Thursday, 4 June 2020
Picha : KAMPUNI YA VINYWAJI VIKALI EAST AFRICAN SPIRITS (T) LTD YATOA MSAADA WA VIFAA VYA KISASA KUJIKINGA NA CORONA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA
Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis Amtuhumu Trump Kwa Kutaka Kuwagawa Wamarekani Kwa Matabaka
Amesema taifa hili linashuhudia matokeo ya jitihada za makusudi za miaka mitatu za Trump za kuwagawa wananchi wa Marekani.
Mattis ambaye ni jenerali mstaafu aliachia ngazi mwishoni mwa mwezi Februari mwaka 2018, baada ya kuhitalifiana na Trump
Kama jibu lake kuhusu ukosoaji huo, Trump alituma mfululizo wa ujumbe kwenye Twitter ambapo alisema..."Sikupenda mtindo wake( James Mattis ) wa uongozi au yeye mwenyewe sikumpenda na wengine wengi wanakubaliana na hilo, "Afadhali aliondoka mapema"
...His primary strength was not military, but rather personal public relations. I gave him a new life, things to do, and battles to win, but he seldom “brought home the bacon”. I didn’t like his “leadership” style or much else about him, and many others agree. Glad he is gone!— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) June 4, 2020
Vigogo Wanne Wizara ya Maliasili na Utalii Wasimamishwa Kazi
Watatu Watiwa Mbaroni Dar es Salaam kwa tuhuma za mauaji ya dereva tax (UBER)
JNHPP MW 2115, uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika.
Wednesday, 3 June 2020
DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)
DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST Employer: Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) POST DETAILS POST DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST POST CATEGORY(S) PHYSICAL & NATURAL SCIENCES STATISTICS AND MATHEMATICS EMPLOYER Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) APPLICATION TIMELINE: 2020-05-20 2020-06-04 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Advise the Director… Read More »
The post DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.
DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)
DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST Employer: Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) POST DETAILS POST DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST POST CATEGORY(S) PHYSICAL & NATURAL SCIENCES STATISTICS AND MATHEMATICS EMPLOYER Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) APPLICATION TIMELINE: 2020-05-20 2020-06-04 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. … Read More »
The post DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.
Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Kesi ya Spika Ndugai na Cecil Mwambe
Mbali na Ndugai, walalamikiwa wengine ni Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Katika kesi hiyo Wakili Kaunda anaiomba Mahakama Kuu kutengua amri ya Spika Ndugai ya kumtambua Mwambe kama Mbunge halali wa Ndanda.
Katika uamuzi mdogo uliosomwa leo Juni 3, 2020 na Jaji Issa Maige aliyekuwa akisaidiana na Jaji Stephen Magoiga na Jaji Seif Kulita amesema mlalamikaji alikosea namna ya kufungua kesi ya kikatiba badala yake alipaswa kufungua kesi kwa utaratibu wa kawaida.
Amesema, kauli ya Spika Ndugai aliyoitoa haikuwa imevunja katiba bali ni ya kiutaratibu katika shughuli zake za kiutendaji hivyo mlalamikaji angekuwa sahihi kama angefungua kesi hiyo kwa utaratibu wa kawaida kwa kutumia Ibara ya 83 (1) badala ya ile ya 26 (2) aliyoitumia.
Jaji Maige amesema Ibara hiyo inaenda sambamba na kifungu cha 37 cha Sheria ya Uchaguzi ambacho kinaeleza kuhusu utaratibu wa kutangaza kiti cha Mbunge ambacho kiko wazi.
Wakili Kaunda alifungua kesi mahakamani hapo dhidi ya Ndugai, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Cecil Mwambe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Katika kesi hiyo Wakili Kaunda anadai Mwambe alitangaza kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) kauli ambayo iliungwa mkono na katibu mkuu wa CCM Dk Bashiru Ally aliyempokea rasmi Mwambe mbele ya hadhira kwa kumkabidhi kadi ya CCM, na Mwambe naye alimkabidhi Katibu Mkuu huyo kadi yake ya Chadema.
Wakili Kaunda anadai kitendo cha Spika kumtambua Mwambe kama mbunge halali wakati ameshajivua uanachama wa chama kilichomdhamini kama Mbunge wa Ndanda (2015-2020), ni ukiukwaji wa ibara ya 71(1)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na hakuna mamlaka yoyote nchini, achilia mbali Spika, yenye uwezo wa ku mrudisha bungeni Mbunge ambaye kwa hiari yake mwenyewe ameamua kujivua uanachama wa chama cha siasa kilichomdhamini kupata ubunge.
Rais Magufuli Ampandisha Cheo Mkuu Wa JKT Meja Jenerali Charles Mbuge
AGAPE YAWAKUMBUKA WATU WENYE ULEMAVU MAPAMBANO DHIDI YA CORONA SHINYANGA
Shirika la AGAPE ACP linalotetea haki za wanawake na watoto mkoani Shinyanga, limewataka wananchi mkoani humo kuwakinga watu wenye ulemavu dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona , pale wanapokuwa wakihitaji msaada wa kuwashika mkono na kuwavusha kwenye vivuko vya barabara.
Hayo yamebainishwa leo Juni 3,2020, na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP John Myola, wakati akikabidhi kifaa cha kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka kwenye ofisi ya Chama Cha Watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA), pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Myola amesema watu wenye ulemavu hasa wasioona wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya virusi vya Corona,kwa sababu mara nyingi huwa wanahitaji msaada wa watu kuwavusha barabara na ni lazima washikwe mikono, hivyo endapo mtu huyo hakunawa mikono ama kujipaka Vitakasa atakuwa katika hatari ya kuambukizwa.
“Natoa wito kwa wananchi mkoani Shinyanga na maeneo mengine hapa nchini, tuwalinde watu hawa wenye ulemavu hasa wasiiona, pale tunapokuwa tukiwapatia msaada mbalimbali ikiwamo kuwavusha barabarani, tuzingatie unawaji mikono ama kujipaka Sanitizer, ili kuwahakikishia usalama wao wasipate maambukizi ya virusi vya Corona,”amesema Myola.
“Sisi AGAPE tumeguswa na kundi hili maalum, na ndiyo maana tumeamua kuwapatia kifaa hiki cha kunawia mikono kwa sabuni na maji tiririka kwenye ofisi yao, pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona ili waendelee kubaki salama,” ameongeza.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richard Mpongo, amepongeza Shirika hilo kwa kuwajali na kuwapatia kifaa hicho pamoja na elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona, jambo ambalo limewafanya kufarijika na wataendelea kujilinda.
Aidha amewataka wananchi mkoani humo kutowanyanyapaa watu hao wenye ulemavu hasa katika kipindi hiki cha Janga la maambukizi ya virusi vya Corona, bali pale wanapokuwa wakihitaji msaada wao wahakikishe wananawa mikono au kujipaka vitakasa mikono (Sanitizer) ndipo wawashike mikono ili wote wabaki kuwa salama.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Shirika la Agape ACP mkoani Shinyanga John Myola akitoa elimu wa watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) namna ya uvaaji wa barakoa na kuzivua ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Afisa mradi wa utu wa msichana kutoka Shirika la Agape Sophia Rwazo akitoa elimu ya kujikinga na virusi vya Corona kwa watu wenye ulemavu.
Mkurugenzi wa Shirika la Agape ACP mkoani Shinyanga John Myola, akitoa elimu namna ya kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richad Mpongo (kushoto), akinawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara baada ya kupewa mafunzo namna ya kutumia kifaa hicho ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Katibu wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Uel Nyange, akinawa mikono kwa sabuni na maji tirika mara baada ya kupewa mafunzo namna ya kutumia kifaa hicho ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino mkoani Shinyanga Yunisi Zabron Manumbu, akinawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.
Zoezi la unawaji mikono kwa sabuni na maji tiririka likiendelea .
Zoezi la unawaji mikono kwa sabuni na maji tiririka likiendelea.
Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richard Mpongo akiishukuru AGAPE kwa kuwapa elimu namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona , pamoja msaada wa kifaa cha kujikinga na Maambukizi ya virusi hivyo.
Na Marco Maduhu- Shinyanga.


























