Monday, 8 November 2021

HAWA NDIYO WASHINDI NBC DODOMA MARATHON, MILIONI 200 ZAKUSANYWA KUPAMBANA NA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI


Mshindi wa kwanza mbio za km 42 wanaume NBC Dodoma Marathon Mtanzania Tumaini Habie akiiibuka akimaliza mbio hizo baada ya kutumia muda wa saa 02:17:15.
*****
Mbio za hisani za kimataifa zilizoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) “NBC Dodoma Marathon” zimefanikiwa kukusanya fedha zaidi ya Mil 200 kwa ajili ya kusaidia mapambano dhidi ya Saratani ya mlango wa Kizazi kwa akina mama huku ikishuhudiwa wanariadha kutoka Tanzania wakifanya vizuri zaidi kwenye mashindano hayo kwa kuibuka vinara kwenye mbio za km 42 na km 21.

Katika mbio hizo zilizofanyika jijini Dodoma  na kupambwa na uwepo wa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa ilishuhudiwa Mwanariadha Mtanzania Tumaini Habie akiiibuka mshindi wa kwanza kwenye mbio za KM 42 upande wa wanaume baada ya kumaliza kwa muda wa saa 02:17:15, akifuatiwa na mshiriki kutoka nchini Kenya Eyanae Paul aliyetumia muda wa saa 02:18:31.

Mtanzania Abrahamu Too alimaliza katika nafasi ya tatu kwa kutumia muda wa saa 02:19:04

Upande wa wanawake mshindi wa kwanza katika mbio za km 42 ni Mkenya Cheruto Isgah aliyetumia muda wa saa 02:45:03 akifuatiwa na Watanzania Jackline Sakilu na Sara Ramadhani waliotumia muda wa saa 02:45:46 na 02:46:13 kila mmoja.

Mwariadha wa Kimataifa kutoka Tanzania Alphonce Simbu aliibuka mshindi wa kwanza kwenye mbio za KM 21 hizo baada ya kumaliza kwa muda wa saa 01:03:46, akifuatiwa na watanzania wengine katika nafasi ya pili na ya tatu ambao ni Joseph Panga pamoja na Daniel Giniki waliotumia muda wa saa 01:04:18 na 01:05:37 kila mmoja.

Upande wa wanawake mshindi wa kwanza katika mbio za km 21 ni Mtanzania Failuna Abdi aliyetumia muda wa saa 01:14:50 akifuatiwa na Wakenya Lelei Jepkemboi na Tanui Euliter waliotumia waliotumia muda wa saa 01:15:18 na 01:17:21

Katika mbio hizo ilishuhudiwa mshindi wa kwanza wa kilometa 42 kwa wanaume na wanawake kila mmoja akiondoka na Sh milioni 5.5 huku upande wa kilometa 21, mshindi akiondoka na kitita cha Sh milioni 3.5, wakati katika kilometa 10, mshindi alipewa Sh milioni 1.5 na mshindi wa kilometa tano alipewa Sh milioni 1.

Akikabidhi hundi ya mchango huo yenye thamani ya sh mil 200 kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dk. Julius Mwaiselage pamoja na zawadi kwa washindi wa mbio hizo, Waziri Bashungwa pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa kuandaa vema mbio hizo alisema licha ya faida nyingine za kimichezo umuhimu wa mbio hizo unapimwa zaidi katika lengo lake la kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kina mama.

“Tangu kuanzishwa kwa mbio hizi huu ukiwa ni msimu wa pili sasa, serikali imekuwa mstari wa mbele kuziunga mkono kutokana na dhima yake kuu ya kuwasaidia kina mama dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi. Tunashukuru kuona nia hiyo imefanikiwa na sasa tunakwenda kuokoa maisha ya maelfu ya kina mama kupitia jitihada za kimichezo.’’ Alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi aliwashukuru washiriki pamoja na wadhamini wa mbio hizo kwa kufanikisha lengo kuu la mbio hizo la kuchangia huduma za afya katika Hospitali ya Ocean Road, hasusani matibabu ya saratani ya shingo ya kizazi, ambayo ndiyo inayoongoza kwa vifo vitokanavyo na saratani nchini.

Alisema kupitia mbio hizo mwaka jana waliweza kukusanya fedha kiasi cha sh mil 100 kwa ajili ya kukabiliana na changamoto hiyo na mwaka huu lengo lilikuwa ni kukusanya kiasi cha sh mil 200 zilizopatikana kupitia usajili wa washiriki wa mbio hizo pamoja na michango mbalimbali kutoka kwa wadhamini wa mbio hizo.

“Ndio maana pamoja na yote tunatumia fursa hii kujipongeza sisi sote tukiwemo waandaaji, washiriki pamoja na wadhamini wetu kwa kufanikisha lengo hili muhimu. Pamoja na kwamba tumepata washindi wa mbio hizi lakini bado kila mshiriki ni mshindi kwasababu amefanikisha kuokoa maisha ya mama zetu,’’ alisema.

Akipokea msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dk. Julius Mwaiselage aliishukuru benki hiyo kwa jitihada hizo huku akibaisha kuwa msaada huo unakwenda kusaidia mapambano hayo katika maeneo mbalimbali hususani mikoani ili kuwahi matibabu kwa wagonjwa ambao wamekuwa wakifika hospitalini wakiwa katika hatua ya mwisho ya ugonjwa huo.

Awali akizungumzia matokeo hayo Rais wa Shirikisho la Riadha Taifa (RT) Bw Silas Isangi alisema kufanya vizuri kwa watanzania katika mbio mbalimbali hapa nchini ni kutokana na maandalizi mazuri yanayofanywa na wanariadha hao huku akibainisha kuwa huo ni mwanzo tu kwa kuwa matokeo hayo mazuri ya watanzania yanatarajiwa hadi kimataifa.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa (wa tatu kushoto) akikabidhi hundi yenye thamani ya Tsh mil 200 kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dk. Julius Mwaiselage ikiwa ni mchangp wa mbio za NBC Dodoma Marathon ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa uzazi kwa kina mama. Wengine ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (wa tano kushoto)


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa (kushoto) akikabidhi zawadi ya fedha taslimu kwa mshindi wa mbio za Km 21wanawake katika mbio za NBC Dodoma Marathon Failuna Abdi (Kulia) zilizofanyika hii leo jijini Dodoma.



Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa (kushoto) akikabidhi zawadi ya fedha taslimu kwa mshindi wa mbio za Km 21 wanaume katika mbio za NBC Dodoma Marathon Alphonce Simbu (Kulia) zilizofanyika hii leo jijini Dodoma. Kulia ni mshindi wa tatu wa mbio hizo Daniel Giniki kutoka Tanzania.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa (wa tatu kushoto) akikabidhi zawadi ya fedha taslimu kwa mshindi wa mbio za Km 21 katika mbio za NBC Dodoma Marathon Alphonce Simbu (wa pili Kulia) zilizofanyika hii leo jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Hassan Abbasi (Kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (wa tatu kulia) Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo (wa pili kulia) na Rais wa Shirikisho la Riadha Taifa (RT) Bw Silas Isangi (Kulia)




Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa (kulia) akikabidhi zawadi ya fedha taslimu kwa mmoja wa washindi wa mbio za walemavu katika mbio za NBC Dodoma Marathon zilizofanyika hii leo jijini Dodoma.






Tupo tayari kuanza mbio!




Washiriki wa mbio za NBC Dodoma Marathon wakipoza miili yao kwenye moja ya kituo cha maji wakati wakiendelea na mbio zao.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa mbio za NBC Dodoma Marathon wakiwemo wadhamini wa mbio hizo


Baada ya mbio washiriki walipata fursa ya kujipumzisha, kufahamiana na kubadilishana mawazo wakati wakisubiri zawadi zao.


Baadhi ya washiriki wa mbio hizo wakiendelea na mashindano


Mmoja wa washiriki wa mbio hizo upande wa walemavu akiendelea na mashindano.


Msemaji wa Benki ya NBC Bw William Kallaghe akitoa neno la shukrani kwa washiriki na wadhamini wa mbio hizo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi akiwashukuru washiriki pamoja na wadhamini wa mbio hizo kwa kufanikisha lengo kuu la kuchangia huduma za afya katika Hospitali ya Ocean Road, hasusani matibabu ya saratani ya shingo ya kizazi, ambayo ndiyo inayoongoza kwa vifo vitokanavyo na saratani nchini.

Mwariadha wa Kimataifa kutoka Tanzania Alphonce Simbu aliibuka mshindi wa kwanza kwenye mbio za KM 21 wanaume NBC Dodoma Marathon baada ya kumaliza kwa muda wa saa 01:03:46
Share:

Weighbridge Operator 6 Job Opportunities at TANROADS

Weighbridge Operators (6 Posts)   Ref. No. AB.322/267/01/02 The Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Agency under the Ministry of Works and Transport which is responsible for the Development and Maintenance of the Trunk and Regional Roads Network in Tanzania Mainland. Apart from this, it is also responsible in conducting Axle Load Control Operations using […]

This post Weighbridge Operator 6 Job Opportunities at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Drivers 6 Job Opportunities at TANROADS

Drivers   Ref. No. AB.322/267/01/02 The Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Agency under the Ministry of Works and Transport which is responsible for the Development and Maintenance of the Trunk and Regional Roads Network in Tanzania Mainland. Apart from this, it is also responsible in conducting Axle Load Control Operations using Weighbridges. The […]

This post Drivers 6 Job Opportunities at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Weighbridge Shift In-Charge at TANROADS

Weighbridge Shift In-Charge (3 Posts)   Ref. No. AB.322/267/01/02 The Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Agency under the Ministry of Works and Transport which is responsible for the Development and Maintenance of the Trunk and Regional Roads Network in Tanzania Mainland. Apart from this, it is also responsible in conducting Axle Load Control Operations […]

This post Weighbridge Shift In-Charge at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 8, 2021

Magazetini leo Jumatatu November 8,2021


Share:

Sunday, 7 November 2021

CCM YAMTEUA SHANGAI KUGOMBEA UBUNGE NGORONGORO, GULAMHAFEEZ MUKADAM, MASUMBUKO KUGOMBEA UMEYA SHINYANGA


Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa imekutana katika kikao maalum Jumapili 7 Novemba, 2021 Ikulu ya Chamwino, Jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan.

Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Ndugu Emmanuel Lekishon Shangai kuwa mgombea wa Ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Ngorongoro katika uchaguzi

mdogo utaofanyika tarehe 11 Disemba, 2021 kufuatia kifo cha Marehemu William Tate Ole Nasha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo.

Kamati Kuu imewateua Ndugu Gulamhafeez Abubakar Mukadam na Ella's Ramadhani Masumbuko kugombea kiti cha Umeya katika Manispaa ya Shinyanga.

Katika hatua nyingine kamati kuu imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya ujenzi wa taifa Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa.

Kamati Kuu imempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kutimiza mwaka mmoja tangu kuingia madarakani kuwa Rais wa nane wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na kuendeleza mshikamano, kulinda tunu ya Umoja, Amani, utulivu sambamba na utekelezaji makini na imara wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020 - 2025.
Share:

WAOMBOLEZAJI WAKIMBIA MAZISHI YA JAMAA ALIYEDAIWA KUFA KISHA AKAIBUKA GHAFLA MSIBANI

Wakaazi wa Kongelai huko Pokot Magharibi nchini Kenya walikula kona kwa hofu na mshtuko wakati mwanaume waliyemdhania kuwa ameaga dunia kuibuka wakati wakiendelea na shughuli za mazishi yake. 

Kangrok Muriumeler ambaye ni mfanyabiashara wa mifugo, aliripotiwa kutoweka wiki jana baada ya kuzuru jiji la Nairobi.

Wachuuzi wa mboga katika soko la Konglai walidai mwili uliokuwa ukioza ulitupwa karibu na soko katika eneo hilo na kuwafahamisha maafisa wa polisi waliouchukua. 

Wakazi hao walidai baada ya kutambuliwa, familia ilisema mwili huo ulikuwa ni wake Muriumeler na mara moja wakaanza kuandaa mazishi yake.

Mmoja wa wachuuzi wa mboga mboga, Nelly Pusha ambaye alizungumza na The Nairobian alisema aliwafahamisha polisi kuhusu mwili huo ambao ulikuwa umetupwa katika eneo hilo.

 "Tulihisi harufu kali kwa siku kadhaa kabla ya kuwafahamisha wakazi wengine na baada ya uchunguzi, tulipata mwili uliokuwa ukioza uliofanana na Muriumeler," alisema. 

Mchuuzi huyo alisema jamaa zake walisambaza habari kwamba alitoweka baada ya kupeleka ngombe Nairobi kuuzwa lakini hakurudi tena.

Aliongeza kuwa familia ilipouona mwili huo mara moja walithibitisha kuwa ulikuwa ni wa mpendwa wao na papo hapo maandalizi ya kumzika yakaanza.

Hata hivyo, Muriumeler alisema wenyeji na ndugu zake walidhani alikuwa ameaga dunia na baada ya kufika nyumbani, alishtuka kukuta mipango ya mazishi yake tayari inaendelea.

 Alisema alichukua muda mrefu kuwaeleza jamaa zake kuwa bado yu hai, lakini bado hawakuamini. "Nilikuwa narudi nyumbani kutoka soko la Chepareria nilikutana na watu waliokuwa wakiangalia kiajabu. Waliniambia marafiki na familia yangu walikuwa wakiomboleza kifo changu,” alisema.

 “Nilipowasili kutoka Nairobi, sikurudi nyumbani mara moja. Nilifululiza hadi Chepareria kuwaona marafiki zangu na nikalala huko siku mbili.”

Muriumeler alisema kwa mshtuko mkubwa alipokuwa akielekea nyumbani kwake Kongelai, alikutana na waendesha bodaboda ambao walimwambia watu walikuwa wakiomboleza kifo chake.

“Nilikuwa na wakati mgumu kuwathibitishia kwamba nilikuwa hai. Wapo waliokuwa wakiniambia kuwa nimefariki dunia, na kiwiliwili changu kilikuwa kimewatembelea,” alisema huku akitaka kusitishwa kwa mipango ya mazishi mara moja.

OCS wa Kapenguria Lucas Wamocha alisema mwili huo ambao haujulikani ulirudishwa katika makafani ya Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kapenguria.

 "Mwili bado haujatambuliwa. Haukuwa na majeraha popote. Inaonekana marehemu aliuawa kwingine na kutupwa. Tumesambaza taarifa hizo kwenye mtandao wetu wa polisi, lakini hatujapata taarifa za watu waliopotea,” alisema.

Jamaa alifunga safari hadi jijini Nairobi kwenda kuwauza mifugo lakini akatoweka kwa wiki moja

Jamaa wake walimsaka na mwili tofauti ukapatikana huku jamaa wa familia wakifikiria ni mpendwa wao

Shughuli za mazishi zilianza na kabla ya mwili kuzikwa aliyekuwa ametoweka alirejea nyumbani na wakazi kufikiri ilikuwa ni mizuka

 Baadaye ripoti ziliibuka kuwa ameuawa na mwili wake kupatikana katika soko la Konglai ambapo ulikuwa umetupwa na kuanza kuoza.

Wakazi walihofia kuwa alikuwa amefariki na walichokuwa wakishuhudia ilikuwa ni mizuka na wala si jamaa wao.

 Visa vya familia kuwazika watu wasio wao hufanyika wakati mwingi haswa ambapo DNA haijafanywa ili kuidhinisha kweli miili iliyopatikana. Kisa kama hicho kilifanyika Rongo ambapo familia ya Fred Ochieng ilikuwa imeandaa mazishi yake kabla ya kurejea nyumbani.

 Alikuwa ametoweka nyumbani kwa miezi miwili na baadaye familia ikapata mwili ambao iliamini ni wake na kuanza kuandaa mazishi.

 Alibaki kinywa wazi alipofika nyumbani na kupata kuwa alikuwa akizikwa huku jamaa wa familia wasiamini




Share:

MWENYEKITI WA CCM SAMIA SULUHU AFUNGA MAFUNZO YA MAKATIBU WA CCM


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifunga mafunzo ya makatibu wa wilaya na mikoa wa Chama hicho

Na Dotto Kwilasa, DODOMA.

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefunga mafunzo ya makatibu wa wilaya na mikoa wa Chama hicho katika ukumbi wa NEC Makao Makuu ya Chama Jijini Dodoma jana Jumamosi tarehe 6 Novemba, 2021.

Aidha mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku nne kuanzia tarehe 3 Novemba, 2021,yanatajwa na wanachama wa Chama hicho kuwa yataongeza tija na ari ya uongozi na hatimaye kifikia maendeleo ya pamoja.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya habari na Katibu wa uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka ,amesema Rais Samia ameridhia utaratibu wa mafunzo ndani ya Chama Cha Mapinduzi na kwamba utakuwa endelevu.

Aidha kutokana na umuhimu wake katika kukidhi mahitaji ya wakati na mabadiliko ya mwenendo wa siasa za Sasa,mafunzo hayo yatakuwa na manufaa katika kuleta mabadiliko ya kiutendaji na ufanisi.

Shaka amesema,mafunzo hayo ni nyenzo muhimu sana katika kuongeza weledi na ufanisi wakufikia malengo ya taasisi yoyote ile.

"Chama Cha Mapinduzi tutafanya utaratibu huu kuwa endelevu ili kukidhimahitaji ya wakati na mwenendo wa mabadiliko ya siasa za dunia,kutokana na mafunzo haya Mama Samia ametuonyesha namna ambavyo uongozi ni kushirikishana,lakini pia ametukumbusha kutimiza wajibu wetu kwa wakati,"amesema Shaka.

Licha ya hayo Shaka ameeleza Katika taarifa yake kwamba Katika mafunzo hayo Rais Samia amehimiza umoja,mshikamano na maelewano miongoni mwa viongozi na wanachama wa CCM ilikazi ya kuendelea kukiimarisha chama katika kuwatumikia wananchi iweniendelevu na ya kudumu.

"Tukifanya hivi hatimaye tutaleta tija hasa ikizingatiwa kuwa Chama ChaMapinduzi kimebeba matumaini makubwa ya watanzania katika kuwaleteamaendeleo endelevu ya kiuchumi,kijamii na kisiasa,"amefafanua.

Mbali na hayo ameeleza mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wa kiutendaji Viongozi hao ikiwa ni pamoja na uweledi na ufanisi.

"Tuna imani sasa kwamba Watendaji wa CCM wa Mikoa na Wilaya katika kusimamia katiba ya chama,kanuni,ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025,maelekezo ya vikao na masuala mbalimbali ya kuisimamia serikali na ujenziwaTaifa,"amesisitiza.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Rais Samia Suluhu Hassan akipunga mkono kwa Watendaji wa Chama hicho ngazi ya mikoa na Wilaya jijini Dodoma
Katibu wa uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka akizungumza kwenye mafunzo hayo
Makatibu wa wilaya na mikoa wa CCM wakiwa Katika mkutano, ukumbi wa NEC Makao Makuu ya Chama Jijini Dodoma Jumamosi tarehe 6 Novemba, 2021.
Share:

WANANCHI WATAKIWA KULINDA MIUNDO MBINU YA TANESCO



.........................................................


Wananchi wametakiwa kulinda miundo mbinu ya Tanesco dhidi ya watu wasiowaadilifu wanaoiba miundo mbinu hiyo huku wananchi wenye tabia ya kuchoma nguzo wametakiwa kuacha tabia hiyo mara moja .


Akitoa elimu kwa wananchi juu ya masuala ya ulinzi wa miundo mbinu ya Tanesco mkoani Morogoro katika vijiji vyote vilivopo mkoani Afisa kutoka kitengo cha masoko makao makuu Tanesco Bi Jennifer Mgendi amewasisitiza wananchi kulinda miundombinu kwa kuwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzake.


Aidha Bi. Mgendi ameendelea kutoa ushauri kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya matapeli (VISHOKA) wanao watapeli na kujifanya wanatokea TANESCO kwa kuwadhulumu fedha .


“Fedha zote za serikali hulipwa kwa kupitia control namba pekee mtu yoyote asije akawadanganya mkampa fedha bila kutumia control namba watu wanaibuka ili kuwaibia nyie wananchi msiojua hivyo kila mmoja asikubaili kulipa fedha yoyote na kwa mtu yoyote bila kutumia control namba”amesema Bi.Mgendi.


Hata hivyo wananchi wametakiwa kuchangamkia fursa ya umeme kwa kuwanufaisha katika kuwaingizia kipato lengo ikiwa ni kuwainua kiuchumi .


“Umeme ni kitu muhimu sana kwa maendeleo katika maisha kukua kwa sayansi na teknolojia umeme huu umetusaidia kurahisisha maisha na ndio maana tunahakikisha kila mwananchi anapata umeme bila kujali hali ya maisha aliyonayo.”Amesema Bi. Mgendi.


Amesema wananchi wametakiwa kutokufanya shughuli za kijamii chini ya miundo mbinu kama laini au transfoma kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha afya zao .
Share:

MWANAFUNZI AKUTWA AMEFARIKI HOSTELI


Familia moja mjini Kisii Nchini Kenya imeziomba mamlaka za uchunguzi kubaini kilichomuua mtoto wao wa kiume aliyekutwa amefariki kwenye kitanda chake ndani ya bweni lao shule yao.

Taarifa zinaeleza kuwa marehemu Enock Morara ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Upili ya St.Paul Amasago eneo la Keumbu, kaunti ya Kisii alilala kama kawaida lakini hakuamka kama wenzake walivyoamka na baadaye akagundulika amefariki.

Uchunguzi wa kitabibu uliofanyika katika hospitali ya Rufaa ya Kisii bado haujabaini chanzo cha kifo cha mtoto huyo.

Wakati huo huo, maofisa wa Polisi nao wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusu kifo cha mwanafunzi huyo.
Share:

Picha : RAIS SAMIA AONGOZA KIKAO CHA NEC IKULU, DODOMA



Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Novemba 7, 2021 ameongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa iliyokutana Ikulu, Chwamwino Mkoani Dodoma.
PICHA NA IKULU
Share:

RC HOMERA ASHIRIKI MAKABIDHIANO YA TREKTA NDOGO 24I KWA WAKULIMA MBARALI - MBEYA


Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera hivi karibuni akiwa mgeni rasmi amekabidhi Trekta ndogo (Powertillers) aina ya Kubota 241 zenye thamani ya Tshs. 2.6 Billion, vifaa hivyo vimetolewa na kampuni ya Agricom Africa Kwa udhamini wa mkopo kupitia CRDB Bank kwa wakulima wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya matrekta yaliyotolewa na Agricom Africa ltd Kwa udhamini wa mkopo kupitia CRDB Bank Ltd
Mtendaji Mkuu wa Agricom Africa Ltd Bw. Alex Duffar akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya matrekta yaliyotolewa na Agricom Africa ltd kupitia udhamini wa mkopo wa CRDB Bank
Mwakilishi wa Meneja wa kanda WA Benki ya CRDB nyanda za juu kusini akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya matrekta yaliyotolewa na Agricom Africa ltd kupitia udhamini wa mkopo wa CRDB Bank Igurusi mbeya
Mkuu wa mkoa akiwasha mojawapo ya trekta
Picha ya pamoja Kati ya mkuu wa mkoa wa Mbeya na wakulima waliokabidhiwa trekta ndogo aina ya Kubota Powertillers

Mkuu wa mkoa wa Mbeya,mwakilishi wa Meneja wa kanda WA Benki ya CRDB na Mtendaji Mkuu wa AGRICOM AFRICA LTD wakiwa na funguo kama ishara ya makabidhiano ya matrekta yaliyotolewa na Agricom Africa ltd kupitia udhamini wa mkopo wa CRDB Bank.
Mtendaji Mkuu wa AGRICOM AFRICA LTD akifurahia picha ya pamoja na wakulima waliokabidhiwa trekta ndogo aina ya Kubota Powertillers kwenye ofisi za Agricom Africa ltd Igurusi
Wakulima waliokabidhiwa trekta ndogo aina ya Kubota Powertillers
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger