Wednesday, 6 January 2021

Waziri Aweso Amuagiza Katibu Mkuu Wizara Ya Maji Kutengua Uteuzi Wa Meneja Wa Ruwasa Mkoa Wa Mara


WAZIRI wa Maji, Mhe.  Jumaa Aweso (Mb) amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga kutengua uteuzi wa Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara, Mhandisi Sadick Chakka na mwenzake wa Wilaya ya Tarime Mhandisi Marwa Murasa kwa kushindwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maji.

Maelekezo hayo yametolewa Wilayani Tarime  tarehe 5 Januari, 2021 alipokuwa kwenye mradi wa maji wa Magoto ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Mara.  

Awali akipokea taarifa ya miradi, Ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Waziri Aweso alisisitiza kwamba taarifa haina uhalisia na aliwaelekeza wataalam hao kueleza halihalisi ya miradi na sio kudanganya.

Akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa taarifa, Mbunge wa Tarime Vijijini na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Mwita Waitara (Mb) ambaye aliambatana na Waziri Aweso alimueleza kuhusu  adha ya huduma ya maji kwa wananchi wa Tarime.

Mhe. Mwita alisema kwamba miradi mingi ya maji Wilayani Tarime inachangamoto na hivyo alimuomba Waziri Aweso kuchukua hatua stahiki kwa wote wanaohusika kuchelewesha utekelezwaji wa miradi

Taarifa ya miradi sambamba na maelezo ya Naibu Waziri Mwita na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri kuhusu hali halisi ya miradi ya maji wilayani humo ilimsukuma Waziri Aweso  kutofuata ratiba ya kukagua miradi iliyokuwa imepangwa na wataalam hao na badala yake alielekeza kupelekwa kwenye miradi mingine yenye changamoto ambayo haikuwepo kwenye ratiba.

"Nimepitia taarifa ya wataalam wetu hapa na hii ratiba waliyopanga sikubaliani nayo, sasa nataka mnipeleke kwenye miradi mingine na siyo hii mliojipangia nyinyi ili tu kunifurahisha,” Waziri Aweso aliwaelekeza wataalam hao.

Waziri Aweso aliijadili taarifa hiyo ya utekelezwaji wa miradi Wilayani Tarime na huku akimtaka Meneja huyo wa Mkoa kueleza hali ya mradi mmoja baada ya mwingine na huku akibainisha kiasi cha fedha kilichopo kwenye akaunti ambacho kilipaswa kuwa kimetumika kutekeleza miradi.

“Bora hata kisingizio ingekua fedha kama ambavyo hua mnadanganya lakini sasa hapa Mkoani Mara tumeleta zaidi ya shilingi bilioni nane na fedha iliyopo kwenye akaunti kwa sasa ni zaidi ya shilingi bilioni 3 hivi ni nani atakuelewa watu hawana maji wewe kwenye akaunti unayo fedha ya kutosha,”  Waziri Aweso alihoji.

Alisema lengo la kuanzisha RUWASA ni kuhakikisha wananchi wanapata maji na kwamba maelekezo ya awali ni kwamba kabla utekelezwaji wa miradi haujaanza kila Meneja wa RUWASA Mkoa alipaswa kuwasilisha taarifa ya kuainisha miradi kichefuchefu yaani miradi iliyokuwa ni kero kwa wananchi lakini RUWASA Mkoa wa Mara haikufanya hivyo.

“Wananchi wanachohitaji ni maji bombani, hatutokubali kumuona Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli akiumia na kusononeka kuona wananchi wake wanateseka hawana maji na sisi tupo, hii haipendezi hata mbele za Mungu, tumemuahidi kufanya kazi na sasa tunahakikisha wananchi wanapata huduma ya uhakika ya majisafi na salama,” alisema Waziri Aweso.

Aliongeza kuwa taarifa ya hali ya miradi wilayani humo inasikitisha kwani tathmini aliyoifanya inaonyesha miradi mingi imekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 lakini haitoi maji na hivyo aliwataka wataalam kote nchini kutumia vyema utaalamu wao badala ya kujiamulia kujenga miradi kiholela.

“Haiwezekani mradi upo asilimia 98 na hautoi maji, unawezaje kujenga tenki hali yakuwa huna uhakika kama maji yapo? Ulipaswa kujiridhisha na chanzo chako kwanza ili kuhakikisha maji yapo yakutosha na hatua zingine zinafuata,” Waziri Aweso alisisitiza.

Baada ya mahojiano ya muda mrefu na Mameneja hao kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Waziri Aweso alielekeza msafara alioambatana nao kutembelea mradi wa maji wa Magoto ili kujionea hali halisi ya utekelezwaji wake.

Aidha, mara baada ya kutembelea mradi huo na kujionea hali halisi sambamba na kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo, Waziri Aweso alijiridhisha pasi na shaka kwamba mradi huo haujatekelezwa kama inavyopasa.

Hali hiyo kwa ujumla na taarifa iliyowasilishwa kwake hapo awali pamoja na maelezo ya viongozi na wananchi wa Kata ya Nyakonga ilipelekea Waziri Aweso kumuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutengua uteuzi wa Mameneja hao na alimtaka kufika Mkoani Mara ili kujionea hali ya miradi sambamba na kuunda kamati itakayochunguza miradi kichefuchefu yote mkoani humo.

“Namuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutengua uteuzi wa Mameneja hawa mara moja na wapewe wengine watakaomudu majukumu haya ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya uhakika na toshelevu,” alielekeza Waziri Aweso.

Alisema miradi mingi Mkoani Mara hairidhishi na hivyo ni muhimu Katibu Mkuu akaitupia jicho RUWASA hususan watendaji wake na kwamba wasiokuwa na uwezo waondolewe na alisisitiza kwamba ni muhimu kujiridhisha uwezo wa wataalam kabla ya kuwapanga.

Waziri Aweso vilevile alielekeza miradi yote ya maji iwe shirikishi, viongozi na wananchi wa maeneo husika wawe na uelewe wa pamoja wa kinachoendelea ili kuepuka kucheleweshwa ujenzi wake.

Waziri Aweso yupo Mkoani Mara kwa ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maji hususan inayotekelezwa maeneo ya vijijini.


Share:

Dkt. Ndugulile Awataka Wafanyakazi Wa Wizara Kuacha Kufanya Kazi Kwa Mazoea


 Na Prisca Ulomi, WMTH
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amewataka wafanyakazi wa Wizara yake kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye kazi kwa ubunifu, kujituma, watumie TEHAMA kutatua changamoto za wananchi, wahakikishe TEHAMA inachangia kikamilifu pato la taifa kwa kuwa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ni barabara ya dunia ya sasa ya kidijitali

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo wakati wa kikao chake na wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika Dodoma na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi na wajumbe wa Menejimenti ya Wizara hiyo mpya

Amewataka wafanyakazi hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na yeye sio muumini wa michakato bali anahitaji kuona matokeo ili kuhakikisha kuwa TEHAMA inatumika kujibu changamato za wananchi ili mwananchi apate huduma za Serikali mahali popote alipo badala ya kufuata watendaji walipo

“Nataka kuona bwana shamba anatumia mawasiliano kupata mbegu, pembejeo na wakulima watumie TEHAMA kupata masoko, waalimu tulionao watumie TEHAMA kufundishia wanafunzi kwa kuwa Wizara hii ina dhamana na masuala ya TEHAMA, ndiyo yenye sera ya TEHAMA, inatoa miongozo, sheria, kanuni na viwango kwa taasisi zote za Serikali, sekta binafsi na wananchi”, amesisitiza Dkt. Ndugulile

Amefafanua kuwa sasa hivi Serikali inatumia fedha nyingi kununua mifumo ya TEHAMA nje ya nchi, hivyo anataka wabunifu wa TEHAMA wazuri waliopo nchini watumike kutengeneza mitandao yetu ya kijamii na mifumo yetu ya TEHAMA ambayo ina jibu changamoto za wananchi ili Tanzania tuwe na mitandao yetu na mifumo yetu ya TEHAMA ili kuongeza pato la Taifa

Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kikao hicho kitawawezesha wafanyakazi kuwa na dira na mwelekeo wa pamoja katika kutekeleza majukumju ya Wizara mpya na Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi amemshukuru Waziri kwa kikao hicho na kuongeza ari kwa wafanyakazi kutumikia wananchi

Naye Mwenyekiti wa TUGHE wa Wizara hiyo, Laurencia Masigo amemweleza Dkt. Ndugulile kuwa wafanyakazi wako tayari kufanya kazi kwa ushirikiano, kujituma na kushirikiana na Menejimenti na kushauri yapi yafanyike katika nyanja ya TEHAMA ili kukuza uchumi wa taifa letu

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari


Share:

Wimbo Mpya : NTEMI OMABALA 'NG'WANA KANG'WA' - NDAGU


Msanii maarufu wa Nyimbo za asili Ntemi Omabala 'Ng'wana Kang'wa' kutoka Kahama Mkoani Shinyanga ameachia wimbo mpya 2021 unaitwa Ndagu. Usikilize hapa 

Share:

MKE AJIUA KISA MUME WAKE KATOKA JELA


Jesca Samson (37) mkazi wa mtaa wa Katoma, Kayanga wilayani Karagwe anadaiwa kujiua kwa kunywa sumu ya panya baada ya kusikia mume wake aliyefungwa kutokana na ugomvi wao ameachiwa kutoka jela.

Mwanamke huyo, kabla ya kifo chake anadaiwa pia alimnywesha sumu hiyo mtoto wake, Jordan Samson (3), ambaye hata hivyo alinusurika kifo.

Kamanda wa Polisi wa Mkao wa Kagera, Revocatus Malimi alisema tukio hilo lilitokea Januari Mosi saa 8:00 usiku baada ya mama huyo kutoka katika mkesha wa Mwaka Mpya 2021.

Jesca, akiwa na ndugu zake, wakitoka kwenye mkesha, alipata taarifa kuwa mume wake ameachiwa huru na baada ya kusikia hivyo, aliwaacha njiani aliokuwa nao na kuwahi nyumbani kisha akanywa sumu hiyo.

Kamanda Malimi alisema baada ya ndugu zake kufika nyumbani, Jesca aliwaambia kuwa amekunywa sumu ya panya, ndipo walimpeleka hospitali ya Wilaya Nyakahanga pamoja na mtoto wake, na mwanamke huyo alifariki dunia Januari 2, huku mtoto wake akipona.

Mumewe ambaye hakutajwa jina, alikuwa amefungwa kifungo cha miezi mitatu jela kutokana na mgogoro wa kifamilia.

“Mgogoro uliokuwapo kati yake na mumewe ulitokana na mwanaume huyo kuuza kipande cha ardhi bila kumshirikisha mkewe na mwanamke akamshtaki katika mahakama ya mwanzo. Mume alihukumiwa kwenda jela miezi mitatu,” alisema Malimi

Alisema baada ya kusikia mme wake ameachiwa kutoka gerezani Desemba 31, 2020 alijenga hofu na hivyo kuchukua hatua za kunywa sumu ya panya na kunywesha mtoto wake.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Nyakahanga kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 6,2021















Share:

Tuesday, 5 January 2021

WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUINGILIA KATI MRADI WA MAJI ULIOGHARIMU MIL.511 LAKINI WANANCHI HAWAPATI MAJI

Na Dinna Maningo,Tarime

WANANCHI wa Kata ya Nyakonga wamemuomba Rais John Magufuli kuingilia kati na kufika kushuhudia mradi wa lambo la maji uliogharimu zaidi ya milioni 511 uliojengwa na kampuni ya EDOS lakini zaidi ya miaka 10 wananchi hawapati maji.

Wakizungumza na Malunde 1 blog wananchi wamesema kuwa wanapata adha kubwa ya maji ambapo wakati wa kiangazi hununua ndoo moja kwa sh.300 lakini pia hata wagonjwa wanaopatiwa huduma ya afya katika kituo cha afya Magoto hupata shida ya maji na hivyo kulazimika kutoka na maji nyumbani kwao.

Maliam Nyeikobe mkazi wa kijiji cha Nyakonga ambaye pia ni mjumbe wa Serikali ya kijiji cha Nyakonga alisema kuwa Serikali ilitoa fedha kujenga Lambo la maji ili kumtua mama ndoo kichwani  lakini ni miaka kumi hawapati maji tangu lijengwe lambo hilo.

"Lambo lilijengwa kwa ajili ya kusambaza maji kwenye maeneo mbalimbali ya wananchi,kituo cha afya kinategemea maji ya kuvuna ya mvua yakikatika wananunua ndoo moja sh 300,ukienda kupata huduma kama kujifungua inabidi utoke na maji yako nyumbani ukafulie nguo", alisema Nyeikobe.

Elizabeth Ryoba alisema kuwa amechoka kufanya usafi na kulinda bomba kavu lisilotoa maji na kwamba wanateseka kupata huduma ya maji licha yakuwepo lambo la maji hivyo anaiomba Serikali kuwasaidia kupata maji kwakuwa walitoa maeneo yao kwa hiari kupitisha maji lakini hawajanufaika na mradi wa maji.

Joseph Gekobe alisema kuwa mradi wa Lambo ulianza kujengwa mwaka 2011 na kwamba sababu ya mabomba kutotoa maji ni kuwekwa kwa mipira ya kusambaza maji kutoka kwenye lambo la maji ambayo ni ya chini ya viwango.

"Mipira iloyowekwa ni miembamba sana na tanki la maji liko mlimani walipofungulia maji mipira ikashindwa kuhimiri kasi ya maji yote ikapasuka walifungulia siku moja ikapasuka yote maji yakashindwa kufika kwenye mabomba yaliyosambazwa kwa wananchi", alisema Gekobe.

Festo Gichonge alisema kuwa Lambo hilo lina maji lakini lipo kama pambo haruhusiwi mwananchi kuchota maji wala kunywesha mifugo na hivyo kuendelea kuteseka kutafuta maji kwenye visima vya asili.

Mnanka Robert alisema kuwa limejengwa chini ya kiwango na likakabidhiwa kinyemera kwenye kamati ya maji ya kijiji badala ya kukabidhi uongozi wa Serikali ya kijiji na wananchi

Getaro Gikaro ambaye pia ni mjumbe wa Serikali ya kijiji cha Nyakonga alisema kuwa baada ya mradi kukamilika ulipaswa kukabidhiwa kwa wananchi kwakuwa ni mradi wa wananchi ili nao waridhie kwakuwa umegharimu pesa nyingi za Serikali.

Zakaria Gikaro alisema kuwa wakati wa ujenzi Serikali ya kijiji haikushirikishwa katika hatua zote za ujenzi wa mradi zaidi tu ya kupewa taarifa ya ujenzi wa mradi.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mkuyuni Waitara Marwa kuliko lambo la maji alisema kuwa mipira ya kusambaza maji ilishindwa kuhimiri kasi ya maji yaliyokuwa yanatoka kwenye tenki kubwa la maji nakwamba wakati mradi unajengwa ilielezwa kuwa mradi huo utahudumia vijiji vinne.

Daud Chacha alisema : "jinsi lilivyochimbwa ni mbinu ya kujitengenezea fedha maana ni kwanini miradi mingine Serikali inafuatilia sana lakini huu mradi una zaidi ya miaka kumi hatupati maji lakini Serikali haijawahi kufatilia wala kuibana kampuni iliyojenga mradi na hata wakati wa kuchukua eneo la kujenga lambo wananchi walilipwa fidia kidogo ambao hawakuwa na maeneo wakalipwa fidia kubwa".

Mwenyekiti mstaafu Gabriel Matiko alisema kitendo cha kampuni kujenga mradi kwenye kijiji bila kushirikisha wananchi na uongozi wa Serikali ya kijiji ndiyo sababu ya miradi kujengwa chini ya viwango kwakuwa hakuna mtu wa kuwakagua au kuhoji.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Magoto Zabron Magabe alisema kuwa mradi huo ulikabidhiwa kwenye kamati ya maji ukiwa na mapungufu mengi.

"Hivi karibuni walifika watu wa maji wakasema wanakarabati Lambo cha hajabu wakatoa tope eneo dogo wakarundika udongo kandokando ya lambo bado tope zimo ndani tunaomba walete mabomba mapya waweke wasituwekee viraka",alisema Magabe.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyakonga John Ryoba alisema awali Lambo hilo lilikuwa linasimamiwa na idara ya maji halmashauri ya wilaya ya Tarime ambapo zaidi ya milioni 511 zilitumika na kwa sasa mradi huo unasimamiwa na Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) ambao nao unadaiwa  kutumia milioni 40 kati ya 75 kufanya ukarabati wa lambo.

"Hili lambo limejengwa chini ya kiwango mvua ikinyesha maji machafu yanatiririka kutoka mlimani yanaingia kwenye lambo,RUWASA walikuja wakasema wanakarabati lambo lakini walichokifanya ni kusafisha tu,hata kingo zilizowekwa kuzuia maji kupita zimepangwa tu mawe ambayo hayajachapiwa kwa saruji na pengine wametumia saruji kidogo kuta zinabomoka", alisema.

"Waziri mkuu Majaliwa katika Ziara yake Tarime wakati anapita Nyakonga wananchi walijiandaa kusimamisha msafara wake ili wamweleze kero zao wakiwa na mabango ya kumwonyesha kuhusu lambo la maji lakini tukazuiwa tumuoneshe mabango Waziri akapita wananchi tukanyimwa haki ya kueleza matatizo yao",alisema Ryoba.

Ryoba aliiomba Serikali kuingilia kati huku akimuomba Rais Magufuli kuwasaidia ili waweze kupata maji kwa kuwa mradi huo umetumia fedha nyingi za Serikali jambo ambalo wananchi wanashangaa kuona hatua hazichukuliwi kuhakikisha wanapata huduma ya maji.


Mwenyekiti wa kijiji cha Nyakonga akionyesha maji yanavyotiririka kuingia kwenye lambo la maji




















Share:

Jaji: Assange atajiua akihamishwa hadi Marekani


 Mahakama ya Uingereza imekataa ombi la Marekani la kumuhamisha mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks, Julian Assange hadi Marekani anapokabiliwa na mashtaka ya ujasusi.

Mahakama imeamua kuwa hatua ya kumuhamisha Assange, ni “Ukandamizaji” kutokana na Afya yake ya kiakili.

Jaji Vanessa Baraitser amesema Assange huenda akajiua iwapo atahamishwa hadi Marekani. Hata hivyo, serikali ya Marekani imesema itakata rufaa juu ya uamuzi huo.

Waendesha mashtaka wa Marekani wanamshtumu Assange kwa makosa 17 ya ujasusi na matumizi mabaya ya Kompyuta kwa kuchapisha mtandaoni nyaraka za siri juu ya oparesheni za jeshi la Marekani nchini Iraq na Afghanistan muongo uliopita.

Iwapo atapatikana na hatia, Assange huenda akapewa kifungo cha miaka 175 jela.


Share:

TCRA yaifungia Wasafi TV miezi sita kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekifungia kwa miezi sita kituo cha teloevisheni cha Wasafi kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji katika matangazo yake ya moja kwa moja ya tamasha la ‘Tumewasha na Tigo’.


 Uamuzi huo umefikiwa leo Jumanne Januari 5 baada mamlaka hiyo kukutana na uongozi wa Wasafi TV na kusikiliza utetezi wao.


Kaimu Mkurugenzi wa TCRA, Johanes Kalungule amesema ukiukwaji huo ulifanyika Januari 1, 2021 ambapo televisheni hiyo ilirusha maudhui yaliyomuonyesha msanii Gigy Money akicheza katika mitindo iliyoonyesha utupu wake.


Kalungule amesema kosa hilo ni kinyume na kanuni za utangazaji, hivyo kuanzia muda uliotolewa uamuzi huo Wasafi TV imetakiwa kusitisha matangazo yake na kuomba radhi mfululizo.



Share:

GIGGY MONEY AIPONZA WASAFI TV... YAFUNGIWA KURUSHA MATANGAZO MIEZI 6


Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

Mamlaka  ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeisitisha utoaji huduma za utangazaji kwa Televisheni ya Wasafi TV kwa muda wa miezi 6 kuanzia Januari 6 mwaka huu hadi Juni 2021 kwa makosa ya kukiuka taratibu za utangazaji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Johannes Kalungula, amesema maamuzi hayo yanakuja kufuatia kipindi cha "Tumewasha Concert," Wasafi Tv cha Januari Mosi, 2021 majira ya saa mbili hadi saa tano usiku iliyorusha maudhui ya picha jongefu yaliyomwonesha msanii wa bongo Fleva Gift Stanford Mwakyusa maarufu kama Giggy Money akicheza katika jukwaa kwa mitindo iliyokuwa ikionesha utupu wa mwili wake kinyume na kanuni namba 11 (1) (b) (c) na (d) za kanuni za Mawasiliano ya kielektroniki na Posta (Maudhui ya utangazaji wa Redio na Televisheni,) ya mwaka 2018 inayomtaka mtoa huduma wa maudhui kuhakikisha kuwa hatangazi maudhui yasiyozingatia utu na maadili ya Jamii.

Aidha Wasafi TV wametakiwa kutumia siku ya leo iliyobaki kuahirisha matangazo yote na kutumia muda wote uliobaki siku ya leo kuomba radhi kwa Umma wa watanzania wake kufuatia ukiukaji wa kanuni za utangazaji kupitia kipindi cha "Tumewasha Live Concert." Na wakikaidi au kukataa hatua zaidi za kisheria na udhibiti zitachukuliwa dhidi ya Wasafi TV.
Share:

MAYALA : WAFUGAJI WA KUKU MJIKITE ZAIDI KATIKA KUMKINGA KUKU DHIDI YA MAGONJWA BADALA YA TIBA

Mtaalamu wa Magonjwa ya Kuku kutoka Silver Land Tanzania Bw. Daudi Mayala
Na Josephine Charles - Shinyanga
Rai imetolewa kwa wafugaji wa kuku kujikita zaidi katika kumkinga kuku dhidi ya magonjwa na siyo tiba.

Rai hiyo imetolewa na Mtaalamu wa Magonjwa ya kuku kutoka Silver Land Tanzania Bw. Daudi Mayala wakati akizungumza Katika Kipindi cha Mambo Leo kinachorushwa na Radio Faraja fm stereo kila Juma tatu hadi Ijumaa saa tatu asubuhi hadi saa saba kamili mchana. 

Amesema wafugaji wengi wa kuku hawana tabia ya kumkinga kuku dhidi ya magonjwa badala yake wan kuwa wa kwanza kumwambukiza kuku magonjwa pasipo wao kujua kwa kutokuzingatia mavazi na usafi wakati wa kuingia kwenye vibanda vya kuku hivyo hujikuta wamewapelekea kuku virusi vinavyosababisha ugonjwa kwa kuku na ndipo huanza kuhangaika kutafuta dawa za kutibu ule ugonjwa matokeo yake huchelewa na kusababisha kuku kufa. 

Ameyataja baadhi ya magonjwa ambayo huwapata kuku mara kwa mara kuwa ni Kideri,Gumboro,Ndui,Koraiza,Typhoid,TB na ugonjwa wa mfumo wa upumuaji ambapo baadhi ya hayo magonjwa mengine huwapata kuku kwa njia ya Virusi na Bakteria.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger