Wednesday, 3 June 2020

WAZIRI WA ELIMU ATOA SIKU TATU KWA VYUO VIKUU WAPEWE FEDHA ZA KUJIKIMU


Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako ametoa muda wa hadi kufika Ijumaa wiki hii ambayo itakuwa Juni 5, 2020, vyuo vyote vya elimu ya juu hapa nchini viwe vimemaliza kuwapa fedha za kujikimu wanafunzi wote na si vinginevyo.

Amesema hayo leo Juni 6, 2020 wakati akizungumza baada ya kukabidhi magari manne kwa chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

Ndalichako amesema, serikali haitakuwa na mswalia mtume katika hili kwa kuwa tayari ilishatoa fedha hizo na hakuna sababu ya kuchelewa kuwapa wanafunzi fedha hizo

"Hakuna sababu ya kuwacheleweshea fedha wanafunzi wakati serikali imeshatoa Sh.bil 122.Rais alishatoa maelekezo na lazima yatekelezwe.Sasa ole wao vyuo vitakavyokuwa havijatekeleza agizo .Suala la wanafunzi kukataa kusaini siyo kweli, hatutakuwa na msalia mtume.

"Ifikapo Ijumaa wiki hii wanafunzi wote wa vyuo vikuu wawe wameshapata fedha zao za kujikimu, hatutakuwa na msamaha kwa vyuo ambavyo vitakuwa havijatekeleza agizo hilo.

"Kama kutakuwa na wanafunzi ambao watakuwa hawajasaini fedha za kujikimu achaneni nao, wapeni ambao wameshaini"-Waziri wa elimu, Prof. Joyce Ndalichako

Vyuo vimefunguliwa Juni 1, 2020 baada ya kusimama  kutokana na janga la Corona. Serikali tayari imeshathibitisha kuingiza fedha za mikopo kwa wanafunzi hivyo kuacha jukumu kwa vyuo kukamilisha kuwapatia wanafunzi.



Share:

GGML YATOA MILIONI 100 UJENZI WA CHUO KIKUU HURIA – GEITA


Makamu Rais wa GGML, Simon Shayo
Na Mwandishi Wetu
Katika kukuza sekta ya elimu ya juu nchini, Kampuni ya Geita Gold Mining Ltd. (GGML) kupitia sera yake ya uwajibikaji kwa jamii imetoa kiasi cha Sh milioni 100 kusaidia ujenzi wa Kituo cha Chuo Kikuu Open University cha Mkoa wa Geita. 

Awamu ya kwanza ya mradi huo inajumuisha ujenzi wa jengo la utawala linalojumuisha chumba mikutano cha viongozi, maktaba, chumba cha maabara ya kompyuta na ofisi nyingine tano. 

Pia kiasi hicho cha pesa kilichotolewa na GGML ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi na malipo ya mafundi ujenzi. 

Akizungumzia mradi huo, Makamu Rais - Maendeleo Endelevu katika kampuni hiyo, Simon Shayo alisema uwezeshaji huu unatarajiwa kufaidisha wanafunzi 500 wanaotokea katika vituo vitatu vya Mkoa wa Geita ambavyo ni Chato, Nyang’wale na Geita mjini. 

Alisema GGML kwa kushirikiana na wananchi imeamua kuunga mkono juhudi za serikali kufadhili mradi huo kwani mbali na kuongeza mazingira bora ya upatikanaji wa elimu pia utazalisha wahitimu bora wenye weledi ndani ya jamii wataokuwa na uwezo wa kusukuma gurudumu la maendeleo ya Taifa mbele kwa kupitia elimu waliyoipata. 

Alisema Chuo cha Open University - Geita, kama vilivyo vyuo vingine kimekuwa kikifanya shughuli zake katika majengo ya kukodi ambayo hutumika kama madarasa na ofisi za utawala. 

“Mradi huu unaifanya Geita kuwa mkoa wa (1, 2, 3) katika ukanda wa ziwa na wa (2, 10, 20) nchini Tanzania kunufaika na miundombinu inayomilikiwa wa Open University. 

"Kwa ufadhili huu, tuna hakika kwamba chuo kikuu kitapunguza gharama za uendeshaji na kuboresha ufanisi. Zaidi ya hayo itaunda uhusiano mzuri kati ya wanafunzi kutoka Geita na vyuo vingine 30 vya Open University Tanzania. Mradi huu moja kwa moja unasaidia Serikali kufikia lengo la 4 la maendeleo endelevu (SDGs), ambalo ni upatikanaji wa elimu bora ifikapo 2030 kama ilivyotarajiwa ”alisema Shayo. 

Aidha, Mkurugenzi wa Open University Geita, Ally Abdu aliishukuru GGML kwa msaada huo ambao unaongeza mazingira mazuri ya kusoma na kukidhi idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu ambao wanaongezeka kila mwaka. 

"Malengo ya Chuo kikuu huria ni kutoa elimu inayofaa na yenye ubora, elimu iliyo rahisi kupatikana na nafuu kwa njia ya mtandao. Elimu iliyojitosheleza kwa tafiti zenye kutoa suluhu ya matatizo ndani ya jamii kwa maendeleo ya uchumi wa Tanzania na dunia kwa ujumla. 

“Kupitia msaada huu wa GGML, sasa tuna uhakika kwamba tutapunguza gharama zetu za uendeshaji na kuboresha ubora wa elimu katika tawi letu la Geita, " alisema Ally. 

Hata hivyo, Shayo aliongeza kuwa kufuatia marekebisho ya Sheria ya Madini mwaka 2017, Kampuni ya Dhahabu ya Geita kupitia mpango wake wa uwajibikaji kwa jamii imeungana na serikali za mitaa za Geita kutekeleza miradi ya jamii yenye thamani ya Sh bilioni 18 katika Mkoa wa Geita. 

“Kabla ya marekebisho GGML ilikuwa imewekeza kihistoria katika miradi endelevu ya kimkakati kwa jamii ikiwa ni pamoja na shule ya Sekondari ya Wasichana ya Nyankumbu, mradi wa maji safi wa mji wa Geita na mradi wa Kilimanjaro Challenge unaolenga kutokomeza maambukizi ya VVU/UKIMWI nchini,” alisema. 

Share:

Mtangazaji Maarufu wa Clouds FM Hamisi Mandi (B Dozen ) atimkia E-FM

Aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha Redio cha Clouds FM Hamis Mandi maarufu B Dozen amejiunga na Kituo cha redio cha EFM- Tanzania

Mandi ambaye anafahamika zaidi kwa jina la utangazaji la B-Dozen (The Navigator, Msafiri) kwa muda mrefu alikuwa akiongoza kipindi cha XXL cha Clouds FM, pamoja na vingine.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram, E-FM wameandika mbobezi huyo wa utangazaji amejiunga nao, na kwamba kinachofuata ni kupaa juu, na kuhakikisha mafanikio zaidi kwa Tanzania.


Share:

WASIOSHIRIKI MISIBA SASA KUCHARAZWA VIBOKO

Diwani wa Kata ya Mwangata, Manispaa ya Iringa, Edward Nguvu


Na Zuhura Zukheir, Iringa
Wakazi wa Kata ya Mwangata, Manispaa ya Iringa wamepongeza uamuzi wa Diwani wa Kata ya Mwangata, Edward Nguvu kutaka watu wasiohudhuria misibani wacharazwe viboko ili iwe fundisho kwa wengine.

Akizungumza na Majira kwa niaba ya wananchi wenzake, mmoja wa wananchi hao amesema hivi sasa kumekuwa na tabia ya waombolezaji kwenye kata hiyo kuchagua misiba, jambo ambalo halikubaliki hata kidogo.

Mwananchi huyo ambaye hakutaka jina lake kutochapishwa gazetini amesema zamani mwitikio wa wananchi kushiriki misibani ulikuwa mkubwa, lakini sasa hivi ni kinyume, ndiyo maana wanaunga ushauri wa diwani wao.

Diwani Nguvu alishauri watu hao wawe wanacharazwa viboko jana alipohudhuria mazishi ya mkazi wa kata hiyo, Wilbart Mgongolwa yaliyofanyika katika makaburi ya Mlolo Mjini hapa.

Amesema baadhi ya watu wamekuwa wakiendekeza majukumu yao ya kimaisha na kutojihusisha na shida za kijamii kama kushiriki shughuli za misiba na mazishi

Ameongeza kwamba vijana wamekuwa wakikimbilia kwenye misiba ya jamaa zao kwa kwenda kuchimba kaburi, huku misiba mingine wakiachiwa wahusika wenyewe hali inayoelezwa kuleta mpasuko ndani ya jamii.

Ametolea mfano msiba wa Wilbert Mgongolwa, Diwani Nguvu alisema watu wengi hawakuhudhuria katika msiba huo kwa dharau au kutokuwa na msukumo kutoka kwa viongozi wa mtaa.

Amesema kufuatia kuwepo kwa watu wasioshiriki shughuli za misiba wala kutembelea wagonjwa kwa makusudi hivi sasa ipo haja kwa Serikali ya Mtaa kuanza utaratibu wa kuwacharaza viboko wale wote wanaobaki nyumbani bila kuwa na udhuru wowote.

“Sasa hivi imejitokeza tabia ya dharau na watu kutokwenda misibani kwa makusudi, sasa tabia hii inabidi ikomeshwe kwa nguvu zote, nashauri wenyeviti mliopo kwenye kata yangu anzisheni utaratibu wa kuwacharaza bakora wale wote wasiohudhuria msibani ili kesho wao wawe wa kwanza kufika,”amesema Nguvu.
Share:

FAMILIA YASHEREHEKEA KIFO CHA BIBI WA MIAKA 126 MOSHI


Kushoto ni Bibi Susana Mmari wakati wa uhai wake, kulia ni mazishi yake.

Hivi karibuni kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, zilisambaa video na picha zikionesha watu wakisherehekea kifo cha Bibi mmoja aliyejulikana kwa jina la Susana Benjamin Mmari, aliyefariki na umri wa miaka 126, kilichotokea Mei 27 na kuzikwa Mei 30, 2020, huko Old Moshi Kidia.

Mmoja wa wajukuu wa Bibi huyo, anayejulikana kwa jina la Noel Mmari na kusema kuwa waliamua kuugeuza msiba huo kama sherehe, kwa sababu ilikuwa ni shukrani kwa Mungu kutokana na Neema kubwa aliyowapa kupitia maisha ya Bibi yao.

"Bibi alikuwa na watoto sita, wakiume 4 na wanawake walikuwa 2, na wawili tayari walishafariki, kaacha wajukuu 97, vitukuu 370, hivyo jumla ameacha uzao wa watu 586, tulimzika kwa shangwe kwa sababu afya yake mwishoni ilikuwa kama anateseka, kwahiyo kitendo cha kutwaliwa tukaona tukisikitika tutamkosea Mungu, sababu katupa Neema ambayo tunatakiwa kumshukuru siyo kusikitika" amesema Noel.

Aidha Noel amesimulia Bibi Suzana alikuwa ni wa aina gani, "Bibi alikuwa akiamka asubuhi anaenda shamba na alichokuwa anakilima ndiyo hicho hicho alikuwa anakula na wanaye na wajukuu na mimi alinilea baada ya kumaliza chuo na kupata kazi, ilibidi nimchukue niishi naye, kwahiyo amefariki akiwa kwenye mikono yangu, mimi ni miongozi mwa wajukuu zake wadogo, nina miaka 40 sasa".

Chanzo- EATV
Share:

Daladala Dar Ruksa Kusimamisha Wanafunzi Wanne

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ameagiza daladala za mkoa huo, ziruhusu wanafunzi wanne kusimama ili kuondoa changamoto ya usafiri.

Makonda alitoa agizo hilo jana jijini Dar es Salaam wakati akipokea vifaa tiba na vifaa vya ujenzi na kueleza kuwa, agizo hilo la kubeba wanafunzi lianze mara moja.

“Sitaki kusikia mwanafunzi anaachwa eti konda na dereva wanasema wanabeba abiria kulingana na viti, wabebwe ili waende kwenye masomo,” alisema.

Alisema daladala litakalokuwa limebeba wanafunzi wasiozidi wanne, trafiki haruhusiwi kulikamata, lakini kama amesimamisha abiria wachukue hatua.

Pia, alisema alitoa maelekezo ya bodaboda na bajaji kuingia katikati ya jiji kubeba abiria, lakini kuna mtu mmoja ameanza kuwakamata na kumweleza kuwa hakuna Mkuu wa Mkoa mwingine.

“Hakuna Mkuu wa Mkoa mwingine, nipo na bado nipo, bodaboda, bajaji mnaendelea kuingia katikati ya mji kuendelea na shughuli zenu za kiuchumi kama nilivyoelekeza kauli hii sijaitengua na hakuna mwingine wa kuitengua katika mkoa huu labda mamlaka nyingine kutoka juu yangu,” alisema.


Share:

DC Macha Awatoa Hofu Wanafunzi Wa Kidato Cha Sita Kuhusiana Na Covid 19

SALVATORY NTANDU
Serikali wilayani Kahama mkoani Shinyanga imewatoa hofu wanafunzi wa kidato cha sita walioanza masomo June Mosi mwaka huu katika shule sita zilizopo wilayani humo kuhusiana na ugonjwa wa homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona.

Pia imewataka kuchukua tahadhari kwa kuhakikisha wanazingatia maelekezo ya wataalamu wa afya yaliyotolewa na Wizara ya Afya katika kipindi hiki ambacho wanajiandaa na  mitihani ya  mwisho ya Taifa inayotarajia kufanyika hivi karibuni.

Wanafunzi nikutoka shule za sekondari, Busoka, Anderleck, John Paul, Mwendakulima,  Mwalimu Nyerere na Dakama na kuwataka walimu wa shule hizo kuhakikisha kila darasa linakuwa na ndoo za kunawia mikono,Vitakasa mikono pamoja na matumizi ya Barakoa wakati wa masomo.

Anamringi Macha ni mkuu wa wilaya ya Kahama, aliyabainisha hayo June 2 Mwaka huu katika ziara ya kukagua maandalizi ya Mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha sita kuhusiana na namna viongozi wa shule hizo walivyotekelza maagizo ya serikali ya kujikinga na ugonjwa wa Covid 19 kwa wanafunzi.

Aidha Macha alisema kuwa Ugonjwa wa Corona bado upo lakini hapa nchini maambukizi yameshuka ukilinganisha na hapo awali,na kuwataka wanafunzi kutokuwa na hofu juu ya ugonjwa huo na badala yake wajikite na maandalizi ya mitihani yao ya Mwisho.

“ Wanafunzi wangu msiazimane barakoa na muache tabia za kutembeleana katika mabweni nyakati za usiku,kumbukeni moja ya sababu ya kuambukizana kwa ugonjwa huu ni kuazimana,nguo,barakoa,kugusana na kutonawa mikono,”alisema Macha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala, Simon Berege alisema kuwa,watahakikisha wanawapatia wanafunzi huduma zote katika kipindi hiki cha mitihani ikiwemo, chakula na malazi ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao ya Mwisho.

“Walimu wapo tayari kuwasaidia kwa masomo yote na hakuna mwanafunzi ambaye ataruhusiwa kwenda kuzurura nje ya maeneo ya shule tumejipanga vizuri na ndoo,vitakasa mikono na sabuni zipo kwa wingi hivyo tunaamini watamaliza mitihani yao salama,”alisema Berege.

Mwisho.


Share:

Mtoto Afariki Kwa Kushambuliwa Na Fisi Shinyanga, RPC Atoa Wito Kwa Wazazi

SALVATORY NTANDU
Wazazi na Walezi Mkoani Shinyanga wametakiwa kuchukua tahadhari kwa watoto wao dhidi ya  wanyama aina ya Fisi ambao wamekuwa wakionekana katika maeneo mbalimbali  na kusababisha madhara kwao ikiwemo ya vifo.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba June 2 wakati akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na tukio la kushambuliwa  hadi kufariki dunia kwa mtoto wa miaka miwili na nusu  aliyehamika kwa jina la Charles Christian katika kitongoji cha Mwagala kata ya Ibadakuli.

Amesema  tukio hilo limetokea June Mosi mwaka huu majira ya saa moja usiku akiwa anacheza na watoto wenzake nje ya nyumba yao alijeruhiwa kwa kung'atwa na fisi sehemu za usoni na kisha kuburuzwa umbali wa mita 50 ndipo wananchi walipoamua kumfukuza akamuachia na kukimbia baada ya kuzidi kwa kelele za wananchi hao.

“Wanyama hawa wamekuwa wakizurura ovyo hivyo ni Budi kila mzazi /Mlezi kuhakikisha watoto wao wanakuwa salama na kwani matukio ya watu kushambuliwa na fisi ama mifugo yamekuwa ni mengi hivyo chukueni Tahadhari,”alisema Magiligimba.

Amefafanua kuwa  Charles  alifariki dunia akiwa njiani akisafirishwa kwenda katika hospitali ya rufaa ya kanda ya  Bugando jijini Mwanza  kwa matibabu na mwili wake  umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga kwaajili ya kukabidhiwa ndugu zake kwaajili ya Matibabu.

Mwisho.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano June 3



















Share:

Tuesday, 2 June 2020

Aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu anashikiliwa na TAKUKURU.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inamshikilia aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Lojistiki wa MSD, Byekwaso Tabura, kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kusibabishia serikali hasara.



Share:

RC Malima Ataka Wakulima Wauze Kahawa Yao Kwa Bei Nzuri ....Aunga Mkono Wanunuzi Binafsi

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Mara
Uongozi wa Mkoa wa Mara umesisitiza kuendelea kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kuhusu wanunuzi binafsi wakati akizungumza na wananchi wa Kyaka, Rwamisheye, Kemondo Muleba, Nyakabango na Kyamyorwa mkoani Kagera tarehe 11 Julai 2019.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe Adam Malima leo tarehe 2 Juni 2020 wakati akizungumza Kwenye kikao kazi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Prof Jamali Adam ofisini kwake Mjini Musoma ambapo amesisitiza kuwa wanunuzi binafsi wataruhusiwa kununua Kahawa kupitia Vyama vya Ushirika badala ya kwenda moja kwa moja kwa wakulima.

Amesema kuwa serikali iliamua kuanzisha Ushirika kwa ajili ya wakulima ili waweze kuuza mazao yao kwa bei nzuri hivyo wanunuzi binafsi ni ruksa lakini wanapaswa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

"Uuzaji wa Mazao ya wakulima kupitia Vyama vya Ushirika tumeuweka ili kama wakulima wakiibiwa au kupunjwa sisi iwe rahisi kumpata muhusika na tunachukua hatua kali dhidi ya wote watakaofanya ubadhilifu, lakini tukimkuta mnunuzi binafsi ameingia mpaka shambani ni kama ameingia chumbani atapata balaa" Amesisitiza Mhe Malima

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mara Mhe Adam Malima ameitaka Bodi ya Kahawa kutafuta wanunuzi binafsi kadri iwezavyo ili kuongeza ushindani na wakulima waweze kupata bei nzuri kwani jambo hilo itasaidia kukabiliana na unyonyaji dhidi ya wakulima wa kahawa pamoja na Mazao mengine Mkoani Mara.

"Mkulima yoyote akisikia bei nzuri ya kahawa lazima atauza hawezi kwenda Kwenye bei ndogo wakati ameona kuna mahala kuna bei nzuri inayoendana na jasho lake" Amesema Mhe Malima

Pamoja na mambo mengine Mhe Malima ameipongeza Bodi ya Kahawa kwa kutoa Miche 40,000 kwa ajili ya mkoa wa Mara huku akiisisitiza umuhimu wa Bodi hiyo kuwaongezea wakulima miche mingi zaidi ili kuongeza Uzalishaji wa kahawa nchini.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania Prof Jamal Adam amesema kuwa Bodi ya Kahawa imejiwekea malengo muhimu ya kuongeza Uzalishaji wa kahawa nchini, kuhakikisha kunakuwa na Bei nzuri, na kujenga mazingira bora ya Biashara kwenye tasnia ya kahawa.

Pia ameongeza kuwa Bodi ya Kahawa itaendelea kusimamia na kutekeleza maagizo ya serikali ikiwemo upatikanaji wa Miche Bora kwa wakulima, Malighafi Kwenye viwanda vya kahawa na kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri kupitia kuongeza ushindani Kwenye soko la kahawa la awali na soko la pili.

Kadhalika, amewawasisitiza wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali nchini walioombwa vibali na wanunuzi binafsi na wenye viwanda kufanya hivyo kwa wakati ili Bodi iweze kutoa leseni mapema  


Share:

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya Kumi (10)

Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA
“Nawe pia mwanangu, ila ni vibaya kwa mtoto wa kike kulala chini huku mimi mwanaume niliye komaa nikilala kitandani. Huo utakuwa ni unyanyasaji mkubwa sana na nina weza nisipate usingizi kabisa mwanangu. Ninacho kuomba ni wewe uweze kulala kitandani na mimi uniache nilalale chini”
“Hapana baba wewe ni mgeni haina shinda. Wewe lala tu kitandani”
Magreth alizungumza huku akisimama, ila kwa bahati mbaya kitando cha nabii Sanga kumzuia katika kusimama kwake, kukapelekea tenge lake kulegea kishikizo alicho kuwa amekichomeka kifuani mwake na kupelekea tenge hilo kuanguka chini na kumfanya Magreth abaki kama alivyo zaliwa na kumfanya nabii Sanga ashuhudie uumbaji wa Mungu alio kuwa akiutamani kuuona siku zote mubashara.


ENDELEA
Magreth akahisi kama amepigwa shoti ya umeme, hakutamani hata siku moja maungo yake yaweza kuonakana mbele ya mwanaume ambaye hajawahi hata kumfikiria akilini mwake. Akainama kwa haraka na kulikota tenge hilo na kuanza kujifunga. Nabii Sanga akatakamani kuupeleka mkono wake wa kulia huku akiendelea kumeza mate ya uchu, ila akajikuta akishindwa kwani tayari Magreth amesha sogea mita kadhaa.
“Ahaa….nalala hapa chini”
Magreth alizungumza huku akijilaza chini. Ni asilimia chache sana ya wanaume ambao wana weza kuvumilia pale wanapo yaona maungo ya ndani ya mwanamke ambaye wana mtamani kwa kipindi kirefu. Nabii Sanga, akajikuta akisimama na kuvua taulo lake na kumfanya Magreth apigwe na butwaa, huku akimtazama jo wa nabii Sanga, jinsi alivyo kisawa sawa. Magreth kwa haraka akakurupuka chini hapo, kwani kwa kuendelea kujilaza kuna weza kumrahisishia nabii Sanga kukamilisha ushetani wake ambao tayari amesha anza kuudhihirisha mbele yake.
“Baba una fanya nini?”
Magreth alizungumza huku akiwa amerudi nyuma hadi ukutani.
“Mage natambua kwamba…..kwamba mimi pia ni binadamu. Nina hisia za kibinadamu. Tafadhali nina kuomba japo kidogo tu”
“Hapana baba, mimi ni mwanao tena mwanao wa kiroho, jifunge basi taulo lako.”
“Mage siwezi kuvumilia zaidi ya hapa, hembu tazama jinsi ... ilivyo . Tafadhali Magre nionee huruma”
Nabii Sanga alizungumza mithili ya mtu aliye changanyikiwa. Wadhifa, heshima yake ambavyo watu wengi wana mpatia vyote amevitupa pembeni. Magreth akazidi kushangaa mara baada ya kumuona nabii Sanga akipiga magoti chini huku machozi yakimwagika usoni mwake.
“Magreth usiku wa leo ukipita hivi hivi nina weza kufa. Ninaweza kufa Mage”
Nabii Sanga alilalama huku akiendelea kupiga magoti mbele ya Magreth ambaye ukifananisha hadhi zao ni sawa na mbingu na ardhi. Hapa ndipo ule usemi wa mapenzi hayanaga komando ndipo unapo chukua nafasi. Magreth kwa haraka akachanganua akili yake na kuikumbuka video ya ngono kati ya Mrs Sanga na Tomas. Akaichukua simu yake kwa haraka na kumfanya nabii Sanga kutokwa na macho.
“Mage una taka kunipiga picha hivi!!?”
“Hapana”
Magreth alijibu huku vidole vyake vikiwa na kazi ya kuchambua ni faili lipi lina video hiyo. Mara baada ya kuliona, akanyoosha mkono wake ulio shika simu na kumfanya nabii Sanga ashangae kidogo.
“Nini?”
“Tazama”
Nabii Sanga akaichukua simu ya Magreth, akaanza kuitazama video hiyo. Hamu ya kumtamani Magreth yote ikakata. Akasijikuta akikaa chini sakafuni huku akiwa uchi kabisa. Hasira na uchungu wa kuibiwa mke na mtu wake wa pembeni vikazidi kuutawala moyo na mwili wake.
‘Samahani nabii Sanga, sikupanga kukuonyesha video hiyo kwa wakati huo. Nimefanya hivi ili kuokoa usichana wangu’
Magreth alizungumza huku akiendelea kumshuhudia nabii Sanga jinsi anavyo tetemeka kwa hasira huku j wake akilala                                 ***
“Kila mtu avae bulletproof yake”
Rama D alitoa agizo hilo kabla ya kushuka kwenye gari lake. Wadogo zake wakafanya hivyo, kila mtu akashuka kwenye gari lake huku bunduki yake akiwa ameikoki kisawa sawa.
“Shukeni kwenye magri”
Mkuu wa kikosi cha polisi, aliwaamuru askari wake na wakatii. Wakashuka huku gari hizo mbili za askari zikiwa zime kaa sawa. Wakafungua milango ya gari hizo kwa ajili ya kuzuia risasi ambazo zimesha anza kungurumishwa kutoka kwa majambazi hao. Umbali wa mita hamsini walizopo, ziliweza kuwapa nafasi ya mapambano hayo kudumu kwa muda mrefu huku wote wakishambulia kwa kusubiriana.
“Mkuu wa namna hii hatuto weza kuwadhuru, tuna maliza tu risasi zetu”
“Inabidi wawekwe kati”
“Ndio mkuu, nimewasiliana na askari wengine, wapo njiani wana kuja wakitokea nyuma yao. Tukiwaweka kati nina imani tuna washinda”
“Kazi nzuri, hakikisheni muna tunza risasi zenu”
“Poa poa’
Askari wote wakaacha kushambulia na kuwafanya Rama D na wadogo zake kushangaa.
“Wana mpango gani mbona wameacha kutushambulia?”
Selemani aliuliza huku akichungulia jinsi askari walivyo jificha kwenye magari hayo.
“Sijajua kwa kweli”
Rama D alijibu huku jasho likimwagika usoni mwake. Siku zote Rama D na wadogo zake wamekuwa wakitekeleza kazi za utekaji wao kwa urahisi sana kwa maana hao wateja wao huwavamia kwa kustukiza. Ila leo wamekutana na kikosi cha askari ambao nao wana mafunzo ya hali ya juu.
“Fuc** wametuweka kati”
Selemani alizunugmza mara baada ya kuona gari nne zikija nyuma yao.
“Sisi tudili na hawa wa nyuma na wewe Abdalah dili na hawa wa mbele’
Rama D aligawa majukumu hayo kwa wadogo zake hao wawili walio salia. Wakaanza mashambulizi upya na kuwafanya askari wanao kuja kwa nyuma yao kusimamisha magari yao umbali kidogo na kuanza kujibu mapigano hayo. Askari hawakuwa wajinga wa kupoteza risasi zao kirahisi, jinsi Rama D na wadogo zake wanavyo mimina risasi pasipo mpangilio, kukawapa askari uvumilivu ambao wana imani kwamba ukifikia hatua fulani, basi wata imaliza vita hiyo kirahisi sana.
“Risasi zimekwisha”
Selemeni alizungumza huku akitazama bunduki yake inayo toa moshi mbele, kwani ameachia risasi nyingi sana na magazine nne alizo kuwa ana zibadilisha kila baada ya magazine moja kuisha, nazo zote zimekwisha.
“Kwenye gari lako kwani huna magazine?”
Abdalah D alimuuliza Selemani huku akimgeukia.
“Zimekwisha”
“Ohooo hata mimi hapa magazine yangu ina kwenda kuisha”
Abadlah alizungumza huku akisitisha kuwashambulia askari.
“Hata mimi nimeishiwa na risasi”
Kauli hizi zikaanza kuwaogopesha Rama D na wadogo zake. Kila mmoja matumaini yake ya kuishi tena yameanza kupotea taratibu. Abdalah akatoa magazine iliyopo kwenye bunduki yake na kukuta zikiwa zimebaki risasi tatu.
“Zimebaki risasi tatu na sina za ziada kaka”
Abdalah alizungumza kwa unyonge sana huku akikaa chini.
“Siwezi kukamatwa kijinga, tupigeni dua kisha tujiue. Mungu atatupokea vizuri”
Rama D alizungumza, wakashikana mikono wote watatu, wakaanza kusali dua hiyo huku wote wakiwa wamekaa chini. Dua hiyo haikuchukua dakika hata tatu tayari wakawa wamesha imaliza.
“Nitakuwa wa kwanza”
Rama D alizungumza huku akiichukua bunduki hiyo aina ya AK47 kutoka mikononi mwa Abdalah. Akajiwekea mdomo wa bunduki chini ya kidevu chake. Bila ya majadiliano, akaachia risasi moja ambayo haikufanya kosa zaidi ya kukifumua kichwa chake kwa juu.
Selemani D akamtazama mdogo wake Abdalah D anaye tokwa na machozi ya uchungu sana juu ya kushuhudia kaka yake akifa mbele ya macho yake. Woga wa Abadlah ukaanza kujidhihirisha usoni mwake na kumfanya Selemeni D kumtazama kwa sekunde kadhaa.
“Samahani Abdalah”
Selemeni D alizungumza na akampiga mdogo wake risasi ya kichwa na akapoteza maisha hapo hapo. Selemani D, akatoa kiberiti na pakti ya sigara mfukoni mwa suruli yake. Akatoa sigara moja na kuibana na lipsi zake, akaiwasha na akaanza kupiga mafumba mazito mazito, huku akishuhudia damu za ndugu zake jinsi zinavyo tapakaa kwenye barabara hiyo ya lami.
Selemani D akaivua bulletproof yake kisha akasimama huku bunduki hiyo akiwa ameishika mkononi mwake, akajitokeza kwa askari na akaachia risasi moja iliyo salia kwenye bunduki hiyo, huku akitambua nini kinakwenda kumpata.
    Askari wenye hasira kali sana na wenye uchu wa kuua wakaanza kuvurumisha risasi zisizo na idadi, kuelekea eneo alilo simama Selemani D. Hapakuwa na askari aliye piga risasi yake pembeni na risasi zote zikampata Selemeni D na kumuangusha chini huku mwili wake ukiwa umechakaa kwa kupigwa risasi hizo na huo ndio ukawa mwisho wa maisha yake.
Ukimya kutokea katika eneo zilipo gari za majambazi, zikawafanya askari kuanza kujitokeza kwenye magari yao huku wakianza kuzifwata gari hizo za majambazi kwa umakini sana. Wakamfikia Selemeani D na mmoja wa askari akaipiga teke bunduki iliyopo karibu na mwili wa Selemani D na kuifanya bunduki hiyo iserereke hadi pembezoni mwa barabara.
“Majambazi wote wame kufa”
Askari walianza kupeana ripoti huku wakikagua magari ya majambazi hao. Wakajikuta wakistushwa sana kwa kuto kumuona nabii Sanga katika eneo hilo.
“Nabii Sanga hayupo”
“Hayupo…………!!!?”
Mkuu wa kikosi hicho alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana, kwani lengo la oparesheni hiyo ni kumuokoa nabii Sanga na kuwaangamiza majambazi hao.
                                ***
“Yaani hawakuona sehemu ya kufanyia uchafu wao hadi kanisani kwangu tena ndani ya ofisi yangu?”
Nabii Sanga alizungumza huku akiwa ame fura kwa hasira.
“Ndio baba na hapo wamezungumzia juu ya kuniuua mimi”
Magreth alizungumza huku machozi yakimlenga lenga.
“Una MB humu ndani?”
“Ndio”
Nabii Sanga akajitumia video hiyo kwenye email yake, kisha akamrudisha Magreth simu yake. Akasimama na kujifunga taulo ambalo alilifungua kimakusudi.
“Baba naomba usitishe ule mpango wa kunifungulia mgahawa na kunipangishia nyumba. Wataniua kirahisi, nitaendelea kuishi maisha yangu ya kawaida na nitaendelea kuifanya biashara yangu ya kuuza maandazi baba. Kama Mungu hakunibariki kwa kupitia wewe basi ata nibariki kwa njiani nyingine.”
Magreth alizungumza huku machozi yakimwagika.
“Mage una ongea nini? Nitafanya kila kitu kwa ajili yako na kama yule mwana haramu Tomas wale jamaa zake watakuwa hawaja mfanya nilicho waagiza nita hakikisha kwamba nina muua kwa mkono wangu mimi mwenyewe”
Nabii Sanga alizungumza huku mwili mzima ukimtemeka kwa hasira. Leo hii amejua ubaya wa mke wake, si kuisaliti ndoa yao, bali amekwenda mbali sana hadi kupanga kumteka.
“Mke wako naye?”
“Nitadili naye ninavyo jua mimi. Ili kukuhakikishia kwamba sijabadilisha mawazo yangu ya kukusaidia, kesho kuki pambazuka, nitampigia simu muhasibu wangu aje hapa, mutaenda benki na utafungua akaunti yako na atakuingizia pesa nitakayo ihitaji mimi”
“Lakini baba, mke wako ata niua?”
“Achana na wasiwasi wa mke wangu. Niamini mimi, hembu njoo hapa”
Nabii Sanga alizungumza kwa kujiamini sana. Magreth akaka kitandani hapo huku wote wakibubujikwa na machozi.
“Hivi mwanamke kama huyu, katili, jambazi na ana analiwa hadi ***** kweli ana stahili kuwa mke wangu. Ana stahili kuendelea kuitwa mama mchungaji? Hapana siwezi kuishi na adui nyumba moja na sijapewa upako wa kumvumilia mtu wa namna hii Mage”


Nabii Sanga alilalama kwa uchungu sana hadi Magreth akajikuta akiingiwa na roho ya huruma.
“Mimi najichunga siku zote. Yeye kweli ni wa kunisaliti mimi. Ona jinsi kanisa linavyo muheshimu. Ona kila siku ninavyo simama madhabahuni mwa bwana na kukanya watu wasitende mabaya, wasitumie miili yao vibaya katika swala la mapenzi. Kumbe makatazo yangu ndio anayo yafanya mke wangu, ehehee?”
Nabii Sanga alizidi kulia kama mtoto mdogo. Taratibu Magreth akakilaza kichwa cha nabii Sanga katika bega lake la mkono wa kulia na kuanza kumbembeleza.
“Pole sana baba”
Nabii Sanga akayatupia macho yake kwenye kifua cha Magreth na akayaona maziwa ya mwanamke huyu anaye zidi kumchanganya na kumpagawisha. Taratibu nabii Sanga akaupeleka mkono wake wa kulia kifuani mwa Magreth na kushika z*wa lake moja, huku akijifanya ana endelea kulia. 


Kitendo hicho kikausisimua sana mwili wa Magreth, ikiwa ndio mara yake ya kwanza maishani mwake kukumbwa na hali hiyo. Magreth akajikuta akikaa kimya na kumfanya nabii Sanga azidi kulitomasa zwa hio la Magreth ambalo limenona kisawa sawa.

    Taratibu nabii Sanga akamlaza Magreth kitandani. Joto kali analo lihisi Magreth mwilini mwake, likamfanya azidi kuwa mpole huku akitamani joto hilo liweze kushushwa haraka. Nabii Sanga, akalifungua tenge la Magreth na akabaki kama alivyo .


Nabii Sanga alivyo hakikisha kwamba amesha mlegeza Magreth, taratibu aka.....
“Pole baby”


Nabii Sanga alizungumza huku akiendelea kuvunja ungo wa Magreth. 


Baada ya dakika kumi na tano za mwendo wa taratibu, nabii Sanga akajikuta akifika tamati huku jasho likimwagika mwili mzima. Ukimya ukatawala kati yao huku kila mmoja akitamani kumuanza mwenzake.
“Mage”
“Bee”


“Nina kupenda sana. Nina kuamini sana na nipo tayari kukufanyia kila kitu. Nitahakikisha kwamba una kuwa tajiri na umasikini una usahau. Umenielewa mama?”
“Ndio”


Magreth alijibu kwa sauti ya upole na iliyo jaa aibu kubwa sana. Hakutarajia siku hata moja kama atakuja kumkabidhi nabii Sanga mwili wake tena na bikra yake ambayo alikuwa akiitunza kwa ajili ya mwanaume atakaye muoa.


“Ila nina ombi moja. Endapo atatokea mwanaume akakuchukua mara ya mimi kukubadilisha kimaisha. Haki ya Mungu, nitamuua mbele yako na utashuhudia jinsi nitakavyo ufanya ukatili huo. Kwani sinto kuwa na huruma kabisa na yeye”


Maneno ya nabii SANGA yakamstua sana Magreth, kwani moyo wake haupo kabisa kwa nabii Sanga kwani mwanaume anaye mpenda kuliko kitu chochote ni Evans ambaye yupo hospitalini akipatiwa matibabu kwa pesa za nabii Sanga.


 ITAENDELEA
Haya sasa, nabii SANGA amesha jipatia utamu alio uhitaji kutoka kwa Magreth na kutoa onyo kali ikiwa moyo wa Magreth haupo kwake, je nabii Sanga ata fanikiwa kulinda penzi la Magreth lisivuje kwa Evans? Nini kitatokea? Endelea kufaatilia kisa hikii cha kusisimua, usikose sehemu ya 11.
 


Share:

KIJANA AMUUA BABA YAKE KWA KUMTWANGA NGUMI USONI MOROGORO


Polisi mkoani Morogoro inamshikilia Yohana Isaya Lameck (17) mkazi wa Manyani wilayani Gairo kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi Isaya Lameck (41) kwa kumpiga ngumi usoni na kumkanyaga sehemu mbalimbali za mwili.

 Kamanda wa polisi mkoa wa wa Morogoro SACP Wilbroad Mutafunga amethibitisha.
Share:

ALIYEKUWA MTENDAJI MKUU WA BOHARI YA MADAWA -MSD BWANAKUNU NA MWENZAKE MBARONI KWA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA

Laurian Bwanakunu



Share:

CCM YATOA ONYO RUSHWA WANAOJIPITISHA MAJIMBONI KUGOMBEA UCHAGUZI MKUU…TOA TAARIFA KWENDA NAMBA HII


Chama cha Mapinduzi (CCM), kimeweka utaratibu wa kuboresha namna ya kusimamia maadili kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu kwa kuanzisha kituo cha taarifa za uchaguzi kitakachosaidia kubaini viongozi wanaolaghai watu kwa kutoa rushwa ili wapigiwe kura.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumanne Juni 2, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ametoa namba ambazo watu wanaweza kutoa taarifa hizo kwa kutuma ujumbe wa maneno au kutuma ushahidi wa video au sauti katika mtandao wa whatsapp.

Polepole amesema katika uchaguzi huu rushwa haina nafasi na kwamba chama kiko imara kwenye kusimamia maadali ikiwamo kuwatafuta kokote walipo wanaotumia rushwa kutafuta uongozi.

“Wapo watu wanaojipitisha wilayani na majimboni kwa kigezo cha kuchangisha fomu ya mgombea wa urais, kwa mujibu wa taratibu na mila zetu mgombea wa urais anafahamika, hao wanaochangisha kwa ajili ya fomu ya rais wakamatwe tena muwatolee taarifa kwa vyombo vya dola.

“Iwapo katika mkoa au wilaya iwe Bara au Zanzibar, chama kikibaini baadhi ya viongozi walijihusisha na tabia, mienendo na vitendo vya rushwa tutawanyima uongozi halafu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wasipokuwa wameng’amua hili, chama hakitasita kuelekeza serikali kuwa maofisa waliopewa dhamana katika maeneo hayo hawatoshi,” amesema Polepole.

Aidha ameongeza kuwa ni vema kuwaacha wale ambao bado wanatumikia wananchi wamalize muda wao kwa amani na salama ili kuondoa migongano isiyokuwa na tija ambayo inadhoofisha umoja wa chama hicho.

Share:

MTOTO WA MIAKA MIWILI AFARIKI DUNIA KWA KUNG'ATWA NA FISI SHINYANGA


Picha ya Fisi

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mtoto aliyejulikana kwa jina la Charles Christian Makilika mwenye umri wa miaka miwili na nusu amefariki dunia baada ya kung’atwa na fisi akicheza na wenzake nje ya nyumba yao katika kitongoji cha Mwagala maeneo ya Ugweto kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba tukio hilo limetokea jana Jumatatu Juni 1,2020 majira ya saa moja jioni (1: 00) huko kitongoji cha Mwagala, maeneo ya Ugweto katika Manispaa ya Shinyanga. 

“Mtoto aitwaye Charles Christian Makilika, mwenye umri wa miaka miwili na nusu, mkazi wa Ugweto akiwa anacheza na watoto wenzake nje ya nyumba yao alijeruhiwa kwa kung'atwa na fisi sehemu za usoni kisha kuburuzwa umbali wa mita 50 ambapo fisi huyo alimuachia baada ya kusikia kelele za wananchi waliokuwa wakimfukuza”,amesema Kamanda Magiligimba.

Kamanda Magiligimba amesema mtoto huyo alifariki dunia akiwa njiani akisafirishwa kwenda hospitali ya rufaa ya Bugando mkoani Mwanza kwa matibabu na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga. 

"Natoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha kwamba watoto wako mazingira salama muda wote, wasiachwe peke yao , wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari hasa kwa kipindi hiki ambacho fisi wamekuwa wakionekana maeneo mbalimbali ya mkoa wetu wa Shinyanga",amesema Kamanda Magiligimba.
Share:

Mkataba Mpya Waliosaini Yanga,GSM Na La Liga

Uongozi wa Klabu ya Yanga wakishirikiana na wadhamini wao Kampuni ya GSM Mei 31 wameingia mkataba wa misimu minne wa makubaliano ya kimaendeleo ya timu hiyo na kampuni La Liga 

Makubaliano ya kuingia mkataba huo yalifikiwa juzi kwenye Hoteli ya Serena, jijini Dar ambayo yatahusisha maendeleo ya mchezo wa soka nchini kupitia La Liga ambayo yanahusisha masuala ya ufundi na vifaa mbalimbali.

Klabu ya soka ya Yanga, mbali ya kufaidika na mfumo mpya wa uendeshaji, pia itapata fursa ya mafunzo kwa wachezaji, makocha na viongozi kutoka klabu ya Sevilla ya Hispania.

Mkataba huo ambao msingi wake ni kuifanya Yanga kuwa na mfumo wa kisasa wa uendeshaji, umeenda mbali zaidi ambapo licha ya kucheza mechi mbili kwa mwaka baina ya Sevilla na Yanga, pia utatoa fursa kwa wachezaji chipukizi kujiunga na shule ya michezo ya timu hiyo yenye historia kubwa ya soka.

Kwa mujibu wa ofisa habari wa Yanga, Hassan Bumbuli kutakuwa na mechi mbili kwa mwaka baina ya timu yao na Sevilla ambayo moja itafanyika Hispania na nyingine hapa nchini.

Malipo ya kwanza ya mkataba huo yanatarajiwa kufanyika kati ya kipindi walichoingia mkataba huo hadi Agosti 31, mwaka huu kwa Yanga na GSM kuilipa La Liga kiasi cha euro elfu 80 ambayo ni sawa na Sh milioni 204 baada ya makato iwapo yatatokea.

Wakati malipo ya pili ambayo yatafanyika msimu ujao katika kipindi kati ya Septemba mwaka 2020 hadi Juni 2021

Mbali ya mapendekezo ya mfumo wa uendeshaji, pia kutakuwa na suala mabadiliko ya Katiba ya klabu ambapo mpango wa klabu ya Yanga ni kuwahsirikisha wanachama na wadau wote kwa muda wa siku 21.

Mwenyekiti wa Yanga, Dk Mshindo Msolla alisema wawakilishi wa matawi kutoka kila pande za Tanzania watapata mafunzo maalumu jijini Dar es Salaam na kupewa makabrasha ambayo watayatumia kuendesha elimu ya mabadiliko hayo pindi watakaporejea kwenye matawi yao




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger