Monday, 17 July 2023

BENKI YA CRDB SASA KUTOA MIKOPO NAFUU KWA WASANII


Baada ya miezi sita ya uzoefu wa Mfuko wa Utamaduni na Sanaa kutoa mikopo kwa wasanii nchini, umeingia mkataba na Benki ya CRDB kutanua wigo wa fursa hizo ili ziwanufaishe wananchi wengi zaidi kupitia mtandao wake mpana wa matawi na mawakala.


Mpaka sasa, mfuko huo uliozinduliwa Desemba 2022 umeshakopesha shilingi bilioni 1.077 kwa miradi 45 ikiwamo 29 inayomilikiwa na kuendeshwa na wanaume, 12 ya wanawake na kikundi kimoja.

Akizungumza kwenye hafla ya kuingia makubaliano ya mkataba huo, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Pindi Chana amesema kwa muda mfupi ambao mfuko huo umetoa fedha hizo, Serikali imeona mahitaji makubwa yaliyopo hivyo kuamua kuipeleka jirani na wananchi.


“Benki ya CRDB ina matawi nchini kote. Tunataka mikopo hii ipatikane kila mahali alipo msanii ili kukuza kipaji chake kwani sasa hivi jamii imeiona faida ya sanaa na wazazi wengi wapo tayari kuwaruhusu watoto wao kuingia kwenye usanii. Kwa mikopo hii kupatikana kwenye matawi ya benki, itawapunguzia wanufaika gharama za kuifuata Dar es Salaam,” amesema Waziri Pindi.


Licha ya kuwapa mikopo, waziri amesema wizara imeanza kuwatafutia wasanii fursa za nje ya nchi ambako wakishiriki matamasha hayo wanajiongezea mtandao wa washirika hivyo kutanua fursa za kipato zaidi.


“Mikopo hii itapatikana kwa riba ya asilimia tisa tu. Hiki ni kiwango cha chini kikilinganishwa na riba zilizopo sokoni kwa sababu Serikali imeweka mkono wake. Nawasihi wasanii popote walipo nchini wajitokeze kunufaika na fursa hii,” amesisitiza waziri.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, Abdulmajid Nsekela amesema wanafanya kila wawezalo kuinua ubora wa kazi za utamaduni na sanaa ili ziweze kujiendesha kibiashara na kutengeneza ajira nyingi kwa vijana nchini kwa kuwapa mikopo na mafunzo tangu uliposajiliwa mwaka 2020.


“Kati ya mikopo tuliyoitoa, metoa wanaume wamepokea shilingi milioni 737 huku wanawake wakichukua shilingi milioni 275. Kikundi kimoja kilichojitokeza kimekopeshwa shilingi 10 pamoja na kampuni tatu zilizowezeshwa shilingi milioni 55. Kiwango cha marejesho kinaridhisha kwani ni asilimia 88 na tutazidi kusimamia ipasavyo ili kifikie asilimia 95 inayotakiwa,” amesema Nsekela.

Ili kuwawezesha wanufaika kuzitumia fedha za mikopo inayotolewa kwa malengo yaliyokusudiwa, Nsekela amesema mfuko umetoa mafunzo kwa wadau 7,216 katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Kilimanjaro, Morogoro, Tanga na Pwani na kufanikisha ununuzi wa vitendea kazi kwa vyuo vitano ambavyo ni Simba Scratch Academy, Koshuma Training Institute, Mwanamboka Ujuzi-Hub, Dage School of Dressing na AM Fashion.

“Naomba kuwafahamisha wadau kuwa, mpango huu watakaoushuhudia leo utakuwa suluhisho la changamoto zilizokuwa zinawakumbuka wasanii hivyo nitaomba tuuamini, tuupokee na kutoa ushirikiano ili kutimiza ndoto za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Nsekela ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa Benki ya CRDB.


Akisaini mkataba huo, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema leo ni siku ya kihistoria kuona mkakati wa unatafsiriwa kwa vitendo kwa kuishirikisha sekta binafsi ili kuwafikia wasanii wengi kadriiwezekanavyo.

“Benki ya CRDB imeingia katika mpango huu kuhakikisha malengo ya mfuko yanafikiwa. Tuna imani kuwa kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, pamoja na taasisi za serikali, tutafanikisha kuyafikia malengo ya mfuko huu. Tumekuwa tukiona jitihada za serikali kujenga mazingira rafiki kwa wadau wa utamaduni, sanaa na michezo ili kuwawezesha kupata matunda ya kazi zao kupitia vipaji walivyonavyo kwa manufaa yao binafsi, familia zao hata jamii na Taifa kwa ujumla,” amesema Raballa.

Ili msanii apate mkopo ambao ni kuanzia shilingi 200,000 mpaka shilingi milioni 100, Raballa amesemaa atatakiwa kupeleka maombi yake ofisi za mfuko huo zinazopatikana nchi nzima ili kufanya uhakiki wa awali kisha kupendekeza maombi hayo yaende Benki ya CRDB. Ombi likikidhi vigezo, mfuko utalipeleka kwenye tawi la Benki ya CRDB lililo Jirani na msanii husika.


Kwa kukamilisha utaratibu huo, Raballa amesema wasanii wanaojishughulisha na kazi za sanaa na utamaduni waliosajiliwa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Bodi ya Filamu na namlaka nyingine za serikali watakuwa wamejihakikishia kupata mkopo wanaoulenga.

Hata waliomo kwenye vikundi, vyama vya utamaduni na sanaa, vituo vya elimu na mafunzo yanayohusiana na utamaduni na sanaa pamoja na asasi za kiraia zinazojihusisha na utamaduni na sanaa zinaweza kunufaika hivyo wasanii wa filamu, muziki, sanaa za ufundi na maonyesho, lugha na fasii na fani nyingine zenye mlengo wa utamaduni na sanaa.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 17,2023



























Share:

Sunday, 16 July 2023

ASKOFU RINGIA AWATAKA WATANZANIA KUUKUBALI MKATABA WA BANDARI

Askofu Wilbard Ringia wa Kanisa la Mizaituni miwili,Pentecoste Assemblies(MMPA)akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 16,2023 Jijini Dodoma.


Na Dotto Kwilasa,Dodoma
Kutokana na kuwepo maneno mengi ya kubeza Mkataba wa uwekezaji wa  Bandari,hatimaye Askofu Wilbard Ringia wa Kanisa la Mizaituni miwili,Pentecoste Assemblies(MMPA)amejitokeza na kuwataka Watanzania kuwa watulivu na wenye kuheshimu mamlaka ili mambo mengine yaendelee.




Askofu Ringia ameyasema

 hayo leo Julai 16,2023 Jijini hapa wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusiana na uwekezaji huo ambapo amesema maneno mengi yanayobeza hayautukuzi utukufu wa Mungu.

 

Amesema Mamlaka zote ulimwenguni huwekwa na Mungu hivyo watanzania hawapaswi kuwa na hofu na serikali iliyopo madarakani kwani kila jambo linalotokea limepangwa na Mungu.

 

“Kila mwanadamu ameumbwa na mungu,hata kuwepo madarakani kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan pia ni mipango ya Mungu hivyo hatuna sababu ya kumlalamikia kwani yote anayoyafanya yanatokana na Mwenyezi Mungu kwa kuwa tunaamini Mungu humtengeneza mtu kuwa Kiongozi tangu anapokuwa tumboni mwa mamaye,”amesisitiza

 

Pamoja na hayo amesisitiza kuwa Mamlaka ya mungu huanzia duniani kupitia viongozi wakuu wanchi hivyo watanzania hawana haja ya kuwa na shaka na maamuzi yoyote yanayotolewa na viongozi hao.

 

“Tuiachie Serikali ifanye maamuzi na hatma ya maendeleo yetu kwa sababu inao wataalamu wengi ,nataka niwaambie watanzania kuwa Serikali huwa haikurupuki badi huanza kufanya upembuzi wa mambo kupitia wataalamu wake kabla ya kutoa suluhu,msiwe na wasiwasi,”amesema na kuongeza;

 

Haisaidii kuleta maneno maneno

uwekezaji ni jambo muhimu mno kila mtu anajua, Ningeshauri tuheshimu mamlaka ya nchi na kufuata maelekezo ya viongozi wa dini ili kuwa na maarifa zaidi,najua yote haya yanatokea kwa kuwa watu wengi hawana maarifa , watu wanapotea kwa sababu hawajui maandiko,hebu kila mmoja asimame kwenye nafasi yake ili tuungane kuijenga nchi yetu,”amesema

 

Askofu huyo pia ametumia nafasi hiyo kuwaasa watanzania kukataa kuishi kwa kusikiliza hadidhi za uongo zinazokwamisha maendeleo na badala yake  wafuate muongozo wa Serikali inavyotaka.

  

“Si adabu wala heshima kumdharau Rais tumpe nafasi ashughulikie uchumi wetu

Mungu hataki fujo wala kudharauli,”amesisitiza

 

Share:

MEYA ADAIWA KUPIGWA AKIZOZANA NA DIWANI WA MJI MPYA KWENYE KIKAO


Meya wa Manispaa ya Moshi, Zuberi Kidumo

Baada ya kusambaa taarifa kwenye mitandao ya kijamii inayodai kuwa Meya wa Manispaa ya Moshi, Zuberi Kidumo alipigwa na diwani wa Mji Mpya, Abuu Shayo baada ya kurushiana maneno katika kikao cha kamati ya mipango miji ya Halmashauri hiyo. Kidumo amekanusha kuwapo kwa tukio hilo.

Taarifa zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii juzi jioni zimedai katika kikao hicho kulijitokeza sintofahamu iliyosababisha meya huyo kupigwa.

Purukushani hiyo inadaiwa imesababisha askari wa halmashauri kuingilia kati na hata diwani Shayo alipotoka nje ya ukumbi alisikika akisema yuko tayari kujiuzulu wadhifa wake, na hata akigombea kama mgombea binafsi atashinda.

Share:

MAKAMBA AYATAKA MAKAMPUNI YA BIMA NCHINI KUTUMIA FURSA KATIKA SEKTA YA NISHATI

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.

********************

Makampuni ya Bima nchini, yametakiwa kuhakikisha kwamba yanazitumia fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati, kuzitambua na kufahamu kuwa wana nafasi ya kuzifikia na kuzipata.

Wito huo umetolewa tarehe 15 Julai, 2023 na Waziri wa Nishati, January Makamba wakati wa ufunguzi wa Semina ya kujadili ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati.

Waziri Makamba ametoa wito kwa wadau, wahusika makampuni ya Bima na wadau wengine, kufahamu kuwa, kwa upande wa Wizara ya Nishati, mlango uko wazi kuendelea kushirikiana nao, na kuwasiliana kwa karibu lakini pia kuna uwekezaji kwa upande wao wa ujuzi, maarifa ya mahitaji mahsusi ya Sekta ya Nishati ikiwemo upanuzi wa mtaji kutokana na ukubwa wa uwekezaji katika Sekta ya Nishati.


Akizungumzia kuhusu madhumuni ya mkutano huo, Waziri Makamba ameeleza kuwa, umelenga kujadiliana kati ya makampuni ya Bima ambayo yametengeneza umoja wao ambao unataka kujishughulisha na fursa zilizoko katika Sekta ya Nishati hasa Miradi ya Gesi na Mafuta, Miradi ya Umeme na miradi mingineyo katika Sekta ya Nishati.


“Kama mnavyofahamu, tunaelekea katika utekelezaji wa miradi mikubwa sana ya kimkakati ya Nishati ikiwemo Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Hoima-Uganda hadi Chongoleani Tanga, Mradi wa kuchakata na kusindika Gesi Asilia kule Lindi. Moja ya fursa zilizopo katika Miradi hiyo mikubwa ya kimkakati ya Nishati ni Bima.” Alisema Waziri Makamba.


Waziri Makamba alifafanua zaidi kuwa, Bima ni sehemu ya huduma ya fedha, ni Biashara kubwa na kuwa yapo makampuni 22 ambayo yametengeneza umoja wao hapa nchini na yameialika Wizara ya Nishati ili kufanya mazungumzo nao kueleza ni fursa zipi zilizopo za Bima katika Miradi ya Nishati na wanaweza kuzifikia vipi fursa hizo, ushirikiano ambao unaweza kuwepo kati ya Serikali, kati ya Wizara ya Nishati na Taasisi na kampuni hizi.


Amesema, mazungumzo ya kutengeneza Mradi wa Kusindika na Kuchakata Gesi kule Lindi Mradi yamemalizika na kulikuwa na mazungumzo na vipengele vinavyohusu Bima.


Waziri huyo wa Nishati ameeleza kuwa, Mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Lindi ni fursa kubwa, thamani yake ni takribani shilingi trillioni 97 ambapo inabidi ukatiwe Bima. na Bima yake ni kubwa hivyo, makampuni hayo 22 yamejenga umoja ili kuhakikisha kwamba fursa hiyo wanaitumia na wanaifikia.


Makamba amesema, hapa nchini, ni Watanzania wachache wanaotumia Bima na mtawanyiko na matumizi ya Bima nchini bado ni madogo hivyo, ni matumaini kuwa mkutano huu ulioandaliwa na TIRA pamoja na makampuni mengine ya Bima itakuwa chachu katika kukuza Tasnia ya Bima hapa nchini.


Ameyapongeza Makampuni ya Bima nchini kwa kuchukua uamuzi huo wa kuanzisha umoja huo na kuipongeza sana TIRA kwa kuwaratibu na kuwakutanisha na Wizara ya Nishati.


Akijibu swali wakati wa mahojiano na Waandishi wa Habari, tofauti ya mahitaji ya Bima miradi ya Mafuta ikilinganishwa na miradi mingine, Waziri Makamba amesema, miradi ya kutafuta Mafuta na Gesi na Miradi ya uchakataji wa Mafuta na Gesi, ni miradi ambayo kwanza ni mikubwa, ya gharama kubwa, Teknolojia kubwa, ina mahitaji mahsusi na riski yake ni kubwa.


“mfano, unaweza ukachimba kisima cha bilioni 100 ukitegemea kupata mafuta au gesi na usipate. Unaweza ukichimba visima 100, ni visima 36 tu ndio unaweza kupata Gesi na Mafuta na mwekezaji yeyote anayetaka kuanza kuchimba mafuta au gesi anakata Bima ili asipopata ule uwekezaji urudishiwe.” Alisema Makamba.


Hivyo, Tasnia ya Gesi na Mafuta ni Tasnia Mahsusi, yenye mahitaji ya Bima mahsusi, kutokana na teknolojia yake, ukubwa wake na mahitaji yake. Hivyo, ni muhimu semina kama hizi kufanyika ili kupata uelewa wa pamoja kati ya Makampuni ya Bima lakini pia na Wataalam wa Tasnia ya Mafuta na Gesi.


Amesema, Wizara ya Nishati itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo haswa kwa upande wa Sekta ya Nishati kuhakikisha kwamba, makampuni ya ndani ya Bima yanazifikia hizo fursa, na kwamba zipo sheria ambazo zinaelekeza kuhakikisha kwamba kwa kadri inavyowezekana makampuni ya ndani, wajasiria mali wa ndani, wanufaike na uwekezaji huu unaokuja.


Lakini vilevile ili kunufaika na fursa hizi kuna mahitaji ya ukuaji, utaalam zaidi, uelewa zaidi wa Sekta ya Nishati kwa sababu, mtaji unaotumika ni mkubwa, teknolijia kubwa hivyo kuna mahitaji pia ya makampuni ya Bima kuelewa kuhusu mahitaji mahsusi kuhusu Sekta ya Nishati.


Amesema, kwa kadri makampuni ya ndani yanavyonufaika, yawe ni Bima, yawe ni ya ulinzi, usafirishaji, mabenki, ndivyo ambavyo uchumi wa nchi unapata manufaa zaidi, ajira zinaongezeka zaidi, kodi zinapatikana zaidi, kwa hiyo kuna manufaa mapana kwa nchi yetu pale wajasiria mali wa ndani wanapoweza kushiriki katika fursa hizi.


Akifafanua kuhusu ushiriki wa wazawa upande wa Bima kwenye miradi ya Nishati wakati wa Semina hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka ameeleza kuwa, ni nia ya Serikali kuhakikisha kuwa Makampuni ya Bima ya hapa nchini yanashiriki kikamilifu kwenye miradi ya Nishati.


Awali, Akizungumza wakati wa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi, kwenye Semina ya konsotia ya Mafuta na Gesi, Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware alisema, lengo la kuunda Konsotia (Ushirika wa Makampuni yanayoweka mitaji yao pamoja) ni kutokana na ukweli kuwa, miradi ya Nishati inahitaji mitaji mikubwa na pia ni miradi ambayo vihatarishi vyake au majanga viko juu sana ambapo kampuni moja moja inaweza kupata changamoto kwenye kumudu kukinga majanga yanayoweza kutokea kwenye miradi hivyo, na hivyo kupelekea muungano huo.


Amesema, ili kuweza kukinga miradi ya Nishati ni muhimu makampuni kuungana na kuweka mitaji pamoja ambapo jumla ya Makampuni 22 ya Bima yaliyosajiliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA) yameshaweka mitaji yake pamoja yenye thamani ya dola milioni sita ili kukinga majanga kwenye miradi ya Nishati


Dkt. Baghayo Saqware, ameeleza kuwa, Kampuni Kiongozi ni Phoenix Insurance Company ambayo imeweka share kubwa katika Konsotia hiyo, ambapo itahusika na utafutaji wa masoko na kupokea sehemu ya majanga ambayo Konsotia haitaweza kuyamudu.


Ameeleza zaidi kuwa, Shirika la Bima la TANRE litashughulikia ulipaji wa madai ya majanga yaliyotokea na uwekezaji mitaji kwenye Konsotia.


Amesema, lengo la semina ni kutoa uelewa kwa Wizara ya Nishati pamoja na Wataalamu wa Timu ya Majadiliano ya Kitaifa ya Miradi ya Nishati kuhusiana na Konsotia, majukumu, manufaa na uendeshaji wa Konsotia pamoja na jinsi Konsotia inavyoweza kushiriki kwenye miradi mbalimbali ya Nishati pamoja na maeneo ya ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima kwa ajili ya uratibu wa Miradi mbalimbali ya Nishati.


Dkt. Saqware amesema, Konsotia hiyo ilizinduliwa tarehe 16 Novemba 2022 na Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Chande.


Semina hiyo pia ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dunstan Luka Kitandula, Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Iddi Kassim Idd, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Daniel Sillo, Mjumbe Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Mhe. Dkt. Charles Kimei, Mjumbe Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Mhe. Zaituni Swai, Mkurugenzi Mtendaji PURA, Mha. Charles Sangweni, Naibu Kamishna wa Bima, Bi. Khadja Issa Said, baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Nishati na PURA.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.
Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka akizungumza wakati wa kufunga Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dunstan Luka Kitandula akizungumza wakati wa majadiliano kwenye Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.


Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mha. Charles Sangweni, akizungumza wakati wa majadiliano kwenye Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha. Kushoto kwake, wakimsikiliza Mha. Sangweni, ni Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dunstan Luka Kitandula
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Daniel Sillo, akichangia jambo wakati wa majadiliano kwenye Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dunstan Luka Kitandula.
Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akifuatilia hotuba iliyokuwa inatolewa na Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware wakati wa Semina ya kujadili ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu PURA Mha. Charles Sangweni na kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka, akifuatilia maoni yaliyokuwa yakitolewa na washiriki wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Daniel Sillo na kushoto ni Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania, Bi. Khadja Issa Said.
Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware akifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Nishati, January Makamba, wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe.Dunstan Luka Kitandula.
Kamishna Msaidizi Sehemu ya Maendeleo ya Petroli wa Wizara ya Nishati, Marwa Petro, akifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Nishati, January Makamba wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha.
Washiriki wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati iliyofanyika tarehe 15 Julai, 2023 jijini Arusha, wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Nishati, January Makamba, wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kujadili Ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati.

Share:

Saturday, 15 July 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 16,2023























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger