Wednesday, 19 July 2023
PROF. MKENDA ASISITIZA TAASISI ELIMU YA JUU KUFANYA MAPITIO YA MITAALA
NDERIANANGA AWATAKA WATANZANIA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA
Na Mathias Canal, Moshi-Kilimanjaro
Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) akiwa katika ziara mkoani Kilimanjaro amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa imani kubwa aliyompatia ya kumteua kuwa Naibu Waziri.
Akizungumza Katika mkutano na wananchi uliofanyika katika kijijini kwao Lotima ambapo ndipo alipozaliwa katika Kata ya Makuyuni ambapo ameeleza umuhimu wa shule za kata katika kuimarisha elimu nchini kwani zimeongeza chachu ya mafanikio kwa wananchi ambapo ametolea mfano yeye ambaye alisoma katika shule hizo.
Amesema kuwa Rais anafanya kazi usiku na mchana hivyo watanzania wanapaswa kumtia moyo na kumuunga mkono ili aweze kufikia dhamira ya kuwaletea maendeleo endelevu.
"Mhe Rais Samia ana upendo mkubwa na wana Kilimanjaro na sisi wanamakuyuni tumeona upendo wake, tumeona kujali kwake na kuthamini kwake" Amekaririwa Mhe Nderiananga.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Kimei amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuboresha huduma mbalimbali za maendeleo ikiwemo utengenezaji wa barabara ya Himo-Makuyuni kwa kiwango cha lami ambayo imeshaanza kutengenezwa.
Amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo utarahisisha huduma za kijamii ikiwemo usafirishaji wa mazao ya chakula na biashara.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe Kisare Makori ameshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Kwa miradi mingi ya maendeleo katika Wilaya ya Moshi.
Tuesday, 18 July 2023
SERIKALI, ABBOTT FUND KUIMARISHA SEKTA YA USTAWI WA JAMII




WAKALA WA CRDB SHINYANGA MJINI AKABIDHIWA ZAWADI YA PIKIPIKI KWA KUKIMBIZA SANA MIAMALA
JINSI YA KUCHEZA MCHEZO WA KASINO-HOT SHOTS MINES
Hii ni kwa wapenzi wa michezo isiyo ya kasino kama vile kubashiri mubashara na kucheza bahati nasibu, ni mchezo wa Hot Shots Mines. Huu ni mchezo wa mkakati wa awamu ambao ni mzuri kwa wapenzi wa soka na michezo ya kasino ya mtandaoni, mchezo huu wa Hot Shot Mines unachezwa kwenye uwanja wa soka katika msitu wa kuvutia.
Hot Shot Mines una vyumba 25, kazi yako ni kuvifungua moja baada ya jingine. Ogopa sana kadi nyekundu, hufanya kutomaliza zamu yako. Kadri unavyofungua masanduku zaidi, ndivyo unavyopata zawadi/ushindi zaidi.
Hatua ya Kucheza Hot Shots Mines Kasino ya Mtandaoni.
Unapoucheza huu mchezo wa kasino ya mtandaoni ya Meridianbet unapaswa kuchagua kadi moja, mbili, tatu, tano, saba, kumi, au kumi na tano nyekundu. Idadi ya Kadi nyekundu unazozidi kuchagua, ndivyo dau la ushindi linavyozidi kuongezeka na malipo kuwa makubwa zaidi.
Ushindi Na Malipo
Hot Shots Mines kutoka kasino ya mtandaoni ya Meridianbet una matoleo tofauti kulingana na idadi ya kadi nyekundu utakazo chagua, Malipo kwa kila toleo la mchezo ni kama ifuatavyo:
Toleo la Kadi tano nyekundu:
NB: Ukijisajili Meridianbet unapewa bonasi ya mizunguko ya bure kucheza michezo ya kasino ya mtandaoni. Jisajili na Cheza.
KUPITIA UCHUMI WA BLUU WANANCHI WANAWEZE KUJIONGEZA KIPATO
Na Oscar Assenga, TANGA
MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu amesema kuwa kupitia fursa ya uchumi wa bluu wananchi wa Jiji la Tanga wataweza kujiongezea fursa ya shughuli za kiuchumi ikiwemo kujiongezea kipato kupitia fursa za ufugaji na kilimo kupitia bahari.
Ummy ambaye pia ni Waziri wa Afya aliyasema hayo wakati alipotembelea miradi inayotekelezwa na Taasisi ya Tanga Yetu kupitia ufadhili wa Shirika la Botnar Foundation katika Jiji la Tanga huku akiwashukuru kwa kukubali ombi lake kutekelezwa miradi hiyo ambayo itasaidia kukuza uchumi wa bluu.
Miradi hiyo ni ya uvuvi, kilimo cha mwani, jongoo bahari na unenepeshaji wa kaa pamoja na ufugaji wa samaki, kuku na kilimo cha mbogamboga katika kata za Tongoni, masiwani, Tangasisi, Usagara na Central.
Aidha Botnar foundation pia wamefadhili miradi ya Afya, Elimu na kujenga Forodhani ya Tanga.
Katika miradi hiyo jumla ya fedha zilizotumika hadi sasa ni kiasi cha shilingi bilioni 5.65 zimetumika ambayo kwa asilimia kubwa zimewasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi.
Alisema kutokana na umuhimu wa uchumi wa bluu katika kukuza uchumi wa wananachi hivyo Jiji hilo limejipanga kuwa kinara katika uzalishaji wa majongo bahari, unenepeshaji wa kaa pamoja na kilimo cha mwani kwa kutumia fursa ya bahari iliyopo kwenye Ukanda wa Pwani.
Alisema kwa sababu mkoa wa Tanga una eneo kubwa la bahari na tayari mafanikio yamekwisha kuyaona hivyo tumejipanga kuongeza uzalishaji Ili tuweze kuwa vinara wa kutumia fursa za uchumi wa buluu Kwa maendeleo ya watu wetu sambamba na nchi kupata mapato yake”amesema Waziri Ummy.
Alisema kutokana na uwepo wa fursa wanapaswa kulikumbatia zao la mwani kwa sababu ni zao ambalo kilimo chake sio kigumu zaidi na faida yake ni kubwa.
“Mimi kama Mbunge wa Jimbo la Tanga nitashirikiana na wadau Botnar Foundation kuendeleza kilimo cha mwani kikubwa tuwape elimu na ujuzi wananchi hususani wanawake ikiwemo kuwapa vitendea kazi ambayo vitasaidiaa kufanya vizuri katika kilimo cha Mwani na kutafuta masoko”Alisema Mbunge Ummy.
Aidha alisema kwamba amejipa kazi maalumu ya kutangaza mazao makubwa matatu Tanga mjini kutokana na kwamba wanataka mwambao wa Tanga uwe maarufu kwa kuzalisha mazao ya Mwani,Majongoo Bahari na kunenepesha kaa.
Alisema kwamba hayo mazao matatu amevutiwa nayo na kama watawekeza kwenye uchumi wa bluu utasaidia watu wengi sana kupata kipato na hivyo kuweza kujikwamua kiuchumi.
“Lakini niwahaidi kwamba nitafatuta kiwanda cha mwani ili wakiweke kwenye Jiji la Tanga hivyo niwahamasishe watu wengi walime mwani na nimewaomba botnar watusaidie hivyo wananchi tusikate tamaa mapema mwani utalipa hivyo tujitume kulima”Alisema Mbunge Ummy
Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwakilishi wa Botnar Tanzania Dkt. Hassan Mshinda amemuhakikishia Mbunge Ummy kuwa Botnar itaendelea kushirikiana nae na Halmashauri ya Jiji la Tanga katika kutatua kero za maendeleo kwa wakazi wa Tanga Mjini hususan vijana na watoto.

















































