Thursday, 7 January 2021
Wednesday, 6 January 2021
Software Engineer at AA TANCH Holding Company LTD
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job title: Software engineer (1 position) Location: ARUSHA, Head office Reports to: Managing director Projects: SOKOKUUONLINE AND TANCH EXPRESS APP SUMMARY: AA TANCH holding company ltd is a private limited company established in 2018.It focused on connecting buyers to seller, dedicated in providing easy, reliable and secure trades as well as shipment and delivery of products from china. As […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
TANAPA: Names Called for Interview at UTUMISHI on 16th – 19th January, 2021 | Walioitwa Usaili TANAPA 2021 | Tanzania National Parks, 2021
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Tanzania National Parks (TANAPA) PRESIDENT’S OFFICE PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT (PSRS) Ref.No.EA.7/96/01/L/11 – Posted: 05th January, 2021 Overview: The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) is a government organ with a status of independent Department established specifically to facilitate the recruitment process of employees to the Public Service. Public Service Recruitment Secretariat was established by […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
PROF.MKENDA APANIA KUREJESHA HADHI YA USHIRIKA NCHINI
Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Warajis Wasaidizi wa mikoa ya Tanzania Bara leo 6.1.2021 katika hafla ya kukabidhi vitendea kazi yakiwemo magari pamoja na kompyuta katika Ofisi za Tume ya Maendeleo ya Ushirika Jijini Dodoma.
Mrajis Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege akitoa taarifa wakati hafla ya kukabidhi vitendea kazi yakiwemo magari pamoja na kompyuta katika Ofisi za Tume ya Maendeleo ya Ushirika Jijini Dodoma.
Sehemu ya Warajis kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara wakimsikiliza Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda leo Jiji Dodoma.
Waziri wa Kilimo Prof.Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi kompyuta mpakato (laptop)Afisa Ushirika wa Mkoa wa Geita Dorah Mwabeza(Kushoto)kwa niaba ya Mrajis wa Mkoa huo.Prof. Mkenda amekabidhi laptop 20 pamoja na kompyuta za kawaida 50 zilizotolewa naTume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma kwa warajis.Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege
Waziri wa Kilimo Prof.Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi funguo za gari Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Simiyu Ibrahimu Kadudu (Kushoto).Prof. Mkenda amekabidhi magari matano yenye thamani ya milioni 275/= yaliyotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege
Waziri wa Kilimo Prof. Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi funguo ya gari Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro Henjewele John (Kushoto.

Waziri wa Kilimo Prof. Adolph Mkenda (Katikati) akikimkabidhi kompyuta mpakato (laptop)Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Njombe Bi.Consolata Kiluma (Kushoto).Prof. Mkenda amekabidhi laptop 20 pamoja na kompyuta za kawaida 50 zilizotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma.Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege

Sehemu ya magari manne aina ya Nissan Hard N 300 Double Cabin 4WD yenye thamani ya Shilingi 275,091,670/- kwa pamoja yalikabidhiwa kwa Warajis Wasaidizi wa mkoa wa Simiyu, Kilimanjaro, Njombe na Dar es Salaaam na gari moja lililotumika kwa mkoa wa Kigoma.
Na Alex Sonna, Dodoma
SERIKALI imeahidi kuendelea kutatua changamoto ya vitendea kazi kwa watumishi Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini(TCDC) ili wafanye kazi kwa ufanisi na kurejesha hadhi na heshima ya ushirika nchini.
Sambamba na hilo, imeapa kutofumbia macho mtu yeyote atakayebainika kuchezea fedha za ushirika.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda hafla ya kukabidhi magari matano na komputa 70 kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi kwa watumishi wa Tume hiyo.
Amesema anafahamu watumishi hao wanafanya kazi kwenye mazingira magumu hivyo serikali inapambana ili kuhakikisha wanaondoa kero zinazowakabili.
Hata hivyo ameeleza bado kunahitajika mapambano ya wizi na ubadhirifu kwenye vyama vya ushirika licha ya kuonekana kupungua kutokana na jitihada zilizofanywa na serikali za kurudisha mali za ushirika.
"Hatutachekeana na mtu anayecheza na mali za ushirika kwasababu ukifanya hivyo unakatisha watu tamaa, watakuwa hawana hamu ya kujiunga na ushirika, Warajis Wasaidizi tusimame kidete kwenye hilo,"amesema.
Pia amesema licha ya ubadhirifu kupungua lakini bado kuna tatizo la vyama kushindwa kuandaa vyema hesabu zake na kusababisha kukosa hati safi.
Kuhusu Sheria, Waziri huyo amesema kuna kazi ya kurudisha imani za watu kwenye ushirika kwa kupitia upya Sheria ya Ushirika na tayari kazi imeshaanza.
Awali Mtendaji Mkuu wa Tume hiyo ambaye pia ni Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Dk.Benson Ndiege, amesema Tume itaendelea kupambana na kero zinazoukabili ushirika ikiwamo ubadhirifu na uongozi mbovu kwenye vyama hivyo.
Aidha, Dk.Ndiege amesema Tume ipo kwenye mpango wa kuimarisha ofisi za ushirika nchini na itahakikisha kila mkoa una gari kabla ya mwaka wa fedha 2020/21 kukamilika.
"Leo kwa kutumia mapato ya ndani Sh.Milioni 275 zimenunua magari manne ambayo yataenda kwa Warajis wa mikoa ya Dar es salaam, Simiyu, Kilimanjaro na Njombe na pia tutatoa gari moja kwenda Kigoma kutokana na umuhimu wa kilimo cha michikichi,"amesema.
Aidha amesema wamegawa komputa 70 ambapo kati ya hizo 20 ni komputa mpakato(laptops) ambapo komputa 50 zimetolewa na Benki ya CRDB na hizo zingine zimenunuliwa kwa mapato ya ndani.
WAFUGAJI WA NYUKI NA WAFANYABIASHARA WA MAZAO YA NYUKI NCHINI WATAKIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA USHIRIKA
| Kamishna Msaidizi - Ufugaji Nyuki, Hussein Msuya akiwaeleza Mipambo mbalimbali ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania katika kuhakikisha wananufaika na fursa mbalimbali wanazozitoa kwa vikundi na kuwataka wajiunge ili waweze kuwa na sifa wakunufaika. |
Rudia Issa ni Mwenyekiti wa iliyokuwa TABEDO akiwasisitizia wanachama wake umuhimu wa kujiunga na Chama vya ushirika vilivyopo na vile vitakavyoanzishwa.
Wajumbe wa mkutano
Wajumbe wa mkutano
Mjumbe wa mkutano
Wajumbe wa mkutano
THIS IS SIMBA BWANAA!!! YAITANDIKA PLATNUMS YA ZIMBABWE 4G
WATAALAM SEKTA YA MAJI WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO VIZURI

Na Mohamed Saif, Tarime
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amewataka wataalam Sekta ya Maji kote nchini kutumia utaalam wao ili wananchi wapate huduma ya uhakika na toshelevu ya majisafi na salama
Ametoa maelekezo hayo Januari 5, 2021 wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa maji wa Gamasara Wilayani Tarime Mkoani Mara na kuzungumza na wanufaika wa mradi huo ambao kwa nyakati tofauti walimueleza changamoto zilizopo kwenye mradi.
Miongoni mwa changamoto zilizoelezwa na wananchi hao ni pamoja na mradi kushindwa kutoa maji inavyopasa kwani kuna wakati mabomba hua hayatoi maji.
Mara baada ya kujionea hali halisi ya mradi na maelezo ya wananchi wa maeneo husika, Waziri Aweso alisisitiza kuwa dhamira ya Serikali ya Rais. Dkt. John Pombe Magufuli ni kuwafikishia huduma ya maji wananchi wake na kwamba hatokubali kuwa kikwazo cha kufikiwa kwa dhamira hiyo na hivyo aliwataka wataalm wote kwenye Sekta ya Maji kujitathmini.
Waziri Aweso aliielekeza Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara kuhakikisha maboresho yanafanyika ili mradi uweze kutoa maji kama inavyopasa kwa lengo la kuhudumia wananchi wengi zaidi.
Alisema kuwa wananchi wanachohitaji ni maji na aliwaelekeza wataalam katika Sekta ya Maji kujiepusha na porojo badala yake wahakikishe wanajikita na kudumu kwenye falsafa ya maji bombani.
“Wataalam wetu kwenye Sekta ya Maji acheni porojo, elekezeni taaluma zenu na ubunifu katika kuhakikisha wananchi wanaondokana na kero ya maji,” alielekeza Waziri Aweso.
Aliongeza “unapokuwa mtaalam lazima utoe ushauri kulingana na utaalamu wako, tunapoanzisha mradi maana yake ni wananchi wapate huduma, wataalam tutumie taaluma zetu kusaidia wananchi wapate maji,” alielekeza Waziri Aweso
Aidha, Waziri Aweso alizielekeza Jumuia za Watumia Maji kote nchini kuhakikisha zinasimamia vizuri miradi ya maji kwenye jumuia zao ikiwa ni pamoja na kuongeza umakini kwenye makusanyo kwa lengo la kuwa na miradi endelevu.
“Miradi mliyokabidhiwa inapaswa kuwa endelevu, sasa ni jukumu lenu kuhakikisha hili linafikiwa, hakikisheni mnashirikiana, mnaitunza na mnisimamia vizuri,” alielekeza Waziri Aweso.
SHIRIKA LA RAFIKI SDO LACHANGIA MIFUKO YA SARUJI UJENZI WA MADARASA MAZINGE SEKONDARI
Walimu Wakuu shule za msingi watakiwa kusimamia fedha zinazotolewa na Serikali
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka walimu wakuu wa shule za msingi nchini kuhakikisha wanasimamia fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa kufuata sheria na taratibu katika matumizi.
Akifungua mkutano mkuu wa pili wa umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania Bara jana , Jijini Dodoma Mhandisi Nyamhanga amesema serikali inapeleka fedha za ruzuku mashuleni kwa kila mwezi ili ziweze kununua vifaa vya kufundishia, kujifunzia hivyo ni jukumu la walimu kusimamia kwa umakini na kuhakikisha wanafunzi hao wanapata elimu bora.
Mhandisi Nyamhanga anafafanua kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha elimu ya msingi hapa nchini inakuwa bora kwa kuboresha miundombinu ya elimu, hivyo ni wajibu wa Wakuu wa Shule za Msingi kuhakikisha fedha hizo zinasimamiwa kikamilifu.
“Serikali iko makini kuhakikisha suala la elimu linakuwa mbele zaidi kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maboresho ya miundombinu katika ujenzi wa vyoo,nyumba za walimu na mabweni ni kazi yenu kuhakikisha fedha hizo zinasimamiwa ili ziweze kutumika katika miradi iliyokusudiwa ,”amefafanua Mhandisi Nyamhanga
Mhandisi Nyamhanga amesema Serikali imeweka mikakati ya kuimarisha elimu ya msingi na kusisitiza kuwa fedha za programu ya elimu bila malipo zitatumika kufidia malipo ya ada,posho kwa walimu wakuu pamoja na huduma nyingine za msingi.
Aidha, Nyamhanga ametumia fursa hiyo kuweka wazi kuwa Serikali inalaani vitendo vya udanganyifu wa mitihani na kuwataka walimu wakuu nchini kuendelea kudhibiti vitendo hivyo ili kuboresha elimu ya msingi.
“ Ni jambo la kusikitisha kuona katika ulimwengu huu bado walimu hamuwezi kudhibidi wizi wa mitihani,tunawakatisha tama wanafunzi wanaojituma,”amesema Mhandisi Nyamhanga.
Mhandisi Nyamhanga amesema vitendo vya udanganyifu wa mitihani bado ni tatizo ambalo lipo linatia doa doa kubwa kwani kwa kipindi cha mwaka jana pekee jumla ya wanafunzi 1065 walifutiwa matokeo ya mitihani kwa udanganyifu na kuwataka walimu hao wakuu kuangalia namna ya kudhibiti na kwamba hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa watakaovujisha .
Wakati huo, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Gerald Mweli ametoa rai kwa umoja huo kujituma katika kutoa elimu bora kwa jamii ili kuzalisha wataalamu watakaotosha nchini.
Naye Rehema Ramole Mwenyekiti wa umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania Bara ameishukuru serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kulipa walimu mishahara yao kipindi chote shule zilipofungwa kutokana na ugonjwa wa Corana.




























