Wednesday, 22 March 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 22,2023





























Share:

Tuesday, 21 March 2023

UTARATIBU WA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA AJIRA ZA MUDA KWA KAYA ZA WALENGWA


Miradi ya ajira ya muda kwa walengwa wa TASAF ni utaratibu wa utekelezaji miradi ya jamii yenye kutumia nguvu kazi, inayoshirikisha walengwa kufanya kazi na kulipwa ujira.

 Miradi hiyo inawezesha jamii kupata rasilmali /miundombinu inayotoa huduma na ujuzi kwa jamii kupitia ushiriki wao katika kutekeleza miradi hiyo.

 Washiriki wa kazi zinazotoa ajira ya muda kwa walengwa ni watu wenye uwezo wa kufanya kazi wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 65.

 Kila kaya ambayo inashiriki katika ajira za muda kwa walengwa inaandikisha watu wawili, ambapo mtu mmoja kutoka kwenye kaya ndiye atashiriki kazi- kwa wakati mmoja. 


Utekelezaji wa miradi ya ajira ya muda huchukua miezi sita ambapo walengwa hufanya kazi kwa siku kumi tu kwa kila mwezi. Kwa siku mlengwa anatakiwa kufanya kazi kwa muda usiozidi masaa manne ili aweze kupata muda wa kufanya shughuli nyingine.


Wazee, watu wenye ulemavu, wakina mama wajawazito na wenye watoto wadogo ambao hawajatimiza miaka miwili hawaruhusiwi kufanya kazi za ajira za muda kwa walengwa.

 Wasimamizi wanaopanga kazi za walengwa hawatakiwi kuwapangia kazi watu hao na wanapaswa kutoa taarifa kwa wajumbe wa kamati ya usimamizi wa mradi (CMC) na Waratibu ili majina ya watu hao yaondolewe kwenye orodha ya watu walioandikishwa kufanya kazi za ajira ya muda. 

Kaya yenye watu ambao hawaruhusiwi kufanya kazi za ajira ya muda watapokea ruzuku ya msingi.


Uongozi wa TASAF umetoa waraka kwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Ufuatiliaji kupitia orodha za watu walioandikishwa kufanya kazi kwenye miradi ya ajira za muda na kuwaondoa wale ambao hawaruhusiwi kufanya kazi kwenye miradi hiyo. 

Aidha utoaji wa elimu kwa viongozi wa jamii, wasimamizi na walengwa kuhusu taratibu za utekelezaji wa miradi ya ajira za muda kwa kaya za walengwa utaendelea kutolewa katika kipindi chote cha utekelezaji.

Imetolewa na

Kitengo cha Habari na Mawasiliano MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII TASAF
Share:

TBS YAWATAKA WADAU KUSHIRIKI KATIKA UANDAAJI VIWANGO

Meneja wa uandaaji Viwango TBS, Mhandisi Yona Afrika akizungumza na waandishi wa habari hapo jana Machi 20,2023 katika Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam

Afisa Viwango TBS, Mhandisi Prosper Godfrey akizungumza na waandishi wa habari hapo jana Machi 20,2023 katika Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam

*************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KATIKA kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Viwango Barani Afrika, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka Wadau mbalimbali kushiriki katika uandaaji Viwango ili kuweza kujijengea uelewa mkubwa kwenye masuala ya uzalishaji na uandaaji wa bidhaa zenye viwango vinavyotakiwa.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana Machi 20,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa uandaaji Viwango TBS, Mhandisi Yona Afrika amesema maadhimisho hayo Kitaifa yanatarajiwa kufanyika Kanda ya nyanda za juu Kusini Mbeya Machi 27 hadi 28,2023 ambapo wadau wote wanakaribishwa kushiriki.

Aidha amesema kuwa kwa mwaka huu wanataka kuangalia kazi ya uandaaji viwango inavyoweza kuwakuza wajasiriamali wadogo hasa wa kilimo kwenye suala zima la ushiriki katika uandaaji waa viwango.

Kwa upande wake Afisa Viwango TBS, Mhandisi Prosper Godfrey amesema katika maadhimisho hayo Machi 27 kutakuwa na mafunzo kwa wadau mbalimbali wanaojihusisha mazao ya vyakula ikiwemo mchele, matunda na mbogamboga ambapo pia maadhimisho hayo yataendana na utoaji zawadi na tuzo kwa washindi waliopatikana kwenye shindano la Insha.

Amesema TBS ilipokea zaidi ya Insha 250 ambazo zilishindanishwa na kupata washindi 10 ambao watapewa zawadi Machi 28 siku ya kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Viwango barani Afrika.

"Insha hizi huwa zinafanyika kwa lengo la kukuza uelewa kwa wanafunzi ambao tunatarajia watakao kuja kuwa wazalishaji na watumiaji wa bidhaa wa kesho kwani wanaoandika wanaongeza uelewa juu ya viwango na pia kupitia wao tutazidi kuelimisha jamii juu ya suala zima la umuhimu wa viwango ". Amesema Mhandisi Godfrey.
Share:

JINSI YA KUSHINDA KIRAHISI MERIDIANBET KASINO YA MTANDAONI

Sloti ya Deuces Wild Poker

 

Unapenda kucheza karata na umeshaonesha ubingwa wako kwa washikaji zako na sasa unatafuta sehemu ya kujiingizia kipato kutokana na kipaji chako cha kucheza karata? Meridianbet kasino ya mtandaoni inakuja na sloti pendwa ya Deuces Wild Poker iliyotengenezwa na Habanero.

 

Ukiingia katika Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, utakuta mchezo wa Deuces Wild Poker ambao ni mchezo wa karata unaopendwa na watu wengi sana duniani kote!  Mchezo huu wa Poker au karata unaweza kukurudishia mpaka 97.58% ya dau lako!

Unachezaji Sloti ya Deuces Wild Poker?

Sio hata ngumu sana kama michezo mingine, sloti hii ya Deuces Wild Poker kutoka Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet unavyokua unacheza ni kama unamsukuma mlevi vile. Unaweza kujaribu sloti nyingi rahisi kama Aviator, Poker na Roulette.

 

Hatua ya 1: Bofya idadi ya mikono unayotaka kucheza, unaweza kuchagua kati ya 1, 5, 10, 50 au 100. Baada ya kuchagua mikono, utapelekwa kwenye sehemu yenyewe ya mchezo ambapo utaweza kuchagua kiasi cha sarafu “coin” unazotaka kucheza ni kuanzia 1 mpaka 5 lakini kila mstari una kiwango chake cha sarafu. Weka kiwango unachotaka ukiwa unategemea ushindi mkubwa kupitia Meridianbet kasino ya mtandaoni!

 

Hatua ya 2: Anza kucheza kwa kubonyeza  kitufe cha "Deal" ambacho kitakupa karata tano mkononi, unaweza kuchagua zile za kucheza na zile za kuzihifadhi kwa mzunguko unaofuata. Meridianbet kasino ya mtandaoni kwa kushirikiana na Habanero wamekupa chaguo la “Auto Hold” ambalo linakusaidia kuchagua karata za kuhifadhi pembeni kwa matumizi ya baadae ya sloti hii.

 

Ukishaanzisha mchezo, subiri ushindi mkubwa! Usisahau karata ulizozihifadhi zinaweza kutumika na kukupa mpaka ushindi wa mara 250 papo hapo.

 

Ingia mchezoni na hatojutia kuijachagua kasino ya mtandaoni ya Meridianbet yenye sloti kibao za kijanja kama Aviator, Poker, Roulette inayokupa bonasi kibao, kwa wewe unayebashiri mubashara soka, mtandaoni au bila bando au kupitia kwenye duka la ubashiri unapata odds kubwa na machaguo kibao.

 


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MACHI 21,2023

























Share:

Monday, 20 March 2023

TBS YATOA ELIMU KWA WANANCHI 6,500


Jumla ya wananchi 6,500 kutoka mkoani Mbeya wamepatiwa elimu kuhusu umuhimu wa kununua bidhaa zilizothibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) sambamba na kuwahamasisha wafanyabiashara kusajili maduka ya chakula na vipodozi.

Wananchi hao walipatiwa elimu hiyo kupitia kampeni ya kutoa elimu kwa umma iliyoendeshwa na shirika kwenye wilaya hizo ambayo imemalizika mapema wiki hii.

Kampeni hiyo ya elimu kwa umma ilifanyika katika maeneo mbalimbali yakiwemo masoko, stendi, minadani na maeneo mengine ya wazi ambapo wananchi walijitokeza kwa wingi kupata elimu na ufahamu wa masuala mbalimbali yahusuyo ubora wa bidhaa.

Afisa Masoko wa TBS Deborah Haule, aliwakumbusha wananchi kuwa vita ya bidhaa hafifu sio ya TBS pekee, bali ni ya Taifa kwa ujumla.

"Kampeni hii imeweza kuwafikia zaidi ya wananchi 6,500 kutoka Mbeya mjini na wilaya za Chunya, Busokelo na Mbarali," Alisema Haule.

Haule aliwafafanulia wananchi umuhimu wa viwango katika maisha yao ya kila siku vilevile kuwafahamisha fursa ya huduma bure kwa wajasiriamali wadogo.

Alitaka wawe mabalozi wazuri wa kuhamasisha ubora katika jamii wanazoishi.

Vilevile aliwasisitiza wananchi kuendelea kutoa taarifa pindi wanapokutana na bidhaa zilizokwisha muda wake au wanapotilia shaka bidhaa yoyote katika soko au ziĺizopigwa marufuku kama vile nguo za ndani za mitumba na baadhi ya vipodozi.

Alitoa mwito kwa wafanyabiashara kufuatilia taratibu sahihi za usajili wa bidhaa au majengo kupitia mawasiliano waliyopewa pamoja na kutembelea ofisi ya TBS iliyopo karibu au kupiga katika kituo cha huduma kupitia mawasiliano waliyopewa.

Afisa Tawala mkoa wa Mbeya, Bw. Rodrick Mpogolo aliipongeza TBS kwa kutoa elimu hiyo kwa wananchi katika ngazi ya wilaya, kwani itaongeza ufahamu na kuhakikisha suala la uuzaji wa bidhaa hafifu sokoni linapungua kama sio kwisha kabisa.

Kwa upande wake mjasiriamali mdogo Aristidias Justin kutoka soko la SIDO Mbeya ameishukuru TBS kwa kuwatembelea na kutoa elimu ambapo ameahidi kufanyia kazi elimu waliyopatiwa ili kuzalisha na kuuza bidhaa zinazokidhi matakwa ya viwango.
Share:

BARRICK YAAHIDI DOLA MILIONI 30 ZA MAENDELEO YA SHULE KWA UBIA NA TANZANIA


 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Dola za Marekani (USD) 30,000,000.00 kutoka kwa Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Briston kwa ajili ya shughuli mbalimbali za Elimu, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 20 Machi, 2023. Fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa Mabweni 273 pamoja na Madarasa zaidi ya 1094 kwa Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Briston, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 20 Machi, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Briston mara baada ya mazungumzo Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 20 Machi, 2023.


Dodoma, Tanzania, Machi 20, 2023 – Kampuni ya Dhahabu ya Barrick (NYSE:GOLD) (TSX:ABX) - Katika mkutano wa leo kati ya rais na afisa mtendaji mkuu wa Barrick, Mark Bristow na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kampuni hiyo ilithibitisha ahadi yake ya Dola Milioni 30 (takriban shilingi bilioni 70.5 za fedha za Tanzania) kwa ajili ya upanuzi wa miundombinu ya elimu nchini Tanzania kwa ushirikiano na Serikali.



Programu ya Barick-Twiga ya Kusongesha Mbele Mustakabali wa Elimu, iitwayo “Barrick-Twiga Future Forward Education Program” inalenga kujenga madarasa 1,090, majengo ya maliwato na vyoo 1,640 na mabweni 270 katika shule 161 nchini kote ili kusaidia kuwapatia malazi wanafunzi takribani 49,000 kati ya wanafunzi wapatao 190,000 wanaotarajiwa kuanza masomo yao ya sekondari ya juu (A-level) Julai mwaka huu. Dola milioni 10 za kwanza zitalipwa mwezi Aprili na albaki itatolewa kadiri programu hiyo itakavyokuwa inaendelea.


“Tunaamini kuwa elimu ni muhimu kwa maendeleo ya nchi. Migodi yote miwili ya dhahabu ya Bulyanhulu na North Mara inaendelea kusaidia sekta ya elimu kwa kujenga vyumba vya madarasa na kuboresha miundombinu ya elimu katika maeneo yanayoizunguka migodi hiyo, jambo ambalo limefanikisha baadhi ya shule hizo kuwa miongoni mwa shule zinazoongoza mara kwa mara katika mikoa hii,”
alisema Bristow.



North Mara tayari imetumia dola milioni 1.9 (shilingi bilioni 4.5) katika shule 87 za msingi na sekondari wilayani Tarime, shule 14 kati ya hizo zikiwa zile zilizofanya vizuri zaidi wilayani humo. Bulyanhulu imetumia dola milioni 1.8 (shilingi bilioni 4.2) katika miradi 80 ya elimu katika eneo linalouzunguka mgodi huo na hivi sasa inajenga Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi katika Kijiji cha Bunango. Uwekezaji wa Barrick katika eneo linalouzunguka mgodi huo umewezesha wasichana wa Kitanzania 7,557 kupata elimu mwaka 2022.


“Licha ya msaada wa kampuni wa kustawisha elimu, mwaka jana, North Mara ilitambuliwa rasmi kama mlipakodi mkubwa zaidi nchini Tanzania na Bulyanhulu ilitunukiwa Tuzo ya Mwajiri Bora anayezingatia matakwa ya sheria, ambayo ilitolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii. North Mara na Bulyanhulu pia zilipata tuzo za mshindi wa kwanza na wa pili, mtawalia, kwa uuzaji wa madini nje ya nchi na kwa kuingiza fedha za kigeni nchini. Kampuni zote mbili zimetoka mbali sana na tunatarajia kuendelea na safari hiyo kupitia ubia wetu wa Twiga na serikali.”



Bristow alisema tangu Barrick ilipoichukua migodi hiyo mwaka 2019, imeingiza dola bilioni 2.4 katika uchumi wa Tanzania. Kupitia kamati zake za maendeleo ya jamii, migodi hiyo imewekeza zaidi ya dola milioni 10 katika miradi ya kuboresha huduma za afya, elimu, upatikanaji wa maji ya bomba na miundombinu ya barabara.

 

Kwa maelezo zaidi kutoka Barrick

Meneja wa nchi wa Mawasiliano na uhusiano

wa Kampuni

Georgia Mutagahywa

+255 754 711 215

Baruapepe: georgia.mutagahywa@barrick.com

Mahusiano ya Kampuni na wawekezaji na vyombo vya habari

Kathy du Plessis

+44 20 7557 7738

+27 83 266 5847

Baruapepe: barrick@dpapr.com

Tovuti: www.barrick.com



Cautionary Statement on Forward-Looking Information

 

Certain information contained or incorporated by reference in this press release, including any information as to our strategy, projects, plans, or future financial or operating performance, constitutes “forward-looking statements”. All statements, other than statements of historical fact, are forward-looking statements. The words “pledge”, “create”, “continue”, “opportunity”, “helping”, “objective”, “projects”, “currently”, “continue”, “towards”, “would”, “will”, and similar expressions identify forward-looking statements. In particular, this press release contains forward-looking statements including, without limitation, with respect to: the potential for Barrick’s partnership with the Government of Tanzania to deliver long-term value to the Tanzanian economy and create benefits for local stakeholders; Barrick’s sustainability initiatives in Tanzania including planned investments by Barrick in Tanzania including to develop education, healthcare, potable water and road infrastructure; and Barrick’s contributions to the local economy including its tax contributions, education funding, local hiring and procurement programs and spending.

 

Forward-looking statements are necessarily based upon a number of estimates and assumptions including material estimates and assumptions related to the factors set forth below that, while considered reasonable by the Company as at the date of this press release in light of management’s experience and perception of current conditions and expected developments, are inherently subject to significant business, economic, and competitive uncertainties and contingencies. Known and unknown factors could cause actual results to differ materially from those projected in the forward-looking statements, and undue reliance should not be placed on such statements and information. Such factors include, but are not limited to: fluctuations in the spot and forward price of gold, copper, or certain other commodities (such as silver, diesel fuel, natural gas, and electricity); the speculative nature of mineral exploration and development; changes in mineral production performance, exploitation, and exploration successes; risks associated with projects in the early stages of evaluation, and for which additional engineering and other analysis is required; risks related to disruption of supply routes which may cause delays in construction and mining activities, including disruptions in the supply of key mining inputs due to the invasion of Ukraine by Russia; timing of receipt of, or failure to comply with, necessary permits and approvals; failure to comply with environmental and health and safety laws and regulations; increased costs and physical and transition risks related to climate change, including extreme weather events, resource shortages and increased regulations relating to greenhouse gas emission levels; uncertainty whether some or all of the targeted investments and projects will meet the Company’s capital allocation objectives and internal hurdle rate; changes in national and local government legislation, taxation, controls or regulations and/ or changes in the administration of laws, policies and practices, expropriation or nationalization of property and political or economic developments in Tanzania and other jurisdictions in which the Company or its affiliates do or may carry on business in the future; our ability to convert resources into reserves; increased costs, delays, suspensions and technical challenges associated with the construction of capital projects; the impact of inflation, including global inflationary pressures driven by supply chain disruptions caused by the ongoing Covid-19 pandemic and global energy cost increases following the invasion of Ukraine by Russia; risks associated with working with partners in jointly controlled assets; damage to the Company’s reputation due to the actual or perceived occurrence of any number of events, including negative publicity with respect to the Company’s handling of environmental matters or dealings with community groups, whether true or not; risks associated with new diseases, epidemics and pandemics, including the effects and potential effects of the global Covid-19 pandemic; litigation and legal and administrative proceedings; employee relations including loss of key employees; and availability and increased costs associated with mining inputs and labor. Barrick also cautions that its guidance may be impacted by the ongoing business and social disruption caused by the spread of Covid-19. In addition, there are risks and hazards associated with the business of mineral exploration, development and mining, including environmental hazards, industrial accidents, unusual or unexpected formations, pressures, cave-ins, flooding and gold bullion, copper cathode or gold or copper concentrate losses (and the risk of inadequate insurance, or inability to obtain insurance, to cover these risks).

 

Many of these uncertainties and contingencies can affect our actual results and could cause actual results to differ materially from those expressed or implied in any forward-looking statements made by, or on behalf of, us. Readers are cautioned that forward-looking statements are not guarantees of future performance. All of the forward-looking statements made in this press release are qualified by these cautionary statements. Specific reference is made to the most recent Form 40-F/Annual Information Form on file with the SEC and Canadian provincial securities regulatory authorities for a more detailed discussion of some of the factors underlying forward-looking statements and the risks that may affect Barrick’s ability to achieve the expectations set forth in the forward-looking statements contained in this press release.

 

Barrick disclaims any intention or obligation to update or revise any forward-looking statements whether as a result of new information, future events or otherwise, except as required by applicable law.




Share:

BARRICK NORTH MARA, POLISI WATOA ELIMU YA USALAMA BARABARANI KWA WAENDESHA BODABODA TARIME, WATOA KOFI NGUMU NA JAKETI

Askari wa usalama barabarani wakitoa elimu kwa waendesha bodaboda.
***

MGODI wa Dhahabu wa Barrick North Mara, umeshirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Tarime, kuwapatia madereva wa pikipiki za abiria (bodaboda) elimu ya usalama barabarani, ili kuepusha ajali katika maeneo yaliyo jirani na mgodi huo.


Elimu hiyo imetolewa wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, yaliyofanyika kiwilaya katika mji mdogo wa Nyamongo uliopo jirani na mgodi huo.


Mgodi huo umetumia nafasi hiyo pia kugawa msaada wa kofia ngumu 100 na jaketi maalumu 200 kwa baadhi ya waendesha bodaboda, huku Jeshi la Polisi likitumia vifaa mbalimbali kuwaelimisha sheria na alama za usalama barabarani.


Mkuu wa Kitengo cha Polisi wa Usalama Barabarani Wilaya ya Tarime, ASP Barnabas Irumba, amesema ajali nyingi zimekuwa zikisababishwa na madereva wa bodaboda wasio na elimu ya matumizi ya vyombo vya moto barabarani.


Awali, viongozi wa vijiji na kata jirani walikemea matumizi holela ya vyombo hivyo vya moto na kuwataka vijana waliojiajiri katika sekta hiyo kubadilika kwa kuhakikisha wanapata mafunzo stahiki na kuheshimu sheria za usalama barabarani.


Naye mwakilishi wa waendesha bodaboda waliohudhuria kilele hicho cha maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, aliyejitambulisha kwa jina la Msofe, ameushukuru mgodi wa Barrick North Mara, kwa msaada wa kofia ngumu na jaketi maalumu, na kwa upande mwingine Jeshi la Polisi kwa mafunzo ya sheria za barabarani, huku akiomba utaratibu uwe endelevu ili kujenga mahusiano baina yao.
Mwakilishi wa Barrick North Mara (kushoto) na viongozi wa Jeshi la polisi waliohudhuria hafla ya maadhimisho Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani
Askari wa usalama barabarani wakitoa elimu kwa waendesha bodaboda.
Waendeshaji wa bodaboda wakifuatilia mafunzo ambapo pia baadhi yao walipatiwa kofia ngumu na jaketi maalumu za usalama kutoka mgodi wa Barrick North Mara.
Waendeshaji wa bodaboda wakifuatilia mafunzo ambapo pia baadhi yao walipatiwa kofia ngumu na jaketi maalumu za usalama kutoka mgodi wa Barrick North Mara.
Share:

TANGA UWASA YAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA MAJI



Mhandisi Salum Ngudy akizungumza jambo na wadau wa Maji kuhusiana na miradi ya kuiboresha huduma ya maji safi jijini Tanga
Mitambo ya kusafirisha Maji kutoka Bwawa la mabayani


Na Salma Amour - Tanga

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi Mazingira Tanga (UWASA) katika wiki ya maji inaendelea kutekeleza miradi muhimu ili kuweza kuzalisha maji ya kutosha na wananchi waweze kupata huduma hiyo kwa muda wa saa 24 kama ilivyokuwa hapo awali ambapo hali hiyo imewaathiri wakazi katika maeneo mbalimbali kutokana na mvua kutokunyesha kwa kipindi kirefu na kusababisha maji kupungu katika bwawa la maji.


Akizungumza katika ziara yake ya kutembelea bwala la Maji huko Pande Mabayani pamoja na mtambo wa kuzalisha Maji Mowe mhandishi wa mamlaka ya Maji Tanga UWASA Salum Ngudy alisema wanaendelea kuboresha huduma ya maji katika jamii.


Awali akiwa katika mitambo wa kutibu Maji mhandisi salum alieleza kuwa Maji yanayotoka kwenye Bwawa kuelekea kwenye mitambo yanasafishwa kila baada ya masaa mawili wanapimwa ili kuhakikisha kuwa hakuna kitu chochote kinachoweza kuwaathiri wananchi kupitia Maji hayo kwa kuwa wataalamu wa maabara wapo makini katika kuhakikisha maji yanakuwa safi na salama muda wote.



Katika hatua nyingine upatikanaji wa Maji kwa siku katika maeneo yote ni lita 30,000 ambayo katika baadhi ya maeneo Maji hayatoki ingawa kwa sasa mtambo uliopo ni kwa ajili ya kutanua uzalishaji ili kufikia Lita 45,000 ambayo itasaidia kukidhi haja za wananchi wote.


"Tuna mitambo minne ambayo miwili ndiyo inatumika kwa sasa inasaidia kupandisha maji mpaka kuwafikia wananchi na mingine miliwi ipo kwa ajili ya akiba kama ikitokea mmoja kati ya hii ikiharibika", alisema


Awali mhandisi Salum aliwashauri wakazi wa Tanga kupanda miti itakayosaidia kutunza mazingira muda wote na kusababisha kunyesha mvua za mara kwa mara ili kuwepo na upatikanaji wa maji.


"Suala la miti kuwa michache katika maeneo yetu tunayoishi ni changamoto niwaombe wananchi kupanda miti ili kusaidia mazingira yetu muimarika na hata mvua ziweze kunyesha ili tupate maji muda wote",aliongeza.


Aliongeza kuwa kumekuwepo na changamoto ya ukosefu wa Maji Tangu mwezi Novemba Mwaka jana lakini mpaka kufikia Machi mwaka huu hali hiyo imeweza kuimarika hivyo amewaomba wakazi wote kutumia maji kwa umakini na kuweza kuyahifadhi kwenye vyombo mbalimbali itakayo wasaidia katika matumizi yao binafsi.


"Kuanzia Machi Mwaka huu hali ya upatikanaji wa maji imeanza kuwa shwari ingawaje haijafikia asilimia 100 , maeneo mengi yanapata maji kwa takribani saa 20 na vilevile Tanga UWASA tumejipanga kutatua changamoto iliyokuwepo",alisema mhandisi Salum.


Aidha mtaalamu wa maabara kutokea kwenye mtambo wa kutibu Maji Amos Rwehangana alibainisha kuwa kwa sasa hali ya kutoka kwa maji ipo shwari katika maeneo mbalimbali yakiwa masafi na hayawezi kuleta athari yeyote katika jamii hii ni kutokana na juhudi walizonazo.


"Wananchi wetu wanapata huduma ya maji Safi na hii ni kutokana na kuyatibu maji haya ambayo chanzo chake ni kwenye mito ikiwemo mto zigi na huwezi kuyatumia hivyo hivyo bila huyatibu hivyo sisi watu wa maabara tunayafanyia vipimo kila baada ya saa mwili, tunayatia dawa na pia zipo dawa za aina nne tofauti tofauti na haijawahi kutokea wananchi kupata maji yenye madhara kwa kuwa tunaujua wajibu wetu,hivyo kutaendelea kupambana ili wananchi wapate huduma bora kwa matumizi yao",alisema.
Share:

RPC TARIME : MFANYAKAZI WA BARRICK NORTH MARA ALIKUFA KWA KUJIRUSHA SHIMONI

Kamanda wa Polisi Mkoa Tarime Rorya, ACP Geofrey Sarakikya

***
Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) Tarime Rorya, ACP Geofrey Sarakikya amesema mfanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara, Emmanuel Chacha (26) hakufa kwa kupigwa risasi.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo asubuhi, Kamanda Sarakikya ametupilia mbali taarifa zilizosambazwa kwenye mitando ya kijamii zikidai kwamba mfanyakazi huyo aliuawa kwa kupigwa risasi.

"Maelezo ya watu waliokuwepo kwenye eneo la tukio,na kutokana na matokeo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu Emmanuel Chacha  uliofanywa na Daktari katika Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza kifo chake kimetokana na majeraha yaliyotokana na kujirusha kwenye shimo lenye urefu wa mita 20. Taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kifo cha Emmanuel Chacha kilitokana na kupigwa risasi siyo za kweli, huu ndiyo ukweli", amesema Kamanda Sarakikya.


Kamanda huyo wa Polisi ametoa ufafanuzi huo kutimiza ahadi aliyoitoa Machi 12, 2023 kwamba atatoa taarifa kamili ya kifo hicho baada ya kupata majibu ya uchunguzi wa kidaktari kuhusu mwili wa marehemu huyo.


Katika taarifa yake ya awali, kifo hicho kilichotokea Machi 11, 2023 katika eneo la Gokona Underground ndani ya mgodi wa Barrick North Mara, Kamanda Sarakikya alisema kuwa, kabla ya kujirusha kwenye shimo, timu ya kikosi kazi ilimkukuta mfanyakazi huyo akiiba mawe yanayodhaniwa kuwa na dhahabu ndani ya mgodi huo.


Alieleza kuwa timu hiyo ya kikosi kazi ilijumuisha afisa madini wa mkoa, maafisa kutoka wa jeshi la Polisi, kitengo cha ulinzi cha mgodi huo na kampuni ya ulinzi ya Nguvu Moja.
Share:

POLISI SHINYANGA WAKAMATA PIKIPIKI, BANGI, TV, MAFUTA YALIYOIBIWA MRADI RELI YA KISASA

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akionesha mali zilizokamatwa na Jeshi la Polisi 

Na Halima Khoya,Shinyanga.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata lita 302 za mafuta ya diesel katika maeneo tofauti ya mradi wa Reli ya Kisasa (SGR), pikipiki 04 zilizokuwa zikitumika kufanyia uhalifu ,dawa za kulevya aina ya bangi kilo 22 mifuko mitatu ya saruji na magodoro 02.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Machi 20 2023, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu amesema mali hizo zimekamatwa katika kipindi cha kuanzia tarehe 28,03,2023 hadi tarehe 20,03,2023 kupitia misako na doria kwenye maeneo mbalimbali mkoani Shinyanga.

Nyandahu amesema Jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata printer 01, kompyuta 01,TV 02,mbolea kilo 30,pamoja na battery 10 za magari ambazo ziliibiwa kwa vipindi na tofauti.

“Watuhumiwa 13 wamekamatwa na wapo mahabusu wakisubiri hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani”,amesema.

Hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea kuwasihi wananchi kuendelea kutoa ushirikiano ili kutokomeza uhalifu na pia linaahidi kuzifanyia kazi taarifa mbalimbali za kihalifu zinazotolewa na wananchi kwa usiri mkubwa.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 20,2023. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 20,2023.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akionesha mali zilizokamatwa na Jeshi la Polisi 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu bangi iliyokamatwa na Jeshi la Polisi 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akionesha mali zilizokamatwa na Jeshi la Polisi 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Leornad Nyandahu akionesha mali zilizokamatwa na Jeshi la Polisi 
Share:

WATU WANNE WAKAMATWA KWA KUCHEZEA VIPIMO KWENYE MADUKA YA KUUZIA NYAMA JIJINI DAR ES SALAAM



************* 

Wakala wa Vipimo Mkoa wa Dar es Salaam imeendeshaukaguzi wa kushtukiza kwenye maduka ya kuuzia nyama kwalengo la kujiridhisha kama Vipimo vinatumika kwa usahihi.Takribani maduka 21 yamekaguliwa na Bucha nne zimebainikakufanya udanganyifu kwa kutokutumia Vipimo kwa usahihi ilikuwapunja wanunuzi wa bidhaa hizo. 

Akizungumza mara baada ya zoezi la ukaguzi wa kushtukizaMeneja wa Wakala wa Vipimo Ilala Bw. Alban Kihullaamesema, kuwa zoezi hilo ni la Kisheria na hufanyika mudawowote, siku yoyote na saa yoyote lengo likiwa ni kuangaliamatumizi ya vipimo kama yanatumika kwa usahihi kwa mujibuwa Sheria. 

Meneja Kihulla amesema, kwa ukaguzi uliofanyikawatuhumiwa wamebainika kuwaibia wateja wao kiasi cha nusukilo katika kila kilo mbili zinazonunuliwa na bucha zinginezimekuwa zikiibia wateja kiasi cha gramu 250 kwenye kila kilo moja ya nyama. 

Kihulla ameeleza kuwa, watuhumiwa wote waliokamatwawamechukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria ya VipimoSura ya 340 Mapitio ya 2002 na marekebisho yake ili iwe funzokwa wafanyabiashara wengine wenye tabia za kuchezea Vipimo. 

Wakala wa Vipimo inatoa wito kwa Wananchi wote kuwamakini wanapoenda kununua nyama kwenye madukambalimbali na kuwataka washiriki kwenye tukio la upimajikuliko kuwa amini wauzaji na endapo watabaini changamotoyoyote wawasiliane nao kwa namba ya simu ya bila malipo ya0800 110097 kwa msaada. 

Kadharika, wito umetolewa kwa wauzaji wote wa nyamakuachana na tabia za kuvunja Sheria kwa kuwaibia wateja waona wahakikishe wanatenda haki kwa kupima nyama kwa usahihina kwenye mizani sahihi iliyohakikiwa kwani kinyume nakufamya hivyo wataondoa uaminifu kwa wateja wao nawatachukuliwa hatua kali za Kisheria. 

Vilevile, wamiliki wa Bucha za nyama wametakiwa kufuatiliamwenendo wa biashara zinavyofanyika kwenye maeneo yao yabiashara kwa kuwa linapotokea tatizo lolote la wizi kwakutotumia mizani kwa usahihi hawatakuwa salamawatachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger