Monday, 11 January 2021

Lukuvi Ataka Usimamizi Wa Ardhi Katika Ngazi Ya Mitaa


Na Munir Shemweta, WANMM SINGIDA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuhakikisha zinashusha usimamizi wa masuala ya ardhi katika ngazi za mitaa na vijiji ili ziweze  kusimamia kuepuka ujenzi holela na kurahisisha ufuatiliaji makusanyo ya kodi ya pango la ardhi.

Akizungumza wakati akikagua ofisi ya ardhi katika halmashauri ya Manispaa ya Singida akiwa katika ziara ya siku moja kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Singida tarehe 10 Januari 2021, Lukuvi alisema ni vyema wakurugenzi katika halmashauri nchini kuwapa wajibu watendaji wa mitaa na vijiji kwa barua kusimamia misingi ya ardhi yenye lengo la kusimimia sheria katika masuala ya ardhi.

Hata hivyo, Waziri Lukuvi alisema Watendaji wa Mitaa na Vijiji watakaokasimia mamlaka ya usimamizi ardhi katika maeneo yao hawatakuwa na jukumu la kugawa, kupanga, kupima na kumilikisha ardhi bali kuangalia yanayoendelea katika mitaa yao na wakikuta ukiukwaji wowote kama vile ujenzi holela basi watakuwa na wajibu wa kusitisha.

” Afisa ardhi katika wilaya hawezi kujua yale yanayoendelea kwenye mtaa au kijiji na hata suala la kodi  mkiwatumia watendaji wa mitaa wataweza kusaidia kuwabaini wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi kirahisi”

Ametaka watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri kuhakikisha wanatengeneza majedwali maalum yenye orodha inayoonesha kila mmiliki wa kiwanja kwa lengo la kuwawezesha watendaji wa mitaa kuwajua wamiliki katika maeneo yao.

” Kumbukumbu zote za masuala ya ardhi wajulishwe watendaji wa mitaa na vijiji ili waweze kufuatilia katika mitaa yao maana katika suala la hati za kimila tumefanya vizur ngazi ya vijiji ila suala la Hati Miliki za Ardhi bado tuko nyuma maana tumeficha taarifa wilayani” alisema Lukuvi.

Waziri Lukuvi alizitaka ofisi za ardhi za mikoa kuhakikisha zitatoa elimu kwa watendaji wa mitaa na vijiji ili kuwajengea ufahamu wa masuala ya ardhi na kuwawezesha kusimamia vyema masuala hayo katika maeneo yao.

Kwa mujibu wa Lukuvi, hata kama Manispaa imepanga matumizi bora ya ardhi ni vyema matumizi yake yakawekwa kwenye vipande vya ngazi ya mitaa na kusisitiza kuwa kazi hiyo ni ya halmashauri kwa kuwa mitaa ni jicho lake la kutoa taarifa katika masuala mbalimbali yakiwemo yale ya ardhi.

Katika ziara yake Waziri wa Ardhi mbali na kutembelea halmashauri za wilaya ya Singida na Ikungi na kusisitiza kuwa halmashauri ndizo zenye jukumu la kupanga, kupima na kumilikisha ardhi katika maeneo yake na jukumu hilo siyo la maafisa ardhi.

Lukuvi alisema Halmashauri zote zijue zina wajibu wa kusimamia ardhi katika maeneo yao na ilichofanya Wizara ya Ardhi ni kuwapatia wataalam watakaowasaidia kujua namna bora  ya kutumia ardhi vizuri.


Share:

RAIS WA MSUMBIJI NYUSI ATUA TANZANIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI KANDA YA CHATO



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshuhudia mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akimwagilia maji mti alioupanda baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya picha ya kuchora ya THE BIG FIVE mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakisikiliza maelezo toka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Januari 11, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha kwa viongozi mbalimbali mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi alipowasili ili kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakifurahia ngoma za utamaduni katika Uwanja wa Ndege wa Geita mara alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021
Share:

Rais Nyusi : Rais Magufuli Anashughulikia Maisha Ya Watu


 Na Immaculate Makilika- MAELEZO, Chato
Rais wa Msumbiji, Felipe Jacinto Nyusi amesema kuwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli anashughulikia maisha ya wananchi kwa kuendelea kuboresha sekta ya  huduma za afya nchini.

Rais Nyusi amesema hayo leo wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda- Chato, iliyopo wilayani Chato mkoani Geita pamoja na kupanda kama kumbukumbu ya upendo na amani

“Nashukuru kwa Rais Magufuli kunipa nafasi ya kuweka jiwe la msingi kwa sababu Serikali inayoaangalia afya ya wananchi hiyo ni Serikali inayopenda wananchi, Rais Magufuli anashughulikia sana maisha ya wananchi wa watanzania kwa kuangalia nyumba bora za  kuishi, huduma za maji, chakula  na afya bora” alisema Rais Nyusi.

Alisisitiza “Kwa hiyo hii ni zawadi kwetu  kwa kutupa nafasi ya kuweka jiwe la msingi katika hospitali hii kubwa, kule Msumbiji tumeanza (Program ya  presidential initiatives) ya kujenga hospitali kila wilaya hii ni zawadi kubwa kwetu ya  kutupa nafasi ya kuweka jiwe la msingi  katika afya ya wananchi.

Tunatakiwa tujue watu wangapi na umbali kutoka hospitali moja hadi nyingine, sasa hiki tulichoona hapa ni mfano mzuri kwa sababu hii ni hospitali kubwa sana ambayo ipo  karibu na mikoa mitano na nchi jirani za Kenya na Uganda  naamini wataweza kuhudumiwa hapa”

Aidha, Rais Nyusi alisema kuwa mkoa wa Geita  ni tajiri kwa kuwa kuna kilimo cha mpunga,  madini ya dhahabu na uvuvi wa  samaki, hivyo kuwataka wananchi wa mkoa huo kufanyakazi kwa bidii.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli alimshukuru Rais Mhe. Filipe Nyusi kwa kumtembelea Chato na kuongeza  kuwa  Msumbiji ni rafiki wa muda mrefu wa Tanzania na nchi hizo  zina makubaliano ya kushirikiana katika mambo mbalimbali ikiwemo biashara.

“Biashara kati ya Tanzania na Msumbiji imeongezeka, hadi kufikia mwaka 2020 ilifikia shilingi bilioni 93.6, kuna makampuni ya Msumbiji yanafanya kazi hapa na baadhi ya makampuni ya Tanzania yanafanya kazi kule.” Alisema Rais Magufuli

Aliongeza  kuwa Januari 9, 1967 Hayati Mwalimu Julius Nyerere alitembelea wilaya ya Chato na kufungua kiwanda cha pamba kilichojengwa kwa shilingi milioni 2 ambacho kilikuwa na uwezo wa kuchakata marobota 20,000.  Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa Mwalimu Nyerere alichangisha fedha na yeye binafsi kuchangia shilingi 2,000 kwa ajili ya kujenga bandari ya Nyamirembe ili iweze  kusafirisha pamba kwenda Mwanza na Dar es salaam kwa hiyo wa Rais Nyusi amefika eneo ambalo alifika Mwalimu Nyerere

“Kwetu sisi tunaona hii ni zawadi kubwa kwa wewe kuja kuzindua hospitali hii ambayo ni kubwa na itahudumia pia nchi za jirani.Nawashukuru Wizara ya Afya na Wakandarasi, nitawabana Wizara ya Afya  ili hospitali hii ikamilike mara moja.” Alisema Rais Magufuli

Naye, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima alisema kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda – Chato ilikadiriwa kutumia sh. bil.16, Serikali imeshatoa sh. bil.14 ambapo ujenzi umekamilika kwa asilimia 90 na makabidhiano yanatarajiwa kufanyika mwezi Machi, 2021.

Aliongeza kuwa awamu ya pili ya ujenzi  imeshaanza kwa jumla ya gharama ya shilingi bilioni 14 ambapo mpaka sasa Serikali imetoa shilingi bilioni 4.1 na utekelezaji wake umefikia asilimia 37.

“Hospitali ya Rufaa ya Kanda – Chato itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi zaidi ya milioni 14 ambapo kwa siku itakuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa kati ya 700 – 1000.” Alisema Waziri huyo wa Afya

Alifafanua kuwa maboresho ya afya nchini  yamesaidia kuharakisha matibabu bobezi na kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda nje kutoka wagonjwa 682 mwaka 2014/15 hadi wagonjwa 42 mwaka 2020.

Rais wa Msumbiji, Felipe Jacinto Nyusi yupo nchini kwa ziara ya siku moja ambapo atafanya mazungumzo na Rais Magufuli kuhusu namna  ya kuboresha maisha  wananchi  pamoja na usalama.


Share:

Jinsi Ya Kuandika CV Nzuri Ambayo Itamvutia Mwajiri na Kukufanya Upate KAZI Kirahisi

WATU wengi nchini wamekosa ajira  kwa sababu ya makosa wanayoyafanya wakati wa kuandika CV zao.

Kumbuka,  makampuni  karibia yote yanayotangaza nafasi za kazi hupokea wastani wa maombi 200-500 ya kazi kwa tangazo moja la kazi. 

Hivyo, CV yako lazima ikae vizuri ili kumshawishi mwajiri. Utaratibu wa kuomba kazi unaweza ukawa tofauti kati ya makampuni na mashirika, ila yote yatahitaji uwatumie CV.

CV ni nini?
CV ni maelezo ya ujumla kwa kiundani ya historia yako ya kazi na shule. Kawaida, inatumika kwenye maombi ya kazi ya nafasi za kati, za juu na za utafiti.

Mambo yafuatayo yatasaidia kuifanya CV yako iwe bora na hivyo, kukusaidia kupata interview za kazi.

👉Soma na kuelewa maelezo ya kazi
Una ujuzi gani? Mwajiri anatafuta mfanyakazi wa aina gani? Maswali haya ni muhimu kujua kama utaiweza hiyo kazi au la. Pia, ni vizuri kujua nini hasa ni muhimu kwa muajiri na kufanya maombi yako yaendane zaidi na mahitaji ya mwajiri.

Kwa mfano, kama kazi inaweka umuhimu kwenye ujuzi wa kutumia mitandao ya kijamii kwa matangazo, hakikisha CV yako ina kazi zote zilizohitaji matumizi ya mitandao ya kijamii.

👉Andika maneno muhimu yaliyotumika kwenye maelezo ya kazi, uyatumie kwenye CV
Usichukue sentensi nzima kutoka kwenye maelezo ya kazi na ukaitumia vile vile kwenye CV yako. Ila, tumia lugha na baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye CV.

👉Fanya utafiti juu ya kampuni iliyotangaza kazi
Pamoja na kuchambua maelezo ya kazi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya kampuni yenyewe. Kama wana tovuti au wapo kwenye mitandao ya kijamii, jaribu kujua ni kazi gani na sekta ipi wanayohusika nayo. 

Pia, ikiwezekana jaribu kuwajua wafanyakazi/meneja wa kampuni hiyo. Hii itakusaidia kujua maadili na muelekeo wa kampuni. Hii itakusaidia kuweka maombi yako ya kazi yaendane na kampuni hiyo.

👉Orodhesha ujuzi wako wakufanya kazi
Hapa, usiweke kazi zote ulizozifanya maishani mwako ila, weka zile ambazo zilikuongezea ujuzi utakayo kusaidia kufanya kazi unayoomba.

==>Format/Staili inayotumika zaidi kwenye kuandika CV:
   1. Lengo la CV na ujuzi wako
    2.Ujuzi wako wa kazi
   3. Mafanikio maalum
   4. Elimu
   5. Ujuzi muhimu binafsi

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Angalizo:
  1.  Tumia maandishi ya kawaida ya Times New Roman
  2.  Tumia size 9 – 12 ya herufi
  3.   Hakikisha unatumia staili moja ya kuandaa CV kote
  4.   CV isiwe zaidi ya ukursasa 2
  5.   Usitumie sentensi ndefu
  6.  Hakikisha CV yako inasomeka kiurahisi na inawasilisha   mafanikio yako kwa uwazi.
  7.  Anza na kazi yako ya sasa hivi au ya hivi karibuni alafu rudi nyuma.
   ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 
   ==>.Hakikisha Yafuatayo:
1.Ukiwa unaandika jina la kampuni uliyo fanya kazi, andika jina la kampuni kikamilifu. 
2.Eleza kwa ufupi kampuni yao inahusika na nini. 
3.Tatu, weka muda uliyofanyakazi hapo (mwezi na mwaka).  
4.Baada ya hapo, orodhesha kazi na majukumu yako kwenye hiyo kampuni.
5.Usidanganye

👉Maandalizi ya Mwisho

1.Pitia kila kitu kwa mara ya mwisho
 -Print CV yako alafu ipitie. Hii huwa inasaidia kuona makosa yako.

2.Mpe Rafiki  yako apitie CV
-Muombe rafiki yako apitie CV yako. Macho manne ni bora zaidi ya mawili!

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Hatua ya kwanza kwenye kupata kazi unayotaka ni kutuma maombi. Tunatumaini kwamba maelezo yaliyoelezwa humu yatakusaidia kuandaa CV bora kwa ajili ya mwajiri.



Share:

Wimbo Mpya : NYANDA MADIRISHA OBHADO 'MALIGANYA' - MITIHANI

Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 unaitwa Mitihani... huu hapa
Share:

Wimbo Mpya : NYANDA MADIRISHA OBHADO 'MALIGANYA' - JIRANI


Huu hapa wimbo mpya wa Msanii wa Nyimbo za asili kutoka Kahama mkoani Shinyanga Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' Shikomba Bhulolo inaitwa Jirani. Sikiliza hapa chini
Share:

DC TANO MWERA AHAMASISHA UJENZI WA MADARASA

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera ametembelea maeneo mbalimbali wilayani Busega kuhamasisha ujenzi wa vyumba vya Madarasa kwaajili ya kukidhi idadi ya Wanafunzi watakaoingia kidato cha kwanza mwaka 2021. Mhe Mwera amewataka Wananchi kushirikiana na Serikali kuhakikisha Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wilayani Busega wanaingia kidato cha kwanza na wanapata haki yao ya Elimu.

“Najua tuna upungufu wa madarasa, lakini isiwe sababu ya kuwafanya hawa watoto kukosa haki yao ya Elimu, tutahakikisha sisi serikali kushirikiana na nyie Wananchi tunafanikiwa kujenga madarasa ili Wanafunzi waweze kusoma”, aliongeza Mhe. Mwera.

Kwa upande mwingine Mhe. Mwera amesema Ofisi yake imetoa mifuko 130 kwaajili ya ujenzi na umaliziaji wa madarasa kwenye maeneo yenye mahitaji makubwa ya vyumba vya madarasa wilayani Busega. Aidha Mhe. Mwera ameeleza nia yake ya kuzungumza na wadau wengine wa maendeleo ili kuona uwezekano wa kusaidia ujenzi wa madarasa, huku ameeleza kwamba michango ya Wananchi ni muhimu katika kufanikisha nia ya Wilaya kuweza kukamilisha mahaitaji ujenzi wa madarasa.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko amesema kwamba upungufu wa madarasa umetokana na ongezeko la waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza, ambapo jumla ya Wanafunzi wapatao 5673 wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2021 katika Wilaya ya Busega. Idadi hiyo inafanya upungufu wa madarasa 69 ili kukidhi idadi ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza.

“Kwakua kuna madarasa yalishaanza kujengwa katika shule ambazo tayari zina wanafunzi lakini pia kuna baadhi ya shule ni mpya hivyo kama Ofisi tutahakikisha juhudi za kuhamasisha viongozi wa kata na vijiji husika wanamalizia vyumba, hivyo michango iendelee ili kufikia lengo, aliongeza Kabuko”.
Share:

RAIS MWINYI AIFUNGUA SKULI YA SEKONDARI YA HASNUU MAKAME....ATAKA WANAFUNZI KUSOMA KWA BIDII NA NIDHAMU

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka wanafunzi kutumia vyema fursa za kuwepo miundombinu bora ya masomo  kwa kusoma kwa bidii na nidhamu.

Dk. Mwinyi amesema hayo  katika Ufunguzi wa Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame , iliopo Kibuteni Mkoa Kusini Unguja.

Amesema wanafunzi watakaopata nafasi ya kusoma katika skuli hiyo wanapaswa kutumia vyema fursa hiyo kwa kusoma kwa bidii, ili waweze kufaulu katika amsomo yao badala ya  kujihusisha na masuala yatakayosababisha kuharibikiwa katika maisha yao ya baadae.

Alisema ni matumaini yake kuwa wanafunzi watakaosoma skuli hiyo watafulu vyema katika mitihani yao ya Taifa, kw akuwa   skuli hiyo iko katika mazingira mazuri, walimu wazuri pamoja na kuwa na vifaa vya kutosha.

Aidha, aliwataka wakuu wa Wilaya na mikoa kushirikiana na wananchi ili kufanikisha wanafunzi wote watakaotoka katika skuli 34 za Sekondari mkoani humona kujiunga katika Skuli hiyo wanafaulu vizuri.

Vile vile aliwataka walimu kutekeleza ipasavyo wajibu wao wa kusomesha vizuri pamoja na wazazi na walezi kufuatilia maendeleo ya elimu ya watoto wao ili kubaini chanagmoto zinazoweza kujitokeza.



Share:

RAIS MWINYI ASAMEHE WAFUNGWA 49

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa msamaha kwa wanafunzi (wafungwa) Arobaini na Tisa (49) waliokuwa wakitumikia Vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za Sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Dk. Mwinyi ametoa msamaha huo kwa mujibu wa kifungu cha 59 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kinachompa mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa waliofungwa gerezani.


Kutokana na msamaha huo, Dk. Mwinyi ameamuru kuwa kifungo kilichobaki cha wanafunzi (wafungwa) hao walionufaika na msamaha katika vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba kuwa kipindi hicho chote kinafutwa na waachiwe huru kuanzia Januari 11.2021.


Kwa vile,  Zanzibar itakuwa inasherehekea miaka 57 ya Mapinduzi Matukufu ya Januari 12, 1964 Dk. Mwinyi ameona kuwa kuna sababu za kutosha za kutoa msamaha kwa walengwa walionufaika na msamaha huo kwa Unguja  ambao ni 46 na Pemba 3.


Msamaha huo hutolewa kila mwaka katika kipindi cha sherehe za Mapinduzi matukufu, huwahusisha wanafunzi ambao ni wazee sana, wenye maradhi sugu au wenye makosa madogo ambao wamebakisha muda mfupi wa kutumikia chuoni, wanaoonesha nidhamu nzuri chuoni na kujutia makosa yao.


Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo, wenye makosa kama vile kuua kwa makusudi, wizi wa kutumia nguvu, wizi wa mali ya Umma, makosa ya kudhalilisha wanawake na watoto, makosa ya dawa za kulevya na wenye makosa mengi ya zamani kwa kawaida huwa hawapewi msamaha.


Share:

Uwepo Wa Regista Ya Watu Wenye Ulemavu Itachangia Upatikanaji Wa Huduma Bora Kwa Wenye Ulemavu Nchini – Naibu Waziri Ummy


 Na: Mwandishi Wetu

Uwepo wa rejista ya Watu wenye Ulemavu nchini utachangia upatikanaji wa huduma bora kwa kundi hilo lenye mahitaji maalum sambamba na kutambua mahali wanapoishi, aina ya ulemavu walionao, hali zao za kimaisha na namna ya kuwawezesha kupata mikopo ya asilimia 2 inayotolewa na halmashauri.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga wakati wa ziara yake ya kuwarejesha baadhi ya wenye ulemavu Mkoani Shinyanga kutoka Jijini Dar es Salaam, kutokana na kundi hilo kutumiwa na watu wenye maslahi binafsi kuwazungusha watu wenye ulemavu kuomba fedha barabarani.

Alieleza kuwa, Serikali ipo katika mkakati wa kuandaa regista ya watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, kata, Halmashauri na Mkoa ili kuwa na takwimu sahihi zitakazoonyesha idadi ya wenye ulemavu waliopo nchini na ambayo pia itasaidia kutambua kujua mahali walipo, wanajishughulisha na nini katika jamii waliyopo.

“Uwepo wa rehista hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa serikali kutambua idadi ya watu wenye ulemavu waliopo kwenye maeneo mbalimbali na hivyo kurahisisha ufikikaji wa huduma kwa kundi hilo kwa urahisi,” alisema Naibu Waziri Ummy

“Leo hii tumewarejesha Watu wenye Ulemavu zaidi ya 38 kutoka Jijini Dar es Salaam kuja hapa Mkoani Shinyanga mahali ambapo wamekuwa wakiishi hapo awali, hivyo kama rejista hiyo ingekuwepo basi zoezi la utambuzi wa baadhi yao ingekuwa rahisi kuwatambua,” alisema

Alisema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam walifanikiwa kufanya ziara za kushtukiza katika maeneo ambayo wamekuwa wakiifadhiwa watu hao wenye ulemavu, wakati wa operesheni hiyo walifanikiwa kuwakamata baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitumika kuwaendesha wenye ulemavu kuomba fedha barabarani, wamiliki wa nyumba hizo za wageni ambazo wamekuwa wakihifadhi wenye ulemavu na pia walifanikiwa kukamata vitimwendo “wheelchair” ambazo zilikuwa zikikodhishwa kwa watu wenye ulemavu.

“Tutaendelea na msako hadi pale tutakapoona wahusika wa mtandao huu wanaacha kabisa vitendo hivyo vya udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu,” alisisitiza Naibu Waziri Ummy

Aliongeza kuwa, Serikali hii ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli inawajali sana Watu wenye Ulemavu na katika kulitambua hilo Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kundi hilo linapata mahitaji wanayostahili kama watu wengine.

Sambamba na hayo Naibu Waziri Ummy alitaka Uongozi wa Mkoa wa Shinyanga na mikoa mingine iliyopo nchini kuhakikisha wanawasaidia watu wenye ulemavu kuanzisha miradi mbalimbali itakayowafanya wajishughulishe na uzalishajimali badala ya kuzunguka barabarani kuomba fedha.

“Nilipofanya ziara ya kuwatembelea watu wenye ulemavu mkoani Dar es Salaam nimeshuhudia mambo makubwa yanayofanywa na baadhi yao ikiwemo uanzishwaji wa viwanda vya uzalishaji, ujasiriamali, hivyo wenye ulemavu watambue wanao uwezo wa kuanzisha miradi mikubwa,” alisema  

Aidha, Naibu Waziri huyo aliwasihi Maafisa Ustawi wa Jamii nchini kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu na wateja wengine kwa kufuata miongozo, kanuni na Sheria zinazoongoza katika utoaji wa huduma za ustawi wa jamii nchini. Pia amewataka maafisa hayo kuimarisha ushirikiano baina yao na watu wenye ulemavu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Yasinta Mboneko alikiri kuwapokea watu hao wenye ulemavu ambao walikuwa wakitumiwa na baadhi ya watu kujinufaisha, huku akieleza kuwa wataanzisha kanzi data kwa ajili ya kuhifadhi taarifa ya watu wenye ulemavu waliopo katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo pia alimuhakikisha Naibu Waziri kuwa watawarejesha salama mahali walipokuwa wanaishi huku wakiweka utaratibu wa kuwafuatilia.

Mhe. Mboneko alitumia fursa hiyo kukemea vitendo hivyo kwa baadhi ya watu ambao wanawatoa wenye ulemavu na kuwapeleka kwenye baadhi ya miji kuomba huku akieleza mtu yoyote atakayebainika anafanya vitendo hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.  

MWISHO


Share:

BI. HARUSI AFARIKI DUNIA GHAFLA BAADA YA KUTOKA FUNGATE

Linet 
Mnamo Disemba 11, 2020, Mastin Mukanga alifunga pingu za maisha na Linet Kavere katika harusi maridadi lakini bibi harusi aliaga dunia siku 18 baadaye.

Wawili hao walikutana katika Chuo Kikuu cha Masinde Muliro wakiwa wanafunzi na kuanza kuwa marafiki wa dhati na kisha baadaye kuchumbiana baada ya kumaliza chuo.

 Mastin alipata ajira kama Mhandisi katika Shule ya Msingi ya Phanero mjini Mbale huku Linet akipata nafasi ya kufunza Kizungu katika Shule ya Wasichana ya Mbihi. 

 Waliidhinishwa rasmi kuwa mume na mke kwenye harusi iliyoandaliwa katika bustani la Sosa, Disemba 2020. 

Wakati wanandoa hao walirejea kutoka kwa fungate yao, walikuwa wanaazimia kuishi maisha ya raha mstarahe hadi kifo kitakapowatenganisha.

 Lakini walitenganishwa siku moja baada ya fungate huku Linet akianza kukumbana na matatizo ya kupumua, akazirai na kisha kukimbizwa katika Hospitali ya Kisumu Specialists ambapo alithibitishwa kufariki saa chache baadaye. 

Humphrey Odanga, mwalimu mkuu wa Mbihi, ambapo marehemu alikuwa akihudumu, alimsifu Linet kwa kuwa mwalimu mwenye bidii. 

“Alikuwa nasi karibia miaka miwili na kando na kuugua magonjwa ya kawaida kama mtu yeyote yule, hakuonyesha dalili zozote za kuwa na changamoto za kiafya," alisema. 

Kulingana na Bi. Jane Ambani, rafiki wa familia hiyo, kifo chake cha ghafla kiliwashtua wengi.

 “Bibi harusi hata hakuwa ameanza kuishi kwa nyumba ya bwana harusi ya Magada tangu harusi yao,” alisema.

 Linet alizikwa Jumamosi, Januari 9, 2021, saa tatu baada ya mwili wake kuwasili kutoka makafani kulingana na sheria za COVID-19.

 Matokeo ya upasuaji ilionyesha kuwa Linet alikumbana na shinikizo la damu kwenye mishipa. 

Wafanyakazi wenzake pamoja na marafiki zake walitoa rambi rambi zao kufuatia kifo chake.

CHANZO - TUKO NEWS


Share:

SERIKALI KUENDELEA NA MSAKO MKALI KWA WANAOTUMIA WALEMAVU...38 WARUDISHWA SHINYANGA


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga (katikati) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Mkoa wa Shinyanga, Ndg. Richard Mpongo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Yasinta Mboneko.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Yasinta Mboneko (kulia) akieleza jambo wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga (pembeni) ni Katibu wa Naibu Waziri huyo Bw. Omary Sama
***

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu, Ummy Nderiananga amesema wataendelea na msako wa watu wanaowatumia walemavu katika vitendo vya kuwadhalilisha mpaka watakap hakikisha wahusika wanafanya vitendo hivyo wanaacha kabisa.

Ummy amesema hayo wakati wa ziara yake ya kuwarejesha baadhi ya watu wenye ulemavu karibu 38 mkoani Shinyanga kutoka Jijini Dar es Salaam, kutokana na kundi hilo kutumiwa na watu wenye maslahi binafsi kuwazungusha watu wenye ulemavu kuomba fedha barabarani.

“Leo hii tumewarejesha Watu wenye Ulemavu zaidi ya 38 kutoka Jijini Dar es Salaam kuja hapa Mkoani Shinyanga mahali ambapo wamekuwa wakiishi hapo awali, hivyo kama rejista hiyo ingekuwepo basi zoezi la utambuzi wa baadhi yao ingekuwa rahisi kuwatambua, Tutaendelea na msako hadi pale tutakapoona wahusika wa mtandao huu wanaacha kabisa vitendo hivyo vya udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu,” alisisitiza Naibu Waziri Ummy

Aidha Naibu Ummy ameeleza serikali ipo katika mkakati wa kuandaa regista ya watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, kata, Halmashauri na Mkoa ili kuwa na takwimu sahihi zitakazoonyesha idadi ya wenye ulemavu ,kujua mahali walipo, wanajishughulisha na nini katika jamii waliyopo.

“Uwepo wa rejista hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa serikali kutambua idadi ya watu wenye ulemavu waliopo kwenye maeneo mbalimbali na hivyo kurahisisha ufikikaji wa huduma kwa kundi hilo kwa urahisi,” alisema Naibu Waziri Ummy.

CHANZO - EATV


Share:

Full Stack Engineer at SMART CODES

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Full Stack Engineer   SMART CODES Dar es Salaam, Tanzania Founder & CEO @SmartCodes with a passion for Technology, Innovation and Advertising | Helping young African startups flourish and grow via @SmartLab255 #UNTILITSDONE Overview Our Technology team is an integral part of our business. We are looking for an experienced Full-Stack Developer bringing creativity and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu January 11



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 11,2021





























Share:

Sunday, 10 January 2021

Syrup Room and Water Treatment Team Leader at Coca-Cola Kwanza

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Syrup Room and Water Treatment Team Leader   Closing Date: 2021/01/18 Reference Number: CCB210108-2 Function Manufacturing Company Coca-Cola Kwanza (Tanzania) Job Type: Permanent Location – Country Tanzania Location – Province Not Applicable Location – Town / City Mbeya Job Description Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Manufacturing Department. We are looking for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Accountant, Call Center Interns, Debt Collection Trainees ,Sales Executives at Credit & Debt Masters Co Ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About us Credit & Debt Masters Co Ltd prides as a premier credit and debt management services provider in Tanzania, devoting our both human and capital resources into helping our clients maximize their cash flows, add value to their organizations and gain a competitive advantage. Our key services includes; Debt Management and Recovery, Credit Control […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger