Friday, 22 November 2024
VETA KIHONDA YASISITIZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WAHITIMU ILI KUJIAJIRI
Thursday, 21 November 2024
JTC YATEMBELEA MTO MALAGARASI AMBAO NI SEHEMU YA MPAKA WA TANZANIA NA BURUNDI
Wednesday, 20 November 2024
IAA YAJIKITA KUIMARISHA HUDUMA ZAKE KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA
Katika ziara hiyo Uongozi wa IAA umetembelea ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza na kukutana na Mheshimiwa Balozi Mbelwa Brighton Kairuki.
Mhe. Balozi amekipongeza Chuo kwa juhudi zake katika kuboresha elimu na pia amejadiliana na viongozi juu ya fursa mbalimbali zilizopo nchini uingereza katika sekta ya elimu na nyinginezo.
Aidha , Novemba 19, 2024 Mkuu wa Chuo Prof. Eliamani Sedoyeka na timu yake wametembelea ARU university (Anglia Ruskin University) mjini Cambrigde ambapo pamoja na mambo mengine mengi wamejadili masuala mbalimbali ya kitaaluma, tafiti na ushauri. Lengo ikiwa ni kujifunza na kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuendelea kuboresha ufundishaji, ujifunzaji na huduma mbalimbali zinazotolewa na Chuo.
Prof. Sedoyeka ameeleza kuwa, ajenda ya serikali ni kuhakikisha Taasisi za Elimu ya Juu zinatoa huduma kwa hadhi ya Kimataifa na IAA kama Taasisi ya Umma tumejipanga kuhakikisha kuwa tunatoa huduma katika ubora wa kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuwa na mitaala inayokidhi viwango vya kimataifa, kuongeza udahili wa wanafunzi wa kimataifa na kuhakikisha wahitimu wetu wanakidhi soko la ajira la ndani na lile la kimataifa.
Katika ziara hiyo Chuo kinatarajia kutembelea vyuo vingine ikiwemo Oxford university, Nottingham University, commonwealth AI academy pamoja na kukutana na Watanzania (Diaspora) waishio Uingereza ambao ni wataalam katika sekta za fedha, uhasibu, uchumi, tehama na nyingine nyingi.
SIMBA SC YAZINDUA JEZI MPYA!!
News Alert! MUDA WA KUPIGA KURA SAMIA KALAMU AWARDS UMEONGEZWA MPAKA NOVEMBA 25! Kura yako ni Muhimu

Zoezi hili linawahusisha wananchi ambao ndio walaji wa maudhui ya habari na ambao watakuwa na nafasi ya kuchangia asilimia 60 ya matokeo. Asilimia 40 ya alama zitakuwa zimetolewa na jopo la majaji kulingana na vigezo vya kitaaluma.
Huu ni wakati muhimu ambapo wananchi wanapata nafasi ya kutoa maoni yao kwa kupiga kura na kutoa maamuzi ya mwisho.
Wanahabari na vyombo vya habari vilivyokidhi vigezo vya kitaaluma vya uandishi wa habari za maendeleo ndivyo vitakavyoshiriki katika tuzo hizi. Makala 1,131 zilizowasilishwa kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar kuwania Tuzo hizi, zimepitia mchakato wa uchambuzi wa kitaaluma na kazi 85 zilizokidhi vigezo zimewekwa kwenye tovuti ya www.samiaawards.tz na kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram (@samiakalamuawards), YouTube, na Facebook (Samia Kalamu Awards).
-
- Tembelea tovuti ya www.samiaawards.tz
- Fungua sehemu iliyoandikwa "Piga Kura"
- Chagua makundi ya Tuzo na namba ya mshiriki kwa kuangalia picha na kazi aliyochapisha
- Bofya Piga Kura ili kumchagua mshindi unayemtaka.
-
Kupiga Kura Kupitia Simu ya Kiganjani
- Nenda kwenye sehemu ya kutuma ujumbe wa kawaida (SMS)
- Andika neno “Kura”, acha nafasi, kisha weka namba ya mshiriki
- Tuma ujumbe kwenda namba 15200
- Utapokea ujumbe wa kuthibitisha kuwa kura yako imepokelewa.
Kaulimbiu ya Tuzo: "Uzalendo Ndio Ujanja"
Tuzo za Samia Kalamu Awards zimegawanywa katika makundi matatu makuu:
- Tuzo Maalumu za Kitaifa
- Tuzo za Vyombo vya Habari
- Tuzo za Kisekta
Lengo kuu la tuzo hizi ni kuhamasisha, kukuza na kupanua wigo wa uandishi wa habari za ndani kupitia vyombo vya habari vya asili na mitandaoni, ili kuchochea maendeleo, uwajibikaji, na kujenga taswira nzuri ya taifa letu.
Tunaomba Ushiriki Wenu!
Karibuni wananchi na wadau wa habari kushiriki kwa wingi katika mchakato huu wa upigaji kura ili kuhakikisha tunapata washindi wanaostahili.
Kwa maelezo zaidi, tembelea www.samiaawards.tz au wasiliana nasi kupitia namba +255716622200 na 0800008272
Kura Yako Ni Muhimu!
Jiunge na zoezi hili la kihistoria na changia kwenye ujenzi wa taifa letu kupitia uandishi wa habari bora.
Tuesday, 19 November 2024
RAIS SAMIA AMUAGIZA WAZIRI MKUU KUHARAKISHA UOKOAJI KARIAKOO

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesikitishwa na ajali ya kuporomoka kwa ghorofa, Kariakoo Mtaa wa Mchikichi na Kongo jijini Dar es Salaam, ambapo amemwagiza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa kushirikiana na timu za uokoaji kuhakikisha kazi hiyo inafanyika kwa haraka na ufanisi.
Kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii ikiwemo 'Instagram' na 'WhatsApp channel' Rais Samia ameandika: " Hivi punde nimezungumza kwa kirefu na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mbunge) kuhusiana na ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa katika Kata ya Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam, na kazi ya uokoaji inayoendelea.
Nimempa maelekezo kuhakikisha kazi hii inafanyika kwa haraka na ufanisi, na niendelee kupata taarifa ya kila hatua ya maendeleo yake"
Akionesha masikitiko yake Rais Samia amesema: Nimesikitika kupokea taarifa ya ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa katika Kata ya Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam.
Nimeuagiza Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, na Idara ya Menejimenti ya Maafa kufanya kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi.
Wakati hilo likiendelea na tukimuomba Mwenyezi Mungu awape pona ya haraka majeruhi, tuwaombee pia utulivu na subra ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wenzetu wanaotafuta riziki zao katika eneo hili muhimu kibiashara nchini ambao kwa namna mbalimbali wameathiriwa na ajali hii.




























































