Wednesday, 13 January 2021

Serikali yaitangaza Wilaya ya Chato kitovu cha uhifadhi na utalii Kanda ya Ziwa


Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Damas Ndumbaro ameitangaza wilaya ya Chato mkoani Geita kuwa kitovu cha uhifadhi na utalii kwa Kanda ya Ziwa, kutokana na eneo hilo kuwa na vivutio vingi vya utalii, uhifadhi wa miti, hifadhi za Taifa pamoja na utalii wa ziwa.

Dkt Ndumbaro ameyasema hayo wakati akikagua shamba la miti la Biharamulo lililopo wilayani Chato mkoani Geita.

Kufuatia tangazo hilo, Waziri huyo wa Maliasili na Utalii amewataka Wafugaji na Wakazi wanaozunguka hifadhi za Taifa zilizopo wilayani humo kuacha mara moja kuingiza mifugo yao ndani ya hifadhi hizo.

Ameonya kuwa, mtu yeyote atakayeingiza mifugo ndani ya hifadhi hizo, akibainika mifugo yake itataifishwa.

Dkt Ndumbaro amewataka Wafanyakazi wa shamba hilo la miti la Biharamulo kuhakikisha wanalitunza ili liendelee kuwa la mfano kwa mashamba mengine.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Dos Santos Silayo amesema kuwa, Wakala huo utahakikisha ndani ya kipindi cha miaka ishirini ijayo wanamaliza kupanda miti katika shamba hilo ambalo ni la pili kwa ukubwa hapa nchini.




Share:

Marekani Yaituhumu Iran Kuwa ni 'kambi mpya' ya mtandao wa al-Qaeda


Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Mike Pompeo ameituhumu Iran kwa kuwa na ushirikiano wa ksiri ya mtandao wa al-Qaeda. 

Kutokana na madai hayo, Pompeo amewawekea maafisa kadhaa wa Iran vikwazo.

Kwenye hotuba yake kwa waandishi wa Habari, Pompeo aliishutumu Iran kwa kuwa na uhusiano wa siri na al-Qaeda huku akitaja duru za ujasusi zinazodai kuwa Iran ilimhifadhi kiongozi wa pili wa mtandao huo Abu Muhammad al-Masri ambaye aliuawa mwezi Agosti na mawakala wa Israel.

 Kauli ya Pompeo imejiri wiki moja tu kabla ya utawala wa Trump kuondoka ofisini, na inaonekana kulenga nia ya rais mteule Joe Biden kuanzisha mazungumzo na Iran kuhusu makubaliano ya mwaka 2015 ya mpango wa nyuklia. 

Rais Donald Trump aliiondoa Marekani kwenye mkataba huo mwaka 2018.



Share:

Pence akataa kutumia ibara ya 25 kumuondoa Trump madarakani


Makamu wa rais wa Marekani Mike Pence amemwambia rasmi spika wa bunge Nancy Pelosi kwamba haamini kuwa hatua ya kutumia ibara ya 25 ya katiba ya nchi hiyo kumuondoa Trump madarakani ni kwa manufaa ya nchi au hata kuendana na katiba.

Ujumbe wa Pence umejiri mnamo wakati baraza la wawakilishi lilikuwa likijadili pendekezo la kutumia ibara hiyo ya 25.

Hata hivyo inatarajiwa kuwa wabunge wataendelea na mchakato wa bunge kwa lengo la kumuondoa Trump au kuzima matarajio yake kuwania urais baadaye.

Awali katika tukio tofauti, Rais Trump alisema ibara hiyo haitakuwa na maana yoyote kwake. 

Trump alisema pia kuwa wito wa kutaka aondolewe madarakani kwa njia ya mashtaka bungeni vilevile ni baya zaidi.

Kwingineko, majenerali wakuu wa jeshi nchini Marekani, wameshutumu uvamizi uliofanywa na wafuasi wa Rais Trump dhidi ya majengo ya bunge wiki iliyopita.

Kwenye taarifa ya pamoja iliyosainiwa na wakuu wanane wa kijeshi wakiongozwa na mwenyekiti wao jenerali Mark Milley, tukio hilo lilikuwa shambulizi la moja kwa moja dhidi bunge la Marekani na dhidi ya mchakato wa kikatiba.

Shirika la upelelezi FBI limesema tayari limewafungulia watu 170 mashtaka na mamia kadhaa pia watakamatwa na kushtakiwa.

Jeshi la nchi hiyo limesema litawapeleka maafisa wake wa kikosi cha ulinzi wa taifa 15,000 kushika doria siku ya kuapishwa kwa Joe Biden, Januari 20.

 

Credit:DW



Share:

Uganda yafunga mitandao ya kijamii, masaa machache kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu hapo kesho


Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema serikali yake imefungia mitandao ya kijamii nchini humo kuelekea uchaguzi wa rais ambao umepangwa kufanyika kesho Alhamisi.

Museveni aliyezungumza usiku wa kuamkia leo ameishutumu kampuni ya Facebook kwa kile alichokitaja kuwa ujeuri, baada ya kampuni hiyo ya mitandao ya kijamii kufunga akaunti kadhaa zinazohusishwa na kampeni yake kutaka achaguliwe tena.

Museveni amesema ana uhakika serikali imefunga mitandao ya kijamii na amewaomba msamaha Waganda kwa hali hiyo.

Akizungumza kuhusu mtandao wa Facebook, Museveni amesema ikiwa mtandao wowote unataka kufanya kazi Uganda, basi ni lazima utoe nafasi sawa kwa wote, lakini ikiwa unataka kuwa na upendeleo dhidi ya chama tawala basi hauruhusiwi.

Hakukuwa na jibu au kauli ya moja kwa moja kutoka kwa kampuni ya Facebook kuhusu hatua hiyo ya Rais Museveni.

 

-DW



Share:

Waliokaidi Mkataba Wa Narco Kikaangoni Ndani Ya Siku Kumi


Na. Edward Kondela
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ametoa siku kumi kwa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kubaini na kuwanyang’anya maeneo, wawekezaji waliopatiwa vitalu katika ranchi za taifa ambao wamebadili matumizi ya ardhi kinyume na makubaliano ya mikataba yao.

Waziri Ndaki amebainisha hayo jana (12.01.2021) wakati alipotembelea Ranchi ya Usangu iliyopo Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo na kufanya mkutano wa hadhara na baadhi ya wawekezaji, wakulima na wafugaji, ambao wanafanya shughuli zao katika ranchi hiyo na kubaini kuwa baadhi ya wawekezaji waliopatiwa vitalu na NARCO kwa ajili ya kufuga na kulima malisho ya mifugo wamekuwa wakikodisha maeneo hayo kwa wakulima na wafugaji kinyume na mkataba.

“NARCO siku kumi nadhani zinawatosha kubaini watu wanaojiita wawekezaji, waliobadilisha matumizi ya ardhi ambayo siyo kufuga wala malisho wanyang’anywe maeneo kwa kuwa wameenda kinyume na utaratibu wa mkataba kati yao na NARCO, na mimi nitafuatilia nitapenda kupata taarifa mmepata wangapi na wangapi wamenyang’anywa kwa kuwa wameenda kinyume na utaratibu waliokubaliana.” Amesema Mhe. Ndaki

Waziri Ndaki amelazimika kutoa kauli hiyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa baadhi ya wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Mbarali kuwa wamekuwa wakikodishwa maeneo ya ranchi hiyo na wawekezaji kwa shilingi elfu ishirini kwa hekari moja kwa ajili ya kilimo na madebe kumi ya nafaka baada ya mavuno kwa kila hekari moja, huku wafugaji wakilipa takriban shilingi milioni mbili kwa hekari moja katika kipindi cha miezi minne kwa ajili ya kulisha mifugo yao kwenye maeneo ya wawekezaji ambao wamepatiwa vitalu na NARCO kwa mkataba wa kufuga au kulima malisho ya mifugo.

Amefafanua kuwa mkataba wa NARCO na wawekezaji kwa ajili ya kufugia mifugo na kulima malisho hauruhusu wawekezaji kukodisha eneo kwa mtu mwingine kwa ajili ya shughuli zozote kwa kuwa maeneo ya ranchi za taifa ni mali ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO).

Kuhusu deni la zaidi ya Shilingi Bilioni Sita ambalo NARCO inawadai wawekezaji waliopatiwa vitalu katika ranchi za taifa zilizopo kwenye maeneo mbalimbali nchini, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ameutaka uongozi wa NARCO kufikia Tarehe 15 Mwezi Februari Mwaka 2021 saa saba mchana awe amepata taarifa ya wawekezaji waliolipa madeni yao pamoja na ambao bado hawajalipa, kabla ya kuchukuliwa kwa hatua zaidi.

“Wawekezaji wote ambao tunawadai hapa Usangu na kwenye ranchi zingine wote walipe pesa ya NARCO tulipokubaliana kwenye mkataba tulikubaliana mtalipa pesa, mlipe madeni yenu ifikapo tarehe 15 mwezi februari saa saba mchana muwe mmelipa madeni yenu tunataka NARCO ijiendeshe kibiashara, lakini sioni tukielekea kwenye kujiendesha kibiashara na moja ya matatizo yanayotufanya tusifike huko ni kulea watu wa namna hii.” Amefafanua Mhe. Ndaki.

 

Ameongeza kuwa wale ambao hawatakuwa wamelipa hadi kufikia muda huo wanyang’anywe maeneo hayo ili wapatiwe watu wengine ambao wataweza kulipa kwa mujibu wa mkataba ili NARCO iweze kufikia malengo yake na kulalamika kuwa NARCO imechelewa kuchukua hatua kwa watu ambao wamekuwa na madeni ya siku nyingi.    

Amesema kuwa wizara imefanya tathmini juu ya madeni hayo na kuagiza yalipwe katika viwango na tozo mpya zilizowekwa kwa sababu imejiridhisha kwamba kwa gharama hizo NARCO itaweza kujiendesha na kuhudumia vizuri ranchi zake.

Kwa mujibu wa taarifa ya NARCO iliyotolewa na Kaimu Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Bw. Masele Mipawa, maeneo ya vitalu katika ranchi za taifa yanayokodishwa kwa wawekezaji yamegawanywa katika viwango vitatu, ambapo kiwango cha chini ni Shilingi 3,500/= kwa hekari moja kuanzia eneo lenye hekta 1 hadi 2000, kiwango cha kati ni Shilingi 5,500/= kwa hekari moja kuanzia eneo lenye hekta kuanzia hekta 2001 hadi 5000 na kiwango cha juu ni Shilingi 7,500/= kwa hekari moja kuanzia eneo lenye hekta zaidi ya 5001.

Aidha Waziri Ndaki, amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuangalia namna ya kukodisha maeneo ya ranchi za taifa kwa wakulima ambao wanaweza kulima malisho ya mifugo ili kuondokana na migogoro ya wakulima kupata maeneo kwa ajili ya kilimo ili kujikwamua kiuchumi.

Amesema ni muda muafaka kwa wizara kuangalia namna wananchi wanavyoweza kutumia maeneo hayo kwa ajili ya tija kwa taifa badala ya kusubiri wawekezaji ambao baadhi yao wamekuwa wakienda kinyume na makubaliano ya mikataba na kuwafanya wananchi wanaoishi karibu na ranchi za taifa kukosa maeneo kwa ajili ya kufanya shughuli zao za kiuchumi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema atahakikisha anasimamia maelekeo yote yaliyotolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki likiwemo la wawekezaji kulipa madeni ya vitalu walivyokodishwa ili Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) inayomiliki maeneo hayo iweze kujiendesha kibiashara kama moja ya malengo ya kampuni hiyo kupitia maeneo yake.

Katika mkutano huo Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki na baadhi ya wakulima, wafugaji na wawekezaji wanaofanya shughuli zao kwenye Ranchi ya Usangu iliyopo Wilaya ya Mbarali, Bibi Uliya Mahenge amemuomba Waziri Ndaki kuwapatia wakulima maeneo kwenye ranchi za taifa ili waweze kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo huku wakilipa kodi ya serikali ya maeneo hayo watakayokidishwa kama ambavyo wafugaji wanavyopatiwa vitalu kwa ajili ya kufugia mifugo kwenye ranchi hizo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amemaliza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Mbeya ambapo katika ziara hiyo alikuwa na lengo la kufahamu changamoto zilizopo kwenye Ranchi ya Usangu ambayo ni moja ya ranchi zinazomilikiwa na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ambayo ipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 13,2021

















Share:

Tuesday, 12 January 2021

Specialist, DHIS2 at Palladium

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Specialist, DHIS2 We are searching for an experienced Specialist, DHIS2 at our Dar Es Salaam facility. Company Overview Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with foundations, investors, governments, corporations, communities and civil society to formulate […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

WAITARA ASHTUKIA MADUDU FEDHA ZA MIRADI YA UJENZI,KAMATI ZA MANUNUZI KUTOSHIRIKISHWA, ASEMA LAZIMA UCHUNGUZI UFANYIKE

Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na baadhi ya wananchi kijiji cha Nyangoto alipokuwa akikagua ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo

Na Dinna Maningo, Tarime

Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara amemuomba Mdhibiti na Mkaguzi mkuu  wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi kwenye miradi ya ujenzi iliyojengwa kwa fedha za serikali kuu,fedha za mapato ya ndani ya halmashauri na fedha zinazotolewa na mgodi wa dhahabu wa Barrick(CSR).

Waitara alisema kuwa katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya ujenzi ikiwemo ya ujenzi wa madarasa na nyumba za waalimu amebaini uwepo wa matumizi mabaya ya fedha katika ujenzi ambayo hayaendani na hali halisi ya soko kama inavyotakiwa katika miradi inayoelekezwa kwa mfumo wa Force Account.

Mbunge huyo alisema kuwa katika ukaguzi wa miradi hiyo amapeta malalamiko mengi kutoka kwa viongozi wa Serikali za vijiji zikiwemo kamati za manunuzi za vijiji kutoshirikishwa katika manunuzi licha ya miradi ya ujenzi kufanyika ndani ya vijiji.

Akiwa kwenye ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo na ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya Msingi Nyangoto alishangazwa kuona ujenzi ukigharimu fedha nyingi zikiwemo gharama kubwa za manunuzi ya vifaa vya ujenzi lakini pia vifaa kuzidi zaidi ya mahitaji.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya jamii inayojengwa kwa fedha za Mgodi wa Dhahabu wa Barrick (CSR) katika vijiji vinavyozunguka mgodi, Mtendaji wa kijiji cha Nyangoto Chacha Turuya alisema kuwa miradi inayojengwa ni vyumba vitatu shule ya sekondari Nyamongo vitakavyogharimu sh.Milioni 88,761,465 na nyumba ya mtumishi pacha(2 in 1) sh.Milioni 88,734,528,jumla ya fedha zote ni sh.Mil.177,496,013.

Turuya alizitaja changamoto katika utekelezaji wa miradi hiyo kuwa ni pamoja na manunuzi kushindwa kufanyika kwa wakati,wataalamu wa ujenzi kushindwa kufanya ujenzi kwa wakati,mchakato wa malipo ya mafundi kuchukua muda mrefu,mafundi kutofika maeneo ya kazi kwa wakati kwa sababu mbalimbali.

"Gharama kubwa za malighafi za ujenzi hususani zinazotengenezwa viwandani kama vile mchanga na kokoto ikilinganishwa na bei halisi ya soko kama inavyotakiwa katika miradi inayotekelezwa kwa mfumo wa (force account)",alisema Turuya.

Baada ya Taarifa kusomwa Mwenyekiti wa kijiji cha Nyangoto Mwita Msegi na wajumbe wa kamati mbalimbali za kijiji wakatoa nyongo zao na kudai kutoshirikishwa katika hatua za manunuzi na kutolipwa posho zao za usimamizi wa ujenzi.

Msegi alisema kuwa serikali ya kijiji wala kamati ya manunuzi ya kijiji haikushirikishwa kwenye manunuzi ya vifaa vya ujenzi bali halmashauri ya wilaya ya Tarime kupitia idara ya manunuzi ndiyo inahusika katika mchakato mzima wa bei za vifaa na manunuzi.

" Bei zao ni kubwa mfano kokoto zinapatikana hapa Nyamongo kwa sh.120,000 kwa tripu moja wao wanaleta tripu moja ya kokoto kwa roli lenye ujazo wa 4.5 gharama yao ni 360,000,mchanga wa kutoka Nyasaricho ambao serikali ilituelekeza kuchukua huko tripu ni 180,000 wao wanauleta kutoka huko huko kwa ujazo huo kwa 360,000, wananchi wanajenga nyumba zao kwa kutoa mchanga mto Mara na ule unaokusanywa mvua zinaponyesha  tripu ni sh.100,000.

"Tukiwauliza wanasema wao ni wataalamu ndiyo wanaojua manunuzi wanafanya wao wenyewe bila kushirikisha kamati yetu ya manunuzi na mradi uko kwenye kijiji na mpaka sasa jengo liko kwenye hatua za uezekaji lakini hatujawahi kumuona mhandisi akifika kukagua tangu ujenzi uanze hatua ya msingi",alisema Msegi.

Mwenyekiti wa kamati ya mapokezi Tatu Kadama alisema kuwa elimu yao ni ya darasa la saba lakini anashangaa kuona halmashauri ikiwapatia makadirio ya bei za vifaa vya ujenzi (BOQ) zikiwa zimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza jambo linalowachanganya .

"Mimi siulaumu mgodi maana halmashauri ndiyo inapitisha inapeleka mgodini nao wanalipa,halmashauri ndiyo inanunua vifaa kupitia wazabuni wake,kazi yangu ni kupokea tu vifaa kama sasa nimepokea mabati 147 ya kuezeka madarasa matatu lakini mabati kumi yamepungua,nimepokea mabati 100 ya nyumba ya mtumishi na kwanini waandike Kiingereza wengine elimu ni ndogo.

" Kinachonishangaza hivi vifaa tunavipokea kutoka kwa watu tofauti tofauti,utaona misumari analeta huyu,mabati analeta mwingine,nondo mwingine,mbao mwingine yaani ni changanyikeni hakuna utaratibu,mpaka sasa hatujalipwa posho yoyote, natumia gharama zangu za usafiri kwenda shuleni kupokea vifaa hadi wajumbe wengine wamekata tamaa kuja kusimamia",alisema Tatu.

Katibu wa kamati ya ujenzi Chacha Sultani alisema kuwa licha ya kuelezwa kulipwa milioni 3 ambazo zigegawanywa kwa awamu tatu kuwalipa wajumbe 10 kama posho za usimamizi wa ujenzi  ulioanza tangu Septemba 2020 lakini hawajawahi kulipwa kiasi chochote cha fedha na wanapofuatilia huambiwa kuwa wasimamie bure kwa kuwa ni jukumu lao kusimamia shughuli zinazofanywa ndani ya kijiji.

Waitara alimtaka kaimu afisa elimu Sekondari halmashauri wilaya ya Tarime Mukama Mazigo kutoa ufafanuzi kuhusu mambo yaliyoelezwa na wajumbe wa serikali ya kijini ambapo alisema kuwa ukaguzi unatakiwa kufanywa kila hatua ya ujenzi na kwamba tatizo ni idara kutokuwa na gari na halmashauri ina upungufu wa gari zisizotosheleza.

Mbunge Waitara alisema kuwa hata kama idara haina gari ilipaswa kutumia gari zingine za halmashauri kwani kutofanya ukaguzi wa ujenzi imesababisha majengo kujengwa chini ya viwango,lakini pia alisema kuwa haiwezekani madarasa matatu kujengwa zaidi ya milioni 88.

"Lazima ukaguzi ufanyike fedha zimetumika nyingi ikilinganishwa na mradi wenyewe tunaomba CAG aje kufanya ukaguzi wa fedha za Serikali kuu,fedha za mapato ya ndani ya halmashauri na ufanyike uchunguzi wa kina hasa kwenye hizi fedha za CSR kwanini nyumba inayojengwa kwa fedha za Serikali itumie milioni 50 lakini iliyojengwa kwa fedha za CSR itumie zaidi ya Mil. 88 na madarasa matatu yanayojengwa kwa Mil.60 lakini CSR yanajengwa kwa zaidi ya Mil.88 sikubaliani na haya matumizi mabaya ya fedha", alisema Waitara.

Mbunge huyo pia alikagua ujenzi wa Bwalo la chakula linalojengwa kwa fedha za serikali (EP4R) sh.Milioni 100 katika shule ya sekondari Manga kata ya Komaswa ambapo alibaini vifaa kununuliwa kwa gharama kubwa na kuwepo kwa maelekezo mahali pakununua vifaa.

Mkuu wa shule ya Sekondari Manga Editha Nakei alisema kuwa mradi huo unajengwa na mzabuni Abdul Juma Sakumi ambapo vifaa vya ujenzi vinanunuliwa kwenye duka la Jura ambaye ni mzabuni wa vifaa vya ujenzi na hadi sasa zimetumika milioni 47,747,000 na ujenzi unaendelea.

Mjumbe wa bodi ya ujenzi Gorge Sorongai alisema kuwa"tumeelekezwa kununua vifaa kwa Jura huko mjini kwanini tuelekezwe pakununua na mradi upo hapa!mbao moja ya seprasi tunauziwa sh 23,000 na wakati mbao za Seregena zinapatikana kwa sh.15,000" alisema Sorongai.

Mbunge Waitara alisema kuwa halmashauri imefanya makosa kutozishirikisha kamati za manunuzi na bodi"nilichokiona hapa hakuna ushirikishwaji Mkurugenzi anapiga tu simu kachukueni vifaa sehemu fulani bila kuishirikisha 
bodi kujua bei na vifaa haya malalamiko yapo kila mahali ninakopita, karibu shule nyingi vifaa vinanunuliwa kwenye duka moja na wakati kuna maduka mengi ya vifaa kwenye kata mbalimbali,tutaunda kamati za kuchunguza kila mahali ", alisema Waitara.

Waitara alikagua ujenzi wa mabweni ya wasichana katika shule ya Sekondari Nyanungu iliyopo kijiji cha Nyamombara kata ya Nyanungu inayojengwa kwa fedha za serikali kiasi cha sh.Milioni 80 ambapo wananchi walilalamika mbao ,mchanga,mawe,kokoto kununuliwa kwa gharama kubwa licha yakwamba vinapatikana kijijini kwa bei nafuu.

Damian Sungura mjumbe wa bodi ya shule alisema"wametumia fedha nyingi mbao ya 2/3,2/6 ni sh 5,000 zao zinakuja kwa sh 15,000 kwa mbao moja na cha hajabu wanafata mbao mjini na wakati zinapatikana hapahapa miti wanayokata mbao ni hapa hapa kwetu, kwanini bei zao ziwe juu!" ,alihoji kwa mshangao.

Mwenyekiti wa bodi ya shule Shadrack Marwa alisema kuwa utaratibu unaotumika ni wa kuumiza"nina mashaka na manunuzi yanayofanywa na halmashauri maana sisi kama bodi hatujashirikishwa wanahusika walimu kwanini bodi iwekwe kando sisi tunahusishwa kusimamia tu ujenzi"alisema.

Diwani wa kata ya Nyanungu Richard Tiboche alisema kuwa tripu moja ya mchanga inauzwa 150,000 ila kwenye manunuzi inaeleza umenunuliwa kwa sh.200,000, tripu moja ya kokoto kwa bei ya soko ni sh.100,000 wao wanasema wamenunua sh.220,000 na wanazinunua huku huku kwetu,wanatuambia mlunda mmoja ni sh.8,000 na wakati hapa kijijini ni sh.3,000 na ukiupasua unatoa vipande 3 vya mbao,piga kwa bei hiyo itakuwa ni 24,000 badala ya 9,000.

"Hizi mbao wanazotuletea kutoka mjini ni miti inayotoka kwenye vijiji vyetu kwanini wasingenunua miti hapa hapa kijijini wapasue mbao saizi wanazotaka mpaka waende mjini,na kuna maeneo mengine wamesema mbao zimetoka mjini kwa gharama kubwa lakini zimenunuliwa vijijini kwa gharama ndogo alafu wao wakaongeza bei"alisema Tiboche.

Mbunge huyo hali kadhalika alikagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa shule ya msingi Mangucha vinavyojengwa kwa sh.milioni 40 fedha kutoka TAMISEMI ambapo viongozi wa serikali ya kijiji na mtendaji wa kijiji walidai kutoshirikishwa .

Mtendaji wa kijiji cha Mangucha Petro  Mirumbe alisema kuwa vijiji alivyofanya kazi kulikuwa na ushirikishwaji mkubwa lakini tangu afike kwenye kijiji hicho hapewi ushirikiano kwenye miradi ya shule zaidi ya waalimu pekee kuhusika na wala hapewi mihutasari ya utekelezaji wa miradi kwa madai kuwa mradi ni wa shule na siyo mradi wa kijini.

Waitara alieleza kuwa ni lazima fedha zinapoingizwa kwenye akaunti za shule na vijiji wananchi washirikishwe kwa kuwa nao huchangia nguvu zao kwenye miradi na kuitaka halmashauri ya wilaya kufanya kazi kwa uwazi na siyo fedha za serikali kuwa shamba la bibi.

Mbunge huyo katika Ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu alikagua baadhi ya shule za sekondari ambazo ni Regicheli kata ya Regicheli,Kewamamba,Nkerege kata ya Kiore,Manga,Bukenye kata ya Komaswa,Nyanungu kata ya Nyanungu,Kangariani,Bungurere Kata ya Itiryo,Muriba,Nyamongo na shule ya msingi Mangucha,Iramba, Nyangoto na Nyabichune.
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na baadhi ya wananchi kijiji cha Nyangoto alipokuwa akikagua ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na baadhi ya wananchi kijiji cha Nyangoto alipokuwa akikagua ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akisaini kitabu cha mahudhurio wakati wa ukaguzi shule ya Sekondari Nyamongo
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akiwa kwenye ukaguzi wa nyumba ya mtumishi shule ya msingi Nyangoto
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akiwa kwenye ukaguzi wa vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akiwa kwenye ukaguzi wa vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Nyamongo
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na baadhi ya wananchi kijiji cha Nyabichune wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa
Mafundi wakiwa katika ujenzi wa msingi shule ya Sekondari Nyabichune
Mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza jambo wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule mpya ya Sekondari Nyabichune
Share:

MBUNGE MTATURU AENDELEA KUWAKUMBUKA WANAFUNZI JIMBONI MWAKE

 

Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu akigawa sare za shule,madaftari na kalamu zenye thamani ya shilingi zaidi ya milioni 30 kwa  wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wapatao 1161 zilizopo jimboni kwake leo hii.

Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya ya Ikungi, Mwalimu Ngwano Ngwano akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo, Justice Kijazi na Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo amempongeza na kumshukuru Mtaturu kwa dhamira yake ya kusaidia maendeleo ya wananchi kwenye sekta mbalimbali katika jimbo hilo.

Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akizungumza na wananchi wakati akitoa msaada huo.
Msaada wa daftari ukitolewa.
Msaada wa daftari na kalamu ukitolewa.
Msaada wa daftari, kalamu na sare za shule  ukitolewa.
Vifaa hivyo vikipokelewa.
Msaada wa daftari ukitolewa.
Mkutano wa kupokea msaada huo ukiendelea.
Vifaa vilivyotolewa

 

Na Dotto Mwaibale, Ikungi

MBUNGE wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu ameendelea kuwa kumbuka wanafunzi katika jimbo lake kwa kuwanunulia vifaa mbalimbali vya shuleni.

Vifaa alivyotoa ni sare za shule, madaftari na kalamu vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 30 ambapo wanufaika ni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wapatao 1161 kutoka katika familia zisizo na uwezo zilizopo jimboni humo.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa ahadi yake ya kuwasaidia wanafunzi katika jimbo hilo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Magufuli za kutoa elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari.

Akizungumza wakati akigawa vifaa hivyo leo hii Mtaturu alisema amekuwa akifanya hivyo tangu alipo chaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.

“Serikali yetu ya awamu ya tano imewekeza kwenye elimu, inatoa elimu bila ya malipo nami kama mbunge wa jmbo hili nimeona niunge mkono jitihada hizo kwa kusaidia sare na vifaa vya shule ili kusiwepo kikwazo na hivyo kuwezesha lengo la serikali kutimia,” alisema Mtaturu.

Alisema katika utendaji kazi wake kipaumbele chake cha kwanza ni elimu kwa kuwa ndio msingi wa maendeleo hasa kwa watoto.

Mtaturu alisema dhamira yake hiyo ya kuwasaidia wanafunzi hao inaenda sambamba na kauli mbiu yake isemayo  'ElimuYetu, Maendeleo Yetu' inayochochea upatikanaji wa elimu kwa wote ili iwe njia ya kupatikana kwa maendeleo.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya ya Ikungi, Mwalimu Ngwano Ngwano akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo, Justice Kijazi na Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo amempongeza na kumshukuru Mtaturu kwa dhamira yake ya kusaidia maendeleo ya wananchi kwenye sekta mbalimbali katika jimbo hilo.

Share:

AWAUA WAZAZI WAKE, NDUGU NA MFANYAKAZI WA NDANI AKIDAI KUBAGULIWA KWENYE FAMILIA



Kijana Lawrence Waruinge (kushoto) na mpenzi wake (kulia)
**
Lawrence Waruinge na mpenzi wake wamefikishwa mbele ya makahakama Kaunti ya Kiambu, Kenya, kutokana na mauaji ya watu watano wote wa familia ya Lawrence, akiwemo baba yake mzazi, mama yake mzazi, ndugu zake wawili pamoja na mfanyakazi wa ndani.

Mauaji hayo anatuhumiwa kutekeleza Lawrence wiki iliyopita na amekiri kuyatekeleza mauaji hayo. Baada ya kukiri, sasa siku ya Alhamisi Januari 14, 2021, atafanyiwa uchunguzi wa akili kabla ya kesi yake kuanza.

Baada ya kukiri kutekeleza unyama huo Lawrence aliwapeleka maafisa wa upelelezi hadi pale alipoficha vifaa alivyotumia kwenye mauaji hayo, akisema kuwa aliamua kuchukua hatua hiyo, kutokana na kile alichokitaja kama kubaguliwa na familia yake.

Kijana huyu mwenye umri wa miaka 22, atafikishwa tena mahakamani tarehe 25 mwezi huu baada ya uchunguzi kukamilika, pamoja na mpenzi wake, anayesemekana kukodisha chumba walichotorokea kabla na baada ya maujaji, wote wakishtakiwa kwa kosa la mauaji.

 Chanzo - EATV

Share:

Waziri Biteko Akagua Wauza Madini Dar, Aonya Matapeli


Waziri wa Madini, Dotto Biteko amewacharukia matapeli wanaojihusisha biashara ya uuzaji na ununuzi wa madini kinyemela  majumbani mwao na kuikosesha serikali mapato na kuongeza kuwa huo ni uhalifu ambao kamwe  hautavumiliwa.

Waziri Biteko pia amewaonya matapeli wanaowalaghai wageni kutoka nje ya nchi na kuwauzia madini feki jambo alilosema linachafua sifa ya nchi.

Waziri Biteko ametoa kauli hiyo leo alipotembelea na kuwakagua wafanyabiashara wa madini kwenye soko la madini lililopo Jengo la NHC Barabara ya Samora jijini Dar ambapo alisikiliza changamoto zinazowakabili wadau hao na kuahidi kuzitatua haraka.

 “Lengo letu ni kudhibiti utoroshaji wa madini ndio maana tumekuja kuwapa tahadhari kuwa wajiepushe kununua nje ya mfumo wa masoko kwani madhara yake ni makubwa. ukikutwa unanunua au unauza madini nyumbani kwako hata kama upo kwenye gorofa ya 12, fensi kali na kamera za CCTV tutakukamata.

“Lazima tufuate sheria kwa sababu asilimia saba ya pato hilo sio kubwa kiasi cha kukusababishia kwanza tutaifishe madini, nyumba na hata wewe mhusika kupelekwa ndani,” alisema.

Alisema katika kudhibiti mnyororo wa sekta ya madini, Serikali kupitia wizara ya madini pamoja na wizara ya viwanda na biashara inaandaa muswada wa sheria utakaowawezesha masonara wote nchini kutambulika kisheria.

“Tatizo ni kubwa kwa masonara ni kutotambulika… kwa kuwa wapo wengin hata kuwatambua ni ngumu. Tunataka kuweka msukumo mkubwa zaidi katika udhibiti mifumo mingi katika sekta ya madini na sasa tumeweka mazingira rafiki kwa sababu lengo letu ni uongezaji thamani. Kikubwa nawaomba masonara wawe na subira katika hili,” alisema.

Naye Makamu Mwenyekiti Chama cha Wafanyabiashara Wakubwa Wanunuzi na Wauzaji Madini Tanzania (TAMIDA), Osman Tharia aliiomba wizara kuuangalia upya bei ya pango la vizimba walivyokodishwa na Shirika hilo la nyumba sambamba na bei za umeme kwa kuwa zinawakwamisha katika kukuza biashara ya madini nchini.

“Alisema wafanyabiashara zaidi ya 57 waliopo katika vizimba hivyo hulazimika kulipia umeme kulingana na ukubwa wa kizimba jambo ambalo ni gharama kubwa kwani ilitakiwa kulipia kulingana na matumizi ya umeme,” alisema

Aidha, Naibu waziri wa madini, Prof. Shukrani Manya aliwataka wafanyabiashara wa madini kuzingatia sheria kwa kuwa serikali haina nia ya kuwadhoofisha kibiashara bali inataka kuwawezesha kukua na kufanya biashara ya madini kuwa endelevu na yenye tija kwa pande zote.


Share:

Waziri Chamuriho Awataka Wafanyakazi Kuzingatia Mikataba Ya Kazi

Waziri wa ujenzi na Uchukuzi,  Mhandisi  Leonard Chamuriho  amewataka wafanyakazi wa sekta ya uchukuzi kuhakikisha wanatekeleza makubaliano yaliyosainiwa kati yao na wakuu wa taasisi ili kuwe na ufanisi na thamani ya fedha.

Waziri Chamuriho ameyasema hayo mara baada ya kufungua baraza la wafanyakazi wa sekta hiyo, lilifanyika katika ukumbi wa chuo cha Benki Kuu (B.o.T) Mkoani Mwanza na kusisitiza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kwa mtumishi atakayekiuka makubaliano hayo.

“Hatutasita kuchukua hatua pale tutakapobaini kuwa kazi zinafanywa kwa mazoea na kusahau malengo tuliyojiwekea kwa utendaji wa kazi za kila siku. “alisema waziri Chamuriho.

Aidha waziri chamuriho amesisitiza umuhimu wa taasisi za sekta ya uchukuzi kushirikiana ili kuwa na matokeo chanya hususani katika miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa kwenye miundombinu.

Hata hivyo waziri Chamuriho ameeleza changamoto ya vishiria vya uwepo rushwa na kuwataka watumishi wa sekta ya uchukuzi kujiepusha kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi.

“Zipo rushwa za aina nyingi, ikiwemo za kuomba fedha, zawadi, mapenzi  na hata kuwanyima haki watu haki zao, unyanyasaji wa kijinsia, na  ukiukaji wa haki za binadamu “. Alisema Waziri Chamuriho.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Gabriel Migire amemuhakikishia Waziri Mhandisi Chamuriho kuwa maelekezo yote yatafanyiwa kazi na kutoa mrejesho kwa kuzingatia

Katika hatua nyingine Mwenyekiti, Gabriel Migire amempongeza Waziri Chamuriho kwa utendaji uliotoa matokea chanya kwenye miradi ya ki  mkakati ya sekta ikiwemo ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Ununuzi na Ukarabati wa Meli za Mv Viktoria na Butiama, ujenzi wa Chelezo, Ujenzi wa Meli Mpya ya MV. Mwanza na Ununuzi wa Ndege.


Share:

Lukuvi Apiga Marufuku Viongozi Wa Vijiji Na Vitongoji Kuuza Ardhi

Na Munir Shemweta, WANMM SINGIDA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amepiga marufuku viongozi wa vijiji na vitongoji katika maeneo mbalimbali nchini kujihusisha na uuazaji ardhi ikiwemo mashamba kwa kuwa hawana mamlaka ya kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya ardhi Vijji ya mwaka 1999.

Akizungumza wakati akikagua shamba la mikorosho la Mkwese-Masigati wilayani Manyoni mkoani Singida tarehe 11 Januari 2021 akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo alisema, viongozi wa wilaya na halmashauri wanapaswa kukomesha tabia hiyo ya baadhi ya viongozi wa vijiji na vitongoji kuuza ardhi kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Lukuvi, ugawaji ardhi kwenye vijiji lazima ufuate sheria iliyowekwa ikiwemo kuitisha mkutano na siyo kiongozi kujiamulia kugawa ardhi kwa niaba ya kijiji kizima.

“Kijiji kugawa ardhi lazima iwe kwenye mutano siyo mtu anagawa, Mkuu wa Wilaya pita kote na elekeza mikutano ya kugawa ardhi isiitishwe kinyemela na wewe ukasimamie kujua wananchi watapata faida gani kwa ardhi itakayotolewa” alisema Lukuvi.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongeza kuwa, mtu yoyote atakayenunua ardhi kwa mwenyekiti wa Kijiji au kitongoji basi ajue kuwa ni kinyume cha sheria  kwa kuwa ardhi inatakiwa kuamuliwa katika mkutano.

Lukuvi aliipongeza halmashauri ya wilaya ya Manyoni kwa uamuzi wa kugawa mashamba kwa ajili ya kilimo cha korosho na kueleza kuwa uamuzi huo unaifanya Manyoni kusonga mbele na kushauri kupewa muda ili kuona matokeo.

Aliitaka halmashauri ya Manyoni katika mkoa wa Singida kuhakikisha eneo hilo la shamba la Mikorosho linapangwa kimji kwa kubuni mpango wa maendeleo na kufurahishwa  na uamuzi wa halmashauri hiyo kuwa na mpango wa kumilikisha ekari 22,000 na kusisitiza kuwa, wote  watakaomilikishwa lazima wapatiwe hati za ardhi.


Share:

Super Nhesha: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


 DODOMA!! DODOMA!! DODOMA!!
KWA WALE WENYE MATATIZO YA SUKARI AU KITAALAMU: (DIABETES MELLITUS)
NINI CHANZO CHA TATIZO HILI LA SUKARI.

KUNA VYANZO VINAVYOWEZA KUSABABISHA SUKARI:
(1) Shinikizo la damu (B.P) (2) Viwango vya juu vya triglyceride (Mafuta)
(3) Vyakula vyenye mafuta mengi na wanga
(4)Utumiaji wa pombe kupita kiasi 
(5)Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi (6)Mtindo wa maisha usiofaa kiafya (7)Uzito unene uliozidi (8) Kutofanya mazoezi

NINI DALILI ZA KUWA NA TATIZO LA SUKARI
(1) Kuhisi njaa mara kwa mara (2) Kuhisi kiu mara kwa mara
(3) Kupungua uzito 
(4) Maono machafu 
(5) Uchovu mara kwa mara
(6) Ukipata kidonda hakiponi 
(7) Kushuka kwa kinga mwilini pia kwa wanaume wenye tatizo hili wanakuwa na  tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kama vile kukosa hamu ya tendo la ndoa,  kulegea na kusinyaa, kuwahi kufika kileleni, maumivu ya mgongo, Kiuno, Tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kutopata choo vizuri

SASA TIBA IMEWASILI KWA
Kwa kutumia tiba za asili Dawa ya mitishamba ilyokatika mfumo wa vidonge asilia Dawa inaitwa NHESHA POWER kwa kutumia Dawa hizi utapona tatizo hilo ndani ya siku 14 tu na hautaliona tena katika maisha yako.
 
BABU MADUHU atakuwepo Dodoma kuanzia Tarehe 25/01/2021 hadi tarehe 10/02/2021kwa hapa Dar es salaam tunaendelea   kutoa huduma zetu Ofisini hapa Magomeni, Moroco Hotel/Kanisani
Simu No. 0755 684 297, 0788 330 105, 0652 102 152
**** Karibu Tukuhudumie****
 


Share:

Consultant, Governance at Palladium

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

We are searching for an experienced Consultant, Governance at our Dar Es Salaam facility. Company Overview Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with foundations, investors, governments, corporations, communities and civil society to formulate strategies and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger