Saturday, 26 November 2022

MAHAFALI YA 15 YA CHUO KISHIRIKI CHA ELIMU DAR ES SALAAM (DUCE)

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwatunuku Wahitimu Digirii za Umahiri ya Elimu katika Taaluma za Mitaala kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwatunuku Wahitimu Digirii za Umahiri ya Elimu katika Uongozi wa Elimu na Taaluma za Sera kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwatunuku Wahitimu Digirii za Umahiri, Stashahada ya Uzamili na Digirii za Awali kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapatia zawadi ya vyeti wahitimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam.Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar akizungumza kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Prof.William Anangisye akizungumza kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Rasi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Prof.Stephen Maluka akizungumza kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Naibu Rasi-Taaluma, Utafiti na ushauri Elekezi, Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam, Dkt.Christina Raphael Isingo akizungumza kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Boniventure Rutinwa akizungumza kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao akisoma hotuba kwa niaba ya wahitimu kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Baadhi ya Wakuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Chuo hicho Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika Maandamano kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Wahitimu wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) wakiwa kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Wakuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Chuo hicho Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam. Wakuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Chuo hicho Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi yawadau wa chuo hicho kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam.Wakuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Chuo hicho Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) kwenye Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KUPITIA Mradi wa HEET, Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) kinatarajia kutumia zaidi ya shilingi Bilioni kumi na saba kwaajili ya kuendelea kufanya ukarabati wa miundombinu ya majengo ya Chuo, kujenga majengo na miundombinu mingine mipya na kusomesha wanataaluma katika ngazi ya uzamili na uzamivu kwenye Vyuo Vikuu mbalimbali duniani.

Ameyasema hayo leo Novemba 26,2022 Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Balozi Mwanaidi Maajar katika Mahafali ya 15 ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yaliyofanyika chuoni hapo.

Amesema Baraza linaendelea kuiomba Serikali na wafadhili wengine kusaidia kuongeza miundombinu ya ujifunzaji na ufundishaji chuonii hapo kwani kumekuwa na changamoto za maabara na vifaa vingine muhimu vya kufundishia na kujifunzia.

"Neema ya ongezeko la wanafunzi kila mwaka imekuwa haiendi sambamba na ongezeko la miundombinu kama vile kumbi za mihadhara, upungufu mkubwa wa hosteli kwa wanafunzi na gharama kubwa ya kusomesha wanataaluma katika ngazi ya uzamili na uzamivu". Amesema

Nae Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Prof.William Anangisye ameipongeza Serikali kwa kuendelea kutoa rasilimali muhimu zinazohitajika katika uendeshaji wa Chuo.

Amesema Serikali imeendelea kujenga na kuboresha miundombinu muhimu na kutoa fedha za uendeshaji wa Chuo kwa ujumla. Ambapo pia amewashukuru wabia wao wa kitaifa na kimataifa waliochangia gharama za uandaaji na uendeshaji wa programu mbalimbali za masomo ambazo wahitimu wameshiriki na kunufaika nazo.

Kwa upande wake Rasi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Prof.Stephen Maluka amesema kwa mwaka 2022/2023 Chuo kimetenga shilingi 480,035,000/= kwaajili ya mafunzo ya watumishi ambapo kati ya kisi hicho, shilingi 101,448,00/= ni kwaajili ya mafunzo ya muda mfupi na shilingi 378,587,000/= kwa ajili ya mafunzo ya muda mrefu.

Ameeleza kuwa jumla ya watumishi 54 wanatarajiwa kunufaika na mafunzo hayo kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

"Chuo kimetenga dola za Kimarekani 1,000,000 sawa na Bilioni 2.3 za Kitanzania kwaajili ya mafunzo ya muda mrefu ya watumishi kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi ambapo jumla ya watumishi 16 wanasomeshwa Digirii za Umahiri na Uzamivu katika Vyuo mbalimbali duniani". Amesema Prof.Maluka.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 26,2022

















Share:

Friday, 25 November 2022

HUYU MWANAUME ALINITESA SANA KATIKA MAHUSIANO ILA SASA NIMEMTULIZA

Jina langu ni Brenda kutokea Mbeya nchini Tannzania, mimi ni binti wa miaka 24, niliingia katika mahusiano na kijana mmoja, nikampa kila kitu nilichoweza kwa wakati huo.

Nakumbuka kipindi kile nyumbani tulikuwa tuna ng'ombe, niliiba maziwa kila siku na kumpelekea nyumbani kwao, nilimpend sana, penzi letu likawa huru alipoanza maisha yake mwenyewe.

Sikuwa najua lolote kuhusu mapenzi, alinifundisha yeye, nikatengeneza maisha yangu yote kwake, akanifanya nikawa mtumwa wa ngono kila nikienda ghetto kwake.

Kama haikutosha sasa akaanza kunifundisha kunywa pombe, niliamini kuwa ndiye mume wangu mtarajiwa, kwa nini nikatae. Nilimkubalia kila kitu.

Alinilazimisha ngono hata nilipokuwa katika siku zangu, kweli nilikuwa msomi na niliyajua madhara ya kufanya hivyo lakini sikutaka kumuudhi huyo niliyeamini kuwa ni mume wangu.

Nilipenda tutumie kinga lakini aliipinga sana, nikapata mimba ya kwanza!! Hakuwa na pesa lakini alinilazimisha niitoe. Nikachukua hela nyumbani nikafanya alivyotaka, kwa mara ya kwanza nikatoa mimba.

Haikuniuma sana, niliamini kuwa ni yeye atakuja kunioa na atanifichia aibu hii, nilitegemea sasa tutaanza kutumia kinga. Lakini hapana haikuwa hivyo.

Aliendelea kunilaghai, tayari aliujua udhaifu wangu, alinishika hapa na pale, nikishtuka tayari amefanya anavyojua, nikavumilia kwa kuwa alikuwa mume wangu mtarajiwa.

Mume asiyejulikana hata kwa wazazi, nilimfumania na mke wa mtu, niliumia sana kwa sababu nilikuwa nampenda nilimsamehe,

hivyo nilifanya jinsi anavyotaka yeye ila mwisho wa siku nilichoka na kurudi nyumbani kwetu.

Miaka ikapita, miezi ikaenda kipindi nipo mtandaoni nilikutana na maoni ya watu kuwa Dr. Kiwanga anatatua migogoro ya kimahusianpo. Nilichukua namba yake na kumpigia nikamuelezea jinsi mahusiano yangu ulivy vunjika, nashukuru akanipa tiba yake iliyokuja kubadili kila kitu.

Siku chache mbele niliona simu yake akinipigia na kuomba msamaha, kwa sababu nilikuwa nampenda bado niliweza kumsamehe tukaanza maisha mapya. Nilimshukuru sana Dr. Kiwanga kwa kunirudishia mpenzi wangu, kwa sasa amenio na tumeza kujaliwa watoto wawili.

Ukiachana na hilo, Dr. Kiwanga ana uwezo kumfanya mtu kuwa na bahati maishani mwake, kushinda katika michezo ya bahati nasibu, kukukinga na maadui zako, kukufanya ushinde migogoro kama ya ardhi, kuwa na mvuto wa kimapenzi, kuongeza mauzo katika biashara.

Vile vile anatibu magonjwa kama Kaswende, Kisonono, Kifua Kikuu, Presha na mengine mengi, kwa mawasiliano zaidi mtumie barua pepe; kiwangadoctors@gmail.com, tembelea tovuti yake; www.kiwangadoctors.com au piga simu +254 769404965.

Mwisho.
Share:

HAKIRASILIMALI WAHITIMISHA JUKWAA LA UZIDUAJI MWAKA 2022 JIJINI DODOMA, WADAU WAPONGEZA KUPANUA UELEWA SEKTA YA UZIDUAJI

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali Adam Anthony akizungumza wakati wa ufungaji wa Jukwaa la Sekta ya uziduaji mwaka 2022.

Na Marco Maduhu, DODOMA

JUKWAA la Sekta ya uziduaji lililoandaliwa na HakiRasilimali, limehitimishwa Rasmi leo, huku wadau wakiwamo madiwani ambao wanatoka kwenye maeneo ya uchimbaji madini, wakipongeza kupanua uelewa katika ya Sekta ya uziduaji.



Jukwaa hilo la sekta ya uziduaji lilianza jana Novemba 24, 2022 na limehitishwa leo Novemba 25, huku mada mbalimbali zikiwasilishwa pamoja na kujadiliwa kwa lengo la kuikuza Sekta ya uziduaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali Adam Anthony, akizungumza wakati wa kufunga jukwaa hilo, amewashukuru wadau wote wa Sekta ya uziduaji kwa ushiriki wao muda wote ndani ya siku hizo mbili.

Nao wadau wa Sekta ya uziduaji akiwamo Diwani Faustine Shibiliti kutoka Kata ya Igalula wilayani Sengerema mkoani Mwanza, wameshukuru kujumuika kwenye jukwaa hilo la uziduaji, ambalo wamesema limewaongezea uelewa zaidi kufahamu mambo mengi katika Sekta ya uziduaji ambayo inahusisha Madini, Mafuta na Gesi asilia.

Aidha, jukwaa hilo la uziduaji limeshirikisha wadau takribani 200 kutoka katika maeneo mbalimbali ambayo yanajihusisha na Sekta  ya uziduaji, wakiwamo wawakilishi kutoka Serikali Kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Asasi za Kiraia, Makampuni ya Madini, wachimbaji wadogo wa madini, wawakilishi kutoka katika jamii inayoishi maeneo ya migodi, wanataaluma na waandishi wa habari.

Lengo la jukwaa hilo la uziduaji ni kujadili, kubadilisha uzoefu na kujifunza kutoka kwa washiriki namna ya kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika sekta ya uziduaji.


Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali Adam Anthony akizungumza wakati akifunga Jukwaa la Sekta ya uziduaji mwaka 2022.

Diwani wa Kata ya Igalula wilayani Sengerema mkoani Mwanza Faustine Shibiliti akitoa shukrani kwa kupata elimu na kuongeza uelewa zaidi juu ya Sekta ya uziduaji.

Madiwani ambao wanatoka kwenye maeneo ya Sekta ya uziduaji wakiendelea kutoa neno la shukrani, kupata elimu katika Sekta ya uziduaji kupitia jukwaa za uziduaji.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.
Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la  uziduaji mwaka 2022.

Wadau wa Sekta ya uziduaji wakiwa kwenye jukwaa la uziduaji mwaka 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali Adam Anthony akipiga picha ya pamoja na wadau wakubwa wa jukwaa hilo la Sekta ya uziduaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali Adam Anthony, akipiga picha ya pamoja na Bodi ya HakiRasilimali.

Picha ya pamoja ikipigwa kati ya wadau wakubwa wa Jukwaa la Sekta ya uziduaji na wafanyakazi wa HakiRasilimali.
Picha za Pamoja zikiendelea kupigwa na waongoza mjadala kwenye jukwaa hilo la Sekta ya uziduaji.

Picha za Pamoja zikiendelea kupigwa.

Picha za Pamoja zikiendelea kupigwa.

Picha za Pamoja zikiendelea kupigwa.

Share:

WATUMISHI WAASWA KUTUNZA SIRI ZA SERIKALI


MWENYEKITI wa Tume ya Watumishi wa Umma ,Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola, akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya chamwino Mkoani Dodoma wakati wa ziara ya Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma walipotembelea Halmashauri hiyo.


Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma wakisiliza ,Kutoka kulia ni Mhe.Balozi Rajabu Adadi, Mwenye Ushungi Mhe.Hadija Mbala, katikati Balozi John Haule, wa Nne kutoka kulia Mhe.Imaclute Ngwale Wapili kutoka Kushoto Mhe.Suzani Mlawi na Wa kwanza kushoto Mhe.Nasoro Nambira katibu Tawala.


Mtoza Ushuru Stendi ya wilaya ya Chamwino Hajara Ibrahimu akitoa maelekezo jinsi Mashine za POS zinavyofanya kazi kwa Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma walipotembelea Halmashauri ya Chamwino Mkoani Dodoma.


Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Chamwino mara baada ya kutembelea Halmashauri ya Chamwino Mkoani Dodoma.

..............................

Na Alex Sonna-CHAMWINO

MWENYEKITI wa Tume ya Watumishi wa Umma ,Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola, amewataka watumishi wa Umma kutunza Siri za Serikali ili kulinda Maslahi ya Nchi.

Hayo ameyasema wakati wa ziara ya Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma walipotembelea Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino.

Jaji Mstaafu Mhe. Kalombola,amewahimiza watumishi kuwa waminifu katika kulitumikia Taifa kwa kulinda maslahi kwa kutunza viapo vyao na kuacha kuvunjisha siri za utumishi.

''Kuna baadhi ya watumishi wa Serikali wamekuwa na mmomonyoko wa maadili kwa kuvunjisha siri za Serikali hivyo tunawaomba waache tabia hiyo walinde viapo vyao kwa kusimamia maadili ya utumishi wao.''amesema Jaji Mstaafu Mhe. Kalombola

Aidha Jaji Mstaafu Mhe. Kalombola amewataka watumishi kuwa wabunifu katika kazi zao ili kuongeza mapato na kujiletea maendeleo kwenye Taasisi zao na wachukulie changamoto kama sehemu ya kazi zao.

Vilevile Jaji Mstaafu Mhe. Kalombola ameeleza kuwa Tume hiyo katika majukumu yake imejiwekea utaratibu wa kutembelea Taasisi pamoja na maeneo mbalimbali ya Serikali kwa lengo la kuelimisha,kuelekeza uwajibikaji na kubadilishana uzoefu ili kuboresha uendeshaji wa usimamizi na maswala ya utumishi kwa mujibu wa sheria.

"Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassani inawathamini sana watumishi wa Umma Kwa Mchango mnaoutoa katika kuwahudumia wananchi kwenye kuleta maendeleo yao"amefafanua Jaji Mstaafu Mhe. Hamisa

Kwa Upande wake Kamishna wa Tume, Mhe. Nassor Mnambila amewashukuru viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino kwa muitikio wao na mapokezi yao makubwa kwenye ziara hiyo yenye lengo la kutoa mrejesho na kujifunza namna ya ukusanyaji wa mapato.

"Tunawashukuru viongozi wa Halmashauri hii kwa mapokezi yenu na kukubali kuja kwenu kujifunza namna mashine hizi za posi zinavyotumika kukusanya mapato lakini pia tuwapongeze kwa ujenzi wa madarasa Matatu mukishirikiana na wananchi". Amesema Mhe.Nambila

Katika Ziara ya Makamishna wa Tume katika Halmashauri ya Chamwino ilikuwa na lengo la kujifunza, kuelimisha na kuwakumbusha watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma,
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger