Friday, 29 January 2021
RAIS MAGUFULI AZINDUA MRADI WA MAJI ISAKA-KAGONGWA MKOANI SHINYANGA
MHUBIRI ALIYEJIGAMBA KUFUFUA WAFU SIKU YA ALHAMIS AKAMATWA
MHUBIRI ALIYEJIGAMBA KUFUFUA WAFU SIKU YA ALHAMIS AKAMATWA
DIAMOND PLATNUMZ AFUNGUKA KUHUSU BABA YAKE MZAZI

TMDA INAVYODHIBITI UTENGENEZAJI NA UINGIZAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA KUHAKIKISHA USALAMA KWA WATUMIAJI

Ofisi ya Mamlaka ya Dwa na Vifaa Tiba Kanda ya Ziwa.Thursday, 28 January 2021
WADAU WA HABARI KANDA YA ZIWA WAAHIDI KUENDELEA KUFANYA KAZI NA VYOMBO VYA HABARI
SILINDE : TAMISEMI TUTAPAMBANA NA WANAOWANYANYASA MACHINGA

Naibu Waziri wa TAMISEMI David Silinde amesema Wizara ya TAMISEMI imejikita kwenye Kuondoa kero na kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara Wajasiriamali wadogo wadogo almaarufu kama Machinga.
Ameyasema hayo leo Mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wa Kongamano la Machinga lililo fanyika jijini Dar es Salaam likiwa na lengo la kuwashukuru kwa kuiamini Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kutatua kero na changamoto zinazowakabili Machinga
"Kama Wizara ya TAMISEMI Tumepokea na kusikiliza changamoto za Machinga na tunazifanyia kazi. Changamoto ya Mikopo tumetoa nafasi kwa Machinga wakiwa na vitambulisho vya ujasiriamali mkajiunga vikundi mnapewa mikopo",amesema Silinde
Pia amegusia Tatizo la unyanyasaji wa Wafanyabiashara hao unaofanywa na Mgambo na kuahidi kulifanyia kazi.
"Kuna kero pia ya Mgambo kuwasumbua Machinga na sio kwamba wanatumwa na Serikali kuwanyanyasa wananchi bali ni hulka zao binafsi. Serikali ya Rais Magufuli haitavumilia wananchi wake kunyanyaswa tutashuka na kuwashughulikia",amesema.
Pia ameagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinafanya mikutano ya Hadhara kila mwaka na Machinga ili kusikiliza kero zao na kuzitatua.
"Machinga wamekuwa wakiomba mikutano na viongozi wa wilaya ili kusikiliza Changamoto na kero na tumeahidi kila mwaka mikutano miwili hadi mitatu ili kuwaskiliza",amesema Silinde.
UMMY MWALIMU : NEMC MSIFANYE KAZI YA UPOLISI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Ummy Mwalimu ameliagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa umma ili kuwasaidia wenye viwanda na wawekezaji kuzingatia Sheria ya Usimamizi wa Mazingira.
Amesema hayo hii leo, Jijini Dodoma alipokuwa akitoa taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Majukumu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).
Waziri Ummy amesema kuwa kumekuwa na malalamiko ya ucheleweshaji wa vibali, utozwaji wa faini kubwa hivyo ameliagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira kufanya kazi kwa weledi zaidi na kuwaelekeza wawekezaji kufuata taratibu.
“NEMC mna kazi ya kuwasaidia wawekezaji kuzingatia Sheria na taratibu zilizopo na si vinginevyo, mkiwa wakali watu hawatatii Sheria lakini mkielimisha jamii itatii” ,Waziri Ummy alisisitiza.
Awali akiwasilisha taarifa ya Majukumu ya NEMC Mkurugenzi Mkuu Dkt. Samuel Gwamaka amesema kuwa Sheria ya Mazingira, 2004 na Kanuni za Usimamizi wa Mazingira (Tathmini ya Athari na Ukaguzi wa Mazingira) (marekebisho), 2018 zinataka miradi yote inayowekezwa nchini kufanyiwa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kabla ya kuanza kutekelezwa. Miradi iliyowekezwa kabla ya kuwepo Sheria ya Mazingira inatakiwa kufanyiwa Ukaguzi wa Mazingira (Environmental Audit).
“Baraza limesajili jumla ya Wataalam elekezi wa mazingira 908 kwa ajili ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na 423 wa Ukaguzi wa Mazingira. Kati ya hao Makampuni yaliyosajiliwa kufanya EIA ni 173 na EA ni 94”, Dkt. Gwamaka alisisitiza.
Amesema, Baraza limeendelea kuboresha kanzidata ya wataalamu hao na kupata wataalam Washauri 299 wenye sifa za kutoa ushauri wa masuala ya mazingira na kuwasilisha miradi yao. Kati ya Wataalam hao 191 ni wataalam binafsi (Individual Environmental Experts) na 108 ni kampuni (Firms of Environmental Experts).
Kutokana na azma ya Serikali ya kuelekea uchumi wa kati wa viwanda, Baraza limekuwa likipokea miradi mingi na linatarajia ongezeko kubwa la uwekezaji katika sekta hiyo.
Katika kukabiliana na malalamiko ya wadau kuhusu Tozo, kanuni ya ada na tozo za Mazingira ya mwaka 2016, 2018, 2019 imepunguza baadhi ya tozo katika Sekta ya Kilimo, Usajili wa Miradi ya Tathmini ya athari kwenye Mazingira (TAM).
Kwa upande mwingine Mjumbe wa Kamati hiyo Askofu Josephat Gwajima ametoa ushauri kwa Serikali kubuni miradi ya kuchakata taka ili kuzalisha nishati. “Ndugu zangu taka hivi sasa ni mali, naishauri Serikali kutazama suala hili kwa kina na kuhimiza utenganishaji wa taka kuanzia ngazi ya kaya”, Gwajima alisisitiza.
MOI YAWEKA HISTORIA KWA MARA YA KWANZA.... YAANZA KUTOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA MISHIPA YA DAMU KWENYE UBONGO BILA KUFUNGUA FUVU



Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface akiwa katika picha ya pamoja na jopo la madaktari bingwa, wauguzi na wataalamu wa radiolojia kutoka MOI, MNH, AGHAKHAN na JKCI walioshiriki katika tukio la kihistoria la kuchunguza ubongo bila kufungua fuvu.*******************************************
Taasisi ya Mifupa Muhimbili- MOI Imeandika Historia ambapo kwa mara ya kwanza imeanza kutoa huduma ya uchunguzi wa mishipa ya damu kwenye ubongo bila kufungua fuvu la kichwa katika maabara ya kisasa ya upasuaji wa ubongo (Angio Suite).
Uchunguzi huo umefanywa kwa masaa 3 na jopo la madaktari bingwa, wauguzi, watalamu wa radiolojia wazalendo 6 kutoka MOI, MNH,JKCI pamoja na hospitali ya Aghakhan. Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface amesema kuanza kwa maabara hii ni ishara ya mageuzi makubwa katika sekta ya afya hapa nchini kwani maabara ya kisasa kama hii haipo kwenye nchi nyingine kwenye ukanda wa afrika mashariki kati.
“Leo ni siku ya furaha sana kwani tumeanza kutumia maabara yetu ya upasuaji wa ubongo (Angio suite) ,hii imewezekana kutokana na dhamira ya dhati ya Mh Rais Dkt John Pombe Magufuli ya kuboresha huduma za afya hapa nchini kwani maabara hii imejengwa Serikali ya awamu ya Tano kwa zaidi ya Tsh Bilioni 7.9, kwakweli tunamshukuru sana Mh Rais” Alisema Dkt Boniface
Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa Ubongo MOI Dkt Lemery Mchome amesema kuanza kwa maabara hii kumeleta mageuzi makubwa katika huduma za uchunguzi na upasuaji wa ubongo hapa nchini kwani hakuna mgonjwa atakayelazimika kwenda nje ya nchi kufuata huduma hii ambayo ilikuwa haipatikani hapa nchini.
“ Tunashukuru upasuaji umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa, tumeweza kufika kwenye ubongo wa mgonjwa bila kufungua fuvu, tumefanya upasuaji huu katika mazingizra mazuri kwani mitambo hii ni ya kisasa sana, kama mnavyoona mgonjwa yuko macho na anaongea vizuri kabisa ,hana kovu wala maumivu, hii ni hatua kubwa sana kwetu kama wataalamu.
Mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji huo Bwana Hafidhi saidi kutoka mkoani Singida amemshukuru Mungu kwa huduma aliyopata kwani amakuwa akipata maumivu kwa kipindi kirefu bila kujua anasumbuliwa na ugonjwa gani.
“Namshukuru sana Mh Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua vifaa hivi ambavyo vimesaidia leo nimehudumiwa hapa MOI, Nawashukuru madaktari na wataalamu wote walionihudumia, nimefurahi sana na nawaambia watanzania wenzangu wenye shida kama yangu waje wahudumiwe hapa MOI,” Alisema Hafidhi
Huyu ni mgonja wa kwanza kupata huduma katika maabara hii ya kisasa ya upasuaji wa Ubongo iliyojengwa na Serikali ya awamu ya Tano Kwa zaidi ya Tsh Bilioni 7.9
NAIBU WAZIRI UMMY NDERIANAGA: TUNACHUKUA HATUA MADHUBUTI KULINDA NGUVU KAZI YA NCHI




********************************************
Na Mwandishi Wetu
Serikali imesema inachukua hatua za maksudi za kulinda nguvu kazi yake dhidi ya majanga, ajali na magonjwa yatokanayo na kazi ambayo yanaweza kutokea na kuwaathiri wafanyakazi hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inajenga uchumi imara wa viwanda.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Ummy Nderianaga, ameyasema hayo wakati akihitimisha mafunzo ya Usalama na Afya kazini yaliyokuwa yakitolewa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Nderiananga amesema TANESCO ina nafasi muhimu katika kuliwezesha Taifa kufikia agenda yake ya kujenga uchumi wa viwanda ambapo ufanisi wa shirika hilo unategemea uwepo wa wafanyakazi ambao watakuwa salama na wenye afya njema.
“Bila shaka mnatambua umuhimu wenu na Shiriki lenu katika kufanikisha agenda ya nchi yetu ya kuimarisha uchumi kupitia mageuzi ya viwanda ambapo ili kufikia azma hiyo ni lazima kuwe na umeme wa uhakika. Hata hivyo, upatikanaji wa uhakika wa nishati hiyo muhimu unategemea uwepo wa watumishi wenye afya njema na wenye ujuzi stahiki kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao,”alisema Naibu Waziri huyo.
Aidha, Nderianga amesema ili jitihada zinazochukuliwa na serikali katika kuleta maendeleo hususan ujenzi wa miradi mikubwa ya umeme na miradi mingine ziwe na tija ni lazima kuhakikisha kwamba nguvu kazi yake inalindwa ipasavyo.
“Ni kutokana na sababu hii ya msingi ndio maana leo mko hapa ili kupewa nyenzo za kujiepusha na madhara ya ajali na magonjwa yanayoweza kujitokeza katika maeneo yenu ya kazi. Kwasababu hiyo, ninaupongeza uongozi wa Shirika pamoja na OSHA kwakuliona hilo na kuchukua hatua kwa wakati,”aliongeza Naibu Waziri.
Akitoa maelezo ya awali kwa Mgeni Rasmi, Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda, amesema mafunzo hayo ambayo yalijikita katika masuala ya utoaji wa Huduma ya Kwanza mahali pa kazi yalitolewa kwa takribani siku tisa kwa makundi matatu tofauti ya watumishi wa TANESCO ambapo kila kundi lilipata mafunzo hayo kwa siku tatu.
Kwa mujibu wa Mtendaji huyo mkuu wa OSHA zaidi ya watumishi 120 wa TANESCO kutoka katika mikoa mbali mbali hapa nchini wamepatiwa mafunzo ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao katika hali ya usalama na afya.
“Tunafahamu TANESCO mnafanya kazi ambazo ni hatarishi hivyo pamoja na kwamba mna fahamu lakini tumeona kuna umuhimu wa kuendelea kukumbushana ili kuweza kuokoa maisha au kupunguza madhara pale ajali au magonjwa yanapotokea katika sehemu zetu za kazi,” alieleza Mwenda.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Dkt.Phillis Nyimbi ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo amesema OSHA imekuwa ikifanya vizuri katika Kanda ya Ziwa hususan katika kutoa miongozo na maelekezo kuhusu masuala ya Usalama na Afya mahali pa kazi.
Aidha, baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Dativa Mahembe na Elton Mwashala wamebainisha kwamba mafunzo waliyoyapata yataleta tija katika kazi zao za kila siku hususan katika kuokoa maisha au kupunguza athari miongoni mwa wafanyakazi wanaopata ajali au changamoto mbali mbali za kiafya wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kila siku.
“Japo mafunzo haya yamefanyika kwa siku tatu tu, kiukweli tumejifunza mambo mengi sana ambayo ni muhimu si tu katika sehemu za kazi lakini pia hata majumbani na mahali pengine,” alisema Dativa Mahembe ambaye ni mshiriki na pia mratibu wa mafunzo hayo.
OSHA ni taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) ambayo majukumu yake ya msingi ni pamoja na kufanya ukaguzi wa Usalama na Afya katika sehemu za kazi na kutoa mafunzo mbali mbali yakiwemo ya Huduma ya Kwanza, usalama na afya katika shughuli za ujenzi, usalama na afya katika shughuli za mafuta na gesi, Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Uchunguzi wa ajali katika sehemu za kazi na kufanya kazi katika majukwaa (Working at Height).







































