Wednesday, 16 November 2022

TUME YA UCHAGUZI YAENDESHA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA UCHAGUZI MDOGO MOROGORO

Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi wakilakiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Japhet Bwire Manyama wakati wa mafunzo ya wasimamizi hao kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Tanga Jiji na Lushoto ambao wanataraji kufanya uchaguzi mdogo katika kata zao Desemba 17,2022.
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Adv. Magdalena Rwebangira akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya siku tatu ya wasimamizi Uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi pamoja na watendaji wengine wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo na Kata ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa udiwani unaotaraji kufanyika tarehe 17 Desemba, 2022. Mafunzo hayo yanayohusisha washiriki 42 kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Jiji la Tanga na Lushoto yanafanyika Mkoani Morogoro.
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Adv. Magdalena Rwebangira akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya siku tatu ya wasimamizi Uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi pamoja na watendaji wengine wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo na Kata ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa udiwani unaotaraji kufanyika tarehe 17 Desemba, 2022. Mafunzo hayo yanayohusisha washiriki 42 kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Jiji la Tanga na Lushoto yanafanyika Mkoani Morogoro. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Uchaguzi, Stephen Elisante na wengine kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu wa Tume, Felister Ishuza na Mwenyekiti wa Mafunzo hayo ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Handeni, Maryam Ahmad Ukwaju.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Uchaguzi, Stephen Elisante akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Mwenyekiti wa Mafunzo hayo ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Handeni, Maryam Ahmad Ukwaju akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki ambao ni Wasimimizi wa uchaguzi na Wasimamizi wasaidi wa Uchaguzi kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Jiji la Tanga na Lushoto yanafanyika Mkoani Morogoro wakifuatilia mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki ambao ni Wasimimizi wa uchaguzi na Wasimamizi wasaidi wa Uchaguzi kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Jiji la Tanga na Lushoto yanafanyika Mkoani Morogoro wbakifuatilia mafunzo hayo.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Japhet Bwire Manyama akiongoza kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri kwa wazimamizi na wasimamizi wasaidi wa uchaguzi wakati wa mafunzo ya wasimamizi hao kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Tanga Jiji na Lushoto ambao wanataraji kufanya uchaguzi mdogo katika kata zao Desemba 17,2022.
Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi wakilakiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Japhet Bwire Manyama wakati wa mafunzo ya wasimamizi hao kutoka Halmashauri sita za Jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo mji, Kibaha Mji, Handeni Mji, Tanga Jiji na Lushoto ambao wanataraji kufanya uchaguzi mdogo katika kata zao Desemba 17,2022.

**************
Na Mwandishi Maalum, Morogoro
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewataka wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kutoka katika Kata zinazotaraji kufanya uchaguzi mdogo wa udiwani Desemba 17, 2022 kutofanya kazi ya uchaguzi kwa mazoea, badala yake wazingatie sheria, kanuni za uchaguzi pamoja na maelekezo ya Tume katika utendaji wao.

Tume pia imewataka wasimamizi wa nchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kuhakikisha wanavishirikisha Vyama vyote vya Siasa na wadau wengine wa uchaguzi ili kurahisha utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Adv. Magdalena Rwebangira wakati akifungua mafunzo ya siku tatu ya wasimamizi wa Uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata yanayofanyika Mkoani Morogoro.

Adv. Rwebangira amesema Uchaguzi ni mchakato unaojumuisha, hatua na taratibu mbalimbali za kufuatwa na kuzingatiwa kwani hatua na taratibu hizo ndiyo msingi wa uchaguzi kuwa mzuri, wenye ufanisi na hivyo kupunguza kama siyo kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

“Nachukua nafasi hii kuwaasa kuwa pamoja na uzoefu ambao baadhi yenu mnao katika uendeshaji wa uchaguzi, ni vyema mhakikishe mnazingatia maelekezo mtakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea”,alisema Adv. Rwebangira.

Aidha amewataka kujiamini na kufanya kazi kwa weledi, na kwamba katika utendaji wa majukumu yao wanapaswa kuzingatia Katiba ya Nchi, Sheria za Uchaguzi na Kanuni zake, Maadili ya Uchaguzi na Maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume na kuongeza kua jambo hilo lisiishie katika mafunzo na nadharia bali ionekane kufuatiwa katika kutenda.

“Sanjari na hilo nawaasa kukumbuka kuvishirikisha Vyama vya Siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika maeneo yenu katika masuala ya kiuchaguzi ambayo wanastahili kushirikishwa kwani jambo hilo litawarahisishia sana utekelezaji wa majukumu yenu,”alisema  Adv. Rwebangira.

Wasimamizi hao wametakiwa kuhakikisha wanayatambua na kuyajua vizuri maeneo ambayo chaguzi utaendeshwa ikiwemo hali ya miundombinu ya kufika katika Kata na hasa Vituo vya kupigia kura.

“Mfanye utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika kwa lengo la kuhakikisha mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani,”alisema Adv. Rwebangira.

Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Adv. Magdalena Rwebangira pia amewataka wasimamizi hao kuhakikisha kuwa wanaajiri watendaji wa vituo wenye weledi, wanaojitambua na kwa kadri inavyowezekana kuacha undugu au upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi.

Alisema jambo muhimu wanalotakiwa kuzingatia Wasimamizi hao wa uchaguzi ni kujiamini, kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia Katiba ya nchi, sheria za uchaguzi na kanuni zake, maadili ya uchaguzi pamoja na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume.

Aidha Mjumbe wa Tume hiyo ya uchaguzi, aliwasisitizia wasimamizi hao wa uchaguzi kuhakikisha wanafanya utambuzi wa vituo vya uchaguzi mapema kwa lengo la kuhakikisha mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Stephen Elisante, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uchaguzi alisema uchaguzi huo mdogo wa udiwani utafanyika katika Kata 12 za Tanzania Bara ila waliopo katika mafunzo hayo Mkoani Morogoro ni kutoka katika Kata sita za Vibaoni – Halmashauri ya Mji wa Handeni, Lukozi – Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Misugusugu – Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Majohe - Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mnyanjani - Halmashauri ya Jiji la Tanga na Dunda - Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo.

Mapema kabla ya ufunguzi wa Mafunzo hayo watendaji w uchaguzi hao walikula kiapo cha kutunza siri na kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vyao vya siasa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Morogoro, Mhe. Japhet Bwire Manyama.
Share:

WAZIRI MKENDA NA WAZIRI LELA MOHAMED WAONGOZA KIKAO CHA MAPITIO YA SERA NA MITAALA JIJINI DODOMA

 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prf .Adolf Mkenda (Mb) akiteta jambo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Mohamed Hadid .
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar  Lela Mohamed .


Na Mathias Canal, WEST-Dodoma.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prf Adolf Mkenda (Mb) pamoja na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Mohamed wameongoza Kikao cha kazi cha mapitio ya Sera na Mitaala.


Akizungumza katika kikao hicho cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na timu za mapitio ya Sera na Mitaala ya Elimu katika ukumbi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi-Ndejengwa Jijini Dodoma leo tarehe 15 Novemba 2022, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoojia Mhe Prof Adolf Mkenda amesema kuwa mapitio hayo yanahusisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuwa na mtazamo wa pamoja katika sekta ya elimu.


Waziri Mkenda amesema kuwa hatua za awali zimekamilika hivyo kwa sasa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inajiandaa kwa ajili ya kumpitisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika hatua zote zilizofikiwa kabla ya mkutano mkuu wa wadau wote wa sekta ya elimu kujadili mustakabali wa elimu ya Tanzania.


Waziri Mkenda amesema kuwa kabla ya mkutano wa wadau wa elimu nchini pia kutakuwa na mkutano wa kazi wa baraza la Mawaziri na makatibu wakuu wa Wizara zote ili kujadili kwa kina kuhusu mustakabali wa sekta ya elimu na mapendekezo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuhusu sekta ya elimu nchini.


Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Mohamed amempongeza Waziri Mkenda kwa usimamizi madhubuti wa timu zote za mapitio ya sera na mitaala kwani imeonyesha nia ya dhati na umakini wa serikali katika kuhakikisha maboresho ya elimu yanakuwa shirikishi.


Amesema kuwa kazi hiyo ya Mapitio ya Sera na Mitaala yanafanyia kwa upande wa Tanzania Bara pamoja na Tanzania Visiwani-Zanzibar kwa lengo la kuimarisha elimu kwa pande zote mbili za Muungano ili wanafunzi wanapokutana chuo kikuu wawe na uelewa wa pamoja.


"Sisi Mawaziri tumepewa maagizo ya kuhakikisha tunasimamia mabadiliko haya ya sera na mitaala bila kupishana, hata kama wale wanakuwa wakiogelea kule baharini na hawa wanakulia kwenye milima na kwenye madini lakini mwisho wa siku yule mvuvi na yule muwindaji wawe katika lugha moja katika mifumo yetu" Amesisitiza Mhe Lela


Kadhalika, Waziri Lela amepongeza kwa wadau kutoka pande zote mbili za muungano kushirikishwa katika mapitio ya sera na mitaala kwani mjadala huo pia unasaidia kamati ya Zanzibar katika utekelezaji wa majukumu yake.


Amesema kuwa mpaka sasa maoni yote yanayokusanywa bado ni mali ya Wizara kabla ya mapendekezo ya serikali kwa ujumla ambayo inaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan pamoja na Mhe Dkt Hussein Mwinyi kwa upande wa Zanzibar ambaye tayari ameridhia kupitishwa katika hatuazili zofikiwa.



Share:

WMA WASHAURIWA KUJENGA VITUO VYA UHAKIKI VIPIMO KANDA MBALIMBALI NCHINI

Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (aliyevaa miwani) akikagua na kupata maelekezo kutoka kwa Afisa wa WMA katika Chumba maalum cha vifaa vya uhakiki wa vipimo vya Mita za Umeme vilivyopo Misugusugu mkoani Pwani, anayeshuhudia katikati ni Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Pwani, Alban Kihulla. Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Pwani, Alban Kihulla akitoa maelekezo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira waliotembelea Kituo cha uhakiki wa vipimo, kilichopo Misugusugu mkoani Pwani. Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (kulia) akiteta jambo na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu, Wakala wa Vipimo (WMA) Bi. Stella Kahwa wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilipotembelea Taasisi hiyo katika Kituo cha uhakiki wa vipimo, Misugusugu mkoani Pwani.

*************************

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imewashauri Wakala wa Vipimo nchini (WMA) kujenga vituo mbalimbali vya uhakiki wa vipimo vya dira za Maji, Umeme na Malori ya Mafuta kama inavyofanyika kwenye Kituo cha uhakiki wa vipimo hivyo, Misugusugu mkoani Pwani.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea Kituo hicho kilichopo Misugusugu, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. David Kihenzile amewapongeza WMA kwa kazi nzuri inayofanyika ya kutoa huduma bora tangu kuanzishwa Kituo hicho mwaka 2019.

“Kamati tunawapongeza WMA kwa kazi nzuri inayofanyika hapa, lengo sio kumpa Mlaji kitu kisicho bora, lengo tuhakikishe Mlaji anapewa kile kilicho bora, Mfano kwenye uhakiki wa Mita za Maji na hata Mita Umeme, uhakiki uwe wa vipimo stahiki”, amesema Mhe. Kihenzile

Mhe. Kihenzile ameongeza, “Tunashauri vituo hivi viongezwe katika Kanda mbalimbali nchini ili kurahisisha utoaji huduma ya uhakiki na kumlinda Mlaji na yule anayetoa huduma”.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe amesema kuwa mtoa huduma na Mlaji wananufaika na vipimo stahiki kupitia Taasisi hiyo ya Wakala ww Vipimo ambayo ipo chini ya Wizara hiyo.

Mhe. Kigahe amesema Serikali kupitia Wizara hiyo itaendelea kutoa huduma bora kwa Taasisi zake mbalimbali ili kuhakikisha Wananchi wananufaika na fedha za Kodi wanazolipa katika nchi yao.

“Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imetutembelea hapa kwenye Kituo cha uhakiki wa vipimo mbalimbali, tutajitahidi kuwaomba kuongeza Bajeti katika mwaka wa fedha ujao ili Taasisi zetu ndani ya Wizara yetu ziongezewe nguvu ili kufanya kazi kwa ufanisi wa hali juu”, amesema Mhe. Kigahe.

Naye Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu, Wakala wa Vipimo (WMA) Bi. Stella Kahwa amesema watahakikisha wanaendelea kutoa huduma bora kwa Watoa huduma na kuhakikisha Walaji wa mwisho wa huduma hizo wanalindwa.

Bi. Kahwa amesema ujio wa Kamati hiyo ya Bunge, ni fursa kwao WMA na endapo wataongezewa Bajeti katika Taasisi hiyo watahakikisha wanatumia vizuri katika kuboresha mazingira ya Ofisi zake sehemu mbalimbali nchini ili kufanya uhakiki wa vipimo sahihi, kuboresha vitendea kazi na Watumishi wake.

Kituo hicho cha uhakiki wa Vipimo vya dira za Maji, Umeme na Malori ya Mafuta kilijengwa mwaka 2019 katika eneo la Misugusugu, mkoani Pwani ambapo kimekuwa mfano mzuri na kuigwa kwa nchi jirani za Malawi, Uganda, Kenya Zambia katika utoaji mzuri wa huduma zake za uhakiki wa vipimo hivyo.
Share:

TABOA YAUNGA MKONO UTARATIBU UTAKAORUHUSU MABASI YA ABIRIA KUSAFIRI USIKU



*************************

CHAMA Cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) kimeunga mkono na kumpongeza Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson kwa hatua yake ya kuitaka Serikali kuangalia upya utaratibu utakaoruhusu mabasi ya abiria kusafiri usiku.

Akizungumza Dar es Salaam Mweka Hazina wa Taboa ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Usalama Barabarani Taifa Issa Nkya amesema wanaungana na Dkt Tulia katika hilo kwani ni jambo ambalo hata wao wamezungumzia kwa muda mrefu.

Awali akizungumza suala hilo hivi karibuni wakati aliposhiriki Semina kwa Wabunge kuhusu usalama Barabarani iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Jijini Dodoma, Dkt Tulia alisema haoni tatizo kutoruhusu magari ya abiria kutembea usiku ikiwa magari mengine tofauti na ya abiria yanafanya hivyo.

Dkt Tulia alisema ni wazi kuwa hatua hiyo ya kuyazuia magari hayo pamoja na mambo mengine kinarudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi na kutaka wanaohusika kuangaliwa upya utaratibu huo ili kama kuna kikwazo chochote kiweze kutafutiwa ufumbuzi.

“Kuna shida gani ya kuzuia gari ya abiria kusafiri usiku? Tunatamani nchi yetu kuchangamka zaidi kiuchumi sasa kwanini magari haya yawe na zuio wakati magari mengine yanaruhusiwa kusafiri hadi usiku, Kama ni changamoto ya miundombinu basi ishughulikiwe na kama ni usalama Polisi wapo Cha msingi wekeni utaratibu huo ili shughuli zifanyike,” alisisitiza Dkt. Tulia

Aidha kauli ya Dkt Tulia imekuja ikiwa imepita miezi takribani tisa tangu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa azungumze Bungeni kuwa haoni tatizo lolote kwa mabasi hayo kusafiri usiku akisisitiza kuwa hatua hiyo itazidi kuchochea ukuaji wa uchumi.

Alitoa kauli hiyo Februari 10 ambapo alimuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) kujiridhisha na hali ya Usalama sambamba na kuzitaka Mamlaka zote zinazohusika kuweka utaratibu utakaofanikisha suala hilo.

Kwa upande wao TABOA kupitia kwa Mweka Hazina wake Nkya, alisema wao hawaoni tatizo la mabasi hayo ya abiria kutembea usiku na mchana na kwamba wao kama wasafirishaji ni jambo ambalo wamelipigania kwa muda mrefu.

"Kama alivyosema Spika wa Bunge Dkt Tulia, Kuna faida nyingi za kuwa na utaratibu wa kusafirisha abiria Kwa nyakati zote usiku na mchana, watu Kwa sasa wanafanya shughuli za kiuchumi usiku na mchana hivyo kuweka utaratibu wa kusafiri mchana peke yake ni kurudisha nyuma juhudi hizo" amesema Nkya

Amesisitiza wao kama wasafirishaji watakuwa wa watu wa kwanza kutoa ushirikiano utakaohitajika ili suala hilo liweze kufanikiwa ikiwa ni pamoja na kuzungumza na wanachama wao wote nchi nzima ili huduma ambazo watatoa kwa massa yote 24 ziweze kuwa na ufanisi na siyo kuifanya kuwa changamoto.
Share:

Tuesday, 15 November 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 16,2020











Share:

BENKI YA CRDB YAENDESHA SEMINA KWA WATEJA WAKE WA MKOA WA TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba akizungumza wakati akitoa hotuba yake katika ufunguzi rasmi wa Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Afisa Mkuu wa Biasra wa Benki ya CRDB, Boma Raballa akizungumza wakati akitoa mada ya biashara na uwekezaji katika Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Chiku Issa akizungumza katika Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa akizungumza katika Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Hashim Mgandilwa akizungumza katika Semina ya siku moja kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba (kulia) asalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, wakati alipowasili kwa lengo la ufunguzi rasmi wa Semina kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa na wa pili kulia ni Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Tanga, January Kirambata.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba (katikati) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakiwasalimia baadhi ya viongozi waandamizi wa Benki ya CRDB, wakati alipowasili kwa lengo la ufunguzi rasmi wa Semina kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.






Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, muda mfupi baada ya ufunguzi rasmi wa Semina kwa Wateja wa Benki ya CRDB wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga, Novemba 14, 2022.


Share:

TAASISI YA DORIS MOLLEL YAZINDUA RASMI SIKU YA MTOTO NJITI


********************

Taasisi ya Doris Mollel (Mollel Foundation) leo imezindua rasmi Maadhimisho ya Mtoto Njiti Duniani ambayo yanatarajiwa kufikia kilele chake Novemba 20, 2022 ambayo yatafanyika katika Viwanja vya Robanda vilivyopo katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Sea Shell, Kijitonyama jijini Dar, ulihudhuriwa na balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Dkt. Mehmet Gulluoglu.

Siku hiyo ya kilele, taasisi hiyo itakabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 180,190,000 ambavyo vitakwenda katika Hospitali za Wilaya za Serengeti, Ukerewe, Kwimba na Magu pamoja na ufungaji wa mitambo ya hewa ya Oxygen kwa watoto wachanga.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger