Thursday, 27 July 2023

KATIBU MKUU CCM APIGILIA MSUMARI UWEKEZAJI BANDARI DAR, ATOA MAELEKEZO KWA SERIKALI


****************

Na Mwandishi Wetu,- Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Daniel Chongolo amesema Chama hicho kinaelekeza Serikali kuisukuma na kuongeza spidi katika kuhakikisha mjadala wa uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam unafika mwisho ili wananchi waanze kuona matokeo yake.

Chongolo ameyasema hayo leo Julai 26,2023 wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mwanga Center ambapo ametumia nafasi hiyo kuitaka Serikali isiingie kwenye maneno ya siasa na badala yake wasimame kwenye hoja na hatimaye bandari iongeze ufanisi.

"Tunanachotaka ni kuona bandari inaongeza ufanisi,inaletea matokeo na inachangia pato kubwa la Taifa na kuongeza tija kwa nchi ya kuwahudumia Wananchi na sio vinginevyo.Mambo yote ya maneno maneno,siasa hizi tusizipe nafasi.

" Sisi ndio tumepewa dhamana ya siasa,sisi tunakuja kuzungumza na wanasiasa wenzetu na Watanzania waliotupa dhamana,Serikali mambo yao ni ya kutenda na kuleta matokeo,na wasifanye mchezo hata kidogo kutosimamia maslahi ya nchi kwa kila wanachokifanya’’,amesema Chongolo.

Aidha Chongolo alieleza hatua kwa hatua kuhusu uamuzi wa Serikali kuingia makubaliano ya uwekezaji wa kuboresha uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam huku akifafanua lengo kuu ni kuhakikisha bandari hiyo inatoa huduma kwa ufanisi mkubwa.







Share:

Wednesday, 26 July 2023

MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI 41 SHINYANGA, RATIBA HII HAPA KUANZIA KESHO


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Julai 26,2023- Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Julai 26,2023
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akizungumza na waandishi wa habari

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mwenge wa Uhuru utapokelewa Mkoani Shinyanga ukitokea mkoani Simiyu Alhamisi Julai 27,2023 ukitarajiwa kuweka Mawe ya Msingi, kufungua na kuona jumla ya Miradi 41 yenye thamani ya Shilingi 14,027,687,009.20.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatano Julai 26,2023 , Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amesema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika shule ya msingi Buganika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu.


“Katika Mkoa wa Shinyanga Mwenge wa Uhuru utakimbizwa umbali wa kilomita 571.5 ambapo utaweka Mawe ya Msingi, kufungua na kuona Jumla ya Miradi 41 yenye thamani ya Shilingi 14,027,687,009.20”,amesema Mhe. Mndeme.

“Katika Miradi hiyo,Miradi 11 itawekewa Mawe ya Msingi ikiwa na thamani ya Shilingi 7,841,516,050.00, Miradi 14 Itazinduliwa ikiwa na thamani ya Shilingi 3,308,062,056.20, Miradi 4 Itafunguliwa ikiwa na thamani ya Shilingi 1,321,826,665.00 na Miradi 12 Itaonwa ambayo inathamani ya Shilingi 1,556,282,238.00”,ameongeza.

Amefafanua kuwa Miradi hiyo imegharamiwa na Serikali Kuu Shilingi 8,740,635,261.40 huku Halmashauri zikichangia Shilingi 3,921,724,028.00 bila kusahau nguvu za wananchi shilingi 116,464,744.80 ,Sekta binafsi na Wahisani mbalimbali 1,248,862,975.00.


“Nichukue fursa hii kuwaalika na kuwakaribisha Wananchi wote katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utapita ikiwemo sehemu ya kuupokea, Mkesha, na kwenye miradi yote wananchi mjitokeze kwa wingi katika maeneo hayo”,amesema Mndeme.


Ameyataja maeneo ya mkesha wa mwenge wa Uhuru kuwa ni Uwanja wa Stendi ya Mabasi Maganzo (Kishapu), Uwanja wa Sabasaba (Manispaa ya Shinyanga), Uwanja wa Shule ya Msingi Didia (Halmashauri ya Shinyanga), Kituo cha Uwekezaji Nyihogo (Manispaa ya Kahama), Uwanja wa Mseki – Bulungwa (Ushetu) na Uwanja wa Shule ya Msingi Kakola A (Msalala).


Share:

MGEJA ASHITUKIA MCHEZO MCHAFU WA KUITAKA KUICHAFUA SERIKALI


Khamis Mgeja

Na Mwandishi wetu -Kahama

KHAMIS MGEJA ambaye ni mjumbe wa mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga amewatahadharisha wanachama wenzake wa CCM kutahadhari na michezo michafu inayofanywa na baadhi ya watu wasioitakia mema nchi ya Tanzania.

Mgeja ametoa kauli hiyo juzi kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya kisasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ukumbi wa mikutano ya kijiji cha Wame kata ya Kilago wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo yeye binafsi alichangia matofali 200 na fedha taslimu shilingi 100,000.

“Niwapongeze viongozi wetu wa CCM wa Tawi hili la Wame, kwa kweli wameona mbali kuitisha harambee hii, maana Tawi hili limo ndani ya kata ya Kilago ambayo mimi ndiye mwakilishi wake katika mkutano mkuu wa CCM wa mkoa, hivyo lazima Ofisi zetu za chama ziwe ni zile zenye ubora, na iwe mfano kwa wengine,” alieleza.

Akizungumzia kuhusu upotoshaji wa baadhi ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali Mgeja alisema ni ukweli usiopingika kwamba Serikali ya awamu ya sita ina nia njema ya kuwaletea wananchi wake maendeleo lakini bado kuna kundi la watu wachache wanaopotosha ukweli wa mambo yanayotekelezwa.

Akitoa mfano kuhusu upotoshaji huo alisema ni suala la Bandari linakuzwa na kupotoshwa ukweli wake huku ikidaiwa kwamba Bandari ya Dar es Salaam imeuzwa lakini siyo kweli, na kwamba hakuna Serikali yoyote duniani inayoweza kuuza ardhi ya wananchi wake kwa watu wengine lengo ikiwa ni kuichafua Serikali na ichukiwe na wananchi wake.

Mgeja ambaye ni miongoni mwa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga alisema yeye binafsi amebaini kuwepo kwa mchezo mchafu ambao umelenga zaidi kutaka kuwagombanisha watanzania na Serikali yao kwa kusambaza uongo ili wananchi waone hakuna kinachofanyika.

Alisema wanaosambaza habari za uongo mfano huo wa Bandari lengo lao ni kuwatoa watanzania katika kufikiria mambo muhimu ya kimaendeleo yanayotekelezwa na Serikali hivi sasa na badala yake wabaki wakiishutumu Serikali kwa madai haina jambo lolote la maana inalolitekeleza katika kuwaletea maendeleo tarajiwa.

“Nichukue nafasi hii kuwaomba na kuwatahadharisha watanzania wenzangu na wana CCM kwa ujumla, kwa sasa tunapita kwenye kipindi kigumu sana, hivyo lazima tuwe makini tuwaepuka na kuwaogopa kama ukoma wale wanaotutengenezea michezo michafu kwa lengo la kutaka kuichafua Serikali iliyoko madarakani hivi sasa,”

“Yapo baadhi ya mambo yanapotoshwa sana, mfano suala hili la bandari, limekuzwa ili tu lionekane halifai na Serikali imefanya “kituko” kikubwa kutaka kuibinafsisha, hadi watu wamefikia hatua ya kutoa lugha zisizokuwa za staha, kwa mfano kudai suala la bandari watu walitumia akili za matope, hii haikubaliki,” alieleza Mgeja.

Alisema kitendo cha kuendeleza mashambulizi dhidi ya Serikali na Bunge ni kutaka kumchafua Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na mhimili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku wakijitahidi kuhamisha mawazo ya watanzania wajikite zaidi kwenye malumbano yasiyokuwa na maana badala ya kuwaza maendeleo.

“Sasa ndugu zangu niwaulize jambo moja hivi kweli kuna Serikali yoyote duniani inayoweza kudiriki kuuza nchi yake? Inashangaza kabisa wenzetu hawa suala la bandari ndiyo wamelivalia njuga, wanapiga kelele wakidai eti bandari imeuzwa, bandari imeuzwaaa, niwaombe watanzania na wana CCM wote wenye nia njema wapuuze kauli hizi za upotoshaji,”

“Haiwezekani wala haitatokea, Serikali hii ya CCM kuamua kuuza hata kipande kimoja cha ukubwa wa sentimeta moja ya ardhi kwa mtu ye yote asiyekuwa mtanzania, zipuuzeni hizi kelele za bandari imeuzwa, siyo kweli, na Serikali imetoa ruhusa kwa ye yote mwenye mawazo zaidi ya kuiendesha vizuri basi ajitokeza na apeleke ushauri wake,” alieleza Mgeja.

Aliwaomba watanzania wote wenye nia njema na nchi yao waendelee kuiunga mkono Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ili iendelee kuwaletea maendeleo badala ya kuiwekea vikwazo mbalimbali huku wakiikosoa pasipo utaratibu kwa kutumia maneno yasiyokuwa na staha dhidi ya viongozi wake wa Chama na Serikali.

Mgeja alitoa wito kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini kote wawe mabalozi wazuri wa kuwaelimisha watanzania kuhusu mambo mazuri yanayotekelezwa na Serikali ya Rais Samia na kwamba suala la bandari linazungumzika na kila mwenye ushauri mzuri wa jinsi ya kuiendesha au kuingia mikataba mizuri na wawekeza amekaribishwa kutoa maoni yake.
Share:

WAZIRI MABULA ATAKA WAMILIKI WA ARDHI KULIPA KODI KWA WAKATI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi hati milki sita za ardhi mkazi wa Ngara mkoani Kagera Godfrey Niyonzima wakati wa ziara yake mkoani humo.

*****************

Na Munir Shemweta, WANMM NGARA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wamiliki wa ardhi nchini kuhakikisha wanalipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati ili kuepuka kutozwa riba ya malimbikizo ya kodi hiyo.

Dkt Mabula alisema hayo wilayani Ngara mkoa wa Kagera wakati akikabidhi hati miliki za ardhi kwa wananchi wa wilaya hiyo wakati wa ziara yake mkoani Kagera.

Aliwataka wamiliki wa ardhi nchini wanaopatiwa hati milki kuendelea kulipa kodi ya pango la ardhi kila mwaka na kubainisha kuwa, iwapo mmiliki atapitisha mwaka mmoja bila kulipa kodi basi atalazimika kulipa kodi inayoambatana na riba.

‘’kila mwaka wewe kalipe ili uwe mteja mzuri wa serikali, katika ardhi uliyo nayo usilimbilize madeni maana mwisho wa siku utakuja kushindwa na kuanza kushitakiana na serikali kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya bila sababu’’ alisema Dkt Mabula.

Dkt Mabula aliongeza kwa kusema kuwa, wizara yake imeboresha huduma zake kutoka analogia kwenda digitali unaowezesha taarifa za wamiliki wa ardhi kuwa katika mfumo wa kieletroniki na kurahisisha taratibu za utoaji hati.

‘’kwa sasa utendaji wa wizara umebadilika sana ambapo mmiliki wa ardhi anayeomba kumilikishwa anaweza kupata hati ndani ya muda mfupi iwapo atakuwa amekabilisha taratibu zote za umiliki’’. Alisema Dkt Mabula

‘’Kwetu sisi huku ambapo mifumo ya kidigitali haijakaa sawa mwombaji hati anaweza kuchukua mwezi moja ama miwili lakini kwa kule ambapo mifumo ya kidigitali ishaanza kutumika basi inaweza kabisa kuchukua hati ndani ya wiki moja’’ alisema Dkt Mabula.

Vile vile, Waziri wa Ardhi alisema kuwa, kupitia maboredsho ya huduma za sekta ya ardhi hivi sasa wamiliki wa ardhi wanapokea bili za kodi ya pango la ardhi kupitia simu zao za mkononi.

Wananchi waliopokea hati zao wameipongeza wizara ya ardhi kwa kufanya maboresho yatakayosaidia wamiliki wa ardhi kupata hati kwa muda mfupi sambamba na kupata bili za kodi kupitia simu zao za mkononi.

Mkazi wa Ngara Godfrey Niyonzima ameshukuru kwa kupatiwa hati na kukabidhiwa na Waziri mwenye dhamana ya Ardhi hasa baada ya kuzihangaikia kuzipata hati hizo kwa takriban miaka sita.

‘’kwanza nishukuru kwa kufanikisha kupata hati zangu sita za ardhi lakini pia niipongeze wizara ya ardhi kwa kufanya maboresho ambayo naweza kusema yanakwenda kurahisisha upatikanaji hati pamoja ulipaji kodi ya pango la ardhi’’ alisema Niyonzima.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemaliza ziara yake mkoani Kagera na anatarajia kuendelea na ziara zake katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Njombe, Iringa na Morogoro.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi hati milki ya ardhi kwa Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Ngara John Melele wakati wa ziara yake mkoani Kagera
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa wilaya ya Ngara aliowakabidhi hati wakati wa ziara yake mkoani Kagera. Wa pili kushoto waliokaa ni Mkuu wa wilaya ya Ngara kanali Mathias Kahabi (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Share:

POLISI SHINYANGA WAKATA MTANDAO WAUAJI 'WAKATA MAPANGA' , BUNDUKI ZA MAKAMPUNI ZIKIAZIMWA

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha vifaa vya kupigia ramli chonganishi vilivyokamatwa

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kubaini na kukamata mtandao wa wakata mapanga wanaowakodisha ili kutekeleza mauaji huku likikamata bunduki nne zilizokuwa zikitumika katika Makampuni ya ulinzi na kuazimana kinyume na sheria.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatano Julai 26,2023, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu amesema bunduki hizo zimekamatwa kufuatia misako na Operesheni mbalimbali zilizofanyika katika kipindi cha Mwezi mmoja kuanzia tarehe 22/06/2023 hadi tarehe 25/07/2023 kwa lengo la kuzuia uhalifu ili kuendelea kuuweka Mkoa katika hali ya utulivu.


“Kupitia taarifa fiche tumefanikiwa kubaini na kukamata mtandao wa wakata mapanga wanaowakodisha ili kutekeleza mauaji. Tumekamata watuhumiwa wanne. Baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa wamehojiwa na wamekiri kutenda matukio hayo sehemu mbalimbali, Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea na msako mkali kwa kushikiana na Mikoa jirani ili kuhakikisha linaukamata mtandao wote wa wakata mapanga”,ameeleza Nyandahu.


“Pia tumefanikiwa kukamata Bunduki 04 ambazo ni MARK IV yenye namba D.6000, MARK III yenye namba C.3667, MARK III yenye namba K.9234, Shotgun yenye namba 10737 ambazo zilikuwa zikitumika katika Makampuni ya ulinzi na kuazimana kinyume na Sheria, zimekamatwa risasi 73 za Shotgun, maganda 13 ya sisasi za shotgun, Risasi za Pisto 239, Pikiki 02, Bangi Kilo 2 na kete 02, Cappet vipande 02, na Waya wa Fensi Mita 12 mali idhaniwayo kuwa ya Mgodi wa Buzwagi, Mafuta ya Disel Lita 310 yaliyoibiwa katika mradi wa Reli SGR, na Vifaa vya kupiga Ramli chonganishi”,amesema Nyandahu.


Amesema katika kipindi hicho cha Mwezi mmoja kesi 33 za makosa ya Jinai zikiwa na jumla ya washitakiwa 41 ziliweza kupata mafanikio mbalimbali Mahakamani ambapo kesi moja kati ya hizo ya kujeruhi mtuhumiwa alihukumiwa miaka 10 Jela na akitoka alipe pesa Tshs. 100,000/=.

Amefafanua kuwa katika kuendelea kudhibiti matukio hatarishi ambayo yanayosababisha ajali za mara kwa mara kikosi cha Usalama barabani Mkoa wa Shinyanga kimeendelea kutoa elimu ya Usalama barabarani kwa makundi mbalimbali kupitia vijiwe vya pikipiki (bodaboda), nyumba za ibada (kanisani na misikitini), na kupitia Radio zilizopo Mkoani Shinyanga, shule za misingi na Sekondari, kwenye mikusanyiko mfano minadani.


“Hata hivyo Operesheni ya kukamata madereva wanaokiuka Sheria za Usalama Barabarani kwa makosa ya mwendokasi kwa kutumia Speed Radar na mfumo wa ufuatiliji wa Mwendo kwa mabasi ya abiria VTS (Vehicle Tracking System) inaendelea na mpaka sasa jumla ya pikipiki 882 zilikamatwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo ubovu wa pikipiki, kutovaa kofia (Helmet), kutokuwa na Leseni, kutokuwa na bima, na kuzidisha abiria.

 Magari 3,423 yalikamatwa kwa makosa mbalimbali kati ya hayo magari 673 yalikamatwa kwa kuendeshwa kwa mwendokasi na hatarishi kwa kutumia Speed Radar na VTS, Madeva 673 waliandikiwa faini za barabarani kwa magari yaliyoendeshwa kati ya 80kph na 89kph”,amesema Nyandahu.


Amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa wananchi wake kufuata Sheria za nchi na kutojihusisha na vitendo vya kiuhalifu, kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu, na litaendela kuwachukulia hatua kali za Kisheria kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo uhalifu.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatano Julai 26,2023
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akitoa taarifa kwa vyombo vya habari
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akitoa taarifa kwa vyombo vya habari
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akitoa taarifa kwa vyombo vya habari
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha bunduki zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha bunduki zilizokamatwa
Vifaa vilivyokamatwa na jeshi la Polisi
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha mali mbalimbali zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha mali mbalimbali zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Leonard Nyandahu akionesha mali mbalimbali zilizokamatwa
Share:

Tuesday, 25 July 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 26,2023





































Share:

MKUU WA MKOA WA KAGERA AONYA WANAOHATARISHA UHURU NA USALAMA WA TAIFA




Na Mariam Kagenda _ Kagera

Serikali mkoani Kagera imesema  itaendelea kuwachukulia hatua  wale wote  wanaohatarisha uhuru na usalama wa Taifa sambamba na baadhi ya watumishi wasio waaminifu wanaoshiriki  kuandikisha na kuwapa nyaraka mbalimbali za uraia watu ambao sio watanzania.


Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh.Fatma Mwassa amesema hayo wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya siku ya  mashujaa iliyotanguliwa na sala ya kuwaombea mashujaa na kutembelea makaburi  ya mashujaa hao waliopigana  vita vya Kagera mwaka 1978_1979  ambapo maadhimisho hayo yamefanyika katika kambi ya Kaboya kikosi cha 21 JWTZ wilaya ya Muleba.

Mhe. Mwassa amesema kuwa  wameisha baini baadhi na wataendelea kuchukua hatua kwani wale wote wanaowaandikisha watu ambao sio watanzania  na kuwapa hati za  kuonyesha kwamba ni  Watanzania ilihali wanajua  sio Watanzania ni raia wa nchi nyingine   hawatohamishiwa vituo vingine vya kazi bali watafukuzwa. 


Ameongeza  kuwa kuna kila sababu na wajibu wa kulinda mipaka  kwasababu Kagera ni mkoa ambao uko mpakani na umepakana na nchi nyingi na kuna mashujaa ambao walifariki kwa kupigania uhuru hivyo serikali haitokubali kuona mtu anachezea amani na anahatarisha usalama wa nchi ya Tanzania.

Amewahimiza wananchi kuendelea kuwaenzi mashujaa hao kwa vitendo na kulinda rasilimali za nchi ya Tanzania na kuwa wazalendo kama ilivyokuwa kwa mashujaa waliojitoa kwa ajili ya nchi yao.

Kwa upande wake askari mstaafu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania aliyepigana vita vya Kagera Haidari Issa amesema kuwa moja ya sababu ambayo ilipelekea kushinda vita ni umoja na  mshikamano waliokuwa nao licha ya kuwa walikuwa wanapitia wakati mgumu.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger