Saturday, 15 July 2023

MTATURU AMWAGA MAMILIONI VIFAA VYA MICHEZO


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu amegawa vifaa vya michezo vyenye thamani ya Shilingi Milioni 16.6 na kuzindua rasmi Mashindano ya East Singida Inter School Sports 2023,yanayohusisha shule 19 za serikali na binafsi zilizopo Jimboni humo.

Akigawa vifaa na kuzindua mashindano hayo Julai 14,2023,katika viwanja vya shule ya sekondari Ikungi ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Rashid Mohammed Rashid,Mbunge Mtaturu amesema lengo la mashindano hayo ni kuibua vipaji shuleni na kuwaandaa vijana kufanya vizuri kwenye masomo yao.

Amesema vifaa alivyogawa ni seti 38 za michezo zenye gharama ya Sh Milioni 10.6 na mipira 120 yenye thamani ya Sh Milioni 6.

“Hatua hii ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM na kuunga mkono kwa vitendo jitihada za serikali yetu za kuinua soka nchini tukikuza vipaji hivi mapema tutakuwa na vijana watakaoiokoa nchi kwenye tasnia ya michezo,mimi niwahakikishie kuwa nitaendelea na jitihada zangu hizi kila mwaka,”amesema.

Akitaja zawadi za washindi wa mashindano hayo Mtaturu amesema ili kuweka chachu kwa wachezaji wamekubaliana zawadi ya mshindi wa tatu iwe mashine ya uchapishaji moja na mpira,mshindi wa pili atapata kompyuta na mipira miwili na wakwanza atapata mashine ya uchapaji moja,kompyuta moja na mipira mitatu ambazo zitatolewa kwa washindi wa mpira wa miguu na mpira wa pete.

“Kama kamati tuliona tuweke chachu zaidi katika mashindano haya,tukasema safari hii tutoe vifaa vitakavyochochea uboreshaji wa elimu,tulikaa tukasema kwa sababu shul ni kubwa tukitoa Sh Milioni moja watu watagawana kidogo kidogo haitokidhi mahitaji,tukisema tuchinje mbuzi au ng’ombe atachinjwa ataliwa siku moja halafu basi,ndio maana tukaona tuboreshe zaidi,”amesema.

Amesema zawadi hizo pia zitaenda kwa mfungaji bora,mchezaji mwenye nidhamu,mchezaji bora,mdakaji bora kwa upande wa mpira wa miguu ambao kila mmoja atapata Sh 50,000.

“Niwaombe tucheze kwa nidhamu,sisi tunataka mcheze kwa haki msiumizane kwa kuwa michezo ni furaha,”amesema.
Share:

MBUNGE AWASHUKIA WAPOTOSHAJI BANDARI


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu amewaomba watanzania kutokubali kupotoshwa na mtu yoyote kuhusu uwekezaji unaotaka kufanyika baina ya serikali ya Tanzania nay a Dubai na kusisitiza kuwa dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ni njema na kamwe hawezi kuuza nchi.

Mtaturu amesema hayo Julai 14,2023,katika viwanja vya shule ya sekondari Ikungi wakati akizindua Mashindano ya East Singida Inter School Sports 2023,ambayo inahusisha shule 19 za serikali na binafsi zilizopo katika jimbo hilo ambapo pia amegawa vifaa vya michezo vyenye thamani ya Shilingi Milioni 16.6.

Amesema yeye amekuwa kwenye kamati ya miundombinu tangu alipoingia bungeni kamati ambayo inasimamia sekta ya uchukuzi na katika kipindi chote wameona changamoto zilizopo.

“Ndugu zangu niwaombe msipotoshwe na mtu yoyote,ukiona mtu anakwambia eti ooh Rais ameuza nchi muulize kwa Sh ngapi,maana kitu chochote kinachouzwa lazima kiwe na bei ya mauziano,na kwa kuwa kazi yao ni kupotosha utaona mtaagana pale mtakunywa maji na kila mtu ataenda kulala nyumbani kwake ,”amesema.

KWA NINI TURUHUSU UWEKEZAJI

Mtaturu amesema kuna baadhi ya wafanyabiashara wanafaidika na udhaifu wa bandari uliopo ili wao wachukue fedha wapige dili na wawanyonye watanzania.

“Leo tunaenda kumpata mtu atakayefunga mifumo yote itakayoangalia wapi wameingiza kontena ,la nani,kwa gharama kiasi gani ,awali tulikuwa tunakusanya ushuru wa forodha Sh Trilioni 7 kwa mwaka lakini baada ya uwekezaji huu tutaenda kukusanya Trilioni 26 kwa mwaka ,maana yake Trilioni 44 ya bajeti yetu tutaenda kuibeba wenyewe sawa na asilimia 62,

“Hii maana yake tukiongeza mapato yatokanayo na uboreshaji wa shughuli za bandari tutaachana na mikopo ya masharti magumu pia tozo mbalimbali zinazowaumiza wananchi,leo kuna baadhi ya watu wanaleta misaada wanatupangia tuunge mkono ushoga kwa sababu amekupa kitu ili ukubaliane na masharti yake,mama Samia amesema hapana lazima tuwekeze wenyewe tuweze kuleta maendeleo ya watanzania,”ameeleza

Mtaturu ametolea mfano uwekezaji huo kama nyumba ambapo mmiliki anaamua kupangisha baadhi ya vyumba au kuweka fremu ya maduka.

“Bandari ni kama nyumba umepangisha chumba kimoja ama viwili,mbele umefungua fremu ya maduka unaweka wapangaji ili upate kodi,hivyo bandari hii ni lango la uchumi lazima uweke mtu ambaye mwenye tija atakayewekeza nan chi ipate fedha,”ameongeza.

Ametolea mfano uwekezaji wa Kampuni ya TICTS walioongoza bandari hiyo kwa miaka 22 ,ambapo walikuwa wanatoa Sh Bilioni 300 kwa mwaka kwa gati namba 5 mpaka namba 11.

“Tulivyoenda pale tukamtathimini TICTS tukaona kweli huko nyuma tuliona hela nyingi lakini kwa sasa tumeona ni malipo kidogo, lakini pia kulikuwa na malalamiko makubwa ya wafanyabiashara kucheleweshewa kushusha mizigo yao,

“Leo hii pale Dar es salaam pamoja na uwekezaji mdogo uliowekwa meli inaweza kuchukua siku 5 mpaka siku 7 ndio iweze kushusha mzigo na kila siku inachajiwa dola 25,000 sawa na milioni 58 kwa siku moja huyu mfanyabiashara ukimlipisha yeye ataongeza bei ya bidhaa na hukuIikungi itakuwa kuwa juu maana yake serikali inachofanya sasa ni kupata mwekezaji mwenye uwezo atakayetuongezea tija atakayewafanya wafanyabiashara wengi waje washushe mizigo kwetu,”

Amesema hiyo itasaidia kuweza kupata ushuru utakaowezesha kujenga shule,barabara na taa za barabarani kama ambavyo zinawashwa kwenye Mji wetu wa Ikungi.

AWAOMBA WATANZANIA KUUNGA MKONO RAIS SAMIA

“Nawaomba watanzania tuendelee kumuunga mkono Rais Samia,tumuombee maana kuongoza nchi sio jambo dogo,nchi hii ni kubwa ina watu zaidi ya Milioni 61,anawaongoza wananchi wenye mitazamo tofauti ,wengine wana akili timamu lakini wengine kwa makusudi tu wanataka kumkwamisha Rais wetu,niwaombe sanaa hata hili jambo la bandari mnalolisikia ni jambo la kawaida,limeshafanyika na serikali nyingine,”amesema

Share:

JESHI LA POLISI LAONYA WATU WANAOVAA MAVAZI YANAYOFANANA NA SARE ZA MAJESHI LA ULINZI NA USALAMA


Jeshi la Polisi Tanzania limewataka watu wote wenye tabia ya kuvaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya ulinzi na usalama kinyume na sheria za nchi, kuacha tabia hiyo mara moja kwani halitasita kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Jeshi hilo limesema katika siku za karibuni kumeibuka makundi ya watu, kampuni binafsi za ulinzi na baadhi ya walinzi wa viongozi wakivaa mavazi yanayofanana na sare za Majeshi ya Ulinzi na Usalama

Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP David Misime amesema kuwa Sheria ya Kanuni ya adhabu sura ya 16 kifungu cha 178, kinakataza mtu yeyote ambaye si askari wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kuvaa sare za majeshi ambapo ameongeza kuwa sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 kifungu cha 6, inakataza pia.

Aidha Misime ameongeza kuwa Jeshi la Polisi Tanzania linatoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu ili kuendelee kuiweka nchi salama
Share:

TANZANIA KUANDAA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KOROSHO


 

BRYSON MSHANA, MTWARA


Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Kimataifa wa Korosho utakaohusisha nchi 33 zinazolima zao la Korosho Duniani.


Mkutano huo ulioandaliwa na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT unatarajiwa kufanyika Tarehe 11 October 2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa JNICC Jijini Dar es Salaam, ambapo zaidi ya washiriki 500 kutoka katika mataifa mbalimbali wanatarajiwa kushiriki.


Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Mtwara Julai 14, 2023, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Francis Alfred, amezitaja baadhi ya nchi hizo kuwa ni pamoja na Ivory Coast, Cambodia, India, Vietnam, Brazil, Indonesia, Sri Lanka, Nigeria, Guinea Bissau, Burkina Faso, Mali, Benin, Ghana, Madagascar, Zambia, Msumbiji, Kenya, Mauritius, Visiwa vya Komoro na wenyeji Tanzania.”


Ameeleza kuwa mkutano huo pia utashirikisha wadau mbalimbali kutoka nchi ambazo ni walaji wa korosho ikiwa ni pamoja na Marekani, Nchi za Ulaya, China, Uarabuni, Mashariki ya Kati ikiwa ni pamoja na Afrika Kusini na nchi zingine za bara la Afrika.


Bw. Francis amesema kuwa mkutano unakusudia kushirikisha wadau wote walioko kwenye mnyororo wa thamani wa Tasnia ya Korosho kama vile wakulima, wabanguaji, wasindikaji, wakaangaji, wasafirishaji na Vyama vya Ushirika.


Wengine watakaoshirikishwa ni Wasambazaji wa pembejeo, waendesha ghala, watafiti, wazalishaji wa mitambo na vipuli, wasimamizi wa Tasnia, walaji au watumiaji wa bidhaa za korosho, Taasisi za fedha, watunga sera, wawekezaji, wabia wa maendeleo na wadau wengine wengi.


“Bodi ya Korosho Tanzania inaandaa Mkutano huu wa kimataifa wa Korosho wenye wazo kuu la fursa za uwekezaji kwenye tasnia ya Korosho Tanzania (an insight and investment opportunities in Cashew Industry Tanzania) na kauli mbiu ni “wekeza kwenye Korosho kwa mendeleo endelevu” (invest in cashew for sustainable development).


“Mkutano huu unakusudia kutangaza fursa za uwekezaji zilizoko kwenye Tasnia ya Korosho kuanzia shambani ambapo tunategemea kupata uwekezaji wa kwenye 2 mashamba makubwa, Ubanguaji ambapo matarajio ni kuongezeka kwa viwanda vya kubangua na kusindika korosho na bidhaa zake na kuimarika kwa masoko kwa kufungua masoko ya korosho na bidhaa zake ndani na nje ya nchi” Ameeleza Francis


Bodi ya Korosho Tanzania imeandaa fomu ya kidigitali iliyoko kwenye tovuti ya Bodi ya Korosho Tanzania (www.cashew.go.tz) ambayo itatumiwa na washiriki kuomba kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Korosho wa mwaka 2023.


Aidha, washiriki wa ndani ya nchi wataweza kupiga namba ya bure ya Bodi 0800112159 ili kupewa maelekezo ya namna ya kujisali pale watakapokuwa na changamoto kwenye kujaza fomu, sambamba na  fomu za usajili zitakazopatikana kwenye ofisi za Bodi zilizoko Mtwara, Dar es Salaam, Tanga, Tunduru, Manyoni na Morogoro ambazo mshiriki atajaza na kuziacha ofisini.

Share:

WANAFUNZI VINARA KWA KUANDIKA INSHA EAC NA SADC WAPEWA TUZO

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe,akikabidhi zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetoa tuzo kwa wanafunzi ambao ni washindi wa uandishi wa insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 huku ikisisitiza hamasa zaidi ili kupata washiriki wengi zaidi.

Akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo hizo leo Julai 15,2023 jijini Dodoma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. James Mdoe amesema kuwa uandishi wa insha ni sehemu ya mafunzo na inawajengea wigo mpana wa kujifunza masuala muhimu yanayohusu jumuiya hizo.

Prof.Mdoe amesema kuwa umuhimu wa kushiriki Mashindano hayo kwa wanafunzi ni kuwaongezea uwezo katika kukuza ujuzi wa lugha,unawaongezea maarifa kwa ujumla kwa kupata uelewa wa mada mbalimbali za masomo mengine na kuwasaidia kwa siku za usoni kunufaika na mtangamano wa Jumuiya hizo.

"Uandishi wa Insha unawapa wanafunzi fursa ya kutafiti na kupata taarifa zaidi, kuelewa na kuwawezesha kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na Jumuiya zetu na husaidia wanafunzi wa Kitanzania kuchanganua masuala kutoka nyanya mbalimbali na kulinganisha nyanja hizo na Mazingira yetu," amesema Prof Mdoe.

Hata hivyo amewapongeza wanafunzi wote walioshiriki katika shindano hilo tangu ngazi za awali na kubainisha kuwa licha ya changamoto ndogo ndogo zilizopo katika sekta ya elimu lakini ubora wa elimu ni mzuri na hilo linadhihilishwa kwa wanafunzi wengi kuonyesha ushindani mkubwa katika uandishi wa insha ikishirikisha nchi mbalimbali.

Ameongeza kuwa “Ni matamanio yetu siku moja tuone washindi wa kwanza, wa pili, wa tatu hata hadi nafasi ya tano tunakuwa watanzania na hili linawezekana tukitilia mkazo walimu wakuu, wazazi na waratibu wahamasishe zaidi” amesema Prof. Mdoe.

Aidha Prof. Mdoe amewataka Walimu Wakuu na Waratibu wa ndani wa Shule mbalimbali nchini kuhakikisha wanawasaidia wanafunzi wao miongozo inayohitajika katika uandishi wa Insha.

Awali, akisoma risala ya mashindano hayo, Mratibu wa Insha kutoka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Bi.Matuha Masati,ameipongeza Sekretarieti ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Nchi za SADC Kwa kuendesha Mashindano ya Uandishi wa Insha kwani yamekuwa chachu Kwa vijana kufanya utafiti,kujifunza na kufahamu vizuri mchakato na hatua mbalimbali za uimarishaji Kwa nchi wanachama.

Amesema kuwa mashindano hayo husimamiwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) kwa insha za nchi za Afrika Mashariki (EAC) na za SADC husimamiwa na Wizara ya Elimu kwa upande wa Tanzania bara na Zanzibar.

Amesema kuwa Jumla ya wanafunzi 133 walishiriki katika shindano la uandishi wa Insha za SADC Kwa Mwaka 2021 na baada ya usahihishaji wakapatikana washindi 10 katika ngazi ya Taifa ambao wamepewa zawadi na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwa ni tofauti na miaka ya nyuma ambapo zawadi zilikuwa zikitolewa Kwa mshindi wa kwanza mpaka wa tatu tu

" Kwa upande wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki washiriki walikuwa 315 Kwa Mwaka wa 2021 ambapo baada ya usahihishaji wakapatikana washindi 10 ambao wamegawanywa katika Makundi mawili” amesema.

Ameongeza kuwa "Kundi A wanapewa zawadi tofauti tofauti kulingana na nafasi ya ushindi kitaifa na kundi B ni mshindi kuanzia nafasi ya Sita hadi kumi hawa wanapewa zawadi zinazofanana kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,"amefafanua Masati

Katika mashindano ya SADC mshindi wa kwanza amepata Dola za Marekani 500, wa pili amepata Dola za Marekani 300 na watatu amepata Dola za Marekani 200 huku kwa EAC mshindi wa kwanza amepata Dola za Marekani 300, wa pili Dola za Marekani 250 na watatu amepata Dola za Marekani 200 , wan ne amepata Dola za Marekani 150 na watano amepata Dola za Marekani 100.

Aidha, katika kundi la pili kwa EAC lilikuwa na wanafunzi watano ambao kila mmoja amepata Dola za Marekani 50 na Wizara imetoa Sh. 300,000 kwa washindi 20 wa mashindano hayo.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Mratibu wa Insha wa kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Matuha Massati, akisoma risala wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe,akipokea risala kutoka kwa Mratibu wa Insha wa Wizara hiyo Bi. Matuha Massati,wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.




Mwakilishi wa Katibu Mkuu TAMISEMI, Alfred Kazimoto,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Prof. James Mdoe (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Prof. James Mdoe,akikabidhi zawadi mbalimbali kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Mkurugenzi Idara ya Elimu Sekondari Zanzibar Bi.Asya Idd Issa ,akitoa neno la shukrani wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Mratibu NECTA Dodoma Bw.Ezekiel Sekelano,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Mratibu wa Insha Shule ya Sekondari Azania Mwalimu Ndeni Ndossi,akitoa neno la shukrani wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Prof. James Mdoe,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwatunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2021 hafla iliyofanyika leo Julai 15,2023 jijini Dodoma.
Share:

CHONGOLO ATUA MBEYA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA, KUULEZEA UENDELEZAJI BANDARI DAR


Na Mwandishi Wetu, Mbeya

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Daniel Chongolo amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Songwe jijini Mbeya, tayari kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyikaUwanja wa Luanda jijini humo.

Chongolo akiwa uwanja wa ndege amelakiwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wa mikoa jirani pamoja na Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini.

Katika mkutano huo pamoja na mambo mengine Chongolo ataelezea hatua kwa hatua usahihi wa makubaliano ya uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, lengo likiwa kuhakikisha bandari hiyo inatoa huduma kwa viwango vya hali ya juu tofauti na ilivyo sasa.

Kwa mujibu wa ratiba ,mkutano huo utahudhuriwa pia na baadhi ya wananchi kutoka mikoa ya Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger