Monday, 8 June 2020

Brazil kutotangaza waliofariki kwa corona, Yatishia Kujitoa katika Shirika la Afya Duniani (WHO)

Serikali ya Brazil imetangaza kuanzia sasa haitakuwa ikitangaza idadi ya watu waliofariki kwa corona, baada ya kubaini kuwa hatua hiyo haina faida kwa nchi hiyo.

Brazil ni nchi inayoongoza hivi sasa katika nchi za Amerika Kusini kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya corona na pia kwa kuwa na idadi kubwa ya watu waliofariki kutokana na virusi hivyo.

Hata hivyo baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa hatua hiyo ya Brazil ina lengo la kuficha ukweli kuhusiana na vifo vya corona, huku Rais Jail Basonaro wa nchi hiyo akiendelea kushutumiwa kwa uzembe.

Brazil imetishia kujitoa uanachama katika Shirika la Afya Duniani (WHO) endapo shirika hilo litaendelea kuishutumu na kuilazimisha kufanya mambo ambayo haina maslahi nayo.


Share:

Idara ya polisi mjini Minneapolis yavunjwa kufuatia kifo cha Floyd

Idara ya polisi mjini Minneapolis katika jimbo la Minnesota nchini Marekani itafanyiwa mabadiliko makubwa kutokana na kifo cha Mmarekani mweusi George Floyd. 

Halmashauri ya jiji hilo imekubaliana kuivunja kabisa idara ya polisi na kuweka muundo mpya wa utendaji kazi wa polisi. 

Hayo ni kwa mujibu wa mwenyekiti wa Baraza la mji huo Lisa Bender. 

Floyd aliuawa mikononi mwa polisi chini ya wiki mbili zilizopita mjini humo tukio ambalo lilizusha maandamano ya kitaifa nchini Marekani na mengine mengi katika nchi mbalimbali. 

Mwaka jana, afisa mmoja wa polisi wa zamani mjini Minneapolis alihukumiwa kifungo cha miaka 12 na miezi sita jela kwa kumpiga risasi na kumuuwa mwanamke mweupe wa Australia ambaye hakuwa na silaha yoyote, wakati akitoa habari ya tukio la uhalifu.

-DW


Share:

Yara Agronomist at Yara International

Yara Agronomist   Location: Dar Es Salaam, TZ Job Function:  Sales & Marketing Job Type:  Permanent Job Requisition ID:  3358 About the Unit YARA Tanzania is duly registered company under the Laws of Tanzania as a subsidiary of Fertilizers Holdings AS. with headquarters in Dar es Salaam. The aim is developing a market concept that increase the number of… Read More »

The post Yara Agronomist at Yara International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Maintenance Specialist at Yara International

Maintenance Specialist   Location: Dar Es Salaam, TZ Job Function:  Maintenance Job Type:  Permanent Job Requisition ID:  3717 About the Unit YARA Tanzania is duly registered company under the Laws of Tanzania as a subsidiary of Fertilizers Holdings AS. with headquarters in Dar es Salaam. The aim is developing a market concept that increase the number of farmers that… Read More »

The post Maintenance Specialist at Yara International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima Aipongeza Halmashauri Ya Bunda Kwa Hati Safi

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Mkuu wa Mkoa wa Mara ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017.

Akizungumza hivi karibuni wakati  wa uwasilishaji wa hoja za Mkaguzi na Mdhibiti  Mkuu wa  Hesabu za Selikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima  aliipongeza  Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kupata  hati safi kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka wa fedha  2016/2017, 2017/2018 na 2018/2019.

“Halmashauri hii ni ya mfano katika mkoa wa Mara na ninawaomba msibweteke kwa vile mmepata mafanikio haya, bali muongeze bidii” alisema mkuu wa mkoa Malima

Aidha, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali katika  mkoa wa Mara, Patrick Lugisi alisema kuwa mafanikio hayo ni matokeo mazuri ya kazi wanayofanya watumishi wa Halmashauri ya mji wa Bunda.

“Ushirikiano na uwajibikaji  wa Menejimenti  ndio umepelekea Halmashauri hii  kuwa na hoja chache na kuwa na ufanisi, niziombe Halmashauri zingine kuiga mfano huu” alisema Lugisi.

Halmashauri ya mji wa Bunda ilianzishwa Mwaka 2015 na ilianza kutekeleza majukumu  yake Mwaka 2016. Hati safi kwa halmashauri hii imekuwa chachu ya kuongeza tija kwa watendaji wote na hivyo kuwawezesha wananchi kunufaika na huduma bora zinazotolewa  katika sekta za afya, elimu, maji,miundombinu na uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Mwisho


Share:

Nafasi Mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa Wiki Hii

Share:

Local Junior Consultant – Tanzania at Savings Banks Foundation for International Cooperation (SBFIC)

Job Summary Out of our wide range of activities you will work on those tasks most fitting to both your qualification and your interests with a high level of self-responsibility. For example, you will develop conceptual documents, prepare workshops and round tables, organize and accompany trainings, and much more. Minimum Qualification: Bachelor Experience Level: Mid level Experience Length: 1 year Job… Read More »

The post Local Junior Consultant – Tanzania at Savings Banks Foundation for International Cooperation (SBFIC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Sales Team Leader(3 positions) at Platinum Credit Ltd

Job Summary Platinum Credit Limited is private limited company which offers credit facilities to civil servants in Tanzania. Its committed team assures its customers quick solutions to emergent financial needs within 24 hours. In order to enhance its operational efficiency for customer satisfaction, Platinum Credit is looking for competent and qualified high achievers to fill the following vacant… Read More »

The post Sales Team Leader(3 positions) at Platinum Credit Ltd appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Head of Program Quality Job vacancy at  Plan International, Dar es Salaam, Tanzania

Senior Head of Program Quality Job vacancy at  Plan International, Dar es Salaam, Tanzania Organization: Plan International Country: Tanzania City: Dar es Salaam, Tanzania Office: Plan International Dar es Salaam, Tanzania Closing date: Wednesday, 17 June 2020 The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and… Read More »

The post Senior Head of Program Quality Job vacancy at  Plan International, Dar es Salaam, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali Yaanza Rasmi Biashara Ya Kuuza Mafuta Nchini.....Dkt. Kalemani afungua Kituo cha kwanza Mara, TPDC kujenga vituo 100.

Na Zuena Msuya, Mara
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amezindua rasmi biashara ya kuuza na kusambaza mafuta nchini  kwa kufungua   kituo cha kwanza kuuza mafuta ya Petroli na Dizeli cha Serikali kitakachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) kupitia Kampuni yake Tanzu ya Mafuta ( TANCOIL).

Aidha Dkt. Kalemani alisema kuwa kuzinduliwa na kufunguliwa kwa biashara hiyo ni kutimiza azma na nia njema ya Serikali ya kuboresha shirika lake la TPDC,kuwapatia na kuwasogezea karibu wananchi wake huduma ya kupata mafuta yenye viwango vya ubora unaotakiwa, bei nafuu, na yatakayopatikana kwa wingi muda wote.

Dkt. Kalemani alifanya Uzinduzi huo pamoja na kufungua kituo hicho wilayani Musoma, mkoani Mara  Juni 6, 2020, wakati wa ziara yake ya kikazi  katika Mkoa huo, akiwa ameambatana na  Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Zena Said pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Wizara hiyo na Taasisi zilizochini yake.

Alisema baada ya kuanza rasmi kwa biashara hiyo, TPDC kupitia TANCOIL itashirikiana na Halmashauri zote nchini kuhakikisha inafanikisha azma ya Serikali ya kufungua na kuweka vituo vya kuuza na kusambaza mafuta katika kila halmashauri nchini pamoja na miundombinu ya kuhifadhi na kusafirisha mafuta.

“Tumeshaanza biashara ya kuwauzia wananchi wetu mafuta, sitegemei kusikia mafuta yanauzwa kwa bei aghali katika vituo vya serikali, TPDC na TANCOIL mnielewe vizuri hapa!  hii haipo na haitakuwepo, lengo letu sisi serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wapata bidhaa bora za mafuta kwa kiwango kinachotakiwa,  kwa bei nafuu na yatapatikana kwa wingi wakati wote na huduma hii inapatikani jirani na  maeneo yao!,”Alisema Dkt. Kalemani.

Dkt. Kalemani aliwaeleza watanzania kuwa TPDC na TANOIL watashiriki katika biashara ya uagizaji na usambazaji mafuta kama zinavyofanya kampuni zingine za mafuta nchini ili kuongeza ushindani na kutanua wigo wa kampuni za kizalendo kushiriki  katika biashara ya mafuta, ambayo kwa sasa inafanywa na  makampuni kutoka nje ya nchi tu.

Alisema kuwa serikali kupitia TPDC itajenga vituo 100 kwa kipindi cha miaka 5 ijayo, tayari baadhi ya Halmashauri zimeanza kutenga maeneo yatakayojengwa vituo hivyo: Aidha itahakikisha kuwa nusu ya mafuta yote yanayoingizwa nchini yanasimamiwa TPDC.

“Watanzania tutembee kufua mbele na kujivunia vilivyo vya kwetu! Uzinduzi wa biashara hii ya mafuta hapa Musoma leo unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, ya Uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli, ni kutambua juhudi na mchango mkubwa wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika kuimarisha sekta ya Umma ya kukuza uchumi, pia hatuna budi kutambua mchango wake wa kuanzisha TPDC mwaka 1969 pamoja na kiwanda cha kusafisha mafuta cha TIPER mwaka huohuo, ambapo TPDC ilimiliki kiwanda hicho kwa asilimia 50%, mwalimu aliona na kuwaza mbali sana, hii yote ni katika dhana ya kujitegemea kiuchumi,”. Alisisitiza Dkt. Kalemani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini, (TPDC), Dkt. James Mataragio alisema kuwa katika kutekeleza azma hiyo ya serikali, kuanzia mwaka huu wa fedha 2020/2021, TPDC imetenga fedha za kutosha kwa ajili ya mtaji wa kugharamia shughuli za uagizaji, usambazaji na usimamizi wa mauzo ya mafuta nchini kote.

Dkt. Matagio, alisema kwamba TANOIL imejipanga kuhakikisha kuwa, kunakua na usalama wa usambazaji mafuta nchini yaani (security of supply), kunapatikana takwimu sahihi za mafuta, bei na viwango stahiki vya ubora, pamoja na uelewa mzuri na mpana wa biashara ya mafuta nchini.

“Ninafuraha sana leo TPDC inaandika historia mpya na kubwa sana katika nchi yetu, tunaungana na wakazi wa Mkoa wa Mara, kwa niaba ya watanzania wote kuonyesha furaha yetu katika kuandika historia hii mpya ya kwamba shirika letu na maendeleo ya Mafuta, (TPDC) linarudi kwa kishindo katika biashara ya kuuza na kusambaza wa mafuta ya Petroli, Dizeli na bidhaa zake kwa maslahi yetu sote na taifa kwa ujumla”, Alisema Dkt. Mataragio.

Alieleza zaidi kuwa Mwaka 2000, Serikali ilifanya maamuzi ya kuendesha biashara ya mafuta nchini kwa mfumo wa soko huria, hivyo TPDC ikaunda kampuni tanzu ya COPEC kuweza kuingia katika mfumo huo na kushiriki katika soko la ushindani katika biashara hiyo.

TPDC ilinunua na kujenga vituo mbali mbali nchini vikiwemo Segera na Muheza Mkoani Tanga, Makuyuni na Makumira Mkoani Arusha, Singida, Geita, pamoja Mkoani Mara ambapo vilinunuliwa vituo viwili tu cha Musoma na Tarime, vituo vyote hivyo vinamilikiwa na TPDC kwa asilimia mia moja(100% ).

Dkt. alisema kuwa TPDC ilishiriki katika biashara hiyo kupitia katika vituo hivyo,hata hivyo kukosekana kwa Sheria madhubuti ya Mafuta/Petroli, kulififisha ushiriki wa TPDC katika soko lenye ushindani mkubwa.

Aliweka wazi kuwa baada ya kufanyika kwa michakato na mapitio ya rejea , maboresho mbalimbali ya shirika hilo pamoja na mambo mengine, kumewezesha Uwepo wa Sheria madhubuti, pamoja na usimamizi wa kanuni mbalimbali, ambazo sasa unaiwezesha TPDC kuingia katika soko kwa ufanisi zaidi.

Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 imeipa TPDC hadhi ya kuwa Shirika la Mafuta la Taifa (NOC) ili kujiendesha kibiashara, kupitia Sheria hiyo, TPDC imeimarisha kampuni zake Tanzu za GASCO na TANOIL. Awali, TANOIL ilikuwa COPEC. Kampuni ya GASCO inajishughulisha na biashara ya gesi na TANOIL inajishughulisha na biashara ya mafuta, ambayo ndiyo biashara tunayoizindua leo Kitaifa.

Katika mwaka huu wa fedha, TPDC itakamilisha ujenzi wa vituo viwili katika Mkoa wa Singida na Mkoa wa Geita. Aidha, TPDC inaendelea na mkakati wa kutwaa ardhi katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Dodoma na Morogoro. Hatua za utwaaji ardhi katika mikoa ya Dodoma na Tanga zipo katika hatua za ukamilishaji.

“Natumia fursa hii kwa niaba ya TPDC kutoa shukrani zetu za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Nishati unayoiongoza wewe Dkt. Kalemani kwa umahiri, kwa maelekezo na rasilimali fedha zinazoiwezesha TPDC sasa kuingia katika biashara hii, pia Serikali ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano waliotupatia kwa muda wote tangu enzi za COPEC hadi sasa tunapokuwa TANOIL na kufungua ukurasa mpya wa mafanikio ya uzinduzi wa biashara ya mafuta”, Alisema Dkt. Mataragio.

Naye Mkuu wa Mkoa, Adam Malima, aliwaasa wakazi wa wafanyabiashara na watumia wa mafuta ya Petroli na Dizeli kuunga mkono juhudi za serikali za kuanzisha bishara ya mafuta kwa kununua mafuta katika vituo vya serikali.

Sambamba hilo alisema kuwa kutokana mikakati iliyowekwa na serikali kupitia TPDC na TANOIL kufikisha huduma ya mafuta hayo karibu na wananchi,kutaweka katika mazingiza salama na rafiki watumiaji wa mafuta hayo hasa waendesha bodaboda na wafanyabiashara wadogo.

“Wafanyabiashara wadogo wanaowauzia waendesha bodabora na vyombo vingine vidogo vinavyotumia mafuta hayo, wamekuwa wakihifadhi bidhaa hiyo katika hatari kubwa ya kupoteza maisha na mali zao, wanatumia vifungashio duni kama Galoni na chupa za maji, kiukweli hii itaondoa kabisa hatari hii iliyopo katika jamii yetu hasa vijijini”, Alisema Malima.

Historia inatuonesha kwamba katika miaka ya 80 hadi kufikia Mwaka 2000, TPDC licha ya biashara yake kuu ya utafutaji, uchimbaji, uendelezaji na usambazaji wa gesi asilia ilikuwa muagizaji, muingizaji na msambazaji mkuu wa mafuta yote yaliyotumika nchini.

TPDC iliingiza mafuta ghafi nchini na kuyasafisha, na pia uingizaji wa ziada ya mafuta yaliyosafishwa na kutosheleza mahitaji ya mafuta nchini.

Pia TPDC ilibeba jukumu hilo kwa ufanisi na uzalendo wa hali ya juu, ikiwemo kuwa msambazaji pekee aliyesambaza mafuta mstari wa mbele wakati wa vita vya Kagera kati ya Mwaka 1977/78 baada ya makampuni ya binafsi kugoma kupeleka mafuta Kagera.


Share:

Human Resource Officer  at International Rescue Committee (IRC), Dar es Salaam, Tanzania

Human Resource Officer  at International Rescue Committee (IRC), Dar es Salaam, Tanzania Organization: International Rescue Committee (IRC) Country: Tanzania City: Dar es Salaam, Tanzania Office: IRC Dar es Salaam, Tanzania Human Resource Officer Dar es Salaam, Tanzania Job Title: Human Resource Officer Sector: Human Resources Employment Category: Regular Employment Type: Full-Time Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description Specific duties: Ensure the implementation of the HR Policies… Read More »

The post Human Resource Officer  at International Rescue Committee (IRC), Dar es Salaam, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Infectious Disease Specialist Job vacancy at Doctors with Africa CUAMM

Infectious Disease Specialist Job vacancy at Doctors with Africa CUAMM   Doctors with Africa CUAMM is the first NGO in the healthcare area officially recognized in Italy. Founded in 1950 with the aim of training doctors to work in developing countries, CUAMM is working in Angola, Central African Republic, Ethiopia, Mozambique, Sierra Leone, South Sudan, Tanzania and Uganda implementing healthcare projects in… Read More »

The post Infectious Disease Specialist Job vacancy at Doctors with Africa CUAMM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Chief of party Job opportunity at Chemonics | Tanzania | 2020

Chemonics seeks a chief of party for the anticipated USAID Water, Sanitation and Hygiene (WASH) activity in Tanzania. This program will expand and sustain the provision and governance of WASH services through the following four objectives: 1) increase access to sustainable water services managed by the Rural Water Supply and Sanitation Agency and urban water utilities; 2) increase… Read More »

The post Chief of party Job opportunity at Chemonics | Tanzania | 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Team leader Job opportunity at Chemonics

Team leader Job opportunity at Chemonics Team leader | Tanzania | 2020 Deadline Date: Saturday, 20 June 2020 Organization: Chemonics Country: United Republic of Tanzania Organization: Relief International Added: Wednesday, 03 June 2020 Deadline: Tuesday, 30 June 2020 Chemonics seeks a national or international team leader for an anticipated multi-year, DFID-funded education programme in Tanzania. The Shule Bora (quality school) programme… Read More »

The post Team leader Job opportunity at Chemonics appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 8,2020



















Share:

Sunday, 7 June 2020

KIBAKA APEWA KICHAPO CHA MBWA MWIZI BAADA YA KUKWAPUA BIBLIA YA MUUMINI


Na Said Mwishehe,Michuzi TV
Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Ndonga mkazi wa Majumbasita jijini Dar es Salaam amejikuta akipokea kipigo cha 'Paka mwizi' kutoka kwa wananchi wenye hasira kali baada ya kukwapua Biblia ya muumini wa dini ya Kikristo aliyekuwa akielekea Kanisani.

Tukio hilo limetokea leo Juni 7,2020, saa 12 asubuhi Njia Panda ya Segerea eneo la reli ambapo kijana huyo kabla ya kukwapua Biblia hiyo alitoa panga lake na kisha kumpiga na ubapa wa panga mgongoni muumini huyo aliyekuwa akielekea kwenye Ibada ya Jumapili.

Kwa mujibu wa mashuhuda wameiambia Michuzi Blog na Michuzi TV kuwa Ndonga alikuwa katika eneo hilo la relini akiendelea na mawindo na muda mfupi baadae alipita mtu kisha akamsalimia lakini inavyoonekana mtu huyo alishtuka hivyo akaamua kuongeza mwendo.

Hata hivyo, dakika chache baadae akapita muumini huyo mwanamke ambapo Ndonga alimuamkia yule muumini huku akimsogelea na kabla ya kukaa vizuri akashtukia akishambuliwa kwa kupigwa na ubapa wa panga.

Mmoja wa mashuhuda aliyekuwa eneo hilo la tukio amesema baada ya Ndonga kumpiga na ubapa wa panga muumini huyo alichukua Biblia ambayo ilikuwa ndani ya Pochi." Ujue kuna zile Biblia ambazo zinakuwa kama vile ziko kwenye pochi ambapo ukitaka kuifungua unafungua zipo na kisha yenyewe inakuwa ndani.Nadhani yule kibaka alijua muumini amebeba pochi tu."

Kwa mujibu wa mashuhuda baada ya kibaka huyo(Ndonga) kupora hiyo Biblia aliamua kuanza kuondoka kidogo kidogo kwa kufuata reli na wakati huo mwanamke aliyeporwa alibaki akipiga kelele za kuita "Mwizi ...mwizi... mwizi huyooo jamani".

Kelele hizo zikasababaisha baadhi ya vijana waliokuwa na bodaboda kumkimbiza ambapo walifanikiwa kumpata na kisha kumrudisha eneo la barabara ya kuingia mtaani.Hivyo wananchi wenye hasira kali walianza kumshambulia kwa mawe na magongo.

Kipigo kwa kibaka huyo kiliendelea kwani watu waliamua kujipigia tu hadi walipoona amepoteza fahamu kabisa na hajiwezi kwa lolote. Hata hivyo baadhi ya wananchi waliamua kuchukua majiwe makubwa na kumtwanga nayo usoni kiasi cha kuishiwa nguvu.Wapo wanaomini kibaka huyo amekufa ,hata hivyo ni Daktari pekee ndio mwenye uwezo wa kuthibitisha kifo.

Ingawa kwa wananchi wanaamini kibaka huyo ambaye alikuwa tishio kwa muda mrefu katika maeno ya Majumbasita, Kipawa,Karakata ,Sitakishari pamoja na eneo la Kuvuka reli atakuwa amekufa kutokana na kipigo alichokipata." Watu walikuwa na hasira naye sana huyu Ndonga.Amekuwa akipora watu kila siku na wengi wameachwa na majeraha mwilini kwasababu yake," amesema mmoja ya mashuhuda.

Kutokana na tukio hilo askari Polisi wa Kituo cha Stakishari walifika eneo la tukio na kisha kuuchukua mwili na kuondoka nao kwenye gari.Hata hivyo.mmoja wa askari alisikika akisema ndani ya wiki mmoja tayari ana kesi nane za watu waliokwenda kumtolea taarifa za kuporwa na kujeruhiwa na Ndonga.

Baadhi ya wananchi ambao wamezungumzia tukio hilo wamesema kwa sasa watakuwa na amani kwa kijana huyo alikuwa tishio na hawakuwa na furaha,hivyo sasa watapumzika ingawa Ndonga anao.mtandao mkubwa wa vijana wenzake ambao alikua akishirikiana nao kufanya matukio ya uhalifu.
Share:

Yanga Yapigwa Bao 3- 0 Na KMC

Dakika 90 za mechi ya kirafiki kati ya Yanga na KMC Uwanja wa Uhuru  zimekamilika kwa Yanga kukubali kichapo cha mabao 3-0.

KMC ilianza kuandika bao la kwanza kupitia kwa Sadala Lipangile dakika ya 31 kwa pasi ya Charlse Ilanfya na bao la pili likapachikwa na Ilanfya kwa pasi ya Emmanuel Mvuyekule 

Bao la tatu lilifungwa na Hassan Kabunda dakika ya 65 kwa mpira wa adhabu.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger