wa habari wana jukumu kubwa la kuwaelimisha na kuwahamasisha wanawake kujitokeza kugombea nafasi za uongozi. Kupitia redio, wanawake wanaweza kupata taarifa sahihi na motisha ya kushiriki katika siasa, hatimaye kuchangia maendeleo ya jamii kwa ujumla.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger