Tuesday, 9 June 2020
MOTISHA YA MBUNGE ILIVYOCHOCHEA UFAULU SEKONDARI ZA MADABA
Ugonjwa Wa Corona Unaelekea Kuisha Nchini-Waziri Ummy
BREAKING NEWS: Rais wa Burundi aliyemaliza muda wake, Pierre Nkurunziza afariki dunia.
Serikali ya Burundi imetangaza hayo leo kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.
Ujumbe kwenye ukurasa huo umeeleza kuwa serikali ya Burundi inatangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha Rais Nkurunziza na kuongeza kuwa amefariki kutokana na tatizo la moyo.
Nkurunziza alizaliwa Desemba 18, 1963, ambapo alikuwa Mwenyekiti wa chama tawala cha CNDD-FDD, hadi alipochaguliwa kama Rais wa Burundi mwaka 2005.
Breaking : RAIS WA BURUNDI PIERRE NKURUNZIZA AFARIKI DUNIA

Freeman Mbowe Ahamishiwa Dar Es Salaam Kwa Ajili Ya Matibabu Zaidi
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Amjulia Hali Freeman Mbowe
HALMASHAURI YAPEWA JUKUMU UKAMILISHAJI MIRADI MAENDELEO
Hayo yamebainishwa leo Juni 9, 2020 kwenye Baraza maalumu la madiwani wa manispaa hiyo ambalo ni la mwisho, kuwa kuna miradi mingi ya maendeleo ambayo ilianzishwa kipindi cha utawala wa madiwani hao tangu mwaka 2015, ambayo mingine bado haijamalizika kujengwa.
Baadhi ya Madiwani hao akiwemo David Nkulila wa Ndembezi, walisema ndani ya utawala wao wa miaka mitano, kuna miradi mingi ya maendeleo ambayo wameianzisha, ikiwamo ya ujenzi wa maboma ya zahanati, madarasa, mabweni, vyoo vya shule, bararaba, machinjio, dampo, ambapo mengine haijakamilika.
“Sisi madiwani tunamaliza muda wetu wa kutumikia wananchi katika manispaa hii ya Shinyanga, lakini kuna miradi ya maendeleo ambayo tuliianzisha ndani ya utawala wetu wa miaka mitano tangu 2015, ambapo mingine haijakamilika kujengwa, hivyo jukumu hili tunaliacha kwa menejimenti ya manispaa kuikamilisha,” walisema madiwani kwa nyakati tofauti
Naye Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, alisisitiza uongozi huo wa manispaa ya Shinyanga, wazungukie miradi yote ya maendeleo iliyotekelezwa na kuibaini ile ambayo haijakamilika, ili wapate kutengewa fedha kupitia makusanyo ya ndani na kuikamilisha haraka.
Katika hatua nyingine Mboneko aliwataka madiwani watakaorudi kugombea, wakafanye siasa za kistaarabu, ikiwa Serikali imejipanga vyema kuhakikisha uchaguzi huo mkuu utafanyika kwa amani na utulivu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Geofrey Magulumbi, alisema maelekezo yote yaliyotolewa watayafanyia kazi, kwa ajili ya mustakabali wa maendeleo ya manispaa hiyo.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza kwenye baraza la madiwani wa Manispaa ya Shinyanga. Picha zote na Marco Maduhu
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Stephen Masele, akizungumza kwenye baraza hilo.
Mstahiki Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Mkadam akizungumza kwenye kikao cha baraza hilo.
Naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga John Peter Kisandu, akizungumza kwenye kikao cha baraza hilo la madiwani.
Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi, akizungumza kwenye baraza hilo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa.
Madiwani wa manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye baraza lao la mwisho.
Diwani wa vitimaalum Mariam Nyangaka, akizungumza kwenye baraza hilo.
Diwani wa Ngokolo Emmanuel Ntobi, akizungumza kwenye baraza hilo.
Diwani wa Ndembezi David Nkulila, akizungumza kwenye baraza hilo.
Diwani wa Ndala, Wiliamu Shayo akizungumza kwenye baraza.
Watendaji wa kata manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye baraza la madiwani wakifuatilia baraza hilo.
Watendaji wa manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye baraza la madiwani wakifuatilia baraza hilo.
Picha zote na Marco Maduhu
DC MBOGWE AWASHUKIA WATENDAJI WANAOKWAMISHA MAENDELEO YA WANANCHI

Mkuu wa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita, Martha Mkupasi aliyeongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kujionea utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa matundu vyoo 18 katika shule ya msingi kanegere iliyopo Kata ya Bukandwe.


Wananchi wa Kata ya Bukandwe wakijitolea nguvu zao katika kushiriki ujenzi wa vyoo hivyo ili kukabiliana na uhaba uliopo katika shule hiyo ambayo ni miongoni mwa shule saba inayonufaika na mradi wa Milioni 175 kutoka serikali kuu huku shule hiyo ikitengewa shilingi Milioni 27.9 kwaajili ya utekelezaji wa mradi huo wa vyoo vya kisasa, na vyoo vinavyoonekana ni vya zamani.










Developer Internship Opportunities- Internship program at Smart Lab Tanzania
Developer Interns- Internship program at Smart Lab Tanzania Smart Lab is an innovation platform that links learning institutions with corporate partners to empower groundbreaking solutions that will impact African communities. Are you a fresh graduate with a degree in computer science/engineering, aspiring to become a great developer? Smart Lab is looking for you, join a diverse team of… Read More »
The post Developer Internship Opportunities- Internship program at Smart Lab Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
PICHA: Spika Ndugai Awasili Hospitali Kumjulia Hali Freeman Mbowe
Billing Administrator: Postpaid Billing Job vacancy at Vodacom Tanzania
Billing Administrator: Postpaid Billing Job vacancy at Vodacom Tanzania Posting Country: Tanzania, United Republic of Date Posted: 08-Jun-2020 Full Time / Part Time: Full Time Contract Type: Permanent Joining Vodacom is more than a job, what we do matters. We don’t just carry minutes, texts and data – we carry people’s lives. And that’s a huge responsibility. If… Read More »
The post Billing Administrator: Postpaid Billing Job vacancy at Vodacom Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Head Of Marketing at DKT Tanzania Dar es Salaam, Tanzania
Position description The Head of Marketing will be in charge of all DKT Tanzania Marketing activities incorporating all product lines. He/she will be responsible for developing the marketing strategy with his/her team to ensure targets are met and surpassed via a winning strategy that creates even greater health impact. The primary purpose of the position is to accelerate… Read More »
The post Head Of Marketing at DKT Tanzania Dar es Salaam, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Program Support Specialist – Health (Arusha City) at Compassion International Arusha, Tanzania
Program Support Specialist – Health (Arusha City) at Compassion International Arusha, Tanzania Overview The role of Program Health Support Specialist will provide subject matter expertise regarding the health of all program beneficiaries (pregnancy through youth). This role will collaborate with other Support Specialists, Program Trainers and Partnership Facilitators to ensure staff and Implementing Church Partners are adequately informed… Read More »
The post Program Support Specialist – Health (Arusha City) at Compassion International Arusha, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
PICHA: Naibu Spika Dkt Tulia Ackson Akiwasili Hospitali Kumjulia Hali Freeman Mbowe Aliyevamiwa na Kuvunjwa Mguu Dodoma
*****
Naibu Spika, Dk.Tulia Ackson amemjulia hali Mwenyekiti Chadema, Freeman Mbowe katika Hospitali ya Ntyuka, Dodoma anakopatiwa matibabu baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana na kisha kujeruhiwa na kuvunjwa mguu mmoja na kusema kuwa amemuona akiwa na majeraha mguuni na kwamba wanasubiri taarifa ya daktari ili kujua ameumia kwa kiasi gani.
"Ana maumivu ya mguu, mimi nimemuona ila bado wanaendelea kufanya uchunguzi na vipimo vingine, niwatoe hofu watanzania kwamba yupo anaendelea kupata huduma"- Amesema Naibu Spika Baada ya kumtembelea Mbowe




























