Wednesday, 6 January 2021

PROF.MKENDA APANIA KUREJESHA HADHI YA USHIRIKA NCHINI

 

 

Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Warajis Wasaidizi wa mikoa ya Tanzania Bara leo 6.1.2021 katika hafla ya kukabidhi vitendea kazi yakiwemo magari pamoja na kompyuta katika Ofisi za Tume ya Maendeleo ya Ushirika Jijini Dodoma.

Mrajis Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege akitoa taarifa wakati hafla ya kukabidhi vitendea kazi yakiwemo magari pamoja na kompyuta katika Ofisi za Tume ya Maendeleo ya Ushirika Jijini Dodoma.

Sehemu ya Warajis kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara wakimsikiliza Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda leo Jiji Dodoma.

Waziri wa Kilimo Prof.Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi kompyuta mpakato (laptop)Afisa Ushirika wa Mkoa wa Geita Dorah Mwabeza(Kushoto)kwa niaba ya Mrajis wa Mkoa huo.Prof. Mkenda amekabidhi laptop 20 pamoja na kompyuta za kawaida 50 zilizotolewa naTume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma kwa warajis.Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege

Waziri wa Kilimo Prof.Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi funguo za gari Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Simiyu Ibrahimu Kadudu (Kushoto).Prof. Mkenda amekabidhi magari matano yenye thamani ya milioni 275/= yaliyotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege

Waziri wa Kilimo Prof. Adolph Mkenda (Katikati) akimkabidhi funguo ya gari Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro Henjewele John (Kushoto.

Waziri wa Kilimo Prof. Adolph Mkenda (Katikati) akikimkabidhi kompyuta mpakato (laptop)Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Njombe Bi.Consolata Kiluma (Kushoto).Prof. Mkenda amekabidhi laptop 20 pamoja na kompyuta za kawaida 50 zilizotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika leo 6.1.2021 jijini Dodoma.Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt.Benson Ndiege

Sehemu ya magari manne aina ya Nissan Hard N 300 Double Cabin 4WD yenye thamani ya Shilingi 275,091,670/- kwa pamoja yalikabidhiwa kwa Warajis Wasaidizi wa mkoa wa Simiyu, Kilimanjaro, Njombe na Dar es Salaaam na gari moja lililotumika kwa mkoa wa Kigoma.

 Na Alex Sonna, Dodoma 

SERIKALI imeahidi kuendelea kutatua changamoto ya vitendea kazi kwa watumishi Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini(TCDC) ili wafanye kazi kwa ufanisi na kurejesha hadhi na heshima ya ushirika nchini. 

Sambamba na hilo, imeapa kutofumbia macho mtu yeyote atakayebainika kuchezea fedha za ushirika. 

 

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda hafla ya kukabidhi magari matano na komputa 70 kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi kwa watumishi wa Tume hiyo.

 Amesema anafahamu watumishi hao wanafanya kazi kwenye mazingira magumu hivyo serikali inapambana ili kuhakikisha wanaondoa kero zinazowakabili. 

Hata hivyo ameeleza bado kunahitajika mapambano ya wizi na ubadhirifu kwenye vyama vya ushirika licha ya kuonekana kupungua kutokana na jitihada zilizofanywa na serikali za kurudisha mali za ushirika. 

"Hatutachekeana na mtu anayecheza na mali za ushirika kwasababu ukifanya hivyo unakatisha watu tamaa, watakuwa hawana hamu ya kujiunga na ushirika, Warajis Wasaidizi tusimame kidete kwenye hilo,"amesema. 

 Pia amesema licha ya ubadhirifu kupungua lakini bado kuna tatizo la vyama kushindwa kuandaa vyema hesabu zake na kusababisha kukosa hati safi. 

Kuhusu Sheria, Waziri huyo amesema kuna kazi ya kurudisha imani za watu kwenye ushirika kwa kupitia upya Sheria ya Ushirika na tayari kazi imeshaanza. 

Awali  Mtendaji Mkuu wa Tume hiyo ambaye pia ni Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Dk.Benson Ndiege, amesema Tume itaendelea kupambana na kero zinazoukabili ushirika ikiwamo ubadhirifu na uongozi mbovu kwenye vyama hivyo.

 Aidha, Dk.Ndiege amesema Tume ipo kwenye mpango wa kuimarisha ofisi za ushirika nchini na itahakikisha kila mkoa una gari kabla ya mwaka wa fedha 2020/21 kukamilika.

 "Leo kwa kutumia mapato ya ndani Sh.Milioni 275 zimenunua magari manne ambayo yataenda kwa Warajis wa mikoa ya Dar es salaam, Simiyu, Kilimanjaro na Njombe na pia tutatoa gari moja kwenda Kigoma kutokana na umuhimu wa kilimo cha michikichi,"amesema.

 

Aidha amesema wamegawa komputa 70 ambapo kati ya hizo 20 ni komputa mpakato(laptops) ambapo komputa 50 zimetolewa na Benki ya CRDB na hizo zingine zimenunuliwa kwa mapato ya ndani.
Share:

WAFUGAJI WA NYUKI NA WAFANYABIASHARA WA MAZAO YA NYUKI NCHINI WATAKIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA USHIRIKA

MSUYA.JPG
Kamishna Msaidizi - Ufugaji Nyuki, Hussein Msuya akiwaeleza Mipambo mbalimbali ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania katika kuhakikisha wananufaika na fursa mbalimbali wanazozitoa kwa vikundi na kuwataka wajiunge ili waweze kuwa na sifa wakunufaika.


MWENYEKITI TABEDO.JPG

Rudia Issa ni Mwenyekiti wa  iliyokuwa TABEDO  akiwasisitizia wanachama wake umuhimu wa kujiunga na Chama vya ushirika vilivyopo na vile vitakavyoanzishwa.
WADAU.JPGWajumbe wa mkutano
WADAU2.JPGWajumbe wa mkutano
MJUMBE.JPGMjumbe wa mkutano
WAJUMBE.JPGWajumbe wa mkutano
MWENYEKITI NA NAIBU MWENYEKITI WA TABEDO.JPG

Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TBEDO  Ayubu Kamwaga na  Mwenyekiti wake Rudia Issa ni wakicheka kwa Furaha baada ya kuthibitishiwa kuzaliwa uya kwa chama hicho kama chama cha ushirika baada ya kufutwa rasmi na Serikali kwa mujibu wa Sheria.


Wafugaji wa nyuki na wafanyabiashara wa mazao ya nyuki nchini wametakiwa kuimarisha na kujiunga na vyama vya msingi vya ushirika ili waweze kunufaika na huduma zitolewazo na vyama hivyo.
 
Wito huo umetolewa jana Januari 5,2021 na Kamishna Msaidizi - Ufugaji Nyuki, Hussein Msuya alipokuwa akifungua mkutano maalumu wa Jukwaa la Ufugaji Nyuki  nchini – TABEDO katika ukumbi wa Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Dodoma.
 
Msuya alisema, baada ya Serikali kufuta kampuni  zenya ukomo wa ahadi na yasiyo na mtaji ambayo hayafanyi shughuli za kukuza biashara na ukwekezaji yaliyokiwa yamesajiliwa na msajili wa Makampuni (BRELA). TABEDO ikiwemo, imelazimika kukutana na wanachama wake kwa lengo la kujadili hatma yao na kuunda kamati itakayokwenda kufanya tathimini ya vyama vya msingi vya ushirika wa wafugaji nyuki nchini. 
 
“Hivi sasa hatuelewi “status” ya vyama vya msingi hivyo kamati hii itakayokwenda kuundwa leo itafanya tathimini kuona ni nini kinaendelea, tukishaelewa sasa tutaenda kuangalia ni nini hasa kilichopelekea vyama hivi kusinzia au kufa,
 
“na kwa kushirikiana na watu wa ushirika kamati itaangalia ni mambo gani itafanya kuhakikisha vyama hivi vinasimama na kushauri namna bora ya kuunda muunganiko utakakuwa mbadala wa TABEDO na kuja na mfumo mwingine wa kuunganisha vyama vya mushirika vya  msingi” anasema Kamishna Msaidizi huyo.
 
Msuya alitoa wito kwa wananchama kutoa ushirikiano kwa kamati itakayoundwa ili kujitendea haki kwa kile alichokisema “unakata mti unapanda mti sio unaenda kulala”. 
Azima  ya kukuza viwanda haitatimia ikiwa hakutakuwa na ushirika wa wafugaji nyuki ulio imara, ushirika  wa wafugaji nyuki utawezesha kuapta nguvu ya kukuza mitaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki, ambayo ni malighafi ya viwanda vya mazao ya nyuki.
 
Rudia Issa ni Mwenyekiti wa  iliyokuwa TABEDO anasema wako tayari kushirikiana na kamati itakayoundwa ili kuweza kuunda vyama vya ushirika vitakavyokwenda kutoa ufumbuzi wa mahitaji ya wafugaji nyuki nchini.
 
Alisema kila mfugaji nyuki akitambua umuhimu wa kuwa mwanachama wa ushirika, atanufaika na mafao mbalimbali ikiwamo kupatiwa mikopo kutoka katika taasisi za fedha pamoja na soko la uhakika la mazao yake.
 
Lemiona Kimeshua ni mfugaji nyuki na mwananchama wa TABEDO anasema aliacha shughuli za ufugaji nyuki na kubaki kuwa mnunuzi kutokana na kulegalega kwa vyama vya ushirika lakini kutokana na mkazo mkubwa wa Serikali kwenye sekta hiyo ameamua kufufua na kuanzisha mashamba mapya ya nyuki.
 
 
Tulizo Kilaga
Corporate Communication Specialist
Tanzania Forest Service Agency (T F S), 
P.O. Box 40832, 
Mpingo House, Nyerere Road,
Dar es Salaam, Tanzania. 
Mobile phone: +255715/ 623 888887
Office: +255 23 2604387
Share:

THIS IS SIMBA BWANAA!!! YAITANDIKA PLATNUMS YA ZIMBABWE 4G


Na Shishira Mnzava, DAR ES SALAAM
MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamefanikiwa kwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa 4-0 dhidi ya FC Platinums ya Zimbabwe leo Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Simba SC inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 4-1 kufuatia kufungwa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumatano iliyopita mjini Harare.

Hii inakuwa mara ya tatu kwa Wekundu hao wa Msimbazi kutinga hatua ya makundi baada ya mwaka 2003 walipoitoa Zamalek ya Misri waliokuwa mabingwa watetezi na 2018 walipoitoa Nkana FC ya Zambia.
Simba SC inayofundishwa na Mbelgiji, Sven Ludwig Vandenbroeck ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Erasto Edward Nyoni kwa penalti dakika ya 39 baada ya beki mwenzake, Shomari Salum Kapombe kuvutwa jezi na Tawana Chikore.

Kipindi cha pili Kapombe akaifungia Simba SC bao la pili dakika ya 61 akimalizia mpira uliotemwa na kipa Francis Tizayi kufuatia shuti la kiungo Mzambia Rally Bwalya.

Nahodha John Raphael Bocco aliyetokea benchi kipindi cha pili kuchukua nafasi ya mshambuliaji mwenzake, Mnyarwanda Meddie Kagere akaifungia Simba SC bao la tatu dakika ya 90 na ushei akimalizia pasi ya Bwalya tena.

Mzambia mwingine, Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania, kiungo Clatous Chotta Chama akaifungia Simba SC bao la nne kwa penalti dakika ya 90 na ushei baada yay eye mwenyewe kuvutwa kwenye boksi na Gift Bello.

Kagere aliingia dakika ya 76 kuchukua nafasi ya mshambuliaji mwingine, Mkongo Chris Mutshimba Kope Mugalu lakini akaumia dakika ya 85 na nafasi yake ikachukuliwa Bocco.

Baada ya msimu mbaya uliopita timu za Tanzania, Simba na Azam FC zikitolewa mapema michuano ya Afrika – hatimaye mwaka huu mambo mazuri, kwani na Namungo FC imetinga kwneye mchujo wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho. 

Namungo FC imefanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika baada ya sare ya 3-3 na wenyeji, na Al Hilal Obayed jana Uwanja wa Al-Hilal mjini Omdurman, Sudan.

Kwa matokeo hayo Namungo FC inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-3 na sasa itamenyana na moja ya timu zitakazotolewa kwenye Ligi ya Mabingwa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Droo ya hatua ya makundi ya michuano hiyo itafanyika Ijumaa Saa 8:00 mchana makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mjini Cairo, Misri.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Joash Onyango, Pascal Wawa, Erasto Nyoni, Rally Bwalya, Said Ndemla/Ibrahim Ame dk60, Chris Mugalu/Meddie Kagere dk76/John Bocco dk85, Clatous Chama na Luis Miquissone.FC Platinums; Francis Tizayi, Gift Mbweti, Nomore Chinyerere, Gift Bello, Ralph Kawondera, Donald Dzvinyai, Kelvin Madzongwe, Rahman Kutsanzira, Khumalo Denzel/Raphael Muduviwa dk58, Perfect Chikwende na Tawana Chikore.

CHANZO - BINZUBEIRY BLOG

Share:

WATAALAM SEKTA YA MAJI WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO VIZURI

 

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akikagua tenki la maji mradi wa Gamasara Wilayani Tarime Mkoani Mara.

Na Mohamed Saif, Tarime

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amewataka wataalam Sekta ya Maji kote nchini kutumia utaalam wao ili wananchi wapate huduma ya uhakika na toshelevu ya majisafi na salama

Ametoa maelekezo hayo Januari 5, 2021 wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa maji wa Gamasara Wilayani Tarime Mkoani Mara na kuzungumza na wanufaika wa mradi huo ambao kwa nyakati tofauti walimueleza changamoto zilizopo kwenye mradi.

Miongoni mwa changamoto zilizoelezwa na wananchi hao ni pamoja na mradi kushindwa kutoa maji inavyopasa kwani kuna wakati mabomba hua hayatoi maji.

Mara baada ya kujionea hali halisi ya mradi na maelezo ya wananchi wa maeneo husika, Waziri Aweso alisisitiza kuwa dhamira ya Serikali ya Rais. Dkt. John Pombe Magufuli ni kuwafikishia huduma ya maji wananchi wake na kwamba hatokubali kuwa kikwazo cha kufikiwa kwa dhamira hiyo na hivyo aliwataka wataalm wote kwenye Sekta ya Maji kujitathmini.

Waziri Aweso aliielekeza Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara kuhakikisha maboresho yanafanyika ili mradi uweze kutoa maji kama inavyopasa kwa lengo la kuhudumia wananchi wengi zaidi.

Alisema kuwa wananchi wanachohitaji ni maji na aliwaelekeza wataalam katika Sekta ya Maji kujiepusha na porojo badala yake wahakikishe wanajikita na kudumu kwenye falsafa ya maji bombani.

“Wataalam wetu kwenye Sekta ya Maji acheni porojo, elekezeni taaluma zenu na ubunifu katika kuhakikisha wananchi wanaondokana na kero ya maji,” alielekeza Waziri Aweso.

Aliongeza “unapokuwa mtaalam lazima utoe ushauri kulingana na utaalamu wako, tunapoanzisha mradi maana yake ni wananchi wapate huduma, wataalam tutumie taaluma zetu kusaidia wananchi wapate maji,” alielekeza Waziri Aweso

Aidha, Waziri Aweso alizielekeza Jumuia za Watumia Maji kote nchini kuhakikisha zinasimamia vizuri miradi ya maji kwenye jumuia zao ikiwa ni pamoja na kuongeza umakini kwenye makusanyo kwa lengo la kuwa na miradi endelevu.

“Miradi mliyokabidhiwa inapaswa kuwa endelevu, sasa ni jukumu lenu kuhakikisha hili linafikiwa, hakikisheni mnashirikiana, mnaitunza na mnisimamia vizuri,” alielekeza Waziri Aweso.

 

Share:

SHIRIKA LA RAFIKI SDO LACHANGIA MIFUKO YA SARUJI UJENZI WA MADARASA MAZINGE SEKONDARI

Kulia ni Meneja Miradi wa Shirika la Rafiki SDO, Dk. Nyamkongi Lucas akimkabidhi mifuko ya saruji Afisa Mtendaji wa Kata ya Ndembezi, Timothy Timoth kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Shirika la Rafiki Social Development Organization (Rafiki SDO) limechangia mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili kwenye shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga. 

Meneja Miradi wa Shirika la Rafiki SDO, Dk. Nyamkongi Lucas amekabidhi mifuko hiyo yenye thamani ya shilingi 190,000/= leo Jumatano Januari 6,2021 kwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Ndembezi, Timothy Timoth katika shule ya Sekondari Mazinge. 

Dk. Lucas amesema Shirika la Rafiki SDO limetoa msaada huo wa mifuko ya saruji kutokana na kwamba wao ni wadau wa maendeleo hivyo wameguswa ili kufanikisha zoezi la ujenzi wa madarasa kwa sababu linawahusu watu wote katika jamii. 

“Tunahitaji kujenga jamii yenye watu wasomi, hivyo hatuwezi kupata wasomi kama hatujawatengeneza sisi wenyewe. Ni sisi wanajamii tunahusika katika kujenga wasomi hawa hivyo kama sehemu ya jamii tumechangia mifuko 10 ya saruji yenye thamani ya shilingi 190,000/= kuongeza nguvu katika ujenzi wa madarasa”,amesema Dk. Lucas. 

“Tutazidi kushirikiana na serikali katika shughuli za maendeleo kwa sababu sisi jina letu ni Rafiki Social Development Organization kwa hiyo maendeleo ya jamii ni sehemu yetu. Tunapoona jamii inafanya maendeleo sisi kama wadau wakuu wa maendeleo tunawiwa zaidi kushirikiana nao”,ameongeza Dk. Lucas 

Akipokea mifuko hiyo ya saruji, Afisa Mtendaji wa kata ya Ndembezi Timothy Timoth amelishukuru Shirika la Rafiki SDO kwa mchango huo wa mifuko ya saruji akieleza kuwa itasaidia katika kumalizia ujenzi wa madarasa 

Aidha Timoth amewaomba wadau wengine wa maendeleo kujitokeza kwani jambo la ujenzi wa madarasa ni la watu wote katika jamii. 

Amesema shule ya Sekondari Mazinge ina uhitaji wa madarasa manne hivi sasa wanaendelea na ujenzi wa madarasa mawili unaotarajiwa kukamilika Januari 10,2021 huku akibainisha kuwa jumla ya wanafunzi 230 kuanza masomo ya kidato cha kwanza tofauti na mwaka 2020 ambapo wanafunzi walikuwa 196. 
Kulia ni Meneja Miradi wa Shirika la Rafiki SDO, Dk. Nyamkongi Lucas akimkabidhi mifuko ya saruji Afisa Mtendaji wa Kata ya Ndembezi, Timothy Timoth kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga leo Jumatano Januari 6,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Kulia ni Meneja Miradi wa Shirika la Rafiki SDO, Dk. Nyamkongi Lucas akimkabidhi mifuko ya saruji Afisa Mtendaji wa Kata ya Ndembezi, Timothy Timoth kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga.
Mifuko ya saruji iliyotolewa na Shirika la Rafiki SDO kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga.
Kulia ni Meneja Miradi wa Shirika la Rafiki SDO, Dk. Nyamkongi Lucas akizungumza wakati akikabidhi mifuko ya saruji kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga.
Kushoto ni  Afisa Mtendaji wa Kata ya Ndembezi, Timothy Timoth akilishukuru Shirika la Rafiki SDO kwa kuchangia mifuko ya saruji kwa ajili ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge.
Wadau wa maendeleo wakiwa katika eneo la ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga. 
Wadau wa maendeleo wakiwa katika eneo la ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mazinge iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Walimu Wakuu shule za msingi watakiwa kusimamia fedha zinazotolewa na Serikali


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka walimu wakuu wa shule za msingi nchini kuhakikisha wanasimamia fedha zinazotolewa na Serikali  kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu  kwa kufuata sheria na taratibu katika matumizi.

Akifungua mkutano mkuu wa pili wa umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania Bara jana , Jijini Dodoma Mhandisi Nyamhanga amesema serikali inapeleka fedha  za ruzuku mashuleni kwa kila mwezi ili ziweze kununua vifaa vya kufundishia, kujifunzia hivyo ni jukumu la  walimu  kusimamia kwa umakini na kuhakikisha wanafunzi hao wanapata elimu bora.

Mhandisi Nyamhanga anafafanua kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha elimu ya msingi hapa nchini inakuwa bora kwa kuboresha miundombinu ya elimu, hivyo ni wajibu wa Wakuu wa Shule za Msingi kuhakikisha fedha hizo zinasimamiwa kikamilifu.

“Serikali iko makini kuhakikisha suala la elimu linakuwa mbele zaidi kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maboresho ya miundombinu katika ujenzi wa vyoo,nyumba za walimu na mabweni ni kazi yenu kuhakikisha fedha hizo zinasimamiwa ili ziweze kutumika katika miradi iliyokusudiwa ,”amefafanua Mhandisi Nyamhanga

Mhandisi Nyamhanga amesema Serikali imeweka mikakati ya kuimarisha elimu ya msingi na kusisitiza kuwa fedha za programu ya elimu bila malipo zitatumika kufidia malipo ya ada,posho kwa walimu wakuu pamoja na huduma nyingine za msingi.

Aidha, Nyamhanga ametumia fursa hiyo kuweka wazi kuwa Serikali inalaani vitendo vya udanganyifu wa mitihani na kuwataka walimu wakuu nchini kuendelea kudhibiti vitendo hivyo ili kuboresha elimu ya msingi.

“ Ni jambo la kusikitisha kuona katika ulimwengu huu bado walimu hamuwezi kudhibidi wizi wa mitihani,tunawakatisha tama wanafunzi wanaojituma,”amesema Mhandisi Nyamhanga.

Mhandisi Nyamhanga amesema vitendo vya udanganyifu wa mitihani bado ni tatizo ambalo lipo linatia doa  doa  kubwa kwani kwa kipindi cha mwaka jana pekee jumla ya wanafunzi 1065 walifutiwa matokeo ya mitihani kwa udanganyifu na kuwataka walimu hao wakuu kuangalia namna ya kudhibiti na kwamba hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa watakaovujisha .

Wakati huo, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Gerald Mweli ametoa rai kwa umoja huo kujituma katika kutoa elimu bora kwa jamii ili kuzalisha wataalamu watakaotosha nchini.

Naye Rehema Ramole Mwenyekiti wa umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania Bara ameishukuru serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kulipa walimu mishahara yao kipindi chote shule zilipofungwa kutokana na ugonjwa wa Corana.


Share:

Waziri Jafo aipa tano Misungwi ujenzi wa hopsitali ya wilaya


Na Atley Kuni, Mwanza
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo ameoneshwa kufurahishwa na kupongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungi mkoani Mwanza kwa ubora wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.

Mpaka sasa utekelezaji wa ujenzi huo wamekamilisha majengo ya maabara pamoja na jengo la wagonjwa wanje (OPD), baada yakupokea Sh milioni 500 katika awamu ya kwanza ya ujenzi huo.

Akizungumza baada ya kukagua ujenzi wa jengo hilo, Waziri Jafo, amesema: “ miongoni mwa halmashauri zinazo nishawishi kwenda kuomba fedha zingine kwa Mhe. Rais John Pombe Magufuli ni pamoja na Halmashauri hii ya Misungwi.

“Ndugu zangu mimi, niwapongeze kwa kazi kubwa mlio ifanya, haihitaji kuwa na darubini kubaini ubora wa majengo haya, ukiangalia milango, Vigae, vioo nk. mliyotumia lakini hata uimara wa maeneo mbalimbali hii inatia hamasa sana, pamoja na kwamba hamkuwepo katika bajeti iliyopita lakini mmeitendea haki fedha iliyoletwa, hongereni sana.”

Awali akitoa taarifa ya ujenzi huo, Mkurugenzi wa Halmashuri hiyo, Kisena Mabula, amesema kukamilika kwa hospitali hiyo, itakuwa na uwezo wa kuwahudumia watu wapatao 462, 855 wa wilaya hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa mbele ya Mhe. Waziri Jafo, inaonesha hadi kukamilika kwa Hospitali hiyo itatumia kiasi cha Sh 2, 076 468, 848, ambapo katika hatua za awali halmashauri ilipokea kiasi cha Sh milioni 500 kutoka Serikali kuu, zilizo tumika kukamilisha ujenzi wa jengo la maabara pamoja na jengo la wagonjwa wanje (OPD).

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, alimpongeza Mhe. Waziri Jafo kwa ziara yake katika Mkoa huo, huku akimhakikishia kuwa wataendelea kusimamia miradi yote kwa umakini mkubwa kadri watakavyokuwa wanaipokea.

“ Nikuhakikishie mheshimiwa waziri (Jafo) kuwa tutasimiamia kwa umakini miradi yote itakakayokuwa inatekelezwa katika mkoa wetu lakini pia tunatingatia maelekezo ya viongozi wote wa juu akiwepo Mhe. Rais mwenyewe.”

Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ni moja kati ya Hospitali 97 zinazo endelea kujengwa nchi nzima

Awamu ya kwanza ya unejzu wa hospitali za wilaya ilijumuisha kujenga hospitali 67 na katika awamu ya pili inajumuisha ujenzi wa hospitali za wilaya 28 ambazo tayari ujenzi wake umanza ikiwa ni azima ya Serikali ya awamu ya tano kusogeza huduma karibu na wananchi.


Share:

Lindi Iko Nyuma Umilikishaji Ardhi-naibu Waziri Dkt. Mabula


 Na Munir Shemweta, WANMM LINDI
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameiagiza ofisi ya Ardhi mkoa wa Lindi kuhakikisha inatoa  elimu kwa wananchi wa mkoa huo ili waone umuhimu, faida na thamani ya kumiliki ardhi kutokana na mkoa huo kuwa nyuma katika umilikishaji ardhi.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo tarehe 5 Januari 2021 mkoani Lindi wakati akigawa hati za ardhi kwa wananchi wa kata za Mnazi Mmoja na Mingoyo katika halmashauri ya Manispaa ya Lindi akiwa katika ziara ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi mkoani humo.

Dkt Mabula alisema, mkoa wa Lindi uko nyuma kwa wananchi wake kujitokeza kumilikishwa maeneo ya ardhi wànayomiliki na kumbukumbu za mkoa zinaonesha kuna  jumla ya hati 7025 zilizotolewa kwa wamiliki wa ardhi na kusisitiza kuwa idadi hiyo ni ndogo kwa kuwa wananchi wengi hawajaamka na kuona thamani ya kumilikishwa.

“Ofisi ya Ardhi Mkoa mkatoe elimu kwa wananchi umuhimu na faida za kuwa na umiliki wa ardhi, maana hapa shida haiko katika kumilikishwa kwa hati za miaka 99 pekee bali hata zile za kimila hivyo lazima mkatoe elimu hata kwa wale wananchi walio vijijini ili wamilikishwe na kupatiwa hati watakayoitumia kwa faida ya maendeleo” alisema Dkt Mabula.

Aliitaka Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Lindi kujipanga vizuri na kwenda kwenye maeneo ya kata za mkoa huo kuwaelimisha wananchi faida za kuwa na hati ya ardhi kwa kuwa tangu kuanzishwa ofisi hiyo miezi sita iliyopita ni hati 367 pekee ndizo zilizotolewa idadi aliyoieleza kuwa ni ndogo ukilinganisha na mikoa mingine.

Aliwaeleza wakazi wa kata za Mnazi Mmoja na Mingoyo katika Manispaa ya Lindi kuwa, mkoa huo una maeneo mengi mazuri ya uwekezaji na iwapo watazembea kumilikishwa kuna hatari wakayauza kwa bei ya chini kwa kwa kisingizio cha kutopimwa au kuhaulishwa.

“Mkizembea kumilikishwa maeneo yenu sasa na kupatiwa hati, mtu akitaka kuwekeza mtampa kwa bei ya chini kwa kisingizio cha kutopimwa na mwingine atalichukua na baadaye ataliuza kwa bei kubwa kwa kuwa ulimuuzia likiwa halijapimwa” alisema Naibu Waziri Dkt Mabula.

Aliwataka wananchi wa mkoa wa Lindi kujitokeza kupima maeneo yao  na kuchukua hati na kusisitiza kuwa hata kama maeneo hayo hawayahitaji wanaweza kuyapima ili kuongeza thamani na baadaye watakapotaka kuyauza wauze na kupata fedha za kutosha.

Aidha, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini  kuhakikisha wanasimamia ipasavyo makusanyo ya kodi ya pango la ardhi kwa kuwa mapato ya kodi hiyo ndiyo yanayotumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, idara ya ardhi ikisimamiwa vizuri na Wakurugenzi wa Halmashauri wakiiwezesha kwa kuipatia vitendea kazi na bajeti ya kutosha basi inaweza kuingiza mapato mengi kuliko sekta nyingine yoyote kwa kuwa ardhi ndiyo kila kitu.

Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Lindi Said Kijiji alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na ofisi yake kuhakikisha maeneo mengi ya mkoa huo yanapimwa lakini mwamko wa wananchi ni mdogo.

Alisema, ofisi yake ilishatembelea halmashauri za mkoa huo na kuonana na wakurugenzi kwa lengo la kuendesha zoezi la kupima na   kumilikisha maeneo ambapo alisema mafanikio makubwa yalikuwa katika halmashauri ya Mtama.

Kwa upande wao wananchi wa Kata ya Mingoyo Manispaa ya Lindi Zakaria Michael Mwanga na Hadija Rashid Magaya waliokabidhiwa Hati ya pamoja walikuwa na haya ya kusema.


Share:

Meatu yafikia asilimia 90 ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa.

Samirah Yusuph

Meatu.
Juhudi za ziada kati ya wadau wa elimu, jamii pamoja na viongozi wa serikali katika kuhakikisha wanafikia malengo ya kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani hapa zimezaa matunda baada ya ukamilishaji kufikia asilimia 90.

Wilaya ya Meatu ikiwa na jumla ya wanafunzi 4,135 wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza ifikapo Januari 11,2021  inajumla ya vyumba vya madarasa 62 kati ya vyumba 92 vinavyohitajika upungufu ukiwa ni vyumba 39.

Huku madawati yaliyopo ni 2,650 kati ya madawati 4,600  yanayohitajika na upungufu ukiwa ni madawati 1,950.

Ukamilishaji huo umelenga kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika wilaya hiyo wanapata nafasi ya kuanza masomo kwa wakati.

Akizungumzia hatua hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu Fabian Manoza alisema kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari ni zoezi endelevu ambalo linatekelezwa kwa muda mrefu.

Isipokuwa kulikuwa na majengo hitajika ambayo yalikuwa bado hayajakamilika kutokana na sababu mbali mbali hivyo kilichofanyika ni kuhakikisha wanahamasisha  wananchi katika kukamilisha ujenzi ili wanafunzi wa kidato cha kwanza waanze masomo kwa wakati.

"Tumekuwa na ziara ya uhamasishaji kwa kushirikiana ambayo ni kamati ya ulinzi na usalama pamoja na kamati ya siasa, tumetembelea shule zote ambazo zilikuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa tukajionea wenyewe ukamilishaji wa vyumba hivyo," Alisema Manoza na kuongeza kuwa;

"Hadi sasa majengo yote yaliyokuwa yanahitajika yapo tayari na tuna uhakika wa watoto wote waliochaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari wataanza masomo yao bila kikwazo chochote na ifikapo Januari 15 tunatarajia kutembelea shule hizo ili kujihakikishia kama watoto wote wameanza masomo".

Akielezea mafanikio hayo Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Meatu Anthony Philipo alisema kuwa ufanikishaji huo ni matokeo ya muamko wa wazazi na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha watoto wanapata elimu.

"Kilichofanya kufanikisha kwa wakati ni mwitikio wa wananchi katika kuchangia nguvu kazi katika hatua ya ukamilishaji pamoja na utakelezaji mzuri wa majukumu wa watendaji wa serikali". Alisema Philipo na kuongeza kuwa;

"Ujenzi wa vyumba vyote vya madarasa haukutumia wakandarasi umetumia mafundi wa kawaida hivyo gharama za ujenzi ni nafuu na majengo yapo katika ubora wa hali ya juu".

Huku baadhi ya wananchi wakieleza kuvutiwa kwao na utendaji wa mkurugenzi wa Wilaya hiyo jambo ambalo linafanya wamuunge mkono kwa kushiriki nguvu kazi pale wanapohitajika kufanya hivyo.

"Anaye kushika mkono na yeye mshike kama viongozi wetu wa serikali tunawaona wanatufikia na kutuelewesha kuhusu watoto wetu kupata elimu ni lazima tushiriki kwa maana tunaona mchango wa pesa pamoja na nguvu zetu katika shule hizi zinazojengwa," Alisema Saguda Mwihu mkazi wa Kata ya Itinje.

Hadi hatua hii Halmashauri ya wilaya imechangia kiasi cha tsh milioni 360 katika ujenzi wa vyumba vya madarasa, huku mwenyekiti wa halmashauri hiyo akiahidi kutoa kipaumbele cha upatikanaji wa fedha za miradi ya maendeleo kutoka halmashauri katika vijiji ambavyo vitaonyesha ushirikiano mzuri wa nguvu kazi katika kuboresha miundombinu ya shule.


Mwisho.


Share:

Uchaguzi Uganda: Museveni ateua mwanajeshi kusimamia usalama


Rais wa Uganda,
Yoweri Kaguta Museveni, ameamua kumteua Brigedia Kayanja Muhanga, kusimamia masuala ya usalama wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu nchini humo unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 Januari 2021.
 

Uteuzi ho unampa nafasi Brig. Muhanga kuratibu vikosi vyote vya usalama nchini humo ambavyo vitasubiri sauti yake katika utekelezaji wa jambo lolote.

Luteni Deo Akiiki ambaye ni Naibu Msemaji wa Jeshi la Uganda amesema, Brig. Muhanga atakuwa mratibu wa operesheni za vitengo vyote ikiwa ni pamoja na vikosi vya polisi, jeshi na idara ya ujasusi na usalama.

‘Ni kweli kwamba, Brigedia Kayanja Muhanga amepewa nafasi ya kuratibu vikundi vyote vya usalama kwa madhumuni ya kuunganisha shughuli ya usalama wa pamoja hususan katika Mji wa Kampala na nchi yote,’ amenukuliwa Luten Akiiki.

Kuelekea uchaguzi mkuu nchini humo, Tarehe 17 Desemba 2020, Rais Museveni alimteuwa mwanaye Luteni Jenerali Muhoozi Kainerugaba kuwa mkuu wa kikosi cha ulinzi wa Rais (SFC).

Jenerali Muhoozi, ni mtoto wa kwanza wa rais huyo ambaye amekuwa madarakani kwa miongo minne sasa.

Kabla ya uteuzi huo, Jenerali Muhoozi, alikuwa mshauri wa baba yake – Rais Museveni – katika masuala ya ulinzi.



Share:

Trump apata pigo jingine Georgia.....Warnock kutoka chama cha Democratic ashinda katika uchaguzi muhimu wa maseneta


Mgombea wa wa chama cha Democratic Raphael Warnock ameibuka mshindi katika uchaguzi wa maseneta dhidi ya mgombea wa chama cha Republican Kelly Loeffler katika jimbo la Georgia, kulingana na vituo vya habari vya CNN, CBS na NBC leo Jumatano, Januari 6.

Raphael Warnock, mchungaji wa kanisa huko Atlanta ambapo Martin Luther King alifanya kazi, ataandika historia kwa kuwa seneta wa kwanza mweusi aliyechaguliwa katika jimbo hili la kusini.

Chama cha Democratic kinatarajia kushinda uchaguzi mwingine mdogo wa maseneta katika jimbo la Georgia kuchukua udhibiti wa Bunge la Seneti

Hili ni suala kubwa kwa utawala wa Joe Biden, ambaye atakabidhiwa madaraka Januari 20.

Donald Trump alikuja kuwaunga mkono maseneta wawili kutoka chama cha Republican wanaomaliza muda wao ambao wanawania nafasi zao katika Bunge la Seneti Jumanne hii, Januari 5.

Donald Trump anaendelea na msimamo wake wa kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi mpinzani wake kutoka chama cha Democratic, Joe Biden.


Hata hivyo, matokeo ya kura yalihesabiwa mara kadhaa huko Georgia na ni wazi: Joe Biden ndiye ambaye alishinda uchaguzi wa urais na ndiye ambaye alishinda katika jimbo hili kwa kura 12,000 dhidi ya Donald Trump.



Share:

TSC YAAINISHA MAKOSA SUGU YA WALIMU NCHINI


Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Moses Chitama, akiwasilisha mada kuhusu maadili katika mkutano wa pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara , uliofanyika jijini Dodoma, Januari 5, 2021.
Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), anayesimamia Elimu ya Awali na Msingi, Susan Nussu, akisisitiza kuhusu maadili ya walimu, wakati wa mkutano wa pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara (hawapo pichani), uliofanyika jijini Dodoma, Januari 5, 2021.
Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano wa Pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara (hawapo pichani), wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma, Januari 5, 2021. 

*********************** 

Na Veronica Simba 

Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania (TSC), Moses Chitama ametaja makosa sugu yanayofanywa na baadhi ya walimu nchini kuwa ni utoro, ulevi pamoja na kujihusisha kimapenzi na wanafunzi. 

Aliyasema hayo Januari 5 mwaka huu, wakati akiwasilisha mada kuhusu maadili, katika Mkutano wa Pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara, uliofanyika jijini Dodoma. 

Chitama alifafanua kuwa, TSC ikiwa ni Mamlaka ya Nidhamu kwa Walimu nchini, imebaini kuwa makosa hayo matatu ndiyo yanaongoza kuripotiwa kwa sasa, miongoni mwa makosa kadhaa yanayohusiana na utovu wa nidhamu katika kada husika. 

Aliendelea kueleza zaidi kuwa, kwa kulitambua hilo, Tume imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali katika kuhakikisha suala hilo linatokomezwa ikiwemo kutoa elimu kwa wahusika na kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa wanaothibitika kutenda makosa hayo. 

Aidha, Kaimu Katibu Chitama alitumia jukwaa hilo kukemea vikali walimu wenye tabia hiyo na kuwataka kuacha mara moja huku akisisitiza kuwa Serikali kupitia Tume husika, haitawavumilia. 

Alisema kuwa walimu ndiyo chanzo kikuu cha maendeleo ya nchi kwani ndiyo wamepewa dhamana ya kuwalea kiakili na kimwili watoto, ambao wanategemewa na Taifa kuja kuwa viongozi na wataalamu katika nyanja mbalimbali, hivyo wanapaswa kutimiza wajibu wao ipasavyo. 

“Ninyi walimu msiposimamia maadili ya taaluma yenu pamoja na maadili ya watoto mnaowafundisha, tutakuwa na Taifa bovu, lililokosa mwelekeo na lenye mmomonyoko wa maadili. 

Akitoa takwimu, Chitama alibainisha kuwa, katika kipindi cha miaka mitano (2016 – 2020), jumla ya walimu 9,819 walifunguliwa mashauri na waajiri wao, ambapo 5,441 kati yao walifukuzwa kazi. 

Aidha, alieleza kuwa, katika kipindi hicho, walimu 1,803 walipewa maonyo na makaripio, 520 walipunguziwa mishahara, 244 walisimamishiwa nyongeza ya mishahara na 403 waliteremshwa vyeo. 

Kwa upande mwingine, alisema walimu 149 walilipwa fidia na wengine 438 kuachiwa huru. 

Akihitimisha, Kaimu Katibu Chitama aliwataka walimu kuwachukulia wanafunzi kama watoto wao wa kuzaa hivyo wawatendee sawa na wanavyotendea familia zao. 

Akizungumza katika Mkutano huo, Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), anayesimamia Elimu ya Awali na Msingi, Susan Nussu, aliwasisitiza walimu kujiepusha na masuala ya udanganyifu wa mitihani katika shule zao. 

Alisema wengi hutenda kosa hilo kwa tamaa ya kujitafutia sifa ya ufaulu katika shule zao lakini akawataka kukumbuka kuwa kitendo hicho huwaponza wanafunzi wao kwa kuwasababishia kufutiwa matokeo. 

Aidha, aliwataka Walimu Wakuu wa Shule za Msingi kuacha tabia ya kuwapanga walimu wazembe na wavivu kufundisha madarasa ya awali badala yake wawapange walimu wenye weledi ili waweze kuwajengea watoto msingi mzuri wa elimu. 

Mkutano huo wa Pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania, uliongozwa na kaulimbiu isemayo uongozi na usimamizi makini wa elimu, utaimarisha Tanzania katika uchumi wa kati.
Share:

RAIS YOWERI MUSEVENI AMTEUA MWANAJESHI KURATIBU MASUALA YA USALAMA UGANDA


Rais Yoweri Museveni wa Uganda amemteua meja generali Kayanja Muhanga kuwa mratibu wa masuala ya usalama nchini Uganda.

Naibu msemaji wa jeshi luteni kanali Deo Akiiki ameambia BBC kwamba meja jenerali Muhanga atakuwa mratibu wa operesheni za vitengo vyote vya usalama.

‘Ni kweli kwamba Brigedia Kayanja Muhanga amepewa nafasi ya kuratibu vikundi vyote vya usalama kwa madhumuni ya kuunganisha shughuli ya usalama wa pamoja hususan katika mji wa Kampala na nchi yote’ .

"Hiyo ina maana kwamba atakuwa kiunganishi kati ya kikosi cha polisi , jeshi na idara ya ujasusi , alithibitisha luteni huyo.

CHANZO - BBC SWAHILI
Share:

Waziri Simbachawene Akabidhi Cheti Na Shilingi Milioni Moja Kwa Askari Wa Jeshi La Zimamoto Na Uokoaji


 Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (Wakwanza kushoto) akimkabidhi Cheti cha Kutambua Ujasiri na Utendaji Kazi Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Koplo Denis Minja, aliyeokoa maisha ya mtoto wa miaka miwili aliyekuwa ametumbukia kwenye shimo la choo Mjini Karagwe. Tukio hilo limefanyika leo katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo Mtumba, Jijini Dodoma. 


Share:

Waziri Mhagama: Majeruhiwa Ajali Ya Treni Waruhusiwa Wote


MWANDISHI WETU
Majeruhi 66 waliopata ajali ya treni iliyotokea mwishoni mwa wiki (Januari 2, 2021) wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa kutoka hospitali kutokana na  hali zao kuimarika mara baada ya kupatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe Jenista Mhagama ametembelea Januari 4, 2021 na kuwajulia hali majeruhi hao waliokuwa wakipatiwa matibabu katika hospitali hiyo ambapo hadi sasa wameruhusiwa wajeruhi wote.

Waziri alionesha kufurahishwa na huduma zilizotolewa kwa majeruhi hao na kupongeza jitihada zilizofanyika katika kuokoa maisha yao.

Alielezea kuwa, Serikali imefanya Uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya,na hivyo kuwezesha kutoa huduma kwa namna bora na weledi wenye  kwendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Akiwa wodini hapo waziri alipata fursa ya kuzungumza na majeruhi na kuwaeleza adhima ya Serikali ni kuona inaendelea kuratibu na kuboresha miundombinu muhimu ikiwemo ya barabara na afya ili pindi zinapotokea ajali kama hizo kuona jamii haipatwi na madhara makubwa kutokana na uwepo wa miundombinu rafiki inayosaidia kuondokana na madhara ya majanga.

“Kipekee ninawapa pole wale wote waliopatwa na ajali hii  iliyosababisha vifo na majeraha kwa wengine. Serikali imeguswa na ajali hili na tuwaaahidi tupo pamoja na tutaendelea kuhakikisha huduma zetu zinatolewa kwa ubora na wakati,” alisema Waziri

Waziri alieleza kuwa, Serikali kupitia Idara ya Uratibu wa Maafa itaendelea kuweka mikakati thabiti katika kuhakikisha inakuwa na mipango madhubuti ili kuyakabili majanga mbalimbali pindi yanapotokea katika kuokoa maisha ya wananchi na mali zao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe, Gerald Maganga alimshukuru Waziri kwa ziara hiyo na kupongeza shirika la Reli kwa namna walivyosaidia katika kuhakikisha walionusurika wanaendelea na safari zao.

“Niwapongeze watendaji wa shirika la Reli walivyoshiriki kwa kuhakikisha kunakuwa na mabasi yanayotoa huduma kwa abiria walionusurika na ajali hii kwa kupatiwa usafiri na kuendelea na safari zao bila usumbufu wowote,”alisema Bw. Maganga

Naye mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo Bw. Stephano Kasole alieleza furaha yake kuhusu huduma bora zilizotolewa na hospitali hiyo na kuipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu muhimu katika sekta ya afya.

“Tumepokelewa vizuri na kupatiwa huduma kwa wakati, hii imechangia kupata nafuu mapema sana, na leo nimefarijika kwa kuwa nimeruhusiwa kutoka,”alisema Kasole

AWALI

Treni ya abiria ilipata ajali tarehe 02 Januari, 2021 ilikuwa imebeba abiria 720 iliyokuwa safarini kutoka Jijini Dar es Salaam ikielekea maeneo ya Tabora, Katavi (Mpanda), Kigoma na Mwanza ilipata ajali kutokana na mvua zilizonyesha na kusababisha uharibifu wa miundombinu na kupelekea kusobwa kwa tuta la njia ya reli.Ajali ilisababisha vifo vya watu watatu na majeruhi 66.


Share:

Njombe:Watu wanne watiwa nguvuni kwa tuhuma za wizi wa nyaya za umeme


Na Amiri Kilagalila, Njombe
WAKATI Serikali ikielekeza nguvu kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na nishati ya umeme, mkoani Njombe watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika wilaya ya kipolisi mjini Makambako kwa tuhuma za kukutwa na nyaya za umeme zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 43 zinazotumika kusambazia umeme wa mradi wa REA.

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema hatua hiyo imekuja baada ya jeshi la polisi kufanya upelelezi wa kuwanasa watuhumiwa hao, kufuatia aliyekuwa msimamizi wa mradi wa Rea katika kata ya Kichiwa Tarafa ya Makambako kutoa taarifa kwenye jeshi hilo alipogundua dram sita za nyaya za umeme zenye thamani ya shilingi zaidi ya milioni 43 kuibwa .

“Tumekamata gari aina ya fuso na imebeba waya Rol zipatazo sita na hizi rol zipo nyaya za aina mbili tofauti zinazotumika kwenye umeme wa rea hapa mkoani Njombe”alisema Hamis Issa

Kamanda Issa amesema wamefanikiwa kukamata gari hilo kutokana na ufuatiliaji uliofanywa na vikosi vya polisi.

“Tuliweza kubaini kutokana na nyaraka iliyodondoka ya faini iliyotozwa hii gari,ikajulikana iko Dar Es Salaam,amefuatwa tajiri akasema gari iko Katavi na tulipofuatilia tuliikuta Mlele sehemu moja inatwa maji moto”alisema Kamanda Issa.

Vile vile ametoa rai kwa wananchi kuendelea kuliamini jeshi hilo kwa kuwa lipo imara na watahakikisha jeshi linalinda miradi yote ya serikali hivyo wananchi wawe tayari kutoa taarifa miradi inapohujumiwa.


Share:

Waziri Aweso Amuagiza Katibu Mkuu Wizara Ya Maji Kutengua Uteuzi Wa Meneja Wa Ruwasa Mkoa Wa Mara


WAZIRI wa Maji, Mhe.  Jumaa Aweso (Mb) amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga kutengua uteuzi wa Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara, Mhandisi Sadick Chakka na mwenzake wa Wilaya ya Tarime Mhandisi Marwa Murasa kwa kushindwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maji.

Maelekezo hayo yametolewa Wilayani Tarime  tarehe 5 Januari, 2021 alipokuwa kwenye mradi wa maji wa Magoto ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Mara.  

Awali akipokea taarifa ya miradi, Ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Waziri Aweso alisisitiza kwamba taarifa haina uhalisia na aliwaelekeza wataalam hao kueleza halihalisi ya miradi na sio kudanganya.

Akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa taarifa, Mbunge wa Tarime Vijijini na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Mwita Waitara (Mb) ambaye aliambatana na Waziri Aweso alimueleza kuhusu  adha ya huduma ya maji kwa wananchi wa Tarime.

Mhe. Mwita alisema kwamba miradi mingi ya maji Wilayani Tarime inachangamoto na hivyo alimuomba Waziri Aweso kuchukua hatua stahiki kwa wote wanaohusika kuchelewesha utekelezwaji wa miradi

Taarifa ya miradi sambamba na maelezo ya Naibu Waziri Mwita na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri kuhusu hali halisi ya miradi ya maji wilayani humo ilimsukuma Waziri Aweso  kutofuata ratiba ya kukagua miradi iliyokuwa imepangwa na wataalam hao na badala yake alielekeza kupelekwa kwenye miradi mingine yenye changamoto ambayo haikuwepo kwenye ratiba.

"Nimepitia taarifa ya wataalam wetu hapa na hii ratiba waliyopanga sikubaliani nayo, sasa nataka mnipeleke kwenye miradi mingine na siyo hii mliojipangia nyinyi ili tu kunifurahisha,” Waziri Aweso aliwaelekeza wataalam hao.

Waziri Aweso aliijadili taarifa hiyo ya utekelezwaji wa miradi Wilayani Tarime na huku akimtaka Meneja huyo wa Mkoa kueleza hali ya mradi mmoja baada ya mwingine na huku akibainisha kiasi cha fedha kilichopo kwenye akaunti ambacho kilipaswa kuwa kimetumika kutekeleza miradi.

“Bora hata kisingizio ingekua fedha kama ambavyo hua mnadanganya lakini sasa hapa Mkoani Mara tumeleta zaidi ya shilingi bilioni nane na fedha iliyopo kwenye akaunti kwa sasa ni zaidi ya shilingi bilioni 3 hivi ni nani atakuelewa watu hawana maji wewe kwenye akaunti unayo fedha ya kutosha,”  Waziri Aweso alihoji.

Alisema lengo la kuanzisha RUWASA ni kuhakikisha wananchi wanapata maji na kwamba maelekezo ya awali ni kwamba kabla utekelezwaji wa miradi haujaanza kila Meneja wa RUWASA Mkoa alipaswa kuwasilisha taarifa ya kuainisha miradi kichefuchefu yaani miradi iliyokuwa ni kero kwa wananchi lakini RUWASA Mkoa wa Mara haikufanya hivyo.

“Wananchi wanachohitaji ni maji bombani, hatutokubali kumuona Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli akiumia na kusononeka kuona wananchi wake wanateseka hawana maji na sisi tupo, hii haipendezi hata mbele za Mungu, tumemuahidi kufanya kazi na sasa tunahakikisha wananchi wanapata huduma ya uhakika ya majisafi na salama,” alisema Waziri Aweso.

Aliongeza kuwa taarifa ya hali ya miradi wilayani humo inasikitisha kwani tathmini aliyoifanya inaonyesha miradi mingi imekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 lakini haitoi maji na hivyo aliwataka wataalam kote nchini kutumia vyema utaalamu wao badala ya kujiamulia kujenga miradi kiholela.

“Haiwezekani mradi upo asilimia 98 na hautoi maji, unawezaje kujenga tenki hali yakuwa huna uhakika kama maji yapo? Ulipaswa kujiridhisha na chanzo chako kwanza ili kuhakikisha maji yapo yakutosha na hatua zingine zinafuata,” Waziri Aweso alisisitiza.

Baada ya mahojiano ya muda mrefu na Mameneja hao kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Waziri Aweso alielekeza msafara alioambatana nao kutembelea mradi wa maji wa Magoto ili kujionea hali halisi ya utekelezwaji wake.

Aidha, mara baada ya kutembelea mradi huo na kujionea hali halisi sambamba na kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo, Waziri Aweso alijiridhisha pasi na shaka kwamba mradi huo haujatekelezwa kama inavyopasa.

Hali hiyo kwa ujumla na taarifa iliyowasilishwa kwake hapo awali pamoja na maelezo ya viongozi na wananchi wa Kata ya Nyakonga ilipelekea Waziri Aweso kumuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutengua uteuzi wa Mameneja hao na alimtaka kufika Mkoani Mara ili kujionea hali ya miradi sambamba na kuunda kamati itakayochunguza miradi kichefuchefu yote mkoani humo.

“Namuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutengua uteuzi wa Mameneja hawa mara moja na wapewe wengine watakaomudu majukumu haya ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya uhakika na toshelevu,” alielekeza Waziri Aweso.

Alisema miradi mingi Mkoani Mara hairidhishi na hivyo ni muhimu Katibu Mkuu akaitupia jicho RUWASA hususan watendaji wake na kwamba wasiokuwa na uwezo waondolewe na alisisitiza kwamba ni muhimu kujiridhisha uwezo wa wataalam kabla ya kuwapanga.

Waziri Aweso vilevile alielekeza miradi yote ya maji iwe shirikishi, viongozi na wananchi wa maeneo husika wawe na uelewe wa pamoja wa kinachoendelea ili kuepuka kucheleweshwa ujenzi wake.

Waziri Aweso yupo Mkoani Mara kwa ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maji hususan inayotekelezwa maeneo ya vijijini.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger